Thursday, 9 April 2026

GAVANA TUTUBA :TANZANIA IMEPIGA HATUA MIFUMO YA MALIPO YA KIKANDA



Na mwandishi wetu,Morocco

Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Emmanuel Tutuba, amesema Tanzania imepiga hatua kubwa katika kuunganishwa na mifumo ya malipo ya kikanda, hatua inayorahisisha upatikanaji wa huduma za kifedha ndani na nje ya nchi pamoja na kuchochea ukuaji wa uchumi.

Akizungumza leo Aprili 3, 2026 jijini Tangier, nchini Morocco, wakati wa mjadala wa mawaziri katika Kikao cha 58 cha Tume ya Uchumi ya Afrika (ECA), Gavana Tutuba amesema hatua hiyo inaifanya Tanzania kuwa sehemu muhimu ya mtandao wa malipo barani Afrika.

“Tanzania ni sehemu ya mifumo ya malipo ya kikanda ikiwemo Mfumo wa Malipo wa Afrika Mashariki (EAPS) na Mfumo wa Malipo wa Ukanda wa Kusini mwa Afrika (SADC RTGS). Kwa sasa benki za biashara nchini zinaendelea kujiunga na Mfumo wa Malipo wa Afrika (PAPSS), unaowezesha miamala ya kifedha kati ya nchi za Afrika kwa haraka na ufanisi,” amesema Bw. Tutuba.

Ameeleza kuwa kuimarika kwa mifumo hiyo kutachochea biashara ya mipakani na kuongeza ushirikiano wa kiuchumi barani Afrika, huku akibainisha kuwa hatua hiyo ni sehemu ya juhudi za kutumia teknolojia ya fedha kuboresha sekta hiyo.

Aidha, amesema uwepo wa mifumo hiyo ni matokeo ya maendeleo ya teknolojia ya fedha (fintech), akisisitiza kuwa BoT inaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa vijana wabunifu kupitia majukwaa mbalimbali ili kuibua suluhisho za kidijitali zitakazoboresha huduma za kifedha nchini.

Akizungumzia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, Gavana Tutuba amesema teknolojia ya fedha pamoja na ubunifu wa kidijitali vitaendelea kuwa nguzo muhimu katika kujenga uchumi imara, jumuishi na wenye ushindani.

Kikao hicho kimewakutanisha mawaziri wa fedha, mipango na maendeleo ya uchumi pamoja na magavana wa benki kuu kutoka nchi mbalimbali za Afrika kujadili mwelekeo wa uchumi wa bara hilo na namna ya kuimarisha mifumo ya kifedha.
Share:

JAMII YATAKIWA KUSHIRIKIANA NA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA KULINDA AMANI



Jamii imetakiwa kushirikiana kwa karibu na Vyombo vya ulinzi na usalama na mamlaka nyingine za uongozi zilizopo nchini katika kutoa taarifa za matukio ya uvunjifu wa amani, uhalifu na wahalifu pamoja na kutumia vyema mitandao ya Kijamii ili kudumisha na kuendeleza amani, utulivu na usalama wa nchi kama msingi mkuu wa uhai, maendeleo ya kiuchumi, kijamii na ustawi wa haki.

Kadhalika Waandishi wa habari hapa nchini wamehimizwa kutumia kalamu zao vyema na kuandaa maudhui kwenye majukwaa yao ya habari ya kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kudumisha amani nchini ili kuhakikisha kuwa amani hiyo inaendelea kuwepo pamoja na kuendeleza mshikamano wa Watanzania kwa kuuhabarisha kuhusu hatua mbalimbali za maendeleo na namna wanavyoweza kunufaika na amani na utulivu unaoendelea kuwepo nchini.

Wito huo umetolewa na  Epimark Aqwesso na  Gabriel Hilonga Silo, wakazi wa Wilayani Karatu Mkoani Arusha, wakitahadharisha watanzania kurejea katika matukio ya uvunjifu wa amani wakati na baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 na kadhia waliyokutana nayo kutokana na kukwama kwa shughuli za kiuchumi na kijamii.

"Amani tuliyonayo hapa nchini kwetu ndio inatufanya tuendelee kukusanyika na kufanya shughuli zetu nyingine za kijamii na kiuchumi. Mnakumbuka tukio la Oktoba 29, 2025? wengi wetu tulishindwa kufanya shughuli zetu, hofu ilitanda na wengi waliingia mitini na kujificha, hali hii isijirudie tena, Vijana wa sasa (GenZ) tukumbuke kuna maisha kesho na kamwe tusiharibu amani ya nchi yetu." Amesema Bw. Aqwesso.

Kwa upande wake Bw. Silo amehimiza Vijana kutumia vyema fursa ya amani iliyopo nchini kwa kujiendeleza kiuchumi, akieleza namna ambavyo serikali imeendelea kuwezesha wananchi kiuchumi kupitia sekta mbalimbali ikiwemo kilimo na ufugaji, akisisitiza kuwa amani ndio uhai wa Nchi na wananchi wake na kutaka jamii kushirikiana kuilinda.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI APRILI 9,2027



         
Share:

Wednesday, 8 April 2026

SERIKALI YAINUA UTALII WA TIBA: WAGONJWA WA NJE WAFIKIA 3,018



Na Shaban Juma, WAF – Dodoma

Serikali ya Tanzania inaendelea kuchukua hatua madhubuti za kukuza utalii wa tiba, ikiwa ni sehemu ya mikakati ya kuongeza uchumi wa sekta ya afya na mchango wake wa pato la Taifa.

Hayo yamesemwa leo Aprili 08, 2026, na Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Florence Samizi, bungeni jijini Dodoma, akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Dkt. Catherine Canute Joachim, katika Bunge la Kumi na Tatu, Mkutano wa Tatu, Kikao cha Nne.

Akijibu swali kwa niaba ya Waziri wa Afya,.Mhe. Mohamed Mchengerwa, Dkt. Samizi amesema Serikali chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, imewekeza zaidi kwenye uboreshaji wa miundombinu ya hospitali, ikiwemo kujenga majengo mapya na kukarabati yale yaliyochakaa.

Aidha, amesema Serikali inaendeleza upatikanaji wa vifaa tiba vya kisasa kama PET/CT Scan, Angio Suite, Cathlab, na CT Scan, sambamba na kuendeleza mafunzo ya kitaaluma kwa wataalamu wa afya ili kuhakikisha huduma zinakuwa za ubora wa kimataifa.

“Serikali pia inaanzisha huduma mpya za ubingwa bobezi na kuhakikisha hospitali zinapata ithibati za kimataifa, na kuzitangaza katika masoko ya kimataifa ili kuvutia wagonjwa kutoka nje ya nchi,” amesema Dkt. Samizi.

Takwimu zinaonyesha ukuaji wa utalii wa tiba: katika kipindi cha Julai 2025 hadi Februari 2026, wagonjwa 3,018 kutoka nje ya nchi walipatiwa huduma za ubingwa bobezi katika hospitali za rufaa za mikoa, kanda, maalum na taifa.

Aidha, Dkt. Samizi ameongeza kuwa Serikali inaendelea kuwekeza katika rasilimali watu kupitia Samia Health Super-specialization Program, ambapo wataalamu 1,483 wanafadhiliwa kusomea fani za ubingwa na ubingwa bobezi ndani na nje ya nchi, hatua inayolenga kuongeza ubora na uwezo wa hospitali zetu.
Share:

Tuesday, 7 April 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO APRILI 8,2026

Magazeti






Share:

BARRICK NORTH MARA YAWEZESHA VIJANA TARIME KUANZISHA MIRADI YA KIUCHUMI


Vijana wakiwezeshwa kuendesha miradi mbalimbali ikiwemo ya kilimo wataweza kujikwamua kiuchumi kama wanavyoonekana vijana wakiwa shambani kwenye mradi wa kilimo cha mboga wa Matongo unaofadhiliwa na Barrick North Mara (Picha kutoka maktaba)
Mgodi wa Barrick North Mara uliopo wilayani Tarime katika mkoa wa Mara umeendelea kutekeleza moja ya sera ya mkakati endelevu wa kampuni ya kuwezesha wananchi wanaoishi jirani na migodi yake kuwa na maisha bora ambapo kupitia fedha za uwajibikaji kwa jamii (CSR) umetoa shilingi milioni 220 kwa vikundi 13 vya vijana ili kuanzisha miradi ya kiuchumi katika vijiji vyote 11 vinavyozunguka mgodi huo.

Hatua hii ni mwendelezo wa mgodi wa Barrick North Mara kuwezesha kiuchumi makundi mbalimbali katika jamii hususani vijana ambapo mwaka jana iliunga mkono jitihada za Serikali za kuwapatia leseni za uchimbaji ambapo mgodi ulitoa leseni zake na kufadhili mafunzo ya vijana hao zaidi ya 1700 wanaojiandaa kuingia katika uchimbaji wa madini chini ya programu ya Mining For a Brighter Tomorrow (MBT) inayolenga kuboresha usalama, kuongeza tija na kuondoa uvamizi wa mgodi kwa kuwapatia rasmi maeneo ya uchimbaji.

Tayari vikundi hivyo vimepokea fedha hizo, ikiwa ni ruzuku ya (CSR) ya mwaka uliopita kutoka kwa mgodi huo ambao unaendeshwa kwa ubia na serikali kupitia kampuni ya Twiga Minerals.

Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jami wa Halmashauri hiyo, Anthony George Nyange amesema kuwa fedha hizo zimesaidia vijana takriban 100 wanachama wa vikundi hiyo kuanzisha miradi ya mbalimbali ya kiuchumi.
Anthony George Nyange

“Nawashukuru sana Barrick North Mara hususan idara ya mahusiano ya jamii kwa ushirikiano ambao wamekuwa wakitoa katika kufanikisha mpango huu wa ruzuku ya uwajibikaji kwa jamii kwa vijana,” amesema Nyange.

Nyange amesema miradi hiyo imesaidia kutatua changamoto mbalimbali zilizokuwa katika vijiji hivyo kwa ajili ya ustawi wa jamii vinavyouzunguka mgodi huo.

“Wanufaika wengi ni vijana na wamejielekeza kwenye miradi ambayo siyo tu kwa ajili ya kujipatia kipato bali pia kutatua changamoto zilizokuwepo,” amesema.

Ametaja vikundi ambavyo vimenufaika na mpango huo kuwa ni Mokarambe Agribusiness, Hope and Revolution of Economy for Youth, Tunza Mazingira Nyamongo, Amshana Nyamongo na REMHOCHI.

Vingine ni Kazi ni Moyo, Konna Nne, Kiumanya, Ibuka Umoja, Tunaweza Kerende, Nyasa Group, Mtazamo Youth na Kikundi cha Keryoba.

Amesema baadhi ya vikundi hivyo vimeanzisha miradi ya usafi wa mazingira jambo ambalo limesaidia kuweka mji mdogo wa Nyamongo katika hali nzuri ya usafi na mazingira.

“Kwa mfano, kulikuwa na changomoto ya usafi katika mji wa Nyamongo, sasa hali ya usafi ni nzuri kwa sababu kuna kikundi cha mazingira ambacho kinafanya vizuri sana kwenye usafi wa mazingira,” amesema Nyange.

Nyange amesema Halmashauri ya Wilaya ya Tarime itaendelea kutenga sehemu ya fedha za Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) zinazotolewa na mgodi wa Barrick North Mara kwa ajili ya kuwawezesha vijana kuanzisha na kuendeleza miradi ya kiuchumi.

“Tunategemea na mwaka huu pia tutatenga sehemu ya CSR kwenda kuwezesha vijana kwenye miradi ya kiuchumi. Sasa hivi, vijana wengi kule Nyamongo wana shughuli za kufanya kujipatia kipato na hata vitendo vya kihalifu vimepungua,” amesema Nyange.

Amesema mbali na mpango wa Uwajibikaji kwa Jamii (CSR), vijana hao pia wamenufaika na mikopo kupitia asilimia 10 ya mapato ya ndani inayotolewa na halmshauri hiyo kuwezesha wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

“Wanufaika wakubwa ni vijana, na mbali ya kunufaika na mikopo yetu ya halmashauri ya asilimia 10, pia wamenufaika na mpango wa ruzuku ya Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) kwa vijana,” amefafanua Nyange.

Taarifa zinaonesha Halmashauri ya Wilaya ya Tarime inaongoza kwa kutoa kiasi kikubwa cha mikopo ya asilimia 10 kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu katika Mkoa wa Mara.

Mgodi wa Barrick North Mara pamoja na kutekeleza sera ya Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) pia utoaji wa leseni za uchimbaji kwa vijana uliwezesha na mafunzo ya siku 14 yaliyofanywa kwa kushirikiana na serikali.

Lengo la mafunzo hayo ni kuhakikisha sekta ya madini iankuwa na tija zaidi kwa kuzingatia usalama mahali pa kazi na utunzaji wa mazingira , usimamizi wa biashara za madini na kufuata sheria za nchini na usimamizi wa vikundi pamoja na elimu ya masuala ya fedha.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE APRILI 7,2026

Magazeti



 













Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger