Tuesday, 7 January 2020

Ujenzi Wa Ofisi Za Tume Jijini Dodoma Unaendelea Kukamilika




Share:

Job at Nature Conservancy (TNC) – Tanzania, Seaweed-Farming Trainer

Job Opportunity at Nature Conservancy (TNC) – Tanzania, Seaweed-Farming Trainer Position: Seaweed-Farming Trainer in Zanzibar –Tanzania Job Summary Background and Rationale The Nature Conservancy (TNC) is a leading conservation organization working around the world to conserve lands and water on which all life depends. In Africa, TNC works in conservation partnerships with other International Organizations, governments, communities and private sector… Read More »

The post Job at Nature Conservancy (TNC) – Tanzania, Seaweed-Farming Trainer appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Job at Exodus Group Limited – Group Legal & Human Resources Manager

Job Opportunity at Exodus Group Limited – Group Legal & Human Resources Manager Position: Group Legal & Human Resources Manager Job Summary Exodus Group Limited with Head Offices at Chang’ombe Temeke Dar es salaam is looking for a Group Legal & Human Resources Manager. Job Description Managing the administration of the Human Resources policies and procedures and also carry… Read More »

The post Job at Exodus Group Limited – Group Legal & Human Resources Manager appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Job at Fastlink Safaris Limited – Sales and Marketing Personnel

Job Opportunity at Fastlink Safaris Limited – Sales and Marketing Personnel Position: Sales and Marketing Personnel Job Description Our company is looking for a Sales Representative to be responsible for generating leads and meeting sales goals. Duties will include sales presentations and product demonstrations, as well as negotiating contracts with potential clients. Reports to: Branch Manager Duties and Responsibilities:… Read More »

The post Job at Fastlink Safaris Limited – Sales and Marketing Personnel appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Job at DAI Global LLC

2 Job Opportunities at DAI Global LLC Job Title: Communications Specialist Job Summary The Communications Specialist will be responsible for implementation of the LTA Communications Plan. The Specialist will assist in the planning, development, design and production, and manage LTA communications materials and events as required. The Specialist will deliver LTA communications directly at village, district, and national level.… Read More »

The post Job at DAI Global LLC appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Kuwa tajiri kwa mtaji wa laki 2 na Nusu tu kupitia ufugaji wa kuku wa kienyeji. Tazama Hapa

Mpendwa msomaji wetu, yawezekana umekuwa ukiwaza sana nini ufanye ili uweze kufanikiwa na kuondokana na adha za umaskini.  Kulalamika tu vyuma vimekaza haitakusaidia kitu kama hutaki kujiongeza ili uongeze kipato chako.

Yako mambo mengi ya kufanya ili kujikwamua kiuchumi. Usitegemee mshahara wako tu. Mimi nataka kukufungua macho kwa jambo moja tu tena kwa uchache. Jambo hili anaweza kulifanya mwenye mtaji mkubwa au mdogo.
 
Somo  ni dogo tu lakini naamini wapo watakaopata mafanikio makubwa sana.
 
Unaweza kuanza kwa mtaji wa Mil.1 mpaka laki tano au hata chini ya hapo.

==>>Mfano. Unaweza kutumia Tsh 250,000 kununua kuku 25 kwa bei ya Tsh 10,000 kwa kuku mmoja (kadirio la juu) Majogoo watakuwa 5 kwa uwiano wa 1:4.

Hii ina maana kuwa wakishaanza kutaga utakuwa na

vifaranga 20 x 10 = 200 Watunze vizuri.

Wale vifaranga tunakadiria kuwa majike watakuwa 150 ambao ndani ya miezi 3 au zaidi nao wataanza kutaga.

Utakuwa na kuku 200 + 25( ulioanza nao) =225 ndani ya miezi 6. Miezi 6 inayofuata 225 - (majogoo 55) = 170 Hii ina maana kuwa 170 x 10= 1,700.

Ndugu msomaji, hayo niliyotoa ni makadirio ya chini sana hivyo mpaka mwisho wa mwaka utakuwa na kuku zaidi ya 2000. 

Mwaka utakaofuata utakuwa na kuku wangapi baada ya kuuza kuku baadhi  ili upate fedha ya kuwalisha ????

Ukiuza kuku 1000, utabaki na kuku 1000, kati yao tuseme majike ni 750. Ndani ya Miaka 2 maanake ni  750(majike) x 10 = kuku 7500 (uza wengine upate pesa ya kutumia kuwalisha) . 

Tuseme sasa utabakiwa na kuku jike  3000 x 10( jike moja ni mayai 10) = kuku 30,000. 

Hao kuku 30,000  ukiwauza wote utapata; 30,000x 13000( bei ya kawaida kbsa)= 390,000,000. Je, bado utakuwa masikini? Bado vyuma vitakuwa vimekaza?

Nina uhakika, mpaka mwisho wa mwaka huo wa pili utakuwa umefanikiwa sana kuukimbia UMASIKINI.

Kwenye hayo mamilioni, hata ukitoa milioni 100 kwamba  tuseme ndo zimetuka kuendeshea mradi wako, bado utakuwa ni milionea tu. Kumbuka huu ni mwongozo tu, fanya utafiti na ufuatilie zaidi.

NB: Ukiyapata hayo mamilioni ya pesa, kumbuka kutoa Zaka, sadaka na kusaidia masikini wasiojiweza ili ubarikiwe zaidi 




Share:

Jinsi Punyeto Inavyo Sababisha Kusinyaa Na Kudumaa Kwa Maumbile Ya Kiume

Wanaume  wanao  jihusisha  na  upigaji  wa  punyeto  kwa  muda  mrefu  husalia  kuwa  na  maumbile  ya  kiume  yaliyo  sinyaa  na  kudumaa.

Kwa mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, kufanya  punyeto  kwa  muda  mrefu  huathiri  na  kuharibu  mishipa  na  misuli  na  hivyo kusababisha  kujengeka  kwa  mafuta na  tishu  zisizo vutika  kwenye  mishipa  ya  ateri na  hivyo  kuzuia  mishipa ya  ateri  kupanuka na  kuongezeka  pamoja  na  damu  kutiririka  kwenda  kwenye  misuli  ya  uume.

Mambo  hayo  mawili yanapotokea  huathiri  uzalishaji  wa homoni muhimu  zinazo  husika  na ukuaji wa misuli ya  uume, na hatimaye  hufanya  uume  wa  mhusika  kudumaa, kusinyaa, kunywea  na  kurudi ndani  kiasi  cha  kuufanya  uonekane  kama wa  mtoto.

 Homoni  hizo hujulikana   kitaalamu kama  HGH  na  huzalishwa  kwenye  ini.

Sababu nyingine   inayo  tajwa  na  wataalamu  ni kwamba, mtu  anaye fanya punyeto   hutumia  akili,  nguvu na  nishati  nyingi sana, jambo ambalo  huathiri utendaji  wa  ogani  nyingine  muhimu  katika  mwili , likiwemo  ini.

Na kwamba  ini  linapo kosa  nishati   ya kutosha  hushindwa  kufanya kazi  zake  vizuri  na  moja  kati  ya  kazi kubwa  za  ini  ni  pamoja  na  uzalishaji  wa  homoni  zijulikanazo  kitaalamu kama  HGH  ambazo  kama  ilivyo andikwa  hapo juu, zinahusika na  kuchochea  ukuaji  wa  sehemu mbalimbali  katika  mwili  wa  mwanadamu  ikiwemo   misuli  ya  uume.

Mbali na  kuathiri  utendaji  wa  ogani  nyingine  mwilini, upigaji  punyeto  husababisha  athari nyingine  kwenye  mwili wa  mwanadamu  kama  vile uchovu  sugu  wa mwili  pamoja na kunyonyoka kwa  nywele.

Athari nyingine  za  upigaji punyeto  ni  pamoja  na  kupoteza  kumbukumbu, kuwahi  kufika  kileleni  ambako  husababishwa  na  kulegea  kwa  mishipa  ya  ateri, kushindwa  kurudia  tendo  la  ndoa, kukosa  hamu  ya  tendo  la  ndoa, uume  kusimama  katika  hali  ya  ulegelege,   maumivu  wakati  wa  tendo  la  ndoa  husuani  wakati  wa  kurudia  tendo  la pili na    mara  baada  ya  tendo  la  ndoa  la  kwanza.

KWANINI   WATU WENGI  WANAO  JIHUSISHA  NA  UPIGAJI  PUNYETO  WANA  MAUMBILE  MADOGO  YA   YALIYO  DUMAA, SINYAA  NA  KURUDI NDANI.

Uzeofu  unaonyesha  kuwa,  asilimia  kubwa  ya  wanaume  ambao  wamewahi  kufanya  punyeto  kwa  muda  mrefu, wanakabiliwa  na  tatizo  la kuwa  na  maumbile  ya  kiume yaliyo dumaa, sinyaa  na  kurudi ndani.

SABABU  KUBWA   NI  HII  HAPA
Sababu  kubwa  ni kwamba   vijana wengi  wa  kiume, huanza  kujihusisha  na  punyeto   wakiwa  na  miaka  kumi  na sita , kumi na  saba  au  chini  ya  hapo.

Hiki ni  kipindi  ambacho  vijana  hawa  ndio  wanakuwa  wamebalehe.

Na kwa mujibu  wa  tafiti  za kisayansi, katika  kipindi  hiki cha  balehe  ndio  kipindi  ambacho  homoni za  HGH  ambazo huhusika  na  ukuaji  wa  sehemu  mbalimbali  za  mwili  ikiwemo  maumbile ya  kiume, huzalishwa  kwa wingi.

Kama  tulivyo ona  hapo  juu, upigaji  punyeto  huathiri  uzalishwaji  wa   homoni  hizo.

Mwisho wa  siku  maumbile  ya  kiume  ya  wahusika, hushindwa  kukua  na  kuishia  kudumaa na  kusinyaa.

Na  hii ndio  sababu  kubwa  wanaume  wanao  kabiliwa  na  tatizo  hili  husalia  kuwa  na  maumbile yenye  ukubwa  ule  ule  walio kuwa  nao wakati wa  kubalehe

NINI  SULUHU  YA  TATIZO  LA  KUDUMAA, KUSINYAA  NA  KURUDI NDANI KWA  MAUMBILE  YA  KIUME.
Kama maumbile yako yamedumaa, sinyaa, legea, nywea  na  kurudi ndani  kwa  sababu  ulifanya  punyeto  kwa  muda  mrefu  na  unataka  kuondokana  na  hali  hiyo. HII  NI HABARI NJEMA  SANA  KWAKO! 
 
Ipo dawa    ambayo  HUTIBU  na  KUPONYESHA  KABISA  tatizo la  KUDUMAA, KUSINYAA, KUNYWEA  NA  KURUDI NDANI  KWA MAUMBILE  YA  KIUME kunako  tokana  na  ufanyaji  punyeto  wa  muda  mrefu.
 
Ni  dawa  ambayo  hutibu  na  kuponyesha  kabisa  tatizo  la kudumaa  na  kusinyaa  kwa  maumbile yako.

Fika  katika  duka  la  kuuza  dawa  za  aslili  la  NEEMA  HERBALIST.  Tunapatikana  UBUNGO  jijini  DAR  ES  SALAAM  jirani  na  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING  nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA.

Wasiliana  nasi  kwa  simu  namba  :    0693  005 189.


Share:

Jobs at Dar es Salaam Bus Rapid Transit (DART)

Overview Dar es Salaam bus rapid transit is a bus rapid transit system that began operations on 10 May 2016 in Dar es Salaam, Tanzania.The transit system consists of 6 phases and the construction of the first phase began in April 2012 by the Austrian construction company Strabag International GmbH. Construction of the first phase was completed in… Read More »

The post Jobs at Dar es Salaam Bus Rapid Transit (DART) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Mfumo Wa Malipo Kwa Matokeo Kuimarisha Mioundimbinu Ya Maji Vijijini

Na Ismail Ngayonga-MAELEZO
SERIKALI katika kipindi cha mwaka wa fedha 2019/2020 imepanga kutumia Tsh. Bilioni 301 kwa ajili ya kukamilisha miradi ya maji vijijini inayoendelea kutekelezwa katika maeneo mbalimbali nchini, ambapo fedha za ndani ni Tsh. Bilioni 224.03 na fedha za nje ni Tsh. Bilioni 77.22.

Pamoja na juhudi hizo za Serikali sekta ya maji imekuwa inakabiliwa na changamoto ya upotevu wa maji kutokana na uchakavu wa miundombinu iliyojengwa miaka mingi iliyopita.

Katika kukabiliana na changamoto hizo, Serikali imeendelea na jitihada za uwekezaji katika ukarabati wa miundombinu chakavu maeneo mbalimbali ya mijini ikiwemo Mikoa ya Dar es Salaam, Arusha, Dodoma, Mwanza, Morogoro, Singida pamoja na ukarabati wa miradi ya kitaifa ya Makonde, Wanging’ombe, Maswa, Mugango Kiabakari na Chalinze.

Tanzania kupitia miradi ya maji vijijini imejenga zaidi ya vituo 80,000 vya maji ambavyo vimeunganishwa na mfumo wa maji ya bomba, ambapo baadhi ya vituo vimechakaa na kuhitaji matengenezo lakini ukosefu wa takwimu sahihi juu ya vituo hivyo kunaikwamisha Serikali kupanga bajeti ya kuwapatia wananchi wa vijijini huduma bora ya maji.

Takwimu zilizopo katika Ripoti ya Maendeleo ya Sekta ya Maji ya mwaka 2016, zinaonyesha kuwa kati ya mwaka 2010/11 na mwaka 2015/16, Serikali ilipanga kujenga jumla ya vituo vya maji 99,515 lakini ilishia kujenga vituo 42,718 pekee.

Ripoti hiyo iliyotolewa Oktoba mwaka 2016 inaeleza kuwa theluthi moja ya miradi hiyo ya maji haikutekelezwa ndani ya awamu ya kwanza ya Mpango wa Maendeleo ya Sekta ya Maji (WSDPI) jambo lililofanya baadhi ya vituo vya maji vichelewe kujengwa.

Ili kuboresha upatikanaji wa maji maeneo ya vijijini, Serikali kwa kushirikiana na Wadau wa Maendeleo imeendelea kuimarisha Programu ya Uendelevu wa Huduma ya Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini kwa kutumia Mfumo wa Malipo kwa Matokeo (Payment by Results – PbR) unaolenga kuongeza  kasi ya uendeshaji, matengenezo na ukarabati wa miundombinu ya miradi ya maji vijijini.

Kupitia Programu hiyo, Serikali imeanza kuziwezesha Halmashauri za Miji nchini kuviendeleza vituo vya maji vilivyopo na kutumia takwimu kujenga vingine vipya katika maeneo yenye uhitaji mkubwa wa maji.

Ili kufikia malengo ya Programu hiyo, mwaka 2017 wataalamu hao walitembelea vituo 9,0000 katika Halmashauri 56 nchini vijiji ili kujionea hali halisi ya utendaji wa vituo vya maji, ambapo ilibainika kutofautiana kwa taarifa za baadhi ya vituo zilizopo Wizara ya Maji na Umwagiliaji na eneo kilipo ikizingatiwa kuwa maeneo mengi ya vijijini hayana anuani na mitaa yenye mpangilio mzuri.

Akiwasilisha Hotuba ya Makadirio ya Bajeti ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2019/2020, Waziri wa Maji, Prof. Makame Mbarawa anasema katika jitihada za kuhakikisha miradi ya maji vijijini inakuwa endelevu, Serikali kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Uingereza (DFID) inatekeleza Mpango wa Mfumo wa Malipo kwa Matokeo (Payment by Results – PbR) ambao una lengo la kuimarisha uendelevu wa miradi ya maji vijijini.

Anasema kuwa hadi April 2019, awamu ya pili ya programu hiyo imekamilika ambapo Halmashauri 95 zilifuzu na kupewa Shilingi bilioni 8.55 kati ya Shilingi bilioni 53.6 zilizotengwa katika mwaka 2017/2018, ambapo awamu ya tatu inaendelea na inahusisha Halmashauri 181 ambazo zitapewa fedha kwa vigezo vya idadi ya vituo vilivyojengwa na kutoa maji.

‘Kupitia PbR, Paundi 300 hutolewa kwa kila kituo kilichohakikiwa na kinachofanya kazi na Paundi 1,500 hutolewa kwa kituo kipya kitakachojengwa, Katika mwaka 2018/2019, jumla ya Paundi milioni 10 zimetengwa kwa ajili ya kutekeleza programu hiyo kwenye Halmashauri zote nchini’’ alisema Waziri Mbarawa.

Aliongeza kuwa Hadi mwezi Aprili 2019, fedha zilizolipwa katika awamu ya tatu ni Paundi milioni 8.7 sawa na Shilingi bilioni 25.43. Katika mwaka 2019/2020, Shilingi bilioni 46.47 zimetengwa kwa ajili ya utekelezaji wa programu hiyo.

Maji ni rasilimali muhimu  kwa maisha ya binadamu na maendeleo ya jamii na sekta mbalimbali za kiuchumi zikiwemo viwanda, kilimo, uvuvi na utalii, ili kufikia azma ya Serikali ya kuwapatia wananchi majisafi na salama pamoja na kuiwezesha Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati kufikia mwaka 2025, Wizara inatekeleza mipango mbalimbali.

Ni wajibu wa wananchi na wadau wote kuhakikisha kunakuwepo na upatikanaji wa takwimu na taarifa za mwenendo wa rasilimali za maji ili kuimarisha usanifu wa miundombinu ya kusambaza maji nchini.


Share:

Viwanja Na Shamba Vinauzwa kwa Bei Nafuu.....Viko Sehemu Nzuri Sana

VIWANJA  NA SHAMBA SEHEMU NZURI SANA....... viwanja vipo km 2 kutoka Bagamoyo road jirani na Bunju 20/20 Tsh mil 5 , 20/30 Tsh mil 7, 20/40 Tsh mil 10, umeme ,maji vipo .......... 

Pia vipo  MAPINGA upande wa baharini  kwenye upepo mwanana km 2 tu kutoka baharini  bei 20/20 Tsh mil 3.6 , na  20/40 Tsh mil 7.2 pia Hekari 1 Tsh mil 25 ....maongezi  yapo !!

Namba yangu;  0677705808



Share:

Jeshi la Marekani latuma barua ya kuondoka Iraq .....Wizara ya Ulinzi Yaikana Barua hiyo

Waziri wa Ulinzi wa Marekani, Mark Esper amekanusha kwamba Ikulu ya Marekani ilikuwa inajiandaa kuyaondoa majeshi yake Iraq. 

Tangazo hilo limetolewa baada ya jenerali mwandamizi wa Marekani kumpa jenerali mwenzake wa Iraq barua inayosema kuwa vikosi vya Marekani vitaondoka Iraq katika siku na wiki zijazo. 

Mkuu wa kikosi cha Marekani nchini Iraq, Brigedia Jenerali William Seely alituma barua kwa kamandi ya operesheni ya pamoja nchini Iraq, nakala ambayo ilionekana na vyombo vya habari kadhaa ikiwemo shirika la habari la Ufaransa, AFP na Reuters. 

Barua hiyo ilisema kuwa vikosi vya muungano vinavyoongozwa na Marekani kupambana na kundi linalojiita Dola la Kiislamu, IS vitachukua hatua kuhakikisha harakati za kuondoka Iraq zinafanyika salama na kwa ufanisi. 

Lakini wizara ya ulinzi ya Marekani imekanusha kuwa inakusudia kuviondoa vikosi vyake Iraq. Esper amesema hakuna uamuzi wowote wa kuondoka Iraq.

Mkanganyiko huu umekuja mara baada ya jeshi la Marekani kumuua kamanda wa jeshi wa Iran Qasem Soleimani.

Jenerali Soleimani aliuawa katika mapambano ya anga huko Baghdad siku ya ijumaa baada ya rais Trump kuamuru wafanye hivyo.




Share:

Msanii Dudubaya Aitwa BASATA

Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) limemtaka msanii wa Bongo Fleva Tumaini Godfrey maarufu Dudubaya kufika katika ofisi za baraza hilo kesho Januari 7, kwa mahojiano zaidi baada ya kusambaa kipande cha video kikimuonesha akitoa kauli zisizokuwa na maadili.


Share:

Kesi Ya Kutekwa Mfanyabiashara Mohammed Dewji Yapigwa Kalenda hadi January 21

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam imepiga kalenda kesi ya kutekwa kwa mfanyabiashara Mohammed Dewji maarufu kama MO inayomkabili dereva wa taksi Mousa Twaleb na wenzake wanne ambao bado hawajakamatwa na kufikishwa mahakamani hapo.

Kesi hiyo ilitajwa jana mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Rashid Chaungu baada ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi, aliyepangiwa kusikiliza kesi hiyo kwenda likizo.

Wakili wa Serikali, Faraji Nguka, alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika, hivyo aliiomba mahakama kupanga tarehe nyingine ya kutajwa.

Hakimu Chaungu alisema kesi hiyo itatajwa Januari 21, mwaka huu na mshtakiwa ataendelea kukaa mahabusu.

Watuhumiwa wengine ambao upande wa mashtaka inawatafuta ni raia wanne wa Msumbiji na mmoja wa Afrika Kusini, wanaodaiwa kumteka bilionea huyo.


Share:

Naibu Waziri wa Afya Dkt. Ndugulile Ataka Taarifa Utoaji Wa Dawa Hospitali Ya Rufaa Iringa.

Na Mwandishi Wetu Iringa
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile amemuagiza Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Iringa Dkt. Atupele Mwandiga kuhakikisha anapata taarifa ya utoaji wa dawa katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Iringa.

Agizo hilo limekuja mara baada ya ziara ya yake mkoani humo alipotembelea hospitali hiyo kujionea utoaji wa huduma za afya kwa wananchi na kushuhudia mmoja wa mama aliyejifungua Hospitalini hapo kupewa dawa mara moja badala ya mara tatu kama iilivyoandikwa na Daktari.

Dkt. Ndugulile amesema kuwa amekasirishwa na utendaji kazi wa manesi katika wodi ya Mama na Mtoto kwa kutozingatia utoaji huduma hasa kuhakikisha wazazi na watoto wanapewa dawa kwa wakati zinazotakiwa na kwa idadi sahihi.

Ameongeza kuwa lengo la mgonjwa kupewa huduma ni kuhakikisha anapona na sio kufanya aendelee kupata tabu na shida hivyo Serikali ya Awamu ya Tano imewekeza fedha nyingi katika kuhakikisha Sekta ya Afya inaboreshwa nchini.

"Haiwezekani mgonjwa kanunua dawa zake kwa fedha zake lakini bado hata hamzingatii kumpatia dawa mnategemea ataponaje” alisema Dkt. Ndugulile.

Aidha Dkt. Ndugulile ameutaka uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa kuhakikisha wanaratibu utoaji wa huduma hospitalini hapo ili kuepukana na malalamiko ya wagonjwa na kupoteza imani ya wananchi kwa Hospitali hiyo.

"Tukiendelea hivi tutaondoa imani kwa wananchi wetu katika utoaji wa huduma za afya sisi tunatakiwa kutoa huduma kwa wananchi na sio kuwapa kero wananchi" alisema Dkt. Ndugulile.

Kwa upande wake Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Iringa Dkt. Atupele Mwandiga amemuahikikishia Naibu Waziri Dkt. Ndugulile kusimamia utoaji huduma katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa na kusimamia vilivyo ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma inayostahili.

Ameongeza kuwa Serikali ya Awamu ya tano imetoa kiasi cha Billioni 7 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali za Wilaya na maboresho katika Zahanati na vituo vya Afya mkoani humo katika kuhakikisha inaboresha Sekta ya Afya hivyo watasimamia Sekta hiyo kikamilifu.

"Mhe. Naibu Waziri tutahakikisha hatutopoteza imani ya wananchi katika utoaji huduma za afya na tutatendea haki rasimali fedha tulizopewa na Serikali katika kuboresha Sekta ya Afya Mkoani kwetu" alisema Dkt. Atupele

Wakati huo huo Dkt. Ndugulile ametembelea na kujionea utendaji kazi utoaji wa huduma kwa wananchi katika Ofisi ya Bima ya Afya (NHIF), Kampeni ya masuala ya Lishe, Kiwanda cha Ruaha Milling na ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kilolo.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile yuko katika ziara ya siku mbili mkoani Iringa kukuagua shughuli za Afya na Maendeleo ya Jamii mkoani humo.


Share:

Mazungumzo kati ya DPP na Kigogo TAKUKURU Yakwama

Aliyekuwa Mkurugenzi wa Mipango, Ufuatiliaji na Tathimini wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) nchini Tanzania, Kulthum Mansoor amedai wameshindwa kufikia muafaka wa makubaliano baina yake na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).

Wakili wa utetezi Elia Mwingira, alitoa madai hayo jana kwamba awali walimwandikia DPP barua ya kuomba kukiri makosa yanayomkabili mshtakiwa, lakini mazungumzo yamevunjika.

Alitoa madai hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Godfrey Isaya.

Awali, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon, alidai kuwa kesi hiyo ilipangwa kwa ajili ya kutajwa na kwamba upelelezi wake bado haujakamilika.

Wakili wa utetezi Mwingira, alidai kuwa kwa kuwa mazungumzo na DPP yamevunjika upande wa Jamhuri uharakishe upelelezi.

Wakili Wankyo alidai wataelekeza wapelelezi kuhakikisha wanakamilisha upelelezi katika maeneo yaliyobaki.

Hakimu Isaya alisema mshtakiwa ataendelea kukaa mahabusu na kesi hiyo itatajwa Januari 20, mwaka huu.

Mansoor anakabiliwa na mashtaka manane ya kughushi, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kutakatisha Sh. bilioni 1.477.


Share:

Mhasibu wa Wizara ya Afya Kortini Kwa Mashitaka 280

Mhasibu wa Wizara ya Afya, Luis Lyimo (54) na Mtendaji Mkuu wa taasisi ya Christian Social Services Commission, Peter Maduki (61) wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam wakikabiliwa na mashtaka 280 yakiwemo 150 ya kughushi na moja la kutakatisha fedha.

Mawakili wa Serikali , Zakaria Ndaskoi na Genes Tesha wamewasomea mashtaka washtakiwa hao jana  Jumatatu Januari 6, 2020 huku wakipokezana mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Augustina Mmbando.
 
Wakili Ndaskoi amedai washtakiwa hao walitenda makosa hayo kati ya mwaka 2017 na mwaka 2019 ndani ya Jiji la Dar es Salaam

Alidai washtakiwa hao kwa nafasi zao wakiwa na nia ovu walighushi hundi mbalimbali zenye thamani ya mamilioni ya fedha na kusaini kwa jina la Upendo Mwingira bila ridhaa yake huku wakijaribu kuonyesha mshtakiwa, Luis Lymo alikuwa akilipwa na taasisi ya Christian Social Services Commission Fedha hizo kama kamisheni wakati si kweli.

Katika mashtaka ya kuwasilisha nyaraka za uongo washtakiwa hao wanadaiwa kuwasilisha nyaraka mbalimbali walizozighushi katika benki ya Standard Chartered.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo, washtakiwa hao hawakuruhusiwa kuongeza chochote kwa sababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikilizwa kesi ya uhujumu uchumi.

Upande wa mashtaka ulidai upelelezi bado haujakamilika, washtakiwa walipelekwa rumande na kesi imeahirishwa mpaka Januari 20 2020


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumanne January 7





















Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger