Thursday, 9 September 2021

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI SEPTEMBA 9, 2021



















Share:

Wednesday, 8 September 2021

DC HANANG AUNGANA NA WANANCHI KUTATUA KERO YA MAJI

Mkuu wa Wilaya ya Hanang.Janeth Mayanja (kulia) akishiriki kubeba matofali na wananchi wa Kijiji cha Lambo Kata ya Masakta mkoani Manyara wakati wakichimba mifereji jana kwa ajili ya kupitisha bomba za maji zitazoelekea katika kijiji hicho na kijiji cha jirani.
Mkuu wa Wilaya ya Hanang.Janeth Mayanja (katikati) akiwa na wakina mama wakati wa kazi hiyo ya kuchimba mifereji.
Mkuu wa Wilaya ya Hanang.Janeth Mayanja akichimba mifereji.
Mkuu wa Wilaya ya Hanang.Janeth Mayanja (katikati) akiwa na wakina baba wakati wa kazi hiyo ya kuchimba mifereji.
Kazi ikiendelea.
Mkuu wa Wilaya ya Hanang.Janeth Mayanja akichimba mifereji.


Na Mwandishi Wetu, Hanang.


 CHANGAMOTO  ya ukosefu wa maji iliyodumu kwa muda mrefu katika Kijiji cha Lambo Kata ya Masakta wilayani Hanang mkoani Manyara ina kwenda kukoma baada ya mkuu wa wilaya hiyo, Janeth Mayanja kuungana na wananchi wa kijiji hicho kuchimba mifereji kwa ajili ya kupitisha bomba za maji zitazoelekea katika kijiji hicho na kijiji cha jirani.

Wanakijiji wa eneo hilo wamemshukuru Mkuu wa Wilaya ya Hanang.Janeth Mayanja kwa kuamua kuungana nao kwa ajili ya kuhakikisha.maji yanapatikana ndani ya muda mfupi katika kijiji hicho kwani tangu kuanzishwa kwa kijiji hicho huduma ya maji ilikua inapatikana kwa tabu hadi kufikia wanakijiji kushindwa kupata huduma ya maji kwa ukaribu.

Akizungumza katika zoezi hilo Mayanja alisema kuwa  usambazaji wa maji katika eneo hilo lipo chini ya Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira ( RUWASA) Wilaya ya Hanang ambapo alimtaka mkandarasi ahakikishe ndani ya miezi minne kijiji hicho kiwe kimepata maji.

Aidha Meneja wa RUWASA Wilaya ya Hanang Mhandisi Herbert Kijazi amewahakikishia wana kijiji wa eneo hilo pamoja na mkuu wilaya kuwa Ruwasa itahakikisha wanafanya kazi usiku na mchana na ndani ya miezi minne maji yatakuwa yanapatikana katika eneo hilo.

Share:

MTANDAO WA MISITU AFRIKA 'AFF' WAFANYA MKUTANO WA KUBADILISHANA UZOEFU


Kaimu Mkuu wa chuo SUA Profesa Raphael Chibunda

Mtandao wa Misitu Afrika – AFF umefanya mkutano wa kubadilishana uzoefu kuhusu utekelezaji wa mkataba Paris uliotaka kuimarishwa kwa usimamizi wa misitu ili kupunguza madhara yaletwayo na mabadiliko ya tabia nchi.

Mkutano huo uliofanyika kwa njia ya mtandao na kushirikisha nchi nne za Afrika umefunguliwa rasmi na Kaimu mkuu wa chuo kikuu cha Kilimo cha SOKOINE – SUA Profesa Raphael Chibunda katika hotuba yake iliyosomwa na Profesa Esron Karimuribo wa SUA.

Katika hotuba yake Profesa Chibunda amepongeza waandaaji wa mkutano huo kwa kuweza kutumia teknolojia ambayo imewezesha washiriki zaidi ya 200 kukutana na kujadili kuhusu masuala ya misitu na biasahara ya utomvu (gum) ambayo ni zao majawapo la misitu.

Profesa Chibunda amesema majadiliano ya kubadilisha uzoefu na maarifa kuhusu masuala ya misitu ni njia sahaihi ya kuobersha hatua za kukabiliana na adhari za mabadiliko ya tabianchi na hatimaye na kuboresha Maisha ya jamii zinazomiliki misitu hiyo.

Kundi la washiriki wa Tanzania lilikutana katika kituo cha kitaifa cha kufuatilia hewa ukaa – NCMC katika katika chuo kikuu cha Kilimo cha SOKOINE – SUA mkoani MOROGORO.

Nchi zilizoungana na kundi la Tanzania ni Gambia, Botswana na Kenya.

Share:

ICT Officer Grade II (Security Management) at e-Government Authority (eGa)

POST: ICT OFFICER GRADE II (SECURITY MANAGEMENT) – 2 POST   POST CATEGORY(S): IT AND TELECOMS EMPLOYER: e-Government Authority (eGa) APPLICATION TIMELINE: 2021-09-07 2021-09-20 JOB SUMMARY N/A DUTIES AND RESPONSIBILITIES   Plan, design, develop and implement ICT security policies, procedures, standards, and guidelines; Integration of ICT security into day-to-day ICT operational activities and provision of periodic security […]

This post ICT Officer Grade II (Security Management) at e-Government Authority (eGa) has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Underground Mechanical Trainers at North Mara Gold Mine Limited

North Mara Gold Mine Limited is seeking to recruit Underground Mechanical Trainers to join Underground Maintenance team. The successful candidate for this position will carry out assigned mechanical tasks within the guidelines of Company Standard Operating Procedures and Best Practice as well as other assigned tasks within the range of competencies. The position will report […]

This post Underground Mechanical Trainers at North Mara Gold Mine Limited has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

ICT Officer Grade II (Business Analyst) at eGa

POST ICT OFFICER GRADE II (BUSINESS ANALYST) – 1 POST   POST CATEGORY(S) IT AND TELECOMS EMPLOYER e-Government Authority (eGa) APPLICATION TIMELINE: 2021-09-07 2021-09-20 JOB SUMMARY N/A DUTIES AND RESPONSIBILITIES   To analyze and perform the Institutional business modelling as well as their association with technology solutions; To analyze and document business processes and translate […]

This post ICT Officer Grade II (Business Analyst) at eGa has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

ICT Officer II (Application Programmer/Web Developer) at eGa

POST ICT OFFICER II (APPLICATION PROGRAMMER/WEB DEVELOPER) – 1 POST   POST CATEGORY(S) IT AND TELECOMS EMPLOYER e-Government Authority (eGa) APPLICATION TIMELINE: 2021-09-07 2021-09-20 JOB SUMMARY N/A DUTIES AND RESPONSIBILITIES To accomplish Software Application Development Full Lifecycle by:-   Designing, coding, and debugging software applications based on various deployment platforms (e.g. web, mobile, desktop etc.), […]

This post ICT Officer II (Application Programmer/Web Developer) at eGa has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

SERIKALI YAWASHUKURU WABIA WA MAENDELEO KUSAIDIA USAMBAZAJI UMEME VIJIJINI



Veronica Simba – Shinyanga

Serikali imewashukuru Wabia mbalimbali wa Maendeleo kutokana na mchango wanaoendelea kutoa katika kuwezesha utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini.

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Mhandisi Amos Maganga alitoa shukrani hizo Septemba 7 mwaka huu wakati akizungumza na Waandishi wa Habari mkoani Shinyanga.

Akishiriki katika ziara ya Bodi ya Nishati Vijijini (REB) kukagua maendeleo ya utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini, hususan mradi wa ujazilizi mkoani humo, Mhandisi Maganga alibainisha kuwa Wabia hao wa Maendeleo wana mchango mkubwa katika kufanikisha mradi husika.

Aliwataja Wabia hao kuwa ni Serikali za Norway, Sweden pamoja na Umoja wa Ulaya ambao kwa umoja wao wamefadhili shilingi bilioni 147 kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi wa Ujazilizi Fungu la Pili A katika Mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Tabora, Singida, Dodoma, Kilimanjaro na Tanga.

“Wamekuwa nasi bega kwa bega kuhakikisha kwamba azma ya Serikali kuwapatia wananchi huduma mbalimbali ikiwemo nishati ya umeme inafikiwa hivyo kupunguza hali ya umaskini katika maeneo husika,” alisema.

Mhandisi Maganga aliongeza kuwa, wajibu wa REA ni kuhakikisha msaada uliotolewa unatumika kama ilivyokusudiwa na Wabia hao wa Maendeleo ili malengo yaliyodhamiriwa yaweze kufikiwa.

Aidha, alitumia jukwaa hilo kuwakaribisha kutembelea miradi waliyoifadhili katika maeneo mbalimbali nchini ili wajionee maendeleo ya utekelezaji wake.

Bodi inaendelea na ziara katika Mikoa mbalimbali nchini kwa lengo la kukagua maendeleo ya miradi inayotekelezwa kupitia REA.










Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Mhandisi Amos Maganga (kushoto), akizungumza na Mwenyekiti wa Kitongoji cha Ilambabusungu, Kijiji cha Bubiki, Wilaya ya Kishapu, Mkoani Shinyanga, Mwandu Fimbo (kulia) wakati wa ziara ya Bodi ya Nishati Vijijini kukagua maendeleo ya utekelezaji wa miradi ya umeme, Septemba 7 mwaka huu. Wa pili – kulia ni Mjumbe wa Bodi, Oswald Urassa.











Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Wakili Julius Kalolo (kulia) na Ujumbe wake, wakijadiliana jambo wakati wa ziara ya Bodi hiyo mkoani Shinyanga, Septemba 7, 2021 kukagua maendeleo ya utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini.












Wataalam kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wakifuatilia majadiliano ya viongozi (hawapo pichani), wakati wa ziara ya Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Mkoani Shinyanga Septemba 7 mwaka huu, kukagua maendeleo ya utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini. Kutoka kushoto ni Mhandisi Deogratius Nagu, Mhandisi Dunstan Kalugira na Mhandisi Ernest Makale.





Share:

MKANDARASI LIPA MADENI YA WANANCHI - BODI

Veronica Simba – Shinyanga

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) imemtaka Mkandarasi anayetekeleza Mradi wa Ujazilizi mkoani Shinyanga, Kampuni ya Sagemcom kuwalipa wananchi wanaomdai kutokana na kazi mbalimbali walizofanya ikiwemo kuchimba mashimo ya kusimika nguzo za umeme katika Kijiji cha Bubiki, Wilayani Kishapu, Mkoa wa Shinyanga.

Agizo hilo lilitolewa Septemba 7 mwaka huu na Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Wakili Julius Kalolo wakati wa ziara ya Bodi iliyolenga kukagua maendeleo ya utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini.

Maelekezo hayo ya Mwenyekiti yalitokana na madai ya Mwenyekiti wa Kitongoji cha Ilambabusungu, Mwandu Fimbo kuwa Mkandarasi husika hajawalipa wananchi wa eneo hilo waliofanya kazi mbalimbali katika Mradi unaoendelea kutekelezwa mkoani humo.

Akifafanua, Fimbo alieleza kuwa pamoja na kuchimba mashimo ya kusimika nguzo za umeme, wananchi wanadai madeni mengine kufuatia huduma mbalimbali walizompatia Mkandarasi ikiwemo kodi ya nyumba aliyopanga.

Kufuatia hali hiyo, Wakili Kalolo alimwagiza Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Mhandisi Amos Maganga kusimamia suala hilo ili kuhakikisha wananchi wanapata haki yao mapema iwezekanavyo.

Akizungumzia suala hilo, Mhandisi Maganga alitoa muda wa wiki moja kwa Mkandarasi kuwa amelipa madeni yote ya wananchi hao vinginevyo Wakala utachukua jukumu la kumlazimisha kulipa kwa kukata malipo yake ya kazi ya usambazaji umeme na kuwapatia wananchi wanaomdai.

“Tumechukua namba ya Mwenyekiti wa Kitongoji na tutafuatilia. Endapo Mkandarasi atakaidi agizo hili, dhamana hiyo tutaichukua sisi wenyewe kwa kumkata malipo yake ili tuwalipe wananchi,” alisisitiza.

Kwa upande wake, Mkandarasi husika aliahidi kufanyia kazi maelekezo aliyopewa ambapo REA TANZANIA ilishuhudia akiwasiliana na Mwenyekiti wa Kitongoji kupata orodha ya majina ya wanaoidai Kampuni ili aanze utekelezaji.

Katika ziara hiyo, Mwenyekiti wa Bodi alifuatana na Mjumbe Oswald Urassa, Mkurugenzi Maganga pamoja na viongozi na wataalam mbalimbali kutoka REA na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).




Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Wakili Julius Kalolo (kulia), akisalimiana na Mwenyekiti wa Kitongoji cha Ilambabusungu, Kijiji cha Bubiki wilayani Kishapu, Mkoa wa Shinyanga, Mwandu Fimbo wakati Bodi ilipowasili katika eneo hilo ikiwa katika ziara kukagua maendeleo ya utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini, Septemba 7 mwaka huu. Wa pili - kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Amos Maganga.







Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Wakili Julius Kalolo na Ujumbe wake wakiangalia Vibali vya kufanya kazi nchini vya Kampuni ya Ukandarasi Sagemcom kutoka Ufaransa inayotekeleza miradi ya umeme vijijini katika Mikoa ya Mwanza na Shinyanga. Bodi ilikuwa katika ziara ya kazi mkoani Shinyanga, Septemba 7, 2021.







Miundombinu ya umeme katika Kitongoji cha Ilambabusungu, Kijiji cha Bubiki wilayani Kishapu, Mkoa wa Shinyanga. Taswira hii ilichukuliwa wakati wa ziara ya Bodi ya Nishati Vijijini kukagua maendeleo ya utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini, Septemba 7, 2021.







Mwenyekiti wa Kitongoji cha Ilambabusungu, Kijiji cha Bubiki wilayani Kishapu, Mkoa wa Shinyanga, Mwandu Fimbo (kushoto) akimwongoza Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Wakili Julius Kalolo kukagua miundombinu ya umeme katika eneo hilo. Bodi ilikuwa katika ziara ya kazi, Septemba 7, 2021.







Mwenyekiti wa Kitongoji cha Ilambabusungu, Kijiji cha Bubiki wilayani Kishapu, Mkoa wa Shinyanga, Mwandu Fimbo (wa pili-kulia), akizungumza na Ugeni wake ambao ni Ujumbe wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB) ukiongozwa na Mwenyekiti Wakili Julius Kalolo (kulia) aliyefuatana na Mjumbe Oswald Urassa (kofia nyeusi-katikati) na Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Amos Maganga (kushoto). Bodi ilikuwa katika ziara ya kazi, Septemba 7, 2021.







Mwenyekiti wa Kitongoji cha Ilambabusungu, Kijiji cha Bubiki wilayani Kishapu, Mkoa wa Shinyanga, Mwandu Fimbo (wa pili-kushoto), akizungumza na Ugeni wake ambao ni Ujumbe wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB) uliokuwa katika ziara ya kazi, Septemba 7, 2021 kukagua maendeleo ya utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini.




Share:

Rais Mwinyi avunja bodi ya ushauri ya kudhibiti vileo Zanzibar.

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Hussein Mwinyi ameivunja bodi ya ushauri ya kudhibiti vileo Zanzibar.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na kusainiwa na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi, Zena Said imesema hatua hiyo ni kuanzia  Jumanne Septemba 7, 2021.



Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Septemba 8



Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO SEPTEMBA 8,2021














Share:

SIRI 5 AMBAZO MWANAMKE HAPASWI KUMWAMBIA MUME WAKE HATA KAMA ANAMPENDA KIASI GANI


Ndoa ni muhimu, na huwa muhimu kwasababu ni kitu kinachowaunganisha mume na mke na kuanzisha familia, na huleta baraka nyingi kama vile watoto na nyinginezo nyingi.

Hatahivyo siku hizi, ndoa nyingi huishia kuvunjika kutokana na sababu moja au nyingine, hususan kutokana na ugomvi ndani baina ya wanandoa.

Bila shaka haipaswi kuwa siri baina ya wanandoa, lakini kuna baadhi ya vitu ambavyo mwanamke hapaswi kumwambia mume wake, hata kama wanapendana kiasi gani.

Katika jamii nyingi za kiafrika kuna msemo usemao, maskio yasiposikia , moyo hauwezi kukasirika. Na kama tunataka amani ndani ya familia lazima kutakuwa na matukio magumu , na mwanamke anapaswa kusaidia katika utatuzi wa mambo hayo.

Yafuatayo ni mambo 5 ambayo mwanamke hapaswi kumwambia mume wake:

1. Idadi ya wanaume uliojamiana nao kabla ya kuoana na mume wako

Hupaswi kumfahamisja mpenzi wako wa kiume au mume wako ni wanaume wangapi ulikutana nao kimwi kabla ya kuishi naye.

Swababu ni kwamba unaweza kufikiri hautamkose mume wako siku sijazo. Na kama idadi ya wanaume uliyomwambia ni wengi anaweza kufikiri wewe ni kahaba au mzinzi.

Kwahiyo, iwapo atakuuliza ni wanaume wangapi ulishawahi kukutana nao kimwili, unaweza kucheka tu na umwambie :''Ebu wacha tunachane na hayo, lakini swala la ni wangapi halihusiani na safari ya mapenzi. Hebu njoo ".

2. Kusema siri za mpenzi wako wa kiume au mume wako wakati mmoja


Ukiulizwa maswali kumuhusu mwanaume, mujibu machache

Usiseme mambo ambayo yanaweza kumfanya mume au mpenzi wako ahisi kwamba sio bora vya kutosha, au ajihisi kuwa mtu mbaya

Usizungumzie kuhusu -ungependa kuwa na uhusiano na mwanaume tajiri kiasi fulani, mwenye uwezo wa kingono kiasi gani, na ni kwa vipi ungependa ampende mke wake, kwa mume mpya.


3. Usimwambie mume wako kwamba unampenda sana rafiki yako au shemeji yako

Sote tunafahamu kuwa inawezekana kwa rafiki au shemeji kutaka kukuoa.

Lakini, ni hatari kumwambia mume wako kuhusu wazo hili . Sababu ni kwamba mume wako anaweza kuanza kuwa na mashaka kuhusu tabia zake na vitendo vyako kumuhusu mwanaume huyo, jambo linaloweza kusambaratisha ndoa yako.

4. Usijaribu kumwambia kuwa unamchukia mama yake au familia yake

Hata mama mkwe awei mtu nmbaya kiasi gani, usimwambie mume wako kuwa unamchukia. Au unaichukia familia yake. Hata kama umekasirika kiasi gani, usijaribu kusema mambo mabaya kuwahusu, au kumuona mume wako sawa na familia yake.

Kama hauepatani na yeyote katika familia ya mume wako, elezea kwa utulivu, ukiwa na matumaini kuwa ataelewa ni kwanini haupatani nao.

Mume wako pia ataweza kukusaidia kutatua tatizo, na pia itazuwia matatizo mengine ambayo yanaweza kusababisha matatizo makubwa zaidi.

5. Usimtishe mume wako kuwa utakuja kutalikiana naye

Siku utakapomwambia mume wako kuwa utaachana naye wakati mnazozana, jua ndio mwanzo wa malumbano ndani ya ndoa.

Ndoa itaanza kukumbwa na misukosuko, wasi wasi na kutoamianiana.

Kutishia talaka katika ndoa inamaanisha kuwa hauna moyo wa imani katika ndoa, na haupatii umuhimu. Isipokuwa kama katika ndoa kuna unyanyasaji au uhalifu mwingine mbaya, ni vyema kujaribu kushirikiana kutatua changamoto zozote mlizonazo.

CHANZO - BBC SWAHILI

Share:

WAKAMATWA KWA KUTOROSHA WATOTO NA KUWAUZA SHILINGI ELFU 25


Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya,Ulrich Matei

Jeshi la Polisi mkoani Mbeya, linawashikilia watu wawili kwa tuhuma za kuwatorosha watoto 11 wenye umri wa kati ya miaka 10 hadi 14, kutoka maeneo mbalimbali ya mkoa wa Mbeya na kwenda kuwauza kwa wafugaji.

Taarifa hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi wa mkoa huo Ulrich Matei, na kusema kuwa watuhumiwa hao wamekuwa wakiwauza watoto hao kwa gharama ya kati ya shilingi 25,000 hadi 30,000, kwa wafugaji wilayani Mbarali ili wachunge mifugo yao.

Mbali na hili Jeshi la Polisi pia linawashikilia walimu wawili kwa tuhuma za kutaka kuharibu mitihani ya mwisho ya wanafunzi wanaomaliza elimu ya msingi.

CHANZO - EATV
Share:

Kinyasini Secondary School

About Kinyasini Secondary School Kinyasini Secondary School is a secondary school in Tanzania with The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) registration number S2402 – Known as Shule ya Sekondari Kinyasini Secondary School Kinyasini Secondary School Facilities The Kinyasini Secondary School, features a number of facilities designed to meet specific requirements. The School Facilities includes: […]

This post Kinyasini Secondary School has been posted by Udahiliportal Editor 03

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger