Friday, 5 May 2023

HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA TANGA BOMBO KUNUNUA BASI LA WATUMISHI.

 

Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Juma Ramadhani katika akizungumza wakati wa maadhimisho ya siku ya wauguzi duniani katika Viwanja vya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo kushoto Katibu wa Hospitali hiyo Abdiely Makange na kulia ni Muuguzi Mkuu wa Mkoa wa Tanga Peter Chambo
Meza kuu wakifuatilia matukio mbalimbali katika maadhimiosho hayo
Katibu wa Tana Tawi Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Mwanaisha Nyangasa akisoma risala 
Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Juma Ramadhani wa pili kutoka kushoto akiwa na Katibu wa Hospitali hiyo Abdiely Makange wakitembelea mabanda mbalimbali wakati wa maadhimisho hayo
Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Juma Ramadhani akizungumza wakati alipotembelea mabanda mbalimbali
Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Juma Ramadhani katikati akipata maelezo  wakati alipotembelea mabanda mbalimbali kulia ni Katibu wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Abdiely Makange
Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Juma Ramadhani kulia akiwa na watumishi wa Hospitali hiyo wakati wakiwasha mishumaa walipoingia wodini kwa ajili ya kugawa zawadi na kuwafariji wagonjwa
Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Juma Ramadhani kulia akigawa zawadi kwa mgonjwa aliyelazwa kwenye Hospitali hiyo ikiwa ni maadhimisho ya siku ya wauguzu Duniani 
Muuguzi Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Andrew Tusiwe akigawa zawadi kwa wagonjwa katika hospitali hiyo
Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Juma Ramadhani akiwa na Katibu wa Hospitali hiyo kulia Abdiely Makange wakielekea kwenye maadhimisho ya siku wa wauguzi baada ya kupokea maandamano

Maandamano ya wauguzi kutoka Kituo cha Toyota kuelekea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo ikiwa ni kuadhimisha siku ya wauguzi duniani

Wauguzi wakiwa kwenye maandamano hayo

Wauguzi wakianza maandamano ikiwa  ni siku ya maadhimisho ya siku ya wauguzi Duniani
Mkuu wa Idara ya Tehama katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo William Masika akicheza wakati wa maandamano hayo ya siku ya wauguzi duniani yalipopokelewa
Mkuu wa Idara ya Tehama katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo William Masika akicheza wakati wa maandamano hayo ya siku ya wauguzi duniani yalipopokelewa
Sehemu ya wauguzi na wanafunzi wa chuo cha uunguzi wakifuatilia maadhimisho hayo
Sehemu ya wauguzi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa maadhimisho hayo

Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo katika aliyesimama akiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kumalizika kwa maadhimisho hayo



Na Oscar Assenga,TANGA 

KAIMU Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Juma Ramadhani leo amewaongoza wauguzi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa kwenye maaadhimisho ya siku ya Wauguzi Duniani ambapo kilele chake kitafanyika Mei 12 Jijini Mwanzasiku ya wauguzi Duniani. 

Maadhimisho hayo yalianza na maandamano kutoka eneo la Toyota mpaka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo kulipofanyika kilele cha maadhimisho hayo

Akizungumza wakati wa maadhimisho hayo,Dkt Juma alisema kutokana na uwepo wa changamoto ya usafiri kwenye mkoa huo ambayo ilielezwa wakati wa risala ya wauguzi hao alieleza mipango ya uongozi wa hospitali hiyo kwenye bajeti zijazo na jitihada walizoweka kama taasisi wana mpango wa kununua basi ili kupunguza adha ya usafiri kwa watumishi. 

Dkt Juma alisema basi hilo kwa ajili ya Hospitali hiyo ambalo linaweza kupunguza changamoto ya uchelewaji kazini kutokana na hali hiyo na kwamba tayari wameshaliona na wameliweka kwenye mpango wao kuweza kulitatua 

“Hili la changamoto ya kuchelewa kazini kutokana na changamoto ya usafiri kwenye mkoa wetu hilo tumeliona kama uongozi wa Hospitali kwenye bajeti zijazo na jitihada tulizowekeza taasisi wana mpango wa kununua basi kwa ajili ya hospitali ambalo linaweza kupunguza changamoto ya uchelewaji kazini “Alisema Kaimu Mganga Mfawidhi Dkt Juma. 

Awali akisoma risala hiyo Katibu wa Tana Tawi Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Mwanaisha Nyangasa alisema maadhimisho hayo ni kutafakari na kufauta nyayo za mwanzilishi wa huduma za uuguzi na ukunga Bi Florence Night Ngare. 

Alisema wauguzi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo wamemuenzi kwa kutoa huduma mbalimbali wakati wa maadhimisho hayo ikiwemo za uchunguzi wa saratani ya kizazi na matiti kwa wakina mama ,uchunguzi wa kisukari na macho,shinikizo la damu,kuhamasisha uchangia damu ,upimaji wa VVU kwa hiari na sambamba na utoaji elimu ya afya na lishe kwa wateja mbalimbali 

Aidha alisema pia katika maadhimisho hayo wametoa chanjo za Covid 19 ambapo wananchi waliohudumiwa tokea walipoanza maadhimisho hayo ni 154 ambao walihudumiwa kwa siku moja. 

Hata hivyo alisema kwamba Ukunga ni kada muhimu sana katika kufanikisha utoaji wa huduma nzuri za afya kwenye jamii na unapozungumzia afya bora muuguzi ni sehemu sahihi ya kufanikisha kila mtanzania anakuwa na afya bora. 

Alisema kwamba pamoja hayo kuna mafanikio makubwa ikiwemo mazingira ya kufanyia kazi yameboresha na miundombinu ya hospital na kuwezesha wanafanyakazi kufanya kazi kwenye mazingira mazuri. 

Aidha alisema kwamba pia ni wauguzi kupata nafasi ya kujiendeleza kimasomo,wauguzi kupata motisha mbalimbali,kuongezeka kwa hamasa kwa wauguzi . 

Akizungumzia changamoto wanazokabiliana nayo alisema kwamba changamoto kubwa ni upungufu wa watumishi idara ya ukunga na uuguzi kulingana na mahitaji ya jamii kutokana na kuongezeka kwa vitengo na idara ambazo wauguzi wanahitajika. 

Alisema pia changamoto nyengine ni kuchelewa kufika kazini kwa watumishi kutokana na kuwepo kwa changamoto ya usafiri kwenye mkoa wa Tanga hivyo upo umuhimu wa uwepo wa usafiri. 

Mwisho.
Share:

GONJWA LILILO NIKOSESHA NDOA ZA KIFAHARI

Ninayo bahati ya kupendwa yoyote ambaye nimeishi naye katika ukuaji wangu analijuwa hili tayari nilianza kusumbuliwa na wanaume wa kila rika kuanzia niko na umri mdogo sana.Nilipojitambua tu nikaachana na tama za wanaume na kuamuwa kuwa na mwanaume mmoja ambaye atanipenda na kujitambulisha kwa wazazi na mimi niwe wake wa kudumu.

Ethan, ndiye alikuwa mwanaume wangu wa kwanza kumpenda naye pia akanipenda sana tumekuwa naye kwenye kipindi cha mahusiano na uchumba tukachunguzana na kujuwana vizuri kwa muda wa miaka mine bila ya yoyote yule kuona changamoto yoyote juu ya mwenzake.

Sasa kipindi kirefu kilikuwa kimepita na sisi tukakubaliana kama wapenzi ni muda sahihi wa kuwashirikisha wazazi wa pande zote mbili lakini kabla ya kufanya hivyotukaamuwa tupime magonjwa yote nilishangazwa sana na majibu yalitoka kuwa mimi ni mgonjwa wa ukimwi lakini cha ajabu Ethan mpenzi wangu hakuwa na ugonjwa huo, sikuelewa ni nini kinanitokea lakini nikajua kuwa mapenzi yangu na Ethan yameishia hapo na kweli kuanzia siku ile Ethan hakuwahi kunitafuta tena hata jumbe zangu zote nilizomtumia hakujibu yoyote ile.

Siku zikasogea nikaamua nikapime mwenyewe baada ya wiki majibu yakaja kuwa siko na Ukimwi na mimi ni mzima wa afaya nilijaribu kumtafuta ethan alijuwe hilo lakini sikumpata wala sikuwa kwenye akili yake tena.Nikapata mpenzi mwingine jina lake aliitwa Kelvin naye tukawa kwenye mahusiano kwa miaka miwili ila ilipofika wakati wa kupima ukimwi awamu hii nikiwa ninajiamini kwa kuwa nilikwisha kupima mara ya mwisho lakini maajabu akaja kwenye majibu nilikuwa muathirika tena wa ukimwi kwa mara nyingine ya pili.

Likanikondesha tena na kunipa mawazo naye Kelvin akaniambia kuwa hawezi kumuoa mwanamke muathirika pia akaniacha nikawa singo tena upya.

Nilikata tamaa nikajua kuwa mimi niwa kufariki nikaamua nikapime tena peke yangu tena hospitali tofauti nikakuta siko na ugonjwa wowote mimi ni mzima sio muathirika.

Kwa urembo wangu nikajua kuwa haitochukua muda nitapata mtu na kweli nilipata mwanaume mwingine upendo wake ulikuwa wa juu zaidi ya wote niliokuwa nao mwanzoni ilipofika wakati wa kupima tena nilikutwa mimi ni muathirika wa ugonjwa wa ukimwi.

Nikaamua nimwambie ukweli mpenzi wangu kuwa hali hiyo huwa inatokea nikipima na mtu ila nikipima mwenyewe nakutwa ni mzima siko na ugonjwa wowote ule.Kwa upendo wake wa dhati na kwa kujuana kwake na daktari BAKONGWA ambaye alimsaidia kupata ajira huko TRA akanishauri tumtafute kwenye nambari zake za whatsapp +243990627777.

Tukafanya hivyo daktari Bakongwa alifanya mambo yake kisha akaniambia kuwa hali hiyo ni ya kutengenezwa na aliyekuwa mpenzi wangu kipindi cha nyuma sana hakupendezwa na mimi kumuacha na kuamua kunifanyia ukimwi wa kutengenezwa ili nisiolewe.Daktari alinipa dawa ya kutumia na kujilinda ambayo nilitumia siku nne kisha tukaenda kupima tena hospitali ileile tuliyokwenda mwanzoni kila mmoja alishangaa hata madaktari nao walishangaa kuona mimi sio mgonjwa ni mzima wa afya sio muathirika nimepona.

Nakushukuru sana daktari kwa kunitatulia shida hii nisingeolewa na isingekuwa wewe nitakuja kukushukuru vizuri huko kwenye tovuti zako https://bakongwadoctors.com .


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA MEI 5,2023



Share:

Thursday, 4 May 2023

TAMISEMI YATOA MAFUNZO KWA WASHITIRI


Mshauri Mwandamizi katika Usimamizi na Usambazaji wa Dawa kutoka HPSS Bi.Fiona Chilunda,akizungumza wakati akifunga mafunzo ya siku mbili ya kuyajengea uwezo makampuni binafsi yanayotoa huduma ya kusambaza dawa na vifaa tiba yaliyotolewa na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) kwa kushirikiana na Mradi wa Tuimarishe Afya (HPSS) yaliyomalizika leo Mei 3,2023 jijini Dodoma.


Sehemu ya washiriki wakimsikiliza Mshauri Mwandamizi katika Usimamizi na Usambazaji wa Dawa kutoka HPSS Bi.Fiona Chilunda,(hayupo pichani) wakati akifunga mafunzo ya siku mbili ya kuyajengea uwezo makampuni binafsi yanayotoa huduma ya kusambaza dawa na vifaa tiba yaliyotolewa na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) kwa kushirikiana na Mradi wa Tuimarishe Afya (HPSS) yaliyomalizika leo Mei 3,2023 jijini Dodoma.





Meneja Masoko kutoka Nebula Pharmaceutical Ltd, Linda Barnabas,akielezea umuhimu walioupata katika mafunzo hayo ya kuwajengea uwezo Makampuni binafsi yanayotoa huduma ya kusambaza dawa na vifaa tiba yaliyotolewa na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) kwa kushirikiana na Mradi wa Tuimarishe Afya (HPSS) yaliyomalizika leo Mei 3,2023 jijini Dodoma.


Idrisa Mziray kutoka kampuni ya Vasco Pharmaceutical Company Ltd ya Jijini Arusha,akizungumzia jisni walivyojifunza kuhusu Teknolojia ya mfumo mshitiri inavofanya kazi ya kuwahudumia wazabuni katika hatua mbalimbali yaliyotolewa na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) kwa kushirikiana na Mradi wa Tuimarishe Afya (HPSS) yaliyomalizika leo Mei 3,2023 jijini Dodoma.


Mshauri Mwandamizi katika Usimamizi na Usambazaji wa Dawa kutoka HPSS Bi.Fiona Chilunda,akiwa katika picha pamoja na washiriki mara baada ya kufunga mafunzo ya siku mbili ya kuyajengea uwezo makampuni binafsi yanayotoa huduma ya kusambaza dawa na vifaa tiba yaliyotolewa na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) kwa kushirikiana na Mradi wa Tuimarishe Afya (HPSS) yaliyomalizika leo Mei 3,2023 jijini Dodoma.

Na.Alex Sonna-DODOMA

OFISI ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) kwa kushirikiana na Mradi wa HPSS Tuimarishe Afya wamewajengea uwezo makampuni binafsi yanayotoa huduma ya kusambaza dawa na vifaa tiba.

Makampuni hayo ni yale yaliyopata tenda kupitia mfumo mshitiri katika mikoa yote 26 ya Tanzania Bara.

Akizungumza katika mafunzo hayo,jijini Dodoma,Mshauri mwandamizi katika usimamizi na usambazaji wa dawa kutoka HPSS ,Fiona Chilunda amesema kwa siku mbili walikuwa wakiwajengea uwezo makampuni hayo ambayo yanatoa huduma za afya.

Amesema mafunzo yalilenga kuwajengea uwezo wakutumia mfumo ambao TAMISEMI wameutengeneza kwa ajili ya kuagiza na kusambaza bidhaa kwenye vituo vya afya kwa kutumia mfumo mshitiri.

Amesema mfumo huo unatumika nchi nzima.

“Mfumo mshitiri unaruhusu Makampuni binafsi kusambaza bidhaa za afya kwenye vituo vya afya pale tu ambapo Bohari ya Dawa nchini (MSD) watathibitisha kutoweza kusambaza huduma hizo kwenye vituo.”

“Kwa maana hiyo hatutarajii kuwepo na mgogoro wa kimaslahi kwa kuwa mfumo unasaidia upatikanaji wa dawa wakati wote,”amesema Bi. Chilunda.

Kwa upande wake,Idrisa Mziray kutoka kampuni ya Vasco Pharmaceutical Company Ltd ya Jijini Arusha amesema amejifunza jinsi teknolojia ya mfumo mshitiri inavyofanya kazi ya kuwahudumia wazabuni katika hatua mbalimbali.

Amesema teknolojia hiyo ni katika kupokea order na kuhakikisha inafika sehemu husika kwa kufuata utaratibu ambao ni mzuri na m8singi mizuri ambayo imeandaliwa.

“Tunashukuru kwa kutuletea teknolojia hii,tunaamini itasaidia wananchi kupata huduma kwa muda sahihi,”amesema Mziray.

Naye,Meneja Masoko kutoka Nebula Pharmaceutical Ltd, Linda Barnabas, amesema mafunzo hayo yamewasaidia amewapongeza waandaaji wa mafunzo hayo ambayo amesema ni muhimu katika kuboresha utoaji wa huduma za afya.

Amesema mafunzo hayo yatasaidia wananchi kuweza kunufaika na kupata huduma kwa haraka pale ambapo MSD itakwama.

“Wao wataingia katikati na kuwasaidia wananchi waweze kupata huduma kwa haraka.

“Pia teknolojia itasaidia kuboresha zaidi taarifa za usambazaji wa bidhaa za afya nchini”, amesema Linda.
Share:

MASHIRIKA YA VIWANGO EAC YAJIDHATITI KWENYE MASUALA YA BIDHAA NA VIPIMO

MASHIRIKA ya viwango vya ubora wa bidhaa kutoka nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), yamejipanga kuhakikisha masuala ya bidhaa na vipimo yanakuwa sawa, husasan upimaji na magari yanayosafirisha mafuta.
Wakizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha wakati wa mkutano wa 25 wa kujadili masuala ya viwango kwa nchi wanachama wa EAC, Mkurugenzi Udhibiti Ubora Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Lazaro Msasalaga, anasema mkutano huo wa siku tatu umejumuisha wakurugenzi wa viwango kutoka nchi za EAC ni muhimu kwa ajili ya kujadili masuala yahusuyo ubora wa bidhaa.

Anasema mashirika hayo yanakutana kupitia kamati za kitaalam katika masuala ya udhibiti ubora  ikiwemo kupitisha viwango 69 za bidhaa za chakula na vipodozi, ikiwemo viwango vitatu vinavyotoa maelekezo ya taarifa zinawekwa katika vifungashio vya bidhaa kama matumizi ya bidhaa husika na jinsi ya kuhifadhi.

“Hiki ni kikao muhimu na nchi ya Tanzania tutanufaika katika ubora wa viwango ikiwemo uwekaji wa maneno yanayoelezea bidhaa wanazotumia walaji zitaboresha vitu gani, ikiwemo viambata vya kilishe sanjari na ujumla wa kuweka maelezo ya aina mbalimbali katika bidhaa,” amesema.

Mkurugenzi wa Shirika la Ukaguzji wa Ubora wa Bidhaa  kutoka nchini Kenya (KEBS),  Bernard Njiraini, alisema mashirika hayo yanajadiliana viwango walivyokubaliana kwa pamoja,  ili waweze kufanya biashara  kirahisi ndani ya nchi wanachama wakati wa kupitisha bidhaa mipakani.

Meneja Upimaji Wakala wa Vipimo Tanzania, Magesa Biyani, anasisitiza masuala ya vipimo ni eneo muhimu kuhakikisha bidhaa na vipimo vinakua sahihi katika ufanyaji biashara kwa nchi za EAC hususan masuala ya upimaji katika magari yanayosafirisha mafuta, ambapo awali upimaji ulitofautina baina ya nchi na nchi, lakini pia wanatarajia kuanzisha kanuni itayoondoa vikwazo kwa wafanyabishara wanaosafirisha mafuta kwa nchi za EAC, ikiwemo usahihi wa vipimo vya bidhaa zilizofungashwa.




Share:

DKT. CECILIA KUTOKA TAASISI YA NELSON MANDELA ABUNI DAWA YA ASILI YA KUSINDIKA NGOZI

Mhadhiri kutoka Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Dkt. Cecilia China (Kulia) akionyesha dawa ya asili ya kusindika ngozi ambayo inasaidia kuondoa matumizi na utegemezi wa kemikali kutoka nje kwa wananchi waliotembelea banda la taasisi hiyo wakati wa Maonesho ya Wiki ya Ubunifu katika Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.
Afisa Usimamizi wa Tafiti kutoka Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Tekinolojia ya Nelson Mandela Bw, Okuli Andrea akieleza jambo kwa mwananchi aliyetembelea banda la taasisi hiyo wakati wa Maonesho ya Wiki ya Ubunifu katika Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.
Baadhi ya Bidhaa zilizotengenezwa dawa ya asili ya kusindika ngozi ambayo inasaidia kuondoa matumizi na utegemezi wa kemikali kutoka nje iliyobuniwa na Mhadhiri kutoka Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Dkt. Cecilia China.

Na Mwandishi Wetu-DODOMA

Mhadhiri kutoka Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Dkt. Cecilia China amebuni dawa ya asili ya kusindika ngozi ambayo itasaidia kuondoa matumizi na utegemezi wa kemikali kutoka nje.

Dkt. Cecilia alisema hayo wakati wa Maonesho ya Wiki ya Ubunifu yaliyofanyika Jijini Dodoma katika Uwanja wa Jamhuri yaliyoanza Aprili 24 hadi aprili 28,2023 ,ambapo alieleza kuwa ubunifu wa dawa hiyo ambayo imetengenezwa kwa kutumia mitishamba itasaidia kutatua tatizo la upatikanaji wa kemikali za kusindika ngozi.

“Kwa sasa hapa nchini hatuna kiwanda cha kuzalisha kemikali za kusindika ngozi tunaingiza hizi dawa kutoka nje na wajasiriamali wengi ambao wanasindika ngozi na ambao ni wengi hawana uwezo wa kumudu zile dawa kwasababu viwanda vyao vidogo.” amesema Dkt. Cecilia.

Alisema pia matumizi ya dawa isiyo na kemikali itasaidia katika utunzaji mazingira.

“Hata ikitokea mtu amepata hizo dawa, hana uwezo wa kusafisha majitaka kwasababu hawana miundombinu mizuri na zile dawa ni sumu na matokeo yake wanaishia kufungiwa.”Dkt.Cecilia.

Dkt. Cecilia alisema ubunifu huo aliouanza akiwa anasoma shahada yake ya Uzamivu (PhD) katika Taasisi hiyo, ulipata ushindi wa kwanza katika kundi la vyuo vikuu wakati wa MAKISATU ya mwaka 2020.

“Hiyo ilinipa fursa ya kufadhiliwa na COSTECH kwa ajili ya kuendelea, fedha nilizopewa ziliwezesha kubuni mtambo wa kutengeneza dawa na kuilinda kisheria.” Dkt. Cecilia

Alisema kupitia mradi wa Kongani Bunifu COSTECH ilimfadhili ili kuhamisha teknolojia kwa kikundi cha wasindika ngozi chenye wanachama 15 kilichomo Usangi mkoani Kilimanjaro.

Aidha, Dkt. Cecilia alisema kwa sasa wanampango wa kusajili kampuni ya jamii ambayo itahusika kutengeneza dawa kwa ajili ya wajasiliamali wadogo, kufundisha namna ya kutumia na kutafutiwa masoko.

Alisema pia Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknoloji ya Nelson Mandela tayari imefanya upembuzi yakinifu wa soko la dawa hiyo na kugundua kuwapo kwa mahitaji makubwa.

Anazidi kueleza kuwa ili kuongeza uzalishaji unahitajika mtambo wenye thamani ya Sh. milioni 500 hatua ambayo itasaidia kutosheleza soko la ndani na kuunza nje ya nchi.

“Tunahitaji mtambo mkubwa ambao thamani yake ni takribani shilingi milioni 500 ili tuweze kuzalisha dawa inayoweza kukidhi mahitaji. Na uwekezaji huu unaweza kulipa ndani ya miaka mitatu.” Alisema Dkt. Cecilia.

“Lengo letu ni tuchangie kwenye mnyororo wa thamani wa ngozi hasa kutokana na Tanzania kuwa nchi ya pili kwa kuwa na mifugo mingi barani Afrika na tumekuwa tunazalisha ngozi takribani milioni 11 lakini asilimia 80 mpaka 90 tunaziuza nchi za nje zikiwa mbichi.” Alisema Dkt. Cecilia

Alisema pia uongezaji thamani ngozi utawezesha nchi kupunguza uingizaji wa viatu vya plastiki ambapo kwa sasa mahitaji ni mpaka milioni 60 na uzalishaji wa ndani ni jozi milioni 1.2 za viatu.

“Sasa kwanini tusitumia tekinolojia za ndani na malighafi za ndani tukaongeza thamani ya ngozi, tukazalisha viatu na watanzania wakavaa. Sisi tunataka tuchangie kwenye sekta ya ngozi iweze kukua kwasababu inauwezo wa kuajiri vijana wengi.”Alisema Dkt. Cecilia

Naye Afisa Usimamizi wa Tafiti kutoka Taasisi hiyo, Okuli Andrea alisema Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Tekinolojia ya Nelson Mandela imejikita katika kutoa shahada za Uzamili na Uzamivu na kufanya tafiti mbalimbali za kutatua changamoto mbalimbali katika jamii.

“Katika maonesho ya Wiki ya Ubunifu mwaka 2023 tumekuja na bunifu mbalimbali ambazo zinatatua changamoto katika jamii ambazo ni bidhaa za ngozi zisizotumia kemikali, ngwara yenye virutubisho, vyakula lishe na mtambo wa kusafisha maji na bidhaa nyingine mbalimbali.” Alisema Bw. Okuli
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger