Wednesday, 12 August 2026

KATIBU WA BARAZA LA VYAMA VYA SIASA: MARIDHIANO NA MAZUNGUMZO NDIYO NJIA SAHIHI YA KATIBA MPYA


Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa, Juma Ali Khatib, amesema kuwa Rais Samia Suluhu Hassan ameendelea kuonesha dhamira ya dhati katika mchakato wa kupatikana kwa katiba mpya kupitia maridhiano, mazungumzo, na ushirikishwaji mpana wa wadau mbalimbali wa kitaifa.

Kauli hiyo imetolewa kufuatia mkutano uliozikutanisha jumla ya vyama vya siasa 19 vilivyohudhuria Ikulu jijini Dar es Salaam, huku Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kikikosekana baada ya kususia mazungumzo hayo.


Khatib amesisitiza kuwa mchakato wa kupata katiba mpya hauwezi kufikiwa kwa misimamo mikali au kugomea mikutano ya mashauriano, bali unahitaji nia njema na utayari wa kusikiliza mawazo ya wengine kupitia utekelezaji wa falsafa ya 4R inayosisitiza umoja, mshikamano, na ustahimilivu.


Amemuunga mkono Rais Samia kufuatia mipango ya kuunda tume maalumu ya kuchunguza na kutatua masuala ya vurugu za kisiasa zilizopita kwa kuzingatia mapendekezo ya Tume ya Jaji Chande, sambamba na kuimarisha misingi ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa kupitia makubaliano ya hivi karibuni kati ya CCM na ACT Wazalendo huko Zanzibar. Vilevile, serikali imeweka mikakati thabiti kupitia sera za ajira, ujasiriamali, na sekta ya kilimo ili kuwaondoa vijana katika hatari ya kutumiwa kwenye migogoro ya kisiasa na kuwashirikisha kikamilifu katika ujenzi wa uchumi wa taifa.


Viongozi wengine mbalimbali wakiwemo Katibu wa Chama cha Demokrasia Makini, Ameir Hassan Ameir, mgombea wa zamani wa urais wa Zanzibar kupitia NCCR-Mageuzi, Lela Rajab Khamis, na Makamu Mwenyekiti wa UWT, Zainab Shomari, wamempongeza Rais Samia kwa uongozi wake unaojumuisha makundi yote katika ujenzi wa taifa na kuimarisha misingi ya demokrasia na maridhiano nchini
Share:

SERIKALI YAWEKA MKAKATI WA HIFADHI YA BIONUAI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni akiwasilisha taarifa kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira kuhusu mkakati na mpango kazi wa Taifa wa hifadhi ya bioanuai, taarifa hiyo ameiwasilisha Bungeni Agosti 11, 2026.

***************

NA; MWANDISHI WETU, DODOMA

Serikali, kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, imeendelea kuimarisha uwezo wa kitaalamu na utafiti katika masuala yanayohusu bioanuai, pamoja na kujenga na kuimarisha mfumo thabiti wa kisheria na utawala ili kuwezesha uhifadhi na matumizi ya rasilimali za bioanuaii nchini kwa manufaa ya sasa na ya kizazi kijacho.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni ameyasema hayo wakati akiwasilisha taarifa kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira kuhusu mkakati na mpango kazi wa Taifa wa hifadhi ya bioanuai, taarifa aliyoiwasilisha Bungeni Agosti 11, 2026.

Amesema, wadau mbalimbali zikiwemo Wizara za Kisekta, Taasisi za serikali na zisizo za serikali, makampuni binafsi, wadau wa Maendeleo na makundi ya Kijamii, huhitajika kuutekeleza mkakati huu.

“Mkakati huu hutekelezwa kwa kuhuisha masuala ya bioanuai kwenye mipango ya kisekta, ikiwemo Kuandaa programu maalumu ya hifadhi ya bioanuai kwa sekta husika, pamoja na kuandaa na kutekeleza miradi mbalimbali inayohusu hifadhi ya bioanuai.”

Utekelezaji wa Mkakati huu unachangia utekelezaji wa mikakati mingine ya Mazingira ikiwemo; Mpango Kabambe wa Taifa wa Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (2022-2032), Sera naMkakati wa Uchumi wa Buluu (2024).

“Matokeo ya utekelezaji wa Mkakati huu utachangia katika kuimiarisha hali ya uhifadhi wa mazingira nchini kufikia asilimia 25 na kufanya jumla ya asilimia 65 ya uhifadhi nchini ifikapo mwaka 2030.

“Kiasi hicho kitachangia nguzo ya tatu ya Dira 2050 katika eneo la hifadhi ya bioanuai ambapo tunatarajia kwamba ifikapo mwaka 2050 Tanzania itakuwa miongoni mwa nchi kumi (10) bora Afrika katika kuhifadhi mazingira.”

Mkakati wa Taifa wa bioanuai (2025-2030) umeshirikisha wadau mbalimbali katika mchakato wa uaandaji wake. Wadau hao ni pamoja na Wizara za kisekta; Taasisi za serikali na zisizo za serikali; na Makundi ya jamii.

Mkakati na Mpango kazi wa Kitaifa wa Bioanuwai (2025 2030) ni mwongozo wa kitaifa unaotoa mwelekeo na umeainisha mikakati ya inayopaswa kutekeleza ili kuwezesha uhifadhi na  matumizi ya rasilimali za bioanuaii nchini kwa manufaa ya sasa na ya kizazi kijacho.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Jackson Kiswaga amesema kwa kutambua kuwa suala la mazingira ni mtambuka, Ofisi ya Makamu wa Rais iendelee kushirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha programu ya elimu kwa umma kuhusu mazingira inawafikia wadau wengi zaidi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. MhandisiHamad Yussuf Masauni akiwasilisha taarifa kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira kuhusu mkakati na mpango kazi wa Taifa wa hifadhi ya bioanuai, taarifahiyo ameiwasilisha Bungeni Agosti 11, 2026.

PICHA NA OFISI YA MAKAMU WA RAIS
Share:

BITEKO: TANZANIA IMEPIGA HATUA KUBWA KATIKA AJENDA YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA


📌 Asema wajibu wa kila Mtanzania ni kuhakikisha mafanikio yanakuwa endelevu

KIZIMKAZI, ZANZIBAR

Naibu Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Bukombe, Mhe. Dkt. Doto Biteko, amesema Tanzania imepiga hatua kubwa katika utekelezaji wa Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia, huku akisisitiza kuwa ni wajibu wa kila Mtanzania kuhakikisha mafanikio yaliyopatikana yanaendelea kuwa endelevu.

Dkt. Biteko amesema hayo wakati akishiriki mjadala kuhusu “Uongozi wa Kimkakati wa Tanzania katika Kuharakisha Mabadiliko ya Nishati Endelevu na Jumuishi”, uliofanyika katika Mdahalo wa Nishati Safi ulioandaliwa na Taasisi ya Mwanamke Initiative Foundation (MIF), Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.

Amesema uwepo wa Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia ni sehemu ya jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye ameendelea kuipa msukumo ajenda hiyo katika ngazi mbalimbali za uongozi wake na kuifikisha hadi katika majukwaa ya kimataifa.

Dkt. Biteko amesema umuhimu wa kuendelea kuipa kipaumbele ajenda hiyo unatokana na ukubwa wa athari za matumizi ya nishati isiyo safi ya kupikia, ikiwemo uharibifu wa mazingira unaosababishwa na matumizi ya kuni na mkaa, ambapo takribani hekta 470,000 za misitu hupotea kila mwaka nchini.

Aidha, amesema zaidi ya watu 33,000 hupoteza maisha kila mwaka kutokana na magonjwa yanayohusishwa na uchafuzi wa hewa wakati wa kupika, hali inayoonesha umuhimu wa kuongeza kasi ya mpito kuelekea matumizi ya nishati safi.

Ameongeza kuwa matumizi ya nishati isiyo safi yana athari za kijinsia, hususan kwa wanawake ambao hutumia muda mwingi kutafuta kuni badala ya kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji na maendeleo ya kiuchumi.

Amesema athari hizo pia zinawagusa watoto, ambapo baadhi yao hukosa muda wa kutosha wa kuhudhuria masomo kutokana na kulazimika kusaidia familia zao kutafuta kuni kwa ajili ya kupikia.

Katika mjadala huo, Dkt. Biteko amesisitiza umuhimu wa kufanya tathmini za mara kwa mara ili kubaini kiwango cha uendelevu wa matumizi ya nishati safi ya kupikia, hususan baada ya wananchi kuwezeshwa kupata teknolojia na miundombinu husika.

Amesema tathmini hizo zitasaidia Serikali na wadau kubaini changamoto zilizopo, kupima matokeo yaliyofikiwa na kuweka mikakati madhubuti zaidi ya kuendeleza matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.

Pia, Dkt. Biteko ameipongeza Taasisi ya Mwanamke Initiative Foundation (MIF) kwa kuwa miongoni mwa taasisi zinazochangia utekelezaji wa Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia kupitia shughuli mbalimbali, ikiwemo kusaidia upatikanaji wa miundombinu pamoja na kuendesha midahalo inayowakutanisha wadau kujadili namna bora ya kuharakisha matumizi ya nishati safi, salama na endelevu nchini.



Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO AGOSTI 12,2026



magazeti















Share:

Tuesday, 11 August 2026

UCSAF YABORESHA MINARA 431 ILI KUCHOCHEA MAENDELEO


Meneja wa kanda ya Ziwa wa Mfuko wa Mawasiliano kwa wote(UCSAF) Fredy Kandonga, akizungumza kwenye semina hiyo.
Meneja wa kanda ya Ziwa wa Mfuko wa Mawasiliano kwa wote(UCSAF) Fredy Kandonga, akizungumza kwenye semina hiyo.
Meneja wa kanda ya Ziwa wa Mfuko wa Mawasiliano kwa wote(UCSAF) Fredy Kandonga, akizungumza kwenye semina hiyo.
Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari mkoa wa Mwanza(MPC) Edwin Soko akizungumza kwenye semina hiyo.
Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari mkoa wa Mwanza(MPC) Edwin Soko akizungumza kwenye semina hiyo.
Ofisa Mawasiliano Mwandamizi wa UCSAF Celina Mwakabwale, akizungumza kwenye semina hiyo
Baadhi ya Wahariri wa vyombo vya habari vya kanda ya Ziwa wakifuatilia mada mbalimbali katika semina hiyo.
Baadhi ya Wahariri wa vyombo vya habari vya kanda ya Ziwa wakifuatilia mada mbalimbali katika semina hiyo.
Baadhi ya Wahariri wa vyombo vya habari vya kanda ya Ziwa wakifuatilia mada mbalimbali katika semina hiyo.
Baadhi ya Wahariri wa vyombo vya habari vya kanda ya Ziwa wakifuatilia mada mbalimbali katika semina hiyo.
Baadhi ya Wahariri wa vyombo vya habari vya kanda ya Ziwa wakifuatilia mada mbalimbali katika semina hiyo.


Na Mwandishi wetu

Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) umeongeza kasi ya huduma ya intaneti Kanda ya Ziwa baada ya kubadilisha minara 431 kutoka teknolojia ya 2G kwenda 3G/4G, hatua inayolenga kuwawezesha wananchi kupata huduma za intaneti zenye ubora zaidi na kuwaletea maendeleo.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger