Thursday, 9 October 2025

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI OKTOBA 9,2025


Magazeti






Share:

Wednesday, 8 October 2025

UCHAGUZI WA AMANI: WANANCHI WATOA AHADI YA KUJITOKEZA OKTOBA 29




Na mwandishi wetu, DAR

Wananchi wenye haki ya kupigakura katika uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 wamehamasishwa kujitokeza kwa wingi kupiga kura katika uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 ili kuchagua Viongozi wanaoweza kuwaletea maendeleo na kutimiza wajibu wao wa Kikatiba na kidemokrasia.

Wananchi hao pia akiwemo Mwanahuba Jumbe Ramadhani wamesisitiza umuhimu wa kutii sheria na Miongozo ya uchaguzi, akisema ifikapo Oktoba 29, 2025 mara baada ya zoezi la kupiga kura ni muhimu kila mmoja akarejea nyumbani na kuendelea na shughuli zake badala ya kutii wito unaotolewa na baadhi ya wanasiasa wa kulinda kura kwenye Vituo, kazi ambayo ni ya mawakala wa vyama vya siasa na tume huru ya Taifa ya uchaguzi.

Richard Alphonce na Bw. Abdallah Ismail Haruna, wakazi wa Dar Es Salaam wakisisitiza kuwa kura ni haki ya kimsingi, wamebainisha kuwa mabalozi wazuri wa uchaguzi kwa kuhamasisha Vijana wenzao kupiga kura na kujitokeza kwa wingi kwani kura ndio njia pekee ya kidemokrasia ya kuweza kumchagua Kiongozi sahihi pamoja na kuwawajibisha wale walioko madarakani na walioshindwa kutimiza ahadi na matarajio ya wananchi.


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO OKTOBA 8,2025

Magazeti ya leo

 




Share:

Tuesday, 7 October 2025

INEC YATOA TAARIFA KUHUSU WAPIGA KURA NA VITUO VYA KUPIGIA KURA UCHAGUZI MKUU 2025



Share:

MAZOEZI NI KINGA YA TAIFA, SIO VITISHO

Vikosi vya Ulinzi na Usalama nchini vimeendelea kufanya mazoezi ya pamoja, hatua ambayo imeelezwa kuwa ni utaratibu wa kawaida wa kijeshi unaolenga kuimarisha utayari na weledi na wala si mbinu ya kuwatisha wananchi.

Kauli hii inatolewa kufuatia kuwepo kwa upotoshaji wa taarifa kwenye mitandao ya kijamii, unaodai kuwa mazoezi hayo yanatumika kama vitisho au mbinu za kukandamiza.

Vyombo hivyo vimekiri kuwa kuna propaganda hizo zisizo na msingi zinazoenezwa mtandaoni zinafanywa kwa lengo la kuchochea hofu na kuhalalisha maandamano haramu.

Wito umetolewa kwa wananchi wote kupuuza uzushi wa mitandaoni na kutambua kuwa mazoezi haya ni ngao ya taifa, si tishio kwa wananchi.

"Huu ndio uthibitisho kwamba Tanzania inaendelea kuwa nchi ya amani, salama, na thabiti. Mazoezi haya ni kinga yetu kama taifa," ilihitimisha taarifa hiyo.

Vikosi vya ulinzi vimekumbusha umma kuwa mazoezi ndiyo shughuli yao ya msingi, na hakuna sababu yoyote kwa wananchi kuwa na hofu. Lengo la msingi la mazoezi ya pamoja ni kupima uwezo wa vikosi vyote wakati wa kushughulikia mambo mbalimbali yanayohusu taifa, ikiwamo:Ulinzi wa mipaka na amani ya taifa;Kukabiliana na maafa (mfano: tetemeko la ardhi, mafuriko au majanga mengine) na Kudumisha mshikamano wa kiutendaji kati ya vyombo vyote vya ulinzi.

"Mazoezi haya, yanayojumuisha matembezi ya pamoja, mafunzo ya viungo, na mazoezi ya kivita, yanaboresha afya za askari, yanaongeza weledi wa kazi, na kujenga mshikamano wa kikazi," ilisema taarifa iliyotolewa na vyombo hivyo.

Vyombo vya Ulinzi na Usalama vimesisitiza kuwa mazoezi mengi hufanyika hadharani katika barabara na maeneo ya wazi ili kuonyesha uwazi na kuhakikisha wananchi wanatambua utayari wa vyombo vyao vya ulinzi.

"Ukweli unabaki palepale: wananchi wengi wameona kwa macho yao kuwa mazoezi haya ni kielelezo cha utayari wa vyombo vyetu vya ulinzi na usalama," ilisisitiza taarifa hiyo.

Share:

NSSF YAANZA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA JIJINI ARUSHA

Na Bora Fadhili - Arusha 

Meneja wa NSSF Mkoa wa Arusha, Joseph Komba, ameeleza kuwa kuanzia mwezi Julai hadi Septemba, kupitia mifumo ya kidigitali, wameweza kulipa mafao kwa asilimia 98 ya wanachama ndani ya siku 30.

Aidha, Meneja wa Huduma kwa Wateja, Robert Cosmas Kadege, amesema kampeni hii ina umuhimu mkubwa kwa sababu inahamasisha wanachama kuchangia kwa hiari. Kadege alibainisha kuwa mwanachama anaweza kuchangia kwa hiari kupitia njia mbalimbali za kidigitali, na hata wale wasio na simu janja wanaweza kuchangia kwa kutumia menu husika kwenye simu zao za kawaida.

Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Taifa Masha Mshomba, amesisitiza kuwa wiki hii ya huduma kwa wateja inalenga kuonyesha huduma bora kwa wateja na kuwashukuru watumishi kwa jitihada zao katika utoaji wa huduma hizo. "Bila wateja hatuwezi kuwa na mfuko," alisema.

Masha Mshomba pia aliongeza kuwa huduma kwa mfumo wa TEAMA imefikia asilimia 97 na wanatarajia kufikia asilimia 100 kabla ya mwisho wa mwaka huu. Kuhusu changamoto za wateja ambao bado hawajafikiwa, alihakikishia kuwa wataendelea kuwafikia na kuwapatia huduma bora zaidi.

Aidha, alisema kuwa thamani ya mfuko kwa mwaka 2024/2025 imefikia trilioni 9.9, ikionyesha ukuaji mkubwa ikilinganishwa na thamani ya trilioni 4.8 mwezi Machi 2021, ongezeko la zaidi ya asilimia 100. Alimshukuru wafanyakazi wa NSSF kwa ushirikiano wao katika kufanikisha mafanikio haya.

 Aidha Kuhusu michango ya hiari, Masha Mshomba amesema kuwa kwa wale wasioajiriwa serikalini au sekta binafsi, wanaweza kuchangia kwa hiari kila wiki, mwezi au hadi miezi 12 mfululizo bila kupata adhabu yoyote (penaty).

Aliongeza kuwa NSSF ni muhimu kwa sababu husaidia wafanyakazi wakati wa matatizo kama vifo au ugonjwa, ambapo familia na wagonjwa hawatahangaika kutafuta misaada ya kifedha.

Mmoja wa wastaafu aliyeongea katika maadhimisho hayo alisema kuwa pensheni zao huliwa kwa wakati na hawajawahi kukosa malipo, na kwamba wastaafu wamejaliwa sana. Aliwahi kusisitiza umuhimu wa NSSF kwa wafanyakazi wanaoendelea kufanya kazi.

Aidha, Jackiline Emmanuel, aliyepokea mafao ya uzazi, aliipongeza NSSF kwa huduma nzuri alizopata na kusema amefurahia kuwa na mfuko huu unaowajali wanachama wake.

Lightness Emmanuel Munga pia alieleza jinsi NSSF ilivyomsaidia kwa malipo ya wake upo wake wa matibabu baada ya kupata tatizo la mgongo na kuenda India kwa matibabu zaidi, na sasa anaendelea kupata huduma kupitia mfuko huo.

Share:

Sunday, 5 October 2025

MADIWANI SONGEA MJINI WAONESHA UMOJA,KAMPENI ZA CCM ZAZIDI KUSHIKA KASI MSHANGANO

Mgombea nafasi ya Udiwani kata ya Mshangano Benson Sovela akiwa anawasili eneo la uzinduzi wa kampeni katika kijiji cha Chandarua jimbo la Songea mjini 

Na Regina Ndumbaro Mshangano-Songea 

Katika harakati za uzinduzi wa kampeni za udiwani zinazoendelea katika kata mbalimbali za Jimbo la Songea Mjini, madiwani kutoka kata tofauti wameendelea kuonesha mshikamano mkubwa kwa kuungana kumuunga mkono mwenzao Benson Sovela, mgombea wa nafasi ya udiwani Kata ya Mshangano. 

Uzinduzi huo umefanyika leo Oktoba 5, 2025 katika kijiji cha Chandarua na umehudhuriwa na wananchi wengi pamoja na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Mgeni rasmi katika uzinduzi huo ni  Katibu wa CCM Wilaya ya Songea Mjini, James Daniel Mgego, ambaye amemkabidhi rasmi Benson Sovela kitabu cha Ilani ya CCM kama ishara ya kuanza rasmi kampeni. 

Mgego ametumia fursa hiyo kusisitiza umuhimu wa wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba, akieleza kuwa amani na mshikamano ni nguzo kuu za maendeleo nchini. 

Aidha, ameonya dhidi ya propaganda za uchochezi zinazosambazwa mitandaoni na kuhimiza wazazi na wazee kuwahamasisha vijana kushiriki kikamilifu katika uchaguzi.

Katika hotuba yake, Benson Sovela amewaomba wananchi wa Kata ya Mshangano kumpa ridhaa ya kuwa diwani wao kupitia sanduku la kura.

 Ameahidi kuwa kiongozi wa watu wote bila kujali itikadi au tofauti zozote, huku akisisitiza kuwa maendeleo hayana chama na kwamba kazi nzuri ya CCM inapaswa kuungwa mkono. 

Ametaja mafanikio yaliyopatikana kupitia serikali ya CCM, hasa katika sekta za elimu na afya, kuwa ni ushahidi tosha wa dhamira ya kweli ya kuleta maendeleo.

Benson Sovela pia ameahidi kushughulikia changamoto zinazowakabili wananchi wa Mshangano, ikiwemo uboreshaji wa miundombinu ya barabara hasa barabara ya Namanyigu–Mshangano, pamoja na kuhakikisha upatikanaji wa maji safi na salama katika maeneo yenye uhaba wa huduma hiyo. 

Amesema kuwa kupitia ilani ya CCM, miradi hiyo yote itatekelezwa kwa ufanisi iwapo atapewa nafasi ya kuwatumikia.

Uzinduzi huo umeonyesha si tu nguvu ya CCM katika Jimbo la Songea Mjini, bali pia mshikamano na umoja wa madiwani katika kuhakikisha kuwa kila kata inapata kiongozi makini na mwenye maono ya maendeleo. 

Wananchi wamehimizwa kuendelea kudumisha amani na mshikamano kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho


Share:

DK. SAMIA AENDELEA KUAHIDI UJENZI WA BARABARA ZA LAMI, KUONGEZA IDADI YA WATALII NA KUTATUA KERO YA WANYAMA WAKALI MANYARA


Na Jaliwason Jasson, BABATI 

MGOMBEA urais wa Chama cha Mapinduzi(CCM) Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ameahidi kujenga barabara kwa kiwango cha lami zilizoombwa na wagombea ubunge wa majimbo wa mkoa wa Manyara.

Dk. Samia alisema hayo leo Oktoba 4 wakati akiomba ridhaa ya kuchaguliwa tena ambapo alisema  wataendelea kujenga barabara za lami kwa kiwango cha lami ili kuunganisha mikoa.

Alizitaja barabara ambazo zitajengwa kwa kiwango cha lami kuwa ni Simanjiro mpaka Kongwa, Garbab mpaka Mbulu, Mogitu mpaka Haydom na barabara ya Nangwa/Gisamgalang mpaka Kongwa.
Dk. Samia alieleza kuwa wakipewa ridhaa  wataendelea kufungua barabara za vijijini ili kurahisisha usafirishaji wa mazao.

Katika hatua nyingine aliahidi kuongeza idadi ya watalii wa ndani na wa nje kutoka watalii milioni  5.3 miaka mitano iliyopita hadi kufikia watalii  zaidi ya milioni nane.

Vile vile aliahidi kuondoa tatizo la wanyama wakali linalosumbua wananchi wanaoishi vijiji vilivyopo jirani na Hifadhi za Taifa.

"Hatua tutakazochukua ni kujenga vituo vya kudhibiti wanyama wakali na tutachukua vijana wa vijijini wasaidiane na maafisa wa TAWA na TAWIRI,"alisema Dk. Samia.
 
Aliwaomba wananchi kuwa wavumilivu wakati serikali inajipanga kuchukua hatua.

Awali  wagombea ubunge  wa Kiteto Edward Ole Lekaita, James Ole Millya wa Simanjiro, Dk. Emmanuel Nuwas wa Mbulu vijijini, Zacharia Isaay wa Mbulu Mjini na Emmanuel Khambay wa Babati Mjini waliomba kujengewa barabara kwa kiwango cha lami huku mgombea wa ubunge wa Jimbo la Babati vijijini  Daniel Sillo akiomba vijiji 10 vilivyopo jirani na Hifadhi za Taifa ambavyo vinasumbuliwa na wanyama wakali akiomba kutatuliwa kwa changamoto hiyo.



Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger