Saturday, 5 April 2025

NELSON MANDELA KUNADI TAFITI ZAKE USWISI




Balozi wa Uswisi nchini Mhe. Nicole Providoli ( mwenye suti nyeupe) akipata maelezo kuhusu Kompyuta ya Kuchakata Taarifa kwa kasi kubwa ( HPC) kutoka kwa Afisa Tehama Bw. Mdoe Mwamunyange ( kulia) wakati wa ziara ya kikazi , wa kwanza kushoto ni Makamu Mkuu Taasisi ya Afrika Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Prof Maulilio Kipanyula.

.....



TAASISI ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela kushirikiana na Serikali ya Uswisi katika kufanya utafiti na ubunifu kama mkakati wa kukuza masoko ya kazi za tafiti na bunifu .

Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Arusha wakati wa ziara ya kikazi ya Balozi wa Uswisi nchini Mhe. Nicole Providoli, Makamu Mkuu wa Taasisi Prof. Maulilio Kipanyula ameeleza kuwa, Serikali hiyo imekuwa na ushirikiano wa karibu na NM-AIST katika miradi miwili ikwemo Kituo cha Mafunzo ya Kidigitali na Mradi wa Nishati inayotokana na mabaki ya mimea .

“Lengo kubwa la ziara ya balozi katika taasisi yetu ni kuona fursa zilizopo na namna ya kuendelea kushirikiana hasa katika eneo la sayansi, teknolojia na ubunifu, ukizingatia Uswisi wameendelea sana katika sekta hizi hivyo, ni fursa kwetu kujifunza na kujiunganisha na taasisi na kampuni kutoka huko ili kupata masoko ya bidhaa zetu” alisema Prof. Kipanyula

Ameongeza kuwa, eneo lingine la ushirikiano ni pamoja na wanasayansi wa Nelson Mandela kwenda uswisi huku Maprofesa wa uswisi kuja kufundisha na kufanya tafiti za pamoja kwa lengo la kuongeza ufanisi katika kubadilishana uzoefu na ujuzi.

Kwa Upande wake Balozi wa Uswisi nchini Balozi Nicole Providoli amefurahishwa na fursa zinazopatikana NM-AIST na kuahidi kuendeleza ushirikiano, kwa kufanya kazi kwa pamoja katika kubadilishana ujuzi na uzoefu ili kuleta matokeo chanya katika teknolojia, ubunifu na sayansi.

Balozi Nicole Providoli alipata wasaa wa kutembelea Kituo cha Elimu ya Kidigitali ( C-CoDE), Maabara ya Nishati Endelevu ( Sustainable Energy Lab) .pamoja na Kituo cha Tehama chenye Komputa ya Kuchakata Taarifa kwa kasi kubwa (HPC).


Makamu Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Prof. Maulilio Kipanyula ( kulia) akimkabidhi zawadi Balozi wa Uswisi nchini Mhe. Nicole Providoli ( kushoto) mara baada ya ziara ya kikazi.


Makamu Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Prof. Maulilio Kipanyula ( aliyenyoosha mkono kushoto) akielezea historia ya taasisi hiyo kwa Balozi wa Uswisi nchini Mhe. Nicole Providoli ( wa kwanza kulia) wakati wa ziara ya kikazi.


Makamu Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Prof. Maulilio Kipanyula ( aliyesimama) akielezea kuhusu Nelson Mandela Radio kwa Balozi wa Uswisi nchini Mhe. Nicole Providoli ( kulia) wakati wa ziara ya kikazi.


Balozi wa Uswisi nchini Mhe. Nicole Providoli ( katikati aliyekaa) akiuliza swali namna kituo cha elimu kidigitali kinavyofanya kazi ( C-CoDE) kwa Makamu Mkuu wa Taasisi Prof. Maulilio Kipanyula (kulia) wakati wa ziara ya kikazi na Kushoto ni Afisa Tehama wa kituo hicho Bw. Octavian Kanyengele.


Balozi wa Uswisi nchini Mhe. Nicole Providoli ( mwenye suti nyeupe) akipata maelezo kuhusu Kompyuta ya Kuchakata Taarifa kwa kasi kubwa ( HPC) kutoka kwa Afisa Tehama Bw. Mdoe Mwamunyange ( kulia) wakati wa ziara ya kikazi , wa kwanza kushoto ni Makamu Mkuu Taasisi ya Afrika Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Prof Maulilio Kipanyula.


Prof. Maulilio Kipanyula Makamu Mkuu wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Uswisi nchini Mhe. Nicole Providoli ( mwenye suti nyeupe) wakati wa ziara ya kikazi.
Share:

MASHINDANO YA KATAMBI U-17 CUP YAHITIMISHWA KWA KISHINDO! KATUNDA FC MABINGWA



Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Julius Mtatiro akikabidhi zawadi ya fedha kwa washindi wa mashindano hayo.

Na Marco Maduhu,SHINYANGA

MSHINDANO ya Katambi U-17 CUP yametamatika rasmi,huku Timu ya Katunda FC wakiibuka washindi wa michuano hiyo,baada ya kuifunga Busulwa Sec kwa mikwaju ya penati,na kisha kuondoka na Kombe pamoja na kitita cha pesa sh.milioni moja.
Fainali hiyo imechezwa Aprili 4,2025 katika Uwanja wa Chuo cha Ualimu Shinyanga SHYCOM,huku Mgeni Rasmi akiwa na Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Julius Mtatiro.


Mchezo huo umechezwa kwa kipindi cha dakika 90, na kuisha bila ya kufungana Magoli,na kisha kuchezwa mikwaju wa penati, na hatimaye Katunda FC kuibuka na ushindi wa Penati 4 kwa 3 dhidi ya Busulwa Secondari, huku mshindi wa tatu katika michuano hiyo akiibuka Ngokolo Secondari.
Mtatiro akitoa zawadi kwa washindi,amemtangaza mshindi wa Tatu ni Ngokolo Sekondari na wamepata Sh. Laki 5, Mshindi wa Pili Busulwa Sekondari sh.Laki 7, na mshindi wa kwanza Katunda FC sh,milioni 1.


Aidha, amempongeza Mbunge Katambi kwa kuendelea kuunga mkono michezo,kwamba kupitia mashindano hayo amekuwa akiibua vipaji vya vijana.
Katibu wa CCM wilaya ya Shinyanga Mjini Hamisa Chacha, amesema michezo ipo kwenye Ilani ya uchaguzi wa CCM, na kwamba Mbunge Katambi amekuwa Mbunge wa mfano kuendelea kuitekeleza Ilani hiyo, sababu michezo ni sehemu ya kuimarisha afya,kuibua vipaji pamoja na ajira.


Katibu wa Chama cha Mpira wa Miguu wilaya ya Shinyanga (SHIDIFA) Sylevester Budete, amempongeza Mbunge Katambi kwa kuendelea kuandaa mashindano hayo pamoja na kudhamini, huku akimuomba aendelee na jitihada hizo za kuinua michezo Shinyanga.
Nao baadhi ya vijana ambao wameshiriki mashindano hayo, wamemshukuru Katambi kwa kuonyesha vipaji vyao.


Mashindano hayo ya Katambi U-17 CUP yalizinduliwa Febuari 18,2025, na Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga John Siagi, katika Uwanja wa CCM Kambarage, na kushirikisha timu 16.


TAZAMA PICHA👇👇
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Julius Mtatiro akizungumza.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Julius Mtatiro (kulia)akimkabidhi Cheti cha Pongeza Katibu wa Mbunge Katambi,Samweli Jacksoni kwa niaba ya Mbunge kwa kuendesha mashindano ya Katambi U-17 CUP kutoka SHIDIFA.
Katibu wa CCM wilaya ya Shinyanga Mjini Hamisa Chacha akizungumza.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Julius Mtatiro akikabidhi Kombe kwa Washindi wa Mashindano ya Katambi U-17 CUP kwa Kampteni wa Timu ya Katunda FC.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Julius Mtatiro akikabidhi zawadi ya fedha kwa washindi wa mashindano hayo.
Awali Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Julius Mtatiro akisalimiana na wachezaji kabla ya mechi kuanza.
Katibu wa CCM wilaya ya Shinyanga Mjini Hamisa Chacha akisalimiana na wachezaji.
Mechi ya Fainali ikiendelea kuchezwa.
Picha za pamoja na wachezaji.
Share:

Friday, 4 April 2025

MBINU SHIRIKISHI NI MUHIMU KUHAKIKISHA WATU WENYE ULEMAVU WANAJUMUISHWA KATIKA NYANJA ZOTE– MHE. NDERIANANGA



NA. MWANDISHI WETU BERLIN – UJERUMANI

Naibu Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, na Uratibu, Mheshimiwa Ummy Nderiananga amesema ni muhimu kuwa na mbinu shirikishi ili kuhakikisha watu wenye ulemavu wanajumuishwa kikamilifu katika juhudi za maendeleo kitaifa na kimataifa.

Mhe. Ummy amesema hayo aliposhiriki katika mjadala wa: Kuelekea Hatua Jumuishi za Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi Kutoka Berlin hadi Belèm na Zaidi : wakati wa Mkutano wa Kimataifa wa Watu Wenye Ulemavu uliofanyika Berlin Ujerumani tarehe 2-3 Aprili, 2025.

Amesema kuwa ingawa serikali, wadau, na mashirika ya kimataifa wanafanya kazi ya kujenga jamii jumuishi, bado watu wenye ulemavu wanakabiliwa na changamoto nyingi.

“Changamoto hizi zinahitaji suluhisho la pamoja na la muda mrefu ili kuhakikisha fursa sawa na upatikanaji wa rasilimali kwa wote, bila kumwacha mtu yeyote nyuma,” alisisitiza Mhe. Ummy.

Akizungumzia mifano ya mafanikio katika sera za ujumuishi wa watu wenye ulemavu kwenye masuala ya tabianchi, Mhe. Nderiananga alisema kuwa Serikali ya Tanzania imeweka sera, sheria, na mikakati mbalimbali kuhakikisha ujumuishi wa watu wenye ulemavu, hususan katika masuala ya menejimenti ya maafa na mabadiliko ya tabianchi.

Alitaja juhudi muhimu zilizofanywa na serikali kuwa ni pamoja na: Mifumo ya Usimamizi wa Maafa, ili kuhakikisha uwakilishi wa watu wenye ulemavu na kuzingatia mahitaji yao katika kukabiliana na majanga na urejeshaji wa hali baada ya maafa; Sera za Mabadiliko ya Tabianchi, zinazolenga kuimarisha ustahimilivu wa watu wenye ulemavu kwa hatua za kukabiliana na athari za tabianchi;

Mikakati Jumuishi ya Kukabiliana na Maafa, ikizingatia njia salama za uokoaji na mipango ya kuwahamisha watu wenye ulemavu; na Misaada ya Kijamii na Kisaikolojia, ili kusaidia watu wenye ulemavu wakati wa majanga

Aliziambia nchi nyingine kuwa zinaweza kujifunza kutoka Tanzania kwa kushirikiana na mashirika ya watu wenye ulemavu, kuunda sera jumuishi, kuhakikisha miundombinu inafikika, kufanya tathmini za athari, na kutenga fedha maalum kwa ajili ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

“Hatua hizi zinahakikisha kuwa watu wenye ulemavu hawataachwa nyuma katika maandalizi ya kukabiliana na majanga na ustahimilivu wa tabianchi,” alisema, huku akialika mataifa mengine kuja Tanzania kujifunza juhudi zinazofanywa na serikali.

Kuhusu hatua mahsusi za ujumuishaji wa watu wenye ulemavu katika COP30 na sera za tabianchi, Mhe. Nderiananga alisema kuwa Tanzania imeweka mfumo madhubuti wa ujumuishaji watu wenye ulemavu katika mabadiliko ya tabianchi na usimamizi wa maafa kupitia sera, sheria, na miongozo mbalimbali.

Alisisitiza kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na COP na wadau wengine ili kuhakikisha ujumuishaji kamili wa watu wenye ulemavu katika hatua za kukabiliana na tabianchi na itaendelea kushirikiana na mataifa mengine na mashirika ya kimataifa kuhimiza ajenda ya ujumuishaji wa watu wenye ulemavu katika COP30.




Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger