Tuesday, 25 May 2021

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE MEI 25,2021
















Share:

Monday, 24 May 2021

Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi afanya uteuzi wa Wakurugenzi katika Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.



Share:

Majaliwa: Watafiti, Wabunifu Ongezeni Kasi Ya Tafiti


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka watafiti na wabunifu nchini kuongeza kasi ya kufanya tafiti ili nchi iende sambamba na mabadiliko yanayotokea ulimwenguni kote.

Ametoa wito huo leo Mei 24, 2021 wakati wa ufunguzi wa maadhimisho ya sita ya wiki ya utafiti na ubunifu yakiyofanyika katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jijini Dar es Salaam.

“Mabadiliko haya ya teknolojia yanatokea kwa kasi kubwa ulimwenguni yanachochewa na mwenendo wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Hivyo basi, nasi hatunabudi kujipanga vyema ili kuendana na kasi hiyo”.

Amesema kuwa ni lazima watafiti na  wabunifu katika sekta zote wachukue hatua za makusudi katika kubuni na kutumia teknolojia zinazoibuka kwa ajili ya kuleta maendeleo endelevu ya viwanda na jamii yetu.

“Wakati tukifanya hayo yote, ni muhimu pia kujitayarisha kutumia kikamilifu matokeo ya tafiti zetu kama fursa au bidhaa adimu ya biashara”

Aliongeza kuwa baada ya tafiti hizo wahakikishe matokeo ya tafiti yanapelekwa kwa umma ili uweze kufaidika na matokeo hayo kwa kupata suluhisho za changamoto mbalimbali zinazoikabili Jamii badala ya kuyafungia makabati.

Aidha, Waziri Mkuu amevitaka vyuo vikuu vyote nchini kuweka utaratibu wa kufanya utafiti na kisha kuonesha matokeo ya tafiti ili kusaidia kuimarisha uhusiano wa karibu baina ya vyuo na soko la ajira.

Kadhalika Waziri Mkuu ametoa wito kwa wenye viwanda kutoa ufadhili wa tafiti na bunifu zinazohusiana na bidhaa zinazozalishwa katika viwanda vyao.

“Tumieni vizuri wataalamu wa vyuo vyetu kwani wanaweza kuleta majibu ya changamoto mbalimbali katika uzalishaji bidhaa, masoko ya bidhaa, mahitaji ya wateja na mambo mengine mengi”

Pia, Waziri Mkuu amekitaka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kutekeleza mpango wa vitengo vya utafiti kwenye mikoa ikiwemo cha mkoa wa Lindi ambako tayari walikwisha pewa eneo.

Naye Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako amesema kuwa Serikali  itaendelea kuimarisha tafiti ili taifa liweze kunufaika na teknolojia ya kisasa na kutoa huduma kwa jamii.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU


Share:

Ntobo Mik 1....Ni Dawa Ya Asili ya Vidonda Vya Tumbo Iliyofanyiwa Utafiti Kwa Miaka Mingi


 NTOBO MIK 1
Ni Dawa ya vidonda vya tumbo iliyofanyiwa utafiti kwa miaka mingi  mwanga wa matumaini kwa wanao teseka na Vidonda vya Tumbo.

Huwezi kuzungumzia magonjwa yanayotesa Jamii ya watu wengi Duniani bila kuzungumzia Vidonda vya Tumbo.

Ugonjwa huu husababishwa na aina ya bakteria anayeitwa kwa jina la HP (Helicobacter Palory) mtu hujikuta anateseka na maumivu makali ya Tumbo bila kujuwa kuwa ni vidonda vya tumbo

DALILI ZAKE:
1.     Tumbo kuwaka moto
2.     Tumbo kujaa gesi au haja kubwa kuwa ngumu
3.     Kutokupata choo vizuri
4.     Kiungulia cha mara kwa mara
5.     Kichwa kuuma
6.     Maumivu makali ya tumbo lajuu wengi huuita chembe ya moyo
7.     Kukosa hamu ya kula
8.     Kizunguzungu
9.     Kichefu chefu

Ugonjwa huu ukishamili sana mgonjwa hujikuta anatapika damu au kujisaidia choo chenye mchanganyiko na damu.

Nini suluhisho;
BABU MADUHU MTAALAMU MWENYE UWEZO MKUBWA WA KUTIBU VIDONDA VYA TUMBO
BABU MADUHU ANAPATIKANA MAGOMENI MOROCCO HOTEL KITUO CHA KANISANI
PIGA SIMU NO. 0755 684 297/ +255 652 102 152 (WHATSAPP)

 




Share:

Rais Samia akutana na mwekezaji Alhaji Aliko Dangote, Ikulu Jijini Dar es Salaam.



Share:

TARURA yaombwa kurekebieha barabara ndani ya hifadhi kurahisisha utalii


Samirah Yusuph.
Bunda.
Katibu tawala wa  Wilaya ya Bunda Halfan Mtetela ametoa wito kwa wakala wa barabara mjini na vijijini TARURA kufanya marekebisho ya mara kwa mara barabara za ndani ya hifadhi ili kurahisisha shughuli ya utalii.

Wito huo umeutoa jana wakati wananchi wa wilaya ya Bunda walipotembelea hifadhi ya Taifa ya Serengeti  upande wa Kilawira na kusisitiza kuwa  kila mtu ahamasike kutembelea vivutio vya utalii ikiwemo mbuga  za  wanyama na hifadhi za taifa.

“Barabara zikiwa hazijatengenezwa vizuri inakuwa changamoto kupitika ni lazima wakala wa barabara vijijini na mjini (TARURA)  kuona  umuhimu wa kizitengeneza  na ikiwezekana kuongeza bajeti ili kusaidia kwenye matengenezo hayo, zitasaidia  kuvutia watalii na kufika eneo husika kwa urahisi na kwa wakati,”amesema Mtekela.

Alisema Watanzania wanapaswa kuwa wazalendo kwa kupenda  vivutio vyao na kuvitangaza ili  kufanya idadi  ya watanzania wanaotembelea hifadhi na mbinga za taifa iongezeke.

"Kila mmoja anapaswa kuwa balozi wa kutangaza vivutio kwenye mtandano kupokea watalii kutoka ndani na nje  kwani kufanya hivyo kutapelekea kuongeza pato la mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake mkurugenzi wa kampuni ya NCT twende kutalii Albart Chenza alisema katika kuhakikisha watanzania wengi wanatembelea hifadhina vivutio hivyo,kampuni yake kwa kushirikiana na uongozi wa Serengeti wameanzisha mpango wa kutembelea taasisi na wananchi ili kuhamasisha wananchi hao wanatembelea hifadhi hizo

“Hifadhi ya Serengeti imeanzisha mpango unaoitwa mlango kwa mlango…na sisi kampuni yetu tunaunga mkono na kuhamasisha wananchi na mpaka sasa mwamko umeanza kuonekana.

 Nae Gilango Nyarunge mfugaji wa kijiji cha Salangwe Bunda ambaye amepata fursa ya kutembelea hifadhi ya Serengeti alisema amejifunza vitu vingi na kuahidi kuhamasisha wenzake kuwa na desturi ya kutembelea hifadhi hizo.

"Watanzania tupo  zaidi ya milioni 60 kwa sasa lakini ukiangalia idadi ya watu wanaoingia kwenye hifadhi zetu  kuangalia utalii ni wachache kuliko  idadi ya watu waliopo nchini hali hii inaonyesha sisi siyo wazalendo ni  vyema tupende  utalii wa kwetu wa ndani .

mwisho


Share:

Waziri Bashungwa Asisitiza Maafisa Habari kutoa Taarifa kwa Umma


Na Shamimu Nyaki,Mbeya
Waziri wa Habari, Itamaduni, Sanaa na Michezo Mhe.Innocent Bashungwa amewaagiza Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano Serikalini kujituma kwa kasi, ari na weledi ambapo amesema atayezembea hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Mhe.Bashungwa ameyasema hayo Mei 24, 2021 Jijini Mbeya wakati akifungua Kikao kazi cha Maafisa Habari, Mawasiliano na Uhusiano wa Serikali ambapo amesema kikao hicho  kiwe chachu ya kuboresha utendaji  pamoja na kufanya tathmini ya utekelezaji wa majukumu ya maafisa hao  kwa mwaka 2021 ili kutekeleza kauli ya Baba wa Taifa Mwl. nyerere inayosema " Kujikosoa ni Kujisahihisha"

"Nimeguswa na Kauli Mbiu ya kikao hiki kwa mwaka huu isemayo "Utoaji Taarifa kwa Umma ni Takwa la Kisheria Viongozi wa Umma na Maafisa Habari Tuwajibike, Hivyo

Wizara ninayoisimamia inaendelea kufanya mageuzi makubwa katika kusimamia utoaji wa huduma za habari kwa umma, na hii ni utekelezaji wa Sheria ya Huduma ya Habari ya Mwaka 2016, na Sheria ya Haki ya Kupata Habari ya Mwaka 2016" amesisitiza Mhe. Bashungwa.

Aidha Mhe.Bashungwa ametumia nafasi hiyo kutoa rai kwa Makatibu Wakuu wa   Wizara yake na Ofisi ya Rais TAMISEMI kuhakikisha changamoto zote zinazowakabili maafisa hao ikiwemo kutoshirikishwa kwenye ziara za kutembelea miradi mbalimbali inayotokelezwa na Wizara au Taasisi, baadhi ya Maafisa Habari kuwekwa chini ya Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano ( TEHAMA) ambapo majukumu yake hayapewi kipaumbele pamoja na kutokuwa na bajeti, vifaa na bajeti ya Inteneti na Simu zinatatuliwa mara moja

Hata hivyo amewasisitiza Viongozi wa Wizara, Taasisi, Halmashauri za Wilaya, Manispaa Miji na Majiji kuhakisha wanatoa ushirikiano kwa maafisa habari ili watekeleze majukumu yao vizuri.

Kwa Upande wake Naibu Waziri Mhe.Pauline Gekul amesema Wizara yake inagusa watu wengi na ni Wizara inayozungumza, hivyo itaendelea kushirikiana kutatua changamoto za maafisa hao

"Natoa rai kwenu kufanya kazi kwa bidii, tuhabarishe umma mambo yote yanayotekelezwa na Serikali, tufanye kwa wakati na kuzingatia weledi na taaluma ya habari, pamoja na kuwa waadilifu" Mhe.Gekul.

Awali, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt.Hassan Abbasi alitumia kikao hicho kushukuru maafisa hao kwa ushirikiano waliompatia  wakati akiwa Mkurugenzi Idara ya Habari - MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali na kuwasihi kuendelea kutekeleza majukumu yao vyema.

"Tuendelee kushirikiana katika Cheo kipya cha Katibu Mkuu katika Wizara hii ambayo ni Wizara muhimu katika kugusa umma kwa nyanja ya Burudani na Huzuni kutokana na Sekta zake"amesema Dkt. Abbasi.

Hata hivyo wakati kikao kinaendela Katibu Mkuu alipokea ujumbe kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan kwa maafisa hao

Akisoma ujumbe kwa Maafisa Habari na Uhusiano kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan, Dkt.Abbasi amenukuu

"Naomba muendelee kuhimizana kuhusu umuhimu wa taarifa kwa Umma, yale yasiyo mazuri na yasiyo ya lazima kuwe na namna bora ya kutoa taarifa na msiache kusema mpaka wananchi waanze kulalamika ndiyo watoe taarifa"

Naye Katibu Mkuu TAMISEMI Prof. Riziki Shemdoe alisisitiza maafisa hao Maafisa Habari kutangaza miradi ya Serikali kwa umma.

Huku Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe.Juma Homera akitoa rai kwa Wakurugenzi kutenga bajeti kwa ajili ya Maafisa hao na kuwapatia vifaa mbalimbali wanavyohitaji katika kutekeleza majukumu yao.

Vilevile Mwenyekiti wa Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini (TAGCO) Paschal Shelutete akitoa neno la shukrani kwa niaba ya Maafisa hao amesema kikao hicho ni chachu ya kuendelea kuboresha utendaji wa maafisa hao.


Share:

Waziri Wa Maliasili Atangaza Rasmi Operesheni Ya Wavamizi Wa Hifadhi Wilayani Tunduru


 Na Happiness Shayo – TUNDURU
Wizara ya  Maliasili na Utalii imetangaza operesheni kabambe ya kuwaondoa wafugaji wote waliovamia na kufanya shughuli zao katika hifadhi ya Taifa ya Nyerere na maeneo mengine yaliyotengwa kwa ajili ya utalii na uhifadhi wa wanyama mkoani Ruvuma.

 Kauli hiyo imetolewa jana na Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro  wakati akiongea na wananchi wa vijiji vya Kalulu na Jakika wilayani Tunduru, wakati wa ziara yake ya kusikiliza kero ya wananchi kuhusiana na wanyamapori wanaovamia mashamba na kufanya uharibifu wa  mazao wilayani  humo.

Alisema, tatizo la wanyama hususani Tembo wanaokula mazao ya wakulima limechangiwa kwa kiasi kikubwa na wafugaji kuingiza mifugo yao kwenye maeneo yasioruhusiwa kisheria jambo linalosababisha wanyama  hao kukimbia.

Kwa mujibu wa Dkt. Ndumbaro Serikali imeshatenga maeneo maalum kwa ajili  ya shughuli za ufugaji, lakini kutokana na kiburi cha fedha wafugaji  wanawatumia baadhi ya wenyeviti na watendaji wa serikali za vijiji wasiokuwa waaminifu kukaidi kupeleka mifugo  kwenye maeneo waliyotengewa.

Dkt Ndumbaro amewaonya wenyeviti na watendaji hao kujiepusha  na vitendo  vya rushwa kwa kupokea fedha na kuruhusu wafugaji kufanya shughuli zao kwenye maeneo ya utalii kwani tabia hiyo ni  kukiuka sheria za utumishi wa umma.

Waziri Ndumbaro, amewataka wananchi kuepuka  kuishi na kufanya shughuli zao kwenye hifadhi kwani serikali  haitahusika kulipa fidia wala kifuta machozi kwa mtu atakayepoteza maisha, kujeruhiwa na kuharibiwa mazao.

Aidha alisema, ili kukabiliana na wanyama wanaovamia mashamba na kuharibu mazao, Serikali kupitia Wizara ya  Maliasili na Utalii imeanza kutoa mafunzo kwa vijana kwenye vijiji vinavyozungukwa na hifadhi na mapori ya akiba ili kuwajengea uwezo wa kufukuza wanyama pindi wanapofika kwenye makazi ya watu.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Tunduru, Julius Mtatiro alisema, wilaya  hiyo ni ya kilimo lakini changamoto kubwa  kuvamiwa na wafugaji na mifugo mingi kutoka katika maeneo mengine ya nchi jambo lililosababisha kutokea kwa migogoro kati ya jamii ya wafugaji na wakulima.

Alisema, licha ya serikali ya wilaya kutenga zaidi ya vitalu 200 vya ufugaji, lakini jambo la kusikitisha baadhi ya viongozi wa ngazi za vijiji wanaruhusu wafugaji kupeleka mifugo kwenye maeneo yasioruhusiwa.

Mtatiro ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama alisema, katika kukabiliana na changamoto hiyo serikali ya wilaya inafanya operesheni za mara kwa mara kuwaondoa wavamizi wote wanaofanya shughuli za kibinadamu kwenye hifadhi na maeneo yote yasiyoruhusiwa.

Baadhi ya wananchi wa vijiji hivyo, wameiomba serikali kupitia upya viwango vya fedha vinavyotolewa kwa waathirika wa matukio ya kushambuliwa na wanyama wakali  na  wanaoharibu mazao kwani havilingani na hasara inayotokea.

Mwenyekiti wa Baraza la Wazee Wilaya ya Tunduru, Ajili Kalolo alisema, wananchi wanalazimika kuondoa mazao yao mashambani kabla hayajakomaa ili kuepuka kuliwa na wanyama.

Kalolo alisema, kama serikali itaendelea na msimamo wake wa kuwaona wananchi ndiyo wenye makosa kwa kile kinachodaiwa kuvamia kwenye hifadhi basi kuna hatari wilaya hiyo kukumbwa na janga la njaa.

Msanga Rashid mkazi wa kijiji cha  Kalulu, ameiomba Wizara ya Maliasili na Utalii kuwasaidia kukabiliana na wanyama wakali na waharibifu wa mazao, badala ya kuwaona wananchi  ndiyo wakosaji kwani kama serikali itaendelea na msimamo huo kuna hatari  baadhi ya vijiji kutokuwa na watu kwa kuuawa na wanyama.


Share:

WAJASIRIAMALI VIJIJI VINAVYOZUNGUKA MGODI WA BULYANHULU WATUA NA BIDHAA 100 MAONESHO YA WAJASIRIAMALI NA WAWEKEZAJI KAHAMA


Meneja wa Mahusiano ya Jamii Mgodi wa Bulyanhulu, Dkt. Zumbi Musiba (kushoto) na Wajasiriamali kutoka vijiji 14 vinavyozunguka Mgodi wa Bulyanhulu wakionesha bidhaa mbalimbali kwenye Maonesho ya Wajasiriamali na Wawekezaji Kahama yanayofanyika katika Kituo cha Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Nyihogo Mjini Kahama.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Wajasiriamali zaidi ya 33 wanaotoka katika vijiji 14 vinavyozunguka Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu uliopo katika Halmashauri ya wilaya ya Msalala mkoani Shinyanga wanashiriki katika Maonesho ya Wajasiriamali na Wawekezaji wilayani Kahama wakiwa na bidhaa zaidi ya 100.

Maonesho ya Wajasiriamali na Wawekezaji Kahama yaliyoandaliwa na Taasisi ya GS1 Tanzania kupitia Kituo cha Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Kahama yameanza leo Jumatatu Mei 24,2021 yatafikia tamati Mei 30,2021 katika viwanja vya Kituo cha Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Nyihogo Mjini Kahama yakiongozwa na kauli mbiu ya ‘Nunua bidhaa za Kitanzania kuza uchumi wa nchi’.

Akizungumza wakati wa Maonesho hayo,Meneja wa Mahusiano ya Jamii Mgodi wa Bulyanhulu, Dkt. Zumbi Musiba amesema mgodi huo umewaleta wajasiriamali wanaofanya shughuli zao katika Mgodi wa Bulyanhulu na nje ya mgodi kushiriki kwenye maonesho ili kukuza bidhaa, kupata masoko na kujifunza kutoka kwa wajasiriamali wengine ili kuongeza thamani ya bidhaa wanazozalisha.

“Miongoni mwa Wajasiriamali 33 waliowezeshwa na mgodi wa Bulyanhulu ni wale wanaojihusisha na kilimo cha mazao ya nafaka,mboga mboga na matunda, watengenezaji na washonaji wa nguo,wana mitindo, wafugaji wa kuku,wauzaji mayai,wafugaji nyuki,wataalamu wa kilimo na Kikundi cha Geka Hill chenye mradi wa kutokomeza mazalia ya mbu wanaosababisha Malaria.

Tumekuja na bidhaa zaidi ya 100 zinazozalishwa na wajasairimali hawa, tunapenda wapanue mawazo ya kibiashara na kuboresha bidhaa zao ili kujiinua kiuchumi”,ameeleza Dkt. Musiba.

“Wajasiriamali hawa ni sehemu ya shughuli za maendeleo ya jamii ya Mgodi wa Bulyanhulu ambao wamewezeshwa na mgodi kwa kupewa elimu kuhusu ujasiriamali na kwa wale wanaojihusisha na kilimo tuliwapatia mbegu,mbolea na dawa za kuulia wadudu ili walime mazao kibiashara zaidi”,amesema Dkt. Musiba.

Dkt. Musiba ameishukuru Taasisi ya GS1 Tanzania iliyopo chini ya Kituo cha Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Kahama ambacho kipo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu kuandaa maonesho hayo ili kuonesha bidhaa zinazozalishwa na wajasiriamali wa ndani ya nchi ambao pia watapata elimu ya kuongeza thamani ya bidhaa hizo.

Ameitaja changamoto inayowakabili wajasiriamali hao kuwa ni ukosefu wa mitaji hali inayowafanya washindwe kupata mikopo kwenye Benki hivyo wanaangalia namna ya kushirikiana na halmashauri ili wajasiriamali wapate mikopo yenye riba nafuu na isiyo na masharti magumu.

Nao baadhi ya wajasiriamali hao wamesema maonesho hayo yanawapa fursa ya kuonesha bidhaa wanazozalisha ambapo watapata elimu ya namna ya kufungasha bidhaa,urasimishaji biashara,kufungua fursa za masoko.
Meneja wa Mahusiano ya Jamii Mgodi wa Bulyanhulu, Dkt. Zumbi Musiba akizungumza katika Banda la Wajasiriamali kutoka vijiji 14 vinavyozunguka Mgodi wa Bulyanhulu kwenye Maonesho ya Wajasiriamali na Wawekezaji Kahama yanayofanyika katika Kituo cha Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Nyihogo Mjini Kahama leo Jumatatu Mei 24,2021 - Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Meneja wa Mahusiano ya Jamii Mgodi wa Bulyanhulu, Dkt. Zumbi Musiba akizungumza katika Banda la Wajasiriamali kutoka vijiji 14 vinavyozunguka Mgodi wa Bulyanhulu kwenye Maonesho ya Wajasiriamali na Wawekezaji Kahama yanayofanyika katika Kituo cha Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Nyihogo Mjini Kahama leo Jumatatu Mei 24,2021 
Meneja wa Mahusiano ya Jamii Mgodi wa Bulyanhulu, Dkt. Zumbi Musiba akionesha bidhaa zinazozalishwa na Wajasiriamali kutoka vijiji 14 vinavyozunguka Mgodi wa Bulyanhulu kwenye Maonesho ya Wajasiriamali na Wawekezaji Kahama yanayofanyika katika Kituo cha Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Nyihogo Mjini Kahama.
Meneja wa Mahusiano ya Jamii Mgodi wa Bulyanhulu, Dkt. Zumbi Musiba akionesha sabuni inayozalishwa na Wajasiriamali kutoka vijiji 14 vinavyozunguka Mgodi wa Bulyanhulu kwenye Maonesho ya Wajasiriamali na Wawekezaji Kahama yanayofanyika katika Kituo cha Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Nyihogo Mjini Kahama.
Meneja wa Mahusiano ya Jamii Mgodi wa Bulyanhulu, Dkt. Zumbi Musiba akionesha nguo iliyotengenezwa na Wajasiriamali kutoka vijiji 14 vinavyozunguka Mgodi wa Bulyanhulu kwenye Maonesho ya Wajasiriamali na Wawekezaji Kahama yanayofanyika katika Kituo cha Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Nyihogo Mjini Kahama.
Meneja wa Mahusiano ya Jamii Mgodi wa Bulyanhulu, Dkt. Zumbi Musiba akionesha matikiti yanayozalishwa na Wajasiriamali kutoka vijiji 14 vinavyozunguka Mgodi wa Bulyanhulu kwenye Maonesho ya Wajasiriamali na Wawekezaji Kahama yanayofanyika katika Kituo cha Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Nyihogo Mjini Kahama.
Meneja wa Mahusiano ya Jamii Mgodi wa Bulyanhulu, Dkt. Zumbi Musiba akionesha magimbi yanayozalishwa na Wajasiriamali kutoka vijiji 14 vinavyozunguka Mgodi wa Bulyanhulu kwenye Maonesho ya Wajasiriamali na Wawekezaji Kahama yanayofanyika katika Kituo cha Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Nyihogo Mjini Kahama.
Meneja wa Mahusiano ya Jamii Mgodi wa Bulyanhulu, Dkt. Zumbi Musiba (kushoto) akiangalia dawa za kutibu maradhi mbalimbali zinazozalishwa na Wajasiriamali kutoka vijiji 14 vinavyozunguka Mgodi wa Bulyanhulu kwenye Maonesho ya Wajasiriamali na Wawekezaji Kahama yanayofanyika katika Kituo cha Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Nyihogo Mjini Kahama.
Meneja wa Mahusiano ya Jamii Mgodi wa Bulyanhulu, Dkt. Zumbi Musiba na Wajasiriamali kutoka vijiji 14 vinavyozunguka Mgodi wa Bulyanhulu  wakionesha nguo kwenye Maonesho ya Wajasiriamali na Wawekezaji Kahama yanayofanyika katika Kituo cha Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Nyihogo Mjini Kahama.
Meneja wa Mahusiano ya Jamii Mgodi wa Bulyanhulu, Dkt. Zumbi Musiba na Wajasiriamali kutoka vijiji 14 vinavyozunguka Mgodi wa Bulyanhulu  wakionesha nguo kwenye Maonesho ya Wajasiriamali na Wawekezaji Kahama yanayofanyika katika Kituo cha Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Nyihogo Mjini Kahama.
Meneja wa Mahusiano ya Jamii Mgodi wa Bulyanhulu, Dkt. Zumbi Musiba na Wajasiriamali kutoka vijiji 14 vinavyozunguka Mgodi wa Bulyanhulu  wakionesha nguo kwenye Maonesho ya Wajasiriamali na Wawekezaji Kahama yanayofanyika katika Kituo cha Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Nyihogo Mjini Kahama.
Meneja wa Mahusiano ya Jamii Mgodi wa Bulyanhulu, Dkt. Zumbi Musiba na Wajasiriamali akiangalia dawa ya kuua mbu inayotengezwa na Wajasiriamali kutoka vijiji 14 vinavyozunguka Mgodi wa Bulyanhulu  wakionesha nguo kwenye Maonesho ya Wajasiriamali na Wawekezaji Kahama yanayofanyika katika Kituo cha Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Nyihogo Mjini Kahama.
Mwananchi akisikiliza maelezo kuhusu uzalishaji wa mazao mbalimbali katika Banda la Wajasiriamali kutoka vijiji vinavyozunguka mgodi wa Bulyanhulu kwenye Maonesho ya Wajasiriamali na Wawekezaji Kahama yanayofanyika katika Kituo cha Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Nyihogo Mjini Kahama.
Mwananchi (kulia) akiangalia bidhaa zinazolishwa na Wajasiriamali kutoka vijiji 14 vinavyozunguka Mgodi wa Bulyanhulu  kwenye Maonesho ya Wajasiriamali na Wawekezaji Kahama yanayofanyika katika Kituo cha Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Nyihogo Mjini Kahama.
Mjasiriamali Kasanda James Chai kutoka Bufaso AMCOS Bugarama (kulia) akiwaelezea wananchi kuhusu kilimo bustani na mbogamboga kwenye Maonesho ya Wajasiriamali na Wawekezaji Kahama yanayofanyika katika Kituo cha Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Nyihogo Mjini Kahama.
Mjasiriamali Kasanda James Chai kutoka Bufaso AMCOS Bugarama (kushoto) akiwaelezea wananchi kuhusu kilimo mazao ya nafaka kwenye Maonesho ya Wajasiriamali na Wawekezaji Kahama yanayofanyika katika Kituo cha Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Nyihogo Mjini Kahama.
Wananchi wakiwa kwenye Banda la Wajasiriamali kutoka vijiji vinavyozunguka mgodi wa Bulyanhulu kwenye Maonesho ya Wajasiriamali na Wawekezaji Kahama yanayofanyika katika Kituo cha Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Nyihogo Mjini Kahama.
Mjasiriamali Mamuu Albert Makere kutoka Kampuni ya Mamuu Chicken akionesha mayai na kuku katika banda la Wajasiriamali kutoka vijiji vinavyozunguka mgodi wa Bulyanhulu kwenye Maonesho ya Wajasiriamali na Wawekezaji Kahama yanayofanyika katika Kituo cha Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Nyihogo Mjini Kahama.

Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Soma pia:

Share:

HAFLA YA MAKABIDHIANO YA MAGARI YA MRADI WA REGROW JIJINI DODOMA


Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Allan Kijazi akizungumza katika halfa ya kukabidhi magari 9 kwa taasisi za TAWIRI, Wakala wa Huduma za Misitu (TFS), Bodi ya Utalii (TTB) ,Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC) ,Bonde la Mto Rufiji (RBWB) ,na Timu ya Uratibu kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii kwa lengo la kuimarisha utendaji kazi wa taasisi hizo katika shughuli za mradi wa REGROW. Makabidhiano hayo yalifanyika jijini Dodoma.
Mratibu wa Mradi , Aenea Saanya akizungumza kabla ya kumkaribisha Katibu Mkuu kwenye hafla ya makabidhiano ya magari ya Mradi wa Regrow iliyofanyika jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Allan Kijazi akikata utepe katika hafla ya makabidhiano ya magari ya mradi wa REGROW huku akishuhudiwa na Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki, Dkt. Ezekiel Mwakalukwa na mwakilishi wa Tawiri, Dkt. Wilfred Mareale.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Allan Kijazi akimkabidhi funguo za gari mwakilishi wa TAWIRI, Dkt. Wilfred Mareale kwenye hafla ya makabidhiano ya magari ya mradi wa REGROW jijini Dodoma.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Allan Kijazi ( katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na wawakilishi wa Taasisi baada ya kukabidhiwa funguo za magari kwenye hafla ya makabidhiano ya magari ya mradi wa REGROW jijini Dodoma.

(Picha zote na Gladys Lukindo- Afisa Habari, Wizara ya Maliasili na Utalii)
Share:

Relationship Manager, SME – Eastern Zone, Morogoro (Re-advertised) at NMB Bank

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job Purpose Responsible for growing both Liabilities (Deposits) and Assets from Small and Medium Enterprises (SMEs) for Business banking; advising the department on business strategy, assisting SME Business Bankers /Relationship Officers/Branch Managers in recruiting business customers to ensure SME business growth. Main Responsibilities Actively selling SME deposits, lending and cross selling of other banks products […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Spika Ndugai awaapisha Wabunge wapya Muhambwe na Buhigwe

Spika wa Bunge Job Ndugai, leo Jumatatu Mei 24, 2021  amewaapisha wabunge wawili waliochaguliwa hivi karibuni katika majimbo ya Mkoa wa Kigoma.


Wabunge hao ni Dk Florence Samizi wa jimbo la Muhambwe na Kavejuru Felix wa la Buhigwe,  wote wakitokea CCM.

Wabunge hao  wameapishwa baada ya  ushindi waliopata katika uchaguzi mdogo uliofanyika kwa majimbo hayo kuwa wazi kufuatia kifo cha aliyekuwa mbunge wa Muhambwe,  Atashasta Nditiye na Dk Philip Mpango wa Buhigwe aliyeteuliwa kuwa Makamu wa Rais.


Share:

Data Clerks at COCODA

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

JOB VACANCIES ANNOUNCEMENT Community Concern of Orphans and Development Association (COCODA) is a non-governmental organization established in 2000. COCODA’s establishment as its name suggests, resulted from intensifying concern among community members in Njombe over the surging number of orphans, mainly as a consequence to swelling amount of people infected by HIV and dying from AIDS, […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Communication Coordinator at Grumeti

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

COMMUNICATION COORDINATOR (1) JOB PURPOSE Grumeti Fund Trust (Grumeti Fund) is a non-profit organization created in Tanzania in 2003. The GFT mission is to contribute to the conservation of the Serengeti Ecosystem in partnership with local communities and other stakeholders. Grumeti Fund Trust located in the concessions of Western Corridor of the Serengeti Ecosystem, collaborates with […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Moto Mpya Watinga Na Zawadi Kemkem

Sio wengine tena ni wale wale nguli wa simu za Mkononi Tanzania wanakuja na mazawadi kibao kwa wale watakao nunua simu mpya ya Infinix HOT 10T. 

Katika uzinduzi wa Promotion ya nunua na ushinde zawadi iliyotambulishwa na Meneja Mauzo wa Infinix Bi. Winifrida Chumi alipokuwa akizungumza katika kipindi cha Sports Arena kinachoruka kupitia Kituo cha redio ya Wasafi FM alitangaza zawadi zitakazotolewa ni Jiko la Gesi, jiko la Umeme pamoja na Air coolers kama zawadi kubwa.


Pia zawadi ndogondogo ni pamoja na Vikombe, Headphones, Wireless Keybords na zingine kibao. Promotion hii ni kuanzia Tarehe 6/5 mpaka Tarehe 25/5 katika maduka yote ya simu.

Unaweza kujiuliza ni nini cha ajabu kwenye hii simu? Akielezea sifa za simu hii mpya Bi. Eddah Charles ambae ni Afisa Elimu na Mafunzo wa kampuni ya Infinix amesema simu hii kwanza kabisa ina kamera bora yenye uwezo wa mp48 inayokuwezesha kupata picha zenye rangi halisia ya eneo husika vile vile ina wigo mpaka wa kioo cha ukubwa wa nchi6.82” ambacho ni HD+ (Kioo ng’aavu), na processor G70 yenye speed ya ajabu na kuifanya simu yako kuwa nyepesi wakati wa utumiaji.


Sifa nyengine ambayo ni ya ziada Infinix HOT 10 T PEEK PROOF inakifanya kioo cha simu yako kuwa cheusi na kumnyima uwezo wa kuona aliyepo pemebni yako hivyo kutohitaji kuweka glass protector ya Privacy.

Aisee jiunge na wajanja wenzako mjini kwa kujipatia simu yako ya HOT 10T ukatambe na wanao kitaa. Kwa mengi Zaidi tembelea www.infinixmobility.com
au piga nambari ya simu 0744606222.

 


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger