Thursday, 2 July 2026

WAFANYAKAZI WA STANDARD CHARTERED WAADHIMISHA MIAKA 20 YA KUJITOLEA KWA JAMII KWA KUSAFISHA FUKWE






Standard Chartered Tanzania kwa kushirikiana na Nipe Fagio imeadhimisha miaka 20 ya programu ya kujitolea kwa jamii ya Standard Chartered duniani kwa kufanya zoezi la kila mwaka la usafi wa fukwe katika Ufukwe wa Silversand, Kunduchi.

Jumla ya washiriki 74, wakiwemo watoto 20, walishiriki katika zoezi hilo lililolenga kuchangia uhifadhi wa mazingira na kuhamasisha ushiriki wa wafanyakazi katika shughuli za maendeleo ya jamii.

Akizungumza kuhusu shughuli hiyo, Afisa Mtendaji Mkuu na Mkuu wa Kitengo cha Coverage wa Standard Chartered Bank Tanzania, Geofrey Mchangila, alisema:

"Zoezi la mwaka huu lina umuhimu wa pekee kwetu kwani linafanyika wakati Standard Chartered inaadhimisha miaka 20 ya kujitolea kwa jamii duniani kote. Tunaamini kuwa mabadiliko ya kweli huanza pale watu wanapounganisha nguvu zao.


Kupitia ushirikiano wetu na wafanyakazi, familia zao pamoja na Nipe Fagio, tunaendelea kuchangia kulinda ukanda wa pwani wa Tanzania na kujenga jamii zenye afya bora na mazingira endelevu kwa vizazi vijavyo."

Katika zoezi hilo, washiriki walisafisha eneo lenye ukubwa wa takribani mita za mraba 4,000 za ufukwe na kukusanya kilo 506 za taka zilizohifadhiwa katika mifuko 55.


Uchambuzi wa taka zilizokusanywa ulionyesha kuwa plastiki, hususan povu la polystyrene na chupa za plastiki za vinywaji, ndizo zilikuwa taka zilizopatikana kwa wingi, hali inayodhihirisha umuhimu wa kuendelea kuchukua hatua za kudhibiti uchafuzi wa mazingira ya bahari.

Kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita, kupitia ushirikiano wake na Nipe Fagio, Standard Chartered Tanzania imefanikisha jumla ya kampeni tano za usafi wa fukwe, ikihusisha washiriki 594, kusafisha zaidi ya mita za mraba 32,000 za ukanda wa pwani na kukusanya karibu tani tano za taka.

Mpango huu ni sehemu ya mkakati mpana wa Standard Chartered wa kuendeleza uhimilivu wa mazingira na maendeleo endelevu, huku ukiunga mkono Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa (SDGs), hususan Lengo la 13 la Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Lengo la 14 la Kuhifadhi Maisha ya Chini ya Maji na Lengo la 17 la Kuimarisha Ushirikiano kwa Ajili ya Kufanikisha Malengo.

Standard Chartered inapoendelea kuadhimisha miaka 20 ya programu yake ya kujitolea kwa jamii, inaendelea kuwahamasisha wafanyakazi wake kutumia muda, ujuzi na utaalamu wao kuleta mabadiliko chanya na endelevu katika jamii na mazingira.








Share:

TEMESA YAONESHA MAGEUZI MAKUBWA,WAZIRI KAPINGA ATOA PONGEZI





Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga, leo Julai 1, ametembelea banda la Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba, yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, Barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza bandani hapo, Mhe. Kapinga ameipongeza TEMESA kwa kasi ya mabadiliko inayoenda nayo katika matengenezo ya magari na mabadiliko ya mifumo ya utoaji huduma.



“Nawapongeza sana kwa kazi nzuri mnazozifanya katika matengenezo ya magari na pia matumizi yenu ya mifumo katika utoaji huduma. Hongareni sana.” Amesema Mhe. Kapinga.

Waziri wa Viwanda na Biashara alipotembelea banda la TEMESA alipata fursa ya kujionea huduma mbalimbali zinazotolewa na TEMESA, ikiwemo huduma za vivuko, umeme na elektroniki, matengenezo ya magari na mitambo, ushauri wa kihandisi pamoja na mifumo ya kidijitali na ubunifu unaolenga kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.



Maonesho hayo ya biashara yamebebwa na kauli mbiu isemayo “Hii ni Kubwa Kuliko” na yanatarajiwa kuzinduliwa rasmi siku ya ijumaa tarehe 3 Juni, 2026



TEMESA inaendelea kuwakaribisha wananchi, wadau na wageni wote kutembelea banda lake ili kujifunza kuhusu huduma zake, kupata ushauri wa kitaalamu na kufahamu mchango wa Wakala katika maendeleo ya sekta ya ufundi na umeme nchini.





Share:

Wednesday, 1 July 2026

BIMA YA AFYA ZA WEZESHWA KWA WANAGENZI


-IKUJUMUISHWA NA POSHO YA USAFIRI

Na Mwandishi OWM-KAM, Mara

Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano imeendelea kuboresha mazingira ya mafunzo ya kukuza ujuzi kwa njia ya uanagenzi kwa kuwapatia wanagenzi 5,746 bima ya afya na posho ya usafiri ya shilingi 100,000 kwa mwezi kwa kipindi cha mafunzo ya vitendo sehemu za kazi. Hatua hiyo inalenga kuwawezesha wanagenzi kuendelea na mafunzo katika mazingira salama na kuongeza ufanisi wa programu ya taifa ya kukuza ujuzi.

Hayo yalisemwa na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Dkt. Evaline Wilbard Munisi, wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya mafunzo ya kukuza ujuzi kwa njia ya uanagenzi katika Chuo cha Ufundi Stadi St. Anthony, Musoma mkoani Mara, Juni 30, 2026.

Alisema Serikali inaendelea kuwekeza katika maendeleo ya vijana ili kujenga nguvukazi yenye ujuzi, maarifa na ushindani unaohitajika katika soko la ajira la ndani na kimataifa.

Dkt. Munisi alisema maboresho hayo ni sehemu ya utekelezaji wa Programu ya Taifa ya Kukuza Ujuzi, inayolenga kuongeza idadi ya Watanzania wenye ujuzi stahiki wa kujiajiri na kuajiriwa huku ikipunguza pengo la ujuzi katika soko la ajira.

Aidha, Naibu Waziri alisisitiza kuwa Serikali inatarajia kuona wahitimu wanaotumia ujuzi walioupata kuibua suluhisho bunifu kwa changamoto za uzalishaji na utoaji huduma nchini.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Ajira na Ukuzaji Ujuzi, Bi. Alana Nchimbi, alisema kuwa mfumo wa uanagenzi umeendelea kuwa njia bora ya kuziba pengo la ujuzi kwa kuunganisha mafunzo ya darasani na uzoefu wa moja kwa moja mahali pa kazi.

Naye Mkuu wa Chuo cha Ufundi Stadi St. Anthony Fr. Dkt. Constatine Changwe alisema chuo hicho kimepokea wanagenzi 186 wanaofadhiliwa kikamilifu na Serikali katika awamu ya nane ya programu hiyo, huku chuo kikiongeza nafasi kwa wanagenzi wengine 25 kwa ufadhili wa Kanisa Katoliki kutokana na mahitaji makubwa ya vijana waliotuma maombi. Alibainisha kuwa mafunzo yanatolewa katika fani sita zenye mahitaji makubwa katika soko la ajira.

Kwa niaba ya wanagenzi, Neema Abeli aliishukuru Serikali kwa kugharamia ada za mafunzo kwa asilimia 100, kutoa bima ya afya na kuweka utaratibu wa posho ya usafiri kwa kipindi cha mafunzo ya vitendo. Alisema hatua hizo zimeondoa changamoto za kifedha na kuwapa vijana nafasi ya kuzingatia masomo na kujenga ujuzi utakaowawezesha kujiajiri au kuajiriwa baada ya kuhitimu, huku akiomba Serikali iendelee kupanua programu hiyo ili vijana wengi zaidi wanufaike.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO JULAI 1,2026



Magazeti













Share:

Tuesday, 30 June 2026

NAIBU WAZIRI MAHUNDI AHIMIZA WANAWAKE KUTUMIA MIKOPO KUINUA UCHUMI



Na Jackline Minja, Mtwara

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Maryprisca Mahundi, amezindua rasmi Mfuko wa Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi katika Jimbo la Mtwara Mjini (UWEZO Program) na kusema Serikali itaendelea kuunga mkono jitihada za uwezeshaji wa wanawake.

Akizungumza katika hafla hiyo Juni 30, 2026, Naibu Waziri Mahundi amesema Serikali inaamini kuwa maendeleo ya Taifa hayawezi kupatikana bila kuyawezeaha makundi maalum wakiwemo wanawake na vijana.

Amesema ushiriki wa makundi maalum katika shughuli za kiuchumi ni hatua ya kujivunia na kuongeza kuwa mafanikio yatapatikana kwa makundi hayo kupatiwa mafunzo stahiki.

"Serikali inaamini kuwa maendeleo ya Taifa hayawezi kupatikana bila wananchi wake kuwa na uwezo wa kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji mali na hii ndiyo sababu kuwndelea kuweka mazingira wezeshi kwa wanawake na vijana kupata fursa za kiuchumi kupitia sera na programu mbalimbali," alisema Naibu Waziri Mahundi.

Aidha, ameeleza kuvutiwa kwake na Programu ya UWEZO kwa kuanza kutoa mikopo na kuwajengea wanawake uwezo kupitia mafunzo ya ujasiriamali, usimamizi wa fedha, utunzaji wa kumbukumbu za biashara na uundaji wa vikundi, akieleza kuwa msingi huo utasaidia kuhakikisha mikopo inazalisha matokeo chanya na kuongeza maendeleo ya wanawake pamoja na familia zao.

Awali akitoa maelezo kuhusu Programu ya UWEZO, Mbunge wa Jimbo la Mtwara Mjini na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Mhe. Joel Nanauka, amesema wazo la kuanzisha mfuko huo limetokana na ahadi aliyoitoa kwa wananchi wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ya kuwawezesha wananchi kiuchumi.

Amesema kupitia mfuko huo wenye mtaji wa shilingi milioni 150, wanawake zaidi ya 5,000 walitambuliwa kutoka kata zote 18 za jimbo hilo, wanawake 300 walipatiwa mafunzo ya ujasiriamali na wanawake 81 wamekabidhiwa mikopo katika awamu ya kwanza.

"Mikopo hiii haina riba kutokana na ushirikiano kati ya Joel Nanauka Foundation na Benki ya Ushirika (Coop Bank), sababu lengo la programu hii si kutoa fedha pekee bali kujenga wanawake wajasiriamali wenye uwezo wa kujitegemea, kuongeza ajira na kuchangia ukuaji wa uchumi wa Mtwara Mjini na Taifa kwa ujumla". alisema

Nao baadhi ya wanufaika wa Mkopo huo wameipongeza Serikali na kumpongeza Waziri Nanauka kwa maono na kutekeleza ahadi aliyoitoa wakati wa kampeni zake ambapo kwa sasa wataweza kujiendesha kiuchumi na kupunguza makali ya ugumu wa maisha na kuingizia taifa mapato.






Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger