Thursday, 2 September 2021

HESLB Yaongeza Siku 15 Kwa Waombaji Mikopo Elimu Ya Juu.


Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imeongeza muda wa uombaji mikopo kwa siku 15 zaidi kuanzia Septemba 1 hadi 15 mwaka huu ili kuwapa fursa kwa waombaji mikopo ambao wamejisajili katika mfumo kukamilisha maombi yao.

Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Abdul-Razaq Badru ametangaza uamuzi huo  (Jumatano, Septemba 1, 2021) jijini Dar es salaam na kufafanua kuwa uamuzi huo umetokana na maombi na ushauri walioupokea kutoka kwa wadau.

Idadi ya waombaji
“Tulianza kupokea maombi kwa njia ya mtandao Julai 9, mwaka huu na hadi jana ambayo ilikua siku ya mwisho ya kuomba tulikua na waombaji 91,445 waliowasilisha maombi, na kati ya hayo, maombi 12,252 yalikua hayajakamilika na wateja wetu wameomba muda wa kukamilisha,” amesema Badru.

Mkurugenzi Mtendaji alikua akiongea katika mkutano na wanahabari uliofanyika katika ofisi za HESLB jijini Dar es salaam ambao pia ulihudhuriwa na wawakilishi kutoka Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) na Shirika la Posta Tanzania (TPC) ambao pia wanawahudumia waombaji mkopo.

Hatua inayofuata
Kwa mujibu wa Badru, hatua inayofuata ni uhakiki wa nyaraka na taarifa zilizowasilisha na waombaji 79,193 ambao maombi yao yamekamilika kama yanavyoonekana kwenye mfumo.

“Kuna makundi mawili, wale 12,252 ambao maombi hayana viambatisho na hivyo hayajakamilika … na kuna maombi 79,193 yenye nyaraka, sasa tunaanza kuhakiki usahihi wake na baadae tutaangalia kama wamepata udahili na wale wenye sifa ndiyo watapangiwa mkopo,” amesema Badru.

Fursa ya kuomba mkopo vijana waliopo JKT
Kuhusu wanafunzi wahitaji wanaoendelea na mafunzo katika Kambi za Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Badru amesema vijana hao waliopo katika kambi 19 nchini watapata fursa ya kuomba mkopo kwa siku 10 kuanzia Septemba 20 hadi 30 mwaka huu.

“Tumekuwa tukiwasiliana na Makao Makuu ya JKT, na tumekwenda na kukutana na vijana hao katika kambi zote na tuliwaahidi kuwa watapata fursa … ambayo ni kuanzia Septemba 20 hadi 30 mwaka huu, hivyo wasiwe na wasiwasi,” amesema Badru.

RITA na TPC kuendelea kuwahudumia waombaji
Katika mkutano huo, Badru pia ameeleza kuwa HESLB imekubaliana na RITA na TPC kuendelea kuwahudumia waombaji mkopo katika kipindi chote kilichoongezwa.

“Wenzetu wa RITA wanaendelea kuhakiki vyeti vya vifo na kuzaliwa wanavyopokea na wamekuwa wakifanya hivyo hata kabla ya kufunguliwa kwa dirisha la maombi … na Posta (TPC) wameahidi kuendelea kupokea nyaraka kupitia huduma ya EMS katika muda ulioongezwa, tunawashukuru sana” amesema Badru.

Bajeti ya mikopo kwa 2021/2022

Katika mwaka wa masomo 2021/2022, Serikali imetenga kiasi cha TZS 570 Bilioni kwa ajili ya kugharamia mikopo ya wanafunzi 160,000 wa taasisi za elimu ya juu. Kati ya hao, wanafunzi 62,000 wanatarajiwa kuwa ni wa mwaka wa kwanza na wanafunzi 98,000 wanaoendelea na masomo. Bajeti kwa mwaka 2020/2021 ilikua TZS 464 bilioni na zimewanufaisha jumla ya wanafunzi 149,398.

Imetolewa na:
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu


Share:

RAIS SAMIA : TOZO ZA MIAMALA YA SIMU ZITAENDELEA KUWEPO KAMA KAWAIDA


Rais Samia Suluhu Hassan

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa tozo za miamala ya simu zitaendelea kuwepo kama kawaida ili kupata fedha za kuendeleza miradi ya maendeleo na kujiepusha kuwa kwenye mikono ya wafadhili.

Kauli hiyo ameitoa leo Septemba 2, 2021, wakati akiwasalimia wananchi wa Tegeta akiwa njiani kuelekea Bagamoyo kwa ajili ya kurekodi vipande vya filamu vitakavyotangaza utalii wa Tanzania kimataifa, filamu ambayo itazinduliwa nchini Marekani.

"Nataka niwaambie kwamba tozo zitaendelea kuwepo na sitaki kuwaficha, kwa sababu tozo zile miezi miwili tuliyoanza nayo tumekusanya zaidi ya shilingi bilioni 60 na zimepelekwa kujenga vituo vya afya 220 hivyo tunajenga wenyewe ili wafadhili wanaokuja na masharti wasituingilie mambo yetu," amesema Rais Samia.

CHANZO - EATV
Share:

Assistant Lecturer (Insurance and Risk Management) at Institute of Accountancy Arusha IAA

POST ASSISTANT LECTURER (INSURANCE AND RISK MANAGEMENT) – 1 POST   POST CATEGORY(S) ENVIRONMENTAL SCIENCES AND GEOGRAPHY TAXATION AND SOCIAL PROTECTION EMPLOYER Institute of Accountancy Arusha (IAA) APPLICATION TIMELINE: 2021-08-31 2021-09-13 JOB SUMMARY N/A DUTIES AND RESPONSIBILITIES i. To teach up to NTA Level 8 (Bachelor Degree); ii. To prepare learning resources for tutorial exercises; […]

This post Assistant Lecturer (Insurance and Risk Management) at Institute of Accountancy Arusha IAA has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Lecturer (Banking) at Institute of Accountancy Arusha (IAA)

POST LECTURER (BANKING) – 1 POST   POST CATEGORY(S) BANKING, ECONOMICS AND FINANCIAL SERVICES EMPLOYER Institute of Accountancy Arusha (IAA) APPLICATION TIMELINE: 2021-08-31 2021-09-13 JOB SUMMARY N/A DUTIES AND RESPONSIBILITIES i. To teach up to NTA Level 8 for Master’s Degree holders and up to NTA Level 9 for PhD holders; ii. To guide and […]

This post Lecturer (Banking) at Institute of Accountancy Arusha (IAA) has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Relationship Manager, Local & Mid Corporates at Standard Chartered Bank

About Standard Chartered    We are a leading international bank focused on helping people and companies prosper across Asia, Africa and the Middle East. To us, good performance is about much more than turning a profit.  It’s about showing how you embody our valued behaviours – do the right thing, better together and never settle […]

This post Relationship Manager, Local & Mid Corporates at Standard Chartered Bank has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

MEJIMENTI MPYA YAANZA KAZI MAKAO MAKUU YA PAPU


Katibu Mkuu Mtendaji wa Umoja wa Posta Afrika, (PAPU) anayemaliza muda wake Ndugu Younouss Djibrine ( kushoto) akikabidhi Ofisi kwa Katibu Mkuu Mtendaji Mpya Ndugu Sifundo Chief Moyo kwenye Ofisi za PAPU Jijini Arusha, leo Tarehe 1 Septemba 2021. Wanaoshuhudia ni Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe Dkt. Faustine Ndugulile (wa tatu kutoka kulia), Waziri wa TEHAMA na Huduma za Posta Zimbabwe na Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania( TCRA) Dkt. Emmanuel Manasseh (wa kwanza kushoto). PICHA NA: TCRA


Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Dkt Faustine Ndugulile (Mb) akitoa hotuba kwa washiriki wa Mkutano wa Umoja wa Posta Afrika (PAPU) uliofanyika jijini Arusha mapema juma hili. Washiriki wa Mkutano huo wameshuhudia makabidhiano ya ofisi baina ya Katibu Mkuu Mtendaji wa Umoja huo aliemaliza muda wake Younouss Djibrine Katibu Mkuu Mtendaji mpya Ndugu Sifundo Chief Moyo. PICHA NA: TCRA


Waziri wa TEHAMA na Huduma za Posta nchini Zimbabwe Mhe. Supa Mandiwanzira akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika ofisi za Makao Makuu ya Umoja wa Posta Afrika (PAPU) jijini Arusha, Tanzania kushuhudia makabidhiano ya ofisi ya Katibu Mtendaji Mkuu wa umoja huo ; anaeshuhudia ni Katibu Mkuu Mtendaji wa umoja huo aliemaliza muda wake Ndugu Younouss Djibrine. PICHA NA: TCRA


Kutoka kulia ni Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wa Tanzania Mhe. Dkt Faustine Ndugulile (Mb) akiwa sambamba na Waziri wa TEHAMA na Huduma za Posta nchini Zimbabwe Mhe. Supa Mandiwanzira wakifuatilia shughuli za mkutano wa makabidhiano ya Ofisi ya Katibu Mkuu Mtendaji wa Umoja wa Posta Afrika (PAPU) jijini Arusha mapema wiki hii. Aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa umoja huo Ndugu Younouss Djibrine (Cameron) amekabidhi ofisi kwa Ndugu Sifundo Chief Moyo(Zimbabwe). PICHA NA: TCRA


Washiriki wa Mkutano wa Makabidhiano ya ofisi ya Katibu Mkuu Mtendaji wa Umoja wa Posta Afrika (PAPU) wakiongozwa na Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wa Tanzania Mhe. Dkt Faustine Ndugulile. Katika Mkutano huo uliofanyika makao makuu ya PAPU jijini Arusha, Tanzania; Ndugu Younouss Djibrine (Cameron) (wa pili mstari wa pili kulia) amekabidhi ofisi kwa Ndugu Sifundo Chief Moyo(Zimbabwe) wa kwanza mstari wa pili kulia). PICHA NA: TCRA

****************************


Menejimenti mpya ya chombo cha sekta ya posta barani Afrika, Umoja wa Posta Afrika (PAPU) imeanza kazi leo, tarehe 1 Septemba 2021 kufuatia sherehe iliyofana iliyofanyika kwenye jengo la uwekezai PAPU, makao makuu Arusha mjini mkoani Arusha.

Katibu Mkuu WA PAPU aliyemaliza muhula wake, Bwana Younouss Djibrine; alikabidhi uongozi kwa Katibu Mkuu mpya wa Umoja huo, Bwana Sifundo Chief Moyo kwenye shughuli ambayo mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Dr. Faustin Ndugulile (Mb.).

Kma sehemu ya mabadiliko ya uongozi katika chombo hicho cha bara la Afrika, Katibu Mkuu Msaidizi aliyemaliza muhula wake kwenye Umoja huo, Bwana Kolawole Aduloju pia alikabidhi ofisi kwa Bi. Jessica Hope Uwera Sengooba.

PAPU inaendele kutekeleza majumumu yake muhimu ya kujenga ENEO MOJA LA SHUGHULI ZA POSTA wakati wote na katika mazingira yote, kama mchango wake kwenye kufikia azma ya pamoja na ya muda mrefu ya watu wa Afrika ya kuleta maendeleo shirikishi na endelevu kwa jamii.

Mabadiliko ya menejimenti ya Umoja wa Posta Afrika (PAPU) yameainishwa kwenye utaratibu rasmi wa kukabidhiana madaraka kwa mpangilio baada ya kumalizika kwa muhula wa uongozi wenye mafanikio makubwa.

Menejimenti mpya inaingia ofisini kipindi cha janga la UVIKO-19 ambalo limevuruga shughuli za mifumo ya shughuli za kibiashara na ambalo linahofiwa kuleta athari za muda mrefu kwenye maendeleo ya kawaida ya biashara na kwa hivyo kuibua changamoto kwa umma kwa ujumla kutathmini upya njia bora za kukabili athari hizo.

Mikakati ya kutathmini upya na kukabili hali hii inahitajika ili kuweza kugeuza changamoto zilizojitoketa kuwa fursa kwa ama kubadilimifumo ya utoaji huduma au kubadili bidhaa na huduma zinazotolewa ili kuendelea kuwa na wateja na hivyo kuendeleza biashara. Hii itachangia katika kulinda sekta ya posta na kuimarisha uwezo wake wa kugundua mapema na kukabiliana na majanga mengine kama haya mbeleni.
Share:

JINSI DAKTARI WANGU WA KIENYEJI ALIVYOKOMESHA MARADHI HAYA



Niite Anita, mimi ni mama ambaye nimekuwa mgonjwa kwa muda mrefu mno na tumetumia kiasi kukubwa cha hela kwa matibabu yangu bila mafanikio. 

Madaktari bandia wamekula hela zetu wakidanganya kuwa wana uwezo wa kunitibu lakini wote ni matapeli tu.

 Nilizaliwa nikiwa mzima kabisa na hata utotoni mwanangu sikuwahi kuwa mgonjwa kiholela holela lakini nilipofika kidato cha tatu, ndipo hali yangu ya kiafya ilianza kudhoofika. 

Miguu ikaanza kuvimba kidogokidogo. Sikuwahi kudhani ugonjwa huo ungelikuwa mkubwa hadi pale ukalipoathiri miguu yangu yote.

 Wazazi wangu walianza juhudi za kuhakikisha kuwa nimepata matibabu maalum kwa kunipeleka hospitali mbalimbali kote nchini lakini hali ilibakia hivyo hivyo.

 Kwa kweli babangu alifika mahali akaamua kuuza kipande kidogo cha ardhi ili kunilipia matibabu lakini la kushangaza hela hizo zote kima cha shilingi elfu mia sita zilipotelea kwa madaktari bandia.

 Ilikuwa mwaka jana ndipo shangazi wangu mmoja alitutembela na aliponiangalia na kuona hali niliokuwemo, alibubujikwa na machozi kisha akatuibia siri ya Doctor Kiwanga. 

Kiwanga ni daktari aliye na uwezo wa kuyatibu maradhi mbalimbali akitumia miti za kiasili. Shangazi alitusihi atupeleke kwa Kiwanga Doctors na la kushangaza tulipofika tu hivi Daktari alishika mguu wangu wa kwanza akauangalia kisha akainua mguu nwingine na kupaka mafuta fulani baridi. 

Alipomaliza shughuli alituambia turudi nyumbani. Leo hii ninapoongea nanyi mimi ni mzima wa afya. 

Ahsante Kiwanga Doctors; laiti ningelijua mapema hatungekuwa tumearibu pesa zetu kwa madaktari wengine bandia.

 Vile vile, kama unajuwa una matatizo na mambo ya mapenzi kwa nyumba yako tafadhali nakusihi upate matibabu wa Kiwanga. Kiwanga Doctors ni shujaa wa mambo yote. 

Ninatoa wito kwa wenye shida za magonjwa, mapenzi, ndoa, biashara, kikazi na afya kuharakisha kuwatembelea madaktari was Kiwanga. Tovuti au Website yao ni: www.kiwangadoctors.com; Simu: +254 769404965 au wasiliana kwa barua pepe yaani Email: kiwangadoctors@gmail.com.

Sio lazima usafiri hadi ofisi zao. Ongea nao kwa njia ya simu na utasaidika kwa haraka kama vile watu wengine wanavyopata usaidizi.
Share:

Credit Analyst, CCIB at Standard Chartered Bank

About Standard Chartered    We are a leading international bank focused on helping people and companies prosper across Asia, Africa and the Middle East. To us, good performance is about much more than turning a profit.  It’s about showing how you embody our valued behaviours – do the right thing, better together and never settle […]

This post Credit Analyst, CCIB at Standard Chartered Bank has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

MKENDA ATOA WITO KWA USHIRIKA KUONGEZA KASI YA VIWANDA


Waziri wa Kilimo Mhe. Prof. Aldolph Mkenda,akizungumza wakati akizindua rasmi Kongamano la Pili la Kimataifa la Ushirika lililofanyika katika Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU) Septemba 01, 2021 Mkoani Kilimanjaro 


Mrajis na Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Dkt. Benson Ndiege akitoa salamu za Ushirika wakati wa uzinduzi Kongamano la Pili la Kimataifa la Ushirika Septemba 01, 2021 Mkoani Kilimanjaro 


Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika (MoCU) Prof. Alfred Sife akieleza majukumu mbalimbali yanayofanywa na Chuo hicho katika kukuza na kuendeleza taaluma ya Ushirika wakati wa Kongamano la Pili la Kimataifa la Ushirika Septemba 01, 2021 Mkoani Kilimanjaro 


Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Ushirika Theresia Chitumbi akiongea wakati wa Kongamano la Pili la Kimataifa la Ushirika Septemba 01, 2021 Mkoani Kilimanjaro 


Mrajis wa Vyama vya Ushirika na Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Dkt. Benson Ndiege (kulia) pamoja na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (Mocu) Prof. Alfred Sife (kushoto) wakionesha mkataba wa ushirikiano baina ya Taasisi hizo (MOU), katikati mwanasheria wa Tume Bw. Shani Mayosa wakati wa Kongamano la Pili la Kimataifa la Ushirika lililozinduliwa Septemba 01, 2021 Mkoani Kilimanjaro. 

............................................................................. 

Wito umetolewa kwa Vyama vya Ushirika kuangalia namna bora ya kuendeleza viwanda vinavyochakata bidhaa zinazozalishwa na Vyama vya Ushirika kwa kuongeza thamani ya mazao mbalimbali yanayotoka na vyama hivyo ili kuweza kuendana na kasi ya soko la ushindani la ndani na nje ya nchi. 

Hayo yamesemwa na Waziri wa Kilimo Mhe. Prof. Aldolf Mkenda wakati akifungua Kongamano la Pili la Kimataifa la Ushirika katika Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU) mkoani Kilimanjaro. Kongamano hilo limefunguliwa rasmi Jumatano Septemba 01, 2021 hadi Septemba 03,2021 na kuandaliwa kwa ushirikiano wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU) na Tume ya Maendeleo ya Ushirika (TCDC). Kauli mbiu ya Kongamano ilijikita katika masuala ya Ushirika na Maendeleo ya Viwanda kwa kuzingatia maslahi ya wanachama. 

Waziri ameeleza kuwa ni dhamira ya Serikali kuona Vyama vya Ushirika vinaongeza tija kwa kuongeza viwango vya uzalishaji ili iwe ni msukumo wa kuanzisha na kuendeleza Uchumi wa Viwanda kwa kuongeza thamani ya mazao na bidhaa zinazotokana na Vyama, ingawa bado Sekta ya Ushirika inakabiliwa na changamoto zinazopaswa kufanyiwa kazi. 

“Lengo la Serikali ni kuimarisha na kuendeleza Ushirika ingawa ushirika unakabiliwa na changamoto za Kisera, masuala ya Sheria, hitaji la wataalamu katika utendaji wa Vyama vya Ushirika,” alisema Prof. Mkenda 

Mrajis wa Vyama vya Ushirika na Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Dkt. Benson Ndiege katika Kongamano hilo amesema Tume kwa mujibu wa Sheria Na.6 ya mwaka 2013 itaendelea kutekeleza wajibu wa kuvisimamia na kuhamasisha Vyama vya Ushirika 

“Ni wakati sasa Vyama vya Ushirika vifikirie kuwa na viwanda vya kuchakata mazao mbalimbali na kuyaongezea thamani ili kuzalisha bidhaa zinazotokana na maziwa, asali, alizeti na mengine mengi,” alieleza Mrajis 

Mrajis ameongeza kuwa hivi sasa Sekta ya Ushirika ina viwanda mbalimbali 452 ambavyo vinafanya shughuli mbalimbali za uchakataji. Akibainisha juhudi zinazoendelea katika kuendeleza na kuimarisha viwanda vya Ushirika ni pamoja na uanzishaji wa Kiwanda cha vifungashio katika Chama cha Ushirika SONAMCU mkoani Ruvuma, kiwanda cha ubanguaji Korosho TANECU mkoani Mtwara, Kiwanda ambacho kimeanza kazi ya kuchambua Pamba mkoani Shinyanga kinachomilikiwa na KACU pamoja na vingine. 

Akichangia mada wakati wa Kongamano hilo Mtaalamu wa Uchumi Prof. Honest Ngowi ameshauri Vyama vya Ushirika vingi kwa sasa vinazalisha bidhaa na mazao yakiwa ghafi jambo ambalo bado linafanya tija na uchumi wa Vyama kuwa duni. 

Aliongeza kuwa uuzaji na usafirishaji wa mazao yaliyoongezwa thamani nje ya nchi unachangia kuongeza pato la Taifa, fursa za ajira, na uchumi wa mtu mmoja mmoja ambao hatimaye utachangia kupunguza umaskini. Akibainisha kuwa hadi kufikia 2020 Viwanda vinachangia ajira kwa kiasi cha asilimia 40. Jambo ambalo likiimarishwa litainua uchumi hasa wa Sekta binafsi na hatimaye Taifa kwa ujumla. 

Aidha, Mtaalamu huyo wa uchumi ameeleza kuwa wigo mpana wa vyama vya Ushirika kushiriki katika uchumi na maendeleo ya viwanda kutokana na dhana ya ushirika kuwa yenye uwezo wa kushirikisha Nyanja mbalimbali za uchumi ikiwemo vyama vya ushirika wa kilimo, uvuvi na maeneo mengine. 

Pamoja na mambo mengine uzinduzi wa Kongamano hilo ulienda sambamba kwa utiaji saini wa mikataba ya Ushirikiano baina ya Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi na Tume ya Maendeleo ya Ushirika, MoCU na Bodi ya Kahawa, MoCU na Shirikisho la Vyama vya Akiba na Mikopo (SCCULT). 

Mada zinazotarajiwa kujadiliwa katika Kongamano hilo ni pamoja na masuala yanayohusu namna bora ya kuonguza uweledi katika utendaji wa vyama, Hifadhi ya Jamii kwa wanaushirika, mabadiliko na maboresho ya Sheria za Ushirika, Ushirikishwaji wa Vijana katika Vyama vya Ushirika zote zikilenga kujadili changamoto ili kupata mapendekezo ya suluhu za kuboresha Sekta ya Ushirika. 

Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo



Share:

Masukila Secondary School

About Masukila Secondary School Masukila Secondary School is a secondary school in Tanzania with The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) registration number S2062 – Known as Shule ya Sekondari Masukila Secondary School Masukila Secondary School Facilities The Masukila Secondary School, features a number of facilities designed to meet specific requirements. The School Facilities includes: […]

This post Masukila Secondary School has been posted by Udahiliportal Editor 03

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Kajunjumele Secondary School

About Kajunjumele Secondary School Kajunjumele Secondary School is a secondary school in Tanzania with The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) registration number S2061 – Known as Shule ya Sekondari Kajunjumele Secondary School Kajunjumele Secondary School Facilities The Kajunjumele Secondary School, features a number of facilities designed to meet specific requirements. The School Facilities includes: […]

This post Kajunjumele Secondary School has been posted by Udahiliportal Editor 03

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Maghare Secondary School

About Maghare Secondary School Maghare Secondary School is a secondary school in Tanzania with The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) registration number S2060 – Known as Shule ya Sekondari Maghare Secondary School Maghare Secondary School Facilities The Maghare Secondary School, features a number of facilities designed to meet specific requirements. The School Facilities includes: […]

This post Maghare Secondary School has been posted by Udahiliportal Editor 03

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Wednesday, 1 September 2021

Ngulilo Secondary School

About Ngulilo Secondary School Ngulilo Secondary School is a secondary school in Tanzania with The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) registration number S2059 – Known as Shule ya Sekondari Ngulilo Secondary School Ngulilo Secondary School Facilities The Ngulilo Secondary School, features a number of facilities designed to meet specific requirements. The School Facilities includes: […]

This post Ngulilo Secondary School has been posted by Udahiliportal Editor 03

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Thomas Nyimbo Secondary School

About Thomas Nyimbo Secondary School Thomas Nyimbo Secondary School is a secondary school in Tanzania with The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) registration number S2058 – Known as Shule ya Sekondari Thomas Nyimbo Secondary School Thomas Nyimbo Secondary School Facilities The Thomas Nyimbo Secondary School, features a number of facilities designed to meet specific […]

This post Thomas Nyimbo Secondary School has been posted by Udahiliportal Editor 03

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Maria Nyerere Secondary School

About Maria Nyerere Secondary School Maria Nyerere Secondary School is a secondary school in Tanzania with The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) registration number S2057 – Known as Shule ya Sekondari Maria Nyerere Secondary School Maria Nyerere Secondary School Facilities The Maria Nyerere Secondary School, features a number of facilities designed to meet specific […]

This post Maria Nyerere Secondary School has been posted by Udahiliportal Editor 03

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Luhololo Secondary School

About Luhololo Secondary School Luhololo Secondary School is a secondary school in Tanzania with The National Examinations Council of Tanzania (NECTA) registration number S2056 – Known as Shule ya Sekondari Luhololo Secondary School Luhololo Secondary School Facilities The Luhololo Secondary School, features a number of facilities designed to meet specific requirements. The School Facilities includes: […]

This post Luhololo Secondary School has been posted by Udahiliportal Editor 03

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger