Sunday, 26 April 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI APRILI 26,2026

Magazeti






 
Share:

WANANCHI SHINYANGA WAPOKEA RIPOTI YA JAJI CHANDE KWA MATUMAINI YA MARIDHIANO

Wananchi wa mkoa wa Shinyanga wamepokea kwa mtazamo chanya ripoti ya Tume ya Rais ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani, wakieleza kuwa inaweza kuwa chachu ya kuimarisha umoja, amani na maridhiano nchini.

Wananchi hao wamesema wanaamini kuwa utekelezaji wa mapendekezo yaliyomo kwenye ripoti hiyo utasaidia kurejesha mshikamano wa kitaifa na kuzuia kujirudia kwa matukio ya uvunjifu wa amani siku zijazo.

Akizungumza kuhusu ripoti hiyo iliyowasilishwa na Mwenyekiti wa Tume, Mohamed Chande Othman, mmoja wa wakazi wa Shinyanga Mjini, Chief Abdallah Sube, amesema ameipokea vizuri kwa kuwa inalenga kuponya majeraha yaliyosababishwa na matukio ya uvunjifu wa amani.


“Nimeipokea vizuri ripoti, inasaidia kuponya. Sisi Watanzania tumepata uhuru kwa njia ya mazungumzo, siyo kwa vita. Hivyo ripoti hii inatusaidia kukaa pamoja na kufanya maridhiano ili tuendelee kuwa salama,” amesema Sube.

Ameongeza kuwa ni wakati wa wananchi kurejea kwenye misingi ya mazungumzo kwa lengo la kuondoa tofauti zilizojitokeza na kusababisha migogoro, akisisitiza umuhimu wa kusahihishana pale walipokosea.

“Turudi mezani kwa ajili ya mazungumzo ya wazi na ya kujenga ili kuondoa tofauti zilizojitokeza na kusababisha uvunjifu wa amani. Kupitia mchakato huo, tuimarishe umoja wetu na kuwa kitu kimoja tena kama Watanzania. Wale tuliokoseana, ni vyema tukutane, tuzungumze kwa utulivu na kusahihishana pale tulipokosea kwa lengo la kujenga mustakabali bora wa taifa letu.” ameongeza.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, sababu kuu zilizochangia ghasia hizo ni pamoja na mchanganyiko wa malalamiko ya kisiasa, changamoto za kiuchumi pamoja na utendaji usioridhisha wa baadhi ya watumishi wa umma.

Ripoti hiyo imekabidhiwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, katika hafla iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam tarehe 23 Aprili 2026, ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali kutafuta suluhu ya kudumu na kuimarisha amani nchini.


Share:

Saturday, 25 April 2026

WAFANYABIASHARA SOKO LA NAMANGA KAHAMA WALALAMIKIA TOZO NA UKOSEFU WA UWAZI, DC NKINDA AAGIZA TAKUKURU KUCHUNGUZA

 


Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Frank Nkinda akizungumza na wafanyabiashara wasoko la Namanga lililopo Manispaa ya kahama mara baada ya kusikiliza kezo zao


Na Neema Nkumbi, Kahama


Wafanyabiashara wa Soko la Namanga lililopo Manispaa ya Kahama mkoani Shinyanga wameeleza kutoridhishwa na mfumo wa ukusanyaji wa ushuru wakidai kuwepo kwa tozo wanazoziita zisizo rasmi pamoja na ukosefu wa uwazi katika matumizi ya mapato yanayokusanywa sokoni hapo.


Wakizungumza katika mkutano wa kusikiliza na kutatua kero ulioandaliwa na ofisi ya Mkuu wa Wilaya katika soko hilo, wafanyabiashara wamesema wamekuwa wakikumbwa na mzigo mkubwa wa ushuru unaowadhoofisha kiuchumi, huku wakidai kuwa hakuna mrejesho wa wazi kuhusu matumizi ya fedha hizo.
Mfanyabiashara samaki katika soko hilo Irene Thomas amesema kumekuwepo kwa vikundi vinavyohusika na ukusanyaji wa mapato ambavyo havitoi taarifa za kutosha kwa wafanyabiashara, hali inayozua sintofahamu sokoni hapo.


"sisi tunalipa ushuru zaidi ya maduka makubwa wanaolipa TRA, mimi mtaji wangu laki nne mpaka tano lakini kwa mwezi ushuru nalipa laki tatu na elfu tisini nikiwa na kijana na bado sijamlipa kijana, mimi nabakiwa na nini?", amesema Irene.


ameongeza kuwa "halafu hiyo hela ni bora ningejua inaenda serikalini, inaenda kufanya maendeleo ambapo itatengeneza barabara nami nitapita, kuliko kwenda kwenye kikundi ambacho kinakula hela ya mwananchi, kikundi hiki sidhani kama kinalipa TRA maana kinatoa risiti za makaratasi na kikundi kinaingiza zaidi ya milioni nne kwa mwezi na halmashauri inalipwa laki tano na arobaini tu".
Mfanyabiashara mwingine wa samaki amesema " sisi kwenye kikundi hicho hatumo na hatufaidiki kwa chochote mapato yao wanafaidika wenyewe ikifika mwisho wa mwaka wanapeana bahasha wenyewe sasa mimi ninachotakiwa nikilipe ni mapato ya serikali yaliyonyooka na si kulipa vikundi".


Hata hivyo, Mwenyekiti wa Soko la Namanga, Juma Jumeju, amekanusha tuhuma hizo akisema mfumo wa sasa ulianzishwa ili kurahisisha ukusanyaji wa mapato baada ya soko kukumbwa na changamoto za utulivu katika kipindi cha nyuma.


Jumeju amesema uongozi uliingia ubia na baadhi ya wafanyabiashara kuunda kikundi kilichosajiliwa kisheria kwa lengo la kuboresha mfumo wa ukusanyaji wa mapato, akibainisha kuwa kuna mkanganyiko wa uelewa kuhusu majukumu ya kikundi hicho.


“Kwa kipindi cha nyuma soko halikuwa na utulivu, ndipo tukaunda kikundi kilichosajiliwa kisheria ili kurahisisha ukusanyaji wa mapato,” amesema.


Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Frank Nkinda, ameeleza kuwa ni muhimu kupata uhalisia wa suala hilo kabla ya kuchukua hatua, akisema kuna haja ya kusikiliza pande zote ili kuhakikisha haki inatendeka.


Aidha, ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kufuatilia kwa kina malalamiko hayo ili kubaini iwapo kuna mianya ya udanganyifu au ukiukwaji wa taratibu katika ukusanyaji wa mapato sokoni hapo.


“Ninaigiza TAKUKURU kufuatilia suala hili kwa haraka ili tupate uhalisia na tufanye maamuzi sahihi ya kumaliza mgogoro huu,” amesema Nkinda.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI APRILI 25,2026


Magazeti
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger