Thursday, 27 May 2021

Consultant at PSI

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

ADVERTISEMENT FOR MANAGEMENT INFORMATION SYSTEM CONSULTANCY SERVICES With over 45years of experience, working in over 60 countries, Population Service International (PSI) is the world’s leading non-profit social marketing organization. PSI is reimagining health care, by putting the consumer at the center, and wherever possible – bringing care to the front door. We are working to […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Zuma akanusha mashtaka ya ufisadi dhidi yake


Rais wa zamani wa Afrika Kusini Jacob Zuma amekana mashtaka yote 18 ya ufisadi anayokabiliwa nayo katika mahakama ya Pietermaritzburg nchini humo.

Jacob Zuma alisema anapinga makosa yote 18 ya ulaghai, ufisadi, ulaghai, ukwepaji wa kodi na utakatishaji fedha haramu.

Mashtaka hayo yanahusiana na matukio ya zaidi ya miongo miwili - katika siku za mwanzo za demokrasia ya Afrika Kusini - pamoja na mpango mkubwa wa silaha ..

Zuma na washirika wake wanasisitiza kuwa kesi hiyo ni ya kisiasa.Umati wa watu umekusanyika nje ya ukumbi wa mahakama huko Pietermaritzburg kuashiria kuwa Zuma bado ana umaarufu miongoni mwa wafuasi wake.



Share:

Watu Watano wafikishwa mahakama ya Kisutu kwa kukutwa na meno ya tembo


Watu watano wakazi wa Mkoa wa Katavi na Rukwa wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka mawili likiwemo la kukutwa na vipande vinne vya meno ya tembo vyenye thamani ya Sh34.6 milioni.

Washtakiwa hao waliosomewa mashtaka yao na wakili wa Serikali mwandamizi, Wankyo Saimon mbele ya Hakimu Mkazi mwandamizi, Kassian Matembele ni Craft Kileo, Godfrey Kashuli, Richard Kafwa, Moses Zakaria na Benjamin Lushina.

Kabla ya kusomewa mashtaka yao, Matembele aliwaeleza kuwa hawatakiwi kujibu chochote kwa sababu mahakama ya Kisutu haina mamlaka ya kusikiliza kesi ya uhujumu uchumi.

Akiwasomea mashtaka yao, Simon amedai katika shtaka la kwanza linalomkabili Kileo na Kashuli inadaiwa Mei 5, 2021 wakiwa eneo la Ukonga Wilaya ya Ilala walikutwa na vipande vinne vya meno ya tembo ambavyo ni mali ya Serikali bila kuwa na kibali cha mkurugenzi wa wanyamapori.

Katika shtaka la pili linalowakabili washtakiwa wote inadaiwa kati ya Aprili Mosi, 2021 na Mei 5, 2021 wakiwa eneo la Katavi na Dar es Salaam walisafirisha vipande vinne vya meno hayo bila kibali cha mkurugenzi huyo.

Baada ya kusomewa mashtaka yanayowakabili, Matembele aliwaeleza kuwa mahakama hiyo haiwezi kuwapa dhamana kwa sababu sheria inaeleza kuwa thamani ya mali ikizidi Sh10 milioni, dhamana inatolewa na mahakama kuu, kwamba kama wanataka dhamana wakaombe katika mahakama hiyo.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Juni 8, 2021 na washtakiwa wamerudishwa rumande.




Share:

Raia 29 wa Burundi kortini wakidaiwa kuingia Nchini Tanzania bila kibali


Raia 29 wa Burundi wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu tuhuma za kuingia nchini Tanzania bila kuwa na kibali.

Baadhi ya washtakiwa  hao ni Kasimu Kesi, Elias Shadra, Hilary Lozo, Richard Dismas, Ntahondereye Reverie, Nataka Yosam, Meraki Noah, Robert Lazaro, Samson Erick, Kazimana Aimable, John Ayoub na wengine 18.

Washtakiwa hao wamesomewa mashtaka yao janaJumatano Mei 26, 2021 na wakili kutoka Idara ya Uhamiaji, Godfrey Ngwijo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi.

Ngwijo alidai Mei 25, 2021 katika eneo la Kariakoo, washtakiwa hao walikamatwa baada ya kudaiwa kuingia  nchini kinyume cha sheria.

Washtakiwa baada ya kusomewa shtaka linalowakabili, Hakimu Shaidi aliwauliza kama tuhuma zinazowakabili zina ukweli wowote.

Washtakiwa 16 kati ya 29 walikiri makosa huku wenzao 13 wakikana.
 
Wakili wa Serikali, Godfrey, aliomba mahakama iahirishe kesi ili ipangwe tarehe nyingine kwa ajili ya kuwasomea washtakiwa maelezo ya awali.

Hakimu Shaidi alikubali kuahirisha kesi hiyo hadi Juni Mosi mwaka huu kwa ajili ya kuwasomea washtakiwa waliokiri na kuwapa muda washtakiwa waliokana, kutafakari na kufika na vibali vilivyowaruhusu kuishi nchini.

Kesi itakuja Juni Mosi mwaka huu na washtakiwa wote walipelekwa mahabusu isipokuwa watoto ambao walikabidhiwa kwa Idara ya Ustawi wa Jamii hadi tarehe ya kesi ijayo.



Share:

Senior Internal Auditor at INNOVEX

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job Overview The Senior Internal Auditor is responsible for audit planning, execution, reporting and supervision, completing internal audit activities while being consistent with the Institute of Internal Audit (IIA) Standards established policies and procedures. Responsibilities Execute engagement planning activities for a range of complex internal audits Participate in projects and ongoing departmental initiatives. Perform a range […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Credit Risk Analyst at NMB Bank

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job Purpose Identifying, measuring and communicating of the credit risk profile from a second line perspective and conducting periodic monitoring of credit related activities. Providing timely identification and reporting significant risks, losses and effectiveness of credit risk mitigation actions. Partnering with the credit department and business units where needed on credit risk matters to ensure business growth […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Cook, G-2 at IRMCT

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Temporary Job Opening (Duration until 30 September 2021) Cook, G-2       DEADLINE FOR APPLICATIONS          :            08 June 2021  OFFICE                                                :         Registry/ Detention Facility LOCATION                                           :            Arusha JOB OPENING NUMBER                     :                                     2021/IRMCT/REG/UNDF/116-GS United Nations Core Values: Integrity, Professionalism, Respect for Diversity Organizational setting and Reporting: This position […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Call for Interest Individual Contractor Legal Reviewer at IRMCT

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

United Nations International Residual  Mechanism for Criminal Tribunals   Call for Interest Individual Contractor Legal Reviewer                         DEADLINE FOR APPLICATIONS     : 1 June 2021                         DATE OF ISSUANCE                         : 26 May 2021                         OFFICE                                                    : Office of the Prosecutor                         LOCATION                                          : Arusha                         JOB […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo May 27



Share:

Wednesday, 26 May 2021

MWANAMKE AAMUA KUOLEWA NA ROHO MTAKATIFU..ASEMA AMEAGIZWA NA MUNGU



Mwanamke mmoja kutoka kaunti ya Pokot Magharibi nchini Kenya amemtema mumewe kwa madai kwamba aliagizwa na Mungu kufunga ndoa na roho mtakatifu.

Elizabeth Nalem, mama wa watoto sita kutoka Makutano Town, alisema Mungu alimtokea wakati alikuwa amelala na kumuomba aachane na mumewe. 

Tukio hilo lisilo la kawaida liliwashangaza wakazi wa Makutano ambao walikusanyika kushuhudia Bi harusi akijiandaa kuolewa na Roho Mtakatifu.

 "Leo, mimi ni mmoja wa wale ambao wamepokea neno la Mungu. Nimepitia changamoto nyingi maishani na ikanibidi nitafute uso wa Mungu," aliwaambia waandishi wa habari. 

Elzabeth aliingia kanisani akiwa amevalia gauni nyeupe kama pamba huku akifuatwa nyuma na marafiki zake wa karibu.

Ibada ilianza na mahubiri kutoka kwa mchungaji Albert Rumaita, ambaye alimuombea wakati akifungua ukurasa mpya wa maisha.

 Baada ya sherehe hiyo, Nalem alisema alikuwa ameutumikia ulimwengu kwa miaka mingi, na sasa alikuwa mwanamke aliyebadilika tayari kwa kumtumikia Mungu wake. 

Mma huyo wa watoto sita alisema mtumishi wa Mungu alimnunulia gauni, akamtafutia magari na kisha akaandaa sherehe hiyo iliyofanyika katika bustani ya Chelangaa.

 Licha ya kwamba Nalem alidai alikuwa ameshauriana na mumewe, Joshua Nalem, alisema kuwa alishtuka kuhusiana na matukio ya siku hiyo akidai kwamba hakuwa na habari kuhusu hatua ya mkewe.

Aliwaambia waandishi wa habari kuwa kila usiku mkewe alikuwa akiamka kuomba na alipomuuliza alinuna na kuhamia kwa jirani.

"Huyu ni mke wangu na nililipa mahari. Tuna watoto sita. Kifungua mimba wetu alimaliza kidato cha nne juzi," alidokeza.

 Rumaita ambaye aliendesha sherehe hiyo alisema hakuwa na lingine ila kumfanyia mwanamke huyo alivyomuomba.
 
Chanzo - Tuko News

Share:

MWANAMKE AOLEWA NA WANAUME SABA....KAWAJENGEA KILA MMOJA NYUMBA YAKE

Mwanamke huyo akiwa na wanaume zake
Mwanamke huyo akiwa na wanaume zake
**
Mwanamke mmoja ambaye ni Mganga wa Kienyeji nchini Nigeria ameweza kuolewa na wanaume saba tofauti, amesema wanaume wake hawawezi kumsaliti kwa sababu amewajengea nyumba ambazo ana uwezo wa kutembelea kimaajabu muda wowote wakitaka kumsaliti.

Mwanamke huyo amesema hayakuwa maagizo yake kuolewa na wanaume saba bali alipewa maagizo kutoka kwa wazee wake.

"Sikufanya kwa mapenzi yangu niliamriwa na wazee, ilikuwa ni agizo kutoka kwao na hapo ndipo nilipewa madaraka makubwa, Wazee waliniambia nizae watoto zaidi kutoka kwa waume zangu na nisiwe na mtoto mmoja kutoka kwa mwanamume mmoja, hiyi ndio sababu ya mimi kuoa zaidi ya waume sita"

Pia ameongeza kusema "Ilikuwa ya ajabu kwangu lakini ilibidi nitii vinginevyo ningeadhibiwa vibaya, wakati ninawaa-proach wanaume hawa walikuwa hawana chaguo zaidi ya kukubali kwa sababu ya nguvu zangu kuu"

"Nilijenga nyumba kwa kila mmoja wao na kuwatembelea wakati wowote, wakitaka kunisaliti ili kukidhi mahitaji yao, hawawezi kuthubutu kunidanganya nguvu zangu kuu zinanifikia kabla hawajafikiria".

Taarifa kama hii ya mwanamke kuolewa na mwanaume zaidi ya mmoja imetokea nchini Afrika Kusini kwa kusemekana wanawake wanaweza kuolewa na mwanaume zaidi ya mmoja.

Chanzo : Ghpage.com, Instablog9ja, Browngh.com, Minutegoal.com, Larc.org.na, Gistsbaste.com
Share:

Tanzania, Kenya Wajadili Vikwazo Visivyo Vya Kiforodha


Na Mwandishi wetu, Arusha
Timu ya wataalamu kutoka Tanzania imekutana na timu ya wataalamu kutoka Kenya Jijini Arusha kujadili njia za kuondoa vikwazo visivyo vya kibiasha baina ya Nchi hizo kwani vimekuwa vikiathiri biashara, mkutano wa leo Mei 26, 2021 ni maandalizi ya mkutano wa Mawaziri wa Biashara wa pande zote mbili utakaofanyika tarehe 29 Mei 2021.

Mkutano wa leo utafuatiwa na Mkutano wa Makatibu Wakuu utakaofanyika tarehe 28 Mei 2021 na baadaye mkutano wa Mawaziri  tarehe 29 Mei 2021. Mkutano huo utahitimishwa kwa mawaziri wa Kenya na Tanzania kufanya ziara katika mpaka wa Namanga tarehe 30 Mei, 2021 kujionea shughuli za biashara zinavyofanyika katika mpaka huo.

Ujumbe wa Tanzania katika timu wataalam umeongozwa na Mkurugenzi wa Mtangamano wa Biashara kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara Bw. Ally Gugu wakati ujumbe wa Kenya umeongozwa na Bw. Michael Mandu, Mkuu wa Biashara baina ya Nchi na Nchi, Idara ya Maendeleo ya Biashara na Ujasiriamali.  

Mkutano wa wataalamu umetoa fursa ya kujadili masuala yote yanayokwamisha biashara baina ya pande zote mbili ambapo masuala yaliyowasilishwa na Kenya kujadiliwa ni pamoja na kutotoa upendeleo kwa sigara, maziwa, bidhaa za nyama, kutoka Kenya, tozo ya kuingia kwa wafanyabiashara (business pass) kufanya kazi za muda mfupi za kitaalamu.

kwa upande wa Kenya, baadhi ya masuala ambayo Tanzania imewasilisha kujadiliwa ni kuongezwa bei ya vinywaji baridi (uplifting) kutoka Tanzania, kutoza ushuru wa forodha bidhaa za glass, kuzuia mahindi kutoka Tanzania, bei kubwa ya ushuru wa stempu katika bia, kubadili mfumo wa uingizaji mizigo mikubwa ambapo gharama za uingizaji mizigo Kenya zimeongezeka na kuathiri biashara.

Katika kutekeleza maagizo ya Wakuu wa nchi (Tanzania na Kenya) mawaziri wa seka husika kutoka watakutana na kujadili juu ya vikwazo hivyo katika mkutano wao utakaofanyika tarehe 29 Mei, 2021 jijini Arusha.

Tarehe 4 – 5 Mei, 2021 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan alifanya ziara rasmi nchini Kenya ambapo katika ziara hiyo Mhe. Samia Hassan Suluhu na Mwenyeji wake Mhe. Uhuru Kenyatta pamoja na mambo mengine, walielekeza Mawaziri wa Biashara wa pande zote wakutane na kujadili vikwazo vya kibiashara ambavyo vinaathiri biashara kwa lengo la kuviondoa.



Share:

Waziri Lukuvi Azitaka Taasisi za Serikali Kutenga bajeti ya fidia kabla ya kutwaa maeneo


Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amezitaka wizara, taasisi na mamlaka mbalimbali kuhakikisha zinatenga bajeti kwa ajili ya kulipa fidia kabla ya kutwaa ardhi kutoka kwa wananchi.

Lukuvi ameyasema hayo leo Jumatano Mei 26,2021 wakati akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara yake kwa mwaka 2021/22.

Amesema jumla ya migogoro ya ardhi 3,171 ilipokelewa kupitia programu ya Funguka kwa Waziri ambapo hadi kufikia  Mei 15,  2021 migogoro 1,144 ilishughulikiwa.

Amebainisha kuwa kati ya migogoro hiyo asilimia 39 inahusu masuala ya fidia.


Share:

Dola Za Marekani Milioni 140 Kutumika Mradi Wa Umeme Katika Mto Maragarasi


Na, Saidina Msangi na Ramadhani Kissimba, WFM, Dar es Salaam

Serikali ya Tanzania na Benki ya Maendeleo ya Afrika zimesaini mikataba miwili ya mkopo wenye thamani ya dola za Marekani milioni 140 (takriban shilingi bilioni 323.4) kwa ajili ya kufadhili Mradi wa kufua Umeme wa nguvu ya maji –  Malagarasi.  

Mikataba ya mkopo huo wenye masharti nafuu imesainiwa Jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Emmanuel Tutuba, kwa niaba ya Serikali na Bi. Nnenna Nwabufo, Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika, Kanda ya Afrika Mashariki.

Akizungumza wakati wa kusainiwa kwa Mikataba hiyo, Bw. Tutuba alisema kuwa utekelezaji wa mradi huo utaijengea TANESCO uwezo wa usambazaji wa vifaa vya kuunganisha wateja 4,250 katika Wilaya za Kigoma, Kibondo na Kasulu ikiwemo kaya 1,000 zenye kipato cha chini, zahanati 4 na shule za msingi 6.

“Mradi huu utahusisha ujenzi wa kituo kipya cha uzalishaji wa umeme wa gridi ya 49.5 MW chenye uwezo wa   kuzalisha wastani wa GWh 181 za umeme kwa mwaka ili kuboresha usambazaji wa umeme na  kupunguza utegemezi wa uzalishaji wa umeme kwa kutumia mafuta mazito ”, alisema Bw. Tutuba

Alieleza kuwa mradi huo unatarajiwa kugharimu  takribani dola za Marekani milioni 144.1 ambapo Benki ya Maendeleo ya Afrika itatoa dola za Marekani milioni 140 na Serikali ya Tanzania itachangia dola za Marekani milioni 4.14 zilizobaki.

“Kati ya fedha hizo, dola za Marekani milioni 120 zitatolewa kupitia dirisha la Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) na dola za Marekani milioni 20 kupitia Africa Growing Together Fund”, alifafanua Bw. Tutuba.

Aidha, Bw. Tutaba alisema kuwa mradi huo utajumuisha ujenzi wa njia ya usafirishaji wa umeme, upanuzi wa mtandao wa kusambaza umeme wa 132kV na ununuzi wa transfoma mpya 15 ili kuongeza uwezo wa kusambaza wa umeme kwa wananchi.

Aliongeza kuwa kusainiwa kwa mikataba hiyo kutaongeza kiwango cha fedha kilichotengwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika kwa ajili ya kufadhili miradi ya sekta ya nishati nchini Tanzania kutoka takriban dola za Marekani milioni 325.19 hadi kufikia dola za Marekani milioni 465.19 (takriban shilingi trilioni 1.07).

Aliongeza kuwa mradi huo pia ni  sehemu ya utekelezaji wa  vipaumbele vya Benki ya Benki ya Mandeleo ya Afrika vya kuongeza uwekezaji kwenye sekta ya nishati ya umeme ili kuchochea maendeleo ya viwanda na kuboresha maisha ya watu barani Afrika.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika Kanda ya Afrika Mashariki Bi. Nnenna Nwabufo alisema kuwa mradi huo ni moja ya miradi sita iliyoidhinishwa na benki hiyo katika kipindi cha miaka mitatu.

Aliitaja miradi hiyo kuwa ni mradi wa barabara za mzunguko jijini Dodoma wenye thamani ya dola za Marekani milioni 180, Mradi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Msalato (dola 271m), barabara ya Kabingo – Kasulu – Manyovu (dola 256m), barabara ya Bagamoyo – Horohoro – Lunga – Malindi (dola 150m) na Mradi wa usambazaji umeme wa Nyakanazi – Kigoma (dola 123m)

B1. Nnenna alisema kuwa uwekezaji wa Benki yake nchi Tanzania imefikia thamani ya dola za Marekani bilioni 2.33 zilizowekezwa katika sekta za miundombinu ya usafiri na usafirishaji, nishati ya umeme, maji na usafi wa mazingira, kilimo, utawala bora na fedha


Share:

Dkt. Bashiru Atema Nyongo Bungeni Kwa Mara ya Kwanza


Dr Bashiru Ally, Mbunge wa Kuteuliwa na Rais, jana tarehe 25 Mei 2021, amesimama bungeni kwa mara ya kwanza na kutumia jukwaa hilo kuzungumzia masuala mbalimbali yaliyojitokeza nchini, tangu aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano, Hayati John Magufuli, kufariki dunia.

Magufuli alifariki dunia tarehe 17 Machi 2021, kwa ugonjwa wa moyo, katika Hospitali ya Mzena mkoani Dar es Salaam, kisha mwili wake kuzikwa nyumbani kwao Chato mkoani Geita, tarehe 26 Machi mwaka huu.

Akizungumza bungeni jijini Dodoma, Dk. Bashiru amesema Tanzania ilipitia misukosuko mingi kufuatia kifo cha Magufuli, lakini kwa neema za Mungu, ilivuka salama.

“Kwa kuwa ni mara ya kwanza kuongea, nianze kwa kumshukuru Mungu kwa kutuneemesha na kuivusha nchi yetu, katika kipindi cha misukosuko baada ya kupata msiba mkubwa ambao haujawahi kutokea katika nchi yetu. Ninahakika Mungu hatatutupa,” amesema Dk. Bashiru.

Dk. Bashiru aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi siku za mwisho za uongozi wa Magufuli, amesema baada ya kifo cha kiongozi huyo kutokea, kulitokea majaribio kadhaa yaliyokuwa na lengo la kuitikisa nchi, lakini hayakufanikiwa.

“Yalikuwepo majaribio ya kupitisha maneno na kutuchonganisha, wakati mwingine kudhalilisha watu na kutunga maneno ya uongo, ili nchi itikisike. Lakini nasema wameshindwa na wamelegea,” amesema Dk. Bashiru.

Tarehe 27 Februari mwaka huu, Magufuli alimteua Dk. Bashiru kuwa Katibu Mkuu Kiongozi, baada ya aliyekuwa anashika nafasi hiyo, Balozi John Kijazi, kufariki dunia.

Hata hivyo, mwanasiasa huyo alihudumu kwenye nafasi hiyo kwa muda wa siku 32, baada ya Rais wa Awamu ya Sita, Samia Suluhu Hassan, kumteua kuwa mbunge kisha nafasi hiyo kuikabidhi kwa Balozi Hussein Katanga.

Dk. Bashiru amempongeza Rais Samia, baada ya kuapishwa kuwa Rais wa Tanzania, tarehe 19 Machi 2021, Ikulu jijini Dar es Salaam.

Aidha, Dk. Bashiru amemshukuru Rais Samia kwa kumteua kuwa mbunge, huku akimuahidi kutomuangusha katika kuitumikia nafasi hiyo.


Share:

Makatibu Wakuu Afya/ Sheria Na Katiba Kuhakikisha Mfumo Wa Haki Kwa Makosa Ya Ukatili Unaimarika


 Na Mwandishi wetu, Momba
Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii Dkt. John Jingu na Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Profesa Sifuni Mchome wamewataka watendaji wote wanaohusika na upatikanaji wa haki za makosa ya jinai kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi ili kuhakikisha haki inapatikana hasa kwa waathirika wa ukatili.

Wameyasema hayo wakati wa ziara yao ya pamoja Wilayani Momba, Mkoa wa Songwe yenye lengo la kuona namna sekta mbalimbali zinavyoshirikiana katika utoaji wa haki hususani kwa watoto waliokinzana na sheria.

Akizungumza na watendaji wa Mahakama, Magereza pamoja na Wajumbe wa Kamati ya Mpango wa Taifa wa kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA) ya Halmashauri ya Mji Tunduma kwa nyakati tofauti, Dkt. Jingu amesema watoto wanaokinzana na sheria wana haki ya kupatiwa huduma muhimu wanazostahili.

"Watoto wanatakiwa watendewe tofauti kwa sababu wao ni tofauti, tuendelee kufanya kazi, kumekuwa na changamoto sana hasa kwenye eneo la ushahidi, wanajamii wanatakiwa kuona umuhimu wa kushirikiana na vyombo vyetu ili haki iweze kutendeka ili iwe ni fundisho kwa wengine wanaofanya vitendo kama hivyo" alisema Dkt. Jingu.

Jingu pia amesema Jamii ina nafasi kubwa ya kumaliza changamoto mbalimbali hasa migogoro kwa kutumia mifumo yao hivyo kuna umuhimu wa kuimarisha mifumo ya kijamii ambayo itasaidia kupunguza misongamano katika vyombo vingine vya utoaji wa haki.

Dkt. Jingu amesema pia Wazee ni kundi muhimu katika mchakato wa utoaji haki kwenye jamii hivyo wana nafasi kubwa ya kumaliza migogoro iwapo wakitumika vizuri.

Katika hatua nyingine, Dkt. Jingu amezitaka Kamati za MTAKUWWA kuhakikisha wanafanya kazi ya kubadili fikra potofu katika jamii ikiwemo za baadhi ya wazazi kuona ni mzigo kusomesha watoto wao.

Naye Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Mchome amezitaka Mahakama kufanya jitihada za kutumia adhabu mbadala ikiwemo njia za kijamii ili kupunguza idadi ya mahabusu magerezani.

"Kwa sasa hivi takwimu zinaonesha kwamba hali ya mahabusu ni zaidi ya wafungwa ambapo wengi wao ni wale wenye makosa makubwa" alisema Prof. Mchome.

Kwa upande wake Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Momba Timothy Lyon amesema katika Wilaya hiyo kesi za watoto ni chache na wana utaratibu maalumu wa kuzishughulikia ili kulinda haki za watoto japokuwa kuna changamoto ya ukosefu wa mahabusu ya watoto na shule ya maadilisho.

Nao baadhi ya wajumbe wa Kamati ya MTAKUWWA Halmashauri ya Mji Tunduma wameishukuru Serikali hasa Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo  Regina Bieda kwa kuwawezesha kutekeleza majukumu yao hivyo jamii  imeelimika na watoto wanaweza kutoa taarifa za matukio ya ukatili kwa wakati.

Makatibu Wakuu hao wametembelea pia na kujionea ujenzi wa Jengo la Mahakama ya Mkazi Songwe pamoja na kuzungumza na wafungwa wa Gereza la Songwe linalohudumia Wilaya za Mbozi na Momba.

MWISHO


Share:

KAMPUNI YA ASFA HOSE SERVICE YATUA KWA KISHINDO KWENYE MAONESHO YA WAJASIRIAMALI NA WAWEKEZAJI KAHAMA

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger