Monday, 12 May 2025

WACHIMBAJI GEITA WAMPONGEZA RAIS SAMIA KWA MAFANIKIO MAKUBWA YA SEKTA YA MADINI

▪️Wachimbaji Madini wapongeza upatikanaji wa Leseni na mazingira rafiki ya biashara

▪️Waziri Mavunde aainisha mafanikio 16 ya Rais Samia kwenye sekta ya Madini

▪️Aagiza uanzishwaji wa Soko la Dhahabu Katoro

▪️RC Shigela aja na mikakati mizito ya kupaisha sekta ya madini Geita


Katoro,Geita

Wachimbaji na Wafanyabiashara wa Madini wa Mkoa wa Geita wamempongeza Rais Dkt. Samia S. Hassan kwa mafanikio makubwa yaliyopatikana kupitia sekta ya madini katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wake.


Hayo yamesemwa Mei 11,2025 kwenye mkutano wa hadhara ulioandaliwa na wachimbaji hao katika eneo la mnada wa zamani Katoro,Geita kwa lengo la kumpongeza Rais Samia kwa mafanikio yaliyopatikana kupitia sekta ya madini.

Akitoa maelezo ya awali,Mwenyekiti wa Chama cha Wachimba Madini Mkoa wa Geita(GEREMA) Ndg. Titus Kabuo amesema dhumuni kubwa la kusanyiko hilo ni kumpongeza Mh. Rais Dkt. Samia S. Hassan kwa kuiboresha sekta ya madini na kuweka mazingira rafiki ya uchimbaji na ufanyaji biashara hali inayopelekea kukua kwa shughuli za uchimbaji na kuathiri chanya maendeleo ya wachimbaji na uchumi wa nchi.

Naye Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wachimba Madini Tanzania(FEMATA) Ndg. John Bina amesema katika kipindi cha miaka minne ya Rais Samia sekta ya madini imeshuhudia mabadilko makubwa hasa katika upatikanaji wa Leseni kwa wachimbaji na hatua iliyoanzwa na serikali ya kufanya utafiti wa kina ili kuwaongoza vyema wachimbaji madini nchini.

Akiwasilisha hotuba yake,Waziri wa Madini Mh. Anthony Mavunde ameyataja mafanikio 16 ya Rais Samia S. Hassan katika kuipaisha sekta ya madini kubwa ikiwa ni kuongezeka kwa mchango wa sekta ya madini kwenye pato la Taifa kufikia 10.1%,ununuzi wa Dhahabu kupitia Benki Kuu,Kuongezeka kwa makusanyo ya maduhuli kuelekea lengo la kukusanya Shilingi Trilioni moja na upatikanaji wa mitambo ya kuchoronga 15 kwa ajili yaa wachimbaji wadogo.

Aidha, Waziri Mavunde ametumia fursa hiyo kukipandisha hadhi kituo cha ununuzi wa dhahabu cha Katoro na kuwa soko kamili la Dhahabu la Katoro.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wabunge Joseph Msukuma na Tumaini Magesa wamempongeza Rais Samia kwa kuweka mazingira rafiki ya biashara ambayo yamesaidia kupatikana kwa maendeleo makubwa na kukuza uchumi wa watu wa Geita.

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mh. Martin R. Shigela amesema Mkoa wa Geita umejipanga kuchochea shughuli za madini kwa kuboresha mazingira ya uchimbaji ili kukuza uchumi wa wananchi wa mkoa wa Geita kupitia upatikanaji wa Leseni zaidi ya 5308 na mitambo ya Uchorongaji ambayo Mhe. Rais ameitoa kwa kwa wachimbaji wadogo.
Share:

Sunday, 11 May 2025

UNESCO - ALWALEED PHILANTHROPIES KICKS OFF ITS SECOND COHORT OF GRANTEES IN TANZANIA



Michel Toto

 By a correspondent in Dar es Salaam

UNESCO in collaboration with the Alwaleed Philanthropies has kicked off the second cohort of grantees, a move meant to support arts and culture education, capacity building, and sustainable community development.

UNESCO Head of Office Michel Toto made the revelations in Dar es Salaam recently during the Kick-Off Meeting for the Second Cohort of Grantees and Knowledge Sharing Session.

The move comes with testimonies indicating that the support to the first cohort grantees has helped to create a positive impact to communities where it was implemented.
Speaking during the session Rose Ngunangwa, Tanzania Media for Community Development (TAMCODE) Executive Director, a grantee from the first cohort thanked UNESCO and Alwaleed Philanthropies saying through the support, her organization in collaboration with community radios and digital platform journalists had been able to publicize the various economic opportunities in Katavi and Rukwa regions and to promote forest conservation, cultural tourism as well as use of clean energy.

“The support helped TAMCODE to also engage with local policy makers in Mpanda and Sumbawanga districts where we came with guidelines for the enactment of the by law on Intangible Cultural Heritage. We are grateful to district authorities, mayors and councilors in the two districts for their commitment to support us,” said Ngunangwa.

The UNESCO–Alwaleed Philanthropies Programme supports community-based development in Tanzania by enhancing the role of culture and arts through Technical and Vocational Education and Training (TVET).

The initiative contributes to unlocking the economic and social potential of cultural heritage and creative industries, with a strong emphasis on youth and women empowerment.

The hybrid session brought together grantees from the first and second cohort, officials from the ministries of culture in mainland and Zanzibar, development partners, as well as UNESCO staff members from Dar es Salaam & Paris.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI MEI 11,2025





magazeti

Share:

BREAKING NEWS: CHARLES HILARY AFARIKI DUNIA


TANZIA: Aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Mawasiliano Ikulu ya Zanzibar na Msemaji Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Charles Hilary, amefariki dunia alfajiri ya leo Mei 11, 2025.

Charles pia aliwahi mtumishi mwandamizi wa Azam Media Limited kati ya mwaka 2015 na 2023. Alihitimisha muda wake akiwa Mkuu wa Idara ya redio ya UFM, baada ya kuteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Mawasiliano Ikulu ya Zanzibar.
Share:

Saturday, 10 May 2025

NDUMBARO AHAMASISHA UUNGWAJI MKONO KWA SONGEA UNITED KABLA YA MECHI DHIDI YA COSMO

Na Regina Ndumbaro Songea-Ruvuma 

Waziri wa Katiba na Sheria ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini, Mheshimiwa Damas Ndumbaro, ametoa kauli kuhusu mchezo wa kesho Jumapili tarehe 11 Mei 2025 kati ya Songea United na Cosmo Politan kutoka Dar es Salaam. 

Waziri Ndumbaro amesisitiza umuhimu wa mchezo huo na kueleza kuwa Cosmo ni timu iliyowahi kushinda ubingwa mara mbili mbele ya vigogo wa soka nchini, Simba na Yanga, hivyo mchezo huo unatarajiwa kuwa wa ushindani mkubwa.

Aidha, Waziri Ndumbaro ameisifu timu ya Songea United kwa kuonesha kiwango kizuri ilipocheza dhidi ya Yanga, licha ya kufungwa kwa bao moja kwa sifuri katika mchezo uliojaa ushindani mkali na tuhuma za upendeleo. 

Amesema kiwango hicho kinaonesha kuwa Songea United ina uwezo mkubwa wa kushindana na timu kubwa nchini, hivyo inahitaji kuungwa mkono zaidi na jamii ya Songea.

Katika jitihada za kukuza na kuimarisha timu hiyo, Waziri Ndumbaro ametoa wito kwa wenyeviti wa mitaa kuanzisha matawi ya Songea United katika kila mtaa. 

Ameeleza kuwa kuanzishwa kwa matawi hayo kutasaidia kuongeza wanachama, kukuza uchumi wa timu, na kuimarisha mshikamano wa mashabiki wa nyumbani kwa lengo la kuinua soka la Songea.

 Waziri Ndumbaro amewataka wananchi wa Songea kuonesha uzalendo kwa kuvaa jezi za Songea United badala ya kuvaa jezi za timu zingine kama Simba na Yanga. 

Amesisitiza kuwa mafanikio katika soka na maendeleo ya timu ya mkoa yanatokana na mshikamano, ushirikiano na kujitambua kama jamii inayojali maendeleo ya michezo kwao.

Share:

VIONGOZI 4,000 MANISPAA YA SONGEA WAPATIWA MAFUNZO YA KISHERIA


Na Regina Ndumbaro Songea-Ruvuma

Takribani viongozi zaidi ya 4,000 wa ngazi ya mashina katika Manispaa ya Songea, Mkoa wa Ruvuma, wamepatiwa mafunzo ya kisheria kwa kipindi cha siku tatu kuanzia tarehe 10 Mei 2025.

Mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa Kanisa la Anglikana Songea Mjini na yamehusisha mabalozi wa nyumba kumi, wajumbe wa mashina pamoja na watendaji wake.

Lengo la mafunzo hayo ni pamoja na kutoa elimu ya utawala bora, uraia, mbinu mbadala za utatuzi wa migogoro, mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia pamoja na elimu ya uchaguzi.

Akifungua rasmi mafunzo hayo, Waziri wa Katiba na Sheria ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro, ameambatana na timu nzima ya Msaada wa Kisheria wa Mama Samia (Samia Legal Aid).
Waziri Ndumbaro ameeleza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuboresha mifumo ya utoaji haki kwa wananchi, huku akisisitiza kuwa mafanikio hayo ni matokeo ya mshikamano na imani ya wananchi kwa Serikali kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM).

Aidha, Mhe. Ndumbaro ameeleza kuwa msaada wa kisheria uliotolewa kwa wananchi wa Songea ni sehemu ya shukrani kwa ukarimu mkubwa waliouonesha kwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan wakati wa ziara yake ya Tamasha la Sanaa na Utamaduni Mkoani Ruvuma.

Amesema kuwa ziara hiyo siyo tu imeleta heshima kwa mkoa huo, bali pia imechochea Serikali kuendelea kusogeza huduma mbalimbali kwa wananchi zikiwemo barabara, vituo vya afya na huduma za elimu.

Katika kuhitimisha Waziri Ndumbaro ametoa wito kwa wananchi wote waliojiandikisha kuhakikisha wanashiriki kikamilifu katika uchaguzi kwa kupiga kura, akisisitiza kuwa hiyo ni njia mojawapo ya kulinda na kudumisha demokrasia na maendeleo ya taifa.

Amesisitiza kuwa mafunzo hayo ni sehemu ya juhudi za Serikali kuimarisha uelewa wa wananchi kuhusu haki na wajibu wao katika jamii.



Share:

MAREHEMU KAKATAA KUZIKWA NA KUIBUA TAFRANI MJINI



Mji mdogo wa Kisii nchini Kenya ulijikuta katika majonzi na mshangao huku mwili wa Fetty Moraa, anayedaiwa kuuawa na mumewe, ukikataa kuzikwa hadi pale Kiwanga Doctors ambao ni wabobezi wa tiba asilia walipoingilia kati suala hilo.

Tukio hilo la kusikitisha lilitokea mwaka 2021 na kuibua mshtuko kwa jamii, mamlaka za eneo hilo zilichukua hatua haraka za kumkamata mume wa Moraa ambaye ni mshukiwa mkuu wa uhalifu huo wa kutisha.

Walakini, kilichofuata ni hali ambayo sio ya kawaida iliyoacha gumzo katika eneo hilo, hali hiyo ni kwamba mwili huo uligoma kuzikwa jambo ambalo liliwaacha katika sintofahamu waombolezaji.
Share:

Friday, 9 May 2025

TET NA TANZANIA AI COMMUNITY KUSHIRIKIANA KUBORESHA UFUNDISHAJI KWA TEKNOLOJIA YA AI


TAASISI ya Elimu Tanzania (TET) imepanga kufanya mafunzo ya kukuza uwezo kwa wakuza mitaala na walimu nchini kwa kutumia Akili Mnemba (AI) ili kukuza ufanisi wa ufundishaji na ujifunzaji.

Hayo yamebainishwa leo Mei 9, 2025 Jijini Dar es Salaam, wakati TET wakisaini mkataba wa makubaliano ya ushirikiano wa miaka mitatu na Taasisi ya Tanzania AI Community kwa lengo la kuingiza matumizi ya AI katika ufundishaji na ujifunzaji.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa TET Dkt. Aneth Komba amesema jukumu lao kubwa itakuwa ni kuhakikisha kwamba wadau hao wa teknolojia wanapata karikulam, silabasi na vitabu ili waweze kuwasaidia kuweza kutumia AI katika ufundishaji na ujifunzaji.

"Haya ni mapinduzi makubwa kwa hatua zinazoendelea kupigwa, kwa sasa duniani kuna maendeleo makubwa sana katika sayansi na teknolojia, kwahiyo matumizi ya AI katika ufundishaji na ujifunzaji yatampunguzia sana mzigo mwalimu," amesema Dkt. Aneth

Amesema lengo lao ni kuhakikisha kwamba wanawafiki walimu wote nchini wanaoweza kutumia teknolojia hiyo katika jirahisisha ufundishaji na ujifunzaji, na kwamba katika mtaa mpya wataingiza kipengele cha kutumia AI katika ifundishaji na ujifinzaji.

Aidha Dkt. Aneth ameishukuru Taasisi ya Tanzania AI Community kwa kuwa tayari kushirikiana na TET, hivyo wapo tayari kutimiza majukumu yao kama TET kuhakikisha wanaendana na teknolojia iliyopo kwa sasa/

Naye, Mkurugenzi wa Tanzania AI Community, Essa Mohamedal, amesema wamefurahi kushirikiana na Taasisi ya Elimu kwakuwa wataweza kuwaongezea uwezo walimu wote nchini na kuwafanya watekeleze vizuri zaidi majukumu yao.

"Tuko hapa kwaajili ya kuwapatia walimu zana muhimu zitakazowasaidia kufundisha wanafunzi kwa ufanisi zaidi, na tunafurahisana kushirikiana na TET katika kuhakikisha AI inatumika kuleta mapinduzi ya elimu nchini," amesema Mohamedal.

Share:

TANZANIA UAE KUSHIRIKIANA KUWEZESHA ELIMU KIDIJITALI NCHINI


Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia imesaini makubalino na Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) ya kushirikiana katika Teknolojia ya Shule Kidijitali.

Makubaliano hayo yamesainiwa tarehe 8 Mei Jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu Prof. Carolyne Nombo na Dkt Waleed Ali Katibu Mtendaji wa Taasisi ya Shule Kidijitali ya UAE.

Utiaji saini makubaliabo hayo umeshuhudiwa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda na Balozi wa UAE Nchini Balozi Khalifa Abdulrahman Mohamed Abdulrahman Al Marzouqi
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger