Wednesday, 26 April 2023

RC DODOMA ATAKA BUNIFU ZOTE KUINGIZWA SOKONI ZIKATATUE CHANGAMOTO KATIKA JAMII


Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Bi.Rosemary Senyamule,akipata maelezo kutoka kwa Meneja Uhusiano VETA Bw.Sitta Peter mara baada ya kutembelea banda la VETA wakati wa Maonyesho ya Wiki ya Ubunifu 2023 inayowakutanisha wabunifu mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi yaliyoandaliwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia yaliyoanza Aprili 24 hadi 28 mwaka huu katika uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.


Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Bi.Rosemary Senyamule,akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kutembelea banda la VETA wakati wa Maonyesho ya Wiki ya Ubunifu 2023 inayowakutanisha wabunifu mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi yaliyoandaliwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia yaliyoanza Aprili 24 hadi 28 mwaka huu katika uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.


Wanafunzi na wananchi mbalimbali wakipata maelezo katika banda la VETA wakati wa Maonyesho ya Wiki ya Ubunifu 2023 inayowakutanisha wabunifu mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi yaliyoandaliwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia yaliyoanza Aprili 24 hadi 28 mwaka huu katika uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.





Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Bi.Rosemary Senyamule,akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kutembelea banda la VETA wakati wa Maonyesho ya Wiki ya Ubunifu 2023 inayowakutanisha wabunifu mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi yaliyoandaliwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia yaliyoanza Aprili 24 hadi 28 mwaka huu katika uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.


Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Bi.Rosemary Senyamule,akiwa ndani ya gari akiendeshwa na wanafunzi waliobuni gari mara baada ya kutembelea Maonyesho ya Wiki ya Ubunifu 2023 inayowakutanisha wabunifu mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi yaliyoandaliwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia yaliyoanza Aprili 24 hadi 28 mwaka huu katika uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.


Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Bi.Rosemary Senyamule,akizungumza na washiriki wa maonyesho (hawapo pichani) mara baada ya kutembelea na kukagua Maonyesho ya Wiki ya Ubunifu 2023 inayowakutanisha wabunifu mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi yaliyoandaliwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia yaliyoanza Aprili 24 hadi 28 mwaka huu katika uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.


Mkurugenzi wa Mafunzo ya Ufundi Stadi -VETA Ndg.Abdallah Ngodu,akielezea bunifu zinazofanywa na VETA katika Maonyesho ya Wiki ya Ubunifu 2023 inayowakutanisha wabunifu mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi yaliyoandaliwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia yaliyoanza Aprili 24 hadi 28 mwaka huu katika uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.


Mkurugenzi wa Sayansi, Teknolojia na Ubunifu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Maulilio Kipanyula,akizungumzia Maonyesho ya Wiki ya Ubunifu 2023 inayowakutanisha wabunifu mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi yaliyoandaliwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia yaliyoanza Aprili 24 hadi 28 mwaka huu katika uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.


Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Bi.Rosemary Senyamule,akigawa Vyeti pamoja na zawadi kwa washindi wa bunifu zao ambazo zimeshindanishwa na kukidhi viwango Vilivyotolewa na VETA wakati wa Maonyesho ya Wiki ya Ubunifu 2023 inayowakutanisha wabunifu mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi yaliyoandaliwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia yaliyoanza Aprili 24 hadi 28 mwaka huu katika uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.


Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Bi.Rosemary Senyamule,akiwa katika picha ya pamoja na washindi wa bunifu mbalimbali walioshinda wakati wa Maonyesho ya Wiki ya Ubunifu 2023 inayowakutanisha wabunifu mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi yaliyoandaliwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia yaliyoanza Aprili 24 hadi 28 mwaka huu katika uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.


Na.Alex Sonna -DODOMA


Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,Rosemary Senyamule amekoshwa na bunifu mbalimbali zilizopo katika maonesho ya wiki ya ubunifu huku akiwaomba watanzania kufika katika uwanja wa Jamhuri kwa ajili ya kujionea.

Wiki ya ubunifu inawakutanisha wabunifu mbalimbali kutoka ndani na nje ya Nchi na ilianza Aprili 24,2023 katika uwanja wa Jamhuri na yanatarajia kumalizika Ijumaa Aprili 28 mwaka huu.

Akizungumza leo,Aprili 25,2023 mara baada ya kutembelea mabanda,Mkuu huyo wa Mkoa amesema ameshuhudia mambo makubwa ambayo yamefanywa na wabunifu hao.

Ametoa shime kwa watanzania wengine kufika kwenye mabanda hayo kwa ajili ya kujionea bunifu hizo.

RC Senyamule amesema mambo mazuri aliyoyaona ni kijana mmoja kwenye banda la VETA ambaye ametengeneza miwani ambayo dereva akivaa kama akisinzia inamkumbusha kwa kupiga kengele kwa kumwambia asisinzie.

"Tunafahamu kwamba Serikali imekuwa ikihangaika muda mrefu jinsi gani ya kuzuia ajali sasa kijana wa kitanzania ametupatia ufumbuzi tunaimani teknolojia hiyo itaendelea kitumika kupunguza ajali nchini,"amesema Senyamule.

Amesema ubunifu huo ni wa kipekee kwani utasaidia sana hasa kwenye suala la usalama.

Aidha amesema pia amefurahishwa na banda la DIT ambao wametengeza gari linalotumia gesi.

"Na wamesema wameishaunganisha mfumo wa gesi kwenye magari mengi zaidi 2000 nimekuwa nikisikia leo nimejionea, inapunguza gharama za mafuta kwa zaidi ya asilimia 50,"amesema

Amesema kitu kingine kilichomfurahisha ni shule moja ya Arusha wametengeneza gari la kutumia solar.

"Nimeona mabadiliko makubwa ya matumizi ya teknolojia na ubunifu mkubwa,nipongeze sana Wizara ya Elimu kwa kazi nzuri mnayofanya,"amesema RC Senyamule.

Aidha,RC Senyamule amesema maonesho hayo yamepiga hatua kwani ni halisi na kila mwaka yanaendelea kupiga hatua.

"Tumeweza kushuhudia baadhi ya bidhaa ambazo zinaweza kutumika katika maisha yetu ya kawaida majumbani na maofisi.

"Kwa ujumla mimi nipongeze sana Serikali,nipongeze Wizara ya Elimu na taasisi zote ambazo zimeshiriki maonesho haya kwani yameendelea kuongeza thamani,"amesema RC Senyamule.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mafunzo ya Ufundi Stadi -VETA Ndg.Abdallah Ngodu amesema kuwa maonesho ya wiki ya Ubunifu kwa mwaka huu yamekuwa tofauti sana kwani wamepewa nafasi ya kuwa na siku maalumu kwa ajili ya VETA ambayo imekwenda kwa jina la "VETA DAY"

Amesema wameandaa vitu mbalimbali kutoka katika vyuo vya Veta.

Amesema wamekuwa na matukio muhimu ikiwemo mdahalo kwa ajili ya umuhimu wa elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi- katika ubunifu.

"Mdahalo huo utasimamiwa na Msemaji Mkuu wa Serikali ndugu Gerson Msigwa,"amesema.

Amesema wamekuwa na mashindano ya umahiri wa vijana ambao wanapata mafunzo katika vyuo vyao.

Ameeleza kuwa vijana hao wameshindanishwa katika fani za ujenzi,Umeme na urembo.

Amesema wanalenga kujua vijana wamepata ujuzi na wameweza kumudu stadi zipi.

"Kutokana na tukio hili wamependekeza kwamba itakuwa endelevu na hao watakaoshinda watapata tuzo na vyeti,"amesema Ngodu.

Amesema mashindano hayo wamewashirikisha vijana waliohitimu au wale ambao ni wanufaika ambao wamekuja kuonesha kazi wanazofanya.

"Bahati nzuri katika hawa vijana waliomaliza vyuo vyetu wapo ambao wamaliza vyuo vikuu lakini kutokana na mazingira magumu ya ajira basi wamekuja VETA na wameweza kutengeneza vitu mbalimbali,"amesema Mkurugenzi huyo.

Aidha ametoa wito kwa wananchi wafike katika uwanja wa Jamhuri kwa ajili ya kujionea kazi zinazofanywa na Veta.

"Sasa hivi tunatakribani vyuo 50 Nchi nzima ambavyo vinatoa mafunzo na Serikali imetoa fedha kwa ajili ya kujenga vyuo na kutakuwa na vyuo zaidi ya 140 maana yake kila Wilaya itakuwa na chuo,"amesema Mkurugenzi huyo.

Ngodu amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuona umuhimu wa wananchi kupata stadi za ujuzi ili waweze kujiajiri.


Naye Mkurugenzi wa Idara ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu Prof.Maulilio Kipanyula amesema kuwa Maonesho ya wiki ya Ubunifu mwaka 2023 yamekuwa tofauti kwani imeanzi katika ngazi za mikoa na huko wabunifu walianza kuonesha bunifu zao katika ngazi hizo na sasa maonesho hayo yamefikia katika ngazi ya taifa hivyo imewapa nafasi wabunifu wengi kuonesha bunifu zao.

Prof. Kipanyula ameongeza kuwa katika maonesho hayo kutakuwa na siku maalumu kwa ajili ya Taasisi za VETA na Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC)

"VETA leo wameonesha bunifu zao na ndio maana leo ni VETA DAY dhumuni ni kuona ni namna gani uwekezaji uliofanywa na Serikali ya awamu ya sita katika elimu ya ufundi imefanyiwa kazi na kuzalisha wabunifu wenye uwezo wa kuigiza sokoni bunifu kwa ajili ya kutatua changamoto za jamii,"

Na kuongeza kuwa "kwa upande wa Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC) nao watakuwa na TAEC DAY ambapo dhumuni la siku hiyo ni kuifanya Tume hiyo ijulikane na wananchi ,majukumu yake ni yapi, nini faida yake na mengine mengi ambayo yataelezwa.

Prof.Kipanyuka amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika maonesho hayo ili kujionea bunifu mbalimbali ambayo zimebuniwa na wabunifu wa ndani huku ikichagizwa na wabunifu kutoka nchini Afrika Kusini kwani lengo la serikali na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ni kuifanya wiki ya Ubunifu Tanzania kuwa ya kimataifa.
Share:

CHUO CHA TAIFA CHA UTALII (NCT) CHAFANYA MDAHALO KUADHIMISHA MIAKA 59 YA MUUNGANO




Kaimu Mkuu wa chuo cha Taifa cha Utalii (NCT) Dkt. Florian Mtey akizungumza alipokuwa akitoa hotuba yake ya kufungua rasmi Mdahalo wa maadhimisho wa sherehe za miaka ya 59 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar uliofanyika katika Ukumbi wa mikutano wa Chuo hicho Jijini Dar es Salaam.

Mkufunzi katika Chuo cha Taifa cha Utalii (NCT) Dkt. Naiman Mbise akizungumza alipokuwa akitoa mada iliyohusu kutengeneza Viwango ili kutoa Huduma bora katika Seka ya Utalii.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Idara ya Sayansi, Siasa na Utawala wa Umma, Dkt. Richard Mbunda akitoa mada iliyohusu Umoja na Mshikamano ndio nguzo ya kukuza uchumi wetu katika Sekta ya Utalii.

Kaimu Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Utalii (NCT), Taaluma, Tafiti, na Ushauri Bi. Jesca William akizungumza alipokuwa akitoa salamu za utangulizi na kuwatambulisha wageni mbalimbali waliohudhuria Mdahalo huo.
(PICHA NA: HUGHES DUGILO)

Na: Hughes Dugilo, DAR ES SALAAM

Kaimu Mkuu wa chuo cha Taifa cha Utalii (NCT) Dkt. Florian Mtey amesema katika kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan katika kuhakikisha Sekta ya Utalii inaendelea kuchangia pato la Taifa, tayari chuo hicho kimeanza kutekeleza Programu mbalimbali ili kuendana na uhitaji wa soko la ajira nchini. Dkt Mteyi ametoa kauli hiyo Jijini Dar es salaam wakati wa Mdahalo wa maadhimisho wa sherehe za miaka ya 59 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambapo amesema kwa mwaka 2022 pekee Sekta ya Utaii imefanikiwa kukusanya Dola za Kimarekani Bilioni 1.4. Amesema fedha hizo zimetokana na matunda ya Filamu ya ‘Tanzania – The Royal tour’ iliyozinduliwa na Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na mambo mengine, Watalii wameendelea kuongezeka kutoka Mataifa mbalimbali na kuongeza mchango wa Pato la Taifa (GDP). ”Tangu Rais Dkt Samia Suluhu Hassan azindue Filamu ya ‘The Royal Tour’ tumeona wawekezaji wengi wamemiminika katika mbuga zetu, haya ni matunda ya ile Filamu na sisi kama Chuo tunaendelea kuunga mkono jitihada hizi hasa kwa kushirikiaa na wadau pamoja na Sekta Binafsi” Amesema Dkt. Mtey. Kwa upande wake Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Idara ya Sayansi Siasa na Utawala wa Umma Dkt. RIchard Mbunda amesema muungano umeleta faida katika Sekta ya Utalii ikiwemo kurahisisha upatikanaji wa masoko hasa kwa wawekezaji wanaowekezaZanzibar na Tanzania Bara. ”Muungano huu umewasaidia sana wawekezaji hasa kweye upande wa masoko ndmana leo watalii wanaenda Zanzibar lakini wamefikia Dar es salaam au wengine wanaenda kutalii katika visiwa vya Zanzibar lakini wamefikia Dar es salaam” Amesema Dkt Mbunda. Itakumbukwa kuwa mwaka 2015 hadi 2020 Serikali ya Mapinduzi Zanzibar pamoja na Tanzania Bara zilifanya vikao takribani 85 kujadili kero mbalimbali za Muungano ambapo katika vikao hivyo kero 18 ziliibuliwa huku kero 11 zikipatiwa ufumbuzi.
PICHA MBALIMBALI ZA WASHIRIKI
Share:

Tuesday, 25 April 2023

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO APRILI 26,2023


Share:

MAMA ATAFUTWA NA POLISI KWA KUTELEKEZA WATOTO KAHAMA KISA KODI




Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga linamtafuta Mariamu Salumu mkazi wa Kisesa mkoani Mwanza kwa tuhuma ya kutelekeza watoto wawili kwa kile kinachodaiwa kushindwa kulipa kodi na kusababisha waishi katika mazingira hatarishi huku kijana James Julius akishikiliwa kwa kuishi na watoto hao.

Watoto hao mmoja akiwa na umri wa miaka 17 na mwingine miaka miwili walisafirishwa na mama yao mzazi kwenda Kahama ili yule mkubwa akafanye kazi za ndani na kumlea mdogo wake ambapo walipata msaada kwa kijana Julias aliyedai watakwenda kukaa kwa dada yake na kufanya kazi za ndani ambapo leo imebainika wametelekezwa.

Mama mzazi wa watoto hao alibaki Jijini Mwanza akifanya shughuli za vibarua za mama lishe baada ya kuwasafirisha watoto wake kwa basi hadi Kahama kutokana na ugumu wa maisha.

Tangu watoto hao watoke jijini Mwanza na kwenda Kahama siku 60 zimepita, ambapo baada ya kufika Kahama kijana huyo aliwapatia chumba na kumtaka binti kutafuta kazi za ndani ambapo alifanikiwa kupata na kuamuwa kumuacha mtoto wa miaka miwili ndani pekee yake bila kuwa na uangalizi siku nzima kitendo ambacho kilisababisha mtoto huyo kufanyiwa vitendo vya ukatili vikiwemo vipigo.

Mwenyekiti wa Asasi ya Wanawake Laki Moja Mkoa wa Shinyanga Anascholastica Ndagiwe ambao ndiyo walifanya kazi ya kuibuwa watoto hao amesema baada ya kupata taarifa walifuatulia kwa kushirikiana na dawati la jinsia na kufanikiwa kuwapata huku kamanda wa Jeshi la polisi Mkoa wa Shinyanga Janeth Magomi akithibitisha kutokea tukio hilo.

Chanzo - EATV
Share:

Video Mpya : NG'WANA KALANGA - ZAMU YANE

Share:

MTOTO ALIVYOWATOROKA WAZAZI USIKU KUMFUATA RAIS SAMIA KUOKOA MAISHA YAKE

* Walimkataza kutoka nje kuhofia watu watamkimbia au kumpiga kutokana na ugonjwa wake

* Alihangaika sana na kukata tamaa, sasa amshukuru Rais Samia kwa kuokoa maisha yake


Na Mwandishi Wetu 

"Nilisikia Rais Samia anapita Nyakanazi na mimi kwetu ni pale pale Nyakanazi. Wazazi walinikataza, wewe usiende na hali hiyo uliyokua nayo watu wanakukimbia. Unaenda kufanya nini, watakupiga."


Hayo ni maneno ya Hamimu Mustapha Baranyikwa (15), mkazi wa kijiji cha Nyakanazi, Biharamulo, Mkoani Kagera, akisimulia tukio la tarehe 16 Oktoba, 2022, ambalo kamwe hatalisahau katika maisha yake.


"Kaka yangu akaniambia wewe nenda, itakavyokuwa itakuwa. Ninachojua (Rais) anaweza kukusaidia. Mimi kweli niliamka usiku sana ili wazazi wasinione, maana kama wangeniona wangenikataza."


Hamimu, ambaye wazazi wake walihangaika kumpeleka kwa waganga wa kienyeji na hata kuuza mali za familia bila mafanikio, alikuwa amekata tamaa kama angekuja kupona ugonjwa wake wa ajabu 


Ngozi yake ilikuwa imeharibika, uso wake ukawa hautazamiki hadi watu wazima na watoto wakawa wanamkimbia na alishindwa hata kukunja na kukunjua vidole vya mikono yake kutokana na maradhi hayo.


Wahenga wanasema penye nia pana njia. Rais Samia Suluhu Hassan alipofika Nyakanazi wakati wa ziara yake ya mkoa wa Kagera, alimuona mtoto huyo amekaa pembeni ya barabara akiwa amenyong'onyea akawatuma wasaidizi wake waende kuongea naye wajue tatizo lake ni nini.


"Nilipofika nikakaa pembezoni mwa barabara. Ule msafara wake (Rais Samia) ulipofika, yale magari yake wakaniona. Waliokuwa wanaongozana naye (Rais) wakaniuliza maswali... Kuna mmoja aliyekuwa ameongozana nao ni dokta, akanishika ngozi yangu," alisema Hamimu.


Kwa mujibu wa kijana huyo, daktari aliyekuwepo kwenye msafara wa Rais Samia akasema kuwa akipelekwa Muhimbili wanaweza kujua chanzo cha ugonjwa wake wa ngozi na kumpatia matibabu sahihi.


Kufuatia ushauri wa daktari, Samia aliagiza mtoto huyo asafirishwe haraka kutoka Nyakanazi hadi hospitali ya Taifa ya Rufaa ya Muhimbili iliyopo Dar es Salaam kwa uchunguzi na matibabu.


Siku chache baada ya maagizo ya Rais, Hamimu akaanza kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Muhimbili tarehe 21 Oktoba, 2022.


Hamimu alilazwa Muhimbili kwa matibabu kwa muda wa miezi sita kwa msaada wa Rais Samia.


Ilipofika tarehe 19 Aprili 2023, madaktari wake wakajiridhisha kuwa sasa mtoto huyo amepona na anaweza kurudi nyumbani kwao mkoani Kagera.


Kabla ya kurudi kwao Kagera, Hamimu ameomba aonane na Rais Samia kumpa shukrani zake uso kwa uso.


"Rais (Samia) natamani nimuone kwa macho, yeye analinganaje. Yaani naomba kabisa, mnisaidie nimuone. Kwa sababu jinsi maisha yetu yalivyo, mimi sidhani kama ningefika huku," alisema Hamimu.


"Sidhani kama ningepona. Ilifika hatua nikasema, mniache nife. Kwa jinsi nilivyohangaika kupona ilishashindikana. Isingekuwa yeye (Rais Samia) mimi mpaka muda huu sidhani kama ningekuwa hai."


Hamimu anasema kuwa baada ya wazazi wake kuhangaika kumtibu kwa waganga bila mafanikio, walimwambia kuwa wamefikia mwisho hawawezi kumsaidia tena, ndipo alipoamua kuufuata msafara wa Rais Samia kuokoa maisha yake.


Mtoto huyo amewashukuru pia kwa dhati  madaktari na manesi wa Muhimbili kwa kumhudumia kwa upendo hadi alipopona.

Share:

Monday, 24 April 2023

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE APRILI 25,2023



























Share:

KILICHOWATOKEA MADALALI NA MWENYEKITI KWA KUTUUZIA ARDHI ISIYOWAHUSU

Bwana Mwifyusi , Moses Chicago pamoja na Robert mtoto wa Mwakipesile ndiyo madalali wakubwa walioshikilia tenda zote hapa mtaani kwetu kuanzia uuzaji wa viwanja mpaka ununuzi wa magari ya kifahari wakisaidiana na mwenyekiti mwakasita wa kata yetu Sinde mtaa wa Kagwina.

Mwaka wa 2021 mwishoni nilijihusisha sana na ukulima na hivyo nikabahatisha kiasi kikubwa kidogo cha fedha na kuamua kununua ardhi nikiamini kuwa ardhi ndiyo mali ya kudumu maishani.

Bila ya kujua mengi kiundani nikaamuwa kumtafuta dalali Robert kisha akaungana nguvu na wenzake hao wawili wakanipaia uwanja wenye hatua ishirini na tano kwa ishirini, nikawataka wao kumhusisha  mwenyekiti ili kujiondoa kwenye migogoro isiyo na umuhimu kaika fedha zangu na ardhi yangu.

Kwao haikuwa shida nikawapatia fedha wakamlipa mwenyekiti na kiasi chao cha fedha wakachukuwa waliniambia kuwa mwenye kiwanja kile yuko mbali na hivyo alikabidhiwa Chicago na Mwifusyi wa kaimu nafasi hiyo, niliwahesabia pesa takimu milion thelathini na tano tukaandikishana wakaenda zao.

Nilipopumua tena baada ya muda na kuanza kushusha mawe,tofali pamoja na mchanga hapo ndipo nilipoanza kuchanganywa na majirani wakidai kuwa uwanja huwo ulikuwa wao na haukuwahusisha madalali wala mwenye nyumba aliyewakaimisha hakuwepo bali ni habari za kutengenezwa.


Haikuishia hapo na kesi wakanifungulia kwenye mahakama ya mwanzo, kila nilipojaribu kuleta mbele nyaraka za haki walizitelekeza kwa kuwa jirani zangu pia walikuwa na nyaraka nilizunguka kila kona kutafuta suluhisho na kila aina ya hakimu lakini sikupata msaada badala ya kuambiwa niondowe mawe, mchanga na matofali kwenye eneo lao.

Nilipomuhusisha rafiki yangu adam aliniambia kuwa kesi kama zile mara nyingi ni ngumu kushinda kwa kutegemea wanasheria na mahakimu akaniambi habari za daktari BAKONGWA na kunipa nambari zake za whatsapp +243990627777 .

Nilipomtafuta akanipa dawa za kutumia kwa muda wa siku mbili na kunihakikishia kuwa kila kitu kitakuwa sawa, mara baada ya kutuma dawa nilishangazwa kupokea ujumbe wa dalali ukinitaka tukutane tulipokutana akanirudshia pesa zangu na kunitaka radhi.Mahakamani nilikubali kosa na kuomba niuziwe uwanja huo upya na wamiliki halali.


Ninashukuru sana kwa msaada wa uhakika kutoka kwako daktari nitatembelea tovuti zako https://bakongwadoctors.com kutowa shukrani za dhati.

 


Share:

UKIPATA SHIDA YA MACHO USIKIMBILIE DUKA LA DAWA MUONE DAKTARI

 

Na Oscar Assenga, Tanga

DAKTARI Bingwa wa Magonjwa ya Macho katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga –Bombo Dkt Hussein Abbas Tayebji amewashauri wananchi wanapopata shida ya macho wasikimbilie kwenye duka la kununua dawa badala yake wafike hospitalini wachekiwe wanashida gani na watapewa dawa sahihi au miwani.

Dkt Hussein aliyasema hayo leo wakati akielezea matatizo macho ambapo alisema kwamba wagonjwa wanaowapokea kati yao wanawatibu na kutoa ushauri ikiwemo kuwaeleza umuhimu wa kujenga utaratibu wa kucheki macho yao angalau mara moja kwa mwezi.

Alisema kwa sababu dawa nyengine zinaweza kuwaletea shida wakiweke ovyo ovyo kwenye macho ni sumu kwenye macho hivyo iwapo wanakumbana na matatizo ya macho ni vema wakafika hospitalini wachekiwe wanashida gani na watapewa kupewa dawa sahihi.

“Ni muhimu sana kwa wananchi wanapopata tatizo la macho wafike Hospitalini wachekiwe wanashida gani na watapewa dawa sahihi au miwani kama unashida ya miwani kwani sio kila shida ya macho ni miwani”Alisema Dkt Hussein

Dkt Hussein alisema katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo kwa mwezi wanawaona wagonjwa zaidi ya 600 wenye matatizo mbalimbali ya macho.

Alisema katika magonjya ya macho kuna matatizo mengi sana na kati yao wanatibu wanatoa ushauri,kupima miwani na upasuaji wa aina zote mtoto wa jicho ikiwemo kuondoka kinyama cha macho

“Kwa wagonjwa tunaowaona wana presha ya macho sana ndio wanapata kwa sababu haina dalili zozote ukija Hospitali unakuwa umeshachelewa ni vema wananchi waweke utaratibu wa kuchungyza macho yao kila wakati ili kuweza kuepukana na matatizo ya macho ikiwemo mtoto wa jicho”Alisema

 

Share:

WAUMINI ZAIDI YA 20 WAJIUA KWA NJAA WAKIFUNGA BILA KULA WALA KUNYWA MFULULIZO...MCHUNGAJI ALIWAHADAA WAKIFA WATAONANA NA YESU

Jeshi la Polisi nchini Kenya wamefukua miili ya watu zaidi ya 20 ambao ni waumini wa kanisa la News International Church, ambao inadaiwa wamefariki dunia kwa njaa baada ya kufuata maelekezo ya mchungaji wao ya kufunga mfululizo.


Mchungaji Paul Makenzie Nthenge ndiye anayedaiwa kuwapa maelekezo hayo waumini wake, ikidaiwa kwamba aliwaambia wakifunga mfululizo, wataenda kuonana ana kwa ana na Yesu.

Tayari mchungaji huyo anashikiliwa na Jeshi la Polisi nchini humo huku taarifa zikieleza kwamba huenda makaburi mengine yakabainika.


Makachero ambao walifika Malindi eneo la Shakahola wamepata makaburi zaidi katika msitu ambao washirika wa kanisa waliambiwa wafunge hadi kufariki dunia.

Makachero walifika eneo hilo kuwaokoa washirika wa kanisa la Good News International chini ya mhubiri Paul Mackenzie na sasa wamepata makaburi zaidi.
Kufikia sasa makachero wanasema watu watatu, akiwamo msichana wa miaka 16, waliokolewa na kufikishwa hospitali kupokea matibabu. Sasa ripoti zinasema kuwa jumla ya makaburi 27 yameweza kutambuliwa na maswali kuzuka kuhusu watu waliofariki dunia kufikia sasa.


Inaarifiwa wanaochunguza kisa hicho wameweza kupata taarifa muhimu kutoka kwa baadhi ya wafuasi wa Mackenzie ambao wameokolewa. 

Kwa mujibu wa afisa wa watoto eneo la Pwani George Migosi, washirika wa kanisa hilo walikuwa wafunge hadi kufariki wakianza na watoto, kisha kina mama na hatimaye wanaume.

 Sasa maswali yameibuka ni vipi mhubiri aliwachukua washirika wake na kuwapumbaza hadi wakapoteza maisha yao.
Maswali yanayoibuka ni kuhusu ilipokuwa serikali wakati huu ambapo washirika walikuwa kwenye msitu. "Chifu na asasi zingine za serikali walikuwa wapi wakati huu wote wa pasta kuwauzia washirika ajenda za kupotosha," mmoja wa wakazi alisema. 

Maombi hayo yalikuwa yakifanywa kwenye msitu mmoja eneo la Kilifi.


Makachero kutoka Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) wamefukua miili mingi katika Msitu wa Shakahola, Kilifi, inayoaminika kuwa ya wafuasi wa mchungaji tata Paul Mackenzie.


Katika zoezi hilo la Jumapili, Aprili 23, miili sita ilipatikana kwa mara ya kwanza kwenye makaburi matatu yenye kina kirefu.

Kaburi moja lilikuwa na miili mitatu, jingine lilikuwa na miwili na la tatu lilikuwa na moja. Saa chache baadaye, miili 12 zaidi ilipatikana katika makaburi saba, na hivyo kuongeza idadi ya mateka wa mchungaji huo kufikia 39.


Polisi sasa wametangaza boma la kiongozi wa ibada Mackenzie kuwa kaburi la pamoja. Wakati wa uchimbaji, mwanamke mmoja aliokolewa katika moja ya maficho na inasemekana alikuwa katika hali mbaya. Licha ya kuchungulia kifo, alidokezea polisi kwamba hataki kuokolewa. 

Kama ilivyoripotiwa awali, Pasta Mackenzie anatuhumiwa kushawishi waumini wake kufunga, bila kula wala kunywa chochote akiwahadaa kwamba wakifa wataonana na Yesu.

Mnamo Ijumaa, Aprili 21, wapelelezi wa DCI walianza kuweka alama kwenye makaburi na kufukua miili ya watu wanaodaiwa kuwa wafuasi wake wanaoaminika kujiua kwa njaa. Wakati wakiwaokoa wafuasi wa Mackenzie katika msitu wa Shakahola, wapelelezi hao walipatana na makaburi 12 ambayo hayakuwa na alama. Wapelelezi hao pia waliwaokoa watu wengine watatu miongoni mwao, msichana mwenye umri wa miaka 16, ambaye alikimbizwa hospitalini kwa matibabu. Wapelelezi hao pia waliwaokoa watu wengine watatu miongoni mwao, msichana mwenye umri wa miaka 16 ambaye alikimbizwa hospitalini kwa matibabu.
Share:

MIRADI INAYOFADHILIWA NA GGML INAVYOLETA MAGEUZI YA KIUCHUMI GEITA


Mashua ya matibabu inayotoa huduma Ziwa Victoria


Na Mwandishi wetu

TANGU Kampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML), ambayo ni kampuni tanzu ya AngloGold Ashanti ilipoanzishwa mwaka 2000 nchini Tanzania, imekuwa kampuni kinara katika kuhakikisha jamii inayozunguka mgodi huo inanufaika kutokana na uwepo wa shughuli za uchimbaji katika eneo hilo.


Lengo la kimkakati la kampuni ya Geita Gold Mining Limited limejikita katika kuhusianisha shughuli za uchimbaji katika sera za maendeleo ya wana-Geita na Tanzania kwa ujumla kuanzia ngazi ya mitaa, kata, wilaya, mkoa, kitaifa na kikanda.


Ndio maana kwa miaka mingi wadau wakubwa wa sekta ya madini katika tasnia hiyo wamejikita kutoa mchango wao katika huduma za kijamii kama vile afya, elimu, miundombinu ya barabara na ujasiriamali.


Mwaka 2018, GGML ilikuwa kampuni ya kwanza ya uchimbaji madini nchini Tanzania kutekeleza mpango wa uwajibikaji wa kampuni kwa jamii (CSR) kwa kuzingatia kifungu cha 105 cha Sheria ya madini namba saba iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2017. Sheria hiyo iliboresha sheria ya madini namba 14 ya mwaka 2010.


Kwa kuwa GGML inakusudia kuzingatia matakwa ya marekebisho ya sheria hiyo ya madini na kuunga mkono juhudi za Serikali katika kujenga uchumi endelevu unaoweza kudumu hata baada ya mgodi kumaliza shughuli zake, tangu wakati huo, Kampuni inawekeza Sh bilioni 9.2 kila mwaka kufadhili miradi ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi mkoani Geita.


Mwaka 2022/2023 pekee,GGML imetoa zaidi ya Sh bilioni 19 hii ikiwa ni katika kusaidia maendeleo ya kiuchumi, kielimu, kiafya, miundombinu na hata huduma za maji.
Shule ya Sekondari wasichana Nyankumbu
Wanafunzi wakiwa darasani

ELIMU

Kwa kuwa GGML inaamini moja ya nguzo muhimu katika kusukuma gurudumu la maendeleo ya serikali kwa wananchi wake ni elimu, kwenye sekta hii GGML imeunga mkono ujenzi wa shule kadhaa za sekondari na msingi.



Kwa kushirikiana na Halmashauri ya Mji wa Geita, imefanikisha ujenzi wa Shule ya wasichana ya Nyankumbu ambayo ujenzi wake uligharimu zaidi ya Sh bilioni 15 na kuanza usajili wa wanafunzi mwaka 2014.



Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, Georgia Mugashe anasema Nyankumbu imekuwa mkombozi kwa mkoa huo na hata mwaka huu wa masomo imesajili wanafunzi wapya wa kidato cha kwanza 240 huku ikishindwa kuchukua wengine kutokana na wingi wa maombi.



Lakini pia kwa kuwa mkoa wa Geita haukuwa na shule nyingi sekondari za kidato cha tano na sita za bweni , mbali na Nyankumbu pia GGML imeshiriki ujenzi wa shule za kwanza za serikali za kidato cha tano na sita katika halmashauri ya wilaya ya Geita ambazo ni shule za Kamena na Bugando.

Shule hizo mbili zilizoanza usajili wa wanafunzi mwaka 2021/2022, GGML imetoa zaidi ya Sh milioni 287.5 kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya Geita kupitia mpango wa CSR.


GGML KILI CHALLENGE AGAINST HIV & AIDS

Kampeni ya GGM Kilimanjaro Challenge against HIV & AIDS iliyozinduliwa miaka 20 iliyopita, imedhihirisha namna kampuni ya GGML ilivyojikita kushirikiana na serikali kutokomeza janga la VVU/ UKIMWI.
Kampeni hiyo inayoishirikisha pia TACAIDS inalenga kukusanya fedha kwa ajili ya mapambano ya VVU/Ukimwi, inashirikisha wapanda mlima Kilimanjaro kwa kutumia baiskeli na miguu hadi kwenye kilele cha mlima huo mrefu barani Afrika.


Tangu mwaka 2002, zaidi ya watu 800 kutoka maeneo mbalimbali duniani, wamepanda mlima huo na kuchangia zaidi ya Sh bilioni 1.3 ambazo zimesaidia taasisi binafsi zaidi ya 20 zinazotoa huduma kwa waathirika wa janga hilo.


Mojawapo ya wafaidika wa fedha hizo ni Kituo cha AGAPE kilichopo mkoani Njombe ambacho msimu uliopita kilipata ruzuku ya Sh. milioni 29.9 kutokana andiko walilowasilisha kwenye timu ya wataalam wa GGM Kili Challenge.


Mratibu wa Kituo, Enara Nyagawa anasema fedha hizo zimewasaidia kuboresha mazingira ya upatikanaji wa elimu kwa watoto na familia zinazoishi na VVU.

KITUO CHA WATOTO YATIMA- MOYO WA HURUMA

Kupitia kampeni hiyo ya Kili Challenge, GGML kwa kushirikiana na Dayosisi ya Kanisa Katoliki Geita, inaendesha kituo cha watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu cha Moyo wa Huruma. Kituo hicho kilichoanzishwa mwaka 2004, kilianza rasmi shughuli zake mwaka 2006.
Kituo cha watoto wanaoishi katika mazingira magumu- Moyo wa Huruma

Kituo hicho ambacho pia kinaendeshwa kwa ushirikiano na Halmashauri ya wilaya ya Geita na Mji wa Geita, kinahudumia watoto 113 na kuajiri wafanyakazi 14 hadi sasa hutumia zaidi ya Sh milioni 50 kila robo ya mwaka kama mishahara huku mahitaji muhimu ya elimu kwa watoto hao ikigharimu zaidi ya Sh milioni 150.


AFYA

Katika sekta ya afya, GGML imewekeza kwa kiasi kikubwa kupitia miradi hiyo ya CSR kwa kutoa misaada katika vituo zaidi ya 20 vya afya vilivyopo mkoani Geita.


Baadhi ya vituo hivyo ambavyo hupatiwa mahitaji mbalimbali ikiwamo vifaa tiba ni pamoja na Nyamalembo, Nyakahongola, Kasota, Kakubiro, Bukoli na Katoro.


Mathalani zaidi ya Sh milioni 565 zimetolewa na GGML kwa hospitali ya rufaa ya Geita na kusaidia kufanya ukarabati wa hospitali hiyo iliyojengwa mwaka 1957 pamoja na kusaidia kuiboresha hospitali hiyo kutoa huduma za moyo.


Katika afya pia GGML imeshirikiana na taasisi ya Rafiki Surgical Mission kutoka Australia ambapo kwa kipindi cha miaka 20 imetoa misaada ya gari nne za kubeba wagonjwa na kutoa ufadhili kwa wagonjwa zaidi ya 2000 waliofanyiwa upasuaji wa mdomo sungura pamoja na wenye majeraha ya moto.



Mmoja wa wagonjwa aliyekuwa na jeraha la moto, Doto Said anaishukuru GGML kwa msaada huo pamoja na madaktari wa Sekou Toure ambao walimpandikiza ngozi kwenye jeraha lake na kumuwezesha kurudisha tabasamu upya.


Mashua tiba (Jubilee boat)

Katika kuhakikisha wananchi wa kanda ya ziwa hususani mikoa ya Geita, Mwanza na Kagera wanapata huduma za afya kwa urahisi, mwaka 2015 GGML kwa kushirikiana na taasisi ya Vine Trust ya nchini Scotland pamoja na Kanisa la African Inland la Geita, waliingia makubaliano ya kutoa huduma za afya kupitia boti maalumu kwa wakazi wa ukanda huo.


Tangu mashuahiyo inayotoa huduma mbalimbali za matibabu, zaidi ya wananchi 158,000 wamenufaika na mashua hiyo inayotoa huduma katika visiwa mbalimbali vilivyopo kwenye Ziwa Victoria kwa siku 14 kisha kurejea Mwanza kwa ajili ya kuweka mafuta. Oktoba 4 mwaka 2021 GGML iliongeza muda wa mkataba.



MAENDELEO YA BIASHARA KWA WATANZANIA

Katika kuzingatia matakwa ya mabadiliko ya sheria ya madini iliyofanyiwa marekebisho 2017, GGML imekuwa ikitoa zabuni kwa wafanyabiashara wa ndani au wazawa ili kutekeleza mpango wa uwajibika wa kampuni kwa jamii.

Kwa kushirikiana na Baraza la Uwezeshaji wananchi Kiuchumi (NEEC), GGML imetoa mafunzo ya masuala ya manunuzi na biashara kwa ujumla ili kupata zabuni za kampuni hiyo kubwa nchini kwa watanzania 300. Hali hiyo imesaidia watanzania kupata zaidi ya asilimia 76 ya zabuni za kampuni hiyo na kuongeza mnyororo wa biashara kati ya GGML na Watanzania.


Akizungumzia mafanikio ya mafunzo hayo, Meneja wa Kampuni ya Blue Coast Investment Limited ambayo ni mmoja wa wakandarasi waliopata zabuni kutoka GGML, Jeremiah Musa, alisema wamefanikiwa kupata zabuni mbili kutoka GGML ambazo ni kusambaza mafuta pamoja na kusafirisha wafanyakazi wa kampuni hiyo.


“Mbali na kusafirisha asilimia 30 ya mafuta ndani ya GGML pia wametupatia mafunzo mbalimbali jambo ambalo limetusaidia kampuni yetu kukua kwa haraka na kupata fursa ya kujitanua na kutoa fursa za ajira kwa Watanzania kwani mpaka sasa tuna wafanyakazi 400 walioajiriwa,” anasema.


MRADI WA IMTT

Vivyo hivyo, katika kuinufaisha jamii ya Watanzania, GGML inatekeleza mradi wa Mafunzo Jumuishi ya Ujuzi kwa Ajili ya Sekta ya Madini (Integrated Mining Technical Training-IMTT) unaolenga kuongeza nguvu kazi kwenye sekta hiyo ya madini.



Mafunzo hayo, hutolewa na Chuo cha Mafunzo ya ufundi stadi VETA- Moshi ambapo kwa kipindi cha mwaka 2021 pekee, GGML ilitoa zaidi ya Sh milioni 132.


UWEZESHAJI WAKULIMA

Kwa upande wa kilimo, GGML kwa kushirikiana na Taasisi ya Kilimo Cholima mwaka 2015 waliendesha programu maalum ya kuwajengea uwezo wakulima wa Nungwe na Bugulula namna ya kulima mazao hayo kisasa. Mafunzo hayo yaliwafikiwa wakulima wa vijiji saba ambao walianzisha kilimo biashara cha alizeti na mpunga.


Katika kipindi cha miaka sita tangu mradi huo uanze, maisha ya wakulima 220 wanaolima hekta 350 za ardhi yamebadilika na kuwa bora kutokana na ufadhili huo wa GGML ambao umewawezesha kupata mashine za kukoboa mpunga na kukamua mafuta.


Katika mradi huo jumla ya wakulima 700 ambao unajumuisha asilimia 85 ya wanawake, wanalima hekta 600.

Kutokana na elimu waliyoipata pamoja na matumizi bora ya ardhi walifanikiwa kupata mavuno zaidi ya asilimia 250 ya mategemeo.


Mageuzi hayo yanadhibitishwa na mmoja wa wakulima wa alizeti katika Kijiji hicho cha Kasota, Saa Kumi Makungu ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama cha ushirika cha NYABUSAKAMA.


“Tunawashukuru uongozi wa GGML na halmashauri kwa kutuunga mkono kwa sababu tulikuwa tunatembea umbali wa kilomita 25 kufuata mashine ya kukamua alizeti lakini sasa tunakamulia hapa karibu vivyo hivyo kwa mpunga,” anasema.




Share:

MBUNGE UMMY AWAPA POLE WAATHIRIKA WA MVUA MAKORORA TANGA

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger