Saturday, 22 October 2016
Friday, 21 October 2016
Rais Magufuli aagiza HESLB kuongeza kasi ya ukusanyaji wa madeni.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. John Magufuli ameagiza Bodi
ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu kutumia Sheria zilizopo kuongeza
kasi ya ukusanyaji wa madeni kwa wahitimu walionufaika na mikopo.
Rais
Magufuli ametoa agizo hilo leo jijini Dar es salaam wakati akiweka jiwe
la msingi la mradi wa ujenzi wa hosteli za wanachuo katika Chuo Kikuu
cha Dar es Salaam unajengwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kwa
gharama ya shilingi bilioni 10.
Amesema kuwa Serikali inadai takribani shilingi trilioni 2.6 kwa wahitimu walionufaika na mikopo ya Elimu ya juu.
“Serikali
inawadai wahitimu walionufaika na mikopo ya Elimu ya juu takribani
shilingi trillion 2.6 ambazo wanatakiwa kuzirudisha ili ziweze kutolewa
kama mikopo kwa wanafunzi wapya na waliopo vyuoni” alifafanua Dkt Magufuli.
Aidha
Dkt. Magufuli ameitaka Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo
ya Ufundi kusimamia ipasavyo suala la utoaji wa mikopo kwa wanafunzi kwa
kuzingatia vigezo vilivyopo kwani lengo la mikopo hiyo inawalenga
watoto maskini.
Alisema
kuwa kumekuwa na baadhi ya malalamiko ya kuwa Bodi ya Mikopo ya
Wanafunzi wa Elimu ya Juu inafanya zoezi la ugawaji wa mikopo hiyo kwa
upendeleo hivyo kuzitaka uongozi wa Wizara kushughulikia suala hilo.
Mbali
na hayo Rais Magufuli amewataka wanufaika wa mikopo hiyo kutimia mikopo
hilo kwa malengo mazuri katika kujinufaisha na masuala ya Elimu.
Naye
Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Prof. Joyce
Ndalichako alisema kuwa mradi wa ujenzi wa hosteli hizo utasaidia
kuwahudumia wanafunzi 3,840 ambapo unatarajiwa kuisha mwishoni mwa mwezi
Desemba 2016.
Katika
hatua hiyo Prof. Ndalichako alisema kuwa wanafunzi waliodahuiliwa kwa
mwaka huu wapo 58,000 hivyo suala la wanafunzi 66,000 kukosa mikopo hiyo
ni upotoshaji unaofanya na baadhi wa watu.
Mradi
wa Ujenzi wa Hosteli za wanachuo katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
wenye majengo 20 kila jengo gorofa nne zenye vyumba 12 unatarajiwa
kukamilika mwishoni mwa Desemba mwaka huu.
Alichosema Rais Magufuli kuhusu mikopo ya wanafunzi wa Vyuo Vikuu
Rais
wa Tanzania Dkt. John Magufuli amesema Serikali imetenga Shilingi
Bilioni 483 kwa mwaka huu kwa ajili ya mikopo ya elimu ya juu ambapo
wanafunzi zaidi ya 118,000 watanufaika.
Akizungumza
katika uwekaji wa jiwe la msingi la hostel za Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam leo, Rais Magufuli amesema miongoni mwa hao watakaonufaika,
wanafunzi 93,000 ni wanaoendelea na masomo na wanafunzi takribani 25,000
ni watakaoanza masomo mwaka huu huku akiweka bayana kuwa mikopo hiyo
itatolewa kwa wanafunzi ambao wanatoka kwenye familia masikini.
Rais
Magufuli ameiagiza Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kurekebisha
dosari zilizopo katika mfumo wa utoaji wa mikopo ikiwa ni pamoja na
upangaji mbaya wa wanafunzi katika vyuo, kutoa mikopo kwa upendeleo,
kutozingatia sifa za mkopaji, kutoa mikopo hewa na kufungua vyuo kabla
ya mikopo ya wanafunzi kutolewa na pia amewaonya wanafunzi kujiepusha na
vitendo visivyofaa wakati Serikali inarekebisha dosari hizo.
"Na
ndio maana wakati mwingine na wabaya wanapitia humo humo, mara fanye
hivi fanyeni vile, wakati wanajua kuwa mkifanya yasiyofaa Serikali
itawafukuza tu ili mkafanyie mambo yenu huko.
"Kwa
sababu huwezi kuwa unahangaika kutafuta fedha za kuwapa mikopo, wakati
huo huo unahitaji kujenga reli, wakati huo huo unahitaji kujenga
barabara, wakati huo huo unahitaji kulipa mishahara, wakati huo huo
unahitaji kutoa elimu bure, wakati huo huo Karagwe kuna njaa, wakati huo
huo watu wanahitaji dawa hospitali, halafu watu wengine wanataka
kukuendesha kana kwamba hela unayokusanya ni kwa ajili yao tu, ni lazima
tuelewane na mimi ninataka kuwaeleza kwa dhati lazima twende katika
njia iliyonyooka, ni bora uwe Rais usiye maarufu lakini utimize
uliyoyaahidi, asitokee mtu wa kukuendesha, ninajua mmenielewa" amesisitiza Dkt. Magufuli.
Dkt.
Magufuli ameiagiza Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) kujipanga
vizuri kukusanya marejesho ya mikopo kwa wote waliokopeshwa na bodi hiyo
ambapo mpaka sasa bodi inadai takribani Shilingi Trilioni 2.6.
TCU: OPENING OF THE FOURTH ROUND OF APPLICATIONS THROUGH CAS
Tume
ya vyuo Vikuu (TCU) inautangazia Umma kuwa baada ya kukamilisha mchakato wa
maombi ya waombaji wa vyuo vikuu, vyuo Vikuu Vishiriki na Taasisi za elimu ya
juu kwa awamu ya kwanza, ya Pili na ya tatu, na matokeo ya waombaji wote
waliofanikiwa kupata nafasi vyuoni kukamilika, Tume ya vyuo Vikuu imebaini kuwa
bado kuna waombaji takribani 5,301 ambao bado wako kwenye mfumo na
hawajakamilisha maombi yao.
MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOPATA MKOPO CHUO KIKUU MUHIMBILI(MUHAS) 2016/2017
Kindly be informed that the
University has received the list of MUHAS students who have been
allocated with loans for academic year 2016/2017. Take note that only
students who had passed their August/September, 2016 University
Examinations have been allocated with loans. Those who had failed these
exams have not been allocated until they sit and pass their examinations
which started from 17th to 28th October, 2016.
The allocation of grants to eligible MD and DDS students will be done later by the HESLB.
The allocation of grants to eligible MD and DDS students will be done later by the HESLB.
MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI 1204 WALIOPATA MKOPO CHUO KIKUU SUA 2016/2017 BATCH 1
Kama kawaida ya MASWAYETU BLOG huwa hatulembi mwandiko,tumekuwekea hapo chini majina ya wanafunzi waliofanikiwa kupata mkopo chuo kikuu sua mwaka wa masomo 2016/2017
kuona majina
<<bonyeza hapa>>
Shirika la Viwango Tanzania (TBS) Kufumuliwa.....Waziri Mwijage Asema Litaundwa Upya, Vijana 136 Kuajiriwa
WAZIRI
wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage amesema atalifumua
na kuliunda upya Shirika la Viwango Tanzania (TBS) na kwamba wameshaanza
kutafuta vijana 136 watakaoajiriwa katika shirika hilo kwa lengo la
kudhibiti bidhaa, zinazoingizwa nchini chini ya viwango.
Serikali Yakubali Kurejesha Posho ya Sh. 8500 kwa Siku kwa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu Nchini
Bodi
ya Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetuliza hasira za
wanafunzi wa vyuo vikuu kwa kurejesha posho ya chakula na malazi ya
Sh8,500 kwa kila mmoja na kwamba tofauti baina yao itakuwa viwango vya
ada.
Ufafanuzi huu uliotolewa jana usiku na Waziri wa Elimu, Sayansi , Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Profesa Joyce Ndalichako wakati akizungumza katika mahojiano maalimu na kituo cha runinga cha Taifa -TBC utakuwa faraja kwa wanafunzi ambao chini ya Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Daruso) walipanga kushinikiza walipwe posho ya Sh8,500 kwa siku kama ilivyokuwa awali.
Ufafanuzi huu uliotolewa jana usiku na Waziri wa Elimu, Sayansi , Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Profesa Joyce Ndalichako wakati akizungumza katika mahojiano maalimu na kituo cha runinga cha Taifa -TBC utakuwa faraja kwa wanafunzi ambao chini ya Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Daruso) walipanga kushinikiza walipwe posho ya Sh8,500 kwa siku kama ilivyokuwa awali.
Hatua
ya wanafunzi kujenga umoja ili kushinikiza haki katika posho ilitokana
na baadhi yao kuingiziwa kati ya Sh40,000 na 70,000 badala ya Sh
510,000, hali ambayo ilizua sintofahamu.
Ndalichako alisema tofauti ya malipo itakuwa katika ada na siyo posho, “Vigezo
vya mikopo vimebadilika, kila mwanafunzi atapata fedha tofauti lakini
tumefanya marekebisho kwenye posho ya chakula ambayo kila mwanafunzi
atalipwa Sh8,500 kama awali.”
Kwa mujibu wa utaratibu wa Bodi hiyo, malipo hayo ya chakula na malazi hutolewa kila baada ya miezi miwili.
Mapema jana, Daruso iliwataka wanafunzi wa chuo hicho kutotia saini fomu za fedha za mikopo yao mpaka itakapowapa ruhusa ya kufanya hivyo.
Mapema jana, Daruso iliwataka wanafunzi wa chuo hicho kutotia saini fomu za fedha za mikopo yao mpaka itakapowapa ruhusa ya kufanya hivyo.
Rais
wa Daruso, Erasmi Leon alisema hayo jana wakati akizungumza na
wanafunzi wenzake kuhusu kusudio la kwenda HESLB kwa ajili ya kutafuta
haki yao ya msingi.
“Ninachowasihi
tuwe pamoja. Tuwe wamoja na twende pamoja. Tutakwenda wawakilishi
kutafuta nafasi kwa amani waweze kusikia tuna hoja gani lakini
tukinyimwa hii nafasi tutaenda kuitafuta tukiwa wengi,” alisema na kuongeza:
“Tuwe
watulivu kwa sasa tutakapowahitaji muda na wakati wowote kwa lolote
tushirikiane ili twende pamoja tumalize pamoja tuhakikishe tunapata
Sh8,500 kwa kila mwanafunzi kwa chakula na malazi,” alisema.
Kuhusu
suala hilo, uongozi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ulisema
wajibu wake ni kupokea na kusambaza majina na taarifa kutoka Bodi kwa
wanafunzi.
Akitoa
ufafanuzi kwa wanafunzi waliofika ofisini kwake kujua hatima yao na
waliopata mikopo kuchukua fomu za kutia saini, Ofisa Mikopo wa UDSM,
Lugano Mwakyusa alisema wenye jukumu la kujua walio na sifa ya kupata
mikopo ni Bodi ya Mikopo.
“Tunaendelea
kupokea majina kutoka bodi. Tayari hapa kuna majina 949 yameshatoka,
wengine tuzidi kusubiri na wale mwaka wa pili na tatu ambao walikuwa na
mitihani ya marudio taarifa zao zitapelekwa bodi,” Mwakyusa aliwaambia wanafunzi waliokuwa wamejaa ofisini kwake.
Kulikuwa
na hali ya sintofahamu chuoni hapo jana baada ya wanafunzi wengi wa
mwaka wa kwanza kuonekana wakiwa wameshika bahasha za kaki zilizokuwa na
fomu za usajili wanazotakiwa kujaza huku wakihangaika kutokana na
kutojua kiasi cha mkopo.
Juzi, Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, AbdulRazaq Badru
alieleza kwamba ingawa wanafunzi 88,000 waliomba mikopo kutoka HESLB,
uwezo wa bodi hiyo ni kutoa kwa wanafunzi 21,500 pekee sawa na asilimia
24 na waliokuwa wameshapatiwa walikuwa 11,000 sawa na asilimia 12.
Takwimu hizi zinaonyesha zaidi ya robo tatu ya wanafunzi wanaohitaji mikopo watakosa kutokana na uwezo mdogo wa kifedha.


![Audio | Sholo Mwamba – GHETTO [Singeli] | Mp3 Download sholo](http://bekaboy.com/wp-content/uploads/2016/10/sholo-702x336.jpg)
![Audio | Man Fongo [SINGELI] – Nakula Ujana | Mp3 Download man-fongo](http://bekaboy.com/wp-content/uploads/2016/10/MAN-FONGO-640x336.jpg)





















