Saturday, 18 April 2026

WACHIMBAJI WA MADINI MWAKITOLYO WALIA NA TOZO MPYA YA HALMASHAURI,UZALISHAJI WA SUASUA

Share:

RAIS SAMIA AMERIDHIA MILIONI 544 ZILETWE BAHI KUJENGA SHULE YA SEKONDARI CHIFUTUKA - PROF. SHEMDOE



Na OWM - TAMISEMI, Bahi

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amesema Mhe. Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amemuarifu kuwa, Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia ombi la wananchi wa Kata ya Chifutika lililowasilishwa na Mbunge wa Jimbo la Bahi Mhe. Kenneth Nollo la kupatiwa shilingi milioni 544 kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Sekondari Chifutuka ambayo itakidhi uhitaji wa wananchi wa kata hiyo. 

Prof. Shemdoe amesema hayo leo Aprili 17, 2026 wakati wa hafla ya kuwapongeza walimu na wanafunzi waliofanya vizuri kwenye mitihani ya kitaifa darasa la nne, darasa la saba, kidato cha pili na kidato cha nne wilayani Bahi, iliyofanyika kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Chiona wilayani humo. 

“Mhe. Mbunge alinifuata kabla sijasimama kuzungumza, akiomba shule ya sekondari ijengwe Kata ya Chifutika, nikawasiliana na Mhe. Waziri Mkuu na kuliwasilisha ombi hilo kwa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye ameridhia milioni 544 ziletwe kujenga shule ya sekondari,” amesema Prof. Shemdoe.

Kutokana na kuridhiwa kwa kiasi hicho cha fedha, Prof. Shemdoe kwa niamba ya wananchi wa Kata ya Chifutuka Wilayani Bayi amemshukuru kwa moyo wa dhati Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na Mhe. Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchema kwa upendo mkubwa waliouonesha kwa wananchi wa Kata hiyo Chifutuka.

Prof. Shemdoe amefafanua kuwa, fedha hizo zimeridhwa na Mheshimiwa Rais kwasababu lengo la Serikali ni kuendelea kuimarisha elimu nchini,  ikizingatiwa kuwa Bahi imeonesha juhudi kubwa na kuwa Halmashauri ya kwanza kitaifa kwenye ufaulu wa mitihani ya darasa la saba kwa mwaka 2025.






Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI APRILI 18,2026


Magazeti





Share:

Friday, 17 April 2026

OFISI YA AFISA MADINI MKAZI MKOA WA SINGIDA YATOA MAFUNZO KWA WACHIMBAJI WADOGO KWA USHIRIKIANO NA UNDP



Na mwandishi wetu,Singida

Ofisi ya Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Singida, kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), imeendesha mafunzo maalum kwa wachimbaji wadogo wa madini yenye lengo la kuongeza uelewa kuhusu uchimbaji salama, wenye tija na unaozingatia utunzaji wa mazingira.

Mafunzo hayo yamelenga kuwajengea wachimbaji uwezo katika matumizi ya teknolojia bora za uchimbaji, usimamizi wa afya na usalama migodini, uongezaji thamani wa madini pamoja na kuimarisha biashara ya madini kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za sekta ya madini.

Akifungua mafunzo hayo yaliyofanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Singida, Afisa Madini Mkazi wa Mkoa huo, Mhandisi Sabai Nyansiri, amesema Serikali inaendelea kuweka mazingira rafiki kwa wachimbaji wadogo ili kuhakikisha sekta ya madini inachangia kikamilifu maendeleo ya wananchi na uchumi wa Taifa kwa ujumla.

Ameongeza kuwa mafunzo hayo ni sehemu ya juhudi za Serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo katika kuwawezesha wachimbaji wadogo kuongeza tija, kipato na kuendesha shughuli zao kwa kuzingatia misingi ya usalama, uhifadhi wa mazingira na uendelevu wa rasilimali madini.


Share:

MTANDA AAGIZA UKAGUZI MKALI WA MAZINGIRA MWANZA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda, ametoa wito kwa wananchi kushiriki ipasavyo katika kutunza Mazingira huku akilitaka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) pamoja na maafisa mazingira wa Halmashauri kuendelea kufanya kaguzi za mara kwa mara za kimazingira ili kuhakikisha usafi na usalama wa mazingira unaimarishwa.

Akizungumza katika kikao na viongozi wa NEMC pamoja na wanahabari, Mhe. Mtanda alisisitiza umuhimu wa utekelezaji madhubuti wa Sheria za mazingira ili kulinda rasilimali za asili na afya ya jamii.

Alieleza kuwa kwa mujibu wa Sheria ya Usimamizi wa Mazingira Na. 191, Serikali imeweka marufuku kwa shughuli zote zinazochangia uchafuzi wa mazingira, hususan katika maeneo ya vyanzo vya maji na maeneo tengefu.

Aidha, alifafanua kuwa Kifungu cha 57 cha sheria hiyo kinakataza mtu yeyote kujenga, kufanya shughuli au kutupa taka ndani ya umbali wa mita 60 kutoka kwenye chanzo cha maji au eneo la hifadhi, hatua inayolenga kulinda rasilimali hizo muhimu.

Mhe. Mtanda alibainisha kuwa marufuku hiyo imekuja kufuatia ongezeko la vitendo vya uharibifu wa mazingira vinavyohatarisha vyanzo vya maji, afya za wananchi pamoja na uendelevu wa rasilimali za asili.

Hivyo, serikali imechukua hatua za makusudi kuhakikisha maeneo muhimu ya kimazingira yanahifadhiwa ipasavyo.

Katika kuimarisha utekelezaji huo, serikali kupitia mamlaka za mikoa na halmashauri imeongeza juhudi katika usimamizi wa mazingira, ikiwemo kulinda misitu, kuhifadhi vyanzo vya maji na kuboresha miundombinu ya ukusanyaji na utupaji wa taka.

Sambamba na hilo, ukaguzi wa kimazingira unaendelea kufanyika katika maeneo mbalimbali yenye shughuli za kijamii na kiuchumi kama vile baa, kumbi za starehe, viwanda na maeneo ya biashara.

Lengo la ukaguzi huo ni kuhakikisha kuwa shughuli zote zinaendeshwa kwa kuzingatia viwango vya usafi, usalama na utunzaji wa mazingira.

Alionya kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya wote watakaobainika kukiuka sheria za mazingira.

Hatua hizo ni pamoja na kufutiwa leseni za biashara na kuchukuliwa hatua nyingine za kisheria kwa wahusika wa vitendo kama utupaji taka ovyo, ujenzi holela katika vyanzo vya maji na uchomaji wa misitu.

Aidha, serikali inaendelea kushirikiana na wananchi kwa kutoa elimu ya mazingira na kuendesha kampeni za uhamasishaji ili kuongeza uelewa wa umuhimu wa kuhifadhi mazingira.

Ushirikiano huo umetajwa kuwa ni muhimu katika kuhakikisha matumizi endelevu ya rasilimali za asili kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA APRILI 17,2026




magazeti

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger