Friday, 9 May 2025

TET NA TANZANIA AI COMMUNITY KUSHIRIKIANA KUBORESHA UFUNDISHAJI KWA TEKNOLOJIA YA AI


TAASISI ya Elimu Tanzania (TET) imepanga kufanya mafunzo ya kukuza uwezo kwa wakuza mitaala na walimu nchini kwa kutumia Akili Mnemba (AI) ili kukuza ufanisi wa ufundishaji na ujifunzaji.

Hayo yamebainishwa leo Mei 9, 2025 Jijini Dar es Salaam, wakati TET wakisaini mkataba wa makubaliano ya ushirikiano wa miaka mitatu na Taasisi ya Tanzania AI Community kwa lengo la kuingiza matumizi ya AI katika ufundishaji na ujifunzaji.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa TET Dkt. Aneth Komba amesema jukumu lao kubwa itakuwa ni kuhakikisha kwamba wadau hao wa teknolojia wanapata karikulam, silabasi na vitabu ili waweze kuwasaidia kuweza kutumia AI katika ufundishaji na ujifunzaji.

"Haya ni mapinduzi makubwa kwa hatua zinazoendelea kupigwa, kwa sasa duniani kuna maendeleo makubwa sana katika sayansi na teknolojia, kwahiyo matumizi ya AI katika ufundishaji na ujifunzaji yatampunguzia sana mzigo mwalimu," amesema Dkt. Aneth

Amesema lengo lao ni kuhakikisha kwamba wanawafiki walimu wote nchini wanaoweza kutumia teknolojia hiyo katika jirahisisha ufundishaji na ujifunzaji, na kwamba katika mtaa mpya wataingiza kipengele cha kutumia AI katika ifundishaji na ujifinzaji.

Aidha Dkt. Aneth ameishukuru Taasisi ya Tanzania AI Community kwa kuwa tayari kushirikiana na TET, hivyo wapo tayari kutimiza majukumu yao kama TET kuhakikisha wanaendana na teknolojia iliyopo kwa sasa/

Naye, Mkurugenzi wa Tanzania AI Community, Essa Mohamedal, amesema wamefurahi kushirikiana na Taasisi ya Elimu kwakuwa wataweza kuwaongezea uwezo walimu wote nchini na kuwafanya watekeleze vizuri zaidi majukumu yao.

"Tuko hapa kwaajili ya kuwapatia walimu zana muhimu zitakazowasaidia kufundisha wanafunzi kwa ufanisi zaidi, na tunafurahisana kushirikiana na TET katika kuhakikisha AI inatumika kuleta mapinduzi ya elimu nchini," amesema Mohamedal.

Share:

TANZANIA UAE KUSHIRIKIANA KUWEZESHA ELIMU KIDIJITALI NCHINI


Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia imesaini makubalino na Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) ya kushirikiana katika Teknolojia ya Shule Kidijitali.

Makubaliano hayo yamesainiwa tarehe 8 Mei Jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu Prof. Carolyne Nombo na Dkt Waleed Ali Katibu Mtendaji wa Taasisi ya Shule Kidijitali ya UAE.

Utiaji saini makubaliabo hayo umeshuhudiwa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda na Balozi wa UAE Nchini Balozi Khalifa Abdulrahman Mohamed Abdulrahman Al Marzouqi
Share:

Thursday, 8 May 2025

TBS YATOA WITO KWA WAZALISHAJI WA NISHATI SAFI KUFUATA VIWANGO

Na Mwandishi Wetu, Arusha

WADAU mbalimbali wa tasnia ya kutengeneza nishati safi za kupikia nchini wameshauriwa wanapokuwa kwenye mchakato wa kutengeneza nishati hizo kushirikiana na Shirika la Viwango Tanzania (TBS) ili kupata viwango vya kutengeneza nishati hizo.

Wito huo ulitolewa na Afisa Viwango wa TBS, Mhandisi Mohamed Kaila, wakati akizungumza na wadau mbalimbali katika kongamano la siku tatu la nishati safi ya kupikia kwa nchi za Afrika Mashariki lililofanyika jijini Arusha wiki hii.

Alisema TBS ina maabara na vifaa vya kupima vifaa vya nishati safi za kupikia, hivyo jukumu lao ni kuhakikisha vifaa vyote vinavyoingia kutoka nje na vinavyozalishwa nchini vinakuwa vinakidhi viwango vya nishati safi ya kupikia, kwani shirika hilo lina wataalam wa kutosha na kila siku wanapima vifaa hivyo .

Aidha, alisema TBS inathibitisha ubora kwa wazalishaji wa ndani wanaozalisha bidhaa za nishati safi za kupikia na kwamba wakishamthibitisha anakuwa amepata leseni ya ubora kuwa anaweza kuuza ndani na nje ya nchi bila tatizo lolote.

"Kwa hiyo tunatoa wito kwa wazalishaji wa ndani wanaozalisha nishati safi za kupikia na wale wanaoagiza kutoka nje ya nchi kufika TBS ili kuhudumiwa katika suala zima la viwango vya nishati safi pamoja na uthibati," alisema Kaila na kuongeza;

"Kwa hiyo nishati safi ya kupikia bila TBS kutakuwa hakuna nishati safi ya kupikia nchi hii, kwa hiyo tunawashauri wadau wakati wakiwa kwenye tasinia nzima ya nishati safi ya kupikia kukaa na sisi kupata huduma zao za kutengeneza viwango .

Alisema TBS ndiyo wenye jukumu mama la kutengeneza viwango ili kuhakikisha nishati safi ya kupikia inakuwa kweli nishati safi ya kupikia.

Alisema katika kutekeleza jukumu lao hilo kuna vitu vya msingi wanaviangalia ambapo kitu cha kwanza ni usalama wa nishati safi za kupikia lengo likiwa ni kuhakikisha Watanzania wnakuwa na uhakika kuwa vifaa hivyo viko salama.

Aidha, Kaila alisema pia wanaangalia suala la afya ili kumlinda mpishi , kwani wakati wa kupika kuna vitu vinaweza vikatokea kama moshi endapo nishati inayotumika si safi.

"Kwa hiyo kwetu sisi ili kufika kwenye nishati safi ya kupikia TBS tunaangalia suala hilo kwa umakini sana ili kulinda mtumiaji wa hiyo nishati," alisema Kaila.

Alitaja jambo lingine kuwa ni kuhakikisha wanatunza mazingira, hivyo wakati wa kutengeneza viwango vya hizo nishati, TBS wanahakikisha mazingira yanatuzwa..

Kwa mujibu wa Kaila jambo lingine wanaloangalia TBS ni uimara, kwani hawataki mtu anunue jiko leo baada ya miezi mitatu liwe limeharibika.

Pia Kaila, alisema jambo lingine wanaloangalia ni ufanisi wa nishati safi za kupikia ukoje, hivyo kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo Wizara ya Viwanda na Biashara , Wizara ya Nishati pamoja na wadau wa kitaifa na nje kama UNDP wameshirikiana kuweka viwango ili kupata nishati safi za kupikia .

Alisema kulingana na majukumu ya TBS kama hawatafanya vizuri kama wanavyoendelea kufanya vizuri hiyo nishati safi ya kupikia haitakuwa nishati ya kupikia.

Naye Afisa Afisa Viwango Spiradson Kagaba, alisema wakati tunaelekea kuhakikisha asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia wanatakiwa kuhakikisha hakuna kinachoharibika,kwa maana ya kuhakikisha mtumiaji anakuwa salama na mazingira yanakuwa salama.

"Lakini pia mtumiaji aweze kupata kitu ambacho kiko kwa mujibu wa viwango," alisema Kagaba.

Alisema mojawapo ya matakwa ya viwango ni mzalishaji aseme ni kwa namna gani yale majiko yanafaa, anaweza kuja akasema ufanisi wake ni asilimia 90 kama TBS haijasimama ikamwambia yule mtu ni asilimia 80 ni rahisi sana huyo mtu kudanganya.

"Kwa hiyo sisi TBS tunaingia kuangalia yule mtu aliyetuambia ni la asilimia 80 ni asilimia 80 kweli anachosema mzalishaji," alisema.

Alifafanua kwamba TBS imefanya mambo mengi imeandaa viwango ili vitumike kuwalinda watu na kwamba wana viwango vya teknolojia zote kama ilivyotajwa kwenye mkakati.
Share:

WACHIMBAJI MADINI WAIPONGEZA REA KWA KUWAFIKISHIA UMEME

 

📌Ni kupitia Mradi wa kupeleka umeme kwa wachimbaji wadogo na wa kati

📌Umeme umeleta ukombozi, uzalishaji madini waongezeka Geita

Mradi wa kupeleka umeme kwa wachimbaji wadogo na wa kati, Viwanda vidogo na vya kati pamoja na maeneo ya kilimo umepokelewa kwa furaha na wananchi mkoani Geita mara baada ya kupata umeme wa uhakika katika migodi yao.

Hayo yamebainishwa na wachimbaji wadogo wa madini wakati wakizungumza na Bodi ya Nishati Vijijini (REB) mara baada ya kutembelea maeneo ya shughuli za uchimbaji madini katika eneo la Magema katika ziara iliyolenga kukagua miradi ya umeme vijijini inayotekelezwa mkoani Geita.

Share:

BARAZA LA HABARI KENYA LAVUTIWA NA MAIPAC, LAAHIDI KUSHIRIKIANA KUTOA MAFUNZO KWA WANAHABARI


Mkurugenzi mtendaji MAIPAC,Mussa Juma akimkabidhi Mkurugenzi wa mafunzo na Maendeleo wa baraza la habari Kenya Victor Bwire kitabu cha maarifa ya asili katika uhifadhi wa mazingira kilichoandaliwa na MAIPAC ambacho kinasambazwa bure
Mwandishi wetu,maipac

Baraza la Habari la Kenya(KMC),limetembelea Ofisi za Taasisi ya wanahabari ya usaidizi wa jamii za pembezoni(MAIPAC) jijini Arusha na kuvutiwa na kazi za Taasisi hiyo na kuahidi kushirikiana kuwajengea uwezo wanahabari juu ya masuala ya mabadiliko ya tabia nchi na Matumizi sahihi ya akili mnemba(AI).

Mkurugenzi wa Mafunzo na Maendeleo wa baraza hilo,Victor Bwire akizumgumza na watendaji wa MAIPAC baada ya kupata taarifa za utendaji wa shirika hilo,licha ya kupongeza ameahidi baraza hilo kushirikiana na MAIPAC kuwajengea uwezo wanahabari.

"Kuna waandishi wa habari wa Kenya pia wanafanyakazi na hizi jamii za pembezoni hivyo tutawaunganisha na wanachama wa MAIPAC kupata mafunzo zaidi ya juu ya mabadiliko ya tabia nchi na masuala ya AI kwa sababu mazingira yanafanana",amesema.

Bwire amesema, jamii za pembezoni za Tanzania na Kenya zinaendelea kuathirika na mabadiliko ya tabia nchi hivyo kwa wanahabari ni muhimu kusaidia jamii hizo kuwapa elimu ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi lakini pia kuweza kuhimili mabadiliko hayo.

"Nawapongeza sana MAIPAC kwa miradi yenu ,nyie kama wanahabari mnafanyakazi nzuri sana katika jamii hizi katika miradi ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi,miradi ya kurekodi maarifa ya asili lakini pia miradi ya kupinga ukatili dhidi ya wanawake na watoto",amesema.

Awali, Mkurugenzi Mtendaji wa MAIPAC Mussa Juma amesema taasisi ya MAIPAC inaundwa na waandishi wa habari kutoka mikoa mbalimbali Tanzania ambao wamekuwa wakiandika masuala ya mazingira na katika jamii za pembezoni.

Juma amesema , MAIPAC imekuwa na miradi kadhaa ikiwepo kurekodi maarifa ya asili kwa jamii za pembezoni katika uhifadhi wa mazingira,misitu na vyanzo vya maji.

"Lakini pia tumekuwa na mradi wa kusaidia jamii kutunza vyanzo vya maji,mradi wa kupinga ukatili dhidi ya wanawake na watoto",amesema

Amesema miradi hiyo,inafadhiliwa na taasisi kadhaa ikiwepo mfuko wa mazingira duniani(GEF) kupitia programu ya miradi midogo ambayo inaratibiwa na shirika la maendeleo la Umoja wa Mataifa(UNDP) Tanzania na ofisi ya makamu wa Rais Mazingira na shirika la kimataifa la Cultural Survival.

Hata hivyo amesema kwa wanahabari wanachama wa MAIPAC wanahitaji sana mafunzo juu ya masuala mabadiliko ya tabia nchi,masuala ya akili mnemba na masuala ya biashara ya hewa ya ukaa na taratibu zake.

Katika ziara hiyo, Bwire ameambatana na viongozi wengine wa MAIPAC, Stella Kaaria Meneja wa utafutaji fedha na mahusiano,Careen Mang'eni na Evaes Teddy.
Share:

Wednesday, 7 May 2025

WAKUU WA TAASISI ZA HABARI WASHUHUDIA UWASILISHAJI BAJETI YA HABARI

 Wakuu wa  Taasisi za Kihabari nchini kwenye picha ya Pamoja na Waziri wa Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo, Profesa Paramagamba Kabudi, Naibu Waziri Hamis Mwinjuma na  Katibu Mkuu na Msemaji Mkuu wa Serikali Greson Msigwa baada ya uwasilishwaji wa bajeti ya Wizara ya habari, utamaduni, Sanaa na Michezo  Bungeni Leo Jijini Dodoma. 

Wakuu hao ni pamoja na Katibu wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Ernest Sungura, Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF),  Deodatus Balile, Mwenyekiti wa Misa Tanzania {Misa Tz), Edwin Soko, Mjumbe wa Bodi ya Chama cha Wafanyakazi Waandishi wa Habari Nchini (Jowuta) na Mjumbe wa Kamati Tendaji ya Jukwaa la Wahariri TEF, Caren-Tausi Mbowe pamoja na  Mhariri Mkuu mstaafu wa Magazeti ya Serikali (TSN), Tuma Abdallah.

Share:

MKAGUZI WA USHIRIKA MKOA WA RUVUMA ATOA MAFUNZO YA USIMAMIZI NA UHASIBU KWA VYAMA VYA USHIRIKA MBINGA NA NYASA


Mkaguzi wa Ushirika Jackson Sinde akitoa Mafunzo ya Usimamizi na Uhasibu kwa Vyama vya Ushirika Mbinga na Nyasa katika ukumbi wa Mbicu Hotel Wilayani Mbinga Mkoa wa Ruvuma
Wajumbe wakiwa kwenye mafunzo
Wajumbe wakiwa kwenye mafunzo

Na Regina Ndumbaro Mbinga-Ruvuma 

Katika juhudi za kuimarisha usimamizi wa fedha na uwajibikaji ndani ya vyama vya ushirika, Mkaguzi wa Ushirika Mkoa wa Ruvuma, Bw. Jackson Sinde kutoka Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika mkoa wa Ruvuma(COASCO)ameendesha mafunzo kwa watendaji na wajumbe wa bodi wa vyama vya ushirika katika halmashauri za Mbinga Mji, Mbinga Vijijini na Nyasa. 

Mafunzo hayo yamelenga kutoa elimu juu ya taratibu za uhasibu, umuhimu wa ukaguzi wa hesabu, na wajibu wa bodi katika kulinda mali za vyama kwa kuzingatia sheria, kanuni na miongozo ya ushirika.

 Mafunzo hayo yamefanyika kwa watendaji wa vyama ambapo wamekumbushwa umuhimu wa kuzingatia taratibu za uhasibu kwa uwazi na usawa katika miamala ya kifedha. 

Vilevile, wameelekezwa namna bora ya kujiandaa kwa ajili ya ukaguzi wa hesabu unaofanywa na COASCO na kuhamasishwa kujiendeleza kitaaluma ili kuongeza uwezo wao wa kutekeleza majukumu ya kila siku kwa ufanisi.

Tarehe 07 Mei 2025, mafunzo hayo yameendelea katika ukumbi wa Mbicu Hotel ambapo yamewahusisha wajumbe wa bodi waliopata mwongozo wa kusimamia kwa karibu utendaji wa watendaji, kuhakikisha taarifa za kifedha zinaandaliwa kwa wakati na kwa usahihi, na kuhakikisha zoezi la ukaguzi linafanyika kwa mujibu wa ratiba. 

Pia wamesisitizwa kuwajibika kwa kuhakikisha vyama vyao vinafuata miongozo ya usimamizi na uendeshaji wa ushirika.

Hata hivyo, changamoto kubwa iliyobainika ni kuwepo kwa vyama takribani 30 kutoka halmashauri hizo tatu ambavyo bado havijawasilisha taarifa za fedha na nyaraka muhimu kwa ajili ya ukaguzi wa hesabu, licha ya kutakiwa kufanya hivyo hadi kufikia tarehe 30 Septemba 2024. 

Hili imeonyesha hitaji la kuimarisha uwajibikaji zaidi na kufuatilia utekelezaji wa wajibu wa vyama hivyo kwa karibu.
Share:

POLISI POLISI WAZIONDOA HOFU ASASI ZA KIRAIA USALAMA WAKATI WA UCHAGUZI MKUU


Nihifadhi Abdulla

JESHI LA POLISI ZANZIBAR limezitoa hofu Asasi za Kiraia zinazoendelea kusimamia haki za Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu ZNZ ambapo limesema litaendelea kuhakikishia Haki, Ulinzi na Usalama kwa makundi hayo katika kipindi cha Uchaguzi Mkuu Mwaka huu 2025 zinalindwa kikamilifu.

Kauli hiyo imetolewa na Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar, Khamis Kombo Khamis alipokuwa akizungumza na wawakilishi wa Asasi za Kiraia zinazotetea haki za Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu zilizofika katika Afisi kuu za Jeshi hilo Ziwani Wilaya ya Mjini Unguja katika kikao maalum cha kujadili mustakbali wa ulinzi na usalama wa makundi hayo wakati wa Uchaguzi.


Aidha Kamishna Khamis ameziasa asasi hizo kufikia pia wadau na taasisi nyengine muhimu nchini ili kwenda sambamba na azma hiyo.


Alizitaja taasisi nyengine kuwa ni pamoja na Vyama vya Siasa, Vikosi vyengine vya Ulinzi na Tume ya Uchaguzi. Alieleza pia kuna haja ya kuwaelimisha wananchi jinsi ya kujiepusha na vitendo vya uvunjaji wa sheria ili kujiweka katika hali ya usalama.


Kamishna amesisitiza pia kuwa Jeshi la polisi lina utaratibu mzuri wa kuwawajibisha maafisa wake pindi wakienda kinyume na utaratibu wa kazi.


Wakizungumza katika kikao wana Asasi hao wameliomba Jeshi hilo kuendelea kuwa msimamizi namba moja wa amani wakati wa uchaguzi sambamba na kuwalinda Wanawake pamoja na Watu wenye Ulemavu ili waweze kuwa salama na kushiriki kikamilifu katika mchakato huo wa kidemokrasia kama wapiga kura, wagombea na mawakala.


Walisema mwaka 2020 baadhi ya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu walipatwa na kadhia ya uvunjifu wa haki zao kutoka kwa Vikosi vya Ulinzi na Usalama nchini kama wagombea na mawakala na hivyo kujenga hofu kuhusu ushiriki wao kwa mwaka 2025.


Asasi hizo zimeahidi kuendelea kutoa mashirikiano kwa Jeshi la Polisi ikiwa ni pamoja na kujenga uwezo kwa makundi hayo na kufatilia ushiriki wao katika kipindi hicho cha Uchaguzi Mkuu.


Kikao hicho kilichofanyika Mei 2 huko katika Ofisi za Makao Makuu ya Jeshi hilo zimewakutanisha Wawakilishi kutoka Asasi za Kiraia Zanzibar zinazotetea, kulinda na kusimamia haki za Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu zikiwemo Jumuiya ya Mazingira, Jinsia na Utetezi Pemba (PEGAO) Jumuiya ya Wanawake Wenye Ulemavu Zanzibar (JUWAUZA), Jumuiya inayoshughulika na Changamoto za Vijana Zanzibar (ZAFAYCO) na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA ZNZ).
Share:

MHE. CHATANDA AMPONGEZA RAIS KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI RUFIJI


Na Mwandishi Wetu..

Mwenyekiti wa UWT- CCM Taifa, Mhe. Mary Pius Chatanda amekagua miradi mbalimbali ya maendeleo yenye thamani ya zaidi ya bilioni 25 inayotekelezwa wilayani Rufiji na kumpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi hiyo.

Mbali na kumpongeza Mhe. Rais Samia, pia amempongeza Mbunge wa Rufiji kwa kusimamia utekelezaji wake ambapo amesema miradi hiyo imesimamiwa vizuri na ina tija kubwa kwa wananchi.
"Hapa naomba niungane na watanzania wote kumpongeza Rais wetu kipenzi Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa ambayo ameifanya nchi nzima, na hapa leo Rufiji tunashuhudia kazi nzuri ambayo imetekelezwa kupitia miradi hii" amesisitiza Mhe Chatanda

Mhe Chatanda ambaye yupo kwenye ziara ya siku mbili katika jimbo la Rufiji amekagua mradi wa ujenzi wa daraja la Mbambe linalojengwa kwa urefu wa mita 81 na ujenzi wa barabara ya lami inayounganisha barabara kuu ya kilomita 3 itakayogharimu bilioni 24.1.
Mkataba wa daraja hilo ulisainiwa na Wakala wa Barabara Tanzania na Mkandarasi M/S Nyanza Road Works Ltd ya Mwanza ambapo kazi hiyo inatarajia kukamilika katika kipindi Cha miezi 6 kuanzia sasa.

Akizungumza mara baada ya ukaguzi wa daraja hilo Mhe. Mchengerwa alifafanua kuwa mradi wa ujenzi wa daraja hilo ni moja ya mikakati ya Serikali ya kuharakisha maendeleo ya kiuchumi na kijamii wilayani Rufiji maeneo jirani.
Rashid Salum Mkazi wa Ikwiriri amemshukuru Mhe Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwaletea fedha kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo ambapo amesema kukamilika kwake kutakuwa msaada mkubwa kutokana na adha kubwa walihokuwa wakipata hapo awali.

Aidha, Mhe. Chatanda ameshuhudia utiaji saini wab mikataba ya ujenzi wa miradi ya maji katika vijiji vya Mloka, Mbinju Mvuleni na Ndundutawa ambapo pia ameshuhudia zoezi la kupewa mabati 45 na Mhe. Mbunge vijana wa bodaboda wa kijiji cha Mloka ili kuezekea eneo la kuegesha bodaboda zao.

Akitoa taarifa ya mradi huo, Meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini ( RUWASA) Wilaya ya Rufiji Mhandisi Alkam Omari pamoja na uwekezaji mkubwa ambao umefanywa na Serikali katika kuwapatia wananchi maji safi na salama, mahitaji ya maji yamezidi kuongezeka ambapo amesema mradi huu unakwenda kuwa suluhisho.


Share:

Tuesday, 6 May 2025

TEHAMA KUBORESHA ELIMU KWA MAFUNZO YA WALIMU


TEHAMA ni nyenzo muhimu katika sekta ya elimu, kwa kutambua hilo Serikali imewezesha mafunzo kwa walimu ili kuongeza maarifa na kuboresha mbinu za ufundishaji na ujifunzaji ngazi mbalimbali za elimu.

Ameeleza hayo Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo Aprili 06, 2025 akizungumza na Clouds TV kuhusu maandalizi ya Kongamano la eLearning Africa 2025 kuanzia tarehe 7 hadi 9 Mei, 2025 JNICC jijini Dar es Salaam.

‘’matumizi ya TEHAMA yanatumika kikamilifu katika sekta ya elimu, walimu wote wamefundishwa namna ya kutumia teknolojia katika kufundisha, lengo letu ni kuhakikisha wana maarifa na mbinu za kidijiti zinazochagiza ujifunzaji’’ Alisema Prof. Nombo.

Amesema kongamano hilo linatoa fursa mbalimbali kwa nchi, ikiwa ni pamoja na maonesho ya bunifu na teknolojia zikiwemo zilizobuniwa na vijana wa kitanzania zinazolenga kutoa suluhu za kidijiti na kielimu.
Share:

AMREF TANZANIA YAADHIMISHA SIKU YA MKUNGA DUNIANI 2025



Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Anamringi Macha (kushoto) akipewa maelezo katika banda la Amref Tanzania wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mkunga Duniani yaliyofanyika kitaifa mkoani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Anamringi Macha akizungumza na wananchi, wageni na wadau mbalimbali waliohudhuria maadhimisho ya Siku ya Mkunga Duniani yaliyofanyika kitaifa mkoani humo.
Wananchi na wageni mbalimbali wakipata maelezo katika banda la Amref Tanzania wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mkunga Duniani yaliyofanyika kitaifa Mkoani Shinyanga.
Wageni na wadau mbalimbali wakifuatilia hotuba wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mkunga Duniani yaliyofanyika kitaifa mkoani Shinyanga.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Anamringi Macha akiwa katika picha ya pamoja na wageni na wadau wa maendeleo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mkunga Duniani yaliyofanyika kitaifa mkoani humo.
Watumishi wa Shirika la Amref Tanzania katika picha ya pamoja wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mkunga Duniani yaliyofanyika kitaifa mkoani Shinyanga.

****
Katika kuadhimisha Siku ya Mkunga Duniani kitaifa iliyofanyika mkoani Shinyanga, Shirika la Amref Health Africa Tanzania limeeleza mafanikio makubwa ya Mradi wa Thamini Uzazi Salama, unaolenga kuboresha huduma za afya ya uzazi kwa wanawake na watoto wachanga kupitia uwezeshaji wa wakunga na wahudumu wa afya ngazi ya jamii.

Akizungumza katika maadhimisho hayo yaliyofanyika katika viwanja vya Zimamoto, Meneja wa Programu ya Afya ya Uzazi, Mama, Mtoto na Vijana wa Amref Tanzania, Dkt. Serafina Mkuwa alisema:

 “Mradi huu unafadhiliwa na Global Affairs Canada (GAC) na unasimamiwa na UNFPA. Unalenga kuongeza upatikanaji wa wakunga wenye ujuzi na kuboresha huduma katika vituo vya afya, taasisi za mafunzo na kwa wahudumu wa afya ngazi ya jamii”.

Dkt. Mkuwa aliongeza kuwa kwa kipindi cha Januari hadi Desemba 2024, mradi huo umefanikiwa kuwafikia watu 17,167 kupitia uhamasishaji wa afya ya uzazi, jinsia na ukatili wa kijinsia (GBV), kutoa mafunzo kwa waelimishaji rika wa kiume 142, na kuimarisha uwezo wa wasimamizi 112 wa wahudumu wa afya ngazi ya jamii (CHW) kupitia jukwaa la LEAP.

 “Mradi pia umewezesha CHW 112 kwa kuwapatia simu za mkononi, kuwawezesha viongozi wa jamii 424 kuhusu jinsia na haki za afya ya uzazi, na kuwajengea uwezo wajumbe wa kamati za usimamizi wa vituo vya afya na wakuu wa vituo 518 kuhusu bajeti na mipango ya afya,” alieleza zaidi Dkt. Mkuwa.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anamringi Macha, aliishukuru Serikali kwa kuimarisha miundombinu ya afya mkoani humo, akisema:

Kati ya mwaka 2015/2016, asilimia 66 ya wanawake walijifungulia katika vituo vya afya. Kwa sasa idadi imeongezeka hadi asilimia 85. Hii ni hatua kubwa kuelekea kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi.”

Rais wa Chama cha Wakunga Tanzania, Dkt. Beatrice Milike, alisisitiza mchango wa wakunga nchini.

Wakunga hutoa asilimia 90 ya huduma za afya ya uzazi nchini. Ikiwa watawezeshwa kwa mafunzo na vifaa, wanaweza kupunguza vifo vya mama na mtoto kwa zaidi ya asilimia 87,” alisema Dkt. Milike.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni “Mkunga ni Nguzo Muhimu katika Kila Janga”, ikionyesha umuhimu wa wakunga hasa katika nyakati za dharura kama vile majanga ya kiafya na kijamii.

Mradi wa Thamini Uzazi Salama umeendelea kuwa mfano bora wa ushirikiano kati ya serikali, mashirika ya kimataifa na jamii katika kuhakikisha uzazi salama na kupunguza vifo vinavyoweza kuzuilika kwa mama na mtoto nchini Tanzania.
Share:

MATHIAS CANAL ASHINDA TUZO YA SAMIA KALAMU AWARDS, WAZIRI ULEGA AMPA SHAVU MBELE YA RAIS SAMIA









Na Dotto Kwilasa,DAR




Mwanzilishi na Afisa Mtendaji Mkuu wa WazoHuru Media Group Limited Ndg Mathias Canal ameshinda Tuzo mbili za SAMIA KALAMU AWARDS sekta ya Ujenzi na chombo bora cha mtandaoni.




Pamoja na zawadi ya Cheti, Ngao, Tsh Milioni 10, lakini pia Mathias Canal amezawadiwa safari ya kwenda nchini Japani pamoja na kufanya kazi ya kusafiri nchi nzima kueleza kwenye vyombo vya habari mafanikio na utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2020-2025.







Tuzo hizo zimetolewa leo tarehe 5 Mei 2025 katika ukumbi wa Super Dome Masaki Jijini Dar es salaam ambapo mgeni rasmi katika tukio hilo alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan








Tuzo hizo zimetolewa kwa wanahabari watanzania kwa lengo la kuhamasisha, kuhimiza na kukuza wigo wa uchakataji, utangazaji na uchapishaji wa maudhui ya ndani kupitia vyombo vya habari.






Tuzo hizi zitahusisha maudhui yaliyochapishwa kupitia magazeti, redio, televisheni, majukwaa ya mtandaoni pamoja na tuzo kwenda kwa vyombo vya habari. Tuzo hizi zinahusisha habari zilizochapishwa kati ya Januari 01 hadi Oktoba 26, 2024.

Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi Mhe Abdalah Ulega, Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe Innocent Bashungwa (Mb) amesema kuwa pamoja na zawadi ya Tuzo pia Waziri Ulega amempa zawadi ya kufanya kazi katika wizara hiyo hivyo akaripoti Wizarani kwa ajili ya kuanza kazi.


Aidha, utoaji wa tuzo hizi umelenga kuchochea uandishi wa makala zilizofanyiwa utafiti na uchambuzi kuhusu maendeleo ya nchi, uwajibikaji, uzalendo na kujenga chapa na taswira ya nchi.







Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger