Saturday, 13 June 2026

OFISI YA WAZIRI MKUU NA OMDTZ ZAIMARISHA UTAYARI WA JAMII KUKABILIANA NA MAFURIKO DAR ES SALAAM




Na, mwandishi wetu - Dar es Salaam

Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Taasisi OpenMap Development Tanzania (OMDTZ), kupitia mradi wa Ramani Zetu, Sauti Zetu imeendesha warsha ya kupitia na kuthibitisha Mipango ya Kujiandaa na Kukabiliana na Maafa kwa kata tano za Makurumula, Mabibo, Keko, Ubungo na Tabata jijini Dar es Salaam.

Warsha hiyo imewakutanisha viongozi wa serikali za mitaa, Kamati za Usimamizi wa Maafa za Kata, wataalamu wa usimamizi wa maafa, waratibu wa maafa wa mkoa na wilaya pamoja na wadau mbalimbali kwa lengo la kuhakikisha mipango hiyo inakidhi mahitaji halisi ya jamii zinazokabiliwa na hatari ya mafuriko Dar es Salaam.

Akifungua warsha hiyo Mkurugenzi Msaidizi wa Operesheni za Maafa kutoka Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Kanali Selestine Masalamado amesema kuwa ubora wa mpango wa maafa hupimwa kwa uwezo wake wa kutekelezeka na kuleta matokeo chanya kwa wananchi, huku akisisitiza umuhimu wa mipango hiyo kuzingatia mazingira halisi, rasilimali zilizopo na uwezo wa taasisi husika.

“Mradi huu unaofadhiliwa na Zayed Sustainability Prize kupitia Taasisi ya Open Map Development Tanzania (OMDTZ), kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu – Idara ya Usimamizi wa Maafa, umekuja wakati sahihi na tunamatarajio makubwa katika kuleta matokeo chanya kuhakikisha tunaimarisha masuala ya usimamizi wa maafa nchini, ”alisema Kanali Masalamado

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa OMDTZ, Bw. Innocent Maholi, alisema taasisi hiyo itaendelea kushirikiana na Serikali katika kuimarisha ustahimilivu wa jamii dhidi ya maafa kupitia matumizi ya teknolojia, uchoraji ramani shirikishi na uwekezaji katika mifumo ya tahadhari ya mapema katika maeneo hatarishi.


Naye Mratibu wa Maafa wa Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Gerald Sondo, amepongeza ushirikiano huo akieleza kuwa mipango hiyo itasaidia kuongeza utayari wa jamii, kuboresha uratibu wa mwitikio wa dharura na kupunguza athari za mafuriko katika Jiji la Dar es Salaam.

“Kwa kipindi cha miezi mitatu iliyopita, kamati za usimamizi wa maafa katika kata husika zimefanya tathmini ya vihatarishi, kubainisha njia za uokoaji na maeneo salama, kuandaa mifumo ya mawasiliano na uratibu pamoja na kupendekeza hatua za tahadhari ya mapema zinazoshirikisha jamii,”alisema Bw. Sondo.

Aliongezea kuwa, Mipango iliyothibitishwa itatumika kama mwongozo wa vitendo kwa jamii kabla, wakati na baada ya maafa, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha usalama wa wananchi na ustahimilivu dhidi ya mafuriko na majanga mengine.





Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JUNI 13,2026


Magazeti









Share:

CGP. KATUNGU AWATAKA MAAFISA USTAWI KUELIMISHA WAFUNGWA HAKI NA WAJIBU WAO




Na. Ssgt Mawazo Mtondo - Dodoma.

Mkuu wa Jeshi la Magereza, CGP Jeremiah Yoram Katungu, amewataka Maafisa Ustawi wa Jamii wa Jeshi la Magereza kuhakikisha wanawaelimisha wafungwa na mahabusu kuhusu haki na wajibu wao mara wanapopokelewa magerezani pamoja na taratibu zinazopaswa kufuatwa katika kipindi chote wanaposhikiliwa gerezani.

CGP Katungu ametoa maelekezo hayo leo Juni 12, 2026 wakati akifunga rasmi Mafunzo ya Maafisa Ustawi wa Jamii kuhusu Mwongozo wa Utekelezaji wa Programu za Urekebishaji yaliyofanyika kwa siku tatu katika Ukumbi wa Rugimbana, Msalato jijini Dodoma.

Amesema mafunzo hayo ni sehemu ya jitihada za Jeshi la Magereza za kuendelea kuboresha huduma za urekebishaji kwa wafungwa sambamba na kutekeleza maelekezo ya Serikali na mapendekezo ya Tume ya Kuboresha Vyombo vya Haki Jinai.

Akizungumza na washiriki wa mafunzo hayo, CGP Katungu alisema mwongozo huo umebainisha maeneo muhimu yanayopaswa kuzingatiwa katika utekelezaji wa jukumu la urekebishaji, ikiwemo maadili ya kazi, dhana ya urekebishaji wa wafungwa, haki za binadamu katika utekelezaji wa programu za urekebishaji pamoja na matumizi sahihi ya nyaraka na fomu mbalimbali za kazi.

Aliwataka washiriki kutumia maarifa waliyojifunza kwa weledi na ufanisi ili kuleta mageuzi chanya katika utekelezaji wa jukumu la msingi la Jeshi la Magereza la kuwarekebisha wafungwa. Aidha, aliwahimiza kushirikiana na Wakuu wa Magereza kuanzisha na kuimarisha shughuli zinazolenga kuwapatia wafungwa elimu, maarifa na ujuzi wa kujitegemea.

Vilevile, aliwataka maafisa na askari wote wa Jeshi la Magereza kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia haki za wafungwa na mahabusu bila kuathiri usalama wao na wa magereza kwa ujumla. Alisisitiza umuhimu wa kudumisha upendo, mshikamano na umoja miongoni mwa watumishi wa Jeshi la Magereza ili kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu na kuendelea kulitumikia Taifa kwa ufanisi.

Awali akimkaribisha Mkuu wa Jeshi la Magereza, Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, CP Nicodemus Tenga, alimshukuru kwa kuridhia kufanyika kwa mafunzo hayo yaliyolenga kuwajengea uwezo, maarifa na stadi za kiutendaji Maafisa Ustawi wa Jamii.

CP Tenga alisema mafunzo hayo pia yalitoa fursa kwa washiriki kubadilishana uzoefu na kujifunza mbinu mbalimbali za kuboresha utendaji wao katika maeneo ya kazi kwa lengo la kuimarisha huduma za urekebishaji ndani ya Jeshi la Magereza.




Share:

Friday, 12 June 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA JUNI 12, 2026


Magazetini Leo




  

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger