Sunday, 18 January 2026

SAUTI ZA WANANCHI: AMANI NDIO MSINGI WA MAENDELEO NA JIBU KWA MIHEMKO YA KISIASA NCHINI

Watanzania wamehimizwa kulinda amani, umoja, na mshikamano wa taifa kwa wivu mkubwa kama msingi pekee wa kujiletea maendeleo ya kweli, huku wakionywa kuwa pasipo utulivu hakuna maendeleo yanayoweza kupatikana. 

Kauli hizi zimetolewa na wananchi kutoka maeneo mbalimbali nchini, akiwemo Athumani Mkongota, mkazi wa Kibaha Mjini, ambaye amesisitiza kuwa mshikamano ndio nguzo inayolishikilia taifa. 

Mwelekeo huu wa kizalendo unakuja wakati ambapo mijadala ya kijamii imeongezeka kuhusu namna ya kudai haki bila kuhatarisha usalama, huku wananchi wakitakiwa kurudi katika kujitafakari na kuona ni kwa kiasi gani maisha yanaweza kubadilika na kuwa katika taharuki kubwa pindi amani inapotoweka.

Katika kile kinachoonekana kama funzo kutokana na matukio ya hivi karibuni, Daudi Inuka, mkazi wa Bariadi mkoani Simiyu, ametoa mwito wa kutafuta njia mbadala na bora za kudai haki badala ya kukimbilia vurugu ambazo mara nyingi huacha majeraha kwa jamii.

Maoni haya yanaungwa mkono na Musa Mseti ambaye amebainisha kuwa amani ndiyo kila kitu kwa sababu shughuli zote za kiuchumi na kijamii zinafanyika kwa ufanisi pale tu ambapo utulivu umetawala. Wananchi hao wamebainisha kuwa kushuhudia taharuki inayoweza kutokea kupitia vurugu kumejenga ufahamu mpya kuwa amani si jambo la kuchukulia mzaha, bali ni fursa muhimu inayopaswa kulindwa dhidi ya yeyote anayejaribu kuivuruga.

Mjadala huu umepata mwangwi mpana pia katika mitandao ya kijamii ambapo Watanzania wengi wameanza kuhoji nia ya mataifa ya nje, kama Marekani, wakiamini kuwa mataifa hayo mara nyingi huchochea vurugu nje ya ardhi yao huku yakilinda usalama wa ndani. 

Baadhi ya wachangiaji wamebainisha kuwa Tanzania ina akili nyingi na busara kuliko mataifa mengine mengi ya Afrika, na kwamba mabadiliko ya kweli yanapatikana kupitia maridhiano na njia za amani badala ya kufuata mikumbo ya vurugu. Hoja imekuwa ni kwamba, ingawa kuna madai ya haki au changamoto za kimaisha , njia ya kuivuruga nchi haijawahi kuwa suluhu ya kudumu, bali ni mtego unaoweza kumrudisha mwananchi nyuma kimaendeleo.

Hisia za wananchi zimejikita katika ukweli kuwa kufuata mikumbo ya kisiasa bila kutafakari kunaweza kuleta madhara makubwa kwa mtu mmoja mmoja. Watu wengi sasa wamechagua amani kama njia sahihi, wakiamini kuwa haki inaweza kupatikana bila kumwaga damu au kuharibu mali. Mwito uliotolewa kwa Watanzania wote ni kuendelea kuwa na uelewa mpana wa kijiopolitiki na kutambua kuwa kazi na utu ndizo silaha za kusonga mbele. Katika kipindi hiki cha mabadiliko, busara imeshinda mihemko, huku wananchi wakiazimia kusimama kidete kukataa ajenda zozote zinazolenga kuingiza taifa kwenye machafuko, wakitambua kuwa ukombozi wa kweli unajengwa juu ya misingi ya utulivu na siyo mabaki ya nchi iliyovurugika.

Share:

WAZIRI AWESO ATAKA KAZI ZIFANYIKE USIKU NA MCHANA KUKAMILISHA MRADI WA MAJI MKINGA

 

Na Oscar Assenga, MKINGA

WAZIRI wa Maji Jumaa Aweso amemtaka Mkandarasi anayetekeleza mradi wa Maji Mkinga – Horohoro kuhakikisha wanafanya kazi usiku na mchana kuukamilisha kwa wakati ili wananchi waweze kupata huduma ya maji safi na salama.

Aweso aliyasema hayo leo wakati wa halfa ya Mapokezi ya Vitendea kazi (Mabomba) vitakavyotumika katika utekelezaji wa Mradi wa Maji Mkinga-Horohoro ambao unagharimu kiasi cha Bilioni 35.



Halfa hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Tanga Uwasa,Dkt Ally Fungo,Mkurugenzi wa Tanga Uwasa Mhandisi Geofrey Hilly,Meneja wa Ruwasa Mkoa wa Tanga Mhandisi Upendo Lugongo pamoja na watumishi wa Tanga Uwasa,Ruwasa,Viongozi wa CCM na wananchi wa eneo la Manza.

Alisema kutokana na kwamba mradi huo ni muhimu kwa wananchi ambao wanakabiliwa na changamoto ya maji hivyo wahakikishe unakamalika kwa wakati na ujenzi wake uwe tofauti uende na maji katika maeneo yanayolazwa mabomba nao wapate maji.



“Tunajua tuna miradi mingi sana lakini nikuombe Katibu Mkuu utoe fedha ili mradi huo ukamilike kwa wakati ili wana Mkinga waweze kupata huduma ya maji safi na salama”Alisema



“Kama mnakumbuka tulimleta Rais Dkt Samia Suluhu aliweke kuweka jiwe la msingi kukamilika kwake tumuombe Rais aje kuzindua mradi huu wa Mkinga sababu ndio muasisi na ndio aliyweka jiwe la msingi”Alisema

Waziri Aweso aliwataka wafanye kazi hiyo kwa uadilifu na uaminifu ili kuhakikisha hiyo kazi inakamilika na wana Mkinga waweze kupata maji safi na salama



Hata hivyo Waziri huyo alimuahidi Mbunge wa Jimbo la Mkinga Twaha Mwakiojakwamba watafanya kazi kuhakikisha wanakamilisha mradi huo kutokana na kwamba wapo baadhi ya watumishi wanaishi Tanga kutokana na changamoto ya maji wakikamilisha mradi huo watapata maendeleo makubwa.


Alisema maendeleo hayo yatapatikana kwa wana Mkinga na wawekezaji mbalimbali watakwenda kuwekeza hiyo kazi wameibeba na kufanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha mradi unakamilika.


Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Gilbert Kailima alisema wanaishukuru Serikali kutokana na kwamba mradi huo ni mkombozi mkubwa kwa wananchi wa wilaya ya Mkinga na utaondoa adha kubwa ya Maji.


Alisema wanamshukuru Rais kwa kutoa kipaumbele sana katika mradi huo na ndio maana alikuja kuweka jiwe la Msingi katika mradi huo na kuhaidi watajitahidi kusimamia mradi huo kwa karibu kwa kushirikiana na Tanga Uwasa ili utekelezwe kwa wakati ili uanze kufanya kazi kama Rais anavyotamani iwe pamoja nawe.

Aidha alisema katika wilaya hiyo wana miradi mengine mikubwa iliyopo wilayani humo ikiwemo wa Gombero, Mapatano, Muhinduro na Bamba Mwarongo yote ni mikubwa ambayo Serikali chini ya Wizara ya Maji inaendelea kutenga fedha kwa ajili ya utekelezaji wake na ipo katika hatua mbalimbali.


“Kutokana na kwamba umefika leo tunaomba nayo hii miradi waone namna gani inaweza kuisha kwa wakati kama ambavyo wananchi wa Mkinga wanatamani iwe tunaimani sana na utendaji wako na katibu mkuu wa wizara ya Maji “Alisema.


Alitoa wito kwa wananchi wa wilaya hiyo kutoa ushirikiano kwa mkaandarasi ambaye atatoa huduma ya usambazaji wa maji katika mradi huo na kuhakikisha vifaa vyake havihujumiwi badala yake wawe walinzi ili kufanya kazi yake vizuri.

Naye kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Mkinga (CCM) Twaha Mwakioja alisema kwamba katika taifiti iliyofanywa changamoto kubnwa inawakabili zaidi ya wananchi asilimia 80 wamelalamikia hali ya upatikanaji wa maji.



Alisema kwamba mradi huo kabla ya kuanza kutekelezwa wastani wa upatikanaji wa maji katika wilaya ya Mkinga ni asilimia 60 mpaka 69 hivyo wana imani mradi huo utakapokamilika upatinaji wa maji utafika zaidi ya asilimia 88 mradi huo ni mkombozi mkubwa kwao.

Aidha alisema kwamba mradi huo utakakamilika zaidi ya vijiji 37 vinakwenda kupata maji safi na salama ya uhakika na Serikali imeweka fedha nyingi ili kuhakikisha unakamilika ili wananchi waweze kuondokana na adha ya maji.

“Mhe Waziri tunaomba mradi huu kwa maana umesuasua kwa mude mrefu kama unavyotambua upo nyuma zaidi ya miaka miwili na ifikapo julai mradi uwe umekamilika hivyo tunashukuru na wananchi wana mategemeo makubwa sana “Alisema

Mwisho

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JANUARI 18,2026





Magazeti


Share:

Saturday, 17 January 2026

MCHINJITA AONYA SIASA ZA MIHEMKO, APINGA MIITO YA MAPINDUZI YA KIJESHI NA UTEGEMEZI WA MATAIFA YA NJE

 
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo (Bara), Isihaka Mchinjita, ametoa onyo kali dhidi ya kile alichokiita "kugota kifikiri" kwa baadhi ya taasisi na viongozi wa kisiasa wanaohamasisha mapinduzi ya kijeshi au kutegemea mataifa ya nje kuleta mabadiliko nchini Tanzania. 

Akizungumza Januari 15, 2026, jijini Tanga katika ziara yake ya kikazi ya kukutana na viongozi na wajumbe wa jimbo la Tanga Mjini, Mchinjita amebainisha kuwa harakati za kisiasa zinapaswa kujikita katika kutengeneza mbadala wa kufikiri na uungwaji mkono wa umma badala ya kutamani njia za mkato zinazoweza kuliingiza Taifa katika majanga makubwa zaidi.

Akirejea matukio yaliyofuata baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, Mchinjita ameweka wazi kuwa hakushuhudia maandamano ya dhati yenye uongozi madhubuti wa kisiasa, bali aliona matukio yaliyokosa uratibu wa taasisi na vurugu. 

Amewashangaa wadau wa kisiasa wanaofikiria kuwa mapinduzi ya kijeshi yanaweza kuwa nafuu kwa nchi, akisisitiza kuwa utawala wa kiraia, licha ya changamoto zake, unaruhusu uhuru wa kukosoa. Amewakumbusha Watanzania kuwa chini ya uongozi wa kijeshi, matumizi ya nguvu na risasi ni sehemu ya utamaduni wa madaraka, na kwamba mataifa yaliyopitia njia hiyo yameshuhudia ukatili na unyama uliokithiri ambao hauruhusu hata nafasi ya kutoa maoni.

Mchinjita amekosoa vikali tabia ya baadhi ya wanaharakati wa mitandaoni na wanasiasa wanaoshabikia uingiliaji kati wa mataifa ya nje, kama vile Marekani, katika masuala ya ndani ya mataifa mengine. 

Ameeleza kuwa ni kosa kubwa la kifikira kudhani kuwa maslahi ya Watanzania yatalindwa na viongozi wa kigeni, akitolea mfano wa miito ya kutaka mataifa hayo yaingilie kati Tanzania kama ilivyotokea Venezuela. 

Amesema kuwa taasisi yoyote ya kisiasa inayotafuta "miujiza" kutoka nje imepoteza mwelekeo wa safari yake, kwani ukombozi wa kweli unapaswa kuanzia ndani kupitia kujipanga, kuhamasisha umma, na kujenga nishati ya wananchi wenyewe kuwa tayari kupigania mustakabali wao.

Kiongozi huyo ametoa mwito kwa viongozi wa kisiasa nchini kujitathmini na kuchukua hatua zitakazorejesha imani ya umma kwao. 

Amesititiza kuwa jukumu la kiongozi ni kusimama mbele na kuongoza safari ya mabadiliko kwa vitendo na hoja mbadala zinazotekelezeka, badala ya kukaa na kusubiri matukio ya kusadikika. 

Amesema kuwa harakati za kisiasa ni mchakato endelevu unaohitaji uvumilivu na mkakati wa muda mrefu, na kwamba ACT-Wazalendo itaendelea kusimamia njia za kidemokrasia na kistaarabu katika kudai haki na maendeleo ya Watanzania bila kuhatarisha amani ya nchi.


Share:

VIJANA 5,746 WACHAGULIWA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA UANAGENZI


Na: OWM (KAM) – Dodoma

Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano imetangaza vijana 5,746 kujiunga na mafunzo ya uanagenzi ambayo yatawawezesha kupata ujuzi wa vitendo utakao wasaidia kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi kwa kujiajiri na kuajiri wenzao.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Clement Sangu wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari uliofanyika leo Januari 16, 2026, Jijini Dodoma ukilenga kuelezea vijana waliochaguliwa kushiriki mafunzo ya Uanagenzi kwa mwaka 2025/2026.

Aidha, amesema mafunzo hayo yanafadhiliwa na Serikali kwa asilimia 100.

Mhe. Sangu amesema, mafunzo hayo ya ufundi stadi yatatolewa katika vyuo 47 nchini kupitia fani za ubunifu wa mitindo na ushonaji nguo, ufundi bomba, uashi, useremala, uchomeleaji na uungaji vyuma, upakaji rangi na maandishi ya alama, upishi, utengenezaji wa vipuri vya mitambo, ufundi magari na mitambo, umeme wa majumbani na viwandani, umeme wa magari, huduma za hoteli na utalii, ukataji madini na ufundi vyuma.

“Fani hizi ni muhimu sana kwa vijana wetu, kwa kuwa zitawawezesha kupata ujuzi ambao utawawezesha kuajiriwa au kujiajiri,” amesema

Vilevile amesema kuwa, Serikali inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeendelea kuweka mikakati na kutekeleza afua mbalimbali zitakazowezesha kuwa na jamii yenye ustawi na kujenga nguvu kazi yenye ujuzi utakao wawezesha kushindana katika soko la ajira ndani na nje ya nchi.

Amesema, afua hizo ni pamoja na utekelezaji wa Programu ya Taifa ya Kukuza Ujuzi kwa njia ya Uanagenzi inayolenga kuimarisha nguvukazi ya taifa ili kumudu ushindani katika soko la ajira la ndani na nje ya nchi kwa kupata ujuzi unaoendana na mahitaji ya soko la ajira na hatimaye kuweza kuajiriwa au kujiajiri.

Kadhalika, Waziri Sangu amevitaka vyuo vilivyopata dhamana ya kutoa mafunzo hayo, kutoa ushirikiano kwa vijana waliochaguliwa, kuwafundisha na kuwasimamia vyema kipindi chote cha mafunzo yao. Pia, ametoa wito kwa vijana waliochaguliwa kushiriki mafunzo kusoma kwa bidii, kuwa na nidhamu na kufuata sheria na taratibu za vyuo.
Share:

WATUMISHI WAPYA TASAC WATAKIWA KUZINGATIA MAADILI YA UTUMISHI WA UMMA




Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania- TASAC Bw. Mohamed Salum leo tarehe 16 Januari, 2026 amehitimisha rasmi mafunzo kwa watumisi wapya 25 yaliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.


Wakati akifunga mafunzo hayo, Mkurugenzi Mkuu amewaasa watumishi hao kuzingatia maadili ya utumishi wa umma, nidhamu ya kazi, ushirikiano na ubunifu katika kazi.


“Ndugu watumishi, napenda kuwakumbusha na kuwasisitiza kuhusu umuhimu wa kuzingatia maadili katika utumishi wa umma, nidhamu kazini, ushirikiano na kuendelea kujifunza kwakuwa Sekta ya usafiri kwa njia ya maji inakuwa kwa kasi sana kutokana na mabadiliko ya kiteknolojia” amesema Bw. Salumu.


Pia, amewasihi kuzingatia kanuni na miongozo katika kutekeleza majukumu yao.

“Napenda mtambue yakuwa mmepewa dhamana kubwa na serikali hivyo ni vema kuzingatia Kanuni, Sheria, Taratibu na Miongozo mbalimbali inayosimamia utumishi wa Umma ikiwa ni pamoja na kutunza siri, nidhamu na utii kwa viongozi wa serikali, kuendeleza mashirikiano, kutoa huduma bora kwa wateja, kulinda mali za Shirika pamoja na kufuata sheria na miongozo inayoongoza utekelezaji wa majukumu ya TASAC.


Mwisho Mkurugenzi Mkuu aliwakaribisha watumishi wapya TASAC na kuwatakia utekelezaji mwema wa Majukumu yao.




Mafunzo yalikuwa ya siku 14 ambapo watumishi hao wali kabidhiwa vyeti vya ushiriki na kukaribishwa katika utumishi wa umma.



Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JANUARI 17,2026


Magazetini



 


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger