Tuesday, 6 May 2025

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE MEI 6,2025





Magazetini leo
   

Share:

Monday, 5 May 2025

KAMHONGA MKE WANGU SH5.7 MILIONI LAKINI HAJAAMBULIA KITU


Jina langu ni Frey, tumeishi na mke wangu Tuma kwa miaka 12 ndani ya ndoa yetu, naweza kusema kati ya wanaume duniani ambao wamefaidi matunda ya ndoa mimi ni mmoja wapo.

Nasema hivyo kwa sababu tangu nimemuoa huyu mke wangu sikumbuki kama kuna siku tumewahi kugombana au kununiana ndani ya nyumba, muda wote kwetu sisi ni upendo tu.

Pia mke wangu ni nzuri sana kisura na kiumbo, ni vidume wengi sana mtaani na sehemu mbalimbali vimekuwa vikimmezea mate, kila anapokatiza lazima watu wageuke kumtazama hata wanawake wenzake hufanya hivyo.
Share:

SHINYANGA WENYEJI MAADHIMISHO SIKU YA MKUNGA DUNIANI KITAIFA







Na Marco Maduhu,SHINYANGA

MAADHIMISHO ya Siku ya Mkunga Duniani Kitaifa yanafanyika mkoani Shinyanga, huku Mgeni Rasmi akiwa ni Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dk.Seif Shekalaghe.

Maadhimisho hayo yameanza leo Mei 4,2025 na yatahitimishwa kesho Mei 5 na yanafanyika katika Viwanja vya Zimamoto Mjini Shinyanga.

Rais wa Chama Cha Wakunga wa Tanzania (TAMA)Dk. Beatrice Mwilike, akizungumza na waandishi wa habari amesema kuwa maadhimisho hayo mwaka huu wameamua kuyafanyia mkoani Shinyanga, ili kutoa elimu mbalimbali kwa wananchi juu ya masuala ya afya ya uzazi, na kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi.

“Maadhimisho ya siku ya ukunga duniani kitaifa hapa nchini Tanzania, mwaka huu tumeamua kuyafanyia hapa mkoani Shinyanga,na Mgeni Rasmi atakuwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dk.Seif Shekalaghe,”amesema Dk Mwilike.


Aidha,amesema katika maadhimisho hayo, elimu mbalimbali zitatolewa bure kwa wananchi, yakiwamo masuala ya afya ya uzazi,pia kutakuwa na huduma ya utoaji wa damu salama ili kuchangia benki ya damu,na hata kuokoa wazazi wakati wa kujifungua.


Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dk.Yudas Ndungile, ametoa wito kwa wananchi wa mkoa huo,wajitokeze kwa wingi kwenye maadhimisho hayo ya siku ya ukunga dunian mkoani humo ili wapate elimu mbalimbali bure za masuala ya afya na afya ya uzazi.


Kauli Mbiu katika maadhimisho ya siku ya ukunga duniani mwaka huu inasema”Mkunga ni Nguzo Muhimu katika kila Janga.”
Share:

Sunday, 4 May 2025

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU MEI 5,2025




Magazetini



Share:

MBUNGE IDDI KASSIM AWAONESHA NJIA – AWAKABIDHI BAISKELI WENYEVITI WA VIJIJI 92 KUFUATILIA MIRADI

Na Mwandishi Wetu, Malunde 1 blog

Mbunge wa Jimbo la Msalala mkoani Shinyanga, Mhe. Iddi Kassim, ametoa baiskeli 92 kwa wenyeviti wa vijiji vyote vya Halmashauri ya Msalala kwa lengo la kuwawezesha kufuatilia kwa ukaribu utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika maeneo yao.

Baiskeli hizo zenye thamani ya shilingi milioni 23 zimekabidhiwa rasmi katika hafla iliyofanyika leo katika kata ya Bugarama zikiwa ni kwa ajili ya wenyeviti wa vijiji katika jimbo zima la Msalala kwa lengo la kurahisisha usafiri wa viongozi hao kuzungukia miradi ya maendeleo katika maeneo yao.

Zoezi hilo la ugawaji wa baiskeli limefanyika leo Mei 4,2025 likiongozwa na Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Taifa, Mohammed Ali Kawaida, ambaye pia amehutubia wananchi na kuwahimiza kuhakikisha miradi ya maendeleo inalindwa na kutunzwa kwa manufaa ya wote.

“Ni jambo la kuigwa. Mbunge amewawezesha viongozi wa msingi kufanikisha usimamizi wa maendeleo ya wananchi. Nawasihi wenyeviti kutumia baiskeli hizi kwa shughuli zilizokusudiwa,” amesema Kawaida na kupongeza hatua hiyo aliyoitaja kuwa ya kipekee katika ziara yake ya siku 10 nchini.

"Naomba mkazitunze hizi baiskeli ili ziwasaidie katika kuzungukia miradi ya maendeleo inayotekelezwa na ilani ya Chama cha mapinduzi (CCM)", amesema.

Akizungumza katika mkutano huo, Mbunge Iddi amesema kuwa wenyeviti wa vitongoji na vijiji wanafanya kazi kubwa bila kuwa na mshahara na kwamba jimbo la msalala lina utajiri mkubwa unaoweza kuwapa posho wenyeviti hao kupitia mapato ya ndani.

Ameeleza kuwa kila baiskeli imegharimu shilingi 250,000, na kwamba hatua hiyo inalenga kuwawezesha wenyeviti kusimamia kwa karibu utekelezaji wa miradi mbalimbali ili kuhakikisha changamoto zinagunduliwa mapema na kutafutiwa ufumbuzi.

Aidha Mheshimiwa Iddi amewataka viongozi kuwatumikia wananchi kwa kusimamia kwa uaminifu miradi ya maendeleo ili kuinua Uchumi wa taifa na Uchumi wa mtu mmoja mmoja.

“Katika vijiji vyetu, kuna miradi mingi inayoendelea na inahitaji usimamizi wa karibu. Nitashirikiana na viongozi hawa kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na maendeleo ya kweli,” ameongeza.

Wakizungumza mara baada ya kupokea baiskeli hizo baadhi ya wenyeviti wamemshukuru Mbunge Iddi na kwamba baiskeli hizo zitawasaidia katika majukumu yao.

Katika tukio hilo, wanachama tisa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kutoka Wilaya ya Kahama, wakiongozwa na aliyekuwa Mjumbe wa Kamati Tendaji ya wilaya hiyo, Samson Thomas, wamehamia Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kupokelewa rasmi na Mwenyekiti wa UVCCM Taifa.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake, Thomas amesema wameamua kuunga mkono juhudi za serikali ya CCM katika kusukuma mbele maendeleo ya wananchi, na kuahidi kushiriki kikamilifu katika shughuli za chama na uongozi, huku akiahidi kuwa mtiifu kwa chama hicho.



Share:

VIONGOZI WA DINI WATAKIWA KUEPUKA SIASA NA UCHOCHEZI


Na Mwandishi Wetu

VIONGOZI wa dini katika madhebu mbalimbali nchini wameshauriwa wasiwe wanasiasa na wala kuwa sehemu ya kuwa wachochezi kwani wao ni sehemu ya kimbilio pale ambapo nchi itakuwa na changamoto huku wakikumbushwa wajibu wa kuliombea Taifa la Tanzania hasa katika mwaka huu wa Uchaguzi Mkuu.

Pia kwa waumini wa dini mbalimbali ambao ni wanasiasa wamekumbushwa na kuhimizwa kufanya kampeni za kistaarabu lakini wawe wenye kujishusha na kusamehe kwani kila mmoja wetu analojukumu la kuhakikisha amani,umoja na mshikamano unaendelea kuwepo.

Hayo yameelezwa na Wachungaji kutoka Tanzania na Kenya wa Kanisa la Wadventista Wasabato walipokuwa wakihitimisha Wiki ya Uamsho iliyokuwa na maombi mbalimbali yakiwemo ya kuliombea amani ,umoja na mshikamano Taifa la Tanzania ambalo Oktoba mwaka huu linatatajia kufanya uchaguzi Mkuu .

Wiki ya Uamsho imeandaliwa na Kwaya ya Gethsemane Group Kinondoni (GGK) kutokea Kanisa la Wadventista Wasabato Kinondoni Jijini Dar es Salaam ambapo katika maombi hayo pia wamewaalika wachungaji wa Kanisa hilo kutoka nchini Kenya.

Akizungumza baada ya kufanyika kwa maombi ya kuliombea Taifa, Katibu wa Jimbo la Mashariki Kati mwa Tanzania wa Kanisa la Waadvestita Wasabato Tanzania Mchungaji Shashi Musa Wanna amesema walikuwa na maombi katika juma zima ambapo wametumia nafasi hiyo kuwa na mahubiri pamoja na maombi.

“Tulikuwa na wiki ya Uamsho wa kiroho katika Kanisa letu lakini pia kuliombea Taifa letu na Wachungaji wenzetu kutoka Kenya ambao tulikuwa nao wenzetu wanauzoefu mkubwa mambo ya siasa yanayoendelea Kenya.Tumehimiza maombi na umuhimu wa amani katika nchi yetu.

Aidha amesema pia wanawashauri viongozi wengine wa dini wasiwe wanasiasa kwani viongozi wa dini ni sehemu ya kimbilio pale ambapo nchi itakuwa na shida hivyo wanawajibu wa kuombea Taifa lakini wanakazi ya kufanya usuluhishi kwa maana ya waumini wao pia ni sehemu ya wanasiasa.

Pia amesema wanawaambia waumini wawe ni wenye kusamehe na kujishusha huku akiendelea kutoa rai kwa viongozi wengine wa dini nchini kuliombea Taifa letu.”Tusiwe sehemu ya uchochezi bali tuwe sehemu ya kuleta amani kwa maombi na ushauri.”

Kwa upande wake Mhubiri kutoka nchini Kenya Mchungaji Patrick Muthee amesema katika zama hizi ambazo Dunia imeharibika wakati mwingine makanisa na waumini wake wanajaribiwa huku akieleza Kanisa linapoongia katika siasa kunakuwa na changamoto kwasababu ile roho ya Mungu inaondoka

“Kazi ya Kanisa ni kuleta watu pamoja na tunatambua viongozi Mungu ndio huchagua sisi kama waumini Mungu anatutumia katika hali ile ya kupiga kura lakini Mungu anajua njia iliyobora.Hivyo kama Kanisa viongozi,wachungaji , na masheikh tuzungumze na waumini wetu ….

“Kuwaambia jukumu kubwa la kuchagua viongozi ni la Mungu hivyo tumtangulize Mungu, wawe na imani Mungu ndiye anatuchagulia viongozi hatutakuwa na mashindano ,hatutakuwa na vurugu.

Wakati huo huo Mchungaji Haruni Muturi wa Kanisa la Wadventista Wasabato kutoka nchini Kenya amesema katika wiki hiyo ya uamsho wametumia nafasi hiyo kujihoji miyoni mwao na kujitoa upya kwa Yesu Kristo kwasababu wanajua kuna majaribu.

“Na kwasababu ya majaribu hayo Mungu aweze kusikia watu wake ,kuwarejesha katika upendo wake na jinsi tulivyokuwa tumekuja kuombea nchi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hilo nalo ni jambo tumelizingatia sana.

“Kwasababu tunataka waumini wasiwe na vita na Serikali ,wafahamu jinsi ya kufanya kampeni za kuchagua viongozi kwa ustaarabu na wawe watii na kuweka Serikali katika Maombi badala ya vita ,ni jukumu letu pia kuendelea kuomba mpaka uchaguzi utakapokwisha Oktoba mwaka huu.

Awali Mchungaji wa Kanisa la Waadvestita Wasabato Kinondoni Victor Geofrey amesema wamekuwa katika wiki ya Uamsho iliyokuwa na lengo la kukumbushana mambo muhimu katika maisha ya Kikristo na kusimama kama Kristo alivyofundisha na hasa wakijua wako siku za mwisho naye anakaribia kuja upesi .

“Lakini katika wiki ya Uamusho pia tumeomba kwa mambo mbalimbali kwa ajili ya maisha ya kiroho lakini pia kwa ajili ya mambo ya taifa letu la Tanzania kwani tuko katika wakati uliomakini ambao kila Mtanzania anatakiwa kuchukua jambo hilo kwa umakini wake.

“Tumeliombea Taifa amani na mshikamano na tumehitimisha siku ya ya Sabato, siku ya ibada kwa pamoja na tumekutana kumshukuru kwa kuwa ametusikia kwa wiki nzima na maombi haya yatakuwa endelevu kwasababu tumeamshwa maombi ni maisha ya kila siku ya wale ambao wanatazamia maisha ya kiroho.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger