Saturday, 8 August 2026

WAFANYABIASHARA WA MADUKA YA SIMU KARIAKOO WAPATA FURSA YA KUELEZA CHANGAMOTO ZAO KWA TRA


Kariakoo, 7 Agosti, 2026

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kariakoo imeendelea kusogeza huduma karibu na walipa kodi kwa kukutana na wafanyabiashara wa maduka ya simu katika Kijiwe cha Zungu, Kariakoo, kwa lengo la kusikiliza changamoto zinazowakabili na kutoa ufumbuzi wa masuala ya kodi na biashara.

Aidha, wafanyabiashara walipata fursa ya kueleza kwa uwazi changamoto wanazokutana nazo katika shughuli zao za kila siku,ikiwa ni pamoja na ujio wa wageni(wachina) ambao wanauza bidhaa kwa bei rahisi Zaidi huku wakipata ufafanuzi, maelekezo na majibu ya papo kwa hapo kutoka kwa viongozi wa TRA kuhusu namna bora ya kuzitatua.

Hata ivyo, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafabiashara Bw. Severine Mushi amesema kuwa “Kukutana na TRA kunaondoa hofu na kunatupa nafasi ya kusikilizwa, kuongeza uelewa wa masuala ya kodi na kutujengea imani katika utekelezaji wa majukumu ya kikodi kwa ufanisi zaidi.”

Akizungumza katika kikao hicho, Meneja wa TRA Mkoa wa Kariakoo Bw.Edson Issanya alisema mamlaka itaendelea kuwafikia walipa kodi katika maeneo yao ya biashara ili kutoa elimu, kusikiliza maoni yao, kutatua changamoto wanazokumbana nazo na kuendelea kuboresha huduma kwa lengo la kujenga mazingira wezeshi ya biashara.
Share:

TBS YENDELEA KUTOA ELIMU YA UTHIBITISHAJI UBORA WA BIDHAA NANENANE MOROGORO

Meneja wa TBS Kanda ya Dar es Salaam, Bi. Noor Meghji akitoa elimu ya Viwango kwa Wajasiriamali wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam  katika Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki yanayoendelea Mkoani Morogoro

*********

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limewataka wazalishaji wa bidhaa nchini kuhakikisha wanathibitisha ubora wa bidhaa zao ili kuondokana na vikwazo vya kibiashara na kuongeza wigo wa masoko ya kitaifa, kikanda na kimataifa.

Akizungumza wakati wa Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki, Meneja wa TBS Kanda ya Dar es Salaam, Bi. Noor Meghji, amesema shirika hilo linaendelea kuwasaidia wazalishaji na wajasiriamali kuhakikisha bidhaa zao zinakidhi viwango vinavyotakiwa, hatua inayoongeza uaminifu wa bidhaa katika soko.

Amesema katika kutambua umuhimu wa kuwawezesha wazalishaji wa bidhaa mbalimbali, TBS kwa kushirikiana na Shirika la Viwango la Afrika (ARSO), imezindua rasmi Alama ya Ubora ya Afrika, ambayo inalenga kusaidia bidhaa zinazokidhi viwango kuingia katika masoko ya Afrika kupitia Eneo Huru la Biashara Barani Afrika (AfCFTA).

Aidha, amewahamasisha wajasiriamali kuchangamkia fursa ya kuthibitisha ubora wa bidhaa zao kwa kuwa Serikali inagharamia huduma hiyo, hatua ambayo itawasaidia kuondokana na baadhi ya vikwazo vya kibiashara na kuongeza ushindani wa bidhaa zao.

“Hapo awali, bidhaa zilizothibitishwa na TBS ziliweza kuingia katika masoko ya nchi za Afrika Mashariki bila vikwazo vikubwa, lakini sasa wigo wa soko umeongezeka na bidhaa hizo zinaweza kunufaika na fursa zinazotokana na Eneo Huru la Biashara la Afrika (AfCFTA),” amesisitiza.

Kwa upande wake, Meneja wa TBS Kanda ya Mashariki, Mhandisi Cyril Kimario, amewataka wananchi kuhakikisha wananunua na kutumia bidhaa zilizothibitishwa ubora na TBS, huku akiwahimiza kujenga utamaduni wa kusoma taarifa zilizopo kwenye vifungashio.

Amesema kufanya hivyo kutawasaidia wananchi kupata taarifa sahihi kuhusu bidhaa wanazonunua na kuhakikisha wanapata bidhaa zenye ubora unaokidhi viwango.

“Kununua bidhaa zilizothibitishwa ubora wake humhakikishia mwananchi usalama wa afya yake pamoja na uchumi wake, kwani anakuwa amepata kitu bora chenye thamani katika afya na uchumi,” amesema.

Ameongeza kuwa ushiriki wa wananchi katika kuchagua bidhaa zenye alama na taarifa sahihi za ubora ni sehemu muhimu ya kujenga soko lenye ushindani na kulinda afya na maslahi ya watumiaji.
Meneja wa TBS Kanda ya Mashariki, Mha. Cyril Kimario akitoa elimu ya Viwango kwa Wajasiriamali wa Halmashauri ya Kibaha katika Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki yanayoendelea Mkoani Morogoro
Meneja wa TBS Kanda ya Dar es Salaam, Bi. Noor Meghji akitoa elimu ya Viwango kwa Wajasiriamali wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam  katika Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki yanayoendelea Mkoani Morogoro
Afisa udhibiti Ubora Mkuu (TBS) Bw. Stephen Rwabunywenge akitoa elimu ya viwango kwa wajasiriamali kutoka halmashauri mbali mbali za mikoa ya Tanga, Pwani, Morogoro na Dar es Salaam katika Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki yanayoendelea Mkoani Morogoro
Share:

Friday, 7 August 2026

Video Mpya : MALELE MJUKUU WA MALINGITA - DAWA YA UKIMWI

 

Share:

TBS YAENDELEA KUTOA ELIMU YA UBORA WA BIDHAA KATIKA MAONESHO YA NANENANE ARUSHA


SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limehimiza wajasiriamali kuchangamkia fursa ya kuthibitisha ubora wa bidhaa wanaozalisha bure kwa gharama za Serikali, hatua ambayo itawasaidia kuondokana na vikwazo vya kiabiashara.

Mbali na wito huo kwa wajasiriamali, shirika hilo limewataka wananchi kuhakikisha wananunua na kutumia bidhaa zilizothibishwa ubora na shirika hilo kwa kujenga utamaduni wa kusoma taarifa zilizopo kwenye vifungashio.

Wito huo umetolewa na Meneja wa TBS Kanda ya Kaskazini,, Yona Afrika,. wakati akizungumza kwenye Maonesho ya Nanenane yanayoendelea jijini Arusha.

Alisema Serikali inatambua mchango mkubwa wa wajasiriamali katika kukuza uchumi wa Taifa na wao binafsi, ndiyo maana imebeba dhamana ya kuthibitisha ubora wa bidhaa zao bure.

"Kwa hiyo tumeshiriki katika maonesho haya kwa sababu ni fursa ya kukutana na wadau mbalimbali na kuwaelezea shughuli zinazofanywa na TBS na fursa nyingine ambazo zinapatikana kama kuthibitisha bidhaa za wajasiriamali bure," alisema.

Alisema bidhaa zikishathibitishwa na TBS zinaingia masoko ya Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na ya kikanda bila vikwanzo vya biashara.

Alisema nchi za EAC zimeingia makubaliano, ambapo bidhaa zikishathitishwa na shirika la viwango la nchi husika,hazitakiwi kupimwa tena zinapopelekwa kwenye soko la nchi nyingine.

"Kwa hiyo TBS tumeshiriki maonesho haya kusudi kukutana na wadau mbalimbali, ambao tunawafikia na kuwapa taratibu za kufuata kuthibitisha ubora.

"Kwa kweli tunaishukuru Serikali kwa kuendelea kuandaa Maonesho haya ya Nanenane, kwani fursa muhimu ya kukutana na kutoa elimu kwa wadau.

Mfano tunawaambia kuwa wakipata barua ya utambulisho kutoka SIDO wakija kwetu utaratibu wa kuthibitisha ubora wa bidhaa unaanza mara moja, kwa wajasiriamali" alisema Afrika.

Kwa upande wa wananchi waliotembelea banda la TBS, walitakiwa kuhakikisha wanatumia bidhaa zilizothibitishwa ubora ili kulinda afya zao na kuona thamani ya fedha zao.

Alisema ni muhimu kusoma taarifa zilizopo kwenye vigungashio ili kujua kama zina ubora uliothititishwa na shirika pamoja na muda wake wa mwisho wa matumizi.

Share:

Thursday, 6 August 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA AGOSTI 7, 2026

Share:

BALOZI MBAROUK ASEMA ITALIA INA NAFASI KUBWA YA KULETA WATALII NCHINI


📌Aipongeza Wizara Ya Maliasili na Utalii kutangaza fursa za utalii nje ya nchi

📌Jaji Mruma naye atembelea Banda la Maliasili kujionea wanyamapori hai Nane Nane

Na Neema Chalila Mbuja, Dodoma

BALOZI wa Tanzania nchini Italia na Mwakilishi Mkazi  wa Shirika la Chakula na Kilimo la  Umoja wa Mataifa (FAO), Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) na Shirika la Chakula la Umoja wa Mataifa (WFP),  Mhe. Mbarouk  Nassoro Mbarouk leo Agosti 04, 2026,  ametembelea Banda la Wizara ya Maliasili na Utalii  na kusema kuwa nchi ya Italia ina nafasi kubwa ya kuleta watalii wengi nchini.

Mhe. Balozi Mbarouk amesema Tanzania inafanya vizuri kwenye kutangaza utalii na vivutio vyake  na kuipongeza Wizara kwa kazi nzuri inayoifanya.

Katika hatua nyingine Wizara ya Maliasili na Utalii  imepokea ugeni wa Jaji wa Mahakama ya Rufaa Mhe. Rajab Mruma ambaye ameitaka Wizara ya Maliasili na Utalii kubuni mbinu za kutafuta utatuzi wa  changamoto za wanyamapori hai kuingia kwenye makazi ya wananchi kwa kujenga  uzio ili kuzuia uharibifu unaoweza kutokea.

Aidha, Mhe Jaji Mruma ametembelea bustani ya wanyamapori  hai iliyoko kwenye Maonesho ya Nane  Nane yanayoendelea Jijini Dodoma ikiwa ni sehemu ya kutangaza utalii wa ndani kwa wananchi.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger