"Katika kutekeleza sheria Mpya ya Madini kupitia kitengo cha huduma za jamii inayozunguka eneo la Mgodi wa Bulyanhulu, Ako Group Ltd imeajiri mtu mwenye ulemavu wa ngozi 'mtu mwenye ualbino' Gaspal William kutoka kijiji cha Ilogi katika kitengo cha usafi wa ofisi na tayari kikundi kipya cha wanawake cha Mkombozi kutoka Igudija tumekipa utaratibu wa usambazaji matunda safi na mbogamboga kutoka kwenye mashamba yao",aliongeza Kahigi.
Thursday, 1 October 2020
Picha : KAMPUNI YA AKO GROUP LTD YATOA MSAADA WA MIFUKO 200 YA SARUJI KUSAIDIA UJENZI MADARASA SHULE YA BUGARAMA
"Katika kutekeleza sheria Mpya ya Madini kupitia kitengo cha huduma za jamii inayozunguka eneo la Mgodi wa Bulyanhulu, Ako Group Ltd imeajiri mtu mwenye ulemavu wa ngozi 'mtu mwenye ualbino' Gaspal William kutoka kijiji cha Ilogi katika kitengo cha usafi wa ofisi na tayari kikundi kipya cha wanawake cha Mkombozi kutoka Igudija tumekipa utaratibu wa usambazaji matunda safi na mbogamboga kutoka kwenye mashamba yao",aliongeza Kahigi.
Picha : MAGUFULI AKIWAHUTUBIA WANANCHI WA MBALIZI MBEYA LEO ASUBUHI
MWENYEKITI WA MTAA ASIMULIA JINSI MJUKUU WAKE WA MIAKA 7 ALIVYOCHINJWA NA MAMA YAKE
Financial Management Analyst – OSC at U.S. Embassy Dar es Salaam
U.S. MISSION DAR ES SALAAM VACANCY ANNOUNCEMENT The U.S. Mission in Dar es Salaam is seeking eligible and qualified applicants for the position below. Position Title: Financial Management Analyst – OSC Vacancy Number: DaresSalaam-2020-029 Duties Budget Analyst 60% Serves as the Budget Analyst for the Office of Security Cooperation (OSC), with the responsibility of performing […]
The post Financial Management Analyst – OSC at U.S. Embassy Dar es Salaam appeared first on Udahiliportal.com.
Nyasa District Council Jobs September, 2020. Nyasa District is a district of the Ruvuma Region of Tanzania.
The deadline for submitting the application is October 13, 2020
The post Nyasa District Council Jobs September, 2020. Nyasa District is a district of the Ruvuma Region of Tanzania. appeared first on Udahiliportal.com.
MAASKOFU NA WACHUNGAJI WAZINDUA KITABU CHA UONGOZI ULIOTUKUKA WA RAIS JOHN MAGUFULI
Askofu Mkuu wa Makanisa ya Naioth Gospel Assemblies of God ambaye pia ni Katibu Mkuu mstaafu wa Baraza la Maaskofu wa Kipentekoste Tanzania, Dkt. David Mwasota.(kushot) akiwaongoza Maaskofu na Wachungaji kwenye maombi ya kukiombea Kitabu cha Uongozi Uliotukuka wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli katika hafla ya uzinduzi wa kitabu hicho iliyofanyika jijini Dar es Salaam mwanzoni mwa wiki.Wednesday, 30 September 2020
Individual National consultancy at UNICEF
The aim is to assess whether the Parenting Education Programme has been implemented effectively and whether it has brought about positive change in the knowledge and behaviour of parents and caregivers in how to protect their children from violence. UNICEF works in some of the world’s toughest places, to reach the world’s most disadvantaged in […]
The post Individual National consultancy at UNICEF appeared first on Udahiliportal.com.
HESLB Yatoa Siku Tano (05) Kwa Wahitimu Mafunzo Jkt Kuomba Mikopo
Na Mwandishi Wetu, HESLB
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetoa muda wa siku 5 kuanzia Oktoba mosi hadi 5 mwaka huu ili kuwawezesha wanafunzi waliomaliza mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) hivi karibuni kuingia katika mfumo wa kuomba mkopo kwa njia ya mtandao na kukamilisha maombi yao.
Katika taarifa yake aliyotoa kwa vyombo vya habari leo Jumatano (Septemba 30, 2020) Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Abdul-Razaq Badru alisema uamuzi huo unatokana na maombi ya wanafunzi, wazazi na walezi ambao hawakuweza kuomba au kukamilisha maombi yao kutokana na sababu ya kujiunga na mafunzo hayo.
Kwa mujibu wa Badru alisema katika muda huo wa siku tano, mfumo pia utakuwa wazi ili kuwawezesha waombaji ambao maombi yao yana upungufu kurekebisha kwa kuweka nyaraka sahihi ili kuiwezesha HESLB kuendelea na hatua nyingine.
“Kwa wanaorekebisha taarifa, wanapaswa kuingia katika akaunti zao walizofungua kuombea mkopo na watapata ujumbe kuhusu maeneo ya kurekebisha. Tunawasihi watumie muda huu wa siku tano kurekebisha na kukamilisha maombi yao’’ alisema Badru.
Katika mwaka wa masomo 2020/2021, Serikali imetenga TZS Bilioni 464 zitakazowanufaisha jumla ya wanafunzi 145,000. Kati yao, wanafunzi 54,000 watakuwa wa mwaka wa kwanza na wengine 91,000 ni wanafunzi wanufaika wanaoendelea na masomo. Mwaka 2019/2020 jumla ya TZS 450 bilioni zilitengwa na zimewanufaisha jumla ya wanafunzi 132,119.
MWISHO
Barabara za juu kutoka Mwenge kwenda Buguruni katika makutano za barabara ya morogoro,Nelson Mandela na Sam Nujoma zaanza kutumika rasmi leo
Vijana Kagera Watakiwa Kutosubiri Ajira kutoka Serikalini.
Vijana katika halmashauri ya Wilaya ya Missenyi Mkoani Kagera wameaswa kutosubiri ajira kutoka serikalini bali wajikite katika kujiajili haswa katika kilimo,uvuvi na ufugaji ili kuweza kujikwamua na umasikini.
Hayo yamesemwa na bwana Agape Ishabakaki wakati akizungumza na mpekuzi blog ambaye pia ni mratibu wa shirika lisilo la kiserikali la FUAP TANZANIA linalojiusisha na masuala ya kusaidia wakulima na wafugaji ikiwa ni pamoja na kutoa elimu kwa makundi mbalimbali ya watu haswa vijana ili kujenga utamaduni wa kujiajili uku wakiwa wamesubiri ajira kutoka serikalini.
Bwana Agape amesema kuwa shirika hilo kwa sasa limetua mkoani Kagera hususani katika wilaya ya Missenyi na litazungukia kata mbalimbali ili kutoa elimu kwa vijana juu ya faida za kujiajili na kutoa elimu kwa vijana hao kujikita katika kilimo kwa manufaa yao ya badae .
Katika hatua nyingne bwana Agape amesema kuwa zaidi ya miti elfu kumi ya matunda itazalishwa na shirika hilo na zoezi hilo litaanza tarehe mbili mwezi wa kumi katika kata ya Bugorola ili kuwapa fursa vijana pamoja na wananchi wa Missenyi kuwa na elimu juu ya utunzaji mazingira pamoja na kuwa na utamaduni wa kupanada miti katika maeneo yaliyowazunguka.
Kwa upande wake mkurugenzi wa shirika hilo bwana Josephat Joseph John amesema kuwa kwa sasa hivi shirika ilo lina mradi unaoitwa AGRI EXPERIENCE ambapo mradi huo utawawezesha vijana wengi kujifunza na kujua namna ya kufuga kuku wa kisasa pamoja na kufahamu ujuzi mbalimbali wa biashara ya mayai ya kisasa, ufugaji wa nyuki nk.
Bwana Josephat amesema kuwa vijana watumie shirika hilo vizuri kwa kuwa elimu itatolewa bila malipo yoyote na ku ongeza kuwa kabla yakuondoka mkoani hapa vijana wawe wameisha pata maarifa na ujuzi wa kujiajili wenyewe kupitia kilimo na ufugaji wa kisasa uku akitaja kauli mbiu yao kuwa ni “Kijana wa kagera kulima kwa tija kwa maendeleo yao wenyewe na taifa kwa ujumla 2020-2025”.
Serikali Kusimamisha Mishahara Ya Maafisa Utumishi Watakaosababisha Watumishi Kutolipwa Mishahara
Maafisa Utumishi watakaozembea na kusababisha Watumishi wa Umma nchini kutolipwa mishahara yao kwa wakati, watasimamishiwa mishahara na Serikali mpaka watakapohakikisha watumishi hao wamelipwa mishahara yao.
Hayo yamesemwa jana na Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Dkt. Francis Michael wakati akifungua mafunzo ya wiki mbili ya Mfumo Mpya wa Kitanzania wa Taarifa za Kiutumishi na Mishahara kwa kundi la pili la Maafisa Utumishi na Maafisa Tawala 140 kutoka mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Mara, Manyara, Arusha, Kilimanjaro, Tanga, Pwani, Dar es Salaam, Lindi, Mtwara, Kigoma na Tabora yanayofanyika jijini Dodoma katika Ukumbi wa VETA.
DKt. Michael amesema, kuna tatizo katika baadhi ya Taasisi za Umma kwani wapo Maafisa Utumishi wanajifanya miungu watu wakati wajibu wao ni kumtengenezea mazingira mazuri ya kikazi mtumishi ili ajisikie yuko sehemu salama na aweze kutekeleza ipasavyo jukumu la kuwahudumia wananchi.
“Msiwafanye watumishi mnaowasimamia kuona sehemu ya kazi kama jehanamu, hivyo mbadilike kwani Serikali haitomvumilia yeyote atakaye kinzana na azma yake ya kuboresha huduma kwa wananchi”, Dkt. Michael alisisitiza.
Ameongeza kuwa, ni lazima Maafisa Utumishi wabadilike kwa kuwajengea mazingira Watumishi wa Umma kuipenda Serikali yao kwasababu inawajali na kuthamini mchango wao katika maendeleo ya taifa.
Dkt. Michael amefafanua kuwa, Serikali inamhakikishia mtumishi usalama wa ajira yake tofauti na sekta binafsi, hivyo hakuna Afisa Utumishi atakayevumiliwa pindi akisababisha Serikali kulaumiwa na Watumishi wa Umma au Wananchi.
Naye, Mkuu wa Idara ya Utawala na Utumishi, Halmashauri ya Wilaya ya Liwale Bw. Boniface B. Chatila kwa niaba ya washiriki wa mafunzo hayo, ameahidi kuwa, wakirejea katika maeneo yao ya kazi watahakikisha wanatekeleza majukumu yao kikamilifu ili kuondoa kero ya Watumishi wa Umma kufuata huduma Ofisi ya Rais Utumishi Dodoma, huduma ambazo wanastahili kupewa katika maeneo yao ya kazi.
Aidha, Bw. Chatila amemhakikishia Dkt. Michael kuwa, ujuzi watakaoupata kupitia mafunzo ya Mfumo Mpya wa Kitanzania wa Taarifa za Kiutumishi na Mishahara watautumia ipasavyo kuongeza ufanisi kiutendaji ili kuboresha utoaji huduma kwa umma.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini, ACP Ibrahim Mahumi amesema, suala la mtumishi kukosa mshahara hivi sasa linachukuliwa kama ni kosa kubwa hivyo Afisa Utumishi atakayebainika atasimamishiwa mshahara ikiwa ni hatua ya awali na atachukuliwa hatua za kinidhamu ikizingatiwa kuwa, mfumo mpya utaonesha uzembe wa afisa huyo.
Mfumo Mpya wa Kitanzania wa Taarifa za Kiutumishi na Mishahara utaanza kutumika rasmi Mwezi Novemba, 2020 mara baada ya kukamilika kwa mafunzo ya makundi yote ya Maafisa Utumishi na Maafisa Tawala ambao ndio wenye jukumu la kuutumia mfumo huo kiutendaji.
Sumaye aishukia CHADEMA, asema hawawezi kuongoza nchi
Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Frederick Sumaye amesema vyama vya Upinzani nchini haviwezi kuongoza nchi kwa sababu hawana sera.
Ameyasema hayo Leo septemba 30,2020 akizungumza na wananchi wa Jimbo la Mbulu Vijijini katika mkutano wa Mgombea Mwenza Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kunadi Sera za Chama cha Mapinduzi katika viwanja Vya Haydom.
Sumaye amesema Chama alichotoka CHADEMA, ni Chama cha Uwana harakati na hakina sera zozote za kuwasaidia wananchi.
'CHADEMA wanafikiri kuwa nchi ya Tanzania bado ipo mikononi mwa Wakoloni, wanapiga kelele utafikiri bado tunatawaliwa' alisema Sumaye
'Nilienda kule lakini baada ya kugundua hawana chochote nikaamua kurejea nyumbani' alisisitiza Sumaye
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Manyara Simon Lulu amesema Chama hicho kinajiandaa kwa ushindi wa kishindo kwa sababu kimefanya maendeleo kwa wananchi.
Amemweleza Mgombea Mwenza kiti cha Urais Tanzania Samia Suluhu Hassan kwamba katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika oktoba 28 mwaka huu, Upinzani mkoani hapo hawataambulia hata kiti cha Udiwani.
Wahamiaji Haramu 32 Wakamatwa Wilayani Pangani
Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kukamatwa kwa wahamiaji hao Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi wa Hifadhi ya Taifa ya Saadani Grace Lobora alisema kwamba wahamiaji hao walikamatwa Septemba 27 mwaka huu usiku.
Alisema ukamatwa huo waliofanya baada ya kupata taarifa kutoka wananchi wa Kijiji cha Buyuni kupitia Mwenyekiti wa Kijiji hicho Diwani Akida ambaye aliwaeleza uwepo wa mazingira yasiyoridhisha kwenye eneo lake hasa eneo la bahari baada ya boti moja kukwama.
Alisema baada ya kupata taarifa hiyo wao kama wahifadhi wana jukumu la kulinda maliasili na kuangalia usalama kwenye miji yote inayowazunguka waliandaa kikosi kazi cha kwanza waliokwenda eneo la tukio na walipofika waliwakuta wahamiaji hao eneo la bahari karibu na hifadhi hiyo katika kijiji cha Buyuni.
Alisema baadae hapo waliamua kutuma kikosi cha pili na ndipo walipofika na kufanikiwa kukaweka chini ya ulinzi wahamiaji 28 ambao ni raia wa Ethiopia lakini alfarji wakapata taarifa nyingine ya uwepo wa wahamiaji wengine wanne ambao ni raia wa Somalia na wakatuma kikosi na kufanikiwa kuwaweka chini ya ulinzi.
“Kati yao wapo wahamiaji 32 raia wa Ethiopia 28 na raia wa Somalia wanne akiwemo mwanamke mmoja kwa hiyo baada ya kufanikisha tukio hilo tumewafikisha na kuwakabidhi kwenye mamlaka ya Polisi kwa ajili ya hatua zaidi”Alisema
Awali akizungumza kuhusiana na tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga Blasius Chatanda aliwapongeza askari wa Hifadhi ya Taifa ya Saadani kwa kazi nzuri kwa kushirikiana na askari wa Jeshi la Polisi wilaya ya Pangani.
Hata hivyo amesema kwamba hivi sasa wametangaza vita mpya kwa mawakala wanaojishuhulisha na usafirishaji wa wahamiaji haramu mkoani Tanga kwamba hawatasalimika watasakwa popote iwe ni nchi kavu, majini na kisha kufikishwa mahakamani.
Tundu Lissu adai bado hajapokea wito wa malalamiko
Lissu ametoa kauli hiyo hii leo Septemba 30, 2020, wakati akizungumza na waandishi wa habari mkoani Arusha, na na kusisitiza kuwa kwa sababu hana wito wowote yeye ataendelea na ratiba zake za kampeni kama ilivyo kwenye ratiba.
Jana Septemba 29, Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC Dkt. Wilson Mahera alitoa taarifa ya kuthibitisha kumuandikia barua ya wito Tundu Lissu, kufuatia tuhuma mbalimbali anazodaiwa kuzitoa kati ya Septemba 25 na 26 mjini Musoma
Armenia yakataa upatanishi wa Urusi katika mzozo na Azerbaijan Huku Mapigano Yakizidi Kupamba Moto
Waziri mkuu wa Armenia Nikol Pashinyan amesema haitakuwa sahihi kufanya mazungumzo ya amani na Azerbaijan chini ya upatanishi wa Urusi, wakati mapigano ya kuwania udhibiti wa jimbo yakiwa yanaendelea.
"Sio sahihi kabisa kuzungumzia kuhusu mkutano kati ya Armenia, Azerbaijan na Urusi katika wakati wa uhasama mkubwa," amesema Pashinyan wakati akizungumza na shirika la habari la Urusi Interfax.
Ameongeza kuwa hali endelevu na mazingira yanahitajika kwa ajili ya mazungumzo hayo.
Vyombo vya habari nchini Urusi vimeripoti Jumatano kuwa waziri mkuu Pashinya amesema Armenia haifikirii kuweka walinzi wa amani katika jimbo la Nagorno-Karabakh.
Kwa miaka kadgaa, vikosi vya Armenia na Azabajani vimekuwa vikizozania jimbo hilo la Karabakh, ambalo liliamua kutaka kujitenga na Azabajani baada ya kuanguka kwa Umoja wa Kisovieeti katika miaka ya 1990.
Mzozo huo wa muda mrefu uliibuka tena Jumapili huku pande hizo mbili zikirushiana silaha nzito za moto na kulaumiana kwa kuzuka kwa vurugu.
Karibu watu 100 wamethibitishwa kufa katika mapigano hayo ya hivi karibuni na pande zote mbili zinadai kuwa zimesababisha hasara kubwa kwa vikosi vya wapinzani.
DW









































