Tuesday 10 September 2024

DKT BITEKO AWAASA MAMA NA BABA LISHE KUACHA KUTUMIA NISHATI ISIYO SAFI


NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt.Doto Biteko amesema kampuni ya Oryx Gas imekuwa ikitoa ushirikiano kwa Serikali na wamekuwa wakishiriki katika matukio mblimbali ya kugawa mitungi ya gesi na majiko yake kwa wananchi sambamba na utoaji mafunzo ya matumizi salama ya nishati safi ya kupikia.

Ameyasema hayo leo Septemba 8,2024 wakati wa Hafla ya Azimio la Kizimkazi iliyolenga kuunga mkono jitihada za Rais, Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan katika kuhamasisha matumizi ya Nishati safi ya Kupikia ambayo ilienda sambamba na uzinduzi wa Kampeni ya Pika Kijanja inayoendeshwa na kituo cha redio cha Bongo Fm na Televisheni ya TBC.

Aidha ametoa wito kwa Watanzania kuokoa maisha yao kwa kutumia Nishati Safi ya Kupikia ambayo itawaepusha na madhara yanayotokana na Nishati isiyo safi ikiwemo athari katika mfumo wa upumuaji.

Dkt. Biteko amesema, Rais Samia licha ya kuwa kinara wa Afrika kwenye kampeni ya kuhamasisha matumizi ya Nishati safi ya kupikia, pia amedhamiria kuwaondoa kina Mama na Baba Lishe wa Tanzania katika matumizi ya Nishati isiyo safi na pia kuboresha hali zao kwa kutumia Nishati safi ya Kupiki ambapo ametoa mitungi 2,000 kwa kundi hilo kama njia ya uhamasishaji wa nishati hiyo.

"Nipende kumpongeza sana Mhe Rais kwa kuibeba ajenda hii ya Nishati safi ya Kupikia na kwa maono aliyonayo, nitoe agizo kwa Watendaji wa Wizara ya Nishati kuhakikisha Wizara inashirikisha wadau kwenye kampeni hii ili iweze kufanyika kwa ufanisi na hivyo kumuunga mkono Mhe. Rais." Amesema Dkt. Biteko.

Akitoa takwimu za hali ilivyo kwa sasa, Dkt. Biteko amesema watu Bilioni 5.8 duniani ndio wanatumia Nishati Safi huku Bilioni 2.4 wakitumia Nishati isiyo safi ambapo Afrika Pekee ina watu milioni 933 wanaotumia Nishati isiyo safi na hivyo kuwataka wadau kuuganisha nguvu kuunga mkono matumizi ya Nishati iliyo safi.

Awali, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji amesema Serikali inatambua mchango mkubwa unaotolewa na Baba na Mama Lishe nchini na ndio mana kwenye hafla hiyo ya Azimio la Kizimkazi wamealikwa ili kuwahamasisha kuondokana na matumizi ya Nishati chafu na hivyo kuboresha mazingira yao ya ufanyaji kazi kwa kuwapatia Mitungi ya gesi kama Nishati mojawapo iliyo safi.

Amesema kimsingi muktadha wa Mhe Rais kama Kinara wa Nishati safi ya Kupikia Afrika ni utekelezaji pia wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) inayoelekeza Watanzania kupatiwa Nishati Safi ya Kupikia kwa wakati na kwa gharama nafuu na ndio maana mitungi takriban 450,000 iliamuliwa iuzwe bei ya ruzuku ili kuwafikia wananchi.

Akizungumza wakati akitoa salamu za Oryx kwa Serikali pamoja na wageni waalikwa Mkurugenzi Mkuu wa kampuni hiyo Benoit Araman amesema Oryx Gas Tanzania inafanya kazi bila kikomo kila siku ili kutekeleza maono ya Rais Samia ya kwamba asilimia 80 ya Watanzania ipate nishati ssafi ifikapo 2034.

“Mpango huu utafanikiwa tu ikiwa tumejitolea kutumia nishati safi ya kupikia kila siku.Leo hii katika muendelezo ule ule wa kuunga mkono jitihada za Rais Samia tunakabidhi mitungi ya gesi yq Oryx 1000 kwa Mama na Baba Lishe ambao wameungana nasi katika hafla hii ya Pika Kijanja.”

Pia amemshukuru Waziri wa Nishati, Dk Biteko na Naibu Waziri Kapinga kwa kuwashirikisha ambapo mbali ya kutoa mitungi ya gesi wametoa mafunzo yq matumizi salama ya nishati safi ya kupikia.

Akizungumzia faida na kutumia nishati safi ya kupikia ,Benoit amesema kiafya nishati safi inasaidia kuokoa maisha kwani kumekuwa na vifo vinavyotokana na magonjwa ya upuamuji yayanayosababishwa na matumizi yq nishati chafu.

“ Nchini Tanzania, wananchi 33,000 wanakufa kila mwaka kutokana na kuvuta pumzi ya moshi na chembe chembe zinazotokana na mkaa na kuni. Kupika na Oryx LPG kutasaidia kumaliza changamoto hiyo ya kiafya lakini kwa mazingira kupika kwa nishati safi huzuia ukataji miti na hivyo kulinda mazingira”

Ameongeza kuwa kupika kwa nishati safi husaidia kuzuia wanawake kufanya kazi ngumu ya kutumia muda mwingi kukusanya kuni kutoka msituni.Pia kupika kwa nishati safi husaidia kuwaweka wanawake katika hali ya usalama kwani porini kumekuwa na hatari nyingi.


Share:

Monday 9 September 2024

DAWA YA UHAKIKA KWA WANAOSUMBULIWA NA KUVIMBA MIGUU

Kutokana na mtindo wa maisha kubadilika sana ulimwenguni kutokana na ukuaji wa teknolojia, watu wengi wamekuwa wakisumbuliwa na tatizo la kuvimba kwa miguu.

Mimi ni miongoni mwa watu walioteswa sana tatizo hilo kwa zaidi ya miaka minne, nilitumia dawa za kila namna lakini sikuweza kupona hadi kusema huu ni ugonjwa wangu sasa, inanibidi nijifunze jinsi ya kuishi nao tu licha maumivu niliyokuwa napitia.

Jina langu ni Elina kutokea Kigoma, kuna siku niliamka na kukuta miguu yangu imevimba ghafla lakini sikuweza kujua sababu ni nini hasa.

Nilijua ni hali tu ya kawaida na  baada ya muda itaweza kupotea, hata hivyo haikuwa kama ambavyo nilitarajia kwani hali iliendelea kuwa mbaya zaidi hadi kuanza kutembea kwa shida.

Hatimaye niliamua kwenda Hospitali kupata tiba, nilitumia dawa za huko kwa muda mrefu bila matokeo ya aina yoyote ile, hali yangu ya kuvimba miguu iliendelea kunitesa sana.

Baadhi ya rafiki zangu walinishauri niende kwa waganga wakienyeji wakanicheki kama kuna majini nimetupiwa, nilifanya hivyo lakini wataalamu wale walikula fedha zangu bila kupata suluhisho.

Wengi walikuwa wanasema kuna mtu kaniloga hivyo nitoe fedha ili waweze kuniondolea shida hiyo lakini kwa bahati mbaya hakuna hata mmona aliweza kunisaidia kama ambavyo nilitarajia.

Pona yangu ilikuja siku moja ambapo nilisikia kwenye redio kuna mtu anaitwa Dr Bokko anaweza kunisaidia kushinda ugonjwa huo kwa kutumia dawa zake za mitishamba.

Nilisafiri hadi ofini kwake ambapo nilipokelewa vizuri kabisa na kupatiwa dawa ambayo iliniponya moja kwa moja ugonjwa huo ambao ulinitesa kwa miaka mitano.

Tangu wakati huo nimekuwa hata nikiwashauri watu wenye magonjwa sugu kwenda kwa Dr Bokko ambaye kwangu naona ni mtaalamu wa tiba za mitishamba namba moja hapa duniani.

Pia Dr Bokko anatibu magonjwa kama Kaswende, Kisonono, Kifua Kikuu, Presha na mengine mengi. Wasiliana naye kwa simu namba +255618536050.

Mwisho.


Share:

PROF. MKUMBO; SERIKALI HAITAKUWA KIKWAZO KWA AZAKI


Waziri wa Mipango na Uwekezaji Profesa Kitila Mkumbo akizngumza wakati akifungua Wiki ya AZAKI iliyoanza rasmi leo Septemba 9-13, 2024 Jijini Arusha.

Mkurugenzi Mtendaji wa The Foundation For Civil Society FCS - Justice Rutenge, akizunguza lipokuwa akitoa hotuba yake ya utanguliza wakati wa uzinduzi wa Wiki ya AZAKI , Jijini Arusha.
Mkurugenzi Mkazi wa Trademark Africa Elibariki Shammy, akizungumza katika mkutano huo.

PICHA NA FCS

Na; Hughes Dugilo, ARUSHA.

Waziri wa Mipango na Uwekezaji Profesa, Kitila Mkumbo amesema kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na Asasi za Kiraia nchini nakwamba haitakuwa kikwazo kwao katika shughuli zake za kuleta maendeleo, sanjari na kutoa mawazo yatakayojenga zaidi ili kutafuta fursa zilizopo ndani na nje ya nchi.

Profesa Mkumbo amesema hayo wakati akifungua Wiki ya Asasi za Kiraia (AZAKI) iliyoanza rasmi leo Septemba 9, 2024 jijini Arusha.

Profesa Mkumbo amsema ni vema sasa Asasi za Kiraia zikashirikiana na serikali katika kutoa maoni yao ikiwemo kukaa meza moja kutaua changamoto zinazoibuka sanjari na kutafuta fursa za masoko ya ndani na nje ya nchi katika kukuza uchumi

Prof. Mkumbo amesema, lengo kuu la serikali ni kuhakikisha ustawi wa watu wote unakuwa, na ili kufika huko ni vema zaidi kujifunza kupitia kwa watu, kuwa wabunifu na kutoa maoni katika kuhakikisha Dira ya Mendeleo ya Taifa ya mwaka 2050 inaleta tija zaidi hususan katika uwekezaji kwenye elimu, miundombinu ikiwemo umeme wa uhakika.

‘’AZAKI zihakikishe zinaisemea jamii changamoto ambazo wanaziona na kutatuliwa ili kuisaidia serikali kuzishughulikia na si kuilalamikia kuwa haifanyi kazi ilihali hawajazibainisha ili zifanyiwe kazi na jamii iweze kupata mabadiliko’’. Amesema Mkumbo.

Amesema nchi zilizoendelea zimepiga hatua katika maendeleo kwa sababu ya umeme hivyo uwepo wa Bwawa la mwalimu Nyerere nchini Tanzania hadi kukamilika kwake utawezesha umeme kupatikana kwa wingi ikiwemo uchumi kukua kupitia viwanda vinavyozalisha bidhaa ndani ya nchi na kuuza bidhaa hizo nje ya nchi kwakushirikiana na sekta binafsi hususan za kilimo .

Naye rais wa Foundation For Civil Society (FCS), Dk Stigmata Tenga amesisita kuwa lazima mabadiliko ya watanzania yatokee kupitia AZAKI ambazo ndio husemea wananchi wenye changamoto mbalimbali katika sekta za afya ,elimu, miundombinu ya barabara ikiwemo utoaji wa fursa za fedha kupitia taasisi mbalimbali zinazowawezesha wananchi kujikwamua kimaisha kupitia mikopo yenye riba nafuu na kuongeza kuwa rasilimali watu ni muhimu kuzingatiwa katika kuwaletea wananchi maendeleo.

Wakati huo huo, Mkurugenzi Mkazi wa TradeMark Africa Elibariki Shammy amesema mkakati wa serikali ni kuhakikisha biashara za kidigitali zinakua zaidi kwa kushirikisha vijana kwa kasi kubwa kupitia biashara kwa kuwawekea mazingira rafiki yatakayowasaidia kujikwamua kiuchumi kupitia fursa mbalimbali zilizopo nchini.

Awali Naibu Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU), Isabelle Mignucci ameshukuru ushikiano kati ya serikali ya Tanzania na mashirika mbalimbali unaoleta tija katika maendeleo sanjari na kuhakikisha vijana wanapata fursa za maendeleo kupitia teknolojia na ubunifu unaoleta tija zaidi katika ukuaji wa uchumi. 
Naibu Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU), Isabelle Mignucc akizunguza alipokuwa akitoa hotuba yake katika maadhimisho hayo Jijini Arusha.
Share:

FAMILIA YA MAREHEMU KING MAJUTO YAOMBA UMEME

Na Hadija Bagasha Tanga, 

Familia ya aliyekuwa mwigizaji maarufu hapa nchini Alhaji Amri Athumani maarufu kama 'King Majuto'   imeiomba Serikali kuwafikishia  huduma ya umeme katika makazi aliyokuwa akiishi msanii huyo ambapo aliacha Msikiti pamoja na Madrasa  vinavyotumika hadi sasa na jamii iliyopo.

Akizungumza kwa niaba ya familia mtoto wa tatu wa 'King Majuto'  Haruna Athumani  amesema kuwa bado jamii inaendelea kumuenzi na kumkumbuka msanii huyo kutokana na huduma alizozianzisha  ikiwemo Msikiti, Madrasa pamoja na Kisima ambavyo vinawanufaisha wananchi waliopo karibu yao.

"Tunashukuru sana Mkuu wa wilaya kututembelea na kutupa sadaka yake kwaajili ya Mzee wetu lakini pia niwaombe wadau wengine na viongozi wa Serikali kushiriki kwa njia moja ama nyingine kusaidia familia hii hapa tuna shida ya umeme  kwa sababu eneo hili mzee wetu alilianzisha yeye lakini sasa hivi kuna jamii ambayo ipo kwahiyo eneo hili kwa sasa Lina shida ya maji na umeme tukipata hivyo vitu tunashukuru sana kwasababu vitasaidia jamii iliyopo kwa sasa" alisema Haruna.

Familia imetoa ombi hilo mbele ya Mkuu wa wilaya ya Tanga Japhari Kubecha ambaye alitembelea na kudhuru kaburi la msanii huyo na kushiriki dua maalum ya kumwombea pamoja na familiya  yake katika Mtaa wa Kiruku kata ya Mabokweni halmashauri ya Jiji la Tanga.

Kufwatia ombi hilo la familia  Mkuu wa wilaya hiyo Japhari Kubecha amemwagiza kaimu katibu  tawala Mussa Machunda kuwasiliana na ofisi ya Shirika la umeme Tanzania 'Tanesco'  kuangalia uwezekano wa kumaliza changamoto  hiyo.

Amesema Serikali ya wilaya ya Tanga itaendelea kumtambua mchango wa msanii huyo ambaye amekuwa kielelezo kwa jamii kupitia kazi zake za sanaa alizozifanya kuelimisha  na kuburudisha katika nyanja mbalimbali.

"Ki ukweli Mzee Majuto' alikuwa ni msanii ambaye alimtumia sanaa yake kutuunganisha nchi yetu pamoja na kuikuza Lugha yetu ya Kiswahili, kila alipopata nafasi aliubeba utaifa maadili katika sanaa yake alihakikisha analinda heshima na hadhi ya maadili ya mtanzania tofauti na uigizaji wa sasa hivi "

"Kama Serikali sisi tunaahidi kuendelea kutoka mchango wetu kwa familiya ili kuenzi  kazi zake lakini kumtambua kama miongoni mwa wazee maarufu ambao kwa nafasi yake aliitangaza wilaya yetu ya Tanga  kupitia kazi zake, uvaaji wake  hii inaonyesha aliubeba uhalisia wa Tanga na desturi zake" alisema Kubecha.

Msanii King Majuto' mbaye alizaliwa  mwaka 1Augost 1948 Mkoani Tanga  na kufariki 8Augost 2018 aliwahi kutamba na filamu mbalimbali hapa nchini zikiwemo Mama ntilie, Sio sawa, Rent hause ,Mrithi wangu , Ndoa ya utata, Dala Dala, Nimekuchoka na nyinginezo.

Share:

FULL POWER ITAKUSAIDIA KUTIBU NGUVU ZA KIUME

  

Upungufu wa nguvu za kiume ni hali ya kushindwa kufanya tendo la ndoa kikamilifu ,shughuli ya tendo la ndoa huhusisha akili, homoni, neva, misuli, hisia na mirija ya damu. Upungufu wa nguvu za kiume huashiria kutokuwa sawa kiafya hivyo ni tatizo linalohitaji tiba.

CHANZO CHA TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME

Tatizo la nguvu za kiume lina vyanzo vingi ambavyo mara nyingi wengi huvipuuza, hivyo vyanzo huathiri taratibu na vingine huathiri haraka, tunashauri watu kuwa makini sana ili kujiimarisha vizuri. Kuna mitindo ya maisha inayoweza kukuweka hatarini kupata tatizo la nguvu za kiume nayo ni pamoja na;

1. Kuwa na halemu (Cholesterol) na Shinikizo la damu (B.P) au ugonjwa wa moyo

2. Kuvuta sigala na unywaji wa pombe

3. Uzito kupita kiasi na unene uliozidi

4. Ulaji holela wa vyakula vyenye mafuta mengi na sukari nyingi

5. Kisukari

6. Kuwa na mawazo na wasiwasi

7. Matumizi ya madawa mbalimbali

8. Umri hasa wazee

9. Utumiaji wa vinywaji vinavyobadili hali ya mwili

10. Kuwa na tatizo la kibofu

11. Tabia za kujichua kwa muda mrefu

12. Kutopata usingizi kamili

13. Matumizi makubwa ya dawa zenye kemikali za kutibia magonjwa kama kansa, vidonda vya tumbo, moyo, kisukari, B.P, na magonjwa mengine


DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME

Dalili za kuonesha kuwa una tatizo la upungufu wa nguvu za kiume karibia zote zinahusiana na hali itakayo onekana katika tendo la ndoa au mda wa kujamiiana, hizo dalili zake ni kama;


1. Kuwahi kufika kileleni

2. Kukosa hamu ya mapenzi

3. Kushindwa kurudia tendo la ndoa

4. Uume kusimama kwa ulegevu au kushindwa kusimamisha

5. Kuchoka sana baada ya tendo la ndoa na hata kukinai kabisa au hata kusikia kichefuchefu; Miguu, uso na tumbo kuvimba na kujaa maji

6. Kuhisi maumivu wakati wa tendo la ndoa au baada ya tendo hilo

7. Kuchelewa sana kufika kileleni (au kushindwa kufika kileleni kabisa)

8. Kukosa pumzi na uchangamfu wa mwili katika utendaji


TIBA SAHIHI YA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME

FULL POWER
⇨Ni dawa ya vidonge ya miti shamba inaongeza nguvu za kiume na kutibu kabisa tatizo hilo.

⇨Inaongeza hamu ya tendo la ndoa

⇨Inakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya Dakika 30 na kurudia tendo zaidi ya mara nne na zaidi.


ZAT 50
⇨ Inarutubisha maumbile ya uume na kunenepesha urefu nchi 6,unene sentimita 4

⇨Dawa hii ni ya kutibu kabisa tatizo hilo.


Pia tunatibu Magonjwa mengine kama

Matatizo ya pumu,Bawasiri, vidonda vya tumbo, Kisukari, Magonjwa sugu ya zinaa,Kaswende,U.T.I , kiuno,miguu kuwaka moto, Fangasi sehemu za Siri, kupunguza unene wa mwili,tumbo kuunguruma,kujaa gesi, matatizo ya uzazi kwa wanawake, kurutubisha mbegu za uzazi kwa akina baba, matatizo ya meno tunatibu bila kung’oa


Ndugu mteja Epuka midawa inayouzwa mitaani ambayo sio sahihi kwa matumizi ya binadamu JALI AFYA YAKO OKOA NDOA NA MAISHA YAKO

Kliniki yetu inapatikana Zanzibar, Dar es salaam na Shinyanga

Wasiliana nasi kwa simu namba 071770 22 27 au 0754568767  utatumiwa sehemu yoyote ulipo
Share:

Video Mpya : NZALA ITALASHILA - BHOHABHE

 

Share:

Sunday 8 September 2024

WAJASIRIAMALI KUWEZESHWA ZAIDI KUPITIA PROGRAMU YA KUENDELEZA BIASHARA YA WAZAWA YA BARRICK

Mkuu wa wilaya ya Nyang'wale Mhe. Grace Kingalame akiongea katika hafla hiyo.
***
Wajasiriamali 150 kutoka wilaya za Kahama,Nyang’hwale na Msalala wamehitimu mafunzo ya siku 10 ya biashara kupitia Kupitia Programu ya Kuendeleza Biashara za Wazawa (Local Business Development Program) inayotekelezwa na Mgodi wa Dhahabu wa Barrick Bulyanhulu, yaliyolenga kuwajengea uwezo na kuwasaidia waweze kunufaika na fursa zilizopo kwenye sekta ya madini.

Mahafali ya kuhitimu mafunzo hayo ilifanyika mwishoni mwa wiki katika hoteli ya Kitapela,Kakola na kuhudhuriwa na wageni mbalimbali waalikwa wakiwemo wakufunzi, Maafisa wa Serikali, Taasisi za Kifedha na mgeni rasmi alikuwa ni Mkuu wa wilaya ya Nyang'wale Mhe. Grace Kingalame.

Akiongea na wahitimu kabla ya kuwakabidhi vyeti vya kuhitimu mafunzo,Kingalame alipongeza mgodi wa Barrick Bulyanhulu kwa kuandaa mafunzo hayo na aliwataka Kutumia maarifa waliyoyapata Kuleta mabadiliko chanya katika biashara zao sambamba na kuchangamkia fursa za kibiashara zilizopo katika sekta ya madini hususani katika mgodi wa Barrick Bulyanhulu na makampuni mengine yaliyopo katika ukanda huo.

Alisema mafunzo haya yaliyoandaliwa na mgodi wa Barrick Bulyanhulu yamefanyika kwa wakati mwafaka ambao mbali na kulenga kuwawezesha wajasiriamali kuchangamkia sekta zilizopo katika sekta ya madini pia Serikali imetenga mikopo mingi kwa ajili yao ambapo ili kunufaika nayo ni muhimu kupatiwa mafunzo ya kibiashara ili Wale watakaopata Mikopo waweze kuirejesha kwa wakati.

Awali Akiongea kwa Niaba ya Kaimu Meneja Mkuu wa Mgodi wa Barrick Bulaynhulu, Abdallah Kipara, alisema Mgodi Umeweka Kipaumbele katika kuhakikisha mipango ya Serikali inayolenga jamii inafanyika kwa ushirikiano mkubwa na wadau wote kwa kuamini kwamba mafanikio ya mgodi yatakuwa Endelevu ikiwa yatachochea na kuchangia katika kuboresha maisha ya wanajamii wanaotuzunguka.

“Tunajivunia kwa kuongoza njia kwa kufanikiwa kuendesha program hii ya maendeleo ya biashara kwenye maeneo yanayozunguka migodi na tumetimiza wajibu zaidi ya sheria ya maudhui ya ndani (Local content) na tutaendelea kuunga mkono maendeleo ya kampuni ndogo na za kati ambazo ni muhimu sana katika ukuaji wa uchumi wa nchi,” alisema Kipara.

Baadhi ya Washiriki waliohudhuria Mafunzo hayo walisema fursa ya mafunzo hayo waliyoyapata yatawasaidia kukuza biashara zao sambamba na kuchangamkia fursa mbalimbali za biashara ili kuendana na teknolojia na masoko ya kisasa .
Wajasiarimali 150 waliohitimu mafunzo hayo walitunukiwa vyeti vya ushiriki.
Mwakilishi wa Kaimu Meneja Mkuu wa Mgodi wa Barrick Bulaynhulu, Abdallah Kipara
Kaimu Meneja kitengo cha Mahusiano ya Jamii na Mazingira Zuwena Senkondo
Baadhi ya wahitimu wakipokea vyeti kutoka kwa mgeni rasmi
Baadhi ya wahitimu wakipokea vyeti kutoka kwa mgeni rasmi
Baadhi ya wahitimu wakipokea vyeti kutoka kwa mgeni rasmi
Baadhi ya wahitimu wakipokea vyeti kutoka kwa mgeni rasmi
Baadhi ya wafanyakazi wa Barrick katika hafla hiyo
Wageni waalikwa katika hafla hiyo
Baadhi ya wahitimu katika picha ya pamoja na mgeni rasmi
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger