Monday, 17 April 2023

NHC KUJENGA JENGO LA KISASA LA KIBISHARA MANISPAA YA KAHAMA


Meneja wa Shirika la Nyumba (NHC) Angelina Magazi (kushoto) akimkabidhi nyaraka mbalimbali ikiwemo ramani ya ujenzi wa jengo la kisasa la kibiashara linalojengwa katika eneo la kiwanja cha shirika hilo kilichopo eneo la uwekezaji la Bukondamoyo , Halmashauri ya Manispaa ya Kahama anyepokea ni Mhandisi Mburuga Matamwe na Mshauri wa mradi wa Shirika Godfrey Mkumbo na kulia anayeshuhudia ni mkandarasi Mhandisi Masumbuko Majaliwa na kushoto ni Msanifu wa mradi NHC ,Robert Kintu.
Mshauri wa mradi wa Shirika la Nyumba Tanzania ( NHC) Godfrey Mkumbo akiwaonesha eneo mradi wa ujenzi wa jengo la kisasa linalojengwa eneo la uwekezaji la Bukondamoyo , Halmashjauri ya Manispaa ya Kahama , litakalokuwa na vyumba vya maduka vya kisasa, Migahawa, Super Market , sehemu ya kuosha magari , wengine ni meneja wa NHC mkoa wa Shinyanga , Angelina Magazi, meneja Mradi wa NHC , Mhandisi Mburuga Matamwe na Msanifu wa Mradi NHC ,Robert Kintu.
Msanifu wa Mradi wa NHC Robert Kintu wa katikati akiwaonesha maafisa wa NHC ramani ya ujenzi wa jengo la kisasa litakalokuwa na vyumba vya maduka 84 , Migahawa, Super Market na eneo la kuonsha magari ambalo linajengwa katika eneo la uwekezaji lililopo Bukondamoyo , Manispaa ya Kahama.
Meneja wa NHC wa mkoa wa Shinyanga , Angelina Magazi wa katikati akiongoza maafisa wa Shirika hilo katika mradi wa ujenzi jengo la kisasa litakalokuwa na vyumba vya kisasa vya maduka , migahawa , super market , sehemu za kuonya magari ambalo mradi huo umeanza kutekelezwa katika eneo lao la Bukondamoyo , Halmashauri ya Manispaa ya Kahama.
Msanifu wa Mradi wa NHC ,Robert Kintu wa ujenzi wa jengo la kisasa katika eneo la uwekezaji la Bukondamoyo katika Halmashauri ya Manispaa ya Kahama unaotekelezwa na shirika hilo ambalo jengo hilo litakuwa na vyumba vya kisasa vya maduka 84 , Super Market , Migahawa na sehemu ya kuonya magari akiwaonesha maafisa wa NHC ramani ya mradi huo ulioanza kutekelezwa wilayani Kahama


Na Patrick Mabula , Kahama .


Shirika la Nyumba Tanzania (NHC) limeanza kutekeleza mradi wa ujenzi wa jengo la kisasa katika eneo la uwekezaji lililopo Bukondamoyo katika Halamashauri ya Manispaa ya Kahama kwenye eneo lake ambako wanajenga vyumba vya kisasa vya maduka , migahawa, Super Market pamoja na sehemu ya kuoshea magari.


Akiongea katika eneo la mradi huo leo, Meneja wa Shirika la Nyumba wa Mkoa wa Shinyanga , Angelina Magazi amesema mradi huo umeanza kutekelezwa katika kiwanja cha shirika hilo kilichopo eneo la viwanda la Bukondamoyo maarufu kwa jina la Dodoma Manispaa ya Kahama.


Magazi amesema NHC katika mradi huo kutakuwa na vyumba vikubwa vya kisasa vya maduka vipatavyo 84, Migahawa, Super Market na sehemu ya kuosha magari na watapangisha kwa wateja watakao kidhi masharti kwa gharama nafuu kwa lengo la kusaidia ajira kwa watu.


Meneja Mradi wa Shirika la Nyumba Tanzania , Mhandisi Mburuga Matamwe amesema ujenzi wa mradi huo wa majengo ya kisasa ni uwekezaji mkubwa unategemea kugharimu kisasi cha zaidi ya shilingi bilioni moja na tayari mapema utekelezaji wake umeshaanza.


Mshauri wa mradi huo , Mhandisi Godfrey Mkumbo amesema ujenzi wa jengo hilo litakalokuwa na vyumba vikubwa vya maduka vya kisasa utekelezaji wake unatarajia kukamilika katika kipindi cha miezi sita ijayo na hiyo itakuwa ni fursa kwa watu kupangishwa kwa gharama nafuu.


Kwa upande wake mkandarasi wa mradi huo , Mhandisi Masumbuko Majaliwa amesema tayari ameanza utekelezaji wa maradi huo na kuahidi kukamilisha ndani ya kipindi atakachokuwa amepewa kadri ya mkataba unavyosema.

Naye Msanifu wa mradi huo Arch Robart Kintu amesema mradi huo upo eneo zuri lililopo karibu na stendi ndogo ya magari ya abiria ya Bukondamoyo , katika eneo la viwanda la Manispaa ya Kahama ambapo watu watapata fursa ya kujiajiri na pale utakapokamilika katika kipindi cha miezi sita na utachochea maendeleo katika manispaa ya Kahama.


Share:

MFUNGWA AFARIKI KWA KUSHAMBULIWA NA KUNGUNI WENYE NJAA KALI GEREZANI


Familia moja nchini Marekani inataka uchunguzi wa uhalifu ufanyike kuhusu kifo cha jamaa wao aliyefariki akiwa jela baaa ya kudaiwa kung'atwa na kunguni.


LaShawn Thompson, 35, alipatikana akiwa amefariki katika seli chafu ya jela baada ya kuliwa akiwa hai na kunguni mnamo Septemba 2022.

Wakili wa familia hiyo alitoa picha zinazoonyesha mwili wa Thompson ukiwa umejaa kunguni. 

“Jela alilowekwa Thompson halikufaa hata kwa mnyama mgonjwa. Hakustahili kutendewa hili,” ilisoma taarifa ya wakili huyo kwa vyombo vya habari.


Kulingana na ripoti ya Mkaguzi wa Matibabu wa Kaunti ya Fulton, Thompson alipatikana akiwa hana fahamu akiwa jela miezi mitatu baada ya kukamatwa.

 Alithibitishwa kufariki kufuatia majaribio ya polisi wa eneo hilo na wafanyikazi wa matibabu kutaka kumuamsha, kwa mujibu wa ripoti ya USA Today.

 Wakili Harper anasema rekodi za jela zinaonyesha maafisa wa kizuizini na wafanyikazi wa matibabu waligundua kuwa Thompson alikuwa akidhoofika lakini hawakufanya chochote kutoa msaada au kumsaidia vinginevyo.


“Mwili wake ulipopatikana mmoja wa maafisa wa kizuizini alikataa kumfanyia CPR kwa sababu kwa maneno yake ‘alichanganyikiwa.’ Jela alilowekwa Thompson halikufaa hata kwa mnyama mgonjwa. Hakustahili hili.” 

Ripoti ya mchunguzi wa matibabu ilisema kulikuwa na “uvamizi mkali wa kunguni” katika seli yake katika wodi ya wagonjwa wa akili lakini akaongeza hakuna dalili za wazi za kuonyesha kwamba alipata mfadhaiko wa akili kwenye mwili wa Thompson. 

Picha za kutisha zilizoambatanishwa na taarifa ya Harper zinaonyesha seli ya Thompson, ambayo ni chafu mno.


Moja ya picha hizo zinamuonyesha Thompson, ambaye uso na kiwiliwili chake vinaweza kuonekana vikiwa vimefunikwa na wadudu. 

Ripoti ya mchunguzi wa afya wa Kaunti ya Fulton inaorodhesha sababu ya kifo cha Thompson kama haijabainika lakini anabainisha kulikuwa na "uvamizi mkali wa kunguni" kwenye seli yake.

 Kulingana na mtaalamu wa wadudu katika Chuo Kikuu cha Kentucky, ambaye ni mtaalamu wa kunguni, kuumwa na kunguni kwa kawaida hakusababishi kifo.


Hata hivyo, katika baadhi ya matukio nadra, Potter alisema, kuwa katika mazingira ya mrundiko wa kunguni kwa muda mrefu kunaweza kusababisha upungufu wa damu mwilini yaani anemia kali, ambayo inaweza kuwa mbaya ikiwa haitatibiwa.
Share:

JAMAA ASABABISHA MSONGAMANO WA MAGARI BAADA YA KURUSHA MAMILIONI YA FEDHA BARABARANI


Mwanaume mmoja kutoka Oregon amesababisha msongamano wa magari kwa kurusha rundo la pesa kwenye barabara kuu yenye shughuli nyingi. 

Tukio hilo lilitokea kwenye barabara kuu ya I-5 mjini Eugene katika jimbo la Oregon, Marekani.

Kulingana na Fox 2, walioshuhudia tukio hilo walisimamisha magari yao na kukimbilia kuchukua kima cha $100 (KSh 13,000) zilizotawanyika kando ya barabara. 

Watu kadhaa walipiga simu kuarifu maafisa wa polisi wa Jimbo la Oregon kuhusu tukio hilo.

 Polisi waliwasiliana na mtu huyo, Colin Davis McCarthy, mwenye umri wa miaka 38, mkazi wa Eugene, ambaye alisema kuwa alitaka kutoa pesa hizo kama zawadi na kukadiria kuwa alitoa $200,000 sawa na takribani Milioni 460 za kitanzania

Japo hapakuwa na njia ya kudhibitisha kiasi halisi cha pesa kilichotolewa.

Ukarimu wa McCarthy ulisababisha msongamno mkubwa wa magari na hivyo kuwachochea maafisa wa usalama kumkanya kutupa pesa nje ya dirisha lake. 

McCarthy alitii na kukubali kuacha kurusha pesa barabarani. 

Jamaa wa McCarthy waliwaambia polisi kwamba hiyo ilikuwa tabia yake ya kawaida na kwamba alipata pesa hizo kwa kutumia akaunti ya benki ya pamoja ya familia yake, na kuwaacha bila senti.

"Madereva wanaosimama kando ya barabara kuu na kuingiza trafiki ya watembea kwa miguu kwenye barabara kuu huleta hatari kwa waendeshaji magari na watembea kwa miguu wenyewe," Kapteni Kyle Kennedy alisema. 

Aliongeza: “Njia za dharura zimekusudiwa kwa ajili ya dharura, hivyo kuegesha magari pembezoni mwa maeneo hayo si salama kwa ujumla, tunawaomba wananchi waepuke eneo hilo ili kuepusha hali ya hatari na pia kwa sababu hatuamini kuwa hakuna kitu kinachoweza kutokea kwa wakati huu."
Share:

NAIBU KAMISHINA TIRA APONGEZA MKAKATI WA BENKI YA CRDB KUCHOCHEA UJUMUISHI WA BIMA KUPITIA CRDB WAKALA

Naibu Kamishna wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima (TIRA), Khadija Said (watatu kushoto) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa kampeni ya “10 na Kitu” ya Benki ya CRDB inayolenga katika kuadhimisha miaka 10 ya huduma za CRDB Wakala. Wengine pichani ni Mkurugenzi wa Wateja Wago na wa Kati wa Benki ya CRDB, Bonaventura Paul (Wapili Kushoto), Mkuu wa Kitengo cha CRDB Wakala, Ericky Willy (watatu kuli), Mkuu wa Kitengo cha CRDB Al Barakah, Rashid Rashid (wakwanza kuli), Meneja wa Kanda ya Mashariki Benki ya CRDB, Badru Idd, na Meneja wa Ubora na Udhibiti wa Viatarishi TIRA, Zakaria Muyengi.Picha zote na Othman Michuzi.
Dar es Salaam 17 April 2023 – Ikitimiza miaka 10 tokea uanzishwaji wa mfumo wa utoaji huduma wa CRDB Wakala, Benki ya CRDB leo imetangaza kuanzisha huduma za bima kupitia mawakala wake ikiwa ni mkakati wa kusaidia jitihada za Serikali kukuza ujumuishi wa bima nchini.


Mkakati huo umepongezwa na Naibu Kamishina wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima nchini (TIRA), Khadija Said, akisema utakwenda kusaidia kufanikisha lengo la Serikali la kuongeza ujumuishi wa bima kutoka asilimia 15 hivi sasa kufikia asilimia 50 ifikapo mwaka 2030.


“Natambua kuwa Benki ya CRDB ndio kinara kwa idadi ya Mawakala katika sekta ya benki ikiwa na CRDB Wakala zaidi ya 25,000 nchi nzima. Kwa idadi hii nidhahiri kuwa kasi ya ufikishaji na ufikiaji wa huduma za bima itakwenda kuongezeka kwa Kiasi kikubwa,” alisema Naibu Kamishina TIRA huku akiwataka mawakala kufuata miongoz iliyowekwa.


Naibu Kamishina pia aliipongeza Benki ya CRDB kwa mapinduzi makubwa ambayo imeyafanya katika sekta ya fedha nchini katika kipindi cha miaka 10 ya CRDB Wakala. Alisema CRDB Wakala imetoa mchango mkubwa katika kufikisha huduma za fedha kwa wananchi.
Aidha, alipongeza Benki hiyo kwa kuboresha huduma zinazopatikana kupitia CRDB Wakala ambapo sasa hivi wateja wanaweza kupata zaidi ya asilimia 95 ya huduma kupitia mfumo huo ikiwamo huduma ya kufungua akaunti zote za benki ikiwamo akaunti za Al Barakah zinazofuata misingi ya sharia.

“Niwapongeze pia kwa uzinduzi wa kampeni ya ‘10 na Kitu’ ambayo inakwenda kutoa elimu kwa wananchi juu ya huduma zinazotolewa kupitia CRDB Wakala ikiwamo huduma za bima. Niwaombe Mawakala tukashiriki kikamilifu”, aliongezea Naibu Kamishna.
Akielezea kuhusu kampeni ya “10 na Kitu”, Mkurugenzi wa Wateja Wadogo, na wa Kati wa Benki ya CRDB, Bonaventura Paul alisema mbali na kusherehekea maiaka 10 ya CRDB Wakala, kampeni hiyo pia inalenga katika kuhamasisha Mawakala kuongeza kasi ya utoaji huduma kwa kufanya miamala mingi zaidi ili kuchochea ujumuishi wa kifedha.

“Kila mwezi tutakuwa tukitoa zawadi kwa CRDB Wakala ambao watakuwa wamefanya miamala mingi, kufungua akaunti nyingi, na kuuza huduma za bima. Jumla ya zawadi zote katika kampeni hii ni Pikipiki 40, Bajaji 5 na gari aina ya Toyota Alphad kwa mshindi wa jumla,” alibainisha.
Katika kipindi cha maiaka 10, CRDB Wakala imekuwa na mchango mkubwa katika ufikishaji wa huduma za Benki ya CRDB kwa wateja. Bonaventura alisema kuwa takwimu za Benki hiyo zinaonyesha kuwa hivi sasa CRDB Wakala inatoa huduma za kifedha kwa Watanzania zaidi ya milioni 3 kwa mwezi ambapo asilimia 40% ni wateja wa Benki hiyo na asilimia 60 ni wananchi wengine.

Pamoja na mafaniko hayo, taarifa za utendaji za Benki ya CRDB zinaonyesha zaidi ya miamala milioni 100 yenye thamani ya shilingi Trilioni 50 imekua ikifanyika kupitia CRDB Wakala kwa mwaka. Lakini pia, CRDB Wakala imetoa ajira kwa Watanzania zaidi ya 35,000.




Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Mashariki, Badru Idd akuzungumza katika hafla ya kuadhimisha miaka 10 ya huduma za CRDB Wakala iliyoenda sambamba ya uzinduzi wa kampeni ya “10 na Kitu” ya Benki ya CRDB, iliyofanyika kwenye Ukumbu wa. Golden Memory, Sinza jijini Dar es salaam leo.



Mkuu wa Kitengo cha CRDB Wakala, Erick Willy akuzungumza katika hafla ya kuadhimisha miaka 10 ya huduma za CRDB Wakala iliyoenda sambamba ya uzinduzi wa kampeni ya “10 na Kitu” ya Benki ya CRDB, iliyofanyika kwenye Ukumbu wa. Golden Memory, Sinza jijini Dar es salaam leo.



Mkuu wa Kitengo cha CRDB Al-Barakah, Rashid Rashid akuzungumza katika hafla ya kuadhimisha miaka 10 ya huduma za CRDB Wakala iliyoenda sambamba ya uzinduzi wa kampeni ya “10 na Kitu” ya Benki ya CRDB, iliyofanyika kwenye Ukumbu wa. Golden Memory, Sinza jijini Dar es salaam leo.















Share:

MSEVENI AKAMATWA TUHUMA ZA KUMBAKA MTOTO WAKE AKIMLEWESHA KWA POMBE NA CHIPSI


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi akizungumza na waandishi wa habari leo Ijumaa Aprili 7,2023. 

Na Salvatory Ntandu - Kahama 

Mkazi wa mtaa wa Nyasubi wilayani Kahama mkoani Shinyanga Mseveni Mchele (35-40) anashikiliwa na jeshi la Polisi kwa tuhuma ya kumbaka mtoto wake wa kufikia mwenye umri wa miaka 12 Mwanafunzi darasa la saba shule ya Msingi Nyasubi.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi amethibitisha kukamatwa kwa Mseveni na kudai kuwa Jeshi la Polisi wanaendelea na upelelezi wakikamilisha atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili.

Alisema kuwa kitendo alichokifanya Mchele ni kiyume na maadili ya Kitanzania kwani haiwezekani baba kumbaka mwanae hata kama hajamzaa,na kuwataka wazazi na walezi kutokengeuka na badala yake watimize wajibu wao katika Malezi bora ya Watoto.

“Katika hili jeshi la Polisi mkoa wa Shinyanga hatutakuwa na mhali kwa mtuhumiwa kwani kitendo alichonya sio cha kiungwana haiwezekani baba kubaka mwanae tutahakikisha hatua kali za kisheria zinachukuliwa kwake ili iwefundisho kwa watu wengine,’alisema Magomi.

Naye Afisa ustawi wa jamii Manispaa ya Kahama Abrahaman Nuru alisema kuwa baada ya Mseveni kukamatwa walilazimika kumpeleka hospitali mwanafunzi huyo kwa ajili ya vipimo ambapo daktari alibainisha kuingiliwa.

“Mseveni baada ya maafisa Ustawi kumkamata alikiri kutenda kosa hilo kwa madai kuwa ulevi ndio umemsababishia kufanya kosa jambo lililosababisha kumpeleka kituo cha polisi Kahama kwa taratibu za kisheria,”alisema Nuru.

Kwa upande wake Mhanga wa tukio hilo ambaye jina lake limehifadhiwa alikiri kubakwa na baba yake wa kambo kwani alikuwa anamletea Chipsi na Kimiminika cheupe chenye asili ya Kilevi ambacho alikuwa anamlazimisha kunywa kwa madai kuwa ni dawa ya kutibu ugonjwa wa UTI.

“Wiki mbili zimepita baada ya Mama yangu kusafiri kwenda mkoani Morogoro kwenye matibabu baba amekuwa akinipa vimiminika hivyo na kujikuta nimelewa na nipo chumbani kwake nikiwa nimevuliwa nguo,”alisema Mhanga wa ukatili.

Hata hivyo Mama mkubwa wa Mhanga wa ukatili huo ambaye hakutaka jina lake litajwe alisema kuwa taarifa za kubakwa kwa binti huyo zilitolewa na majirani zake baada ya kusikia kelele usiku za mwanae kufanyiwa ukatili huo na baba yake wa kambo ndipo walipotoa taarifa kwa ustawi wa jamii Kahama.

“Kwa sasa nimemchukua mwanangu wakati tunamsubiraia mama yake atoke kwenye matibabu mkoani Morogoro,kitendo alichokifanya baba yake wa kambo hakifai na tunaiomba serikali ichukue hatua kali za kisheria ili iwe fundisho kwa wazazi wanaowafanyia ukatili watoto wao,”alisema Mama mkubwa mhanga wa ukatili.
Share:

TANROADS KUPITIA WAKANDARASI WAZAWA, YAKAMILISHA UJENZI WA BARABARA KWA KIWANGO CHA LAMI RUDEWA-KILOSA (KM 24)


Na Mwandishi Wetu, Morogoro 

Mradi wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami Dumila-Kilosa-Mikumi sehemu ya LUDEWA-KILOSA yenye urefu wa kilometa 24 umefikia asilimia 90 ambapo mradi huo unatarajiwa kukamilika Julai, mwaka huu.

Kazi iliyobakia ni ujenzi wa madaraja matatu huku ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami ikiwa imekamilika na kuendelea kutumika.

Hayo yamesemwa Aprili 16, 2023 na Kaimu Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Morogoro Mhandisi Mussa Kaswahili akitembelea miradi ya Ludewa-Kilosa na daraja la Kiyegeya lililopo wilayani Gairo ambapo amesema barabara hiyo ni sehemu ya barabara ya mkoa huo ambayo inaanzia Dumila hadi Mikumi.

Mhandisi Kaswahili ameongeza kuwa, hapo awali watumiaji wa barabara hiyo walikuwa wanatumia muda mrefu barabarani hadi kufika wakitokea Dumila kwenda Rudewa au Kilosa kutokana na ubovu wa barabara iliyokuwepo.

"Hapo awali kabla ya ujenzi wa barabara ya Dumila hadi Kilosa, ilikuwa kutoka Dumila hadi Ludewa ilikuwa ni masaa matatu lakini kwa sasa ni takribani dakika 40 tu unakuwa umefika" alisema Mhandisi Kaswahili.

Mhandisi Kaswahili ameendelea kwa kusema kuwa, mradi wa Ludewa-Kilosa ulibuniwa ili kuwajengea uwezo wakandarasi wazawa katika kuongeza ushiriki wako kwenye miradi ya ujenzi wa miundombinu.


"Mradi wa Ludewa-Kilosa ulibuniwa ili kuwajengea uwezo wakandarasi wazawa, katika mradi kuna wakandarasi 7 walioungana na kuunda Umoja Kilosa JV lengo ni kutumia wakandarasi wazawa badala ya kutumia wakandarasi wa kigeni hapo baadaye" alisisitiza Mhandisi Kaswahili

Wakiongea kwa nyakati tofauti, Meneja wa mradi LUDEWA-KILOSA kutoka kampuni ya ushauri ya Pidael JV Consulting Engineers Mhandisi Protas Mwasyoke na msimamizi wa mradi upande mkandarasi, Mhandisi Leons Msoka wamesema kwa mwenendo wa kazi za ujenzi zinavyoendelea na kwa kazi ikiyobakia ya ujenzi wa madaraja matatu, kazi hiyo itakamilika kwa wakati mwezi Julai, mwaka huu.

Akiwa katika daraja jipya la Kiyegeya wilayani Gairo, Mhandisi Kaswahili emeeleza kuwa, daraja hilo limejengwa kwa viwango na teknolojka ya kisasa na kumaliza kabisa changamoto iliyokuwa ikitokea hapo zamani hususan nyakati za mvua na hata kupelekaa daraja la zamani kubomoka na kuathiri shughuli za usafiri na usafirishaji.

Kufuatia hatua hiyo, serikali iliiingia katika mpango wa dharura na kutenga fedha haraka kwa ajili ili kujenga daraja jipya la Kiyegeya chini ya usimamizi wa Kitengo cha wahandisi washauri wa TANROADS Mkoa wa kwa kushirikiana na TANROADS makao makuu.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa daraja la kisasa la Kiyegeya Mhandisi Kaswahili amesema,

"Ujenzi wa daraja la Kiyegeya limegharimu kiasi cha shilingi bilioni 6.9 ambao mradi wa ujenzi wa daraja hilo ulikamilika Februari 28, 22022 na linatumika kwa asilimia 100 na kuongeza kuwa

"Nipende kuishukuru serikali ya awamu sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutenga na kuleta fedha ili miradi ya kimkakati ikiwemo mradi huu (ujenzi wa daraja la Kiyegea) iweze kutekelezwa na kufungua shughuli za uchumi za nchi na kwa mwananchi mmoja mmoja"

Mkoa wa Morogoro una madaraja takriban 2,029 huku mtandao wa barabara ukiwa takriban kilometa 2070. Serikali inaendelea kutenga fedha ili kuhakikisha barabara hizo zinahudumiwa ili kuweza kuhakikisha kwamba zinapitika muda wote na majira yote ya mwaka.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger