Thursday, 6 November 2025

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA NOVEMBA 7, 2025

Share:

MRADI WA SHULE BORA KUKAMILISHA UJENZI WA DARASA SHULE YA MSINGI BIRIKANI – HANDENI MJI




Na Mwandishi Wetu, Handeni TC 

MRADI wa Shule Bora upo hatua za mwisho kukamilisha ujenzi wa darasa jipya katika Shule ya Msingi Birikani, Halmashauri ya Mji Handeni, hatua inayotarajiwa kuongeza ufanisi wa ufundishaji na ujifunzaji kwa wanafunzi wa shule hiyo.

Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Elieskia Mmbuji, ametoa taarifa hiyo kwa Timu ya Usimamizi ya Halmashauri iliyoongozwa na Mkurugenzi wa Halmashauri, Maryam Ukwaju, wakati wa ziara ya ukaguzi wa maendeleo ya mradi huo.

Mmbuji amesema kuwa hadi sasa jumla ya Sh.11,774,310 zimetumika katika hatua mbalimbali za ujenzi, kati ya Sh. milioni 15 zilizopokelewa kutoka Mradi ya Shule Bora mnamo Mei 27, 2025.

Ameeleza kuwa ujenzi huo umeanzishwa kwa lengo la kupunguza changamoto ya mrundikano wa wanafunzi na kuimarisha mazingira ya kujifunzia, jambo litakalosaidia walimu kutoa elimu bora zaidi.

“Ukamilishaji wa darasa hili utapunguza msongamano wa wanafunzi madarasani na kuboresha mazingira ya kujifunza, hivyo kuongeza ubora wa elimu katika shule yetu,” amesema Mmbuji.
Share:

SAMUU PRIMARY SCHOOL YANG’ARA KITAIFA, YAPATA DARAJA A KWA WOTE MATOKEO DARASA LA SABA 2025!



SAMUU PRIMARY SCHOOL YANG’ARA KITAIFA, YAPATA DARAJA A KWA WOTE MATOKEO DARASA LA SABA 2025!

Shule ya Msingi Samuu Primary School iliyopo katika Manispaa ya Shinyanga imefanya vizuri kwa kiwango cha juu katika matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Darasa la Saba (PSLE) mwaka 2025, baada ya wanafunzi wake kufaulu kwa asilimia 100 na shule hiyo kupata Daraja A (Bora).

Kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA), jumla ya wanafunzi 63 walifanya mtihani huo na wote wamefaulu kwa mafanikio makubwa, huku shule ikipata wastani wa alama 272.3968.

Kati ya wanafunzi hao, wasichana 28 na wavulana 35 walishiriki mtihani, ambapo wanafunzi 59 wamepata daraja A, na wanafunzi 4 wakipata daraja B. Hakuna mwanafunzi aliyepata daraja C, D au E – ishara kwamba shule hiyo imejipambanua kuwa miongoni mwa shule bora zaidi katika Mkoa wa Shinyanga na hata kitaifa.

Mafanikio hayo yanatajwa kuwa matokeo ya juhudi kubwa za walimu, ushirikiano mzuri wa wazazi pamoja na nidhamu na bidii ya wanafunzi, chini ya uongozi makini wa walimu wakuu wa shule hiyo.

Wazazi na wananchi wameipongeza shule hiyo kwa kuendelea kuwa kielelezo cha ubora wa elimu, huku wakihamasisha shule nyingine kuiga mfano wake wa mafanikio.

Wasiliana na Samuu Primary School 
kwa simu : 0765018834/0754765336
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI NOVEMBA 6,2025



Magazeti







Share:

Wednesday, 5 November 2025

SportPesa Tanzania named Africa’s best sports betting brand at the best brand Africa awards

 

From over 12,000 brands across the continent, SportPesa Tanzania has emerged as a continental champion — recognized as Africa’s Best Sports Betting Brand at the Best Brand Africa Awards.

This recognition isn’t just a title; it’s proof that the brand’s commitment to trust, technology, and customer experience is setting new benchmarks for sports betting in Africa.

A journey built on vision and trust

SportPesa Tanzania’s journey began with one clear mission — to redefine how fans experience sports betting in Tanzania through innovation and integrity.

Out of thousands of competing brands, SportPesa’s customer-first approach distinguished it as the ultimate leader. The Best Brands Africa Awards evaluation — combining market data and consumer sentiment — validated SportPesa’s influence beyond borders, reshaping how Africa engages with sport, betting, and entertainment.

Customer trust at the core

In an industry where credibility is king, SportPesa Tanzania has made unprecedented investments in secure betting systemsfast payment options, and data protection protocols to safeguard every user. Players can bet confidently, knowing their funds and personal data are protected by top-tier encryption and compliant standards.

“This win is proof that with a clear vision, consistency, and dedication, we truly make it count,” said Jason Ndambala, head of PR at SportPesa Tanzania. That trust has transformed SportPesa into a household name — synonymous with reliability, integrity, and fair play.

Innovation that keeps fans ahead

SportPesa’s success lies in its relentless drive to innovate. From live betting and mobile-first platforms to a growing portfolio of casino games in Tanzania, the brand is redefining what a modern, interactive betting experience feels like.

Continuous updates, smarter tools, and improved personalization keep SportPesa ahead of trends — giving users a truly world-class experience designed for both excitement and safety.

A win that reflects passion and consistency

This award is a celebration of SportPesa’s commitment to responsible gaming, customer satisfaction, and technological leadership. But beyond the accolades, it honors the millions of fans and players who make SportPesa their home for entertainment, community, and winning moments.

“Being named Africa’s Best Sports Betting Brand is not just a milestone — it’s a celebration of belief, innovation, and doing things right,” added the company.

Setting the standard for Africa

This continental recognition cements SportPesa Tanzania as a true leader in the digital gaming industry. For fans, it’s a mark of quality. For competitors, it’s a challenge. For Africa, it’s proof that homegrown excellence can rival global standards. Choosing SportPesa means choosing reliability, innovation, and trust — values that continue to power the brand’s rise beyond Tanzania’s borders.

SportPesa Tanzania’s victory at the Best Brand Africa Awards signals more than industry leadership — it’s a defining moment for African innovation. As the brand continues to inspire with its commitment to transparency and customer-first thinking, it’s clear that SportPesa is not just betting on sports — it’s betting on Africa’s potential.

 


Share:

Tuesday, 4 November 2025

WANANCHI WOTE RUKSA KUREJEA KWENYE SHUGHULI ZAO KUANZIA NOVEMBA 4, 2025



TAARIFA KWA UMMA

Kama alivyoelekeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa hotuba yake baada ya kuapishwa leo jijini Dodoma, kuanzia kesho Jumanne tarehe 4 Novemba 2025, wananchi wote nchini wanajulishwa kurejea kwenye shughuli zao za kila siku za kiuchumi na kijamii. 

Aidha, wananchi wanaaswa kuendelea kuzingatia tahadhari na miongozo ya kiusalama kadri itakavyokuwa inatolewa na Vyombo vya Ulinzi na Usalama katika maeneo yao. 

Imetolewa na 
Katibu Mkuu Kiongozi
3 Novemba 2025

Share:

DR. SAMIA AAPISHWA KUWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA


Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameapishwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ikulu Chamwino mkoani Dodoma leo Jumatatu Novemba 3,2025



Share:

Monday, 3 November 2025

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO OKTOBA 29, 2025

Magazeti
Share:

Wednesday, 29 October 2025

DKT. SAMIA APIGA KURA CHAMWINO



Na Dotto Kwilasa, Dodoma


Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Jumatano Oktoba 29, 2025, amejitokeza kupiga kura katika kituo cha Kijiji cha Chamwino, mkoani Dodoma, wakati wa zoezi la Uchaguzi Mkuu linaloendelea kote nchini.

Dkt. Samia alipowasili kituoni hapo mapema asubuhi, alijiunga na wananchi wengine kwenye mstari wa foleni akisubiri zamu yake kupiga kura  tukio lililopokelewa kwa hisia kubwa za furaha na hamasa kutoka kwa wananchi waliokusanyika kushuhudia tukio hilo la kihistoria.

Baada ya kupiga kura, Dkt. Samia amewataka Watanzania wote kujitokeza kwa wingi kutekeleza haki yao ya Kikatiba kwa utulivu, akisisitiza kuwa amani na mshikamano ni msingi wa maendeleo ya taifa.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger