Monday, 27 November 2023

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU NOVEMBA 27,2023






Share:

Sunday, 26 November 2023

MAKATIBU WAKUU WAFANYA ZIARA HANDENI WANAPOHAMIA WAKAZI WA NGORONGORO


Makatibu Wakuu wakikagua maendeleo ya ujenzi nyumba na miundo mbinu ya kuhamisha wananchi wanaotoka eneo la Hifadhi ya Ngorongoro kwenda Kijiji cha Msomera Wilaya ya Handeni  wakati wa ziara yao mkoani Tanga.

Na Mwandishi wetu - Tanga

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge na Uratibu, Dkt. Jim Yonazi Dkt. Yonazi amesema Serikali imejipanga katika kuhakikisha kuwa wizara zote za kisekta zinashiriki kikamilifu katika kuhakikisha kuwa miradi iliyopo katika Kijiji cha Msomera inakamilika kwa wakati ili kuwezesha wananchi wanaoendelea kujiandikisha kuhamia katika eneo hilo ili kuendelea shughuli zao. 

Dkt. Yonazi aliyasema hayo wakati  wa ziara ya kikazi  ya Makatibu Wakuu wa Wizara za kisekta waliyoifanya katika  Kijiji cha Msomera, Wilaya, Handeni mkoani Tanga kujionea hatua mbalimbali za ujenzi wa miundombinu  kabla ya kuanza kwa awamu ya pili ya kuhamisha wananchi wanaoishi katika hifadhi ya Ngorongoro waliojiandikisha kuhama kwa hiari.

Amesema Makatibu Wakuu  hao wamekagua ujenzi wa miundo mbinu mbalimbali ikiwemo maji, umeme, madaraja, barabara, shule, Nyumba za makazi na uboreshaji wa huduma za mawasiliano.

“Niwaombe wanaohamia eneo hili waiamini Serikali kwamba inawatengenezea mazingira yaliyo bora sana hapa Msomera, nyumba  zinazojengwa  na huduma zote zina ubora ili wananchi wetu wanufaike  na Serikali yao waachane na upotoshaji kwa sababu imewekeza fedha nyingi kuhakikisha wanaishi katika mazingira salama,”Amesema Dkt. Yonazi.

Naye  Kamanda wa Kikosi  Kazi cha Ujenzi wa nyumba 5000  kutoka Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Brigedia Jenerali Hassan Mabena amesema kila taasisi ya kisekta na Wizara  zinawajibika ipasavyo kuhakikisha ujenzi huo unakamilika kwa wakati  akisema kuwa  licha ya changamoto za mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali lakini kazi inaendelea vizuri .

“Mpaka sasa ujenzi wa Msomera  ambao tumeugawanya katika vitalu kuanzia A mpaka D tuko katika hatua mbalimbali za ujenzi nyumba 1000 katika eneo la Msomera B kitalu F viwanja 768  taratibu zake zimekamilika eneo liko tayari kwa ajili ya uchimbaji na kuanza msingi na kuendelea na hatua za ujenzi,”Ameeleza Brigedia Jenerali Mabena.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mhe. Albert Msando  amewashukuru Makatibu Wakuu hao kwa kutembelea mradi huo hatua inayoongeza kasi yake kusonga mbele akiahidi kusimamia kwa karibu mradi huo ambao umefanyika kama hatua ya kuboresha maisha ya watanzania kila mwananchi kuishi katika hali ya ustawi pamoja na uwepo wa miundo mbinu muhimu pamoja na huduma za kijamii.

“Hii inaonyesha nia ya dhati ya Serikali  ya kukamilisha mradi huu muhimu kwa wakati siyo tu kuhamisha watu lakini unaenda kuboresha maisha ya watanzania tunaendelea kuwaahidi kwamba tutasimamia kwa karibu tunajua unatekelezwa wakati wa mvua ambapo kwetu ni fursa ya kuona namna ya kuyavuna maji  kwa ajili ya matumizi,”Amebainisha  


Aidha Mwenyekiti wa Kijiji cha Msomera Bw. Martin Oleikayo Paraketi amempongeza Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kufanya mradi huo akisema umekuja kwa wakati muafaka kwani umesaidia  wakazi waliokuwa wakiishi katika maeneo hayo kupata huduma muhimu zikiwemo mawasiliano, ujenzi wa shule za sekondari, kituo cha afya na barabara.

“Hii kwetu ni neema kubwa sana Serikali inafanya kazi kubwa na niwaambie waliopo Ngorongoro wasikubali kupotoshwa na watu wachache wasio na nia njema  kijiji cha Msomera ni kijiji mojawapo  kati ya Vijiji 91 ndani ya Wilaya ya Handeni mradi huu umeleta faida kubwa kupitia wenzetu waliohamia kutoka Ngorongoro,”Amepongeza Mwenyekiti huyo.



Share:

RC SENYAMULE AWATAKA VIJANA KUCHANGAMKIA FURSA YA KILIMO BIASHARA

 


Na Okuly Julius-Dodoma

MKUU wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule, amewataka vijana kuchangamkia fursa za kilimo biashara ili kuinua uchumi wao, kuongeza pato la Taifa na kutatua changamoto ya ajira.

Senyamule ametoa wito huo Novemba 24,2023 jijini Dodoma , wakati akifunga kongamano la siku tatu la kujenga uelewa na kubadilishana uzoefu kwa wadau wa kilimo liloandaliwa na Taasisi ya Kuendeleza Mifumo ya Kimasoko katika Kilimo (AMDT).

Amesema watu walikuwa wakiongelea kilimo kwa dhana tofauti kuwa wanaofanya shughuli hizo ni maskini lakini ukweli ni kwamba kutokana na mapinduzi yaliyofanyika katika sekta hiyo kilimo ni utajiri.

“Katika hizi siku tatu mlizokaa hapa mtoke na maadhimio ambayo yatawawezesha wananchi wetu wanaojihusisha na shughuli za kilimo kuwa na uratibu wa pamoja,"

Na kuongeza kuwa:”Tunataka kundi kubwa la vijana liingie katika kilimo kwasababu huko kuna utajiri, watainu vipato vyao, wataongeza pato la taifa na kututa changamoto ya ajira kwasababu watajiajiri na kuajiri wengine.

Katika hatua nyingine Senyamule, amempongeza Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kwa utashi wake na kuweka nguvu kubwa katika sekta ya kilimo.

Amesema katika uongozi huu wa serikali ya Awamu ya Sita imebadili sekta ya kilimo na kuwa chanzo cha uchumi wa Mtanzania



“Namshukuru Rais Dk.Samia kwasababu ya utashi wake ambao unafanya sekta ya kilimo inaendelea kuimarika siku hadi siku. Watu walikuwa wakiongelea kilimo kwa dhana ya umaskini lakini sasa hivi kila mtu anatamani kufanya kilimo kwani utajiri upo hukom”amesema Senyamule 

Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa AMDT Charles Ogutu, alisema, kongamano hilo limehusisha wadau kutoka katika sekta mbalimbali za maendeleo lengo ni kujifunza na kubadilisha uzoefu.

Amesema kongamano hilo pia lilihusisha wadau maalumu ambao wanahusika na kukopesha fedha na vifaa kwa ajili ya kuwawezesha wakulima kuinuka na kufanya kilimo chenye tija.

“Wadau wamekubaliana kuwa na mikakati ya kujisimamia wwenyewe kwasababu tunamini kuwa tunaweza kufanya mambo makubwa zaidi. Baada ya kutoka hapa kila mtu atatumia kile alichojifunza na kuingiza katika mpango mkakati wake,"ameeleza Ogutu

Naye Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini wa AMDT Dk.Mary Shetto alisema katika kipindi cha mwaka mmoja wamefikia wakulima zaidi ya 100,000 katika mikoa mbalimbali

Amesema wameweka kipaumbele katika uzalishaji wa zao la alizeti kwasababu ndio zao ambalo serikali inatumia fedha nyingi kuagiza mafuta nje ya nchi.

“Lengo la kuweka nguvu kubwa katika uzalishaji wa zao la alizeti ni kuunga mkono jitihada za serikali za kuongeza uzalishaji wa zao hilo ili kukidhi mahitaji na kuepuka uagizaji wa bidhaa hiyo nje ya nchi,”amesema Shetto

MATUKIO KATIKA PICHA WAKATI WA UKAGUZI WA MABANDA YA WATAALAMU WA KILIMO NA WAUZAJI WA VIFAA MBALIMBALI VYA KILIMO.


Share:

NEC: MWITIKIO NI MKUBWA UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA KATA ZA NG'AMBO NA IKOMA




Mkurugenzi wa Daftari na Tehama , Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC Bw. Geofrey Mpangala akishuhudia wakati msimamizi wa kituo cha Masempele katika Kata ya Ng'ambo , Bi. Mwatano Juma Gervas, akimkabidhi kadi ya mpiga kura Wilson Shango mwananchi wa Kata ya Ng'ambo Halmashauri ya Tabora mara baada ya kujiandikisha katika kituo cha Masempele.
Mkurugenzi wa Daftari na Tehama , Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC Bw. Geofrey Mpangala akipata maelezo kutoka kwa msimamizi wa kituo cha Masempele katika Kata ya Ng'ambo , Bi. Mwatano Juma Gervas wakati akichukua taarifa za Wilson Shango mpiga kura wa Kata ya Ng'ambo Halmashauri ya Tabora alipokuwa akijiandikisha katika kituo cha hicho.
Afisa Tehama Mkuu Tume ya Uchaguzi NEC Bw. Lazaro Madembwe akishuhudia wakati Mwandishi Msaidizi Tume ya Uchaguzi Bw. Mwandishi Msaidizi NEC Bw. Emmanuel Madaha alipokuwa akichukua taarifa na mmoja wa wananchi waliofika kwenye kituo cha Masempele ili kujiandikisha kwenye daftari la Kudumu la Mpiga kura katika Halmashauri ya Tabora.
Gasper Kiswaga Msimamizi wa kituo cha Kizigo akiendelea kuchukua taarifa za mpiga kura Zuhura Masoud aliyefika kujiandikisha katika kituo cha Kizigo Halmashauri ya Tabora mkoani humo.
Akimu Gervas Kinyaga Mwandishi Msaidizi Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC akimuandikisha Bw. Simon Nicholas Mlimanazi katika kituo cha kujiandikisha cha Kizigo Halmashauri ya Tabora.
************
Na Mwandishi Wetu, Tabora.
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imesema zoezi la uboreshaji wa majaribio wa daftari la kudumu la mpiga kura katika Kata za Ikoma iliyoko wilayani Rorya mkoani Mara na Kata ya Ng'ambo iliyoko Halmashauri ya Manispaa ya Tabora, Mkoa wa Tabora linaendelea vizuri, huku kukiwa na mwitikio mkubwa wa watu.


Akizungumzia zoezi la uboreshaji wa majaribio ya daftari la kudumu la wapiga kura katika kituo cha Masempele, Kata ya Ng'ambo Mkurugenzi wa Daftari na Tehama , Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC Bw. Geofrey Mpangala, amesema , kuwa zoezi linaendelea vizuri na hadi kufikia Novemba 24, 2023 mwitikio wa wananchi ni mkubwa.


Amesema Kata ya Ikoma kuna vituo sita na kata ya Ng'ambo vituo kumi ambapo kwa kata ya Ikoma jumla ya wapiga kura 310 walijiandikisha na walioboresha taarifa zao walikuwa 71. Hata hivyo hakuna aliyeondolewa kwenye daftari la mpiga kura.


Ameongeza kuwa kwa Kata ya Ng'ambo jumla ya wapiga kura wapya 484 walijiandikisha, huku walioboresha taarifa zao wakiwa 309 na aliyeondolewa kwenye daftari la mpiga kura alikuwa mtu 1 tu.


Takwimu za Jumla mpaka jana kwa kata zote mbili wapiga kura wapya waliojiandikisha walikuwa 704 na walioboresha taarifa zao walikuwa 380 huku aliyeondolewa kwenye daftari alikuwa mmoja.


"Tunao mfumo wa kuboresha taarifa za wapiga kura kwa njia ya mtandao (OVRS ) Lakini mpaka sasa hakuna aliyeboresha taarifa hizo kwa njia ya mtandao. Hivyo, kuna kila sababu ya kuelimisha zaidi wananchi ili wauelewe zaidi mfumo huo wa kuboresha taarifa zao kwa njia ya mtandao na waweze kuutumia", Amesema Mpangala.


Naye msimamizi wa kituo cha Masempele katika Kata ya Ng'ambo , Bi. Mwatano Juma Gervas, amesema kuwa zoezi linaendelea vizuri kwani wapiga kura wote wanaofika katika Kituo hicho wanafuata taratibu zote za uandikishaji kwa kutoa taarifa zao muhimu kwa ajili ya kuandikishwa au kuboresha taarifa zao.


Aidha, mpiga kura aliyefika katika Kituo cha Kizigo kwa ajili ya kujiandisha Bw. Simon Mlimanazi, amesema kuwa zoezi linaendelea vizuri kwani katika kituo hicho amepata huduma kwa wakati na amekamilisha taratibu zote hatimaye amekabidhiwa kadi yake ya mpiga kura.


Ametoa wito kwa wakazi wa eneo hilo kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kabla muda haujaisha na kuboresha taarifa zao katika daftari la kudumu la mpiga kura kwakuwa hili ni jambo muhimu kwa maendeleo ya Taifa.


Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) hivi karibuni ilitangaza kuanzia tarehe 24 hadi 30 Novemba, 2023 kuanza zoezi la uboreshaji wa majaribio wa daftari la kudumu la wapiga kura katika Kata ya Ng’ambo iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Tabora, Mkoa wa Tabora na Kata ya Ikoma iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Rorya, Mkoa wa Mara .
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI NOVEMBA 26,2023

Share:

Friday, 24 November 2023

TABORA,MARA WAANZA UBORESHAJI WA MAJARIBIO WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA


Uboreshaji wa Majaribio wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura umeanza leo Novemba 24,2023 katika Kata ya Ikoma iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Rorya na Kata ya Ng’ambo iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Tabora.


Mjumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji wa Rufaa Mhe. Mwanaisha Kwariko ametembelea vituo vya kuandikisha wapiga kura katika Kata ya Ikoma na kushuhudia wananchi wa kata hiyo wakijitokeza kujiandikisha na kuboresha taarifa zao.


Akizungumza baada ya kutembelea vituo hivyo, Mhe. Mwanaisha amesema wananchi wa Kata ya Ikoma wamejitokeza mapema kwenye vituo na uboreshaji unafanyika kwa amani na utulivu.


Hivyo ametoa wito kwa wananchi wa Kata ya Ikoma ambao wana sifa za kujiandikisha na wale wanaotaka kuboresha taarifa zao wajitokeze kwa wingi ili kuboresha taarifa zao.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Bw. Ramadhani Kailima akizungumza na wananchi na wapiga kura waliojitokeza kujiandikisha na kuboresha taarifa zao kwenye Kituo cha Kuandikishia Wapiga Kura cha Shule ya Sekondari Kazehill iliyopo Kata ya Ng'ambo Halmashauri ya Manispaa ya Tabora, mkoani Tabora.


"Tume inafanya majaribio ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwenye kata hiyo kuanzia leo tarehe 24 hadi 30 Novemba, 2023. Uboreshaji huo unafanyika pia katika Kata ya Ikoma iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Rorya, mkoani Mara",amesema.


Mkurugenzi wa Uchaguzi ametembelea vituo vyote 10 vya kuandikishia wapiga kura kwenye kata hiyo. Zoezi hilo linaendelea vizuri ambapo vituo vimefunguliwa saa 2:00 asubuhi na vitafungwa saa 12:00 jioni.








Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger