Thursday, 9 October 2025
Wednesday, 8 October 2025
UCHAGUZI WA AMANI: WANANCHI WATOA AHADI YA KUJITOKEZA OKTOBA 29
Tuesday, 7 October 2025
MAZOEZI NI KINGA YA TAIFA, SIO VITISHO
Vikosi vya Ulinzi na Usalama nchini vimeendelea kufanya mazoezi ya pamoja, hatua ambayo imeelezwa kuwa ni utaratibu wa kawaida wa kijeshi unaolenga kuimarisha utayari na weledi na wala si mbinu ya kuwatisha wananchi.Kauli hii inatolewa kufuatia kuwepo kwa upotoshaji wa taarifa kwenye mitandao ya kijamii, unaodai kuwa mazoezi hayo yanatumika kama vitisho au mbinu za kukandamiza.
Vyombo hivyo vimekiri kuwa kuna propaganda hizo zisizo na msingi zinazoenezwa mtandaoni zinafanywa kwa lengo la kuchochea hofu na kuhalalisha maandamano haramu.
Wito umetolewa kwa wananchi wote kupuuza uzushi wa mitandaoni na kutambua kuwa mazoezi haya ni ngao ya taifa, si tishio kwa wananchi.
"Huu ndio uthibitisho kwamba Tanzania inaendelea kuwa nchi ya amani, salama, na thabiti. Mazoezi haya ni kinga yetu kama taifa," ilihitimisha taarifa hiyo.
Vikosi vya ulinzi vimekumbusha umma kuwa mazoezi ndiyo shughuli yao ya msingi, na hakuna sababu yoyote kwa wananchi kuwa na hofu. Lengo la msingi la mazoezi ya pamoja ni kupima uwezo wa vikosi vyote wakati wa kushughulikia mambo mbalimbali yanayohusu taifa, ikiwamo:Ulinzi wa mipaka na amani ya taifa;Kukabiliana na maafa (mfano: tetemeko la ardhi, mafuriko au majanga mengine) na Kudumisha mshikamano wa kiutendaji kati ya vyombo vyote vya ulinzi.
"Mazoezi haya, yanayojumuisha matembezi ya pamoja, mafunzo ya viungo, na mazoezi ya kivita, yanaboresha afya za askari, yanaongeza weledi wa kazi, na kujenga mshikamano wa kikazi," ilisema taarifa iliyotolewa na vyombo hivyo.
Vyombo vya Ulinzi na Usalama vimesisitiza kuwa mazoezi mengi hufanyika hadharani katika barabara na maeneo ya wazi ili kuonyesha uwazi na kuhakikisha wananchi wanatambua utayari wa vyombo vyao vya ulinzi.
"Ukweli unabaki palepale: wananchi wengi wameona kwa macho yao kuwa mazoezi haya ni kielelezo cha utayari wa vyombo vyetu vya ulinzi na usalama," ilisisitiza taarifa hiyo.
NSSF YAANZA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA JIJINI ARUSHA
Na Bora Fadhili - Arusha
Aidha, Meneja wa Huduma kwa Wateja, Robert Cosmas Kadege, amesema kampeni hii ina umuhimu mkubwa kwa sababu inahamasisha wanachama kuchangia kwa hiari. Kadege alibainisha kuwa mwanachama anaweza kuchangia kwa hiari kupitia njia mbalimbali za kidigitali, na hata wale wasio na simu janja wanaweza kuchangia kwa kutumia menu husika kwenye simu zao za kawaida.
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Taifa Masha Mshomba, amesisitiza kuwa wiki hii ya huduma kwa wateja inalenga kuonyesha huduma bora kwa wateja na kuwashukuru watumishi kwa jitihada zao katika utoaji wa huduma hizo. "Bila wateja hatuwezi kuwa na mfuko," alisema.
Masha Mshomba pia aliongeza kuwa huduma kwa mfumo wa TEAMA imefikia asilimia 97 na wanatarajia kufikia asilimia 100 kabla ya mwisho wa mwaka huu. Kuhusu changamoto za wateja ambao bado hawajafikiwa, alihakikishia kuwa wataendelea kuwafikia na kuwapatia huduma bora zaidi.
Aidha, alisema kuwa thamani ya mfuko kwa mwaka 2024/2025 imefikia trilioni 9.9, ikionyesha ukuaji mkubwa ikilinganishwa na thamani ya trilioni 4.8 mwezi Machi 2021, ongezeko la zaidi ya asilimia 100. Alimshukuru wafanyakazi wa NSSF kwa ushirikiano wao katika kufanikisha mafanikio haya.
Aidha Kuhusu michango ya hiari, Masha Mshomba amesema kuwa kwa wale wasioajiriwa serikalini au sekta binafsi, wanaweza kuchangia kwa hiari kila wiki, mwezi au hadi miezi 12 mfululizo bila kupata adhabu yoyote (penaty).
Aliongeza kuwa NSSF ni muhimu kwa sababu husaidia wafanyakazi wakati wa matatizo kama vifo au ugonjwa, ambapo familia na wagonjwa hawatahangaika kutafuta misaada ya kifedha.
Mmoja wa wastaafu aliyeongea katika maadhimisho hayo alisema kuwa pensheni zao huliwa kwa wakati na hawajawahi kukosa malipo, na kwamba wastaafu wamejaliwa sana. Aliwahi kusisitiza umuhimu wa NSSF kwa wafanyakazi wanaoendelea kufanya kazi.
Aidha, Jackiline Emmanuel, aliyepokea mafao ya uzazi, aliipongeza NSSF kwa huduma nzuri alizopata na kusema amefurahia kuwa na mfuko huu unaowajali wanachama wake.
Lightness Emmanuel Munga pia alieleza jinsi NSSF ilivyomsaidia kwa malipo ya wake upo wake wa matibabu baada ya kupata tatizo la mgongo na kuenda India kwa matibabu zaidi, na sasa anaendelea kupata huduma kupitia mfuko huo.
Sunday, 5 October 2025
MADIWANI SONGEA MJINI WAONESHA UMOJA,KAMPENI ZA CCM ZAZIDI KUSHIKA KASI MSHANGANO
Na Regina Ndumbaro Mshangano-Songea
Katika harakati za uzinduzi wa kampeni za udiwani zinazoendelea katika kata mbalimbali za Jimbo la Songea Mjini, madiwani kutoka kata tofauti wameendelea kuonesha mshikamano mkubwa kwa kuungana kumuunga mkono mwenzao Benson Sovela, mgombea wa nafasi ya udiwani Kata ya Mshangano.
Uzinduzi huo umefanyika leo Oktoba 5, 2025 katika kijiji cha Chandarua na umehudhuriwa na wananchi wengi pamoja na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Mgeni rasmi katika uzinduzi huo ni Katibu wa CCM Wilaya ya Songea Mjini, James Daniel Mgego, ambaye amemkabidhi rasmi Benson Sovela kitabu cha Ilani ya CCM kama ishara ya kuanza rasmi kampeni.
Mgego ametumia fursa hiyo kusisitiza umuhimu wa wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba, akieleza kuwa amani na mshikamano ni nguzo kuu za maendeleo nchini.
Aidha, ameonya dhidi ya propaganda za uchochezi zinazosambazwa mitandaoni na kuhimiza wazazi na wazee kuwahamasisha vijana kushiriki kikamilifu katika uchaguzi.
Katika hotuba yake, Benson Sovela amewaomba wananchi wa Kata ya Mshangano kumpa ridhaa ya kuwa diwani wao kupitia sanduku la kura.
Ameahidi kuwa kiongozi wa watu wote bila kujali itikadi au tofauti zozote, huku akisisitiza kuwa maendeleo hayana chama na kwamba kazi nzuri ya CCM inapaswa kuungwa mkono.
Ametaja mafanikio yaliyopatikana kupitia serikali ya CCM, hasa katika sekta za elimu na afya, kuwa ni ushahidi tosha wa dhamira ya kweli ya kuleta maendeleo.
Benson Sovela pia ameahidi kushughulikia changamoto zinazowakabili wananchi wa Mshangano, ikiwemo uboreshaji wa miundombinu ya barabara hasa barabara ya Namanyigu–Mshangano, pamoja na kuhakikisha upatikanaji wa maji safi na salama katika maeneo yenye uhaba wa huduma hiyo.
Amesema kuwa kupitia ilani ya CCM, miradi hiyo yote itatekelezwa kwa ufanisi iwapo atapewa nafasi ya kuwatumikia.
Uzinduzi huo umeonyesha si tu nguvu ya CCM katika Jimbo la Songea Mjini, bali pia mshikamano na umoja wa madiwani katika kuhakikisha kuwa kila kata inapata kiongozi makini na mwenye maono ya maendeleo.
Wananchi wamehimizwa kuendelea kudumisha amani na mshikamano kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho



DK. SAMIA AENDELEA KUAHIDI UJENZI WA BARABARA ZA LAMI, KUONGEZA IDADI YA WATALII NA KUTATUA KERO YA WANYAMA WAKALI MANYARA





















