Saturday, 8 April 2023

MIAKA MIWILI YA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN TARURA MKOA WA RUVUMA KAZI INAENDELEA


KATIKA kipindi cha miaka mwili ya uongozi wa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mtandao wa barabara za vijijini na mijini kwa Mkoa wa Ruvuma zimeimarika maradufu.

Hatua hii imetokana na uamuzi wa dhati wa Rais Samia wa kuongeza bajeti kwa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mkoa wa Ruvuka kwa zaidi ya mara mara tatu.

TARURA Mkoa wa Ruvuma inahudumia jumla ya kilomita 7,146.202 za barabara, kati ya hizo kilomita 2,312.83 sawa na asilimia 32.36 ni za mjazio, kilomita 3,873.85 sawa na asilimia 52,85 ni mkusanyo na kilomita 959.52 sawa na asilimia 13.43 ya mtandao mzima wa mkoa ni za jamii/kijiji.

Anapozungumzia mafanikio ya miaka miwili ya Mheshimiwa Rais Samia, Meneja wa TARURA Mkoa wa Ruvuma Mhandisi Wahabu Nyamzungu anasema mwaka 2020/21 mkoa ulitengewa Sh bilioni 7.973 za Mfuko wa barabara zilizotumika kufanya matengenezo ya kawaida ya kilomita 549.61 kwa Sh bilioni 1.356, sehemu korofi kilomita 137.29 kwa Sh bilioni 1.165, madaraja madogo 4, boksi kalavati 17, makalavati 11, madrifti 5 na mifereji ya maji yenye urefu wa mita 2,000 kwa gharama ya Sh bilioni 1.113,

Anasema hali ya mtandao wa barabara ulikuwa na kilomita 890.449 za barabara za changarawe sawa na asilimia 12.46, kilomita 93.635 barabara za lami sawa na asilimia 1.31, kilomita 3.92 barabara za zege na kilomita 6,159.19 zilikuwa barabara za udongo ambazo ni asilimia 12.46.

Anasema kuwa barabara zenye hali nzuri zilikuwa ni kilomita 1,391.453, hali ya kuridhisha kilomita 1,572.083, hali isiyoridhisha kilomita 4,182.667, madaraja 471, makaravati 1,940 na drifti 63.

“ Kwa kweli hali ya utekelezaji wa miradi ya barabara ilikuwa changamoto kubwa kwa kuwa bajeti ya utekelezaji wa miradi kwa mwaka ilikuwa finyu.”

Mhandisi Nyamzungu anasema kuwa mwaka 2021/22 ikiwa ni ndani ya miaka mwili ya uongozi wa Rais Samia TARURA Mkoa wa Ruvuma ulitengewa Sh bilioni 20.166 ambazo za tozo ya mafuta ni Sh bilioni 7, fedha za jimbo Sh bilioni 4.5, mfuko wa barabara Sh bilioni 7.383 na mfuko wa maendeleo Sh bilioni 1.283.

Anasema kwa mwaka 2022/23 Mkoa wa Ruvuma imetengewa bajeti ya Sh bilioni 23.757 na kati ya hizo fedha za tozo ya mafuta ni Sh bilioni 10.025, mfuko wa barabara ni Sh bilioni 6.918, fedha za miradi ya maendeleo ni Sh bilioni 1.39 na fedha za majimbo Sh bilioni 4.5.

“ Hivyo kwa miaka mwili ya uongozi wa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan TARURA Mkoa wa Ruvuma tumepokea shilingi bilioni 43.924 zikiwa ni fedha za matengenezo ya barabara na madaraja.”

Anasema baada ya ongezeko la bajeti hali ya barabara kwa Mkoa wa Ruvuma imeimarika zaidi ambapo kilomita 1,372.581 ni barabara za changarawe, kilomita 118.688 ni barabara za lami, kilomita 6.92 ni barabara za zege na kilomita 5,658.41 ni barabara za udongo.

“Kwa sasa barabara zinazopitika kwa mwaka mzima zimefikia asilimia 35. Pia barabara zenye hali nzuri ni kilomita 2.250.387, zenye hali ya kuridhisha ni kilomita 1,767.889 na zile zilizo katika hali isiyoridhisha ni kilomita 3,127.913 na kuna madaraja 511, makalavati 2,130 na drifti 63.”

Anasema pia utekelezaji wa miradi ya barabara kwa sasa imeimarika ambapo ndani ya miaka mwili TARURA Mkoa wa Ruvuma umefanya matengenezo ya barabara kwa kiwango cha changarawe kilomita 482.132, ujenzi wa barabara za lami kilomita 25.053, ujenzi wa madaraja 40, ujenzi wa mifereji ya maji ya mua urefu wa mita 3,400.

Pia ujenzi wa barabara za zege katika maeneo yenye miinuko na miteremko kilomita 6.92, ufunguzi wa barabara mpya kilomita 500.03 ambazo hazijawahi kufunguliwa tangu tupate uhuru na kupunguza kiwango cha barabara za udongo kutoka kilomita 6,159.19 hadi kufikia kilomita 5,658.41.

Aidha, ongezeko la uwekaji wa taa za barabarani imeongezeka kwa kiwango kikubwa kutoka idai ya taa 34- hadi kufikia taa 383 ikiwa bado idadi ya taa zinazotarajiwa kuweka mpaka kufikia Juni mwaka huu kufikia taa 420.

Mhandisi Nyamzungu anataja baadhi ya miradi ya kimkakati ambayo TARURA Mkoa wa Ruvuma imeitekeleza katika kipindi hicho ni ujenzi wa barabara ya Luhindo-Mpepo-darpori kwa kiwango cha changarawe urefu wa kilomita 27.52.

“Barabara hii imeongeza tija kwa wakulima wa kahawa na sekta ya usafiri na usafirishaji kwani kabla ya maboresho gari zilizokuwa zikitumiwa na wananchi wa Kata ya Mpepo ni landrover pekee lakini sasa basi za abiria zimeweza kufika.”

Mhandisi Nyamzungu anasema pia kufungua barabara za fukwe za Ziwa Nyasa kwa ajili ya kuhamasisha utalii katika Wilaya ya Nyasa ambazo zimeboreshwa kwa fedha za tozo za mafuta.

“Eneo la fukwe za Nyasa kata ya Kilosa na Mbamba Bay halikuwa na barabara zilizoboreshwa lakini katika kipindi cha miaka mwili ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan tumeweza kufungua kilomita 14 za barabara za changarawe, barabara hizi zitaboresha na kuleta hamasa katika sekta ya utalii wa picha na kufutia wawekezaji wa ufukweni.”

Mhandisi Nyamzungu anasema pia kuondoa vikwazo kwa kujengwa madaraja na makalavati, kujenga barabara za lami kwenye katika miji na makao makuu ya kila wilaya, kufungua barabara mpya hasa katika maeneo ya uwekezaji mkubwa wa sekta ya kilimo na uchimbaji wa makaa ya mawe.

Kuendeleza barabara za mitaa kwa kiwango cha changarawe na kuweka taa katika miji mbalimbali kwenye maeneo ya miji.

“Tunachukua nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kuongoza kwa mafanikio hasa katika sekta ya mundombini na kuondoa vikwazo vya usafiri na usafirishaji wa mazao vijijini.”

“ Kwa kuongeza fedha kumeongeza ufanisi kwenye utekelezaji wa miradi, kuinua uchumi kwa wananachi wa kawaida hasa wakulima kwa kuwawezesha kusafirisha mazao ya kwa urahisi kuyafikia masoko na hatimaye kukidhi mahitaji yao kwa urahisi.”

Mhandisi Nyamzungu anaongeza: “tunamwomba Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kuendelea kutuwezesha TARURA ili tuweze kutimia kauli mbiu yetu isemayo ‘Tunakufungulia barabara kufika kusiko fikika’.”
Share:

LORI LAUA WAENDESHA BODABODA ZAIDI YA 10 KIJIWENI


Watu kadhaa wamepoteza maisha baada ya lori lililokuwa likisafirisha changarawe kupoteza mwelekeo na kugonga kundi la bodaboda waliokuwa wameegesha eneo lao (kijiweni) mjini Migori nchini Kenya.

Tukio hilo la asubuhi ya Jumamosi - Aprili 8,2023 limeshuhudia umati mkubwa wa watu ukimiminika eneo la tukio ili kuwanusuru majeruhi na kuwakimbiza hospitalini kwa matibabu. 

Kwa mujibu wa raia mmoja aliyeshuhudia na kuzungumza na runinga ya TV47, breki za lori hilo zilifeli na kuingia katika kundi hilo la bodaboda ambao walikuwa wanasubiri abiria. 

Ajali hiyo imefanyika karibu na shule ya msingi ya Migori. Eneo la tukio lilikuwa limejaa damu na miili. 

Vyuma pia vilikuwa vimetapakaa eneo hilo.

Eneo la tukio linaripotiwa kuwa na zaidi ya miili kumi huku ambulansi na wazima moto kutoka kwa serikali ya kaunti ya Migori wakifika eneo la ajali hiyo.
Share:

RIPOTI ZA CAG: UFISADI HAUJAZIDI NCHINI, KILICHOZIDI NI UHURU


Na Mwandishi Wetu, Dodoma


Ripoti za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali (CAG) zimeibua mjadala mkubwa na mpana nchini tangu zitolewe hadharani siku chache zilizopita.


Ripoti hizo za mwaka wa fedha wa 2021-2022 zimeweka bayana kasoro mbalimbali kwenye serikali kuu, tawala za mikoa na serikali za mitaa pamoja na mashirika ya umma.


Kasoro hizo ni pamoja na tuhuma za ubadhirifu wa pesa za umma na uendeshaji wa hasara wa baadhi ya mashirika ya umma.


Lakini, mambo yaliyoibuliwa na ripoti hizi mpya za CAG siyo mapya na siyo ishara ya kuongezeka kwa ufisadi nchini.


Mfuatiliaji yoyote makini wa ripoti za CAG atabaini kuwa mambo yaliyoibuliwa kwenye ripoti za mwaka huu yamekuwa yakiibuliwa pia kwenye ripoti za awamu zilizotangulia kwa miaka kadhaa sasa.


Kuna tofauti kuu saba zifuatazo kati ya mazingira ya utoaji wa ripoti za CAG chini ya Awamu ya Tano na utoaji wa ripoti za CAG kwenye Awamu hii ya Sita:


1. Kuongezeka kwa uhuru wa CAG


Tangu aliyekuwa CAG, Profesa Mussa Assad, kung’olewa kazini na utawala wa Awamu ya Tano kinyume na katiba kwa kusema ukweli na kusimamia kile anachokiamini, ofisi ya CAG imekosa uhuru wa kufanya kazi yake, hadi ilipoingia madarakani Serikali ya Awamu ya Sita na kurejesha uhuru huo kwa CAG.


Kwenye awamu iliyopita, CAG hakuwa na uhuru wa kukagua na kutoa ripoti za miradi ya kimkakati ya maendeleo, ikiwemo reli ya SGR, ununuzi wa ndege za ATCL, TTCL na ujenzi wa mradi wa kufua umeme wa JNHPP, tofauti na sasa kwenye Awamu ya Sita ambapo amepewa uhuru kufanya ukaguzi na kubaini kasoro kadhaa kwenye miradi hiyo.


2. Kuongezeka kwa uhuru wa vyombo vya habari


Uhuru wa habari umeimarika kwenye Awamu ya Sita na kuvipa vyombo vya habari fursa ya kuripoti tuhuma zilizoibuliwa na CAG bila woga wa kufungiwa au kushughulikiwa na watu wasiojulikana.


Maana yake ni kwamba, maudhui yaliyomo kwenye ripoti za CAG yameripotiwa kwa uzito mkubwa na vyombo vya habari tofauti na hali ilivyokuwa chini ya Awamu ya Tano, ambapo wanahabari waliogopa kuripoti taarifa hizo.


3. Kuongezeka kwa uhuru wa vyama vya upinzani

Awamu ya Sita imerejesha uhuru wa vyama vya siasa kufanya mikutano ya hadhara, na hiyo imewapa fursa viongozi wa upinzani kuzunguka nchi nzima kuzungumzia ripoti za CAG kwenye majukwaa ya siasa na hivyo basi kusambaza mjadala huo kila kona ya nchi.


Kiongozi mmoja wa chama kimoja cha upinzani alisikika akisema juzi kwenye mkutano wa hadhara kuwa angekuwepo aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano, wote waliotajwa kwenye ripoti za CAG “wasingekuwepo.”


Kauli hiyo imewashangaza hata wafuasi wa chama hicho, kwani kiongozi huyo huyo wa upinzani alikimbia nchi kusalimisha maisha yake kwenye utawala wa Awamu ya Tano na mikutano ya hadhara ya vyama vya upinzani ilipigwa marufuku, ambapo asingeweza kuwa na jukwaa la hadhara la kuzungumzia ripoti za CAG.


4. Kuongezeka kwa uhuru wa wanaharakati

Taasisi zisizo za kiserikali pamoja na wanaharakati wamepata uhuru zaidi kwenye Awamu ya Sita kuzungumzia mambo mbalimbali, ikiwemo ripoti za CAG, tofauti na hali ilivyokuwa kwenye awamu iliyopita.


5. Kuongezeka kwa uhuru wa wabunge wa CCM

Wabunge wa chama tawala, ambao kwenye awamu iliyopita walizibwa mdomo na hawakuwa na uhuru wa kuikosoa serikali ndani na nje ya Bunge, sasa wanatumia uhuru wao chini ya Serikali ya Awamu ya Sita kupaza sauti zao juu ya kasoro zilizotajwa na CAG.


6. Kuongezeka kwa uhuru wa wastaafu

Viongozi mbalimbali wastaafu ambao kwenye Awamu ya Tano waliambiwa wakae kimya waache “kuwashwa washwa” sasa hivi wana uhuru wa kuongea, kushauri na hata kuikosoa serikali bila hofu yoyote.


7. Kuongezeka kwa uhuru wa kuongea wa wananchi


Tofauti na hali ilivyokuwa kwenye Awamu ya Tano ambapo wananchi walikosa uhuru wa kuongea na kuikosoa serikali, wananchi sasa wamerejeshewa uhuru huo chini ya Awamu ya Sita na wanautumia kujadili ripoti za CAG kwa uwazi bila woga.


Wachambuzi wa masuala ya utawala wanasema kuwa uamuzi wa Serikali ya Awamu ya Sita wa kurejesha tunu za taifa za uhuru na haki kwa kiasi kikubwa utachochea utulivu wa kisiasa na maendeleo endelevu nchini.


Mjadala unaoendelea wa ripoti za CAG umedhihirisha kuwa kilichozidi nchini siyo ufisadi wala uendeshaji mbovu wa mashirika ya umma, bali kilichozidi kwenye Awamu ya Sita kulinganisha na awamu iliyopita ni uhuru. Na hili ni jambo jema sana kwa mustakabali wa taifa letu.

Share:

Friday, 7 April 2023

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI APRILI 8,2023



























Share:

YESU WA TONGAREN AGOMA KUSULUBISHWA


Eliud Wekesa almaarufu yesu wa Tongaren kutoka kaunti ya Bungoma nchini Kenya ameonekana kuwajibu watu waliotaka asulubishwe wakati huu wa pasaka jinsi Yesu Kristo alivyofanyiwa.

Katika Video iliyosambazwa mtandaoni yesu wa Tongaren anasikika akisema kuwa katika maandiko yake na kuelewa kwake kwa kitabu kitakatifu hakuna mahali ambapo yesu alisulubishwa mara mbili.

"Sijawahi kuona mahali popote hata katika chuo changu cha mbinguni kwamba waliandika yesu atasulubiwa mara ya pili," Yesu wa Tongaren alisema. 

Yesu wa Tongaren alisema kuwa imeandikwa kuwa yesu atakaporudi atakuwa sawa na bali hatorejelea tena katika usulubissho aliopitia kuwakomboa wanadamu.

Yesu wa Tongaren ameongoza ibada ya maombi ya siku kuu ya pasaka katika kanisa lake na kusema kuwa watafunga kwa kwa siku tatu wakiomba.
Share:

AUAWA KWA KUCHOMA KISU BAADA YA KUOMBA MAJI YA KUNYWA TANGA

Jeshi la Polisi Mkoani Tanga linamshikilia Hassan Nyundo (25) Mkazi wa Kijiji cha Vue kata ya Mowa Wilayani Mkinga kwa tuhuma za kumchoma kisu Amiri Mohamed (30) huku ikidaiwa kwamba sababu mojawapo ya ugomvi ni kitendo cha Amiri kumuomba maji ya kunywa wakati akifahamu kuwa Hassan amefunga Mwezi Mtukufu wa Ramadhan.

RPC Henry Mwaibambe amesema kuwa 05/04/2023 majira ya saa sita mchana Amiri na Mtuhumiwa walikuwa wakiishi nyumba moja hivyo hadi mauti yanamkuta Amiri alimshinikiza Mtuhumiwa kumpatia maji ya kunywa kitendo kilichomchukiza Hassan (Mtuhumiwa) na kusababisha ugomvi uliopolekea kumchoma kisu kulikosababisha kufia njiani wakati akiwaishwa Hospitali.

Kamanda Mwaibambe amesema hadi sasa kuna taarifa mbili juu ya tukio hilo ambapo wengine wanasema Mtuhumiwa alichukizwa na kitendo cha Amiri kumuomba maji pamoja na kunywa maji wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhani lakini wengine wanasema ni ugomvi wa kawaida.

“Kwakweli hadi sasa chanzo kamili cha tukio hilo bado hakijajulikana kwani hawa wawili ni ndugu waliokuwa wakiishi nyumba moja, ni mauaji ya kusikitisha sana haiwezekani ugomvi wa maji tu unachomoa kisu una mchoma mwenzako, kwakweli huu ni mmomonyoko mkubwa wa maadili”.
Share:

LEMBELI ATEMBELEA MAENEO YA KIHISTORIA NEW YORK - MAREKANI..ASEMA TANZANIA INALIPA KIPAUMBELE SUALA LA UHIFADHI NA ULINZI WA MAZINGIRA


Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Jane Goodall Tanzania Bw. James Lembeli ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi ya Taasisi hiyo nchini Marekani na Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kahama akiwa katika Bustani ya New York City Park.
**
Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Jane Goodall Tanzania Bw. James Lembeli ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi ya Taasisi hiyo nchini Marekani na Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kahama amesema Tanzania,kama ilivyo kwa nchi nyingine inalipa kipaumbele suala la ulinzi wa mazingira na uhifadhi kuepusha janga linaloweza kutokea kutokana na athari za mabadiliko ya tabia nchi ambazo tayari katika nchi nyingine zimeanza kuleta madhara makubwa.


Ametaja madhara hayo ni mafuriko,vimbunga,joto kali na kuyeyuka kwa theluji huko antaktika na ktk vilele vya milima ikiwemo kilimanjaro kuwa ni mifano halisi.


Lembeli amesema hayo juzi mjini New York wakati akiongea na wadau wa masuala ya mazingira kutoka sehemu mbambali za Dunia wakati wa ghahla ya kumpongeza mwanzilishi taasisi ya Jane Goodall kutimiza miaka 89 na miaka karibu miaka 63 tangu atue Kigoma,Tanzania kuanza kazi ya utafitiwa wa Sokwe na wanyama wengine aina ya Nyani.


Amesema,Kwa kutambua msimamo wa Tanzania ktika sekta za mazingira na uhifadhi,serikali ya Marekani kupitia shirika lake la misaada USAID ilitoa msaada wa Dola milioni 20 kwa ajili ya mradi wa kuimarisha na kuboresha mazingira katika mikoa ya Kigoma na Katavi ulioanza mwaka 2013 na ambao utamalizika novemba mwaka huu.


Mradi huo umejikita hususani katika elimu ya kuhifadhi misitu ya asili katika maeneo hayo,afya na elimu ya kujitegemea hususani Amina mama na vijana vijiji.


Taasisi ya Jane Goodall ambayo chimbuko lake ni Gombe, Kigoma Tanzania ambako muasisi wake (Jane Goodall) alifika kuanza kazi ya utafiti wa Sokwe na wanyama aina ya nyani inafanya kazi ktk nchi zaidi ya 60 ulimwenguni ikiwa imejikita kuhusani katika suala la elimu ya uhifadhi wa mazingira kupitia programu yake ya vijana ya Roots and Shoot-lengo likiwa ni kuiponya Dunia na tatizo la uharibifu wa mazingira hivyo kuwa sehemu Bora ya kuishi wanadamu na viumbe vingine.


Akiwa New York,lembeli licha ya kuhudhuria kikao cha Bodi ya Wakurungenzi ya Jane Goodall-Marekani pia alipata fursa ya kukutana na watu mbalimbali na kutembelea maeneo mbalimbali ya kihistoria ikiwa pamoja na kanisa Kuu katoliki la Mtakatifu Patrick ambapo alipata fursa ya kuingia na kusali, Bustani kubwa ya mjini New York, New York Central Park, Makumbusho ya Brooklyn na Lockfeller Center.


Sherehe ya miaka 89 ya kuzaliwa Jane ilifanyika katika hoteli maarufu ya mjini New York Litz Calton.
Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Jane Goodall Tanzania Bw. James Lembeli ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi ya Taasisi hiyo nchini Marekani na Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kahama akiwa katika Bustani ya New York City Park
Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Jane Goodall Tanzania Bw. James Lembeli ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi ya Taasisi hiyo nchini Marekani na Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kahama akiwa katika Bustani ya New York City Park
Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Jane Goodall Tanzania Bw. James Lembeli ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi ya Taasisi hiyo nchini Marekani na Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kahama akiwa katika  kanisa kuu la Mtakatifu Patrick-New York
Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Jane Goodall Tanzania Bw. James Lembeli ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi ya Taasisi hiyo nchini Marekani na Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kahama akiwa katika  kanisa kuu la Mtakatifu Patrick-New York
Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Jane Goodall Tanzania Bw. James Lembeli ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi ya Taasisi hiyo nchini Marekani na Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kahama akiwa katika Rockefeller Center
Studio za radio na NBC tv
Share:

PROGRAMU YA TAIFA YA KUKUZA UJUZI YAWAKUNA WABUNGE


Mbunge wa Kigoma Mjini Mhe. Kilumbe Ng'enda ameipongeza Ofisi ya Waziri Mkuu kwa namna inavyoshoghulikia changamoto ya ajira kwa vijana nchini kupitia Programu ya Taifa ya Kukuza Ujuzi ambayo imekuwa chachu ya vijana kujiajiri na kuajiri wenzao. 

Akichangia Aprili 6, 2023 bungeni mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2023/24, Mbunge huyo amesema programu hiyo iwe endelevu kwa kuwa ina manufaa yenye tija kwa nguvukazi ya Taifa kupata ujuzi unaowawezesha kujiajiri sambamba na kujikwamua kiuchumi.

 "Nimetembelea Chuo cha VETA Kigoma nimeshuhudia kijana ameweza kutengeneza redio na anarusha matangazo mwenyewe katika jamii inayomzunguka, hivyo kijana huyo akiendelezwa anaweza kufanya mambo makubwa sana," amesema. 

Vilevile, amesema uwepo utaratibu wa kuwawezesha vitendea kazi vijana hao wanapomaliza mafunzo yao ili waweze kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi. 

Pia, ameshauri serikali kuweka utaratibu maalum wa kuendeleza vipaji vya vijana wabunifu ambao wamenufaika na programu hiyo.
Share:

WAZIRI MHAGAMA,SIMBACHAWENE WAKABIDHIANA OFISI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na Watumishi wa Ofisi hiyo (hawapo pichani)  wakati wa makabidhiano ya Ofisi kati yake na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi  wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene yaliyofanyika Jijini Dodoma..





Aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. George Simbachawene  ambaye kwa sasa ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi  wa Umma na Utawala Bora akimkabidhi nyaraka  Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu)  Mhe. Jenista Mhagama  wakati wa hafla ya  makabidhiano ya Ofisi  kati yao.  Kulia ni Katibu  Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. Jim Yonazi katika Ukumbi wa Ofisi hiyo  Aprili 06, 2023 Jijini Dodoma.


Na Mwandishi wetu, DODOMA.


WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama amewataka watumishi wa umma kutekeleza  majukumu yao ipasavyo  kwa ajili ya maendeleo ya wananchi na Taifa kwa ujumla.

Ameyasema hayo wakati wa hafla ya makabidhiano  kati ya aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene na aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Jenista Mhagama mara baada ya uteuzi uliyofanywa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia  Suluhu Hassan  Aprili 01 mwaka 2023.

Waziri  Mhagama  amesema dhamira ya mtumishi wa umma Nchini ni kuhakikisha anatimiza wajibu wake kikamilifu katika kuwahudumia wananchi mahali na kwa nafasi yoyote anayopangwa  kwa kuzingatia miongozo na taratibu  zilizopo.

“Mara zote dhamira ya mtumishi wa umma  Nchini ni kuhakikisha kila unapopangwa unafanya kazi kwa nguvu zako zote pamoja na utii  na kuwa tayari kutumikia Taifa mahali popote kwahiyo kurudi kwangu hapa najihesabu ni sehemu yenu pia kama mtumishi wa umma,” Amesema Mhe. Jenista.

Pia amebainisha kwamba Ofisi ya Waziri Mkuu ambayo ina jukumu la kuratibu shughuli za Serikali haiwezi kufanikiwa ikiwa watumishi wake watashindwa kujidhatiti na kufanya kazi kwa moyo kwa kuzingatia mazingira husika.

“Msingi wa tija katika utendaji wa kazi Serikalini  unatutaka  kuwa na uratibu mzuri unaozingatia sera, miongozo na kanuni zilizopo kwa kuzingatia jukumu kubwa la Ofisi ya Waziri Mkuu ni kuratibu shughuli zote za Serikali na tuna jukumu la kusimamia Bunge kama mhimili mwingine ndani ya Nchi hivyo bila kuwa na ushirikiano hatutafikia malengo tunayokusudia,” Ameeleza.

Kwa upande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene amemshukuru  Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa  kumuamini na kumpa  fursa ya kulitumikia Taifa pamoja na watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu  kwa ushirikiano wakati wote wa utekelezaji wa majukumu yake.

“Nitumie nafasi hii kumshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kuniamini  kuendelea  kuwatumikia wananchi katika nafasi hii na watumishi pia nawashukuru kwa ushirikiano mlionipatia na kuwezesha kufanikisha shughuli za uratibu kwa kipindi chote,” Ameshukuru Mhe. Simbachawene.

Naye Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Dkt. Jim Yonazi amemshukuru Mhe. Simbachawene kwa utumishi wake mwema katika Ofisi hiyo.

Aidha ametumia nafasi hiyo kumkaribisha Mhe. Waziri Mhagama katika Ofisi ya Waziri Mkuu na kuahidi kumpa ushirikiano ili kufikia malengo ya Serikali ya kuwatumikia wananachi.

 

 

Share:

Thursday, 6 April 2023

SHEIKH WALID KAWAMBWA AIPONGEZA PUMA ENERGY TANZANIA KWA KUWAUNGANISHA WATANZANIA

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Puma Energy Tanzania, Fatma Abdallah, akiwashukuru wageni waalikwa mbalimbali baada ya futari iliyoandaliwa na kampuni hiyo, Dar es Salaam, Miongoni mwa wageni waaalikwa kwenye futari hiyo ni Kaimu Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam Walid Alhad Kawambwa.
*******************

Na Mwandishi Wetu

KAIMU Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam Walid Alhad Kawambwa ameipongeza Kampuni ya Puma Energy Tanzania kwa kuwaunganisha Watanzania kupitia programu zake mbalimbali za kibiashara.

Amesema kampuni hiyo inajali kazi zake, kwa sababu ni chombo cha kibiashara na moja ya utaratibu wa biashara ni kuvuta soko ambalo halipatikani bila kutanguliza mapenzi ya dhati ya shughuli zake.

Sheikh Walid ametoa pongezi hizo, wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na kampuni hiyo, Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wageni wadau mbalimbali huku kwa upande wa Puma wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wake Fatma Abdallah na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Puma Energy Tanzania Dk. Suleiman Majige.

Amesema walichokifa Puma Energy Tanzania, kimeonesha wameelewa maagizo ya Mwenyezi Mungu ya kutaka watu kuishi pamoja, huku akisisitiza kampuni hiyo inajali kazi zake.

“Niwapongeze Puma Energy Tanzania, kwa wakati huu tuliokuwepo wa Mwezi wa Ramadhan, ambao Mwenyezi Mungu anatuagiza tufanye mengi ya kheri yanayomridhisha yeye,” amesema.

Amesisitiza kwamba kampuni hiyo inajali kazi zake kwa sababu ni chombo cha kibiashara na moja ya utaratibu wa kibiashara ni kuvuta soko ambalo halipatikani bila kutanguliza mapenzi ya dhati kwa shughuli zake.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Puma Energy Tanzania, Dk. Suleiman Majige, alisema wanaendelea kuiombea kampuni hiyo kwani ni mali ya Watanzania, iendelee kufanya kaza vizuri.

Pia, Dk. Majige ameishukuru Menejimenti ya Puma Energy Tanzania kwa kazi walioifanya ya kuwaunganisha na kuwakaribisha katika hafla hiyo, pamoja na kuwatakia mfungo mwema wa Ramadhani inayoendelea.

Aidha amewataka kuwa karibu na Mungu katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani ambao ni muhimu kumuomba Mungu kila wakati aendelee kuleta neema na mapenzi mema.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Puma Energy Tanzania Fatma Abdallah(wa kwanza kulia), Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Puma Energy Tanzania Dk . Suleiman Majige ( wa pili kulia) wakibadilishana mawazo na Kaimu Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam Walid Alhad Kawambwa( kushoto) wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa na Kampuni hiyo jijini Dar es Salaam

Kaimu Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam Walid Alhad Kawambwa akitoa salamu kwa wageni waalikwa mbalimbali waliohudhuria hafla ya futari iliyoandaliwa na Kampuni ya Puma Energy Tanzania .Hafla hiyo imefanyika jijini Dar es Salaam wakiongozwa
Kaimu Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam Walid Alhad Kawambwa (katikati) waliokaa mbele akiwa katika picha ya pamoja na maofisa mbalimbali wa Kampuni ya Puma Energy Tanzania wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji Fatma Abdallah ( wa kwanza kushoto) na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Puma Energy Tanzania Dk Suleiman Majige ( wa pili kulia)


Share:

WAZIRI JAFO ATAKA UHIFADHI WA MAZINGIRA MLIMA KILIMANJARO KUENDELEZWA

waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na mazingira Dkt.Seleman Jafo akizungumza Leo Bungeni Jijini Dodoma.
Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na mazingira Dkt.Selemani Jafo akizungúmza na Naibu waziriwa wa Wizara hiyo Hamza Hamis Chillo leo April 6,2023 Bungeni Dodoma.


Na Dotto Kwilasa, DODOMA.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt.Selemani Jafo ametoa wito kwa Watanzania kuhifadhi na kuutunza Mlima Kilimanjaro ili uendelee kuinufaisha nchi.


Ametoa wito huo leo Aprili 04, 2023 Bungeni Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Same Mashariki Mhe. Anne Kilango Malecela aliyetaka kufahamu mkakati wa Serikali katika kukabiliana na matukio ya uchomaji moto Mlima Kiliamanjro.


Mhe. Jafo amesema kuwa Serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii ina dhamira ya dhati katika kuhakikisha matukio hayo yanakoma.


Amesema pamoja na Serikali kuunda timu ya kufanya utafiti wa matukio ya moto wananchi wana wajibu wa kuacha vitendo vya ukataji miti na uchomaji moto eneo la hifadhi ya Mlima Kilimanjaro. 


Awali akijibu swali la msingi la Mbunge wa Hai, Mhe. Saashisha Mafuwe, Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis Hamza Khamis amesema Serikali kupitia Taasisi mbalimbali za ndani ya nchi zikiwemo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Chuo Kikuu Cha Kilimo cha Sokoine, na Chuo Kikuu cha Nelson Mandela vinaendelea kufanya tafiti kuhusu suala hili. 


Hata hivyo amebainisha kuwa baadhi ya sababu zilizobainishwa kuchangia hali hiyo ni pamoja na kuongezeka kwa wastani wa joto duniani, shughuli za binadamu zisizoendelevu,ukataji wa miti na uchomaji moto misitu.


“Napenda kuchukua fursa hii kuhimiza uongozi na wananchi wa Mkoa wa Kilimanjaro kuongeza jitihada za kutunza Mazingira ya Mlima huo kwa kudhibiti uchomaji moto ovyo na kuongeza jitihada za kuhifadhi na kupanda miti,” amesema.


Katika hatua nyingine, Naibu Waziri Khamis amesema Serikali inahakikisha Mradi wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabianchi kwa Kutumia Mifumo Ikolojia Vijijini (EBARR) unaotekelezwa kwenye Wilaya ya Kaskazini A, Unguja na Mradi wa Kurejesha Ardhi iliyoharibika Kuongeza Usalama wa Chakula katika Maeneo kame nchini (LDFS) unaotekelezwa katika Wilaya ya Micheweni, Pemba inakamilika kwa wakati.


Hivyo, amesema tayari Serikali imechukua hatua za kiutendaji kwa kuwataka waratibu wa miradi kitaifa kuhakikisha miradi inakamilika kikamilifu na kwa ubora.


Aidha, naibu waziri amesema Ofisi ya Makamu wa Rais (SJMT) imeendelea kuwasilina na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais (SMZ) ili Kusimamamia utekelezaji wa miradi hiyo kwa upande wa Zanzibar ili Miradi hii ikamilike kwa wakati. 


Mhe. Khamis ameyasema hayo wakati akijibu swali la Mbunge wa Chaani Mhe. Hamad Juma Usonge aliyeuliza

 Serikali ina mpango gani wa kukamilisha Miradi ya muda mrefu ya mazingira na mabadiliko ya tabianchi inayotekelezwa Zanzibar.

Share:

MCHANGO WA SEKTA YA MADINI KWENYE PATO LA TAIFA WAZIDI KUONGEZEKA





Na Mwandishi wetu,TABORA.

IMEELEZWA kuwa katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Sita mchango wa Sekta ya Madini umeendelea kukua  hadi kufikia asilimia tisa.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wachimbaji wadogo  wanaojishughulisha na shughuli za uchimbaji wa madini ya dhahabu Wilayani  Nzega mkoani Tabora kupitia mahojiano maalum wamesema kuwa mafanikio hayo yametokana na usimamizi mzuri wa Serikali kupitia Tume ya Madini  wa Sekta ya Madini hali iliyopelekea  kuongezeka kwa uzalishaji wa madini unaofanywa na wachimbaji wadogo kwa kutumia  teknolojia za kisasa.

Akizungumza kwa niaba ya wachimbaji wadogo wa eneo hilo, Peter Mashiri, kutoka Kikundi cha  Msilale kilichopo katika eneo hilo  amesema kuwa kuongezeka kwa mapato yatokanayo na Sekta ya Madini kumetokana na matumizi ya teknolojia za kisasa na jitihada za Serikali za kuhakikisha makundi yote yanashiriki katika sekta hiyo.

Akizungumzia manufaa ya kikundi hicho kwa jamii inayouzunguka mgodi wake Mashiri amesema kuwa kikundi cha Msilale kimesaidia kutoa ajira kwa vijana wanaozunguka mgodi ambapo hadi sasa watu zaidi ya 48 wameajiriwa.

“Tunaipongeza Serikali kwa namna inavyowajali wachimbaji wadogo kwa kutoa leseni  kwa makundi hayo ambayo imesaidia kuongeza wigo wa ajira kwa wananchi na kuongeza pato la mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla, tunaiomba Serikali iendelee kuwagawia maeneo ambayo bado yanamilikiwa na wachimbaji wakubwa bila kuendelezwa.

Kwa upande wa Katibu wa kikundi hicho, Magreth Emmanuel amewataka wanawake kujitokeza kwa wingi kushiriki katika Sekta ya Madini kwa kuwa Serikali imeweka mazingira wezeshi.

Ameongeza kuwa uwepo wa Sekta ya Madini umefungua fursa na hamasa kwa wanawake wengi ambao kwa sasa wameanza kujihusisha na shughuli za uchimbaji, uchenjuaji, na biashara ya madini sambamba na kutoa huduma kwenye migodi ya madini na kujipatia fedha kwa ajili ya kujikimu na kuhudumia familia zao.

Naye Msimamizi wa Mazingira wa kikundi hicho amesitiza kuwa mgodi huo umeendelea kuboresha mazingira yake kwa kuweka mitambo ya kisasa ambayo inawasaidia kuingia na kutoka ndani ya migodi, tofauti na awali ambapo walikuwa wanatumia kamba kushuka chini jambo ambalo lilikuwa ni hatari kwa usalama wao.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger