Saturday, 4 October 2025

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI OKTOBA 4,2025


Magazeti


Share:

Friday, 3 October 2025

UTOAJI WA MIKOPO KUPITIA SACCOS WAPAA KWA TRILIONI 1.20



Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Bw. Elijah Mwandumbya,akizindua Taarifa ya Utendaji wa SACCOS kwa mwaka 2024 uliofanyika jijini Arusha.

Na.Mwandishi Wetu.

Serikali imesema itaendelea kuimarisha na kusimamia Vyama vya Ushirika wa Akiba na Mikopo (SACCOS) ili viwe chachu ya kasi ya maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi.


Kauli hiyo imetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Bw. Elijah Mwandumbya, wakati wa uzinduzi wa Taarifa ya Utendaji wa SACCOS kwa mwaka 2024 uliofanyika jijini Arusha.



Bw. Mwandumbya amesema wanachama wanapopata huduma za mikopo, hususan katika sekta binafsi, na kuzitumia kwenye biashara pamoja na shughuli za kiuchumi, huchangia kwa kiasi kikubwa katika ukuaji wa pato la taifa.

Akiwasilisha taarifa hiyo, Mrajis wa Vyama vya Ushirika, Dkt. Benson Ndiege, amesema kuwa ripoti inaonesha ukuaji wa Sekta ya Ushirika wa Akiba na Mikopo nchini.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, mali za SACCOS zimeongezeka kutoka Shilingi trilioni 1.32 mwaka 2023 hadi trilioni 1.46 mwaka 2024. Aidha, utoaji wa mikopo umeongezeka kutoka Shilingi trilioni 1.1 mwaka 2023 hadi kufikia trilioni 1.20 mwaka 2024.

Uzinduzi huo ulihudhuriwa na wawakilishi wa taasisi mbalimbali zikiwemo Wizara ya Kilimo, Benki Kuu ya Tanzania (BoT), SCCULT, Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU), Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania (TFC), COASCO, DSIK pamoja na viongozi wa SACCOS husika.
Share:

SERIKALI INAENDELEA KUIMARISHA MIUNDOMBINU YA UFUNDISHAJI NA UJIFUNZAJI KUWEZESHA WALIMU KUTOA ELIMU BORA




Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, amesema kuwa chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Serikali imefanya kazi kubwa ya kuboresha mazingira ya walimu, ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya shule ambayo imeongeza ufanisi wa ufundishaji na ujifunzaji.

Akizungumza katika Maadhimisho ya Siku ya Mwalimu Duniani Oktoba 03, 2025 Wilaya ya Bukombe, Mkoani Geita, Prof. Nombo ameeleza kuwa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, pamoja na majukumu ya kutunga na kusimamia utekelezaji wa sera ya elimu, inasimamia pia maendeleo ya elimu msingi, mafunzo ya ualimu tarajali, na mafunzo ya walimu kazini jambo linaloonesha uzito wa nafasi ya walimu katika nyanja zote za elimu.

Prof. Nombo amesisitiza kuwa juhudi hizo zimewapa walimu uwezo wa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi, na kuongeza umahiri katika kufundisha na kujifunza.

Aidha, ameongeza kuwa Wizara kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais - TAMISEMI pamoja na wadau mbalimbali, imeandaa miongozo ya mafunzo endelevu ya walimu kazini (MEWAKA), inayotekelezwa katika shule na vituo vya walimu ili kuwawezesha walimu kujiendeleza kitaaluma, kuimarisha mbinu za ufundishaji, na kuinua viwango vya ufaulu wa wanafunzi.

Prof. Nombo amebainisha kuwa Mpango wa MEWAKA umetambuliwa na Mkurugenzi wa Elimu wa Benki ya Dunia kama mfano bora wa kutambua na kuthamini juhudi za walimu ambapo kupitia mpango huo, walimu wamepata mafunzo katika maeneo ya utekelezaji wa mitaala, ufundishaji wa masomo ya sayansi, hisabati, TEHAMA, tathmini, ushauri na unasihi, usawa wa kijinsia, ujumuishi, na utunzaji wa mazingira.

Akizungumzia maslahi ya walimu, Prof. Nombo amesema kuwa kutokana na Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014/2023, Wizara imeandaa mkakati wa kuboresha mazingira ya kazi na maslahi ya walimu katika ngazi zote za elimu, na Serikali inaendelea kusimamia utekelezaji ili kuwahimiza walimu kuendelea kutoa mchango katika sekta ya elimu.

Katibu Mkuu huyo alihitimisha kwa kusema kuwa kwa kushirikiana na wadau kama Mtandao wa Elimu Tanzania (TEN/MET), Wizara imeanzisha programu ya Leaders in Teaching, inayolenga kuimarisha mbinu za ufundishaji, kutoa mafunzo ya ujasiriamali kwa walimu, na kuwatia motisha ili kuboresha elimu nchini.
Share:

Thursday, 2 October 2025

SportPesa Tanzania’s aviator and Spin the Wheel are turning small stakes into big winnings

 SportPesa Tanzania’s Aviator and Spin the Wheel are revolutionizing digital entertainment, transforming small stakes into big winnings. Every day, thousands of Tanzanians log in to SportPesa Casino seeking fast, fair, and thrilling experiences—and they’re finding it in these two electrifying games. From Mwanza to Dar es Salaam, Arusha to Morogoro, Aviator and Spin the Wheel are turning ordinary moments into unforgettable wins, sparking excitement and conversations across communities nationwide.

SportPesa Tanzania’s Aviator and Spin the Wheel are built on three things players value most—speed, simplicity, and fairness. With just a small stake, these games deliver the thrill of control and the chance for big wins. Aviator tests timing and discipline as the multiplier climbs, while Spin the Wheel offers instant results with every turn. Together, they are transforming everyday play into a wave of excitement from Dar es Salaam to Arusha, Mwanza to Morogoro—making SportPesa Casino the home of Tanzania’s most electrifying entertainment.

Why Tanzanians can’t stop playing Aviator and Spin the Wheel

These aren’t complicated casino games. They’re fast, raw, and built for Tanzania’s digital generation.

  • Adrenaline on demand – In Aviator, your cash-out timing decides everything.
  • Suspense that hooks – Spin the Wheel can double, triple, or end in “Game Over.” Every spin is a gamble with destiny.
  • Built for mobile life – Easy to play on smartphones, feature phones, and the SportPesa app.
  • Social buzz everywhere – Wins and near-misses spread instantly on WhatsApp groups, TikTok videos, and Twitter timelines.

This is entertainment designed for today’s culture — short, intense, and shareable.

More than play — a new digital thrill

“Every night my friends and I play Aviator,” said Aisha K. from Dodoma. “One of us always cashes out too early and gets roasted in the group chat. Spin the Wheel is the same — we post our results, celebrate, and keep spinning. It’s not just a game anymore. It’s part of our night.”

From student hostels in Dar to late-night gatherings in Arusha, players are making Aviator and Spin the Wheel a shared experience. Through SportPesa Tanzania’s casino games, they have become more than entertainment — a digital thrill connecting friends and communities across the country

How the games work

Aviator

  1. Place your stake.
  2. Watch the plane climb higher and higher.
  3. Cash out before the crash.

Spin the Wheel

  1. Place your stake.
  2. Spin for multipliers or risk “Game Over.”
  3. Celebrate every win — or chase the next spin.

It’s that simple. Fast play. No delays. No complications.

SportPesa’s commentary

“At SportPesa Tanzania, our goal is to create thrills that fit into everyday life,” said Jason Ndambala. “Aviator and Spin the Wheel give players instant excitement with clear rules, fair play, and the chance to share unforgettable moments with friends. It’s about fun, timing, and community — all in one.”

Access for everyone

  • Easy access anytime – Just like SportPesa’s sports games, Aviator and Spin the Wheel are designed to be simple and convenient for players across Tanzania.
  • Seamless experience – With reliable play through the SportPesa app and website, fans from Dar to Dodoma, Moshi to Mwanza can enjoy smooth gameplay wherever they are.

Don’t just watch the stories — become one. Log in to SportPesa Tanzania Casino today, play casino games and stand a chance to win millions.

Your next story could be just one spin away.

New stories emerge every single day: a student hitting x20 on Aviator, a boda-boda rider in Arusha doubling his stake, a group of friends in Morogoro sharing spins on WhatsApp. This is more than entertainment — it’s a movement of players who want thrill, suspense, and the rush of timing it just right.

Share:

TANZANIA , KENYA ZAKAMILISHA HATUA MPYA KUONDOA VIKWAZO VYA BIASHARA



Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara nchini Tanzania Dkt. Hashil Abdallah na Katibu Mkuu Idara ya Biashara, Wizara ya Uwekezaji, Biashara na Viwanda wa Jamhuri ya Kenya wakionyesha hati ya makubaliano wakati wa Mkutano wa Tisa (9) wa Kamati ya Pamoja ya Biashara baina ya Tanzania na Kenya unaofanyika katika Hoteli ya Johari Rotana Dar es Salaam nchini Tanzania Oktoba 01, 2025.

......

Tanzania na Kenya zimeondoa vikwazo vya biashara visivyo vya kiushuru vinne (4) kati ya 14 vilivyojadiliwa katika Mkutano wa Tisa (9) wa Kamati ya Pamoja ya Biashara baina ya nchi hizo ambapo hatua hii inatimiza vikwazo 58 vilivyotatuliwa kati ya 68 vilivyokuwepo huku vikwazo 10 vilivyobakia kutatuliwa ifikapo Machi 31, 2026

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Dkt. Hashil Abdallah Oktoba 1, 2025 wakati wa Mkutano huo uliofanyika Dar es Salaam ambapo nchi hizo mbili zilijadili vikwazo hivyo na kutia saini makubaliano hayo ili kutumiza maelekezo ya makubaliano yaliyowekwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan na Rais wa Kenya, Mhe Dkt. William Ruto, wakati wa Ziara nchini Tanzania Oktoba 9–10, 2022 kwa lengo la kuimarisha uhusiano wa Biashara’s baina ya Nchi hizo.

Aidha Dkt Abdallah amebainisha vikwazo vilivyoondolewa vikijumuisha kuondoa kodi ya zuio kwa bia za TBL kwenda Kenya, Mihuri ya ushuru (Tax Stamps Pamoja na Ada na Tarantino usafirishaji wa Bidhaa za mifugo kutoka Kenya kutekelezwa kwa kufuata maamuzi ya Baraza la Kisekta la Fedha na Uchumi la Jumuiya yaAfrika Mashariki (EAC) na kuondoa Bima ya COMESA kwa kuwa haihusiani na Tanzania

Vilevile, amesema Nchi hizo zimeahidi kushirikiana katika kuhakikisha biashara kati ya Tanzania na Kenya inafanyika kwa haki, kwa kuzingatia mikataba ya EAC na kuwasilisha masuala mapya kupitia njianza idiomatic ndani ya Mwezi mmoja baada ya Mkutano huo.

“Tumekubaliana kwamba ndani ya miezi sita, ifikapo Machi 31, vikwazo vyote vitakuwa vimekwisha na suluhu zao zitatolewa kikamilifu. Kila sekta na idara ina jukumu la kukutana na upande wa pili, kujadiliana kwa pamoja na kutafuta njia za kudumu za kuyatatua. Wataalamu pia wanashirikiana kwa karibu kusaidia wafanyabiashara kuhakikisha biashara inafanyika kwa urahisi na ufanisi.

Kwa upande wa Kenya, Katibu Mkuu wa Biashara katika Wizara ya Uwekezaji, Biashara na Viwanda, Bi Regina Ambam, alieleza kuwa makubaliano hayo ni hatua muhimu katika kurahisisha mifumo na kuweka mazingira bora kwa wafanyabiashara wa Afrika Mashariki na ustawi wa wananchi kwa ujumla huku

Aidha, alisisitiza umuhimu wa kujiandaa kwa biashara ya kidijitali na ni hatua ya kihistoria katika kuimarisha uhusiano wa pande mbili na kuchochea ujumuishaji wa kikanda na kuiweka Afrika Mashariki katika nafasi ya ushindani duniani,”

Naye Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wa Kenya Bi Carolyne Karugu amesema Kamati Hiyo ya Pamoja imefanikiwa kuondoa vikwazo hivyo vya biashara visivyo vya kiushuru kwa asilimia 78. yanatokana na makubaliano yaliyowekwa wakati wa ziara rasmi ya Rais wa Kenya, Dkt. William Ruto, nchini Tanzania Oktoba 9–10, 2022 Kwa ajili ya ustawi wa Jumuiya nzima ya Afrika Mashariki.” hatua inayoimarisha uhusiano ya nchi mbili na kuleta athari chanya za kiuchumi.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara nchini Tanzania Dkt. Hashil Abdallah na Katibu Mkuu Idara ya Biashara, Wizara ya Uwekezaji, Biashara na Viwanda wa Jamhuri ya Kenya wakisaini hati ya makubaliano wakati wa Mkutano wa Tisa (9) wa Kamati ya Pamoja ya Biashara baina ya Tanzania na Kenya unaofanyika katika Hoteli ya Johari Rotana Dar es Salaam nchini Tanzania Oktoba 01, 2025.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara nchini Tanzania Dkt. Hashil Abdallah na Katibu Mkuu Idara ya Biashara, Wizara ya Uwekezaji, Biashara na Viwanda wa Jamhuri ya Kenya wakibadilishana hati ya makubaliano wakati wa Mkutano wa Tisa (9) wa Kamati ya Pamoja ya Biashara baina ya Tanzania na Kenya unaofanyika katika Hoteli ya Johari Rotana Dar es Salaam nchini Tanzania Oktoba 01, 2025.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara nchini Tanzania Dkt. Hashil Abdallah na Katibu Mkuu Idara ya Biashara, Wizara ya Uwekezaji, Biashara na Viwanda wa Jamhuri ya Kenya wakionyesha hati ya makubaliano wakati wa Mkutano wa Tisa (9) wa Kamati ya Pamoja ya Biashara baina ya Tanzania na Kenya unaofanyika katika Hoteli ya Johari Rotana Dar es Salaam nchini Tanzania Oktoba 01, 2025.
Share:

DKT. ABBASI AKABIDHI VIFAA VYA KUKABILIANA NA WANYAMA WAKALI NA WAHARIBIFU



Na Mwandishi Wetu- Goha,Korogwe

Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi amekabidhi mabomu baridi mia nne (400), pikipiki mbili na ndegenyuki (drone) moja kwa kituo cha askari uhifadhi Goha wilayani Korogwe mkoani Tanga kwa ajili ya kukabiliana na changamoto za wanyamapori wakali na waharibifu hususan tembo.

Akikabidhi vifaa hivyo leo Septemba 28, 2025 Dkt. Abbasi amesema hiyo ni hatua hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa Mkakati wa Kitaifa wa kudhibiti mwingiliano wa binadamu na wanyamapori ili kupunguza madhara kwa jamii.

“Mnafahamu nchi nzima kuna maeneo mengi yenye changamoto za muingiliano wa wanyama wakali na waharibifu ambao wanaharibu mazao, mimea mingine na wanashambulia binadamu hivyo kama Wizara tuna mkakati wa kitaifa wa kukabiliana na changamoto hiyo” amesisitiza Dkt. Abbasi.

Amesema Serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali za kukabiliana na changamoto hiyo kisayansi na kioparesheni ikiwa ni pamoja na kuchimba mabwawa ikiwepo ya Wilaya ya Same, kutumia helikopta kuwarudisha wanyama hifadhini na kutumia ndegenyuki ambazo zilishakabidhiwa katika kituo hicho na kote nchini.

“Tunaamini vifaa hivi vitaongeza ufanisi wa kuwafukuza hasa wanyama wakali kama tembo ili wananchi wetu wazidi kuwa salama na waweze kufanya shughuli zao kwa amani” amefafanua Dkt. Abbasi.

Dkt. Abbasi amewaomba Wananchi kuzingatia maelekezo wanayopewa wakati wa kukabiliana na changamoto hiyo na pia kutoa taarifa kwa askari kupitia namba maalum za askari inayotumika katika wilaya zote ili kuepusha taharuki.

Naye, Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi, Bw. Emmanuel Moirana ameishukuru Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kukabidhi vifaa hivyo na kusisitiza kuwa vitaenda kutatua changamoto ya Wanyama wakali na waharibifu kwa kuwa ni kubwa katika eneo hilo.

Ameongeza kuwa lengo ni kuboresha ufukuzaji wa tembo, kuongeza upataji wa taarifa sahihi tembo walipo na kubaini chanzo cha tatizo hivyo amewaomba wananchi kutoa ushirikiano wa kutosha ili kupunguza madhara ya tembo.

Makabidhiano hayo ni muendelezo wa utekelezaji wa mkakati wa kukabiliana na wanyamapori wakali na waharibifu nchini.
Share:

RAIS SAMIA ANATHAMINI MCHANGO WA WAONGOZA WATALII NCHINI


Na Mwandishi Wetu- Karatu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anathamini na kujua kazi na mchango wa waongoza watalii nchini Tanzania.

Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi ameyasema hayo katika tukio la Fainali ya Safari Field Challenge Toleo la 10, likiambatana na maadhimisho ya Miaka 10 ya mashindano haya, sambamba na Maadhimisho ya Siku ya Utalii Duniani lililofanyika kwenye ukumbi wa Oasis Wilayani Karatu, Arusha usiku wa Septemba 27,2025.

“Rais Samia anafahamu tunafanya tuzo hapa leo na ameangalia challenge zote mlizofanya na amekubali na akasema anawapenda sana na anawaelewa sana na ndio maana alifanya filamu ya Tanzania the Royal Tour, alikwenda Pemba akavua Samaki” amesema Dkt. Abbasi.

Aidha, Dkt. Abbasi ametumia fursa hiyo kuwahimiza waongoza watalii kushiriki katika tuzo za utalii na uhifadhi zinazotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba 2025.

“Tumezindua tuzo za utalii na uhifadhi, ni tuzo za ushindani watu watashindanishwa kwenye kategoria mbalimbali hivyo mshiriki katika kupambania kategoria mbalimbali ikiwemo ya safari guide, mountain guide n.k” amesema Dkt. Abbasi.

Amesema kuanzi tarehe 10 mwezi Oktoba tuzo zitafunguliwa na zitakuwa na kategoria saba zenye tuzo zaidi ya 56, na tarehe 19 itakuwa ni usiku wa tuzo.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger