Thursday, 17 September 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI SEPTEMBA 17,2026




Magazeti


Share:

Wednesday, 16 September 2026

SIMBA SC YAICHAKAZA AZAM FC NYUMBANI


Kikosi cha Wekundu wa Msimbazi, Simba SC, kimeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Azam FC katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliochezwa leo, Septemba 16, 2026, kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.

Mabao yote ya Simba yalifungwa kipindi cha pili, ambapo Rushine De Reuck alifunga dakika ya 59, kabla ya Clatous Chama kuongeza la pili dakika ya 69.

Azam ilijaribu kutafuta mabao ya kusawazisha, lakini ilishindwa kupata nafasi ya kuvunja ulinzi wa Simba hadi mchezo ulipomalizika.

Matokeo hayo yanaifanya Simba kufikisha pointi 18 baada ya kucheza michezo sita, ikiwa na rekodi ya kushinda michezo yote sita hadi sasa.

Simba inafikisha pointi hizo sawa na Yanga SC, ambayo pia ina pointi 18 baada ya kucheza michezo sita.

Kwa upande wa Azam FC, timu hiyo inabaki na pointi 14 baada ya kucheza michezo saba.
Share:

SOMALIA, FCC ZAKUBALIANA KUIMARISHA USHIRIKIANO WA KIBIASHARA





Na.Mwandishi Wetu

Tume ya Ushindani ya Somali imefanya ziara ya siku moja nchini Tanzania kwa lengo la kujifunza uzoefu na mbinu zinazotumiwa na Tume ya Ushindani Tanzania (FCC) katika kusimamia ushindani wa kibiashara, kudhibiti bidhaa bandia na kulinda maslahi ya walaji.

Ziara hiyo imefanywa na Mkurugenzi wa Masuala ya Uchumi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ya Jamhuri ya Shirikisho la Somalia na Kamishna wa Mamlaka ya Ushindani ya Afrika Mashariki (EACA), Bw. Ahmed Warsame pamoja na Mkurugenzi wa Biashara na Upatikanaji wa Masoko wa Wizara ya Biashara na Viwanda ya Jamhuri ya Shirikisho la Somalia, Bw. Abdihalim Osman.

Katika ziara hiyo, ujumbe huo umekutana na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Khadija Ngasongwa, pamoja na uongozi wa Tume, ambapo walipata fursa ya kujifunza namna FCC inavyotekeleza majukumu yake ya kukuza na kulinda ushindani, kumlinda mlaji na udhibiti wa bidhaa bandia.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, uongozi wa ujumbe wa Somalia umepongeza utendaji wa FCC, ukieleza kuwa uzoefu wa Tanzania katika kusimamia ushindani na kulinda mlaji ni muhimu kwa Somalia katika kuimarisha mifumo yake ya usimamizi wa soko na kukuza mazingira bora ya biashara.

Ujumbe huo umeeleza kuwa kujifunza kutoka FCC kutasaidia kuongeza uelewa na uwezo wa taasisi za Somalia katika kukabiliana na changamoto zinazohusu ushindani usio wa haki, bidhaa bandia na vitendo vinavyoweza kuwadhuru walaji.

Kwa upande wake,Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Khadija Ngasongwa, amesema kuwa Tanzania ipo tayari kuendelea kushirikiana na taasisi za Somalia na nchi nyingine katika kubadilishana uzoefu, maarifa na mbinu bora za usimamizi wa ushindani na ulinzi wa walaji.

Ziara hiyo ya siku moja imekuwa fursa muhimu kwa Somalia kujifunza uzoefu wa Tanzania katika eneo la ushindani wa kibiashara, udhibiti wa bidhaa bandia na ulinzi wa mlaji, hatua inayotarajiwa kuimarisha ushirikiano wa kitaasisi na kuchangia katika ujenzi wa masoko yenye ushindani wa haki na biashara endelevu.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO SEPTEMBA 16,2026



Magazeti



Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger