Tuesday, 2 December 2025

TUTAPONYA WAATHIRIKA WA MATUKIO YA OKTOBA 29, 2025



Jaji Mkuu mstaafu na Mwenyekiti wa Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya uvunjifu wa amani wakati na baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 Mohammed Chande Othman amesema katika kutekeleza wajibu wa Tume hiyo, wanatarajia kuponya waathirika wa vurugu hizo pamoja na watuhumiwa wa matukio hayo ya Oktoba 29.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu Disemba Mosi, 2025, Jaji Chande amesema watawatafuta walioshiriki, Vyama vya siasa, asasi za kiraia, wasimamizi wa uchaguzi na Tume huru ya Taifa ya uchaguzi, Viongozi wa dini na Watu wengine ili kuzungumza nao kuhusu matukio hayo.

Aidha pia ameeleza kuwa watazungumza pia na wajasiriamali, wafanyabiashara, watu mashuhuri, mamlaka za serikali za mitaa katika maeneo yaliyoathirika, Vyombo vya ulinzi na usalama, wanahabari na sekta binafsi pamoja na washirika mbalimbali wa maendeleo.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE DESEMBA 2,2025

 

Magazeti


  
                     


Share:

RC KUNENGE KUZINDUA MBIO MAALUMU ZA ADEM BAGAMOYO


Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu-ADEM umepanga kufanya mbio maalumu za marathon zitakazohusisha wadau mbalimbali wa elimu, mashirika na taasisi yanayojihusisha na usimamizi wa elimu, wanachuo wa vyuo mbalimbali katika Mkoa wa Pwani na wananchi wote zikilenga kuhamasisha umoja, amani na utulivu katika Taasisi za kielimu pamoja na kuchangisha fedha kwa ajili ya kuboresha miundo mbinu katika Chuo cha ADEM kilichopo Bagamoyo Mkoani Pwani.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Disemba 02, 2025 Mtendaji Mkuu wa ADEM Dkt. Maulid J. Maulid amewakaribisha wadau wote wanaojihusisha na masuala ya elimu nchini katika Mkoa wa Pwani na kwingineko nchini kuja kushiriki katika mbio hizo zitakazofanyika siku ya Jumamosi tarehe 06 Disemba, 2025 kuanzia saa 12 kamili Asubuhi ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Aboubakar Kunenge.

Pia kuhusu utaratibu wa namna ya kushiriki Dkt. Maulid amesema washiriki watachangia gharama kidogo ili kufanikisha lengo la Wakala la kukusanya fedha kwa ajilo ya kuboresha miundombinu yake na watapatiwa vifaa kwa ajili ya kushiriki mbio hizo ikiwemo jezi, kofia n.k huku washindi katika mbio hizo wakipatiwa zawadi mbalimbali za fedha taslimu.

Aidha, Dkt. Maulid amesema mbio hizo zitafanyika katika umbali wa Kilomita 10 na Kilomita 5 kuanzia ADEM Bagamoyo na kisha kuelekea katika viunga vya Mji huo mpya wa Bagamoyo kwa umbali uliotajwa. Aidha, amesisitiza wanaotaka kushiriki mbio hizo kuwasiliana na Wakala kwa Simu Namba: 0752 160555/0742 777222

Kauli mbiu ya mbio hizo inasema “Miundombinu Bora kwa Uongozi Thabiti wa Elimu” ikichagiza kuchangia uboreshaji wa miundombinu ya Elimu ili kuimarisha utoaji wa Elimu Bora.
Share:

Monday, 1 December 2025

MOTO WA CHUKI WAKEMEWA: WATANZANIA WATAKA UMOJA NA UTULIVU UTUNZWE

Watanzania, hasa vijana, wamehimizwa kukataa vikali moto wa chuki na mgawanyiko, wakisisitizwa kuwa maendeleo hayawezi kustawi bila amani na umoja. 
Wito huo unaelekezwa kwa vijana wa Taifa la Kesho kujiepusha na vurugu ambazo huzua hofu, msongo wa mawazo, na huzuni.

Ujumbe mkuu unaojirudia katika jumbe mbalimbali za wananchi ni: “Maendeleo hayawezi kustawi kama kuna moto wa chuki na mgawanyiko. Amani si tu ukosefu wa vita, bali ni hali ya utulivu, heshima, na umoja inayotuwezesha kujenga pamoja.”

Vijana  wanakumbushwa kwamba wao ndio Nguvu ya Sasa na Taifa la Kesho, na hivyo wanapaswa kuthamini amani ya Tanzania ambayo imebarikiwa kuwa "kisiwa cha amani" katika ukanda huu.

Wananchi wanatoa wito wa wazi wa kukataa mgawanyiko: “Kataa kabisa fikra, matendo, au kauli zinazotaka kutugawa kwa misingi ya dini, kabila, au siasa. Sisi ni Watanzania Kwanza! Umoja wetu ndio silaha yetu kubwa.”

Ili kudumisha amani, wanahimizwa kujenga maridhiano kwa kutumia lugha ya staha, kusikiliza wengine, na kutatua tofauti kwa mazungumzo na upendo.

Wananchi mitandaoni wamesema kwamba amani ndiyo tunu, msingi, na dira ya maisha bora na maendeleo. "Amani ni dira ya maendeleo na maendeleo ndio safari yetu," ilisema moja ya jumbe za wananchi, ikionya kwamba vurugu sio njia ya kudai haki bali ni njia ya kuvunja amani moja kwa moja.



Share:

“VIJANA ACHENI GHASIA, MTATUUA KWA NJAA” — MACHOZI YA MACHINGA KARIAKOO

Katika hali ya wasiwasi inayoendelea nchini, hasa kuhusu uwezekano wa kuzuka kwa vurugu zingine, kuanzia Desemba 9 sauti ya wazazi na wafanyabiashara wadogo inazidi kupaaa  ikihimiza watoto wao waepuke vurugu, wakisisitiza kwamba maisha yao yanategemea amani na utulivu.
Mama Zawadi, mchuuzi mzoefu wa soko la Kariakoo, amekuwa kinara wa kuakisi hofu ya Watanzania ambao maisha yao huhesabiwa kwa faida ya siku. 

Akizungumza kwa hisia, Mama Zawadi alieleza: “Mimi ni Mama Zawadi, mchuuzi wa soko la Kariakoo, na naongea kwa niaba ya maelfu ya Watanzania ambao maisha yetu hutegemea kupata riziki ya kila siku. Ninaposikia wito wa maandamano yenye vurugu, moyo wangu unajawa na hofu isiyoelezeka.”

Woga wake mkubwa unahusu jinsi ghasia zinavyokwamisha shughuli za kiuchumi. "Maandamano yanamaanisha masoko kufungwa, biashara kusimama, na uwezekano wa kupoteza kipato ambacho ndio mlo wa watoto wetu," alifafanua. 

Alitoa onyo kali kwa vijana: "Tunaweza vipi kupata chakula kama hatuwezi kufanya kazi? Kusimamisha nchi ni sawa na kutuhukumu kifo kwa njaa.”

Aidha, Mama Zawadi aliweka bayana athari za machafuko kwa kundi la wagonjwa sugu, kama wa UKIMWI na Kisukari, ambao maisha yao yanategemea upatikanaji wa huduma za afya bila kukosa. 

Alisimulia maelezo ya mmoja wa wagonjwa alisema, "Kukiwa na machafuko, hospitali zinasita kufanya kazi, usafiri unakwama. Tutapata wapi dawa zetu? Bila dawa, afya yetu inazidi kuzorota. Tunaomba huruma!’”

Mama Zawadi alimalizia kwa kuwataka vijana kutafuta suluhu kupitia mazungumzo na kuonya: "Kuna ndugu zetu tayari wamepoteza wapendwa wao... maandamano yenye ghasia yataacha majonzi ya kudumu."


Share:

DKT. MWIGULU AWATOA WASIWASI WATANZANIA: “AMANI YETU HAIUZWI!”

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amesema serikali imeendelea kufanya mikutano na viongozi wa taasisi mbalimbali za dini, ikiwemo Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), na viongozi wa kimila ili kuwaeleza hali halisi ya usalama nchini na kuwataka kuendelea kudumisha amani.

Kauli hiyo aliitoa wakati akizungumza na wananchi wa Arusha katika ziara byake ya kikazi ambayo poia ameitumia kuangalia uharibifu uliofanywa katika vurugu ya Oktoba 29.

Waziri Mkuu amesisitiza umuhimu wa amani kama msingi mkuu wa maendeleo ya taifa.

Katika ziara hiyo pia  aliwapa wananchi salamu za pole zilizotolewa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kufuatia athari za  vurugu zilizotokea hivi karibuni.

Waziri Mkuu alitembelea na kukagua uharibifu uliotokea wakati wa vurugu za Oktoba 29, 2025, ambapo Kituo cha Polisi cha Kikatiti, Mahakama ya Mwanzo ya Maji ya Chai, na kituo cha mafuta cha Total Energies vilichomwa moto. Aidha, alibaini kuibwa kwa mali katika soko kuu na kubomolewa kwa sefu ya kutunzia fedha.

Waziri Mkuu amewaonya wananchi kuwa kuchagua vurugu ni sawa na kuchagua kufukuza maendeleo na kuongeza umaskini kwa mtu mmoja mmoja, akisisitiza kuwa ahadi za maendeleo kama maji na barabara zitafanyika endapo tu nchi itakuwa na amani.


Share:

DKT. MWIGULU AFICHUA NJAMA: ‘WANAHARAKATI WANALIPWA MAMILIONI KUIVURUGA TANZANIA’

 Serikali imefichua kuwa chokochoko na vurugu zinazoendelea nchini zimeletwa na wanaharakati wanaolipwa kwa lengo la kuharibu uchumi wa nchi na kurudisha nyuma maendeleo. 

Waziri Mkuu Dkt Mwigulu Nchemba amewataka Watanzania kukataa kushawishiwa na wanaharakati hao.

Waziri Mkuu ameeleza kuwa baadhi ya vijana walio nje ya nchi wamebainika kupokea kiasi cha Dola za Marekani milioni mbili (sawa na takribani shilingi bilioni 4.5) ili kuchochea vurugu nchini.

 Alihimiza watanzania kujiuliza maswali kuhusu maslahi na ajenda ya watu wanaotoa malipo hayo kwa nchi.

Kulingana na maelezo ya Waziri Mkuu, lengo kuu la wachochezi hawa ni kunyakua rasilimali adimu za Tanzania. Alitaja ugunduzi wa Uranium (Tanzania ikiwa nchi ya tisa duniani na ya kwanza Afrika kwa tani za ujazo 890,000) na maendeleo ya miradi ya gesi asilia kama vivutio vikubwa vinavyowafanya waivuruge Tanzania.

"Hawa watu wanalenga tugombane ili wachukue madini adimu (rare earth minerals)... Wanajua Tanzania ina gesi asilia nyingi na inakaribia kuanza," alionya Waziri Mkuu.

Amesisitiza kuwa mbinu hizi zimetumika katika nchi zingine barani Afrika, ambapo chokochoko huanzishwa ili kuruhusu uvurugaji na uchukuaji wa rasilimali, kabla ya wachochezi kuondoka baada ya rasilimali kuisha. 

Waziri Mkuu ametoa wito kwa Watanzania "kuamka na kuchukua tahadhari" dhidi ya mchezo huu, akisisitiza kuwa ajira na uondoaji wa umaskini utapatikana tu nchi ikiwa na amani.


Share:

Sunday, 30 November 2025

VIJANA TUMUUNGE MKONO RAIS SAMIA KATIKA UJENZI WA TAIFA- CHILONGOLA



Na mwandishi wetu, Dar

Bw. Joseph John Chilongola, Mkazi wa Dar Es Salaam ameeleza kufurahishwa na Uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan na jitihada mbalimbali anazozichukua katika kuupata muafaka wa Kitaifa, akiwataka wananchi kujiepusha na mikumbo na hamasa za uvunjifu wa amani zinazotolewa Mitandaoni.

Chilongola ameeleza namna ambavyo Rais Samia amekuwa akiongozwa na uzalendo kwa nchi yake, suala ambalo limemfanya kuwekeza zaidi katika maendeleo ya watu ikiwemo ujenzi wa miundombinu mbalimbali ya barabara tena kwa kiwango cha lami katika mikoa yote nchini.

"Mfano ni hapa Msongola, Kata yetu ilikuwa na shida kubwa sana ya barabara lakini sasa kwa asilimia kubwa, barabara hizo zinaelekea kutunufaisha." Amesisitiza Mwananchi huyo.

Chilongola ameeleza pia kuhusu namna ambavyo vijana wamekuwa wakitumika katika matukio ya uvunjifu wa amani, akiwasihi kujiepusha na matukio hayo na kushirikiana na serikali ya awamu ya sita katika ujenzi wa Taifa lao.

Amesisitiza pia kumtomkatisha tamaa Rais Samia, akitaja mchakato wa maridhiano kama jambo muhimu kwa Taifa katika kuondoa changamoto na tofauti zilizopo pamoja na kusaidia katika kudumisha amani ya Tanzania.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger