Sunday, 12 April 2026

Video Mpya : MAMA USHAURI - MILEMBE

Share:

Saturday, 11 April 2026

Video Mpya : YOGATI - MAISHA

Share:

MOIL ENERGIES YAIPONGEZA TRA KWA MFUMO MPYA WA ULIPAJI KODI YA MAFUTA

 


Kampuni ya Uingizaji na Usambazaji wa mafuta Jamii ya Petrol nchini ya 'MOIL Energies' imesema imefurahishwa kwa kuanzishwa kwa mfumo mpya wa ulipaji kodi ya nishati hiyo kabla ya kuyatoa vituoni na kwenda sokoni (BIL) kwa kiasi kikubwa umesaidia kudhibiti 'ujanja ujanja' uliokuwepo hapo awali.

Akizungumza Dar es Salaam Meneja Mkuu wa Kampuni hiyo nchini, Dkt. Sajad Habib Rai amesema wao kama Kampuni ya kwanza nchini kutoa mapendekezo ya kuanzishwa kwa mfumo huo kwa EWURA na Wakala wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (PBPA) na baadae kuanzishwa rasmi na Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA), wanajivunia kuona umetekelezwa kwa kuwa dhamira yao ilikuwa kuona huduma ya usambazaji wa mafuta nchini na nje ya nchi unaleta tija kwa Taifa.

"Tumefurahi kuona TRA wameusimamia kikamilifu mfumo huu kwa kuwa unazuia ukwepaji kodi ambao hapo awali ulikuwa ukifanywa na wafanyabiashara, hivi sasa TRA inapata kodi yake mapema kabla ya kuyaingiza mafuta sokoni" amesema Dk Sajad ambaye pia ni Meneja MKAZI wa 'Mansoor Industry Limited'.

Hivi karibuni Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ilitangaza rasmi kuanza kutumika kwa mfumo huo ambao kwa kiasi kikubwa unalezwa kuleta tija kwa Serikali kwa kuwa umesaidia kudhibiti upotevu wa mapato unaotakana na Kodi za uingizaji wa mafuta hayo nchini.

Kupitia mfumo huo mpya na wa kisasa, kila mwagizaji au muingizaji wa mafuta atalazimika kutaja kiasi cha mafuta alichokiingiza nchini ambapo kupitia Shirika la Viwango Tanzania (TBS) watayataweka vinasaba kama alama ya kila mwagizaji kwa lengo la kuwatambua wahusika wote na kiasi alichoagiza ili kuwakadiria viwango vya Kodi wanavyopaswa kulipa.

"Nawapongeza TRA kwa kuona tija na umuhimu wa kuutumia mfumo huu, sisi kama wafanyabiashara tunaozingatia taratibu halali za uingizaji na Usambazaji wa mafuta tunaiona kuwa hatua hii ni kubwa na inayostahili kupongezwa kwa kuwa italeletea manufaa Taifa", ameongeza Dkt. Sajad.

Utaratibu huo wa kikodi unawataka wamiliki wa mafuta hayo kuyalipia kodi kabla ya kuyaingiza sokoni ili yanapoingizwa sokoni yanaendelea na taratibu za uuzwaji hali ambayo inarahisisha usambazaji na kuwafikishia wateja huduma ya mafuta kwa wakati sambamba na kudhibiti kubaki nchini mafuta ambayo kimsingi yanapaswa kusafirishwa kwenda nje ya nchi.

Aidha akizungumza wakati wa ziara yake aliyoifanya hivi karibuni katika bohari za kuhifadhia mafuta zilizopo Jijini Dar es Salaam, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Yusuph Juma Mwenda pamoja na mambo mengine alisema lengo la TRA kuweka utaratibu huo ni kuwezesha biashara kufanyika kwa urahisi na kuondoa changamoto zilizokuwepo hapo awali huku akitoa wito kwa wafanyabiashara watakaokutana na changamoto zozote kuwasiliana na TRA.

Pamoja na mambo mengine pia Kamishina Mwenda alisema Mamlaka hiyo pia umeweka utaratibu wa kufanya kazi kwa Saa 24 ili kuharakisha utolewaji wa huduma kwa walipakodi ambao ni waingizaji, wasambazaji na wauzaji wa mafuta hayo.

Share:

PROF. SHEMDOE AELEKEZA WAFANYABIASHARA SOKO LA SIMU 2000 KUENDELEA NA BIASHARA



Na OWM - TAMISEMI, Dar es Salaam

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe ameelekeza hatua za haraka zichukuliwe kuwarejesha wafanyabiashara wa Soko la Mawasiliano (Simu 2000) ili kuendelea na shughuli za biashara katika soko hilo ambalo lilipata ajali ya moto iliyoteketeza soko hilo Aprili 04, 2026.

Prof. Shemdoe ametoa maelekezo hayo Aprili 10, 2026 alipolitembelea soko hilo na kuridhishwa na utekelezaji wa Maelekezo ya Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba aliyoyatoa Aprili 6, 2026, alipofika kukagua madhara ya tukio hilo la moto na kuelekeza soko hilo kusafishwa mara moja ili kuruhusu wafanyabiashara kuanza taratibu za kurejesha shughuli zao.

“Nimeridhishwa na utekelezaji wa maelekezo aliyotupatia Mhe. Rais na Mhe. Waziri Mkuu, hivyo naelekeza haraka iwezekanavyo wafanyabiashara warejeshwe kuendelea na shughuli zao lakini wasijenge vibanda na badala yake waweke meza pamoja na miamvuli ili kujikinga dhidi ya jua na mvua,” amesisitiza Prof. Shemdoe.

Prof. Shemdoe amemtaka Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila kusimamia kikamilifu maelekezo aliyoyatoa, huku akimtaka Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe. Albert Msando kufanya ufuatiliaji wa kila siku ili wafanyabiashara wa soko hilo warejee haraka kuendelea na shughuli zao.

Aidha, katika hatua nyingine Prof. Shemdoe ameilekeza DART na Mkandarasi anayejenga soko jipya la Mawasiliano kuhakikisha ujenzi unakamilika kwa viwango ndani ya miezi minne badala ya sita ili wafanyabiashara hao wanaorejeshwa kwa kutumia meza wapate vibanda vya kufanyia biashara.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila amempongeza Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe. Albert Msando kwa usimamizi mzuri wa utekelezaji wa maelekezo ya Mhe. Waziri Mkuu ambayo yanayowezesha urejeshwaji wa haraka wa wafanyabiashara hao walioathirika na ajali ya moto katika soko hilo la mawasiliano (simu 2000). 

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe. Albert Msando amesema, ameelekeza ndani ya siku tatu kuanzia leo kufanyike zoezi la utambuzi wa wafanyabishara wote kwa majina matatu na vitambulisho ili kuepuka changamoto ya watu kuchukua vibanda na kuwapangisha wafanyabiasharana kuongeza kuwa atahakikisha wafanyabiashara watakaopata mikopo ni wale waliothirika na janga la moto na wenye sifa na stahiri ya  kupata mikopo.





Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI APRILI 11,2026


Magazeti
Share:

Friday, 10 April 2026

MWANAMKE CHUMA MAENDELEO GROUP YATOA MSAADA KWA WAFUNGWA WANAWAKE GEREZA LA KAHAMA 'TAMASHA KUBWA LA MWANAMKE CHUMA 2026 NI KESHO'


Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Katika kuendeleza jitihada za kijamii na kuonesha mshikamano wa dhati kwa wanawake wenzao, Kikundi cha wanawake maarufu kinachojulikana kama Mwanamke Chuma Maendeleo Group kimetoa msaada wa vifaa mbalimbali kwa wafungwa wanawake katika Gereza la Kahama Mkoani Shinyanga, ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea kilele cha Tamasha la Mwanamke Chuma 2026 litakalofanyika Aprili 11, 2026 Mjini Kahama.

Msaada huo uliokabidhiwa unajumuisha mahitaji muhimu ya kila siku kama vile sabuni, taulo za kike, dawa za meno, nguo, lishe ya watoto, kandambili (ndala) pamoja na mafuta ya kujipaka ikiwa ni hatua ya kupunguza changamoto ndogondogo zinazowakabili wafungwa hao na wakati huo huo kuwapa faraja ya kihisia.

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo leo Ijumaa Aprili 10,2026 , Mwenyekiti wa Mwanamke Chuma Maendeleo Group, Bi. Neema Moshi, amesema kuwa hatua hiyo inatokana na dhamira ya kundi hilo kuhakikisha kuwa wanawake wote, bila kujali walipo, wanapata faraja na kuendelea kuamini katika thamani yao.
Neema Moshi akizungumza

“Tukiwa na kaulimbiu ya ‘Nguvu ya Ujasiri’, tumeona ni muhimu kuwafikia wanawake wenzetu waliopo gerezani ili kuwatia moyo na kuwaonesha kuwa hawako peke yao. Tumekuja kama wawakilishi wa wanachama wetu kuwapa ujumbe wa matumaini na mshikamano,” amesema Bi. Moshi.

Kwa upande wake, Mratibu wa Tamasha la Mwanamke Chuma 2026 ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kituo cha Redio cha Gold FM, Bi. Neema Mghen, amesisitiza kuwa lengo kuu la ziara hiyo ni kuhamasisha matumaini na ujasiri kwa wanawake waliopo gerezani.
Neema Mghen akizungumza

“Tumekuja kuwaambia kuwa walipo si mwisho wa maisha yao. Ndoto zao bado zina thamani na wana nafasi ya kuanza upya. Wanapaswa kuendelea kuwa na ujasiri na kujiandaa kuwa wanawake imara watakapotoka hapa,” ameeleza Bi. Mghen.

Naye Mkuu wa Gereza la Kahama, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza Bonis Njoka Gervas, ametoa shukrani kwa kundi hilo kwa msaada na faraja walioutoa, akieleza kuwa hatua hiyo inachangia kwa kiasi kikubwa katika mchakato wa urekebishaji wa wafungwa.
Bonis Njoka Gervas akizungumza

“Wafungwa wanahitaji sana faraja na kutiwa moyo. Msaada kama huu unasaidia kuleta utulivu na amani gerezani huku ukiwajengea matumaini wanapokuwa wakisubiri kumaliza vifungo vyao au kesi zao,” amesema.

TAMASHA LA MWANAMKE CHUMA 2026 

Maandalizi ya Tamasha la Mwanamke Chuma 2026 yamekamilika, ambapo tukio hilo kubwa linatarajiwa kufanyika Jumamosi, Aprili 11, 2026 katika Ukumbi wa Malex Hall, Kahama kuanzia saa 11 jioni.

Tamasha hilo, linaloandaliwa na Kituo cha Redio cha Gold FM, limejipambanua kama jukwaa muhimu la kuwawezesha wanawake kijamii na kiuchumi kupitia elimu, mitandao na fursa mbalimbali.
Tamasha la mwaka huu linatarajiwa kupambwa na burudani mbalimbali kutoka kwa wasanii mbalimbali akiwemo msanii mkongwe wa muziki wa Taarab, Mzee Yusuph, huku mtaalamu wa maendeleo ya familia na uchumi, Dkt. Chris Mauki, akitoa mada maalum zitakazolenga kuwainua wanawake na jamii kwa ujumla. 

Aidha, shughuli hiyo itasindikizwa na ucheshi na uchangamshi kutoka kwa MC maarufu, Dkt. Kumbuka.

Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, ambaye atahitimisha rasmi tamasha hilo linalotarajiwa kuvuta washiriki kutoka maeneo mbalimbali ya Kanda ya Ziwa.

Mbali na burudani na elimu, tamasha hilo pia litahusisha utoaji wa tuzo kwa wanawake waliofanya vizuri katika nyanja mbalimbali, ikiwemo ubunifu, ujasiriamali, ushonaji, upishi, saluni pamoja na wanawake wenye ushawishi chanya katika jamii.

Kwa mujibu wa waandaaji, tamasha hilo ni zaidi ya burudani, ni jukwaa la kuibua vipaji, kuhamasisha uthubutu na kuimarisha mchango wa mwanamke katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Wananchi wa Kahama na maeneo jirani wanahimizwa kujitokeza kwa wingi kushiriki tukio hilo muhimu ambalo linabeba ujumbe wa matumaini, uthubutu na nguvu ya mwanamke wa kisasa.










Share:

MUYINGA AISHUKIA CHADEMA KUHUSU KIINI CHA VURUGU ZA OKTOBA 29



Na mwandishi wetu, Dar

Mwanaharakati wa kijamii, Alphonce Patrick Muyinga ameonya kuhusu baadhi ya wanasiasa na wanaharakati kutumia nguvu kubwa kuvuruga na kuanzisha chokochoko dhidi ya Tume huru ya kuchunguza matukio ya uvunjifu wa amani wakati na baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, akiwataka kuiacha Tume hiyo kukamilisha kazi yake kwa mustakabali wa amani na haki ya Watanzania.

Muyinga amebainisha hayo leo Ijumaa Aprili 10, 2026, siku moja mara baada ya Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kuzungumza na wanahabari na kuhamasisha maandamano nchini pamoja na kuishutumu serikali kuhusu kuendelea kushikiliwa kwa mwanasiasa Tundu Lissu, akisema zote hizo ni njama za kuvuruga utendaji wa Tume ya Oktoba 29.

"Watanzania wote tunajua Rais Samia aliunda Tume hii kuchunguza yaliyotokea Oktoba 29, leo Tume inakaribia kumaliza kazi tujiulize kwanini Heche na genge lake la wanakaa kuchochea, kutengeneza propaganda, kutumia nguvu kubwa kuvuruga uchunguzi wa tume. Wanaficha nini? Kuna nini hawataki tume ije kusema? Tuache! Tume imalize kazi yake ije iseme. Suala la Lissu ni la kisheria na lipo mahakamani kama zlivyo kesi za wengine." Amesema Muyinga.

Muyinga amemkosoa Makamu Mwenyekiti huyo wa Chadema pia kuhusu namna ambavyo amekuwa akikwepa kuzungumzia ajenda za maendeleo nchini na badala yake kuhamasisha vurugu na kutaka Vijana kupinga na kuharibu jitihada mbalimbali za maendeleo nchini, akiwataka Vijana kuzinduka na kujifunza kuhusu Chadema na siasa zao za mihemko wanazofanya wao pamoja na washika wao.

Mwanaharakati huyo amehimiza utulivu kwa watanzania na wapenda haki wote wa ndani na nje ya nchi katika kipindi hiki ambacho Tume ya Oktoba 29 inapokwenda kukamilisha jukumu lake, akiwasihi pia kuwakataa kwa nguvu wale wote wanaoanzisha uchochezi na tuhuma mbalimbali dhidi ya Tume na serikali kwa lengo la kuikwamisha Tume hiyo kumaliza kazi yake na kukabidhi kwa mamlaka kwa hatua zaidi.
Share:

Thursday, 9 April 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA APRILI 10, 2026

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger