Wednesday, 3 June 2026

VYUO VIKUU MALAYSIA VYAANZA MAONESHO YA ELIMU DAR


Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Tanzania na Malaysia zimefungua ukurasa mpya wa ushirikiano katika elimu ya juu kupitia ubia wa vyuo vikuu, tafiti za pamoja, ubadilishanaji wa wanafunzi na wahadhiri, ufadhili wa masomo pamoja na ushirikiano katika sayansi na teknolojia.

Akizungumza katika kikao cha Kuimarisha Ushirikiano wa Elimu ya Juu Kati ya Tanzania na Malaysia** kilichofanyika katika Hoteli ya Serena, Dar es Salaam, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Daniel Mushi, amesema ujio wa ujumbe wa elimu kutoka Malaysia ni wa wakati muafaka wakati Tanzania ikiendelea kuimarisha na kutangaza kimataifa mfumo wake wa elimu ya juu.

Kikao hicho kiliandaliwa na kuratibiwa na Education Malaysia Global Services (EMGS), chini ya Wizara ya Elimu ya Juu ya Malaysia, kwa kushirikiana na Global Education Link Ltd (GEL).

Prof. Mushi amesema ujio wa ujumbe huo umevitambulisha vyuo vya Malaysia nchini Tanzania na kutoa nafasi kwa pande zote mbili kujadili maeneo ya ushirikiano yatakayowanufaisha wanafunzi, wahadhiri na taasisi za elimu ya juu.

Amesema Tanzania inatarajia kuona ushirikiano utakaoimarisha programu za pamoja, kubadilishana maarifa, tafiti, ubunifu na kuongeza uwezo wa taasisi za elimu ya juu nchini.

Kwa mujibu wa Prof. Mushi, Malaysia imepiga hatua kubwa katika kutumia elimu, teknolojia na ujuzi kama nyenzo ya mageuzi ya kiuchumi, jambo ambalo Tanzania inaweza kujifunza katika safari yake ya kujenga uchumi unaotegemea maarifa na teknolojia.

Amesema kipaumbele kinapaswa kuwekwa katika kuwaandaa wanafunzi wa Tanzania kwenye maeneo ya sayansi, hisabati, kemia, sayansi ya takwimu, ujifunzaji wa mashine na akili mnemba.

Aidha, amesema wanafunzi wanaotaka kusoma nje ya nchi wanapaswa kuandaliwa si kitaaluma pekee, bali pia kilugha na kitamaduni ili waweze kushindana na kufanikiwa katika mazingira ya kimataifa.

“Ushirikiano wa aina hii ni muhimu kwa sababu unawapa wanafunzi na taasisi zetu nafasi ya kupata maarifa mapya, mifumo mipya na njia mpya za kujenga rasilimali watu kwa maendeleo ya taifa,” amesema Prof. Mushi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Elimu ya Juu katika Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Stephen Maluka, amesema kikao hicho kimetoa jukwaa la vitendo kwa taasisi za Tanzania na Malaysia kujadili namna bora ya kujenga ushirikiano rasmi.

Amesema majadiliano yamelenga kuanzisha mahusiano ya moja kwa moja kati ya vyuo vikuu, wizara na taasisi za elimu kutoka nchi zote mbili kwa lengo la kuendeleza elimu, sayansi na teknolojia.

Prof. Maluka amesema Tanzania inahitaji ushirikiano unaokwenda zaidi ya udahili wa wanafunzi na kuingia katika maeneo ya tafiti za pamoja, programu za pamoja, ufadhili wa masomo, ubadilishanaji wa wahadhiri, maboresho ya mitaala na ushirikiano wa kitaaluma.

Amesema ufadhili wa masomo utasaidia wanafunzi wa Tanzania wenye sifa kupata nafasi za masomo Malaysia, hususan katika maeneo ambayo nchi hiyo imepiga hatua kubwa.

Aidha, amesema ubadilishanaji wa wahadhiri unaweza kusaidia kuongeza ubora wa ufundishaji, usimamizi wa tafiti na kuwapa wanataaluma uzoefu wa mifumo tofauti ya elimu ya juu.

Prof. Maluka ametaja teknolojia, sayansi ya takwimu na akili mnemba kuwa miongoni mwa maeneo muhimu ya ushirikiano wa baadaye.

Amesema ushirikiano katika maeneo hayo unaweza kusaidia Tanzania kuongeza uwezo katika teknolojia chipukizi na kuwaandaa wahitimu kwa dunia inayoongozwa na ubunifu na mabadiliko ya kidijitali.

“Sasa ni muhimu kutoka kwenye mazungumzo ya jumla na kuingia kwenye mifumo ya utekelezaji itakayoongoza ushirikiano kati ya taasisi,” amesema Prof. Maluka.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Global Education Link Ltd, Bw. Abdulmalik Mollel, amesema GEL inajivunia kuratibu mpango huo unaounganisha taasisi za Tanzania na vyuo vikuu pamoja na mamlaka za elimu kutoka Malaysia.

Amesema mpango huo hauhusu kutangaza fursa za kusoma Malaysia pekee, bali pia kujenga daraja la muda mrefu la elimu kati ya Tanzania na Malaysia.

“Ushirikiano huu unalenga kujenga daraja la kweli kati ya Tanzania na Malaysia katika elimu ya juu. Tunataka kuona vyuo vya pande zote mbili vikishirikiana katika tafiti, programu za kitaaluma, ubadilishanaji wa wanafunzi, ubadilishanaji wa wahadhiri na mafunzo yanayotegemea teknolojia,” amesema Mollel.


Share:

BEI YA PETROLI YASHUKA, SERIKALI YAWEKA RUZUKU KWENYE DIZELI



Na mwandishi wetu

Watumiaji wa petroli wamepata afueni mwezi Juni 2026 baada ya bei ya mafuta hayo kushuka ikilinganishwa na mwezi uliopita. Kwa Dar es Salaam, petroli sasa itauzwa kwa bei kikomo ya shilingi 4,086 kwa lita, hatua inayotarajiwa kupunguza gharama kwa watumiaji wa kawaida na baadhi ya shughuli za usafiri.

Kwa upande wa dizeli, watumiaji wanakabiliwa na ongezeko dogo la bei, ambapo kwa Dar es Salaam bei kikomo imefikia Shilingi 4,333 kwa lita. Ongezeko hilo limechangiwa na kupanda kwa gharama za mafuta katika soko la dunia pamoja na kuongezeka kwa gharama za uagizaji wa bidhaa hiyo.

Licha ya changamoto hizo za kimataifa, Serikali imeendelea kuchukua hatua za kulinda uchumi na wananchi kwa kuweka ruzuku ya Shilingi 534.91 kwa kila lita ya dizeli. Hatua hiyo imelenga kupunguza athari za ongezeko la bei kwa sekta muhimu kama usafirishaji, viwanda na huduma za kijamii.

Mabadiliko haya yameathiriwa kwa kiasi kikubwa na vita vinavyoendelea Mashariki ya Kati, vinavyohusisha Marekani, Israeli na Irani. Mgogoro huo umeathiri uzalishaji, uhifadhi na usafirishaji wa mafuta duniani, huku kufungwa kwa Mlango Bahari wa Hormuz kukiongeza gharama za usafirishaji na bima za meli za mafuta.
Share:

Tuesday, 2 June 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO JUNI 3,2026

Magazeti
 



Share:

Breaking : HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOPANGIWA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2026

 

Ofisi ya Rais – TAMISEMI imetangaza rasmi uchaguzi wa wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano pamoja na Vyuo vya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa mwaka 2026.

👉 BOFYA HAPA KUONA ORODHA YA WANAFUNZI 

Share:

Monday, 1 June 2026

TI3P YATAJWA KUCHOCHEA MAPINDUZI YA SEKTA NDOGO YA MAZIWA


Na Mwandishi Wetu, Iringa

WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Kakurwa, ameipongeza Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) kwa utekelezaji wa Mradi Shirikishi wa Wasindikaji na Wazalishaji wa Maziwa (TI3P), akisema umekuwa chachu ya mageuzi katika sekta ndogo ya maziwa kwa kuongeza uzalishaji, kuimarisha mnyororo wa thamani na kuboresha maisha yawafugaji nchini.

Dkt. Bashiru alitoa kauli hiyo alipotembelea banda la TADB katika Maonesho ya 29 ya Wiki yaMaziwa yanayoendelea katika Viwanja vya Mwembetogwa mkoani Iringa, ambapo alipokea taarifa ya utekelezaji wa mradi huo kutoka kwa Mratibu wa TI3P, Joseph Mabula.

Alisema mafanikio yanayoonekana kupitia mradi huo yanadhihirisha umuhimu wa uwekezaji katika sekta ya mifugo, hususan sekta ndogo ya maziwa, ambayo imeendelea kuwa nguzo muhimu ya usalama wa chakula, lishe, ajira na uchumi wa wananchi wa vijijini.

"Wakati umefika kwa taasisi nyingine za kifedha kuona fursa zilizopo katika sekta ya mifugo na kuongeza nguvu katika utoaji wa huduma za kifedha kwa wafugaji kama ambavyo zimekuwazikifanya katika sekta nyingine za uzalishaji," alisema Dkt. Bashiru.

Aidha, aliwataka wadau wa maendeleo, taasisi za kifedha, wasindikaji wa maziwa na vyama vya ushirika kuimarisha ushirikiano ili kuongeza tija katika uzalishaji, ukusanyaji, uchakataji namasoko ya maziwa nchini.

Alisisitiza kuwa vyama vya ushirika vina nafasi kubwa katika kuwa unganisha wafugaji wadogo, kuwawezesha kupata pembejeo, huduma za ugani, mikopo na masoko yenye uhakika, jamboambalo ni muhimu katika kujenga sekta ya maziwa yenye ushindani.

Mafanikio ya mradi wa TI3P yanaonekana moja kwa moja kwa wanufaika wake. Mwenyekiti waChama cha Ushirika cha Wafugaji wa Ng’ombe wa Maziwa cha IDCOS LTD cha mkoani Iringa, Alex Nyalusi, alisema chama hicho kimepata mafanikio makubwa baada ya kuwezeshwa naTADB kupitia mradi huo kupata mkopo wa ng’ombe 25 wa maziwa.

Nyalusi alisema uwekezaji huo umeongeza uzalishaji wa maziwa kutoka wastani wa lita 700 hadi lita 1,000 kwa siku, hatua iliyoongeza mapato ya chama na wanachama wake 84.

Alisema kabla ya kupata uwezeshaji huo, wafugaji wengi walikuwa wakikabiliwa nachangamoto za uzalishaji mdogo na kipato kisichokidhi mahitaji yao, lakini hali imeanzakubadilika kutokana na kuongezeka kwa uzalishaji na ubora wa mifugo.

"Leo hii wanachama wetu wanaona matokeo ya moja kwa moja ya mradi huu. Kipatokimeongezeka, uwezo wa kuhudumia familia umeimarika na ari ya kuwekeza katika ufugaji wakisasa imeongezeka kwa kiasi kikubwa," alisema Nyalusi.

Aliongeza kuwa chama hicho sasa kinaangalia hatua inayofuata katika kuongeza thamani yamaziwa kwa kuwekeza katika uchakataji wa bidhaa mbalimbali zitokanazo na maziwa.

"Tunatarajia kurejea TADB kuomba uwezeshaji wa kupata mitambo ya kuchakata maziwa ilikuanza kuzalisha mtindi na yoghurt. Hii itatusaidia kuongeza thamani ya maziwa yetu, kupanuasoko na kuongeza mapato kwa wanachama," alisema.

Pamoja na mafanikio hayo, Nyalusi alisema sekta ndogo ya maziwa bado inakabiliwa nachangamoto mbalimbali zinazohitaji kushughulikiwa ili kuongeza kasi ya ukuaji wake.

Alitaja changamoto hizo kuwa ni pamoja na uhaba wa wataalamu wa uhimilishaji, upungufu wamaafisa ugani, changamoto za upatikanaji wa malisho bora, magonjwa ya mifugo pamoja namiundombinu duni katika baadhi ya maeneo ya uzalishaji.

Wadau wa sekta ya maziwa wanaamini kuwa kuongezeka kwa uwekezaji katika uzalishaji, ukusanyaji, uhifadhi na uchakataji wa maziwa kutasaidia kuifanya sekta hiyo kuwa moja yanguzo kuu za uchumi wa mifugo nchini.

Mradi wa TI3P unaotekelezwa na TADB umeendelea kutajwa na wadau mbalimbali kama mojaya mifano ya uwekezaji wenye matokeo chanya katika sekta ndogo ya maziwa, kutokana na mchango wake katika kuwaunganisha wazalishaji na wasindikaji, kuongeza tija ya uzalishaji nakuinua ustawi wa wafugaji wadogo nchini.

Share:

Sunday, 31 May 2026

MZUMBE YALENGA KUIBUA MAPINDUZI YA UTALII NA KILIMO TANGA, YAZINDUA PROGRAMU MAALUMU ZA ELIMU NA KUFUNGUA FURSA MPYA ZA UWEKEZAJI

Na Hadija Bagasha Tanga

Katika juhudi za kuimarisha sekta za utalii na kilimo ambazo ni miongoni mwa nguzo muhimu za uchumi wa Tanzania, Chuo Kikuu Mzumbe Kampasi ya Tanga kimeanzisha programu maalumu za elimu zitakazolenga kuzalisha wataalamu wenye ujuzi na maarifa ya kisasa watakaosaidia kuendeleza sekta hizo na kuongeza mchango wake katika maendeleo ya taifa.

Hatua hiyo imetangazwa wakati wa Maonyesho ya 13 ya Biashara na Utalii yanayoendelea jijini Tanga, ambapo baadhi ya wahadhiri wa chuo hicho wamesema kuwa uwekezaji katika elimu ya utalii na kilimo ni mkakati wa muda mrefu wa kuandaa rasilimali watu wenye uwezo wa kukabiliana na mahitaji ya sasa na ya baadaye ya soko la ajira.

Akizungumza katika maonyesho hayo, Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu Mzumbe, Dk. Felchesmi Lyakurwa, amesema chuo hicho kimeanzisha programu za ngazi ya cheti na stashahada katika masuala ya kilimo na utalii kwa lengo la kuongeza idadi ya wataalamu watakaoweza kutoa mchango mkubwa katika maendeleo ya sekta hizo nchini.

Amesema Tanzania imebarikiwa kuwa na vivutio vingi vya utalii vinavyoendelea kuvutia wageni kutoka ndani na nje ya nchi, huku Mkoa wa Tanga ukiwa miongoni mwa maeneo yenye fursa kubwa za utalii ambazo bado hazijatumika kikamilifu kutokana na uhaba wa wataalamu wa kutosha katika sekta hiyo.

"Tumefikia uamuzi huu kwa sababu tunahitaji wataalamu wengi zaidi katika eneo la utalii. Mkoa wa Tanga una vivutio vingi vya utalii, na Tanzania kwa ujumla ina hazina kubwa ya vivutio vinavyohitaji wataalamu wenye ujuzi wa kisasa, "

" Kupitia programu hizi, tutatoa vijana waliobobea watakaosaidia kuongeza tija na ushindani katika sekta ya utalii," amesema Dk. Lyakurwa.

Ameongeza kuwa programu hizo zitawajengea wanafunzi uwezo wa kuelewa mifumo ya kisasa ya usimamizi wa utalii, huduma kwa wageni, uhifadhi wa mazingira na matumizi ya teknolojia katika kukuza utalii endelevu.

Kwa upande wa kilimo, Dk. Lyakurwa amesema programu hizo zimeandaliwa kwa kuzingatia mahitaji ya sasa ya sekta ya kilimo, ambayo inaendelea kuwa mhimili muhimu wa uchumi wa nchi na chanzo kikubwa cha ajira kwa Watanzania wengi.

Amesema elimu itakayotolewa itawasaidia vijana kupata maarifa ya kisasa yatakayowawezesha kuwa wataalamu watakaosaidia jamii kuendesha kilimo chenye tija, kuongeza uzalishaji na kutumia teknolojia mbalimbali zinazoboresha sekta hiyo.

"Tunataka kuona vijana wakipata maarifa yatakayowasaidia kuhamasisha na kuendeleza kilimo cha kisasa, chenye tija na kinachoweza kukidhi mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi," amesema.

Wakati huo huo, Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu Mzumbe, Dk. Lihoya Chanwali, amesema kuanzishwa kwa Kampasi ya Tanga ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kusogeza huduma za elimu ya juu karibu zaidi na wananchi kwa kuhakikisha vyuo vikuu vinaenea katika mikoa mbalimbali nchini.

Amesema Serikali imekuwa na dhamira ya kuongeza fursa za elimu ya juu kwa vijana wanaohitimu kidato cha sita, na Chuo Kikuu Mzumbe kilipata nafasi ya kuunga mkono jitihada hizo kwa kuanzisha kampasi yake katika Mkoa wa Tanga.

Kwa mujibu wa Dk. Chanwali, uwepo wa kampasi hiyo utaongeza nafasi za udahili kwa wanafunzi wengi zaidi wanaotaka kuendelea na elimu ya juu, huku ukiwa pia ni fursa kwa Chuo Kikuu Mzumbe kupanua huduma zake na kuwafikia wananchi katika maeneo mengi zaidi nchini.

"Uwepo wa Chuo Kikuu Mzumbe Kampasi ya Tanga unasaidia kuongeza nafasi kwa wahitimu wa kidato cha sita kujiunga na elimu ya juu.

 Aidha, ni fursa kwa chuo kupanua huduma zake na kuongeza mchango wake katika maendeleo ya elimu nchini," amesema.

Ameeleza kuwa chuo hicho kimeshiriki Maonyesho ya 13 ya Biashara na Utalii kwa lengo la kutoa elimu kuhusu fursa mbalimbali zinazopatikana chuoni, pamoja na kutangaza rasmi ujio wa Kampasi ya Tanga ambayo itaanza kutoa programu za masomo kuanzia ngazi ya cheti, stashahada na shahada.

Mbali na kutoa elimu, chuo hicho pia kinatafuta ushirikiano wa wawekezaji ili kusaidia maendeleo ya miundombinu katika kampasi mpya iliyopo Kijiji cha Gombero, Wilaya ya Mkinga, Mkoa wa Tanga.

Dk. Chanwali amesema eneo linalozunguka kampasi hiyo bado lina fursa nyingi za uwekezaji ambazo hazijatumika kikamilifu, hali inayofungua milango kwa wafanyabiashara na wawekezaji kuwekeza katika huduma mbalimbali zitakazohitajika kadri shughuli za chuo zinavyoongezeka.

Amesema kampasi hiyo inatarajiwa kuanza kwa kudahili wanafunzi wapatao 1,200, lakini kwa sasa uwezo wa mabweni yaliyopo ni kuchukua wanafunzi 360 pekee, jambo linaloacha upungufu wa nafasi za malazi kwa zaidi ya wanafunzi 900.

Kutokana na changamoto hiyo, chuo kinalazimika kuanza shughuli zake kwa idadi ndogo ya wanafunzi wakati kikisubiri upanuzi wa miundombinu ya malazi.

"Iwapo tutapata wawekezaji watakaosaidia kujenga mabweni ndani au nje ya kampasi, tutakuwa na uwezo wa kudahili wanafunzi wengi zaidi. Hii pia itasaidia kuongeza shughuli za kiuchumi katika Kijiji cha Gombero na maeneo ya jirani," amesema.

Aidha, amesema kampasi hiyo inakabiliwa na uhaba mkubwa wa nyumba za wafanyakazi. Kwa sasa chuo kimefanikiwa kujenga nyumba nne pekee, wakati mahitaji halisi yanazidi nyumba 100 kutokana na idadi ya watumishi wanaotarajiwa kufanya kazi katika kampasi hiyo.

Kwa mujibu wa takwimu za chuo, Kampasi ya Tanga inatarajiwa kuwa na wafanyakazi zaidi ya 100, wakiwemo watumishi wa kitaaluma na wasio wa kitaaluma, hali inayofanya uwekezaji katika nyumba za watumishi kuwa moja ya maeneo muhimu yanayohitaji kipaumbele.

Kuanzishwa kwa Kampasi ya Tanga kunatajwa kuwa hatua muhimu si tu katika kupanua wigo wa elimu ya juu nchini, bali pia katika kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika Wilaya ya Mkinga na Mkoa wa Tanga kwa ujumla, kupitia ajira, biashara, uwekezaji na ongezeko la mahitaji ya huduma mbalimbali zinazotokana na uwepo wa taasisi kubwa ya elimu ya juu katika eneo hilo.












Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger