Friday, 26 June 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA JUNI 26, 2026


Magazetini Leo


Share:

Thursday, 25 June 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI JUNI 25,2026

Magazeti


 



Share:

SERIKALI YAWAHAKIKISHIA AMANI WANANCHI


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi, amewahakikishia wananchi wa Tanzania kuendelea kufurahia amani na utulivu, huku akiwataka kushiriki shughuli za kiuchumi na maendeleo bila hofu.

Katambi ametoa kauli hiyo wakati wa hafla ya kufunga Mafunzo ya Awali Kozi Na. 6/2026 katika Chuo cha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Chogo, wilayani Handeni mkoani Tanga, ambapo jumla ya askari 1,000 wamehitimu mafunzo hayo.

Amesema vyombo vya usalama vimejipanga kikamilifu kulinda amani ya nchi, ikiwa ni pamoja na kukabiliana na taarifa zinazosambazwa mitandaoni kuhusu maandamano yanayodaiwa kufanyika nchi nzima.

Kwa upande wake, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, John Masunga, amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa kibali cha kuajiri askari hao 1,000 na kuthibitisha kukamilika kwa taratibu zote za ajira.

Mafunzo hayo yanayohitimishwa leo yanajumuisha wataalamu katika kada za Uzimaji Moto wa Kemikali, Maokozi ya Angani,nchi kavu na majini ambapo wanaume wapo 651 na wanawake 349.
Share:

Tuesday, 23 June 2026

SERIKALI YASISITIZA HAKI YA KUPANDA MADARAJA KWA WATUMISHI ,YATAMBUA VIPAJI VYA WENYE ULEMAVU



Na Dotto Kwilasa, Dodoma

Serikali imeagiza hatua za haraka zichukuliwe dhidi ya maafisa rasilimali watu wanaochelewesha watumishi wa umma kupanda madaraja licha ya kukidhi vigezo vinavyotakiwa, huku ikisisitiza uwajibikaji na haki katika usimamizi wa rasilimali watu serikalini.

Akizungumza wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma jijini Dodoma, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Profesa Riziki Shemdoe, alisema baadhi ya watumishi wamekuwa wakipata usumbufu mkubwa kufuatilia stahiki zao licha ya kutimiza masharti yote ya kupandishwa madaraja.

Amesema ni muhimu kwa maafisa rasilimali watu kutekeleza majukumu yao kwa wakati ili kuondoa malalamiko yasiyo ya lazima na kuongeza motisha kwa watumishi wa umma.

"Jaribuni kuvaa viatu vya watumishi hawa,Wapo wanaotoka maeneo ya mbali na kutumia muda na fedha nyingi kufuatilia stahiki zao hapa Dodoma ilhali wamekidhi masharti yote yanayotakiwa," amesema Prof. Shemdoe.

Kutokana na hali hiyo,ameagiza  kufanyika tathmini maalumu ya maafisa rasilimali watu waliosababisha ucheleweshaji wa madaraja katika mwaka wa fedha 2025/2026 ili hatua stahiki zichukuliwe.

Katika hatua nyingine,ameeleza kufurahishwa na mafanikio ya vijana wenye ulemavu wanaopata mafunzo ya ufundi stadi na kuibua vipaji vinavyoweza kuchangia maendeleo ya taifa.

Miongoni mwa waliovutia ni kijana Joseph ambaye ameonesha uwezo mkubwa katika usanifu wa majengo kwa kutumia mifumo ya kompyuta, jambo lililopelekea kuagizwa kutafutiwa ufadhili wa masomo pamoja na kuanza mchakato wa kupatiwa ajira ya kudumu serikalini.

Aidha, Serikali imeagiza kufanyika sensa ya mifumo yote ya TEHAMA inayotumika katika taasisi za umma ili kubaini kiwango cha matumizi yake na kuhakikisha mifumo hiyo inaunganishwa kwa lengo la kuongeza ufanisi, kupunguza urudufu na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Hatua hiyo ni sehemu ya mkakati mpana wa Serikali wa kuimarisha utawala bora, matumizi ya teknolojia na utoaji wa huduma bora kwa wananchi kupitia taasisi za umma.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger