Friday, 17 July 2026

How SportPesa Tanzania’s SP Score is changing the way fans follow every match

 

A game of football can change in a heartbeat. One side goes quiet as a late goal is scored and the other goes crazy celebrating. A red card, a missed penalty or a sudden comeback can turn a regular fixture into a story that fans talk about long after the final whistle.


Today, Tanzanian football fans follow the game with the same intensity every day. They want team news before kick-off, live updates during the game and clear results after. SportPesa Tanzania is responding to that demand with the SP Score app, a fast, all-in-one sports companion that brings live scores, fixtures, lineups, stats, match updates and sports news right at fans’ fingertips.

A matchday companion for today’s fans

SP Score gives fans instant access to match information across major sports and competitions. Football fans can follow competitions such as the Tanzania Premier League, the English Premier League and the UEFA Champions League, alongside other major leagues and tournaments. The app lets users follow live scores, fixtures, lineups, results, and match stats, all in one place, eliminating the need to search across multiple platforms.

Tanzanian fans follow football with passion and focus. They want to know who starts, who scores, who gets booked, and how the match shifts after every substitution. Through the SP Score app, SportPesa offers these fans a clearer, more connected way to stay engaged with the game.

“SP Score is about bringing the matchday experience closer to the fans. Whether someone is checking team news before kickoff, following a live score during the game or reviewing the result after full time, the app helps them stay connected to the sports they love” said SportPesa Tanzania Head of Marketing Tracy Humplick.

Live scores that keep fans in the moment

A goal can change a match in seconds. A red card can shift the pressure. A late substitution can turn a close game into a story fans remember. SP Score helps fans follow those moments as they happen.

Get live football scores, match events, results, and updates across leagues and tournaments around the world. Fans can follow their favorite teams, check key match moments, and stay informed even when they cannot watch the game live. That access makes SP Score useful for fans at work, on the road, at home, or in a crowded viewing space.

Stats that help fans understand the game

Today’s fans want more than the final score. They want to understand why a team won, how a player performed, and what changed the match. SP Score supports that habit with useful match statistics and game details.

The app gives fans access to lineups, formations, match stats, and team information. It helps supporters read the game with more context. A fan can follow possession, goals, cards, substitutions, and other key details while the match unfolds.

Built for more than football

Football sits at the heart of many Tanzanian sports conversations, but fans also follow other major sports. SP Score provides updates across football, basketball and tennis, giving users one place to follow scores, fixtures, results and key match information. The platform also plans to introduce cricket and rugby coverage, which will give fans access to an even wider range of sports.

This wider coverage makes SP Score a useful sports results app for daily sports followers. A fan can follow football in the evening, tennis during a major tournament, and basketball when the playoffs heat up. SportPesa Tanzania gives those fans one platform that supports their wider sports interests.

Why SP Score matters during major tournaments

The demand for quick, easy, and precise match updates rises during major competitions. When a goal, red card, comeback, or late equalizer changes the course of a game, fans don't want to wait for delayed scores or search through numerous pages. As the action takes place, SP Score provides users with a single, easy-to-use platform to track fixtures, results, lineups, statistics, and match news.

Every World Cup game has the potential to alter group standings, momentum, or a knockout path. With the speed and context that fans now expect, SP Score enables fans to follow teams from the first games to the championship game. The app makes every phone feel like a matchday screen. SportPesa Tanzania is moving closer to fans by giving them the information they need before, during and after every match.

Turning sports interest into daily fan engagement

The app gives SportPesa a daily role in the life of sports fans, even before a bet is placed. The app delivers value before the match starts, during the action, and after the final result. It helps fans follow sports with greater focus, better context, and faster access to the information they need.

Its impact goes beyond live scores. SP Score keeps fans coming back whenever they want fixtures, lineups, results, stats, or match updates. By supporting fans even before they decide to place a bet, the app builds trusted reliability and makes SportPesa Tanzania an essential part of the full matchday routine.

Conclusion

SportPesa Tanzania’s SP Score gives fans more than just live scores. The app allows you to follow the matches faster, get the key moments and stay connected to football, basketball and tennis. Fans can download SP Score from Apple App Store or Google Play Store. Fans can visit the official SP Score website to find out more and start following their favourite teams and competitions.


Share:

SERIKALI YASISITIZA UKUZAJI TIJA KATIKA SEKTA YA UMMA



Na: OWM (KAM), Dodoma

Watumishi wa umma vijana na wanawake katika wizara na taasisi wamepatiwa mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo katika kukuza tija na kuimarisha utendaji kazi kwa lengo la kuongeza ufanisi wa utoaji huduma bora na kuchochea maendeleo .

Mafunzo hayo yametolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Korea Kusini (KOICA) jijini Dodoma 16 Julai 2026 ambapo watumishi vijana na wanawake kutoka Ofisi ya Rais Utumishi na Maendeleo ya Vijana pamoja na wanufaika wa programu za KOICA (Almni)

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo Kaimu Mkurugenzi wa Ajira na Ukuzaji Ujuzi Bi. Alana Nchimbi aliyemwakilisha Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano Bi.Mary Maganga amesema vijana na wanawake wana mchango mkubwa katika ukuzaji tija kwenye utumishi wa umma.

Bi. Alana aliongeza kusema vijana na wanawake ni sehemu muhimu ya nguvu kazi na kwa kuwa wana uwezo mkubwa wa kuchangia ukuaji wa tija, kuongeza ufanisi na kuboresha utendaji wa sekta ya umma huku ikihakikisha vikwazo vya kiutendaji vinaondolewa

“Yatupasa kwa pamoja kuongeza jitihada za kuondoa vikwazo kwa vijana na wanawake, hivyo Ofisi ya Waziri Mkuu itaendela kushirikiana na Korea Kusini kutoa nafasi za mafunzo ya kuongeza tija kwa watumishi wa umma ili wananchi wapate huduma bora” alisisitiza Bi.Alana.

Kwa upande wake Balozi wa Korea Kusini nchini Tanzania Mheshimiwa Eunju Ahn amesema kuwa Serikali ya Jamhuri ya Korea kupitia Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Korea (KOICA) itaendelea kufanya kazi kwa karibu na Serikali ya Tanzania katika kuimarisha uwezo wa sekta ya umma kwa kutoa programu za mafunzo kwa vijana na wanawake.

Balozi Ahn aliongeza kusema watanzani wengi wameendelea kufadhiliwa kushiriki mafunzo ya aina mbalimbali nchini Korea Kusini ambayo yamewajengea ujuzi na maarifa ya kukuza tija kwenye utumishi wa umma.

Katika hatua nyingine Balozi huyo aliwapongeza wanufaika wa programu za mafunzo za KOICA kwa kuandaa mafunzo haya nchini Tanzania hatua inayoonesha kwa dhati kukuwa kwa uhusiano baina ya nchi hizi mbili.

Naye mmoja wa wanufaika wa mafunzo hayo ambaye pia ni Mhadhiri Msaidizi wa Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini (IRDP) Dominic Joseph amesema mafunzo hayo yamelenga la kubadilishana uzoefu na kujengeana uwezo wa kukuza tija kwenye utekelezaji wa maeneo yao ya kazi kufuatia mafunzo waliyoyapata nchini Korea Kusini kwa miaka tofauti tofauti.

Kadhalika aliongeza kusema mafunzo hayo yanatarajiwa kuwa chachu ya mabadiliko kwa washiriki waliopata mafunzo kwa kuwapa maarifa na mbinu zitakazowawezesha kuhamasisha wanawake na vijana kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya sekta ya umma na kuongeza mchango wao katika maendeleo ya taifa.





Share:

WAZEE WA KIMILA TARIME WAMWOMBA RAIS SAMIA AMFIKIRIE LISSU, WASISITIZA KULINDWA KWA AMANI



Na Mwandishi wetu, Mara

Wazee wa kimila kutoka koo 12 za Wilaya ya Tarime, mkoani Mara, wamemuomba Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutumia falsafa yake ya 4R (Maridhiano, Ustahimilivu, Mageuzi na Kujenga Upya) kumfikiria na kumuachia huru Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, huku wakisisitiza umuhimu wa kulinda amani kwa maslahi ya ustawi na maendeleo ya Tanzania.

Wito huo umetolewa leo Alhamisi Julai 16, 2026, wakati wazee hao walipozungumza na waandishi wa habari ambapo kwa niaba ya Koo ya Nyabasi, Mzee Moris Mung'osi amesema wanaamini Lissu amekaa mahabusu kwa muda mrefu na huenda amejifunza kutokana na yaliyotokea, hivyo akamuomba Rais Samia amfikirie kupitia sera yake ya maridhiano.

"Tunamuomba Rais Samia Suluhu Hassan kupitia falsafa yake ya maridhiano (4R) amfikirie Tundu Lissu ambaye amekaa ndani muda mrefu na huenda amejifunza na kubadili tabia yake ya kutotambua viongozi walioko madarakani. Aachiwe huru." Amesema Mung'osi.

Kwa upande wake, Mzee wa Koo ya Bumera, Joseph Maricha, ameipongeza Serikali kwa kuendelea kudumisha amani nchini na kuwataka vijana kutokubali kushawishiwa kujiingiza katika vitendo vya uvunjifu wa amani, akibainisha kuwa matukio yaliyotokea Oktoba 29, 2025 yalichangiwa na ushawishi wa watu wasiopenda utulivu wa nchi.

Naye Mzee Charles Mwita Mugogo wa Koo ya Bukimbaru amempongeza Rais Samia kwa juhudi zake za kuleta maendeleo nchini, akisema mazingira ya amani ndiyo msingi wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo, akiwataka wananchi, hususan vijana, kuwakataa wanasiasa wanaohamasisha vurugu na vitendo vinavyoweza kuhatarisha usalama wa taifa.

Wazee hao walihitimisha kwa kusisitiza kuwa taasisi za kimila zina wajibu wa kuendelea kuhamasisha umoja, mshikamano na amani, huku zikihimiza vijana kushiriki katika shughuli za maendeleo badala ya kujiingiza katika vitendo vinavyoweza kuvuruga utulivu wa nchi.





Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JULAI 17, 2026

Share:

Thursday, 16 July 2026

SIMAMMIENI MIRADI YA MAENDELEO, PINGENI UKATILI DHIDI YA WATOTO: NAIBU WAZIRI MAHUNDI



Na Jackline Minja, WMJJWM - Kakonko

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, amewataka wananchi wa Wilaya ya Kakonko mkoani Kigoma kuendelea kushirikiana na Maafisa Maendeleo ya Jamii, kusimamia na kuendeleza miradi ya kiuchumi inayotekelezwa katika maeneo yao ili kuongeza kipato, kuinua ustawi wa familia na maendeleo ya jamii kwa ujumla.

Mahundi metoa rai hiyo Julai 15, 2026, wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli mbalimbali za maendeleo wilayani humo, ikiwemo shughuli za Kikundi cha Wanawake Ubihumwe Kata ya Gwarama, kikundi cha vijana Tuinuane na Shule ya Msingi Itumbike yenye kitengo cha watoto wenye mahitaji maalum.

Amekutana pia na kikundi cha watu wenye ulemavu Kakonko pamoja na kuzindua jengo la kivuli cha Soko la Kijiji cha Kanyonza.

Amesema, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuweka mazingira wezeshi kwa makundi mbalimbali ya wananchi kupitia mikopo, mafunzo na miradi ya maendeleo, hivyo ni wajibu wa wananchi kuitunza na kuisimamia miradi hiyo ili iwe na tija ya kudumu kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

Aidha, amewataka wazazi na walezi kutimiza wajibu wao wa malezi kwa kuwajenga watoto katika maadili mema na kuhakikisha wanakuwa mstari wa mbele kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia vinavyoathiri watoto na wanawake katika jamii.

"Tupige kelele kukataa ukatili wa kijinsia na tuwalinde watoto wetu ili wakue katika mazingira salama yatakayowafanya kuwa raia wema na wenye mchango kwa Taifa," alisema Naibu Waziri Mahundi.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Kakonko, Mbunge wa Jimbo hilo, Mhe. Allan Mvano amesema ataendelea kuwa sauti ya wananchi wake kwa kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuhakikisha ahadi alizozitoa kwa wananchi zinaendelea kutekelezwa kwa kushirikiana na Serikali, wadau wa maendeleo na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, kuhakikisha kunapatikana matunda katika sekta mbalimbali ya elimu, uwezeshaji wa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu pamoja na kuboresha miundombinu ya huduma za kijamii.








Share:

MRADI WA BARABARA YA LUTUKIRA-SONGEA WABUNGE WATAKA HAKI NA USALAMA KWA WAFANYAKAZI

barabara ya Lutukira-Songea yenye urefu wa kilomita 100 pamoja na barabara ya mchepuko yenye kilomita 16 iliyotembelewa na wabunge wa mkoa wa Ruvuma yenye thamani ya shilingi bilioni 150
Meneja wa TANROADS mkoa wa Ruvuma mhandisi Saleh Juma wa kwanza kutoka kulia akiwa na wabunge wa mkoa wa Ruvuma walipotembelea na kukagua maendeleo ya mradi huo wa barabara ya Songea-lutukira yenye kilomita 100 na barabara ya mchepuko yenye kilomita 16

Na Regina Ndumbaro Songea-Ruvuma.

Wabunge wa mkoa wa Ruvuma wamezitaka taasisi zinazosimamia ujenzi wa barabara ya Lutukira–Songea yenye urefu wa kilomita 100 pamoja na barabara ya mchepuko ya kilomita 16, kuhakikisha haki za wafanyakazi zinalindwa kwa kuzingatia sheria, kanuni na miongozo ya kazi.

Share:

Wednesday, 15 July 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI JULAI 16, 2026

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger