Sunday, 26 April 2026
WANANCHI SHINYANGA WAPOKEA RIPOTI YA JAJI CHANDE KWA MATUMAINI YA MARIDHIANO
Wananchi hao wamesema wanaamini kuwa utekelezaji wa mapendekezo yaliyomo kwenye ripoti hiyo utasaidia kurejesha mshikamano wa kitaifa na kuzuia kujirudia kwa matukio ya uvunjifu wa amani siku zijazo.
Akizungumza kuhusu ripoti hiyo iliyowasilishwa na Mwenyekiti wa Tume, Mohamed Chande Othman, mmoja wa wakazi wa Shinyanga Mjini, Chief Abdallah Sube, amesema ameipokea vizuri kwa kuwa inalenga kuponya majeraha yaliyosababishwa na matukio ya uvunjifu wa amani.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, sababu kuu zilizochangia ghasia hizo ni pamoja na mchanganyiko wa malalamiko ya kisiasa, changamoto za kiuchumi pamoja na utendaji usioridhisha wa baadhi ya watumishi wa umma.
Ripoti hiyo imekabidhiwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, katika hafla iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam tarehe 23 Aprili 2026, ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali kutafuta suluhu ya kudumu na kuimarisha amani nchini.
Saturday, 25 April 2026
WAFANYABIASHARA SOKO LA NAMANGA KAHAMA WALALAMIKIA TOZO NA UKOSEFU WA UWAZI, DC NKINDA AAGIZA TAKUKURU KUCHUNGUZA
Magazeti




















