
Wednesday, 28 January 2026
KIJANA APITIA MATESO MAZITO LAKINI AKAJA KUWA MTU MAARUFU DUNIANI

Tuesday, 27 January 2026
TWIGA, TANGA CEMENT WAPEWA SAA 48 KUJISALIMISHA













WAASISI CCM RUVUMA WATOA WITO WA KUZINGATIA KATIBA NA KUWASIKILIZA WANACHAMA WA NGAZI ZA CHINI
Katibu wa CCM Kata ya Mjini Bi Mikaela Komba akimkabidhi muasisi wa tawi la Mjini Bi Janet Mangula au Mama Mhagama walipomtembelea nyumbani kwake kama ishara ya kuwaenzi waasisi wa chama cha mapinduzi CCM kutambua mchango wao mkubwa katika ujenzi na uhai wa Chama Cha Mapinduzi
Bi Marry Nyanjako muasisi wa CCM kutoka Tawi la Mashujaa kata ya mjini akiwa amekaa nyumbani kwake baada ya kutembelewa na viongozi wa kata ya mjini ukiongozwa na Diwani wa Kata hiyo Mathew Ngalimanayo pichani hayupoNa Regina Ndumbaro Songea-Ruvuma
Waasisi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Ruvuma wamewataka wanachama na viongozi wa chama hicho kuzingatia Katiba, Sheria na Kanuni za CCM ili kukiendeleza na kukilinda chama, hasa katika kipindi hiki cha kuelekea maadhimisho ya miaka 49 tangu kuanzishwa rasmi kwa CCM tarehe 5 Februari 1977.
Wito huo umetolewa wakati wa ziara za kuwatembelea waasisi wa chama katika matawi yao mbalimbali ndani ya Manispaa ya Songea, hususan Kata ya Mjini.
Muasisi wa CCM Bi. Marry Nyanjako amesema chama hakina tatizo bali changamoto zinatokana na wanachama na viongozi kushindwa kuzingatia misingi ya Katiba, Sheria na Kanuni za chama.
Amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa juhudi kubwa anazozifanya kukiongoza chama na taifa, huku akisisitiza umuhimu wa viongozi kushuka chini kuwasikiliza wanachama na kutatua kero zao.
Bi. Marry amekumbusha desturi za zamani enzi za Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambapo maadhimisho ya CCM yalihusisha kusikiliza wananchi moja kwa moja, akisisitiza kuwa chama huanzia ngazi za chini na ndipo hupatikana suluhisho la changamoto zake.
Kwa upande wake, Mzee Ndauka, muasisi wa CCM kutoka Tawi la Mahenge C, amesema kuwa chimbuko la CCM na maendeleo ya taifa lipo chini, hivyo mabalozi wa mashina na viongozi wa msingi wana wajibu mkubwa wa kulinda amani na mshikamano wa nchi.
Amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anajitahidi kwa kiwango kikubwa, lakini mafanikio ya juhudi hizo yanategemea ushirikiano wa viongozi wa ngazi za chini kwa kutekeleza Ilani ya CCM, kufanya vikao vya mara kwa mara na kufuatilia wageni wanaoingia na kutoka katika maeneo yao.
Katika kuonesha mshikamano na kuthamini mchango wa waasisi, uongozi wa CCM Kata ya Mjini ukiongozwa na Katibu wa Kata hiyo Mikaela Komba pamoja na Diwani wa Kata ya Mjini, Mathew Ngalimanayo, uliwakabidhi zawadi waasisi wa chama kama ishara ya upendo, heshima na kutambua mchango wao mkubwa katika ujenzi na uhai wa Chama Cha Mapinduzi.




Katibu wa kata ya mjini Bi Mikaela Komba Akizungumza baada ya kumkabidhi muasisi wa chama cha mapinduzi CCM tawi la Mpambalioto iliyopo katika Kata ya MjiniCCM MIAKA 49: WAZAZI WAONGOZA MAPAMBANO YA UTUNZAJI MAZINGIRA SHINYANGA MJINI
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mzee Fue Mrindoko, akipanda mti ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 49 ya CCM.Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga Mjini imeendelea kuthibitisha dhamira ya CCM ya kuunganisha siasa na maendeleo endelevu kwa vitendo, baada ya kushiriki shughuli za kijamii zenye mguso wa moja kwa moja kwa jamii, ikiwemo zoezi la upandaji miti katika Shule ya Msingi Ujamaa iliyopo Seseko, Kata ya Mwamalili, Manispaa ya Shinyanga.
Shughuli hiyo imefanyika leo Januari 26, 2026, ikiwa ni sehemu ya wiki ya maadhimisho ya miaka 49 ya kuzaliwa kwa CCM, kwa lengo la kuhamasisha utunzaji wa mazingira, kupambana na athari za mabadiliko ya tabianchi pamoja na kuunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita katika kulinda na kuhifadhi mazingira kwa maendeleo endelevu ya taifa.
Akizungumza kama mgeni rasmi, Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga, Bi. Regina Ndulu, amewahimiza wanachama wa CCM na wananchi kwa ujumla kuendelea kushiriki kikamilifu katika upandaji miti na kuhakikisha miti hiyo inatunzwa, akisisitiza kuwa mazingira salama ni msingi wa ustawi wa jamii na uchumi wa taifa.
Bi. Regina amesema kuwa utunzaji wa mazingira ni ajenda ya kimkakati ya CCM, inayokwenda sambamba na falsafa ya chama ya kujenga taifa lenye uchumi imara, afya bora na maisha endelevu kwa kizazi cha sasa na kijacho.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Fue Mrindoko, amesema jumuiya hiyo itaendelea kuwa mstari wa mbele katika kuunga mkono juhudi za Serikali na chama katika nyanja za maendeleo ya kijamii, kiuchumi na kimazingira, akibainisha kuwa mazingira bora ni nguzo muhimu ya afya ya wananchi na ustawi wa jamii.
Mzee Fue ameongeza kuwa Jumuiya ya Wazazi CCM itaendelea kuwahamasisha wanachama wake kushiriki kikamilifu katika shughuli za uhifadhi wa mazingira, ikiwemo upandaji na utunzaji wa miti, kama njia ya kulinda vyanzo vya maji, kupunguza ukame na kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.
Aidha, viongozi hao wametumia fursa hiyo kuipongeza Serikali kwa juhudi zake katika kusambaza na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia, ikiwemo mitungi ya gesi, wakisisitiza kuwa matumizi ya nishati safi ni mkakati muhimu wa kupunguza ukataji wa miti unaochangiwa na matumizi ya kuni na mkaa.
Wamesema kuwa nishati safi siyo tu inalinda mazingira, bali pia inaboresha afya za wananchi na kupunguza madhara ya kiafya yanayotokana na matumizi ya nishati zisizo rafiki kwa mazingira.
Kwa upande wao, baadhi ya wanachama wa Jumuiya ya Wazazi CCM wakiwemo wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji, wamesema wataendelea kushirikiana kwa karibu na Serikali pamoja na uongozi wa chama ili kuhakikisha wananchi wanashiriki na kunufaika na fursa mbalimbali za maendeleo, hususan katika sekta za mazingira, afya na maendeleo ya jamii.
Shughuli hiyo imeakisi mshikamano wa wanachama wa CCM katika kuenzi misingi ya chama chao kwa vitendo, huku maadhimisho ya miaka 49 ya CCM yakitafsiriwa kama fursa ya kuchochea uzalendo wa vitendo, kulinda mazingira na kuendelea kujenga taifa lenye maendeleo endelevu na ustawi wa wananchi.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mzee Fue Mrindoko, akizungumza kuhusu umuhimu wa utunzaji wa mazingira na kuunga mkono juhudi za serikali.
























