Mbunge wa Jimbo la Itwangi Azza Hillal Hamad akizungumza na wazee kwenye kijiwe cha Kahawa Butini na kusikiliza kero zao na kuzitolea majibu.
Na Marco Maduhu, SHINYANGA
Mbunge wa Jimbo la Itwangi Azza Hillal Hamad, amefanya mkutano wa hadhara katika kijiji cha Butini Kata ya Itwangi Wilaya ya Shinyanga, wa kusikiliza kero mbalimbali za wananchi na kuzitolea majibu.
TAZAMA VIDEO HAPA👇👇
Akizungumza leo Agosti 3, 2026, wakati wa mkutano huo, amesema baadhi ya kero tayari ameshazifanyia kazi, ikiwamo ukarabati wa barabara ya Itwangi–Mwakasomwe–Welezo, ambapo amesema mkandarasi tayari amepatikana na utekelezaji wa mradi huo utaanza muda wowote.
Pia amesema, barabara ya Butini–Nsalala, ambayo daraja lake lilikatika na kuchukua takribani miaka sita hadi saba bila kutengenezwa, sasa inakwenda kujengwa baada ya kazi hiyo kutangazwa rasmi, huku makalavati yakitarajiwa kujengwa katika maeneo husika.
“Nimekuja kusikiliza kero zenu ambazo ndizo vipaumbele vyenu, na kabla ya kuanza kusikiliza kero zenu, baadhi tayari nimekwisha anza zifanyia kazi zikiwama za ubovu wa miundombinu ya barabara na madaraja,” amesema Azza.
Akizungumzia changamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama, amesema tayari ameshaliwasilisha suala hilo kwa Waziri husika, na pia alilizungumzia bungeni wakati wa mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Maji.
Aidha, amesema ataendelea kupigania kuboreshwa kwa huduma za afya katika Jimbo la Itwangi, akieleza kuwa ndani ya miaka mitano ya uongozi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, wananchi watashuhudia mabadiliko makubwa katika Jimbo hilo.
“Jimbo la Itwangi lina kata 14, lakini lina vituo vya afya viwili tu. Tuna vijiji 58, lakini zahanati zinazotoa huduma ni 23 pekee, ninaamini ndani ya miaka mitano kutakuwa na mabadiliko makubwa chini ya uongozi wa Rais wetu Dk. Samia Suluhu Hassan, ndiyo maana aliligawa jimbo hili ili kuharakisha maendeleo,” amesema Azza.
Katika hatua nyingine, amemshukuru Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kusikiliza kilio cha wananchi wa Butini, Nsalala na Jimbo la Itwangi kwa ujumla, akisema ndani ya kipindi cha miezi sita tayari hatua mbalimbali zimeanza kuchukuliwa kutatua changamoto zinazowakabili.
Baadhi ya wananchi wa Butini waliowasilisha kero zao katika mkutano hu, wamelalamikia ukosefu wa maji safi na salama, uchakavu wa miundombinu ya skimu za umwagiliaji, ukosefu wa nyumba za watumishi wa afya, kutofikishwa kwa huduma ya umeme katika baadhi ya vitongoji, pamoja na ubovu wa miundombinu ya barabara, makalavati na madaraja.
TAZAMA PICHA👇👇
Mbunge wa Jimbo la Itwangi Azza Hillal Hamad akizungumza.
Mbunge wa Jimbo la Itwangi Azza Hillal Hamad akizungumza.
Mbunge wa Jimbo la Itwangi Azza Hillal Hamad akizungumza.
Mbunge wa Jimbo la Itwangi Azza Hillal Hamad akiwashukuru wananchi kwa kumpigia kura nyingi Rais Dk. Samia Suluhu Haasan katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025, pamoja na kumpigia kula yeye na Diwani wa Itwangi Ldya Pius.
Mbunge wa Jimbo la Itwangi Azza Hillal Hamad akizungumza na wazee kwenye kijiwe cha Kahawa Butini na kusikiliza kero zao na kuzitolea majibu.
Mbunge wa Jimbo la Itwangi Azza Hillal Hamad akizungumza na wazee kwenye kijiwe cha Kahawa Butini na kusikiliza kero zao na kuzitolea majibu.
Diwani wa Itwangi Lidya Pius akizungumza.
Katibu wa UVCCM wilaya ya Shinyanga Mkola Kabali akizungumza.
Diwani wa Viti maalumu Anastazia Njile akizungumza.