Tuesday, 4 April 2023

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE APRILI 4, 2023





















Share:

Monday, 3 April 2023

ALIYESHINDA TSH MIL 54 KASINO YA MTANDAONI ATOA SIRI



Mchezo uupendao kuna Aviator, Poker, Titan Roulette na mingine mingi. Kujisajili bonyeza hapa https://a.meridianbet.co.tz/c/GLd6O8

 

 

Safari moja huanzisha nyingine ni usemi ambao unafanya kazi haswa kwa majokeri ambao huishi kwa kutegemea ubashiri wa Soka unaopewa odds kubwa, au Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet yenye Sloti nyingi pendwa na rahisi kushinda kama vile Aviator, Poker na Titan Roulette.

 

Moja ya mtu ambaye atakua ni shahidi kwenye hili ni Mwarabu mkazi wa Dar Es Salaam ambaye Meridianbet wamemtanganza kuwa mshindi mkubwa wa Tsh 54,700,000/= (Milioni Hamsini na Nne na Laki Saba) ambapo alicheza dau dogo la Elfu Hamsini tu (50,000/=) kupitia kasino ya mtandaoni hii ni bahati iliyoje.

 

Gwiji huyu ambaye majina yake kamili yamehifadhiwa alicheza sloti ya 100 Burning Hot inayopatikana kwenye kasino ya mtandaoni ya Meridianbet, sloti hii inalipa sana kwani ushindi ni rahisi kuupata kwa dau dogo tu la kuanzia Tsh 100/=

 

Alipoulizwa kwa njia ya simu kuhusu ushindi huo alijibu “Najisikia furaha sana mwanzoi nilikua nikicheza nakula pesa ndogo ndogo hatimaye leo nimepiga mkwanja huu wa Mamilioni. Kasino ya mtandaoni ya Meridianbet haijawahi niangusha hata siku moja ndiyo maana nacheza kila siku”

 

“Naipenda sloti ya 100 Burning Hot kwa sababu inanipa sloti nyingi za kucheza na zote ni rahisi” Mshindi wa Milioni 54

 

Sloti ya 100 Burning Hot ni miongoni mwa michezo pendwa ya kasino inayotoa mkwanja muda wowote, lakini pia sloti nyingine rahisi kushinda ni Aviator, Poker na Titan Roulette yote unaipata kwenye kasino ya mtandaoni ya Meridianbet kupitia www.meridianbet.co.tz

 

 

Je Unahitaji kufahamu Sloti hii Inakuaje?

 

100 Burning Hot ni sloti rahisi sana kuicheza ina mistari 5 ya ushindi huku kukiwa na mingine 100 ya ziada, sloti hii inakuja na machaguo mengi ya ushindi kama vile namba 7, alama ya dola, na alama ya ushindi mkubwa kabisa ya “Wild’ hiyo inakupa bonasi ya kushinda mara nyingi. Cheza sasa kwa dau dogo la kuanzia Tsh 100/=  kubwa Zaidi Sloti hii inakupatia mizunguko 100 ya bure.



Share:

Video : YALEO KALI - FAGILIA YA ANITHA

 

Share:

LEMBELI ASHIRIKI SHEREHE YA MWANZILISHI WA TAASISI YA JANE GOODALL NCHINI MAREKANI

Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kahama-James Lembeli ( maarufu Ng'wana Maria) katika picha kwenye hafla ya kumpongeza Mwanzilishi wa Taasisi ya Jane Goodall Dk. Jane Goodall na Balozi wa heshima wa Umoja wa Mataifa wa Amani kutimiza miaka 89 iliyofanyika katika Hotel ya Litz Carlton, New York - Marekani iliyohudhuriwa na wanasayansi,wahifadhi,Wana mazingira na viongozi mbalimbali duniani.


Dk. Jane Goodall alifika Tanzania, wakati huo Tanganyika mwaka 1960 na kuanzia utafiti wa wanyama aina ya Sokwe katika hifadhi ya Gombe utafiti ambao unaendelea mpaka leo.

Katika ghafla hiyo,watu mbalimbali walimtakia Jane Goodall afya njema na maisha marefu.
Pia walimpa zawadi ikiwa pamoja pesa,ambazo zote zitapelekwa Gombe, Kigoma kuendeleza kazi za utafiti na uhifadhi katika Hifadhi hiyo nchini Tanzania.
Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kahama, James Lembeli akizingumza na Dk. Jane Goodall.
Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kahama, James Lembeli katika picha ya pamoja na baadhi ya waalikwa.
Share:

Video Mpya Kaliii!! LIMBU LUCHAGULA - MUNGU WANGU

 

Share:

Sunday, 2 April 2023

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU APRILI 3,2023





























Share:

JAMES LEMBELI AENDA NEW YORK, MAREKANI

 
Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kahama-James Lembeli ( maarufu Ng'wana Maria) amendoka nchini mwishoni mwa wiki iliyopita kwenda New York nchini Marekani.


Akiwa mjini,humo Lembeli alitarajiwa kuhudhuria sherehe maalum ya kutimiza miaka 89, muasisi wa taasisi ya Jane Goodall ambayo chimbuko lake ni  Hifadhi ya Taifa ya Gombe,Kigoma ambako alifika mwaka 1960 kuanzia kufanya utafiti wa mnyama aina ya sokwe.


Utafiti huo wa Sokwe,umedumu Kwa zaidi ya miaka 60 na unaendeshwa na taasisi hiyo ya Jane Goodall ambao hivi Sasa unaendeshwa na watanzania.


Jane Goodall,raia wa Uingereza pia ni Balozi wa heshima wa Umoja wa Mataifa wa Amani.


Sherehe hiyo,ilihudhuriwa na wanasayansi na viongozi mashuhuri mbalimbali wa nchini Marekani.


Aidha Lembeli atahudhuria kikao cha Bodi ya Wakurungenzi ya Jane Goodall-Marekani ambako yeye ni mjumbe pekee toka Afrika.


Taasisi ya Jane Goodall ambayo Ina ofisi katika nchi zaidi 100 ulimwenguni inajihusisha hasa na utafiti na uhifadhi wa Sokwe barani Afrika na jamii ya wanyama aina ya nyani.


Nchini Tanzania,mbali ya utafiti katika Hifadhi ya Gombe,taasisi hiyo inaendesha miradi mbalimbali ya uhifadhi wa mazingira hasa misitu ya asili sambamba na miradi ya afya na maendeleo ya jamii ktk mikoa ya Kigoma na Katavi.


Lembeli,ambaye ni Mwenyekiti wa taasisi hiyo hapa nchini aliwahi pia kuwa Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Ardhi,Maliasili na Mazingira ambaye ripoti yake juu ya madudu yaliyojitokeza katika utekelezaji wa operesheni tokomeza ilipelekea mawaziri watatu kutumbuliwa na mmoja kujiuzulu.


Lembeli anatarajiwa kurudi nchini tarehe 13.4. 2023.

Share:

YANGA SC YAICHAPA TP MAZEMBE 1-0 UGENINI


**********************

NA EMMANUEL MBATILO

KLABU ya Yanga imefanikiwa kuondoka na ushindi kwenye mechi yake ya mwisho hatua ya makundi Kombe la Shirikisho barani Afrika baada ya kufanikiwa kuichapa TP Mazembe kwa bao 1-0 , mchezo uliopigwa nchini DR Congo.

Yanga SC imefanikiwa kupata bao kipindi cha pili likifungwa na kiungo mshambuliaji Farid Musa ambaye aliingia akitokea benchi akipihwa na Mudathir Yahya mabadiliko ambayoyalizaa matunda.

Yanga sasa inaenda hatua ya Robo Fainali akiwa anaongoza kundi akijikusanyia alama 13 katika michezo sita hatua ya makundi.

Yanga iliwakosa baadhi ya wachezaji kikosi cha kwanza ambapo walimkosa Djidji Diara ambaye ni goli kipa namba moja, Khalid Aucho, Aziz Ki na Morrison .
Share:

BARRICK YADHAMINI KONGAMANO LA WANAFUNZI WA VYUO VIKUU LILILOFANYIKA CHUO KIKUU CHA DODOMA


Afisa Raslimali Mwandamizi wa Barrick Bulyanhulu,Renatus Malawa, akiongea na Wanafunzi katika kongamano la kuwajengea uwezo lililoandaliwa na taasisi ya AISEC Tanzania na kufanyika katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).
Afisa Raslimali Mwandamizi wa Barrick Bulyanhulu,Renatus Malawa, akiongea na Wanafunzi katika kongamano la kuwajengea uwezo lililoandaliwa na taasisi ya AISEC Tanzania na kufanyika katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).
Mkurugenzi wa elimu ya juu kutoka Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia,Dk.Kenedy Hosea ambaye alikuwa ni mgeni rasmi akiongea wakati wa kongamano hilo.
Wanafunzi wa UDOM na baadhi ya Maofisa wa Barrick wakifuatilia matukio wakati wa kongamano hilo.
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Dodoma, afande Maganga pia alipata fursa ya kuongea na Wanafunzi.
Picha ya pamoja na mgeni rasmi, viongozi wa AISEC Tanzania, Jeshi la Polisi na wafanyakazi wa Barrick.
 ****
Kampuni ya Barrick Gold Corporation, imedhamini na kushiriki katika kongamano la wanafunzi wa vyuo vikuu lililoandaliwa na taasisi ya kuchipua na kuendeleza vipaji vya uongozi kwa vijana (AISEC Tanzania) lililofanyika katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na kuwashirikisha wanafunzi,wahadhiri na wadau mbalimbali.

Kupitia kongamano hili ambalo hufanyika kila mwaka, wanafunzi huweza kufahamu jinsi taasisi mbalimbali nchini zinavyoendesha shughuli zake lengo kubwa ikiwa ni kuwajengea uwezo wa kujua vipaji walivyonavyo, kujifunza jinsi ya kujiamini na kukabiliana na ushindani katika soko la ajira, kujitambua uwezo wao ni jinsi gani wanaweza kushiriki kutoa mchango wa kuendeleza taifa pindi wamalizapo masomo yao.


Maofisa Waandamizi wa Barrick pia walishiriki katika maonesho na kongamano hilo ambapo walipata fursa kuzungumza na wanafunzi kuhusiana na kukabiliana na changamoto mbalimbali ikiwemo ajira,kuendeleza vipaji vyao pia wanafunzi walipata fursa kuelewa jinsi kampuni ya kimataifa ya Barrick, inavyoendesha shuguli zake kwa kutoa kipaumbele kusaidia jamii sambamba na mpango wake wa kuibua na ukuzaji wa vipaji kwa vijana wa kitanzania na wafanyakazi wake.
Share:

BENKI YA CRDB YAWAPA SOMO WANAFUNZI WA CHUO KIKUU DODOMA


Kaimu Mkuu wa Kitengo cha mafunzo na uendelezaji wa wafanyakazi benki ya CRDB Edith Muyombela akizungumza na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) alipoelezea huduma zinazotolewa na benki hiyo lililofanyika Aprili 01,2023 katika ukumbi wa CIVE Auditorium chuoni hapo Jijini Dodoma
Benki ya CRDB kwa imeshiriki katika Kongamano la kuwajengea uwezo wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na kukabiliana na changamoto mbalimbali za kiuongozi pindi wamalizapo masomo, lililofanyika Aprili 01,2023 katika ukumbi wa CIVE Auditorium chuoni hapo.



Benki ya CRDB imekuwa ni moja ya benki kiongozi nchini katika kuhakikisha inashiriki kuelimisha makundi ya vijana wa vyuo mbalimbali nchini kupitia program mbalimbali yakiwemo Mafunzo kwa vitendo ‘Field attachmets’, Mafunzo kazini 'Ínternship’ na Programu maalumu ya Maendeleo ya wahitimu ‘Apprenticeship’ ambayo yalianzishwa mwaka 2020 kwa kuwachukua wahitimu 29 kutoka nchini Tanzania na 2 kutoka nchini Burundi.


Pia Benki ya CRDB kila mwaka huchukua kati ya wanafunzi 300 hadi 500 na kuwaunganisha katika vitengo mbalimbali vilivyopo ndani ya benki hiyo na kwenye matawi yake yaliyosambaa kote nchini ilikuweza kuwapatia mafunzo ya vitendo.


Kongamano hilo lililohudhuriwa na Mkurungenzi wa Elimu ya Juu wa Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia ,Dk Kenedy Hosea, Benki ya CRDB iliwakilishwa na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha mafunzo na uendelezaji wa wafanyakazi, Edith Muyombela.


Wanafunzi wa vyuo nchini wamekuwa wakifurahia huduma mbalimbali za kibenki kutoka Benki ya CRDB ikiwa ni pamoja na upatikananji wa mikopo maarufu kama Boom Advance umekuwa ni mkombozi kwa wanafunzi wengi wanaotumia benki ya CRDB kwakujipatia mikopo rahisi hivyo kurahisisha kukabiliana na changamoto mbalimbali za kifedha.


Pia Benki ya CRDB imewatengenezea akaunti maalumu ya wanafunzi wa vyuo ambayo gharama zake za kufungua akaunti hiyo ni shilingi za Kitanzania Elfu Tano tu (5,000). wastani wa mikopo 20,000 inatolewa kila Mwezi kwa wanafunzi mbalimbali nchini, na wastani wa akaunti 50,000 zinafunguliwa kila mwaka na wanafunzi wanaojiunga na vyuo vikuu nchini.


Kwa miaka kadhaa, Benki ya CRDB imekuwa Mshirika wa Umoja wa Taasisi za Elimu ya juu za wanafunzi nchini Tanzania ‘AIESEC’.

Mkurungenzi wa elimu ya Juu Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia ,Dk Kenedy Hosea (kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Wafanayakazi wa Benki ya CRDB kuhusu huduma zinazotolewa na benki hiyo alipotembelea banda la CRDB Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) lililofanyika Aprili 01,2023 katika ukumbi wa CIVE Auditorium chuoni hapo Jijini Dodoma Kaimu Mkuu wa Kitengo cha mafunzo na uendelezaji wa wafanyakazi benki ya CRDB .Edith Muyombela akiwa kwenye Banda la CRDB ambapo walikua wakielezea kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) huduma zinazotolewa na benki hiyolililofanyika Aprili 01,2023 katika ukumbi wa CIVE Auditorium chuoni hapo Jijini Dodoma
Share:

KAMATI YA BUNGE YAIPONGEZA REA NA KUHAMASISHA WANANCHI KUCHANGAMKIA FURSA ZA UMEME VIJIJINI


Veronica Simba na Issa Sabuni - REA

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) imesema imeridhishwa na utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini mkoani Singida na imewashauri wananchi wanaoishi vijijini waliofikiwa na huduma ya umeme, kuitumia nishati hiyo kwa matumizi yenye tija hususani katika shughuli za kujiongezea kipato na kukuza uchumi.

Akizungumza na wananchi wa kijiji cha Irisya wilayani Ikungi, Mkoa wa Singida, wakati wa ziara ya Kamati hiyo kukagua maendeleo ya utekelezaji wa Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili (R3R2), Aprili Mosi 2023, Makamu Mwenyekiti wa PIC, Augustino Vuma amesema lengo la Serikali kupeleka umeme vijijini ni kuwarahisishia wananchi kutekeleza kwa ufanisi shughuli mbalimbali za kiuchumi ili wajiletee maendeleo hivyo kutoitumia nishati hiyo ni kurudisha nyuma juhudi hizo za Serikali.

“Nitoe rai kwa wananchi kuitumia vizuri fursa hii ya uwepo wa umeme kwa kubuni shughuli mbalimbali za kiuchumi ili sasa ile dhana ya Serikali kuleta umeme hapa iweze kuonekana kwa maana ya kuchochea ukuaji wa uchumi na faida nyinginezo,” amesisitiza.

Aidha, Makamu Mwenyekiti amewaagiza Watendaji wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kuendelea kuwasimamia kwa ukaribu wakandarasi wanaotekeleza miradi ya umeme vijijini ili kuhakikisha wanafanya kazi kwa kuheshimu mikataba yao na kufanikisha azma ya Serikali kuwafikishia umeme wananchi wote waishio vijijini waweze kujikwamua kiuchumi.

Katika hatua nyingine, Makamu Mwenyekiti wa PIC ameeleza kuwa Kamati imeridhishwa na utekelezaji wa Mradi wa R3R2 huku akibainisha kuwa tayari manufaa yake yamekwishaanza kuonekana.




“Leo tumekuwa hapa katika Shule ya Sekodari Irisya na tumeshuhudia kwa macho yetu kwamba wanafunzi wameshaanza kunufaika kwani umeme umeingia kwenye Maabara na kufika katika madarasa hivyo kuwawezesha kujisomea hata nyakati za usiku.”

Akifafanua zaidi, amesema Kamati imeshuhudia uwepo wa umeme katika Maabara ya Fizikia na nyinginezo na kuwawezesha wanafunzi kusoma kwa vitendo. Amesema kuwa, kupitia uwepo wa umeme, matarajio ni kuongezeka kwa idadi ya wanafunzi wa masomo ya sayansi na kwamba ufaulu katika masomo yote pia utaongezeka kwani mazingira yameboreshwa.

Vilevile, ameongeza kwamba kuhusu manufaa kwa wananchi, umeme umeanza kuwafikia hivyo wataweza kufanya shughuli za kiuchumi ikiwemo kuanzisha viwanda vidogo vidogo.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Janet Mbene pamoja na kuunga mkono uhamasishaji wananchi kuunganisha umeme katika makazi na shughuli za kiuchumi, amesema ni faraja kwa REA kuona umeme unaendelea kuwafikia wananchi katika maeneo mbalimbali vijijini.

“Lengo letu ni lilelile, kuhakikisha kwamba kila kijiji kinapata umeme na hatimaye uwasaidie wananchi kiuchumi, kijamii na hata kimaendeleo kwa maana ya elimu na vitu vingine,” amesisitiza.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti mbele ya Kamati ya PIC, Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba na Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Irisya, Ernest Edward wametoa shukrani kwa Serikali kupitia REA kwa kufikisha umeme katika kijiji hicho.

Awali, akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini mkoani Singida kwa Kamati, Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy ameeleza kuwa Serikali kupitia Wakala hiyo imetoa jumla ya shilingi bilioni 73.1 na Dola za Marekani 988,707.60 ili kuhakikisha miradi minne inayotekelezwa mkoani humo inakamilika na wananchi wanapatiwa huduma ya nishati hiyo ili kujipatia maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Aidha, ameeleza zaidi kuwa Mradi wa Umeme Vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili katika Wilaya za Ikungi na Singida unatekelezwa na Mkandarasi M/s Central Electricals International Ltd kwa gharama ya shilingi bilioni 26.3 na katika Wilaya za Iramba, Manyoni na Mkalama, unatekelezwa na M/s CRJE – CTCE Consortium kwa gharama ya shilingi bilioni 31.6




Amesema kuwa, maendeleo ya Mradi kwa wastani yamefikia asilimia 70.21 ambapo kwa Wilaya za Ikungi na Singida, Mkandarasi amefikia asilimia 77.54 na Wilaya za Iramba, Manyoni na Mkalama, Mkandarasi amefikia asilimia 62.87

Mkoa wa Singida una jumla ya vijiji 441 ambapo vijiji 287 vimekwishapatiwa umeme kupitia miradi ya umeme vijijini iliyotekelezwa awali. Vijiji 169 vilivyobaki vinaendelea kuunganishiwa umeme kupitia Wakandarasi waliotajwa.
Share:

DCEA KUANZA MSAKO KUDHIBITI BIASHARA NA MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA



********** 

KAMISHINA Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya DCEA), Aretas James Lyimo ametaja malengo yake ambayo ameingia nayo ili kuhakikisha mamlaka hiyo inadhibiti kabisa biashara na matumizi ya dawa za kulevya nchini.

Ameyasema hayo leo Aprili Mosi, 2023 mkoani Mtwara wakati wa uzinduzi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa ambapo mamlaka hiyo inashiriki kikamilifu katika mbio za mwenge huku akiweka wazi mipango yake ya kuhakikisha wanakabiliana na changamoto hiyo.

"Kwa hiyo nitoe wito kwa watumiaji wa dawa za kulevya kuacha wenyewe kutumia dawa za kulevya, lakini pia kwa wale wauzaji na wasambazaji wa dawa za kulevya kuacha kabisa hiyo biashara ya dawa za kulevya, kwani kuanzia sasa tunafanya operesheni kabambe nchi nzima, lakini tutahakikisha vijiwe vote vya wauzaji, na watumiaji wa dawa za kulevya tunavisambaratisha.

Mbio za Mwenge kitaifa kwa mwaka 2023 katika uwanja wa CCM Nangwanda Sijaona mkoani Mtwara leo Aprili Mosi, 2023 zimezinduliwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri va Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Kassim Majaliwa.

Aidha, Kamishana Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Aretas James Lyimo amesema, ushiriki wao katika mbio hizo una umuhimu mkubwa.

"Tupo hapa Mtwara katika tukio hili la uwashaji wa Mwenge, kwa sababu Mwenge unatembea nchi nzima kwa ajili ya kukemea maovu, kuhakikisha kwamba, maovu yanaondoka kwenye jamii nchini, na sisi kama Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, dawa za kulevya ni sehemu moia wapo va maovu ambayo yanakemewa na Mwenge.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger