Tuesday, 14 May 2019

WHATSAPP SIYO SALAMA...WADUKUZI WAMEFANYA YAO

Wadukuzi wanaweza kuweka programu ya Sofware ya kuchunguza taarifa kwenye simu yako na vifaa vingine vinavyotumiwa kwa kutuma ujumbe wa WhatsApp, imethibitishwa.

WhatsApp, ambayo inamilikiwa kampuni ya Facebook, inasema wanaodukua walilenga "namna walizochagua " za watumiajina waliongozwa na "watumiaji wakuu wa mtandao ".

Udukuzi huo ulibainika siku ya Ijumaa.

Jumatatu WhatsApp iliwaomba watumia bilioni 1.5 wa mtandao huo kufungua upya app zao kama njia zaidi ya kuepuka udukuzi.

Shambulio hilo dhidi ya WhatsApp, lililogunduliwa mapema mwezi huu ,lilikuwa ni la kwanza kuwahi kuripotiwa katika gazeti la Financial Times.

Unawahusisha wadukuzi wanaotumia sauti ya WhatsApp kuzipigia simu wanazozilenga. Hata kama simu hizo hazitapokelewa tayari programu ya udukuzi huwa imewekwa ndani ya simu inayolengwa na mara moja ujumbe wa kumuonyesha mwenye simu kuwa aliitwa na simu fulani hutoweka mara moja kwenye orodha ya simu zilizokuita.

BBC inafahamu kuwa kikosi cha usalama wa WhatsApp kilikuwa cha kwanza kubaini udukuzi huo, na kushirikisha taarifa hiyo makundi ya kutetea haki za binadamu , makampuni kadhaa ya usalama na wizara ta sheria ya marekani mapema mwezi huu.

"Wadukuzi wana kampuni ya kibinafsi ambayo inaripotiwa kufanya kazi na serikali ambazo huwapatia mfumo wa udukuzi ambao huchukua udhibiti wa mfumo mzima wa simu ," ilisema kampuni Jumatatu katika mazungumzo na waandishi wa habariUvamizi huo wa mtandao wa WhatsApp ulibuniwa na kampuni ya usalama ya Israeli inayofahamika kama NSO Group

Imeripotiwa kuwa uvamizi huo wa mtandao wa WhatsApp ulibuniwa na kampuni ya usalama ya Israeli inayofahamika kama NSO Group, kampuni ambayo awali ilielezewa kama "cyber arms dealer".

Programu yake kuu ya software, Pegasus, ina uwezo wa kukusanya taarifa za siri kutoka kwa mlengwa, ikiwemo kuchukua data kwa kutumia kipaza sauti(microphone) na kamera na kukusanya taarifa za mahali alipo mtumiaji wa simu.

Katika taarifa yake kundi hilo lilisema kuwa : "NSO's technology ina kibali cha utendaji wake na imeidhinishwa na wakala wa serikali kwa malengo ya kukabiliana na uhalifu pamoja na ugaidi.

"Kampuni haitumii mfumo wenyewe, baada ya kupewa kibali na kuchunguzwa, ujasusi na watekelezaji wa sheria huamua namna ya kutumia teknolojia kusaidia kazi yao ya kuhakikisha kunakuwa na usalama wa umma. Huwa tunachunguza madai yoyote ya kuaminika ya matumizi mabaya ya data na ikiwezekana tunachukua hatua, ikiwemo kuzima kabisa mfumo.

" Hakuna namna yoyote NSO inaweza kuhusika katika utendaji au kutambua walengwa wa teknolojia yake , ambayo hutumiwa na ujasusi na wakala wa utekelezaji wa sheria. NSO isingeweza au haiwezi kutumia teknolojia yake tkwa haki zake kumlenga mtu yeyote au kampuni , wakiwemo watu binafsi ."
WhatsApp imesema ni mapema kujua ni watumiaji wangapi wameathiriwa na udukuzi huo, ingawa washukiwa wengi walilengwa kwa kiwango kikubwa.

Kwa mujibu wa takwimu za hivi karibuni za Facebook , WhatsApp inajumla ya watumiaji bilioni 1.5 kote duniani.
Chanzo - BBC
Share:

NAIBU WAZIRI IKUPA AIPIGA JEKI UWT DODOMA MIFUKO 30 YA SARUJI

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia watu wenye ulemavu Mhe.Stella Ikupa akisalimiana na Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya UWT Mkoa wa Dodoma Rehema Mwendamaka alipowasili katika ofisi za chama kukabidhi Saruji Mifuko 30 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha watoto.
Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Dodoma Neema Majule akisalimiana na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia watu wenye ulemavu Mhe.Stella Ikupa alipowasili katika ofisi za chama kukabidhi Saruji Mifuko 30 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha watoto.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia watu wenye ulemavu Mhe.Stella Ikupa akisaini kitabu cha wageni katika ofisi ya chama cha CCM mkoa wa Dodoma alipowasili kutoa mchango wake wa saruji mifuko 30 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha watoto kushoto kwake ni Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Dodoma Neema Majule.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia watu wenye ulemavu Mhe.Stella Ikupa akikabidhi Mifuko 30 ya Saruji kwa UWT Mkoa wa Dodoma wa kwanza kulia ni Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya UWT Rehema Mwendamaka (katikati) mwenye T.shirt nyeupe ni Kaimu katibu wa UWT Diana Madukwa na mwingine ni Mwenyekiti wa UWT Neema Majule wakipokea mifuko hiyo.
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya UWT Mkoa wa Dodoma,Rehema Mwendamaka akimpongeza kwa moyo wa dhati Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia watu wenye ulemavu Mhe.Stella Ikupa mara baada ya kuwakabidhi Mifuko 30 ya Saruji kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha watoto.
Kaimu katibu wa UWT Mkoa wa Dodoma,Diana Madukwa akimshukuru Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia watu wenye ulemavu Mhe.Stella Ikupa mara baada ya kuwakabidhi Mifuko 30 ya Saruji kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha watoto.
Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Dodoma,Neema Majule akimpongeza na kumshukuru kwa Moyo wa dhati aliouonesha Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia watu wenye ulemavu Mhe.Stella Ikupa mara baada ya kuwakabidhi Mifuko 30 ya Saruji kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha watoto.
Mwenyekiti wa  UWT Mkoa wa Dodoma,Neema Majule akimsisitiza jambo Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia watu wenye ulemavu Mhe.Stella Ikupa mara baada ya kuwakabidhi Mifuko 30 ya Saruji kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha watoto.

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia watu wenye ulemavu Mhe.Stella Ikupa akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa UWT Mkoa wa Dodoma mara baada ya kuwakabidhi Mifuko 30 ya Saruji kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha watoto.
Sehemu ya ujenzi wa kituo cha watoto kinachojengwa ambapo Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia watu wenye ulemavu Mhe.Stella Ikupa amekabidhi mifuko 30 ya saruji.
Mwenyekiti wa a UWT Mkoa wa Dodoma,Neema Majule pamoja na baadhi ya viongozi wakiagana na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia watu wenye ulemavu Mhe.Stella Ikupa mara baada ya kuwakabidhi Mifuko 30 ya Saruji kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha watoto.

Picha na Alex Sonna-Fullshangwe blog,Dodoma

NAIBU Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia watu wenye ulemavu Mhe.Stella Ikupa ametoa mifuko ya Saruji 30 kwa Umoja wa Wanawake Tanzania mkoa wa Dodoma (UWT) ikiwa ni katika kuunga mkono jitihada zinazofanywa na jumuiya hiyo za kujenga kituo cha kulelea watoto jijini hapa.

Akizungumza na waandishi wa habari jana baada ya kukabidhi saruji hiyo Naibu Waziri huyo amesema kuwa anaupongeza uongozi wa UWT Mkoa w Dodoma kwa ubunifu mkubwa ambao wameendelea kuufanya ikiwemo wa kujenga kituo cha kulelea watoto ambacho sasa ni mardi ambao utakuwa mkubwa sana.

“Nampongeza sana Mwenyekiti pamoja na wale ambao anaambatana nao ,hivyo kutokanana na mradi huu naamini wataondokana na utegemezi”alisisitiza Mhe.Ikupa

Aidha amesema kuwa Saruji hiyo itawasaidia kuwasogeza ,lakini pia amewaomba wadau mbalimbali waweze kujitokeza kusaidia kwani bado UWT wanahitaji vifaa mbalimbli vya ujenzi kama vile Mabati,Mbao ,na vifaa vingine.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa UWT mkoa wa Dodoma Neema Majule alisema kuwa wanamshukuru Waziri Ikupa kwa kuwa na moyo wa kipekee kwa kuwaletea mifuko ya sumenti 30 kwaajili ya kukamilisha ujenzi wa madarasa 3.

“Kiukweli ametushangaza sana wanawake wa Dodoma kwa upendo wake wa dhati maana sikila mtu aliyenacho anatoa,hivyo mimi na mjumbe wangu wa kamati ya utekelezaji, bado tunaendelea kuwaomba wale wote wenye mapenzi mema na uwt waweze kujitokeza kuchangai kwani bado tunahitaji,Mabati,Malumalu,Madirisha na milango ili ujenzi uweze kukamilika”amesema Majule.

Hata hivyo Mwenyekiti huyo alisema kuwa Mradi huo ni wa ccm mkoa lakini utasaidia wilaya zote saba zilizopo Dodoma. “Na lengo letu mara baada ya mradi huu kuanza ambao utakuwa na thamani ya shilingi mil.200,utaweza kabisa kufanya UWT DODOMA kuwa endelevu na utasaidia kuweza kuweka miradi mingine kila wilaya ili wanawake waweze kupata vitega uchumi kila wilaya kwa kujitegemea.

Share:

MENEJA WA WAKALA WA VIPIMO (WMA) ILALA WAKAGUA MIZANI ZA KUPIMIA VYAKULA SOKO LA KISUTU


Bw. Costantine Clement Afisa Vipimo Wakala wa Vipimo (WMA)Mkoa wa Ilala akihakiki mizani ya kupimia vyakula katika soko la Kisutu jijini Dar es salaam leo, kulia kwake ni Meneja wa Wakala wa Vipimo (WMA) Mkoa wa Ilala Bw. Evarist Masengo.

.............................................................................

Meneja wa Wakala wa Vipimo (WMA) Mkoa wa Ilala Bw. Evarist Masengo na maofisa wa WMA  wamefanya ukaguzi wa mizani za kupimia vyakula katika soko la vyakula Kisutu leo ili kujiridhisha kama walaji wanapata huduma zinazostahili wakati wanapofanya manunuzi kwa wafanyabiashara wa soko hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari katika soko hilo Bw.Evarist Masengo amesema ni kawaida ya Wakala wa Vipimo (WMA) kufanya ukaguzi mara kwa mara katika masoko, vituo vya mafuta, taasisi na maeneo mbalimbali ambayo Taasisi hiyo imekuwa ikisimamia katika masuala ya vipimo kwa ujumla.

Ameongeza kwamba Soko la Kisutu ni soko ambalo wafanyabiashara wake wamekuwa wakizingatia masuala ya vipimo kwa kiwango kikubwa hivyo kuwafanya wanunuzi au walaji wa bidhaa zao kupata huduma za manunuzi zenye ubora wa vipimo uliozingatiwa.

Amesema mnunuzi yeyote anayenunua bidhaa lazima awe makini kuangalia mizani kama imekaguliwa kwa sababu wao wanapokagua mizani wanaweka alama ya stika ya Wakala wa Vipimo (WMA) inayoonesha mwaka na tarehe ambayo mizani huo ulikaguliwa ili kumtambulisha mnunuzi kwamba huduma anayopata kutoka kwa mfanyabiashara imekidhi viwango.

Amewaasa wafanyabiashara kuhakikisha mizani zao zinakaguliwa na kuwekewa stika ya Wakala wa Vipimo (WMA) ili kutoa huduma iliyohakikiwa na itakayompa mlaji mahitaji yake kwa ubora.

Maofisa wa Wakala wa Vipimo (WMA) wanafanyika ukaguzi katika maeneo mbalimbali jijini Dar es salaam na maeneo mengine ikiwa ni maandalizi ya maadhimisho ya siku ya vipimo duniani yanayotarajiwa kufanyika Mei 20/ 2019 jijini Dar es salaam.
Meneja wa Wakala wa Vipimo (WMA) Mkoa wa Ilala Bw. Evarist Masengo (kulia) na Bw. Costantine Clement Afisa Vipimo Wakala wa Vipimo (WMA)Mkoa wa Ilala wa pili kutoka (kulia) wakihakiki mizani ya kupimia vyakula katika soko la Kisutu jijini Dar es salaam leo.
Meneja wa Wakala wa Vipimo (WMA) Mkoa wa Ilala Bw. Evarist Masengo akifafanua jambo kwa mwandishi wa habari wa TBC Stanley Ganzel wakati akigfafanua mambo mbalimbali katika soko la vyakula la kisutu katikati ni Bw. Costantine Clement Afisa Vipimo Wakala wa Vipimo (WMA)Mkoa wa Ilala.
Baadhi ya vyakula , mbogamboga na matunda vinavyopatikana katika soko la Kisutu jijini Dar es salaam.
Bi Mary Lazaro Mfanyabiashara wa matunda katika soko la Kisutu akihojiwa na waandishi wa habari katika soko hilo.
Afisa Vipimo Wakala wa Vipimo (WMA) Mkoa wa Ilala Bw.Malaki Nyangasi akimsikiliza Irene John Meneja Mawasiliano na Uhusiano wa Umma Wakala wa Vipimo (WMA) wakati alipokuwa akimueleza jambo.
Afisa Vipimo Wakala wa Vipimo (WMA) Mkoa wa Ilala Bw.Malaki Nyangasi akihakiki mzani mkubwa katika soko la Kisutu kulia ni Meneja wa Wakala wa Vipimo (WMA) Mkoa wa Ilala Bw. Evarist Masengo.
Meneja wa Wakala wa Vipimo (WMA) Mkoa wa Ilala Bw. Evarist Masengo wa pili kutoka kulia akiwa na maafisa wenzake kulia ni Contantine Clement Afisa Vipimo (WMA) mkoa wa Ilala kutoka kushoto ni Afisa Vipimo Wakala wa Vipimo (WMA) Mkoa wa Ilala Bw.Malaki Nyangasi na Irene John Meneja Mawasiliano na Uhusiano wa Umma Wakala wa Vipimo (WMA).
Afisa Vipimo Wakala wa Vipimo (WMA) Mkoa wa Ilala Bw. Malaki Nyangasi akihakiki mzani mkubwa wakati maofisa wa 
MAOFISA WA WAKALA WA VIPIMO (WMA) WAFANYA UKAGUZI WA MIZANI KATIKA SOKO LA KISUTU LEO
Wakala wa Vipimo (WMA) walipokagua mizani katika soko la vyakula la Kisutu leo.
Afisa Vipimo Wakala wa Vipimo (WMA) Mkoa wa Ilala Bw.Malaki Nyangasi akifafanua jambo kwa waandishi wa habari.
Makamu Mwenyekiti wa Soko la Kisutu Bw. Laurent Magali akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya ukaguzi huo uliofanywa na Wakala wa Vipimo (WMA) katika soko hilo katikati ni Afisa Vipimo Wakala wa Vipimo (WMA) Mkoa wa Ilala Bw.Malaki Nyangasi na kushoto ni Meneja wa Wakala wa Vipimo (WMA) Mkoa wa Ilala Bw. Evarist Masengo
Share:

WABUNGE WA BUNGE LA UGANDA WATEMBELEA BUNGE LA AFRIKA

Wabunge wa Bunge la Uganda wametembelea Bunge la Afrika ‘Pan - African Parliament’ katika makao yake makuu Jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini ili kujifunza namna bunge hilo linavyofanya kazi.

Ujumbe huo wa wabunge nane kutoka Uganda ukiongozwa na Mheshimiwa,Ongalo Obote Kenneth umepokelewa leo Jumanne Mei,14 2019 na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mheshimiwa Stephen Masele ambaye anatoka Tanzania,Kanda ya Mashariki ya Afrika.

Mhe. Kenneth alisema lengo la kufika katika Bunge la Afrika ambalo wabunge wake wanaendelea na Mkutano wa pili wa kawaida wa bunge la tano la tano ni kujifunza namna bunge hilo linavyofanya kazi.

“Tumefurahi kufika hapa kuona na kujifunza mambo kadha wa kadha kuhusu Bunge la Afrika, ikiwemo historia yake,muundo wake na namna wanavyoendesha shughuli zao na kuzungumzia masuala ya Afrika,kwa kweli bunge hili ni imara kupitia viongozi wake akiwemo,Mheshimiwa Masele ambaye ni kijana lakini ana uwezo mkubwa wa kuongoza taasisi hiyo kubwa Afrika”,alisema Mhe. Kenneth.

Kwa upande wake, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika, Mhe. Stephen Masele amewapongeza wabunge hao kwa kuona umuhimu wa kutembelea bunge hilo kujifunza kuhusu bunge na siasa za Afrika.

“Nimefurahi kupokea ujumbe wa wabunge wa bunge la Uganda wanaotoka katika kamati mbalimbali,mmejionea jinsi tunavyoendesha shughuli za bunge la Afrika,wamefahamu kuhusu historia ya bunge,historia ya Umoja wa Afrika (AU),ukombozi Afrika na mambo mengine”,alisema Mhe. Masele.

“Bunge la Afrika lina wabunge kutoka nchi mbalimbali barani Afrika,wenye tamaduni na lugha tofauti tofauti,ninaamini kwa siku zote mtakazokuwa hapa bungeni,mtafaidika vya kutosha kuhusu siasa za Afrika”,aliongeza Mhe. Masele.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mheshimiwa Stephen Masele akiwa ofisini kwake katika Makao Makuu ya Bunge la Afrika,Midrand,Johannesburg, Afrika Kusini akizungumza na Ujumbe wa wabunge kutoka Bunge la Uganda waliotembelea Bunge la Afrika leo Mei 14,2019. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog.
Kushoto ni Mhe. Masele akizungumza na Ujumbe wa wabunge kutoka Bunge la Uganda (kulia) waliotembelea Bunge la Afrika.
Wabunge wa Bunge la Uganda wakimsikiliza Mhe. Masele. 
Kiongozi wa Ujumbe huo wa wabunge kutoka Uganda Mhe. Ongalo Obote Kenneth akielezea lengo la ziara yao kutembelea Bunge la Afrika.
Picha ya pamoja,Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mheshimiwa Stephen Masele na wabunge wa bunge la Uganda.
Mbunge kutoka Uganda,Mhe. Mugoya Kyawa(kulia) akiteta jambo na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika,Mhe.Stephen Masele.
Picha zote na Kadama Malunde- Malunde1 blog
Share:

Omar al-Bashir Ashitakiwa Kwa Mauaji

Mwendesha mashtaka wa umma nchini Sudan amemshitaki rais aliyeondolewa madarakani Omar al-Bashir kwa makosa ya kuchochea na kuhusika na mauaji ya waandamanaji.

Mashtaka hayo yametokana na uchunguzi uliofanywa kuhusu kifo cha ddaktari aliyeuawa wakati wa maandamano yaliyosababisha kumalizika kwa utawala wake mwezi uliopita.

Hatma ya Bwana Bashir haijawa wazi. Aliripotiwa kutiwa nguvuni mara baada ya kupinduliwa.
 
Anakabiliwa pia na uchunguzi juu ya madai ya wizi wa pesa na kudhamini ugaidi

Mnamo mwezi Disemba, waandamanaji walianza maandamanano dhidi ya uamuzi wa serikali wa kupandisha mara tatu kwa bei ya mkate.

Maandamano hayo ghafla yalibadilika kuwa hasira iliyosambaa kote nchini dhidi ya kiongozi huyo ambaye alikuwa mamlakani kwa miaka 30, yakiongozwa na madaktari.

Maandamano yalifanyika kwa wiki tano na shahidi mmoja anasema tarehe 17 Januari, vikosi vya usalama viliwafyatulia risasi waandamanaji na kumuua daktari.

Baadaye waandamanaji waliamua kufanya maandamano yao kwa kuketi nje ya makao makuu ya kijeshi, na kudai jeshi limg'oe mamlakani rais.

Baraza la kijeshi lilichukua mamlaka ya nchi tarehe 11 Aprili, lakini waandamanaji wanasisitiza kwamba jeshi lazima likabidhi utawala wa nchi kwa raia.


Share:

Kesi ya wizi wa dhahabu Jijiini Mwanza yaanza kusikiliza ushahidi

Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mwanza imeamuru kuendelea kusikikiza ushahidi katika kesi ya Jinai namba 1 ya mwaka 2019 inayowakabili Askari Polisi wanane. Tazama hapo chini


Share:

Korea Kaskazini yataka irudishiwe meli yake iliyokamatwa na Marekani

Korea Kaskazini imetaka irudishiwe meli yake ya mizigo iliyokamatwa na Marekani wiki iliyopita kwa kukiuka vikwazo vya kimataifa ikisema "kitendo hicho kinakwenda kinyume na sheria na kinakera mno". 

Msemaji wa wizara ya mambo ya kigeni ya Korea Kaskazini ameikosoa hatua hiyo akisema inapingana moja kwa moja na dhamira ya tamko lililotiwa saini na kiongozi wake Kim Jong Un na Rais wa Marekani Donald Trump katika mkutano wao wa kilele wa kihistoria nchini Singapore mwezi juni. 

Siku ya Ijumaa Wizara ya sheria ya Marekani ilisema imeikamata meli ya mizigo ya Korea Kaskazini kwa jina MV Wise Honest, mwaka mmoja baada ya kushikiliwa nchini Indonesia ikisema ilihusika na shughuli haramu zinazokiuka vikwazo ilivyowekewa.

 Ilikuwa mara ya kwanza kwa meli ya Korea Kaskazini kukamatwa na Marekani kwa kukiuka vikwazo, baada ya miaka kadhaa ya mchezo wa paka na panya baharini ambapo meli za Korea zilijificha kwa kutumia bendera bandia na kuzima mitambo ya kuzifuatilia ili keupuka kugunduliwa.


Share:

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa.
 
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.
Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.
Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

Tiba ya Ngiri
Tiba yake ni kufanyiwa upasuaji , ama kutumia dawa za asili ili kupona kabisa tatizo hilo. Wasiliana Nami Kwa Ushauri zaidi wa Tatizo hili. Simu: 0714006521


Share:

Marekani, China Zaendelea Kukomoana

Marekani inatafakari kuongeza ushuru kwa bidhaa zaidi za China zitakazoingia nchini humo zenye thamani ya dola bilioni 300 zikiwemo za kompyuta hatua inayoongeza zaidi mzozo wa kibiashara unaotikisa masoko ya fedha na kuchochea hofu kuhusu ukuaji wa uchumi wa dunia.

Taarifa hii inafuatia tangazo la China hapo jana la kuongezeko ushuru kwa asilimia 25 katika bidhaa zinazoagizwa kutoka Marekani zenye thamani ya dola bilioni 60. 

Mwakilishi wa biashara wa Marekani ametangaza kwamba orodha hiyo mpya ya bidhaa 3,805 ni hatua ya kuelekea kutekelezwa kwa kitisho cha rais Donald Trump wa Marekani cha kuongeza kiwango kikubwa cha ushuru cha asilimia 25 kwa bidhaa zote za China zinazoingizwa Marekani. 

Bidhaa zinazoguswa kwenye orodha hiyo ni pamoja na kompyuta, misumeno, samaki aina ya tuna na vitunguu swaumu.


Share:

RAIS MAGUFULI AMTEUA MKAPA KUWA MKUU WA CHUO CHA DODOMA




Share:

SERIKALI YAIPA AZAM TV LESENI YA KUONYESHA CHANELI ZA NDANI BURE


Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Atashasta Nditiye amelieleza Bunge leo Jumanne Mei 14, 2019 kuwa kituo cha televisheni cha Azam jana Jumatatu kimepokea leseni ya kuonyesha chaneli za ndani bure na kwamba kampuni hiyo imeahidi kufunga mitambo yake nchi nzima kwa ajili ya kurusha matangazo hayo ndani ya kipindi cha miezi saba.

Nditiye ametoa kauli hiyo akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, aliyehoji ni kwa nini Azam wananyimwa haki ya kuonyesha channel za ndani bure.

"Je, Serikali haioni kuwanyima haki hiyo wakati wengine wamepewa ni kukiuka ibara ya 18 ya katiba ambayo inatoa haki ya kupata habari, lakini hata Rais wetu anatumia Azam kurusha matangazo yake hivyo tungejitangaza hadi nje," ameuliza Shangazi.

Katika swali la msingi, Mbunge wa Nyamagana (CCM), Stanslaus Mabula, aliuliza Serikali iwapo haioni kupitia  TCRA kuwafungia local channels (chanel za ndani)  baadhi ya ving'amuzi ikiwamo Azam TV, DSTV na vingine imewanyima wananchi fursa ya kupata habari.

Naibu waziri amesema Serikali inatambua umuhimu wa wananchi kujua mambo yanayoendelea, hivyo imetoa leseni zenye masharti tofauti.

Amesema kwa sasa matangazo ya umma yanarushwa na TBC1 na TBC3 maarufu safari channel.


Share:

ACT Wazalendo wapigilia msumari suala la Wakurugenzi kutumika na NEC

Chama cha ACT Wazalendo kimewapongeza Mwanaharakati Bob Chacha Wangwe, Wakili Fatma Karume na Wanaharakati wote ambao walishiriki katika kufungua kesi ya kupinga Wakurugenzi wa Halmashauri za Miji, Wilaya na Majiji kutumiwa na Tume ya Uchaguzi (NEC) kama wasimamizi wa uchaguzi mkuu.

Katibu Mwenezi wa ACT Wazalendo, Ado Shaibu amesema kuwa historia ya Tanzania itawakumbuka wanaharakati hao walioshiriki kwenye kesi hiyo kwa sababu itaacha alama ya kudumu kwenye historia ya mapambano ya haki, demokrasia na ustawi wa taifa.

"Ingawa ni utekelezaji wa kawaida wa majukumu yao na isingetazamiwa wasifiwe, ACT Wazalendo kinawapongeza majaji Mh. Jaji Dk. Atuganile Ngwala, Mh. Jaji Benhaj Masoud na Mh. Jaji Firmin Matogolo kwa kusimamia haki bila kuyumba kwenye shauri hili," amesema Ado.

Utakumbuka Mei 10 mwaka huu Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam, ilitoa uamuzi kuhusu Shauri la Kikatiba namba 17 la mwaka 2018 lililofunguliwa na Bob Chacha Wangwe kupinga baadhi ya vifungu vua Sheria ya Taifa ya Uchaguzi vinavyohusu Wasimamizi wa Uchaguzi kuwa vinakinzana na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 kama ilivyofanyiwa marekebisho.

 Shauri hilo lilifunguliwa dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Tume ya Taifa yaUchaguzi na Mkurugenzi wa Uchaguzi.

Hata hivyo, hapo jana Serikali imewasilisha notisi Mahakama ya Rufaa kupinga sehemu ya uamuzi wa Mahakama Kuu katika kesi ya Kikatiba iliyofunguliwa na Bob Chacha Wangwe dhidi Mwanasheria Mkuu wa Serikali na wenzake kupinga baadhi ya vifungu vya Sheria ya Taifa Uchaguzi kuhusu Wasimamizi wa Uchaguzi.


Share:

Kujichua Kwa Muda Mrefu Husababisha Maumbile ya Kiume Kusinyaa na Kupungukiwa Nguvu za Kiume

Wanaume  wengi  waliofanya  mchezo wa  kujichua  kwa  muda  mrefu hupatwa  na  madhara  ya kuwa  na  kusinyaa  na  kudumaa  kwa  maumbile  yao  ya  kiume  ambayo  huenda  pamoja  na  tatizo  a  Ukosefu au upungufu wa nguvu za kiume.

Tendo  la  kujichua  kwa  mwanaume  linapofanyika  kwa  kipindi  kirefu huathiri na  kuharibu mishipa  na  misuli  ya uume  na  hivyo  kusababisha  kujengeka  kwa mafuta na tishu zisizo vutika  kwenye  mishipa  ya  ateri.  Jambo  hili  husababisha  makuu mawili; 1. Huzuia  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  kuongezeka jambo  linalotajwa  na  wanasayansi  kama jambo  muhimu  sana  katika  kukua  kwa  uume. 2. Huzuika  kutirika  kwa  damu  kuingia  kwenye  misuli  ya  uume.

Mambo  hayo  mawili  huathiri  sana  ukuaji  wa  maumbile ya kiume  kwa  sababu  yanapo tokea huathiri uzalishaji  wa  homoni  muhimu  zinazo  husika  na  ukuaji  wa  misuli  ya  uume na matokeo  yake husababisha  uume  wa  mhusika  kudumaa, kusinyaa,kunywea  na  kurudi ndani  kiasi  cha  kuufanya  uonekane  kama uume  wa  mtoto.
 
Hii ndio  sababu  kwanini watu  wengi  walio athirika  na  punyeto  hulalamika  kwamba  maumbile  yao  ya  kiume  hayajaongezeka  tangu  walipo anza  kujihusisha  na  punyeto  wakiwa  na  umri mdogo. 

Maumbile  yao  huonekana  kama  ya  watoto  kwa  sababu hayakupata  nafasi  ya  kupokea  vichochea  vya  kuyafanya  yakue  na  kuongezeka  tangu  walipo  anza  kujihusisha  na  punyeto.

Suluhisho  La  Tatizo La Maumbile  Ya  Kiume  Yaliyo  Sinyaa  Kwa  Sababu  Ya  Punyeto.
Kama  bado  unaendelea  kujihusisha  na punyeto  basi  jitahidi  uache  tabia  hiyo  mara  moja  kwani  inakuharibu. Inaweza  isiwe  rahisi  sana  kuacha  mara  moja  lakini  ukiweka  nia  thabiti  basi  unaweza  kuacha  kabisa  kama  walivyofanikiwa  kuacha  wengine  ambao  walikuwa  wametopea  kwenye  tabia  hiyo  lakini  wakajitahidi  kujilazimisha  na  hatimaye  wakafanikiwa  kuachana  kabisa  na  tabia  hiyo.

==>> Acha kuangalia video chafu za ngono.
Video hizi ndio chanzo kikuu cha punyeto kwa watu wengi hua zinajenga picha nyingi kwenye ubongo na kila picha unayoiona utataka ukaipigie  punyeto hivyo kuacha kuziangalia tu ndio nafuu yako.. 


Weka mipango ya kuzuia kupiga punyeto wakati wa kuoga: bafuni ndio sehemu ambayo inatumika sana na watu wengi kupiga punyeto hivyo ni vizuri kua na mikakati ya kujizuia ukiwa huko kwa kuoga haraka na kuondoka, kuoga maji ya baridi ambayo mara nyingi hayatoi muhemko wa kupiga punyeto.

==>>Epuka kukaa nyumbani peke yako;
Mara nyingi kukaa peke yako kunakufanya ushawishike kufanya tendo hilo, hebu ondoka na ujichanganye na watu wengine au tafuta majirani wa kukaa na kuongelea mambo mengine. 


Fikiria kuhusu madhara yake: kila aliyewahi kupiga punyeto kuna madhara mabayo ameshayapata kama vile misuli ya uume kulegea, kushindwa kurudia tendo uwapo na mwenzi wako, kuishiwa nguvu za kiume, maumbile kusinyaa, kurudi ndani na kuwa kama ya mtoto mdogo.

Acha kusema eti hii punyeto ni ya mwisho: siku zote wapiga punyeto wana akili moja ya kufikiria eti sasa leo napiga afu sirudii tena. Hicho kitu hakipo, kwani kesho yake utasema hivyohivo, kama unaacha acha mara moja ili utunze heshima yako mbele ya mwenzi au mke wako.

Kama utaona  kuna  ugumu  wa  kuacha  tabia  hiyo  na tayari ushaapata madhara ya maumbile kusinyaa na kupungiwa nguvu za kiume, basi  wasiliana nasi kwa ushauri zaidi; Simu  0715741788 au 0754741788


Share:

Mkuu Wa Jeshi La Polisi Nchini, IGP Simon Sirro, Amefanya Mabadiliko Madogo Kwa Makamanda Wa Jeshi La Polisi




Share:

Kituo Kikubwa Cha Biashara Cha Afrika Mashariki Kujengwa Nyakanazi- Kagera

Na. Peter Haule na Josephine Majura, WFM, Dodoma
Serikali inatekeleza mpango mkakati wa kujenga Kituo kikumbwa cha Biashara cha Afrika Mashariki katika eneo la Nyakanazi Mkoani Kagera ili kuwanufaisha wananchi wanozunguka eneo hilo na nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki- EAC.

Hayo yameelezwa Bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalaum Mhe. Halima Abdalallah Bulembo, alieuliza kuhusu mpango wa Serikali wa kujenga Kituo cha Biashara katika mkoa wa Kagera unaopakana na nchi nyingi za EAC.

Dkt. Kijaji alisema kuwa, ujenzi wa Kituo cha Biashara eneo la Nyakanazi utawezesha wananchi wa Tanzania pamoja na nchi za Rwanda, Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Uganda kulifikia soko hilo.

Akijibu swali la Msingi la Mbunge huyo kuhusu mpango wa Serikali wa kuifanya Kagera ifaidike na uchumi wa kijiografia, Dkt. Kijaji alisema kuwa, Serikali inatekeleza miradi mbalimbali ya kimkakati mkoani humo ukiwemo mradi wa Reli yenye kiwango cha Kimataifa (SGR) kipande cha Isaka- Rusumo chenye urefu wa kilometa 371 na ukarabati wa barabara ya Lusanga- Rusumo yenye urefu wa kilometa 91.

Aidha inatekeleza mradi wa umeme wa megawati 80 katika mipaka ya Rusumo na Mtukula kwa ajili ya kuimarisha shughuli za kibiashara na nchi jirani za Rwanda na Uganda.

Naibu Waziri Dkt. Kijaji alisema, mazao ya wakulima wa Kagera na bidhaa za baadhi ya viwanda vya kusindika mazao ya kilimo, mifugo, uvuvi na misitu vinafaidika kimasoko na jiografia ya Mkoa huo ikiwa ni pamoja na kiwanda cha kusindika minofu ya Samaki cha Fish Co Ltd na Supreme Perch Ltd.

Viwanda vingine ni Ambiance Distillers Tanzania Ltd kinachozalisha vinywaji vikali, Bunena Development Co. Ltd, NK Botling Co. Ltd na Kabanga Bottlers Co. Ltd vinavyozalisha maji ya kunywa na kiwanda cha Mayawa kinachosindika wine ya Rosella na juisi.

Alisema kuwa, sambamba na utekelezaji wa miradi ya kimkakati, Serikali kupitia Mamlaka ya Biashara (Tan Trade), ilitoa mafunzo ya kuhamasisha kuanzishwa kwa vikundi vya kurasimisha biashara mipakani katika vituo vya Kabanga, Rusumo na Mtukula vinavyopakana na nchi za Burundi, Rwanda na Uganda ili kuwajengea wananchi uwezo wa kutumia fursa za kiuchumi.

Mwisho.


Share:

Mvua yaua watoto wawili Dar, yaharibu miundombinu na kuzua kero kwa wananchi

Watoto wawili wamepoteza maisha kutokana na athari za mvua kubwa za masika zinazoendelea kunyesha katika jiji la Dar es Salaam.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa, alisema tukio la kwanza lilitokea Mei 8, mwaka huu, saa 9:00 alasiri maeneo ya Goba wilayani Kinondoni.

Alimtaja mtoto aliyefariki dunia ni Francis Byabato (6), baada ya kutumbukia kwenye kisima cha futi 30 kilichokuwa wazi nyumbani kwao.

Alieleza kuwa mtoto huyo alitoweka kwa siku mbili na baadaye alikutwa ndani ya kisima hicho akiwa ameshafariki dunia.

Kamanda Mambosasa alisema mtoto mwingine ambaye anakadiriwa kuwa na umri wa miaka (4-5), alifariki dunia Mei 12, mwaka huu maeneo ya Mongo la Ndege.

Alisema mwili wa mtoto huyo ulikutwa ukielea katika Mto Msimbazi ukiwa hauna jeraha lolote na umehifadhiwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Kadhalika, alisema, mvua hizo zinazoendelea kunyesha zimesababisha uharibifu wa baadhi ya majengo ya Shule ya Msingi Mwale iliyopo Kiwalani, Majani ya Chai Kiwalani na Shule ya Sekondari Kibasila iliyopo Manispaa ya Temeke ambayo imejaa maji na kusababisha kushindwa kuendelea na masomo.

Kamanda Mambosasa alitaja madhara mengine ni kufungwa kwa baadhi ya barabara za jiji hilo ikiwamo barabara ya Morogoro katika eneo la Jangwani.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger