Sunday, 7 June 2026

MIGODI YA BARRICK YA BULYANHULU NA NORTH MARA YAADHIMISHA SIKU YA MAZINGIRA KWA KUPANDA MITI NA KUFUATILIA MRADI WA UREJESHAJI UOTO ASILI MTO TIGHITE

Wafanyakazi wa Barrick Bulyanhulu wakiwa kwenye picha ya pamoja na wanafunzi baada ya kushiriki zoezi la upandaji wa miti kwenye maadhimisho ya siku ya mazingira duniani.
Afisa Mahusiano ya Jamii Mwandamizi wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu , Zuwena Senkondo akimwagilia mti baada ya upandaji katika maadhimisho ya siku ya mazingira duniani
Wafanyakazi wa Barrick North Mara wakipanda miti kando kando ya Mto Tighite katika maadhimisho ya siku ya mazingira duniani Wilayani Tarime , Mkoani Mara.
***

Kampuni ya Barrick inayoendesha shughuli zake nchini kwa ubia na Serikali kupitia kampuni ya Twiga, kupitia migodi yake ya Bulyanhulu na North Mara imeadhimisha Siku ya Mazingira Dunia 2026 kwa kushirikiana na jamii zinazoizunguka kwa kupanda miti, kufanya usafi kwenye shule na kukagua maendeleo ya mradi wa kurejesha uoto wa asili wa Mto Tighite uliopo wilayani Tarime.

Mgodi wa Barrick Bulyanhulu ulipo katika Halmashauri ya wilaya ya Msalala mkoani Shinyanga wafanyakazi wake walitembelea Shule ya Msingi Kakola A na kupanda miti pamoja na kufanya usafi pia ulitoa msaada wa miche ya miti ya matunda na kivuli ipatayo 2300.

Kwa upande wa Mgodi wa Barrick North Mara uliopo wilayani Tarime mkoani Mara, Wafanyakazi wake waliungana na jamii kutembelea na kukagua maendeleo ya mradi wa kurejesha uoto wa asili wa mto Tighite uliopo katika Kijiji cha Matongo unaofadhiliwa na mgodi huo kupitia shirika lisilo la Kiserikali la Jumuiya ya Watumiaji Maji Tighite Chini (JWMTC).

Kaimu Meneja Mazingira wa Barrick Bulyanhulu, Arespicius Onesmo akizungumzia kuhusu ushiriki wa Barrick Bulyanhulu katika maadhimisho ya mwaka huu,alisema ni mwendelezo wa utekelezaji wa mkakati wa kampuni ambapo suala la mazingira linapewa kipaumbele kikubwa.

“Tumeshirikiana na jamii kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani kwa kupanda miti, tumeanzia ndani ya mgodi ambapo wafanyakazi wa kila idara wameshirikiana na viongozi wao kupanda miti, na hii inaonesha uwajibikaji wa mgodi katika kulinda na kutunza mazingira vilevile mgodi una programu ya kutoa miche zaidi ya 20,000 katika shule zilizopo katika kata mbili za Bugarama na Bulyanhulu ili kuboresha mazingira”,alisema Onesmo.

Naye Meneja Mazingira wa Barrick North Mara, Frank Ngoloma alisema maadhimisho ya mwaka huu wameyafanya kwa kufuatilia maendeleo ya ukuaji wa miti ya asili iliyopandwa kandokando ya mto Tighite kwa ufadhili wa mgodi na wameridhishwa na usimamizi mzuri wa mradi huo na miti iliyopandwa mwaka jana inaendelea kustawi vizuri

Ngoloma alisema mradi huo ulizinduliwa wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani mwaka jana kwa lengo la kurejesha uoto wa asili wa mto huo unaotegemewa na maelfu ya wananchi kwa ajili ya maji ya matumizi ya majumbani,kunywesha mifugo na shughuli za kilimo.

Akizungumzia ushiriki wa Barrick kushirikiana na jamii kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani kila mwaka, kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Msalala , Humphrey Peter aliupongeza Mgodi wa Bulyanhulu kwa kuthamini maadhimisho hayo na kuona umuhimu wa kushirikiana na jamii katika zoezi la kupanda miti ili kulinda mazingira.

“Tunaushukuru Mgodi wa Barrick Bulyanhulu kwa kutambua siku ya mazingira dunia, kati ya taasisi na mashirika yaliyopo katika wilaya yetu ni Barrick Bulyanhulu pekee ndio wanafanya tukio hili la kipekee na wanakuja kusaidiana na jamii kuboresha Mazingira ,” amesema Humphrey.

Naye Mwenyekiti wa JWMTC, Mwita Seri na Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Matongo,Charles Ryoba wameushukuru mgodi wa Barrick North Mara kwa ufadhili na ushirikiano unaoendelea kutoa kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa kuboresha mazingira ya mto Tighite unaolenga kufanikisha upandaji wa miti ya asili 50,000 .

Kwa mujibu wa taarifa iliyosomwa, JWMTC iliomba Mgodi wa Barrick North Mara ukakubali kutoa shilingi milioni 36.7 kwa ajili ya kuotesha miche kwenye vitalu, kisha kupanda miti ya asili 50,000 katika eneo lenye ukubwa wa hekta 27 kandokando ya Mto Tighite.

Aidha, Mto Tighite ni miongoni mwa vyanzo muhimu vinavyochangia maji katika Mto Mara ambao unamwaga maji yake katika la ziwa la kimataifa - Ziwa Victoria upande wa Tanzania.

Kampuni ya Barrick katika mikakati yake endelevu moja ya sera katika uendeshaji shughuli zake mambo ya mazingira na mabadiliko ya tabianchi yanapewa vipaumbele katika utunzaji wa mazingira , kulinda vyanzo ya maji, uchafunzi wa hali ya hewa na kulinda uoto wa asili.
Wafanyakazi wa Barrick Bulyanhulu wakiwa kwenye picha ya pamoja na wanafunzi na wadau wengine mara baada ya zoezi la upandaji wa miti katika maadhimisho ya siku ya mazingira duniani
Wafanyakazi North Mara wakiongea na wananchi baada ya kutembelea mto Tighite
Wafanyakazi North Mara wakiongea na wananchi baada ya kutembelea mto Tighite

Share:

WALIMU FUNDISHENI VIZURI TUPATE TAIFA IMARA - PROF. SHEMDOE

Na OWM - TAMISEMI, Dar es Salaam

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe ametoa wito kwa walimu wote nchini  wa shule za awali, msingi na sekondari  kufundisha kwa umahiri ili taifa liwe imara na rasilimali watu yenye kutoa mchango katika ukuaji wa uchumi na ustawi wa jamii.

Prof. Shemdoe ametoa wito huo kwa walimu hao Juni 06, 2026 katika Ukumbi wa Maktaba mpya wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, wakati wa hafla ya utoaji wa zawadi kwa washindi wa shindano la taifa la stadi za ufundishaji kwa walimu wa awali, msingi na sekondari nchini.

“Kaulimbiu hii inayosema Ufundishaji Bora, Taifa Imara ina mashiko, hivyo  ninatoa wito kwa walimu mfundisheni vizuri, na wito huu si kwa walimu mlioshinda tu bali ni kwa walimu wote nchi nzima kwani mnapaswa kuzingatia  kuwa ufundishaji bora utatupatia taifa imara,” amesisitiza Prof. Shemdoe.

Ili kuwapatia motisha walimu 35 walioshinda katika shindano la taifa la stadi za ufundishaji, Prof. Shemdoe amewaelekeza wakurugenzi wa halmashauri zote ambazo walimu hao wanafundisha kuhakikisha wanawapatia kiwanja ili waendelee kubaki katika vituo vyao vya kazi na kulitumikia taifa, huku viwanja hivyo vikibaki kuwa ni kumbukumbu ya kudumu ya namna Serikali inavyothamini utendaji kazi wao.

Sanjari na hilo, Prof. Shemdoe amewataka walimu wengi zaidi kujitokeza kushiriki katika shindalo hilo mwakani ili  kuibuka washindi na kutambulika kitaifa kutokana na umahiri wao katika stadi za ufundishaji.

Aidha, Prof. Shemdoe amemshukuru na kumpongeza Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa kipaumbele kikubwa cha kuboresha miundombinu ya sekta ya elimu hususani katika eneo la ujifunzaji na ufundishaji, hatua ambayo imeongeza kiwango cha ufaulu wa wanafunzi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) Dkt. Aneth Komba amesema kuwa shindano hilo limejumuisha halmashauri zote 184 za Tanzania Bara na linaratibiwa na Serikali kupitia TET chini ya Programu ya kuboresha Elimu ya Awali na Msingi (BOOST) na Mradi wa kuimarisha Ubora wa Elimu ya Sekondari (SEQUIP).

Washindi wa shindano hilo la taifa la stadi za ufundishaji kwa walimu wa awali, msingi na sekondari wamepatiwa zawadi ya fedha tasilimu, kompyuta, kompyuta mpakato, vibao vya kidijitali na projekta kwa ajili ya shule zao ili kuongeza ufanisi katika ufundishaji na ujifunzaji.












Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JUNI 7,2026


Magazeti
Share:

Saturday, 6 June 2026

NEMC YAMTUZA JACKLINE KWA UFAFANUZI BORA WA UCHUMI MZUNGUKO


Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limemtambua mwanafunzi wa Darasa la Sita, Jackline Eliabi wa Shule ya Msingi Manyinga, Wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro, kwa uwasilishaji wake bora wa dhana ya Uchumi Mzunguko katika kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani.

Jackline alipata pongezi na kutunukiwa zawadi baada ya kuwasilisha kwa umahiri dhana hiyo muhimu inayohamasisha matumizi endelevu ya rasilimali, upunguzaji wa taka na uhifadhi wa mazingira.

Uwasilishaji wake ulionesha uelewa mkubwa wa masuala ya mazingira na mchango wa wanafunzi katika kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kutunza mazingira kwa maendeleo endelevu.

Zawadi hiyo ilitolewa na Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Immaculate Sware Semesi, ikiwa ni kutambua mchango wa wanafunzi katika kusukuma gurudumu la uhifadhi na usimamizi wa mazingira nchini.

Dkt. Semesi alieleza kuwa wanafunzi ni wadau muhimu katika juhudi za kulinda mazingira na kwamba wao ndio mabalozi wa baadaye wa mazingira watakaosaidia kuendeleza agenda ya maendeleo endelevu kwa manufaa ya taifa na vizazi vijavyo.
Share:

Video Mpya : LUPEMBE LIMBU - NSIYA

 

Share:

MRADI WA VISIMA VYA GESI MNAZI BAY WAONGEZA UZALISHAJI, WANANCHI WANUFAIKA


Mradi wa uchorongaji wa visima vitatu vya gesi asilia unaoendelea katika Kitalu cha Mnazi Bay kilichopo Mkoani Mtwara umeleta manufaa makubwa kwa wananchi na Taifa kwa ujumla kufuatia utekelezaji wenye mafanikio.

Mradi huo unaohusisha uchorongaji wa visima viwili vya uzalishaji na kimoja cha utafutaji ulianza kutekelezwa Februari 06, 2026 ambapo hadi kufikia Juni 05, 2026, uchorongaji wa visima viwili vya uzalishaji vilivyopewa majina ya MB5 na MS2 ulikuwa umekamilika na uchorongaji wa kisima cha tatu kilichopewa jina la KASA-1X ulikuwa unaendelea.

Miongoni mwa manufaa yaliyopatikana kufuatia utekelezaji huo ni pamoja na kuongezeka kwa uzalishaji wa gesi asilia kutoka katika Kitalu cha Mnazi Bay ambapo kisima cha MB5 kimeongeza uzalishaji kwa wastani wa futi za ujazo milioni 40 kwa siku na kisima cha MS2 ambacho bado kinafanyiwa majaribio kinatarajiwa kuongeza ujazo mwingine zaidi wa uzalishaji wa gesi asilia.

Ongezeko hili la uzalishaji wa gesi asilia umewezesha uwepo wa gesi zaidi kwa matumizi ya uzalishaji umeme, viwandani, kwenye vyombo vya usafiri (magari na bajaji) na majumbani.

Kwa wananchi, mradi umeleta fursa za ajira na utoaji wa huduma na bidhaa zinazohitajika ambapo zaidi ya watanzania 320 wameajiriwa katika nafasi mbalimbali na kandarasi zanye thamani ya zaidi ya bilioni 20 za kitanzania zimeenda kwa watoa huduma wakitanzania.

Kwa upande wa uwekezaji, utekelezaji wa mradi huu pamoja na miradi mingine ya utafutaji wa mafuta na gesi asilia inayoendelea umeongeza imani kwa wawekezaji ndani na nje ya nchi kuhusu uhai wa sekta ndogo ya mafuta na gesi asilia nchini

Kukamilika kwa mradi huu wa uchorongaji wa visima vitatu kutaifanya Tanzania kuwa na idadi ya visima 99 vilivyochorongwa tangu kuanza kwa shughuli za utafutaji wa mafuta na gesi asilia nchini kutoka visima 96 vilivyokuwepo awali.
Share:

SERIKALI KUENDELEA UBORESHA NA KUJENGA MIUNDOMBINU YA UVUVI






NA MWANDISHI WETU – SONGEA

Serikali inaendelea kuboresha na kujenga Miundombinu ya uvuvi ikiwemo masoko ,maghala ya kuhifadhia mazao ya uvuvi, vichanja vya kukaushia samaki maghala ya kuhifadhia mazao ya uvuvi na viwanda vya kuchakata mazao ya uvuvi na teknolojia rafiki za ukaushaji ili kubadilisha sekta hiyo kutoka ufugaji na ukulima mdogo kuelekea katika kuimarisha lishe na uchumi wa wakulima wadogo wanaojikita katika uzalishaji na ukuzaji wa viumbe maji nchini ambapo matokeo hayo yanatarajia kuchochea uchumi wa wananchi na taifa kwa ujumla.



Hayo yameelezwa na Bw. Jumanne Mwankoo Kaimu katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma wakati wa tukio la kuhakiki taarifa ya matokeo ya mwisho ya mradi wa kuimarisha lishe kwa wakuzaji wadogo wa viumbe maji (ARNSA) uliokuwa ukiratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge Uratibu wenye Ulemavu kwa msaada wa Shirika la NORAD kupitia Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo Duniani IFAD tarehe 5 Juni 2026.Bw. Mwankoo alisema kuwa Mradi huo wa kikanda uliokuwa katika Nchi za Tanzania, Kenya na Msumbiji na kutekelezeka katika Mikoa ya Lindi Mtwara na Ruvuma nchini,



Ambao umetoa mchango mkubwa katika sekta ya uvuvi ambayo imechangia takribani asilimia 69% ya protini katika lishe bora, uzalishaji wa mazao ya viumbe maji sambamba na ongezeko la ajira kwa vijana na wanawake na kuimarisha lishe kwa wakuzaji wadogo wa viumbe maji, hususan wakulima wa mwani na wafugaji wa samaki katika Halmashauri za Mtama, Ruangwa Songea na Mbinga



Akiongea wakati wa kufunga mradi huo wa Lishe, Mratibu wa Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na wenye Ulemavu Bw. Salimu Mwinjaka Alisema kuwa, mradi huo wa miaka miwili ulijikita zaidi katika katika kilimo cha mwani na uzalishaji wa viumbe maji ulifanikiwa kwa kiasi kikubwa kwani wanufaika wa mdari huo bado wanaendelea na shughuli hizo za uzalishaji kwa kutumia teknolojia za kisasa na ubunifu waliojijengea.








Kwa pande wake Mkurugenzi wa Ukuzaji viumbemaji toka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt Nazaeli Madala alieleza kuwa, Serikali imeweka msisistizo katika kukuza uchumi na mikoa iliyotekeleza mradi huo imeweza kukuza uchumi.








‘Mkoa hiyo imebahatika kupata ardhi nzuri na imekuwa fursa ya kuweza kufuga na kupata chakula na kuwauzia wengine chakula, kupata uzalishaji ulio na tija pamoja na uzalishaji Ajira na huu ndo msukomo wa Serikali.” Alibainisha Dkt Madala.
Aidha Aliwaasa wanufaika wa Mradi huo kuwapatia wengine ujuzi walioupata na kuwa waaminifu wanapopata mikopo kupitia Bank ya Kilimo nchini TADB kwa kuirejesha kwa wakati kwa amendeleo ya Taifa.Afisa Uvuvi kutoka Cameroon Bi Audrely Tchoundi aliwapongeza wafugaji wa Tanzani kwa kuwa wabunifu katika eneo la ufungaji viumbemaji na ukulima wa mwani kwa kutumia mbinu mbadala akitolea mfano wakulima wa Mwani wa Kijiji cha Shuka Mkoani Lindi, pamoja na usimamizi mzuri wa mabwawa ya samaki.



Mmoja wa wanufaika wa Mradi huo mwakilishi wa vijana Bw. Innocent Kikiwa Amesema kuwa mradi huo umemuwezesha yeye kama kijana kuweza kupata uzoefu katika eneo la Ufugaji Viumbemaji na kilimo cha mwani, kuweza kujiajiri kukuza mnyororo wa thamani kwa kuuza mazao yatokanayo na zao la mwani, kuuza samaki anaowafuga pamoja na kutafuta masoko.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger