Sunday, 14 June 2026

TGNP YATAKA NGUVU ZAIDI KATIKA UTEKELEZAJI WA BAJETI YA 2026/2027

Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) umeiomba Serikali kuhakikisha Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2026/2027 inatekelezwa kwa ufanisi ili kufanikisha malengo ya maendeleo ya taifa yaliyowekwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Akizungumza jijini Dar es Salaam wakati wa mjadala na uchambuzi wa Bajeti ya Taifa ya mwaka 2026/2027 kupitia jukwaa la Kijiwe cha Kahawa, mwakilishi wa TGNP, Flora Ndaba, alisema pamoja na bajeti ya mwaka huu kuonesha kuzingatia masuala ya usawa wa kijinsia, bado kuna umuhimu wa kuweka nguvu kubwa katika utekelezaji wake ili matokeo yaliyokusudiwa yaweze kupatikana.
Alisema utekelezaji madhubuti wa bajeti ndiyo utakaowezesha wananchi, hususan wanawake, vijana na makundi yaliyo pembezoni, kunufaika na rasilimali zilizotengwa na serikali.

Kwa upande wake, Evans Exaud alisema bajeti ya mwaka huu imeonesha kuipa kipaumbele sekta binafsi, hususan wafanyabiashara, jambo ambalo linaweza kuchochea ukuaji wa uchumi na kuongeza fursa za ajira kwa wananchi.
Alieleza kuwa mazingira bora ya biashara yatasaidia kufikia malengo ya maendeleo yaliyowekwa na serikali kwa kuongeza uzalishaji na mapato ya taifa.

Wakati huo huo, baadhi ya vijana waliohudhuria mjadala huo walitoa maoni tofauti kuhusu bajeti hiyo, wakisisitiza umuhimu wa serikali kuendelea kuangalia hali halisi ya maisha ya wananchi ili kuhakikisha maendeleo yanayopatikana yanawanufaisha wote.

Awali, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP, Clara Kalanga, alisema jukwaa hilo linalenga kutathmini Bajeti ya Taifa ya mwaka 2026/2027 kwa mtazamo wa kijinsia na kuangalia namna itakavyowezesha kufikiwa kwa malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Kalanga alisema bajeti yenye kuzingatia usawa wa kijinsia ni nyenzo muhimu katika kuhakikisha makundi yote ya jamii yanashiriki na kunufaika na maendeleo ya taifa kwa usawa.
Wadau wa maendeleo, wanaharakati, wataalamu wa uchumi na viongozi wa serikali za mitaa wakifuatilia mjadala wa uchambuzi wa Bajeti ya Taifa ulioandaliwa na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) kupitia jukwaa la Kijiwe cha Kahawa.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JUNI 14,2026


Magazeti



Share:

Saturday, 13 June 2026

OFISI YA WAZIRI MKUU NA OMDTZ ZAIMARISHA UTAYARI WA JAMII KUKABILIANA NA MAFURIKO DAR ES SALAAM




Na, mwandishi wetu - Dar es Salaam

Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Taasisi OpenMap Development Tanzania (OMDTZ), kupitia mradi wa Ramani Zetu, Sauti Zetu imeendesha warsha ya kupitia na kuthibitisha Mipango ya Kujiandaa na Kukabiliana na Maafa kwa kata tano za Makurumula, Mabibo, Keko, Ubungo na Tabata jijini Dar es Salaam.

Warsha hiyo imewakutanisha viongozi wa serikali za mitaa, Kamati za Usimamizi wa Maafa za Kata, wataalamu wa usimamizi wa maafa, waratibu wa maafa wa mkoa na wilaya pamoja na wadau mbalimbali kwa lengo la kuhakikisha mipango hiyo inakidhi mahitaji halisi ya jamii zinazokabiliwa na hatari ya mafuriko Dar es Salaam.

Akifungua warsha hiyo Mkurugenzi Msaidizi wa Operesheni za Maafa kutoka Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Kanali Selestine Masalamado amesema kuwa ubora wa mpango wa maafa hupimwa kwa uwezo wake wa kutekelezeka na kuleta matokeo chanya kwa wananchi, huku akisisitiza umuhimu wa mipango hiyo kuzingatia mazingira halisi, rasilimali zilizopo na uwezo wa taasisi husika.

“Mradi huu unaofadhiliwa na Zayed Sustainability Prize kupitia Taasisi ya Open Map Development Tanzania (OMDTZ), kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu – Idara ya Usimamizi wa Maafa, umekuja wakati sahihi na tunamatarajio makubwa katika kuleta matokeo chanya kuhakikisha tunaimarisha masuala ya usimamizi wa maafa nchini, ”alisema Kanali Masalamado

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa OMDTZ, Bw. Innocent Maholi, alisema taasisi hiyo itaendelea kushirikiana na Serikali katika kuimarisha ustahimilivu wa jamii dhidi ya maafa kupitia matumizi ya teknolojia, uchoraji ramani shirikishi na uwekezaji katika mifumo ya tahadhari ya mapema katika maeneo hatarishi.


Naye Mratibu wa Maafa wa Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Gerald Sondo, amepongeza ushirikiano huo akieleza kuwa mipango hiyo itasaidia kuongeza utayari wa jamii, kuboresha uratibu wa mwitikio wa dharura na kupunguza athari za mafuriko katika Jiji la Dar es Salaam.

“Kwa kipindi cha miezi mitatu iliyopita, kamati za usimamizi wa maafa katika kata husika zimefanya tathmini ya vihatarishi, kubainisha njia za uokoaji na maeneo salama, kuandaa mifumo ya mawasiliano na uratibu pamoja na kupendekeza hatua za tahadhari ya mapema zinazoshirikisha jamii,”alisema Bw. Sondo.

Aliongezea kuwa, Mipango iliyothibitishwa itatumika kama mwongozo wa vitendo kwa jamii kabla, wakati na baada ya maafa, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha usalama wa wananchi na ustahimilivu dhidi ya mafuriko na majanga mengine.





Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JUNI 13,2026


Magazeti









Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger