Wednesday, 21 September 2016

PICHA:BASI LA SUPER SHEM LA MBEYA-MWANZA LIMEPATA AJALI,BAADA YA KUGONGANA NA DALADALA



Basi la Super Shem linalofanya safari za Mwanza kwenda  Mbeya limepata ajari ya kugongana na hiace katika kijiji cha Hungumalwa Mwanza na kusababisha vifo vya watu  wanaodaiwa kufika 11 asubuhi hii.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo, wanaeleza kuwa Basi hilo liliigonga gari hiyo ndogo ambayo iliingia kwenye barabara kubwa bila ya kuwa na tahadhali, Juhudi za kumpata Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza zinaendelea kufanyika ili kuthibitisha tukio hilo.


Share:

Serikali Yatoa Sababu za Shule 44 Kufungwa


 
WIZARA ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi imezifuta shule za awali, msingi na sekondari nchini ambazo hazijasajiliwa zaidi ya 40 kuanzia Julai mwaka jana.

Awali kuanzia Julai hadi Desemba mwaka jana, waligundua kuwepo kwa shule 35 zisizosajiliwa na kuzifuta, jambo lililofanya kutangaza shule zote ambazo hazijasajiliwa kujisalimisha ili kusajiliwa.

Kaimu Mkurugenzi wa Usajili wa Shule katika wizara hiyo, Khadija Mcheka alisema Mei mwaka huu baada kuzipa miezi miwili shule ambazo hazijasajiliwa kufanya hivyo, walizifungia shule nyingine 12.

Mcheka alisema shule zinaweza kufutwa kwa sababu mbili zikiwamo zilizosajiliwa, lakini zikakiuka vigezo ambazo zikitimiza vigezo zinaweza kuomba upya usajili na kupewa.

“Lakini aina ya pili ni zile ambazo hazijasajiliwa na zinaendeshwa kinyume cha sheria ambazo nazo zikifuata taratibu zikatimiza vigezo zinaweza kupewa usajili,” alifafanua Kaimu Mkurugenzi wa Usajili wa Shule.

Alisema katika kipindi hicho mpaka Agosti mwaka huu baada ya tangazo la kuwataka kusajiliwa shule za awali nne, zile za awali na msingi 105 na sekondari 19, walifika wizarani kwa ajili ya kupata taratibu za usajili ambapo zipo zilizosajiliwa na nyingine kupewa vibali.

Alisema katika usajili, kuna wapo waliokidhi viwango na wengine waliopatiwa maelekezo na kupatiwa vibali vya kutumia majengo yaliyopo huku wengine wakipewa vibali vya kujenga majengo ya shule kabla ya kupata usajili.

Alisema kwa shule walizozifungia, waliwaandikia barua za kuwafungia na kuwataka kuhakikisha wanawatawanya wanafunzi katika shule zilizosajiliwa kwa gharama zao bila kuwaathiri wanafunzi.

Alitaja shule zilizofungiwa kwa kuendesha shughuli zake bila usajili kuwa ni shule za awali na msingi za Must Lead ya mkoa wa Pwani, na za mkoa wa Dar es Salaam ni Brainstorm, Pax, Lassana, Grace, Rose Land, Julius Raymod, St Thomas, Mary Mother of Mercy, Noble Sinkonde, Immaculate Heart of Mary, St Columba, Corner stone, Dancraig, Mwalimu Edward Kalunga, Edson Mwidunda, Gisela, Kingstar, St Columba awali, Bilal Muslim, Thado, Hocet , Elishadai, Lawrance Citizen, Comrade, Dar Elite Preparatory na Golden Hill Academy na Hekima.

Nyingine ni Pwani Islamic, St Kizito na Rwazi Encysloped za Kagera, Dancraig na Qunu za Pwani, Hellen’s ya Njombe, Joseph ya Arusha, Samandito na Maguzu za Geita. Alizitaja shule za Sekondari zilizofungiwa kwa sababu hiyo kuwa ni Hananasif, Elu, Hocet, Safina za Dar es Salaam na Namnyaki ya Iringa.

Aidha, Shule ya Fountain Gate ya jijini Dar es Salaam imefungiwa kwa kuendesha bweni bila kibali.

“Baada ya kutoa tangazo kutokana na kubaini kuwapo shule nyingi zisizosajiliwa, wapo waliojitokeza na nyingine tumezifungia kutokana na kutokidhi viwango vya usajili lakini pia tunaamini wapo waliojificha wakiendelea kutoa huduma,” alisema Mcheka na kuwaagiza wakaguzi katika kanda na wilaya, kufanya ukaguzi na kutoa taarifa kwa zile ambazo hazijafungiwa na ikithibitika hazijasajiliwa, kuzifungia mara moja.

Alisema utaratibu uliopo kwa kuhakikisha shule zote zinasajiliwa kulingana na viwango stahili kwa lengo la kutoa elimu bora ni wakaguzi wa kanda, mikoa na wilaya kwa kushauriana na waratibu wa elimu katika kata, kuhakikisha shule yoyote inayochomoza, wanaifuatilia na kuwapa ushauri wa kufuata taratibu za usajili kwa kukidhi viwango stahili.

Alisema wamekuwa wakigundua kuwapo kwa shule, ambazo hazijasajiliwa kutokana na wakati wa mitihani idadi ya wanafunzi inazidi tofauti na walivyosajiliwa na kubainika kuwa wapo waliokuwa wakisoma katika shule, ambazo hazijasajiliwa wanawapeleka katika shule zilizosajiliwa.

“Kuna wenye shule ambazo hazijasajiliwa wakati wa mitihani wanakuja kuomba wanafunzi kufanya mitihani hivyo kuleta usumbufu wa kuwatawanya kwenye shule zilizosajiliwa na kwenda kuwakagua ili kuweza kusajiliwa,” alifafanua.

Msajili huyo alisema madhara yanayotokana na mwanafunzi kusoma shule ambazo hazijasajiliwa ni pamoja na haitajulikana mtoto anachosoma kwani haitajulikana mitaala wanayotumia kutokana na kukosa usajili, hivyo kushindwa kufanya mitihani. Pia mazingira ya shule na mpangilio wake, haitaendana na matakwa ya serikali ya kutoa elimu bora kwani mmiliki atafanya kile anachotaka.

Mei mwaka huu, wizara hiyo ilizipa miezi miwili hadi Julai 30, mwaka huu kuhakikisha shule zote ambazo hazijasajiliwa zinajisajili kabla ya serikali kuzifunga.

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Dk Leonard Akwilapo alisema ifikapo Julai 30, mwaka huu, mmiliki wa shule itakayobainika kutosajiliwa ikiwemo zitakazokosa vigezo vya kusajiliwa, atapaswa kuhamisha wanafunzi waliopo kwa gharama zake.

Alipoulizwa ni shule ngapi ambazo zinajiendesha bila kusajiliwa, Kaimu Mkurugenzi Mcheka alisema tatizo kubwa lipo kwa shule za awali na msingi.
Share:

Tuesday, 20 September 2016

MPYA:HII HAPA LIST YA VYUO VILIVYOTOA SELECTION YA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA VYUO VIKUU MBALIMBALI 2016/2017



Image result for TCU.GO
Habari yako,

Maswayetu blog,tumedhamiria kuwapa vitu roho inapenda hapa
Share:

Breaking news:NACTE-HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI CHETI NA DIPLOMA WALIOCHAGULIWA VYUO VYA UALIMU VYA SERIKALI 2016/2017

Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) linapenda kuwaarifu waombaji
Share:

MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA CHUO KIKUU CHA BIASHARA CBE 2016/2017

CBE: Selected student to join Bachelor Degree Dar es Salaam Campus 2016/2017-Batch 1



cbelogo
Selected student to join Bachelor Degree Dar es Salaam Campus 2016/2017
Share:

IFM: Majina ya wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na chuo kwa mwaka 2016/2017- (Shahada-Degree)



THE FOLLOWING APPLICANTS HAVE
Share:

MPYA:UDOM INATANGAZA NAFASI ZA MASOMO DIPLOMA & CHETI KWA WANAFUNZI WENYE SIFA 2016/2017

Logo
This is to inform the Public that the deadline for online application for Diploma and Certificate Programmes for Academic Year 2016/2017 has been extended to 24thSeptember to allow those failed to apply on time to be able to apply.
Share:

Ndege ya Serikali: Bombadier Q400 yawasili dar


[​IMG]
Share:

MPYA:TAARIFA MPYA KUTOKA TCU KWA WANAFUNZI WA RPL 2016/2017

Image result for TCU.GO.TZ
Share:

UPDATES:PICHA MBALIMBALI AJALI YA BASI LA NEW FORCE ONE ILIYOUA WATU 12 NA KUJERUHI KADHAA HAPO JANA

Share:

UPDATES:PICHA MBALIMBALI AJALI YA BASI LA NEW FORCE ONE ILIYOUA WATU 12 NA KUJERUHI KADHAA HAPO JANA

Share:

WANAFUNZI 200 WANAOTARAJIA KUONDOKA LEO KUSOMA VYUO VYA NJE WAPIGWA MSASA



Mkurugenzi Mtendaji wa Globa Education Link (GEL), Abdulmaalik Mollel akizungumza katika semina ya wazazi na wanafunzi 200 wanaotarajia kuondoka leo kwenda vyuo vikuu vya nchini China, iliyofanyika katika ukumbi wa Makumbusho jijini Dar es Salaam.

Wanafunzi wanaokwenda nje wakichukua tiketi pamoja na viza kwa ajili ya safari kwenda katika vyuo vikuu vya nchini China iliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Sehemu ya wazazi na wanafunzi wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Globa Education Link (GEL), Abdulmaalik Mollel hayupo pichani katika semina iliyofanyika katika ukumbi wa Makumbusho jijini Dar es Salaam. 
MKURUGENZI Mtendaji wa Globa Education Link (GEL), Abdulmaalik Mollel amesema wanafunzi wanaokwenda nje waliohitimu masomo katika vyuo vya nje wanatakiwa watafutwe na waajiri na sio wawe wa kutafuta ajira. 
Mollel ameyasema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati wa semina na wazazi na wanafunzi 200 wanaotarajia kuondoka leo katika vyuo vikuu vya nchini China, amesema kuwa kutokana na vyuo hivyo kuwa na vifaa vya kujifunzia wanafunzi wakitumia vizuri katika soko la ajira watatafutwa. 
Mollel amesema nchi haina tatizo la ajira hivyo watu wanatakiwa kuwa na uwezo binafsi ambao utamfanya mwajiri kutafuta mtu wa kumuajiri hivyo wanafunzi wanaokwenda kusoma vyuo wanatakiwa kutumia maarifa ya kuja kuzalisha nchini. 
Amesema wazazi watumie muda wao katika kuwafuatilia watoto wao wanaosoma nje ili kuweza kuona thamani ya fedha wanazozitoa na elimu wanayoipata. 
Aidha amesema kuwa wale ambao wanahitaji vyuo vya nje bado nafasi zipo na wanafunzi wote watafuata taratibu zote ikiwa ni pamoja Tume ya Vyuo Vikuu nchini kujiridhisha na vyuo wanavyokwenda. Mollel amesema haitakuwa tayari kuona wanafunzi wanahitimu vyuo vya nje kupitia GEL kuwa hawatambuliki.
 Kwa Wenye WhatsApp tu..SAVE nam
Share:

HIZI HAPA KURASA ZA NDANI MAGAZETI YA LEO JUMANNE SEPTEMBER 20,2016


1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMANNE SEP TAREHE 20.9.2016



Share:

Monday, 19 September 2016

UPDATES:PICHA MBALIMBALI BASI LA NEW FORCE ONE LA SONGEA-DAR LILILOPATA AJALI JANA USIKU NJOMBE



Kwa mujibu wa kamanda wa polisi,Watu 12 wamefariki dunia katika ajali ya basi la kampuni ya New Force lililokuwa likisafiri kutoka Dar kwenda Songea, katika watu waliofariki kati yao wanaume ni 4 na wanawake 8. Huku majeruhi wakiwa 10.
Share:

Ajali Njombe: Basi la New Force la Dar - Songea lapata ajali, watu kadhaa wahofiwa kupoteza maisha

ajali songea
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger