Saturday, 11 May 2019

Kutana na Sheikh Omary Mwenye Uwezo wakufanya Dua mbalimbali za Matatizo Yako Na Kutafsiri Ndoto kwa kutumia Vitabu vya QUR-AN

Sheikh Omary Ni bigwa wa kutatua matatizo kwa haraka ni mtu aliye jaliwa KUBULI SHUFAA pia anatoa DUAH   za RUHIA. Ukija na Maradhi yanaondoka hapo hapo bila kungoja kesho, Kama una Majini wa Kichawi pia yanaondoka UKIPEWA MKONO  na Sheikh Omary .
 
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
 
Sheikh Omary  ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOA SHUHUDA WALIVYOSAIDIWA(Rudisha Mahusiano yako Ndani ya Saa 6 tu)
 
Sheikh Omary ni Mtaalamu wa Nyota za Binadamu na ANATIBU KWA KUTUMIA QUR AN. Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
 
Je una NUKSI  zisizo kwisha.!? JE umekimbiwa na Mume/Mke na Anaishi na Mtu Mwingine..!?
 
Hupati kazi kwa mda mrefu na vyeti unavyo
Una kosa bahati ya wanaume au mume wa kukuoa
Unataka nyota ing'ae ukiongea usikilizwe Ipo TARASIMU kwa Ajili yako...
 
Jini mahaba. Kama Unakasirika ovyo ukiwa na bwana au mwanamke wako na  kumchukia Mpaka  kushindwa kufanya nae tendo la ndoa. Kama umezulumiwa Mali irudi ikiwa haija pita Mwezi .
 
Njoo umuone Sheikh Omary  na ujuwe  yanayo kusibu ni mtu mkarimu mpenda watu,Anahudumia  MASKINI  na TAJIRI, NJOO ATAKUSAIDIA.. Sheikh Omary 0673531992 WhatsApp/Call


Share:

VIDEO: Enock Bella - Walifuata Jina

VIDEO: Enock Bella - Walifuata Jina

Share:

JWTZ Yatoa Onyo Kwa Wananchi Wanavamia Maeneo Ya Jeshi

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limewataka wananchi kuacha mara moja kuvamia na kuingilia maeneo ya Jeshi ambapo tayari kuna Oparesheni iliyoanza ya kuwaondoa watu katika maeneo yao.

Akizungumza na waandishi wa habari, Kaimu Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa  JWTZ, Luteni Kanali Gaudentius Ilonda amesema kama wananchi wanataka kununua maeneo karibu na Jeshi basi wafanye tathimini ya kuuliza kwa Jeshi kabla ya kununua ili kuepusha migogoro.

Pia amesema maeneo hayo yanaonekana ni ya wazi ama misitu yameachwa kwa malengo maalumu kwani mchana yanaonekana ni Msitu lakini usiku ndio Hoteli za Jeshi kwa sababu wanafanya warsha na makongamano misituni.


Share:

Madiwani Makambako wakosa Imani na Mkurugenzi

Na Amiri kilagalila-Njombe
Madiwani wa halmashauri ya mji wa Makambako mkoani Njombe wamekiri kuto kuwa na imani na mkurugenzi wa halmashauri ya mji huo kwa madai ya kwamba ameshindwa kusimamia  baadhi ya miradi ya maendeleo tangu afike katika halmashauri hiyo na kusababisha miradi mingi kushindwa kukamilika licha ya kutengewa fedha.

Wamesema kudorora kwa miradi mingi ya maendeleo ukiwemo wa maji , hospitali ya wilaya, kituo cha afya Lyamkena na stendi ya maroli kumesababishwa na utendaji mbovu wa msimamizi mkuu wa halmashauri kwa kuwa amekuwa akikaimisha mara kwa mara ofisi yake.

Devid Tweve,Lucy Mbogela na Iman Fute ni baadhi ya madiwani wakizungumzia suala hiyo wamesema mkurugenzi anadororesha maendeleo ya halmashauri hiyo na kwamba hatua za haraka zinatakiwa

“Leo hii ni miezi kumi lakini bado miradi haijakamilika,haya kuna jengo la halmashauri pale tangia mwaka 2014 tumeanza kulijenga pale mwenge ulipita lakini mpaka sasa hakuna kinachoendelea na pesa zipo tatizo ni nini kwa hiyo sisi tunachojua ni usimamizi mbovu na sisi hatupendi kukaa kwenye nyumba za kupanga,niseme kwamba kwa mkurugenzi wangu huyu ninampenda sana lakini  kufanya naye kazi ni shida”alisema Lucy Mbogela na Devid tweve

Akitoa utetezi wake mkurugenzi wa halmashauri hiyo Paul Malala amesema kusuasua kwa miradi hiyo ukiwemo mradi wa hospitali ya wilaya pamoja na jengo la ofisi za halmashauri kunasababishwa na wakandarasi pamoja taratibu za manunuzi na ulipaji wa serikali.

Kufuatia mgongano huo mwenyekiti wa halmashauri hiyo Hanana Mfikwa anatoa msimamo wa halmashauri kuhusu mapendekezo ya baraza kwa kutoa muongozo uliotolewa na waziri mkuu juu ya kuwachukulia hatua viongozi wakuteuliwa.

“Waraka unasema halmashauri inapaswa kuelewa kuwa haina mamlaka za kuchukua hatua za kinidhamu dhidi ya mkurugenzi wala kumkataa,badala yake zinaweza kujadili utendaji na mwenendo wa mkurugenzi na kuishauri mamlaka yake ya nidhamu ya ajira ambaye ni waziri mwenye dhamana wa serikali za mitaa au katibu mkuu kiongozi kupitia ofisi ya mkuu wa mkoa kwa hatua zake”alisema Hanana Mfikwa


Share:

Kutana na shariff Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Adam shariff Mwenye Uwezo wakufanya Dua mbalimbali Na Kutafsiri Ndoto

Kutana  na shariff Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Adam shariff  Mwenye UWEZO wakufanya dua mbali mbali  Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?

Wasilina na Adam shariff Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO   Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? . Adam shariff Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN  . Anatafsiri Ndoto. , KUSAFISHA NYOTA. Mvuto wa Mwili na Biashara.


Mawasiliano: (+255 )715971688 au (+255  )756914036



Share:

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa.
 
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.
Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.
Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

Tiba ya Ngiri
Tiba yake ni kufanyiwa upasuaji , ama kutumia dawa za asili ili kupona kabisa tatizo hilo. Wasiliana Nami Kwa Ushauri zaidi wa Tatizo hili. Simu: 0714006521


Share:

Maambukizi ya Fangasi katika Sehemu za Siri

Kati ya maambukizi yanayowasumbua wanawake wengi duniani ni maambukizi ya fangasi. Inakisiwa asilimia 75 ya wanawake wote duniani hupata maambukizi haya katika kipindi cha uhai wao.

Maambukizi ya fangasi katika sehemu za siri za mwanamke husababishwa na uwepo wa fangasi wanaojulikana kitaalamu kama Candida albicans. 

Maambukizi haya pia hujulikana kama yeast infection au thrush. Fangasi hupatikana kama vimelea vya kawaida katika mdomo, mpira wa kupitisha chakula sehemu inayojulikana kama pharynx, katika kibofu cha mkojo, uume na hata kwenye uke.

Mfumo mzuri wa kinga wa mwili pamoja aina fulani za bakteria wanaoishi pamoja na fangasi hawa husaidia sana katika kuthibiti maambukizi yanayoyosababishwa na aina hi ya fangasi. 
 
Nini hutokea?
Kwa kawaida, Candida albicans huishi kwenye uke na sehemu nyingine (kama zilivyoelezewa hapo juu) bila kusababisha madhara yoyote yale isipokuwa pale mazingira ya eneo husika yanapobadilika kama vile mabadiliko katika hali ya pH ya  eneo husika (ifahamike ya kwamba pH ya kawaida ndani ya  uke ni 4.0 - 4.5) au uwiano wake na vimelea  (microorganisms) wengine unapoharibiwa kutokana na sababu mbalimbali kama vile matumizi ya madawa aina ya antibiotics, kupungua kwa kinga mwilini kutokana na magonjwa mbalimbali n.k.

Maambukizi haya ya fangasi yanaweza kugawanywa katika sehemu kuu mbili
  1. Maambukizi yasiyo makali yaani uncomplicated thrush: Katika kundi hili, mgonjwa hupatwa na maambukizi  mara moja hadi nne kwa mwaka na dalili zake huwa si mbaya sana na maambukizi haya husababishwa na fangasi wa jamii hii ya Candida albicans.
  2. Maambukizi makali yaani complicated thrush: Katika kundi hili, mgonjwa hupatwa na maambukizi zaidi ya mara nne kwa mwaka, dalili zake kuwa mbaya zaidi au kama maambukizi  yatakuwa yametokea kipindi cha ujauzito, ugonjwa wa kisukari, upungufu wa kinga mwilini. Aina hii kusababishwa na vimelea vya aina nyingine tofauti na Candida albicans.
Vihatarishi
Watu walio katika hatari ya kupata maambukizi ya fangasi hawa ni  wale wenye

• Kutumia sana dawa aina ya detergents kwenye sehemu za siri au douches (vifaa vinavyotumiwa kusafishia uke kwa kutumia maji yaliyochanganywa na siki au antiseptic yoyote ile) kwa sababu hali husababisha kuharibika kwa uwiano wa fangasi na aina nyingine ya vinyemelezi kama bakteria aina ya lactobacilli

• Kutumia sana madawa aina ya antibiotics, steroids ambayo yana tabia ya kushusha kinga ya mwili

• Mabadiliko ya mfumo wa homoni mwilini ambayo husababisha mabadiliko katika s ehemu za siri na hivyo kufanya kuwepo kwa ukuaji wa kasi wa fangasi hawa

• Ujauzito (kutokana na kubadilika kwa mfumo wa homoni mwilini na kupungua kwa kinga ya mwili). Hata hivyo ieleweke hapa kuwa si kila mjamzito hupatwa na maambukizi haya.

• Matumizi ya dawa za kupanga uzazi (vidonge vya majira)

• Upungufu wa kinga mwilini kutokana na magonjwa sugu kama kisukari, saratani aina yoyote ile, ugonjwa aina ya mononucleosis na nk.

• Ugonjwa wa ukimwi (HIV/AIDS)

• Matibabu ya homoni (hormonal replacement therapy) kutokana na sababu mbalimbali

• Matibabu ya kusaidia kushika mimba kwa wale wenye matatizo ya uzazi (infertility treatment)

• Msongo wa mawazo (stress)

• Utapia mlo (malnutrition)

• Kuvaa nguo au mavazi yanayoleta joto sana sehemu za siri kwa muda mrefu kama nguo za kuogelea (swimwear), nguo za ndani (chupi)  zilizotengenezwa kwa kitambaa aina ya nylon, nguo za ndani zinazobana sana nk.

• Kujamiana kwa njia ya kawaida mara tu baada ya kujamiana  kupitia njia ya haja kubwa (anal sex) au matumizi ya vilainishi venye glycerin wakati wa kujamiana pia yamehusishwa na maambukizi haya.

• Kuvimba kwa tezi la koo (goiter)

• Saratani ya tezi la koo (thyroid cancer)

• Wanawake wenye umri wa miaka kati ya ishirini na thelathini wapo kwenye hatari kubwa ya kupata maambukizi haya wakati wale ambao wameshaacha kupata hedhi au wale ambao hawajaanza kupata hedhi kabisa hawako kwenye hatari kubwa.

Kwa wanaume vihatarishi  vya maambukizi haya ni

• Kujamiana na mwanamke mwenye tatizo hili au maambukizi haya

• Upungufu wa kinga mwilini

• Matumizi ya madawa aina ya antibiotics kwa muda mrefu bila ushauri wa daktari

• Magonjwa sugu kama kisukari, saratani ya aina yoyote ile na nk.

Dalili na viashiria kwa wanawake
• Kuwashwa  sehemu za siri  (kwenye tupu ya mwanamke)

• Kuhisi kuwaka moto sehemu za siri (burning sensation)

• Kufanya kama vidonda katika sehemu za siri (soreness)

• Maumivu wakati wa kujamiana (superficial dyspareunia)

• Maumivu  au usumbufu wakati wa kujisaidia haja ndogo (wakati mtu anakojoa)

• Kuvimba na kuwa rangi nyekundu kwa  mdomo wa nje wa tupu ya mwanamke (labia minora)

• Kutokwa na uchafu wa rangi nyeupe au nyeupe kijivu, unaoweza kuwa mwepesi, majimaji au mzito na ambao umefanana na jibini (cottage cheese like discharge) wenye muonekano unaojulikana pia kama curd-like appearance. Kwa kawaida, uchafu huu haumbatani na harufu yoyote isipokuwa panapokuwa na tatizo la ziada kama ugonjwa wa zinaa aina ya Bacteria vaginosis. Uchafu huu unaotoka hapa unaweza kuenea kwenye maeneo mengine yaliyokaribu na tupu ya mwanamke kama kwenye mitoki (groin area) au perineum na kusababisha kuharibika kwa ngozi katika sehemu hizo.

Dalili na viashiria hivi huwa mbaya zaidi wakati  mwanamke anapokaribia  kupata hedhi.

Dalili na viashiria kwa wanaume ni
• Kuwashwa sehemu za siri 
• Kuvimba na kuwa rangi nyekundu kwenye ncha ya uume
• Kuwepo kwa uchafu wa rangi nyeupe (kama nilivyoeleza hapo juu) kwenye sehemu ya juu ya uume.
• Kuwa na vidonda vidogo kwenye uume (sore on the glans)

Hata hivyo, mara nyingi wanaume hawaoneshi dalili zozote zile, ni vizuri kwa mwanamke kumueleza mwenza wake pale anapopata maambukizi haya ili naye pia apate kutibiwa. 
 

Matibabu
Matibabu ya fangasi huusisha dawa za kutibu fangasi (antifungal drugs) kama vile dawa za kupaka za topical Clotrimazole, topical Nystatin, Fluconazole au topical Ketoconazole. 

Wagonjwa wenye maambukizi yasiyo makali yaani uncomplicated vaginal candidiasis wanaweza kutumia dawa za kupaka (cream) kutoka dawa za fangasi za jamii ya -azole kama vile Butoconozale, Miconazole, Clotricomazole nk. 

Dawa hizi hutumika kwa muda wa siku 3-7 kulingana na aina ya dawa. Mgonjwa anashauriwa kupaka dawa ndani ya uke pamoja na maeneo yote yanayozunguka sehemu hiyo. Jinsi ya kupaka dawa hizi ni kuanzia mbele kuelekea nyuma.

Aidha mgonjwa anaweza kupewa dawa za kutumbukiza ukeni ambayo atatumia kwa muda wa siku 3-14 kulingana na aina ya dawa. Dawa hizo ni pamoja na Miconazole, Tiaconazole, Terconazole, Nystatin nk.

Kidonge cha kumeza aina ya fluconzole pia huweza kutolewa. Dawa hizi nilizotaja hapa juu zina kawaida ya kuharibu ubora wa mipira ya kondomu zilizotengenezwa na mpira aina ya latex (latex condoms) pamoja na vifaa vya upangaji uzazi aina ya diaphragms.

Ni vizuri kwa daktari kabla ya kumpa mgonjwa dawa hizi kumfahamisha kwa ufasaha jinsi ya kuzitumia na tahadhari anayotakiwa mgonjwa kuchukua. Inashauriwa kama baada ya matumizi haya bado mgonjwa ana dalili za maambukizi au mgonjwa akapata tena maambukizi haya ndani ya miezi miwili baada ya matibabu ya awali, basi anashauriwa kwenda kumuona daktari ili apate matibabu zaidi.
 
Kinga ya maambukizi ya fangasi
• Kuosha sehemu ya siri kwa kutumia kitambaa kisafi kila siku na kuosha kuanzia mbele kuelekea nyuma, epuka kurudia ukishafika nyuma.

• Epuka matumizi ya sabuni zenye manukato, bubble baths, vaginal deodorant products, feminine hygiene, na bath powder.

• Vaa chupi ambazo hazibani sana na zilizotengenezwa kwa kutumia pamba au hariri (silk), epuka synthetic underwear.

• Epuka mavazi yoyote ya kubana kama jeans za kubana nk.

• Badilisha nguo za ndani (chupi) kila zinapopata unyevunyevu.

• Fua chupi zako kwa maji yenye nyuzi joto 90 na kuendelea.

• Tumia pad wakati tu unapozihitaji (kama umeingia kwenye mzunguko wako wa hedhi)

• Kula mlo wenye virutubisho vyote kamili (balanced diet)

• Epuka kufanya mapenzi  na mpenzi wako ambaye amepata maambukizi ya fangasi.

• Epuka kuoga  maji moto sana (hot baths) tumia maji ya uvuguvugu, hii kwa wale ambao wanaishi kwenye ukanda wa joto (tropical climate).

• Matumizi ya vifaa vya ngono (sex toys), vifaa vya upangaji uzazi (diaphragms, cervical caps) yanaweza kuleta kujirudia kwa maambukizi ya fangasi kama havitaoshwa  na kukaushwa vizuri baada ya kutumiwa.

• Baadhi ya tafiti zilizofanyika, zimethibitisha ya kwamba unywaji wa maziwa ya mtindi yenye live culture, husaidia kupunguza maambukizi ya fangasi.


Share:

Dalili za Mimba Kuharibika

Kuna sababu nyingi zinazoweza kusababisha mama mjamzito mimba yake kuharibika. Sababu kuu huwa ni magonjwa kama vile ugonjwa hatari wa malaria, ugonjwa unaotokana na zinaa kama vile kaswende na kisonono na U.T.I, dawa fulani fulani mfano Albendazole, Misoprostol, Metronidazole na kadhalika.

Lakini pia mjamzito akifanya kazi za kutumia nguvu nyingi anaweza kusababisha mimba yake kuharibika. Lakini kuna sababu nyingi ambazo zinasababisha mimba kutoka huweza kuzuilika kwa kwenda kliniki mapema yaani pale tu unapohisi una mimba hata kama ni wiki mbili na kufuata ushauri wa wataalamu.

Ukweli ni kwamba kuna wanawake wengi mimba zao huharibika na wao hushindwa kugundua mapema na matokeo yake anakaa na mtoto mfu hata miezi kadhaa bila kujua.

DALILI ZA MIMBA KUHARIBIKA
Zipo dalili ambazo husababisha mimba kuharibika kama tutakavyoona leo hapa. Dalili hizo ni hizi zifuatazo:

KUTOKA DAMU NYINGI SEHEMU ZA SIRI
Mjamzito akitokwa na damu nyingi sehemu za siri ni dalili kwamba mimba imeanza kuachia na mlango wa uzazi umeanza kufunguka, na hiyo inaashiria kwamba kuna mambo mawili yameshatokea kwanza inawezekana mtoto ameshafia tumboni au bado hajafa, lakini kama damu imetoka kwa wingi inaashiria kuwa mtoto huyo aliye tumboni atakufa tu.

MTOTO KUACHA KUCHEZA TUMBONI
Ikiwa mtoto ataacha kucheza tumboni ni tatizo kubwa kwani kwa kawaida mtoto huanza kucheza akiwa na wiki ya 18 mpaka 20 kwa wanawake ambao hawajawahi kubeba mimba na wiki ya 16 mpaka 20 kwa wanawake ambao wameshawahi kuzaa. Ikitokea mtoto aliye tumboni ameshawahi kucheza lakini ghafla akawa hachezi au muda huo umepitiliza na bado kimya kuna uwezekano mkubwa ikawa mtoto huyo amefia tumboni, hivyo haraka sana wahi hospitali kumuona daktari.

KUPOTEA KWA DALILI ZA UJAUZITO
Kupotea kwa dalili za ujauzito ni tatizo lingine baya kwa mama mjamzito. Mara kwa mara mwanamke akiwa na ujauzito anakuwa na dalili nyingi kama vile kuwa na kichefuchefu, kukosa hamu ya kula baadhi ya vyakula, kutapika, kulamba vitu vichachu kama vile limao, ndimu, wengine hula udogo na wengi hubadilika sana tabia, hivyo basi dalili zote hizo za mimba zikisimama ghafla basi ujue mimba imeharibika. 

MIMBA KUTOKUA 
Ikiwa mimba itaacha kuongezeka au kukua ni dalili nyingine ya mimba kuharibika. Kila mtu aliye mjamzito anategemea mimba iwe inakua kila siku  na iwe kubwa kulingana na umri unavyozidi kwenda mbele, ikiwa mimba iko vilevile kwa miezi kadhaa, yaani haikui au ukubwa wa tumbo haubadiliki ujue kwamba mimba hiyo imeharibika, ili kupata uhakika wahi hospitali kupimwa.

TUMBO KUWA NA MAUMIVU MAKALI
Ikiwa mjamzito atakuwa ana maumivu makali ya tumbo wakati ni mjamzito hiyo pia ni dalili mbaya. Kwa kawaida maumivu makali ya tumbo hasa kwa mimba kubwa ya miezi zaidi ya mitano au mimba ndogo kama mwezi mmoja, basi kuna uwezekano mkubwa kondo imeanza kujiondoa kwenye kizazi kwa mimba kubwa au mimba ndogo imeshindwa kuendelea kukua na moja kwa moja hiyo inaweza kuwa dalili ya kuwa mimba imeharibika.

KUTOKA VIPANDE VYA NYAMA SEHEMU ZA SIRI
Ikiwa mama mjamzito atakuwa akitokwa na vipande vya nyama sehemu za siri ni dalili mbaya sana. Kutokwa na vipande vya nyama sirini ni kuashiria kwamba kuna mtoto ameharibika tumboni. Hali hiyo ya hatari ikitokea mjamzito anatakiwa asafishwe kuondoa masalio yaliyobaki.


Share:

Mauaji Ya Mwanafunzi Wa Scolastica: Wazee washauri wa mahakama Watoa Ya Moyoni

Wazee washauri wa mahakama katika kesi ya mauaji ya mwanafunzi wa shule ya Scolastica, Humphrey Makundi (16), wametofautiana huku mmoja akisema washtakiwa wote wana hatia ya mauaji ya kukusudia.

Hata hivyo, mmoja wa wazee hao ameona mshtakiwa wa pili, Edward Shayo ambaye ni mmiliki wa shule hiyo apewe adhabu ndogo kwa maelezo kuwa kosa lake ni kuzembea kutoa taarifa ya mauaji.

Kifungu cha 196 cha kanuni ya adhabu sura ya 16, kinaeleza mtu yeyote anayesababisha kifo cha mtu mwingine bila uhalali wa kisheria anatenda kosa la mauaji na adhabu yake ni kunyongwa hadi kufa.

Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni mshtakiwa namba moja, Hamis Chacha ambaye ni mlinzi wa shule na Laban Nabiswa, mshitakiwa wa tatu ambaye ni mwalimu wa nidhamu shuleni hapo.

Kauli za wazee hao zilijitokeza juzi kati ya saa 11:00 alasiri na saa 1:30 usiku wakati Mahakama Kuu chini ya Jaji Firmin Matogolo anayesikiliza kesi hiyo, ilipoketi kupokea maoni ya wazee hao.

Kabla ya kuanza kupokea maoni hayo, Jaji Matogolo aliwasomea wazee hao muhtasari wa ushahidi wa upande wa mashtaka na ule wa utetezi wa washtakiwa pamoja na mashahidi wao waliowaita.

“Nyie (wazee washauri) ni waamuzi wa ushahidi siyo waamuzi wa sheria. Ili kuthibitisha shtaka la mauaji ya kukusudia ni lazima kuwe na kitendo cha kuua na dhamira ya kuua,” alisema Jaji Matogolo.

“Dhamira ya kuua inaweza kuthibitishwa na aina ya silaha iliyotumika kama ipo na nguvu iliyotumika. Mambo mengine ni matendo ya mshtakiwa kabla, siku ya mauaji na baada.”

Jaji alisema, “mmesikia mazingira yote ya kupotea kwa mwanafunzi (Humphrey) na baadaye mwili wake kupatikana mtoni na kutambuliwa kwake. Pia mmesikia sababu za kifo kuwa ni kuumia sana kichwani.

“Naamini pia mlisikia ushahidi wa shahidi wa 14 (Irene Mushi) wa upande wa mashtaka ambaye ni mlinzi wa amani kitu ambacho ndicho kitovu na ubishani mkubwa wa tukio hili.” Shahidi huyo ndiye aliyeandika maelezo ya ungamo ya mshtakiwa Chacha, akidaiwa kueleza hatua kwa hatua namna alivyomua mwanafunzi huyo na baadaye kuwashirikisha Nabiswa na Shayo.

Jaji Matogolo alisema katika mashauri ya mauaji mshtakiwa anaweza kuwa na utetezi na unaweza kuegemea katika ulevi, ukichaa au bahati mbaya na sababu nyingine.

“Lakini Utetezi huo haumuondolei kabisa mshtakiwa kosa la mauaji ya kukusudia, bali linampunguzia tu kutoka kuwa kosa la mauaji ya kukusudia na kuwa kosa la kuua bila kukusudia,”alifafanua jaji huyo.

“Vilevile mliweza kuwapima washtakiwa nani anasema ukweli na nani hasemi ukweli. Katika kesi hii imeegemea ushahidi wa mazingira kwa vile hakuna shahidi aliyeshuhudia mauaji hayo.”

Hata hivyo, Jaji Matogolo alisema ushahidi wa mazingira unakubalika pia kutokana na muunganiko wa ushahidi, hivyo ni wajibu wa wazee hao kupima mambo hayo wakati wanatoa maoni yao.

Baada ya maelezo hayo, mzee wa kwanza, Focus Mrema alisema amesikiliza kesi hiyo na mashahidi kwa umakini mkubwa, na kwamba hakuna ubishi kuwa kifo cha mwanafuzni huyo kilitokana na kuuawa.

Mzee huyo alieleza kwa maoni yake, upande wa Jamhuri umeweza kuthibitisha shtaka dhidi ya washtakiwa wote na akaiomba mahakama iwatie hatiani na iwape adhabu kwa mujibu wa sheria.

Kwa upande wake, mzee wa pili, Fatuma Ndutu, alisema baada ya kusikiliza ushahidi uliotolewa ana maoni kuwa mshtakiwa namba moja (Chacha) ana hatia kwa sababu alikiri kwenye ungamo lake.

Hata hivyo, alisema ana maoni kuwa ushiriki wa mshtakiwa namba mbili (Shayo) na namba tatu (Nabiswa) ni kwa kupitia mshtakiwa wa kwanza, hivyo wao wanaweza kupunguziwa adhabu.

“Jamhuri wamethibitisha shtaka kwa mshtakiwa wa kwanza bila kuacha mashaka, hivyo ana hatia kutokana na kukiri kwake. Mahakama itoe adhabu kwa mujibu wa sheria kwa kila mshtakiwa,” alisema.

Naye Khalfan Abrahaman alisema anaona kuwa upande wa mashtaka umeweza kuthibitisha shtaka la mauaji ya kukusudia dhidi ya mshtakiwa Chacha na Nabiswa.

“Kwa kitendo walichokifanya washtakiwa cha kushiriki kutupa mwili wa mtoto Mto Ghona ni kitendo cha kinyama na huwezi kutupa au kuhamisha mtu aliyekufa bila kuhusika na kifo chake,” alisema.

“Hivyo naiomba mahakama iwaone mshtakiwa wa kwanza na wa tatu wana hatia ya mauaji ya kukusudia. Hao wawili ni wahusika wakuu waliosababisha kifo cha mwanafunzi.”

Alisema, “vilevile pamoja na mshtakiwa wa pili (Shayo) yeye apewe adhabu kutokana na kuzembea ku-report (kutoa taarifa ya mauaji) aliyoipata kutoka kwa mshtakiwa wa kwanza.

Baada ya kumaliza kutoa maoni yao, Jaji Matogolo aliwaeleza wazee hao kuwa kwa kawaida hafungwi na maoni yao, bali anaweza kuyatumia au asiyatumie wakati anafanya uamuzi wa kesi hiyo.

“Kama nilivyosema nyinyi ni waamuzi wa ushahidi na mimi sasa nakwenda mbele zaidi kuangalia sheria inasemaje. Tarehe ya hukumu mtajulishwa na msajili. Hukumu haitachukua muda,” alisema.

Mwanafunzi huyo anadaiwa kuuawa Novemba 6, 2017 na mwili wake kutupwa Mto Ghona uliopo mita 300 kutoka ilipo shule ilipo na baadaye ukazikwa na Manispaa ya Moshi kwa kuwa haukutambuliwa.

Baadaye polisi kupitia Divisheni ya Mashtaka ya Taifa (NPS) waliomba kibali cha kufukuliwa kwa mwili huo na baba mzazi, Jackson Makundi aliutambia na baadaye kuthibitishwa na vinasada (DNA).

Katika kesi hiyo, upande wa mashtaka uliwajumuisha mawakili wanne huku washtakiwa wakitetewa na jopo la idadi kama hiyo ya mawakili.

Credit: Mwananchi


Share:

Aunty Ezekiel awavaa wanaohoji kuhusu mpenzi wake

Staa wa Bongo movie, Aunt Ezekiel amewataka wanaofuatilia mahusiano yake kumwachia mwenyewe, huku akidai suala la yeye kuwa na wanaume aliowazidi umri kwake si tatizo.

Aunt Ezekiel amesema amekuwa akikutana na maneno mengi, huku wengi wakidai amekuwa na tabia ya kutembea na wanaume wadogo kuliko umri wake, kitu ambacho kwake haoni tatizo, kwa kuwa wengi hawajui hayo ni maisha binafsi ya mtu.

“Suala la mimi kutembea na wanaume wadogo sidhani kama linatakiwa liingiliwe, haya ni maisha binafsi ya mtu, najua kila mmoja ana aina ya maisha anayotaka aishi, nadhani sipaswi kuingiliwa katika hili zaidi ya watu kushabikia kile ninachofuata,”alisema Aunt.

Kwa sasa inadaiwa staa huyo ameachana na baba wa mtoto wake, Mose Iyobo, ambaye ni mnenguaji wa lebo ya WCB, ambao walijaliwa kupata mtoto aitwaye Cookie.


Share:

Ufahamu ugonjwa wa Homa Ya Dengue

Dengue ni ugonjwa unaosababishwa na virusi viitavyo Dengue vinavyosambazwa na mbu aina ya Aedes . 

Mbu huyu anayeambukiza homa ya dengue hupendelea kuishi karibu na makazi ya watu na huweza kuuma binadamu mchana na usiku. 

Ugonjwa huu huathiri sana nchi za tropiko kama Amerika ya kusini na Africa. Ni moja kati ya homa kali inayodhoofisha na  kuambatana na maumivu makali. 

Kwa sasa, hakuna kinga ya homa ya dengue, njia pekee ya kuepuka ugonjwa huu ni kuzuia kuumwa na mbu anayesambaza homa ya dengue.
 
Dalili za homa ya dengue

•Homa kali ya ghafla

•Maumivu makali ya kichwa

•Macho kuuma

•Maumivu ya viungo

•Kichefuchefu

•Kutapika

•Vipele ambavyo hutokea siku nne baada ya homa kuanza

•Kutoka damu puani, kwenye fizi na kuchubuka kirahisi

Mara nyingi dalili huwa sio kali na wengi hudhania ni homa ya mafua au maambikizi mengine ya virusi. Dalili hizi huanza kutokea baada ya wiki mbili, lakini kwa wengi huchukua wiki moja ya kwanza na tayari utaanza kuona dalili za dengue.

Matatizo ambayo yanaweza kutokea baada ya maambukizi ya homa hii ni

•Homa kali zaidi

•Kuharibiwa kwa tezi na mishipa ya damu

•Kutokwa na damu zaidi puani na kwenye fizi

•Ini kuwa kubwa

•Na huweza kupelekea kifo

Vipimo

•Damu huchukuliwa na kuangalia virusi vya dengue au

• Kingamwili dhidi ya virusi hizi

Matibabu

Mpaka sasa hamna dawa kwa ajili ya ugonjwa huu ila  dawa za kupunguza homa na maumivu huweza kutumika kwa mfano:

•Paracetamol

•Pumzika vya kutosha

•Kunywa maji

•Nenda hospitali ukapate ushauri wa daktari



Share:

NEC yakana tangazo la ajira la kitapeli

Tume ya Taifa ya chaguzi inapenda kuutaarifu Umma kuwa, haihusiki na matangazo ya nafasi za ajira yaliyobandikwa katika maeneo mbalimbali ya Manispaa ya Moshi Mkoani Kilimanjaro.
 
Matangazo hayo yanaeleza kuwa, Tume imetoa ajira za muda, na wananchi walioomba ajira hizo wamekuwa wakiambiwa watoe kiasi cha fedha kwa madai kuwa ni kwa ajili ya mafunzo.
 
Hatua kali za Kisheria zitachukuliwa dhidi ya mtu au kundi la watu wanaotumia au wanaopanga kutumia jina la Tume ya Taifa ya Uchaguzi kufanya vitendo vya kihalifu.
 
Tunapenda kuwashukuru wananchi na kuwasihi kuendelea kutoa taarifa mara tu wanapohisi uwepo wa watu au kundi la watu wenye nia mbaya ya kulichafua jina la Tume yaTaifa yaUchaguzi.
 
Dkt. Athumani Kihamia
MKURUGENZI WA UCHAGUZI


Share:

Taarifa kuhusu matibabu ya Homa ya Dengue kwa wanachama wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).




Share:

Marekani yatuma mfumo wa kukinga makombora na meli ya kijeshi mashariki ya kati huku wasiwasi kati yake na Iran ukiendelea

Marekani inatuma mfumo wa kujilinda dhidi ya makombora na meli ya kivita katika eneo la mashariki kutokana na hali ya waiswasi iliopo katiya taifa hilo na Iran.

Meli hiyo ya kivita ya USS Arlington, inayosafirisha magari na ndege , itajiunga na kundi la kijeshi la USS Abraham Lincoln katika ghuba , maafisa wanasema.

Makombora ya US B-52 bombers pia yamewasili katika kambi moja nchini Qatar , idara hiyo imesema.

Imesema kuwa hatua hiyo inafuatia vitisho vya operesheni za vikosi vya kijeshi vya Marekani katika eneo hilo.

Marekani imetoa habari chache kuhusu uwezo wa tishio hilo , ambao Iran umepinga kama ujinga, ikitaja hatua hiyo ya Marekani kama vita vya kiakili vyenye lengo la kuitishia nchi hiyo.

Wakati huohuo chombo cha habari cha Isna News Agency kilimnukuu kiongozi mmoja mkuu wa dini , Yousef Tabatabai-Nejad akisema kuwa ''msafara huo wa Marekani unaweza kuharibiwa na kombora moja pekee''.
 
Siku ya Ijumaa idara ya Pentagon ilisema kuwa Marekani haitaki vita na Iran lakini Washington iko tayari kulinda vikosi vya Marekani na mali yake katika eneo hilo.

''Idara ya ulinzi inaendelea kufuatilia kwa karibu vitendo vya utawala wa Iran'', ilisema katika taarifa.

Iliongezea kuwa mfumo huo wa makombora ambao unaweza kutungua makombora ya masafa marefu na yale ya chini chini na ndege za kijeshi pia utapelekwa katika eneo hilo iwapo kuna uwezekano wa shambulio lolote.
 
Maafisa wameambia vyombo vya habari vya nchini Marekani kwamba meli hiyo ya USS Arlington ilitarajiwa kuwasili katika eneo hilo lakini imepelekwa katika eneo hilo mapema ili kutoa uwezo wa amri zitakazotolewa na udhibiti.

Siku ya Jumapili , mshauri wa maswala ya usalama nchini ,Marekani John Bolton amesema kuwa kupelekwa kwa vifaa hivyo vya kijeshi kutatoa ujumbe wa wazi kwa utawala wa Iran kwamba shambulio lolote dhidi ya mali ya Marekani katika eneo hilo litajibiwa na uwezo mkubwa wa kijeshi.

Meli hiyo ya USS Abraham Lincoln ilipita kupitia rasi ya Suez siku ya Alhamisi , kulingana na idara ya ulinzi nchini Marekani


Share:

Taarifa Kwa Vyombo Vya Habari Kuhusu Fursa Za Masomo

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imepokea nafasi za masomo ya muda mrefu katika fani ya Sayansi kutoka Serikali ya Misri.

Masomo hayo ambayo ni  kwa ngazi ya Shahada ya Uzamili na Uzamivu yatatolewa kwenye Chuo Kikuu cha Alexandria kilichopo nchini Misri chini ya udhamini wa Mpango wa Bonde la Mto Nile (Nile Basin Initiative).

Mwisho wa kuomba nafasi hizo ni tarehe 30 Mei 2019. Kwa maelezo zaidi kuhusu kozi hizo na namna ya kuomba, tafadhali tembelea tovuti ifuatayo: www.nbs.alexu.edu.eg
 
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma.
10 Mei 2019


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger