Thursday, 15 May 2025

WANANCHI WA MSISIMA NA MNALAWI WAMEIPONGEZA SERIKALI KWA MRADI WA MAJI SAFI NA SALAMA

Tanki la Maji katika kijiji cha Msisima na Mnalawi halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo Mkoani Ruvuma uliopo chini ya Mradi wa maji safi na salama vijijini (RUWASA)
Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru Ismail Ussi akizungumza na wananchi kabla ya kuweka jiwe la msingi katika mradi huo wa maji kijiji cha Msisima na Mnalawi Wilayani Namtumbo
Na Regina Ndumbaro Namtumbo-Ruvuma




Wananchi wa kata ya Msisima na Mnalawi, Wilaya ya Namtumbo, wameeleza furaha yao kubwa  kuuona mwenge wa Uhuru kwa mara ya kwanza tangu Tanzania ipate uhuru mwaka 1961,baada ya mwenge wa uhuru kufika kijijini kwao. 

Wakiwa katika uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama chini ya Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA), wananchi hao wametoa shukrani zao kwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwaletea maendeleo na kuonesha dhamira ya kweli ya kuwahudumia Watanzania wote bila ubaguzi.

Yasin Dauda na Zainabu Mjomba, wakazi wa vijiji hivyo, wameeleza kuwa mradi huo wa maji utasaidia kuondoa adha waliyozoea ya kutumia maji yasiyo salama, kupunguza umbali wa kutafuta maji na kuimarisha afya za familia zao. 

Wamesema kuwa huduma hii muhimu ni ya kihistoria na kielelezo cha utendaji wa Serikali ya Awamu ya Sita. 

Kwa heshima na kuthamini mchango wa Rais Samia, wameahidi kumpa kura zote katika uchaguzi mkuu ujao mwezi Oktoba, wamesisitiza kuwa hawatamwangusha kiongozi huyo aliyeonesha kuwajali kwa vitendo.

Kwa upande wake, Meneja wa RUWASA Wilaya ya Namtumbo, Ndugu David Mkondya, Ameeleza kuwa utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 60. 

Mradi huo una thamani ya shilingi bilioni 1.1, na unatarajiwa kunufaisha wakazi 481 kutoka vijiji viwili kwa kutumia chanzo cha maji kutoka Mto Msokambale. 

Mradi unahusisha ujenzi wa tanki lenye uwezo wa kuhifadhi lita 200,000, mtandao wa mabomba wenye urefu wa kilomita saba, huku chanzo hicho kikiwa na uwezo wa kuzalisha zaidi ya lita milioni nne kwa siku ikilinganishwa na mahitaji ya lita 242,000 kwa siku. 

Mradi huo wa maji ulianza tarehe 17 Oktoba 2023 na unatarajiwa kukamilika tarehe 13 Juni 2025.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ismail Ussi, amesisitiza kuwa mwenge wa uhuru umebeba ujumbe wa matumaini, amani, upendo na mshikamano kwa Watanzania. 

Ameeleza kuwa asilimia mia moja ya wakazi wa maeneo hayo watanufaika moja kwa moja na mradi huo wa maji. 

Pia amewahimiza wananchi kudumisha mshikamano, umoja na amani ili mradi huo uwe endelevu na kuleta mafanikio ya muda mrefu kwa jamii.

Kwa ujumla, ujio wa mwenge wa uhuru katika kata ya Msisima na Mnalawi umetajwa kuwa chachu ya maendeleo na ukombozi wa kweli kwa wananchi waliokuwa wakikabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa maji kwa muda mrefu. 

Serikali imeendelea kuonesha kwa vitendo kuwa dhamira ya kuwaletea Watanzania maendeleo si ya maneno bali ni ya vitendo, jambo ambalo limepongezwa kwa nguvu na wananchi wa maeneo hayo.

Share:

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE KITAIFA AHIMIZA ELIMU KWA WATOTO


Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Ismail Ussi akizindua jiwe la msingi katika shule ya msingi Mtakanini Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
Shule ya msingi Mtakanini iliyozinduliwa leo na kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Ismail Ussi Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo
Mwenge wa uhuru ulipowasili katika halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo Mkoani Ruvuma ukitoka katika Manispaa ya Songea
Mkuu wa Wilaya ya Songea Kapenjama Ndile akimkabidhi Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo Ngolo Malenya katika makabidhiano yaliyofanyika katika kijiji cha Lumecha Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo

Na Regina Ndumbaro Namtumbo-Ruvuma. 

Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa, Ndugu Ismail Ussi, ametoa wito kwa wazazi na jamii kuhakikisha watoto wote wanapelekwa shule ili wapate elimu bora. 

Akizungumza wakati wa uzinduzi kuweka jiwe la msingi katika Shule ya Msingi Mtakanini iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo, Ussi ameeleza kuwa shule hiyo imeboreshwa na sasa ina miundombinu ya kisasa yenye ubora wa hali ya juu.

Shule ya Msingi Mtakanini ambayo imezinduliwa rasmi leo, ina jumla ya madarasa manne na matundu ya choo sita. 

Uboreshaji huo ni sehemu ya juhudi za Serikali za kuhakikisha mazingira bora ya kujifunzia kwa wanafunzi. 

Kiongozi huyo amesisitiza kuwa jitihada hizi zinaonesha dhamira ya dhati ya Mheshimiwa Rais katika kuhakikisha kila mtoto nchini anapata elimu bora.

Katika hatua nyingine, makabidhiano ya mbio za mwenge yamefanyika leo katika kijiji cha Lumecha, Kata ya Msindo, katika Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo, mkoani Ruvuma.

 Makabidhiano hayo yamefanyika kati ya Mkuu wa Wilaya ya Songea, Kapenjama Ndile, na Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo, Ngolo Malenya.

Mwenge wa Uhuru umekimbizwa kwa jumla ya kilomita 147 katika Wilaya ya Namtumbo, ukitembelea na kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo. 

Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo, Ngolo Malenya, amesema kuwa katika kipindi cha miaka minne ya awamu ya sita chini ya Daktari Samia Suluhu Hassan walipatiwa kiasi cha fedha wilayni humo  katika  utekelezaji wa miradi kiasi cha shilingi bilioni 89 .

Kupitia tukio hili, viongozi hao wamesisitiza umuhimu wa ushirikiano baina ya serikali na wananchi katika kuendeleza maendeleo ya elimu na miundombinu kwa ujumla. 

Mwenge wa Uhuru umeendelea kuwa chombo muhimu katika kuhamasisha maendeleo na uzalendo nchini.

Share:

BENKI YA CRDB YAWAKARIBISHA WANAHISA KWENYE MKUTANO MKUU WA 30

 

Arusha 14 Mei 2025 - Benki ya CRDB imewataka wanahisa wake kujitokeza kwa wingi kushiriki katika Mkutano Mkuu wa 30 wa Wanahisa, unaotarajiwa kufanyika Jumamosi, tarehe 17 Mei 2025, katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 30 ya mafanikio tangu kuanzishwa kwa benki hiyo.

Taarifa hiyo imetolewa leo katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika kwenye hoteli ya Gran Meliá, jijini Arusha, ambapo Benki ya CRDB pia ilizindua Ripoti yake ya Mwaka 2024, inayoonyesha maendeleo makubwa ya kifedha, kiutendaji na kijamii yaliyopatikana katika kipindi hicho.
Akizungumza katika mkutano huo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Dkt. Ally Laay, amesema kuwa Mkutano Mkuu wa mwaka huu utakuwa wa kipekee kwani utatanguliwa na semina maalum kwa wanahisa na umma, itakayofanyika Ijumaa, tarehe 16 Mei 2025, katika ukumbi wa Simba, AICC. “Semina hii ya kihistoria itakuwa chini ya kaulimbiu yetu ya mwaka huu: ‘Miaka 30 ya Ukuaji wa Pamoja,’ na itafunguliwa rasmi na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Philip Isdor Mpango. Ni fursa muhimu ya kutafakari mafanikio yetu ya pamoja, changamoto tulizozishinda, na mwelekeo wetu wa miaka ijayo,” amesema Dkt. Laay.

Ajenda mbalimbali zitajadiliwa katika Mkutano Mkuu wa 30 wa Wanahisa wa Benki ya CRDB ni pamoja na uchaguzi wa wajumbe wa bodi, kuteua wakaguzi wa hesabu, kujadili mapendekezo ya maboresho ya Katiba ya Benki, kujadili na kupokea Taarifa ya Bodi ya Wakurugenzi, na Taarifa ya Hesabu zilizokaguliwa, pamoja na gawio kwa mwaka 2024 ambapo pendekezo la gawio la Sh 65 kwa hisa litawasilishwa sawa.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela amesema maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Wanahisa yamekamilika kwa asilimia 100. Nsekela amesema mkutano huo utafanyika kwa njia mseto “Hybrid Meeting” ili kutoa fursa kwa wanahisa wengi zaidi kushiriki moja kwa moja na kwa njia ya kidijitali. “Tumeweka muongozo wa jinsi ya kushiriki mkutano mkuu kwa njia ya mtandao kupitia tovuti yetu ya www.crdbbank.co.tz, mitandao yetu ya kijamii, lakini pia maelekezo yametumwa kwa ujumbe mfupi kwa Wanahisa,” amesema Nsekela huku akiwahakikishia kuwa Benki hiyo vizuri katika kuhakikisha wanashiriki bila chanagamoto yoyote.
Nsekela amewahamasisha wanahisa kujitokeza kwa wingi kushiriki katika Mkutano Mkuu huo wa kihistoria, akisisitiza kuwa uwepo wao ni muhimu kwa ajili ya kushuhudia mafanikio makubwa yaliyopatikana katika miaka 30. “Tumejenga taasisi imara inayotoa huduma bora, tumeongeza thamani kwa wanahisa, na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa letu. Hii ni fursa adhimu kwa kila mwanahisa kujivunia sehemu yake katika mafanikio haya na kushiriki kuamua mustakabali wa benki yetu katika miaka ijayo,” amesisistiza.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI MEI 15,2025





Magazeti ya leo



Share:

Tuesday, 13 May 2025

AENDEKEZA ANASA CHUO KIKUU NA KUSAHAU MASOMO, MZAZI AFUNGUKA


Mtoto wangu alijiunga na chuo miezi michache iliyopita na kama unavyojua ni furaha ya kila mzazi kuona mtoto wake akifaulu na kupanda ngazi za juu kimasomo, mafanikio yake yamekuwa ya kusisimua sana kwangu.

Hata hivyo, miezi mitatu baada ya kujiunga na chuo kikuu, nilianza kupigiwa simu na marafiki zake kwamba alikuwa anafanya umalaya na kutumia dawa za kulevya na hata kujihusisha na magenge hatari.

Nilidhani ni uvumi lakini baada ya kupigiwa simu uongozi wa chuo kuwa mwanangu amekuwa mlevi wa kupindukia, nilijua hali ni mbaya huko tena sana.
Share:

NAIBU WAZIRI UMMY AZINDUA MIRADI YA KIUCHUMI YA WENYE ULEMAVU



Na Mwandishi wetu- Dar es salaam

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga amezindua miradi ya kiuchumi ambayo iko chini ya Shirika lisilo la Kiserikali la Strategic Alternative Learning Technique (SALT), inayohudumiwa na vijana wenye changamoto za ufahamu.

Mhe. Nderiananga alifanya uzinduzi huo Jijini Dar es Salaam kwa miradi ambayo ni pamoja na Salt Special Supermarket, Mgahawa na Bakery itakayohudumiwa na vijana wenye ulemavu wa ufahamu huku akisema jumla ya vijana na Watoto 83 wamepatiwa mafunzo ya namna ya kutoa huduma kwa wananchi hatua itakayowasaidia kujipatia kipato chao na kuchangia maendeleo ya Taifa.

Aidha, Mhe. Nderiananga aliipongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutenga fedha kwa ajili ya kuwawezesha watu wenye ulemavu katika maeneo mbalimbali ikiwemo elimu, kujiwezesha kiuchumi na kusaidia mashirika yanayoshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu.

“Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Serikali yake ya Awamu ya Sita imeendelea kutoa fedha kwa watu wenye ulemavu ili wafanye kazi zao vizuri. Nimefurahi kuona Shirika hili la SALT linafanya kazi zake kwa ubunifu kwa kuwafundisha stadi za kazi na ubunifu wa mavazi,” alisema Mhe. Nderiananga.

Vilevile, amefafanua kwamba ikiwa kila mmoja atafanya kwa nafasi yake katika kuwawezesha watu wenye ulemavu itaongeza chachu kwao kujituma kufanya kazi kwani vipaji na uwezo wao utatambulika na kuungwa mkono hali itakayoongeza uzalishaji katika Nchi.

“Nitoe wito tuendelee kuliunga mkono Shirika hili na mengine yanayowasaidia watu wenye ulemavu wa aina zote kwani yanafanya kazi kubwa hivyo viongozi wetu wa Serikali za Mitaa tuyapokee mashirika haya na kuwapa ushirikiano kwa manufaa ya Taifa letu.

Aidha alibainisha kwamba watu wenye ulemavu wanahitaji fursa bila kunyanyapaliwa huku akiwataka wazazi na walezi kutosikiliza maneno ya kukatisha tamaa na badala yake wawaamini watoto wao kuwa wana uwezo wa kipekee.

Aliwahimiza wazazi na walezi wa watoto wenye ulemavu kutumia fursa za mafunzo yanayotolewa katika taasisi mbalimbali ili kuwajengea Watoto kujiamini kuwa wanaweza na wanamchango katika jamii.

“Baadhi ya mafunzo yanayotolewa na SALT ni pamoja na uokaji, mapishi, mitindo ya mavazi na wahudumu katika migahawa hatua inayowajengea ujuzi wa kujipatia kipato ili kuendesha maisha hayo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirika lisilo la Kiserikali la Strategic Alternative Learning Technique (SALT), Bi. Rebeca Lebi alieleza kuwa Shirika hilo lilianza mwaka 2019 kwa lengo la kuwasaidia watoto na vijana wenye changamoto za ufahamu ambazo ni Usonji (Autistic Spectrum Disoder), Down syndrome, Mtindio wa ubongo (Cerebral Palsy ), Ulemavu wa akili (Intellectual Impairment) , Kifafa kikali (Severe epilepsy) na changamoto zote zinazohusiana na ulemavu wa ubongo na ufahamu.

Awali akisoma risala Meneja wa Operesheni kutoka Shirika la SALT, Bi. Jasmine Omary Iddy alisema SALT, ilianzisha chuo cha ufundi na uzalishaji (Vocational training and production) ikiwa na malengo ya kumuandaa kijana mwenye changamoto za ulemavu wa ufahamu kuweza kuwa mzalishaji kupitia mpango wa Viwanda 10 ambavyo vitazalisha bidhaa tofauti, kama vile sabuni za kuogea, shampoo, mafuta ya kupaka, vitambaa vya batiki, mikate na ufugaji wa samaki, kuku pamoja na bustani za mbogamboga.

“Kituo hiki kilianzishwa kwa lengo la kuwawezesha vijana wenye changamoto za kiakili na ufahamu kupata stadi za kazi, stadi za maisha na mazingira salama ya kujifunza na kushiriki katika shughuli za kiuchumi. Lengo letu kuu ni kuwapatia fursa ya kujitegemea, kuongeza thamani katika maisha yao na kupunguza utegemezi kwa familia au jamii,” ameeleza Meneja huyo.



Share:

SERIKALI KUTEKELEZA MFUKO WA UBUNIFU WA SAMIA “SAMIA INNOVATION FUND” WENYE THAMANI YA BIL 2.3

Serikali inatarajia kuanza utekelezaji wa mfuko wa Ubunifu wa Samia “SAMIA Innovation Fund” wenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.3 utakaotoa mikopo nafuu kwa wabunifu kwa lengo la kuendeleza na kubiasharisha ubunifu pamoja na kutoa fursa za ajira kwa watanzania kupitia kazi za ubunifu.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof Adolf Mkenda (Mb) amebainisha hayo leo tarehe 12 Mei 2025 wakati akiwasilisha bungeni Jijini Dodoma Makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara hiyo.

Amesema kuwa lengo la mfuko huo itakuwa ni kuimarisha ubora wa kazi za watafiti na kukuza ushindani wa kitaaluma.

Pia amesema kuwa Serikali itaendelea kutoa tuzo yenye thamani ya Shilingi milioni 50 kwa utafiti utakaochapishwa katika majarida yenye hadhi ya juu kimataifa ili kuwahamasisha watafiti na wabunifu kuchapisha na kusambaza matokeo ya kazi zao na kuweza kutumika na wananchi.

Vilevile, Waziri Mkenda amesema kuwa ili kuendana na mabadiliko ya sayansi, teknolojia na ubunifu kikanda na kimataifa, Serikali itaendelea na mapitio ya Sera ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (1996) ili kuwa na sera inayoakisi hali halisi na mahitaji ya sasa katika Sayansi, Teknolojia na Ubunifu.

Waziri Mkenda amesema, serikali itafanya tathmini ya Sera ya Taifa ya Utafiti na Maendeleo 2010, Sera ya Taifa ya Bioteknolojia 2010 na Sera ya Taifa ya Teknolojia ya Nyuklia 2013 ili kubaini hali halisi ya utekelezaji wa sera hizo.

Wabunifu na kazi za ubunifu ni chachu katika kuzalisha teknolojia mpya, kutatua changamoto za kijamii na kuchangia katika maendeleo ya nchi.
Share:

Monday, 12 May 2025

SERIKALI INABORESHA MIUNDOMBINU YA UMEME KIBITI KUONDOA CHANGAMOTO YA UMEME- KAPINGA

 

Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga amesema Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) inatekeleza miradi mbalimbali ya matengenezo na ukarabati wa njia za kusafirisha na kusambaza umeme katika Wilaya ya Kibiti ili kuondokana na tatizo la kukatika kwa umeme kunakotokana na uchakavu wa miundombinu hiyo.

Mhe. Kapinga ameyasema hayo leo Mei 12, 2025 Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Kibiti, Mhe. Twaha Mpembenwe aliyetaka kufahamu mkakati wa Serikali kutatua tatizo la kukatika kwa umeme Jimbo la Kibiti. 

Ameitaja Mikakati hiyo ni kubadili nyanya za umeme kwa kuweka zenye uwezo mkubwa, kubadili nguzo za umeme na kuweka za zege, kubadili Pin insulators na kuweka mpya, na kufunga vidhibiti matatizo (fault auto recloser) kwenye line zenye urefu wa zaidi ya Kilomita 50.

Share:

PROF MKENDA ATINGA BUNGENI, LEO NI BAJETI YA HISTORIA

Waziri wa Elimu Mhe Prof Adolf Mkenda akiwasili bungeni leo tarehe 12 Mei 2025 kwa ajili ya kuwasilisha Makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa mwaka wa Fedha 2025/2026

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger