Tuesday, 19 May 2026

SERIKALI YASISITIZA UHURU WA KUKOSOA SI MATUSI

WAZIRI wa Katiba na Sheria, Dk Juma Homera amesema watu wanaoitukana Serikali, kufanya uchochezi na vitendo visivyo vya maadili mitandaoni, majina yao yameshakabidhiwa kwa Wizara ya Mambo ya Ndani ili Jeshi la Polisi ili wachukuliwe hatua za kisheria.

Aliyasema hayo jana wakati akifungua mkutano wa siku wa mafunzo kwa mawakili wa serikali yaliyoandaliwa na Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali jijini Arusha.

Dk. Homera alitoa kauli hiyo akijibu ombi la Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Dk. Damas Ndumbaro aliyetaka mawakili wa serikali kuisaidia Serikali dhidi mashambulizi na upotoshaji unaofanywa mitandaoni.

Dk. Homera alisema majina ya wahusika wa uhalifu huo tayari yamekabidhiwa Wizara ya Mambo ya Ndani kwa hatua za kisheria.

Alisema kuna Sheria ya Mitandao, sheria za Jeshi la Polisi na sheria ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ambazo zinadhibiti upotoshaji, uchochezi na uvunjifu wa maadili, hivyo serikali itahakikisha inazisimamia ili kukomesha uhali huo nchini.

"Serikali haikatai kukosolewa, lakini ikoselewa kwa jambo la haki na kweli na si jambo la uongo, na kutumia lugha ya matusi au uchochezi, hivyo wahusika watachukuliwa hatua za kisheria ili kuimarisha amani na usalama,"alisisitiza Dk Homera.

Aliongeza"Jeshi la Polisi limeanza kuchukua hatua dhidi ya wanaoitukana serikali, kufanya uchochezi na vitendo visivyo vya maadili mitandaoni."

Kuhusu mafunzo hayo, alisema yatawasaidia mawakili wa serikali kuishauri serikali ipasavyo na kwa weledi, kuwa na uelewa mpana wa masuala mbalimbali, kujengewa uelewa kuhusu miradi ya ubia kati ya sekta ya umma na sekta binafsi (PPP) na masuala mengine mbalimbali.

Alisema Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali inafanya kazi nzuri ya kuitetea serikali katika mashauri mbalimbali na kufanikiwa kuisadia serikali kuokoa zaidi ya shilingi trilioni moja kwa kushinda kesi hizo.

Naye Wakili Mkuu wa Serikali, Dk Ally Possi alisema katika kipindi cha Julai 2025 hadi Machi 2026, kati ya mashauri 641, serikali ilishinda mashauri 595 sawa na asilimia 88.1 na kuokoa Sh bilioni 316.3 ambayo serikali ingelipa kama ingeshindwa mashauri hayo.

Kuhusu mashauri ya usuluhishi, alisema mashauri 18 yamekamilika na serikali kuokoa Sh bilioni 6.8 katika kipindi hicho.

"Kwa hiyo katika mashauri yote ya madai na usuluhishi kuanziaJulai 2025 hadi Aprili 2026, Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali tumeisadia Serikali kuokoa shilingi trilioni 1.35,"alisema Dk Possi.

Aliongeza"Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali ilianzishwa mwaka 2018, na moja ya mafanikio makubwa tuliyoyapata ni kuitetea serikali katika kesi ya kukamatwa kwa ndege yetu na kushinda."

Pia alisema mafunzo hayo kwa mawakili wa serikali yanalenga kulinda kila senti ya mlipakodi, kutetea rasilimali za serikali, kuongeza uwezo wa mawakili katika nyanja mbalimbali, kujinoa kitaaluma, na kuendesha mashauri kwa weledi na umahiri.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Dk. Damas Ndumbaro alisema kuna haja kwa mawakili wa serikali kuja na mpango wa namna ya kuitetea serikali dhidi ya mashambulizi na upotoshaji mkubwa dhidi ya serikali.

"Nini nafasi ya mawakili wa Serikali katika jambo hili? Nashauri kupitia mafunzo haya jadilianeni nini cha kufanya ili kuihudumia nchi na jamii yetu kwa weledi,"alisema Dk. Ndumbaro

Pia alisema kwa kuwa asilimia 36 ya migogoro yote iliyoibuliwa na timu ya Msaada wa Kisheria ya Samia imetokana na ardhi, hivyo alimuomba Wizara ya Katiba na Sheria kulifanyia utafiti jambo hilo ili kujua chanzo na kuja na suluhu ya kuikomesha migogoro hiyo.

Dk Ndumbaro aliwataka mawakili hao wa serikali kujifunza kwa vitendo kupitia mashauri mbalimbali wanayoshinda na kushindwa ili kufanya mabadiliko ya kisheria yanayohitajika kwa maslshi ya taifa na kuleta ufanisi katika sekta ya sheria.

Kwa mujibu wake, Februari 2018, Tanzania ilifanya mageuzi makubwa katika sekta ya sheria nchini kwa kupangilia upya nafasi tatu ikiwemo Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali na Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP).

Alisema mageuzi hayo yamesaidia kuleta ufanisi katika sekta ya sheria nchini.

Naye Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, Alice Mtulo alisema mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo Mawakili wa serikali kuhusu uendedhaji wa mashauri ya madai na usuluhishi.

Alisema jumla ya washiriki 600 wanahudhuria mafunzo hayo wakiwemo mawakili kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, taasisi za serikali na Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali.

Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Samwel Maneno alisema mawakili wa serikali wanawajibu wa kuisaidia serikali kwa kutoa ushauri mzuri wa kisheria pale serikali inapoingia mikataba na sekta binafsi ambayo ni injini ya uchumi wa taifa.

Maneno alisema Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imeshasajili mawakili zaidi ya 30 katika kitengo cha ushirikiano kati ya sekta ya umma na binafsi (PPP) katika kutekeleza miradi ya ubia.

Naye Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Zanzibar, Shaaban Abdalla aliwataka mawakili hao wa serikali kusimamia mashauri ya madai na usuluhishi kwa weledi na uzalendo kupitia mafunzo wanayopewa.

Mtendaji Mkuu wa Mahakama Tanzania, Profesa Elisante Ole Gabriel alisema kwa kuwa Mahakama ni chombo cha juu na cha mwisho katika kutoa haki, hivyo Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali ni mdau muhimu katika jambo hilo.
Share:

SERIKALI KUENDELEA KUBORESHA VITUO VYA MAARIFA NCHINI.



Na, Mwandishi wetu - Pwani

SERIKALI kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) imeeleza dhamira yake ya kuendelea kuboresha Vituo vya Maarifa nchini, hususan vile vinavyotoa huduma kwa madereva wa malori ya masafa marefu kuhusu masuala ya VVU na UKIMWI.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Dkt. Jim Yonazi mapema mwanzoni mwa wiki mara baada ya kutembelea na kukagua Vituo vya Maarifa vinavyotoa huduma za VVU na UKIMWI kwa madereva wa malori ya masafa marefu vilivyopo eneo la Kurasini katika wilaya ya Temeke Jijini Dar es Salaam na Mdaula mkoa wa Pwani ambayo Vituo hivyo vipo chini ya Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS).

Dkt. Yonazi amesema Serikali, kupitia Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS), ina jukumu la kusogeza huduma muhimu za VVU na UKIMWI karibu na wananchi.

“Vituo hivi vina mchango mkubwa katika kuwafikia madereva wa masafa marefu ambao mara nyingi hukaa safarini kwa muda mrefu. Serikali itaendelea kuviboresha hususan kwenye miundombinu ya kutolea huduma na kuongeza wataalam wa afya ili viweze kutoa huduma bora Kwa madereva hao wa masafa marefu kwa kujua afya zao dhidi ya maambukizi ya virusi vya UKIMWI,” amesema Dkt. Yonazi.

Kwa upande wao, madereva wa malori ya masafa marefu wanaonufaika na huduma hizo wameeleza kuwa Vituo vya Maarifa ni msaada mkubwa kwao, kwani vinawapa fursa ya kupata elimu na huduma za VVU na UKIMWI kwa urahisi na bila gharama na kuipongeza Serikali kwa namna inavyoendelea kujali na kuwafikia wananchi wake.








Share:

Monday, 18 May 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE MEI 2026


Magazeti
 

Share:

Wimbo Mpya : GUDE GUDE - DUNIA

 

Share:

SERIKALI KUENDELEA KUBORESHA MAZINGIRA YA BIASHARA KARIAKOO


NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SERIKALI imesema itaendelea kuboresha mazingira ya biashara nchini ili kuhakikisha wafanyabiashara wa Kariakoo wanakuwa na ushindani wa kikanda na kimataifa huku ikiitaja Kariakoo kuwa moyo wa biashara wa Tanzania na injini muhimu ya uchumi wa taifa.

Hayo yameelezwa leo Mei 17, 2026 katika hafla ya Utoaji wa Tuzo za Biashara Kariakoo ambapo Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Bw. Aristides Mbwasi, aliyemwakilisha Waziri wa Wizara hiyo, amesema Kariakoo si eneo la kawaida katika historia ya biashara nchini bali ni alama ya uchapakazi, uthubutu na mafanikio ya Watanzania wengi.

Amesema Kariakoo imekuwa sehemu iliyojenga maisha ya maelfu ya wananchi, huku vijana wengi wakianza biashara kwa mitaji midogo na baadaye kuwa waajiri wakubwa.

“Kila siku maelfu ya watu wanaingia Kariakoo kufanya biashara, kununua bidhaa, kuwekeza na kusafirisha bidhaa kwenda ndani na nje ya nchi ikiwemo DRC, Burundi, Rwanda, Zambia, Malawi, Uganda na Comoro,” amesema.

Mbwasi amesema Serikali imeendelea kuweka mazingira bora ya biashara, uwekezaji na viwanda ili wafanyabiashara waweze kushindana katika soko la kimataifa.

Akizungumzia ujenzi wa Soko Kuu la Kariakoo baada ya janga la moto, amesema Serikali ilihakikisha soko hilo linajengwa upya kwa kiwango kikubwa zaidi ambapo mradi huo uligharimu takribani shilingi bilioni 28 na kuwa na zaidi ya maduka 2,000.

Amesema Serikali inaamini sekta binafsi ni mshirika mkuu wa maendeleo ya uchumi, ndiyo sababu imeendelea kuboresha mazingira ya biashara, kurahisisha uwekezaji, kupanua miundombinu ya masoko na kuimarisha huduma za kidigitali.

Aidha, amewahakikishia wafanyabiashara kuwa Serikali itaendelea kusikiliza changamoto zao na kuhakikisha wanapata mazingira yenye utulivu, uwazi na usalama wa mitaji yao.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kariakoo Business Awards, Zakayo Shushu, amesema tuzo hizo zimeanzishwa kwa lengo la kutambua ubunifu, uwekezaji na juhudi za wafanyabiashara wanaofanya biashara kwa uaminifu na weledi mkubwa.

Amesema tuzo hizo zinalenga kukuza biashara zinazoaminika pamoja na kuchochea ushindani wa kitaalamu ili wafanyabiashara wa Kariakoo waweze kushindana katika soko la ndani na la kimataifa.

“Tunataka kujenga mazingira ya ushindani wa kimataifa na kuhakikisha wafanyabiashara wetu wanakuwa sehemu ya ushindani mkubwa wa biashara duniani,” amesema.

Shushu ameongeza kuwa ajenda nyingine muhimu ni kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na sekta binafsi pamoja na kuhakikisha sauti ya mlaji inasikilizwa na kuthaminiwa.

Amesema kwa kushirikiana na Serikali, wadau wa maendeleo na sekta binafsi, wamepanga kuanzisha majukwaa mbalimbali yatakayoinua Kariakoo pamoja na uchumi wa Tanzania kwa ujumla.

Aidha, amebainisha kuwa kuna mikakati ya kuanzisha mafunzo kwa wafanyabiashara pamoja na kampeni maalumu za kuitangaza Kariakoo duniani kama kitovu muhimu cha biashara.

Amesema maboresho ya miundombinu ya biashara, mazingira ya uwekezaji pamoja na utatuzi wa changamoto za wafanyabiashara yameendelea kuongeza imani ya wafanyabiashara kwa Serikali yao.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger