Wednesday, 28 January 2026

KIJANA APITIA MATESO MAZITO LAKINI AKAJA KUWA MTU MAARUFU DUNIANI



Nilizaliwa kwenye familia ya kawaida sana, bila jina, bila mtaji, na bila mtu wa kunisukuma mbele. Wakati wenzangu walionekana kuwa na mwelekeo maishani, mimi nilikuwa napambana na umaskini, kejeli na kukataliwa kila mahali nilipojaribu.

Shuleni nilidharauliwa, mitaani nilionekana kama asiye na maana, na hata nyumbani nilionekana kama mzigo. Kila nilipoonyesha ndoto zangu, watu walicheka. Mateso yangu hayakuishia hapo. Nilipofika utu uzima, nilipitia kushindwa mara kwa mara.

Kazi nilikosa, miradi ilifeli, marafiki walinigeuka. Nililala njaa siku kadhaa, nikihama makazi mara kwa mara, nikiishi kwa msaada wa watu. Kilichoniumiza zaidi ni kwamba nilikuwa na kipaji, lakini kilionekana kama kimefungwa.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO JANUARI 28,2026




Magazeti






Share:

Tuesday, 27 January 2026

TWIGA, TANGA CEMENT WAPEWA SAA 48 KUJISALIMISHA




•Watakiwa kusimamia bei elekezi

• Wachimbaji wadogo watakiwa kutulia

DODOMA | Januari 26, 2026

SERIKALI kupitia Wizara ya Madini imezipa Kampuni za Twiga Cement na Tanga Cement saa 48 kufika mbele ya mamlaka husika na kujibu hoja zinazowakabili, ikiwemo madai ya kukiuka bei elekezi za madini zinazotolewa na Serikali na kukosa mikataba kwa wauzaji wa malighafi viwandani.

Akizungumza leo katika kikao cha wachimbaji wadogo wa madini ya Jasi (gypsum) kutoka Same mkoani Kilimanjaro kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Gold, Ofisi za Tume ya Madini jijini Dodoma, Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Dkt. Steven Kiruswa, amesema kampuni hizo zikikaidi wito huo, Serikali itachukua hatua kali ikiwemo kusimamisha shughuli zao.

“Kitendo cha kukaidi wito wa Serikali ni kuidharau mamlaka. Wasipofika ndani ya saa 48, tutamshauri Waziri kufuta leseni zao,” amesema Mhe. Dkt. Kiruswa.

Amesisitiza kuwa kampuni hizo zinapaswa kulipa wasambazaji wa madini ya jasi kwa kuzingatia bei elekezi iliyowekwa na Serikali, kutoa mikataba ya kazi kwa wauzaji wa bidhaa, na kuacha kununua kwa bei ya chini inayowaumiza wachimbaji wadogo.

Kauli hiyo imekuja kufuatia malalamiko ya wachimbaji wadogo wa madini ya jasi wa Wilaya ya Same, wakidai kuwa kampuni hizo zinakinyima kazi Chama cha Ushirika cha Wachimbaji Wadogo wa Madini ya Jasi (Kilimanjaro Gypsum Cooperative Society Ltd), na badala yake kushirikiana na watu binafsi wachache wanaolipwa chini ya bei elekezi na bila mikataba.

“Mnaokubali kuuza madini yenu kwa bei ya chini mnajipiga misumari wenyewe. Bei elekezi iheshimiwe,” amesisitiza Mhe.  Dkt. Kiruswa, huku akiwataka wachimbaji kutulia wakati Serikali ikishughulikia changamoto hiyo

Aidha, Naibu Waziri amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Same, Kasilda Mgeni, kuipeleka TAKUKURU kuchunguza madai ya rushwa yanayodaiwa kujitokeza katika viwanda hivyo.

Awali, Kamishna wa Tume ya Madini, Dkt. Theresia Numbi, amesema utoaji wa mikataba ni takwa la kisheria, si hiari.
“Ni lazima Chama cha Ushirika kishirikishwe. Toeni asilimia kwa Chama, na nyingine muwape wale mnaowataka kufanya nao kazi,” amesema.

Kwa upande wake, Meneja Uwezeshaji Uchimbaji Mdogo, Nchagwa Marwa, kutoka Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) amesema uchimbaji ni sekta jumuishi, akiongeza kuwa kuwa kumpendelea mtu mmoja na kukiacha Chama si mwelekeo sahihi.

“Msimamo wa Serikali ni kila Mtanzania anufaike na rasilimali madini. Ndiyo maana kauli mbiu ni Madini ni Maisha na Utajiri. Bei elekezi iheshimiwe,” amesema.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Msafiri Mbibo, amezitaka kampuni kufuata taratibu za utoaji wa oda akisisitiza kuwa Serikali inatoa upendeleo kwa wazawa na matarajio ni wawekezaji kuwalinda wananchi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Same, Kasilda Mgeni, amelaani vikali hatua ya kampuni hizo kudharau wito wa Serikali, akidai hali ya usalama katika maeneo ya Makanya na Ruvu Kajiungeni imeathirika kutokana na mgawanyiko miongoni mwa wachimbaji.

“Viongozi wote tumekuja, Madiwani, Mkurugenzi, Katibu Tawala wa Wilaya kwa lengo la kumaliza mgogoro na kurejesha amani. Kudharau huku ni kudharau Serikali na hata dhamana ya Mheshimiwa Rais. Wizara ichukue hatua stahiki, hata ikibidi kuzisimamisha shughuli za viwanda hadi suluhu ipatikane,” amesema.

Serikali imesisitiza itaendelea kulinda maslahi ya wachimbaji wadogo, kusimamia bei elekezi, na kuhakikisha sekta ya madini inakuwa jumuishi kwa manufaa ya Watanzania wote.












Share:

WAASISI CCM RUVUMA WATOA WITO WA KUZINGATIA KATIBA NA KUWASIKILIZA WANACHAMA WA NGAZI ZA CHINI

Katibu wa CCM Kata ya Mjini Bi Mikaela Komba akimkabidhi muasisi wa tawi la Mjini Bi Janet Mangula au Mama Mhagama walipomtembelea nyumbani kwake kama ishara ya kuwaenzi waasisi wa chama cha mapinduzi CCM kutambua mchango wao mkubwa katika ujenzi na uhai wa Chama Cha Mapinduzi
Bi Marry Nyanjako muasisi wa CCM kutoka Tawi la Mashujaa kata ya mjini akiwa amekaa nyumbani kwake baada ya kutembelewa na viongozi wa kata ya mjini ukiongozwa na Diwani wa Kata hiyo Mathew Ngalimanayo pichani hayupo

Na Regina Ndumbaro Songea-Ruvuma

Waasisi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Ruvuma wamewataka wanachama na viongozi wa chama hicho kuzingatia Katiba, Sheria na Kanuni za CCM ili kukiendeleza na kukilinda chama, hasa katika kipindi hiki cha kuelekea maadhimisho ya miaka 49 tangu kuanzishwa rasmi kwa CCM tarehe 5 Februari 1977.

Wito huo umetolewa wakati wa ziara za kuwatembelea waasisi wa chama katika matawi yao mbalimbali ndani ya Manispaa ya Songea, hususan Kata ya Mjini.

Muasisi wa CCM Bi. Marry Nyanjako amesema chama hakina tatizo bali changamoto zinatokana na wanachama na viongozi kushindwa kuzingatia misingi ya Katiba, Sheria na Kanuni za chama.

Amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa juhudi kubwa anazozifanya kukiongoza chama na taifa, huku akisisitiza umuhimu wa viongozi kushuka chini kuwasikiliza wanachama na kutatua kero zao.

Bi. Marry amekumbusha desturi za zamani enzi za Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambapo maadhimisho ya CCM yalihusisha kusikiliza wananchi moja kwa moja, akisisitiza kuwa chama huanzia ngazi za chini na ndipo hupatikana suluhisho la changamoto zake.

Kwa upande wake, Mzee Ndauka, muasisi wa CCM kutoka Tawi la Mahenge C, amesema kuwa chimbuko la CCM na maendeleo ya taifa lipo chini, hivyo mabalozi wa mashina na viongozi wa msingi wana wajibu mkubwa wa kulinda amani na mshikamano wa nchi.

Amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anajitahidi kwa kiwango kikubwa, lakini mafanikio ya juhudi hizo yanategemea ushirikiano wa viongozi wa ngazi za chini kwa kutekeleza Ilani ya CCM, kufanya vikao vya mara kwa mara na kufuatilia wageni wanaoingia na kutoka katika maeneo yao.

Katika kuonesha mshikamano na kuthamini mchango wa waasisi, uongozi wa CCM Kata ya Mjini ukiongozwa na Katibu wa Kata hiyo Mikaela Komba pamoja na Diwani wa Kata ya Mjini, Mathew Ngalimanayo, uliwakabidhi zawadi waasisi wa chama kama ishara ya upendo, heshima na kutambua mchango wao mkubwa katika ujenzi na uhai wa Chama Cha Mapinduzi.Katibu wa kata ya mjini Bi Mikaela Komba Akizungumza baada ya kumkabidhi muasisi wa chama cha mapinduzi CCM tawi la Mpambalioto iliyopo katika Kata ya Mjini

Share:

CCM MIAKA 49: WAZAZI WAONGOZA MAPAMBANO YA UTUNZAJI MAZINGIRA SHINYANGA MJINI

Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga, Bi. Regina Ndutu, akipanda mti katika Shule ya Msingi Ujamaa, Seseko, Kata ya Mwamalili, Manispaa ya Shinyanga.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga, Bi. Regina Ndulu, akipanda mti katika Shule ya Msingi Ujamaa, Seseko, Kata ya Mwamalili, Manispaa ya Shinyanga.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mzee Fue Mrindoko, akipanda mti ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 49 ya CCM.
Katibu wa UVCCM Wilaya ya Shinyanga Naibu Katalambula akipanda mti.

Na Mwandishi wetu - Malunde 1 blog

Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga Mjini imeendelea kuthibitisha dhamira ya CCM ya kuunganisha siasa na maendeleo endelevu kwa vitendo, baada ya kushiriki shughuli za kijamii zenye mguso wa moja kwa moja kwa jamii, ikiwemo zoezi la upandaji miti katika Shule ya Msingi Ujamaa iliyopo Seseko, Kata ya Mwamalili, Manispaa ya Shinyanga.

Shughuli hiyo imefanyika leo Januari 26, 2026, ikiwa ni sehemu ya wiki ya maadhimisho ya miaka 49 ya kuzaliwa kwa CCM, kwa lengo la kuhamasisha utunzaji wa mazingira, kupambana na athari za mabadiliko ya tabianchi pamoja na kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita katika kulinda na kuhifadhi mazingira kwa maendeleo endelevu ya taifa.

Akizungumza kama mgeni rasmi, Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga, Bi. Regina Ndulu, amewahimiza wanachama wa CCM na wananchi kwa ujumla kuendelea kushiriki kikamilifu katika upandaji miti na kuhakikisha miti hiyo inatunzwa, akisisitiza kuwa mazingira salama ni msingi wa ustawi wa jamii na uchumi wa taifa.

Bi. Regina amesema kuwa utunzaji wa mazingira ni ajenda ya kimkakati ya CCM, inayokwenda sambamba na falsafa ya chama ya kujenga taifa lenye uchumi imara, afya bora na maisha endelevu kwa kizazi cha sasa na kijacho.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Fue Mrindoko, amesema jumuiya hiyo itaendelea kuwa mstari wa mbele katika kuunga mkono juhudi za Serikali na chama katika nyanja za maendeleo ya kijamii, kiuchumi na kimazingira, akibainisha kuwa mazingira bora ni nguzo muhimu ya afya ya wananchi na ustawi wa jamii.

Mzee Fue ameongeza kuwa Jumuiya ya Wazazi CCM itaendelea kuwahamasisha wanachama wake kushiriki kikamilifu katika shughuli za uhifadhi wa mazingira, ikiwemo upandaji na utunzaji wa miti, kama njia ya kulinda vyanzo vya maji, kupunguza ukame na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Aidha, viongozi hao wametumia fursa hiyo kuipongeza Serikali kwa juhudi zake katika kusambaza na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia, ikiwemo mitungi ya gesi, wakisisitiza kuwa matumizi ya nishati safi ni mkakati muhimu wa kupunguza ukataji wa miti unaochangiwa na matumizi ya kuni na mkaa.

Wamesema kuwa nishati safi siyo tu inalinda mazingira, bali pia inaboresha afya za wananchi na kupunguza madhara ya kiafya yanayotokana na matumizi ya nishati zisizo rafiki kwa mazingira.

Kwa upande wao, baadhi ya wanachama wa Jumuiya ya Wazazi CCM wakiwemo wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji, wamesema wataendelea kushirikiana kwa karibu na Serikali pamoja na uongozi wa chama ili kuhakikisha wananchi wanashiriki na kunufaika na fursa mbalimbali za maendeleo, hususan katika sekta za mazingira, afya na maendeleo ya jamii.

Shughuli hiyo imeakisi mshikamano wa wanachama wa CCM katika kuenzi misingi ya chama chao kwa vitendo, huku maadhimisho ya miaka 49 ya CCM yakitafsiriwa kama fursa ya kuchochea uzalendo wa vitendo, kulinda mazingira na kuendelea kujenga taifa lenye maendeleo endelevu na ustawi wa wananchi.

Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga, Bi. Regina Ndulu, akizungumza na wanachama wakati wa maadhimisho ya miaka 49 ya CCM yaliyofanyika Wilaya ya Shinyanga Mjini.Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mzee Fue Mrindoko, akizungumza kuhusu umuhimu wa utunzaji wa mazingira na kuunga mkono juhudi za serikali.
Katibu wa Mbunge Jimbo la Shinyanga mjini Samwel Jackson akitoa salamu za mbunge wa jimbo hilo ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Paschal Patrobas Katambi.
Katibu wa UVCCM Wilaya ya Shinyanga Naibu Katalambula akizungumza kwa niaba ya katibu wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya hiyo.
Katibu wa UVCCM Wilaya ya Shinyanga Naibu Katalambula akizungumza kwa niaba ya katibu wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya hiyo.

Diwani wa kata ya Mwamalili Mhe. James Mdimi (Matinde) akizungumza kwenye hafla hiyo.

Katibu wa UVCCM Wilaya ya Shinyanga Naibu Katalambula akizungumza kwa niaba ya katibu wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya hiyo.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger