Monday, 24 August 2026
Sunday, 23 August 2026
WASIRA: CCM ITAHAKIKISHA UCHUMI WA TANZANIA UNAENDELEA KUWA IMARA

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira, amesema CCM inalenga kuhakikisha uchumi wa Tanzania unakua kwa asilimia saba ifikapo mwaka 2030, huku ukichochea ongezeko la kipato na kuboresha maisha ya wananchi.
Wasira amesema hayo Agosti 21,2026 wakati akizungumza na viongozi pamoja na wanachama wa CCM mkoani Singida.
Amesema katika Ilani ya CCM, chama hicho kimeweka msisitizo wa kukuza uchumi jumuishi unaolenga kumwezesha kila Mtanzania kunufaika na ukuaji wa uchumi.
“Katika Ilani yetu tumesema tunataka uchumi mkuu ambao kila siku mnasikia Tanzania uchumi wako unakuwa kwa asilimia 6.3. Lakini hii haitoshi. Tunataka uchumi huu usaidie maisha ya mtu mmoja mmoja,” amesema Wasira.
Ameeleza kuwa CCM inalenga kuona mapato ya wananchi yanaongezeka, huku akitolea mfano wakulima wa alizeti mkoani Singida ambao, kwa mujibu wake, wana nafasi kubwa ya kuongeza kipato kupitia kilimo na uwekezaji katika viwanda vya kuchakata zao hilo.
Wasira amesema Serikali imeweka hatua mbalimbali, ikiwamo kuongeza kodi kwa mafuta ya kula yanayoagizwa kutoka nje, kwa lengo la kuwahamasisha wakulima wa alizeti kuongeza uzalishaji na hivyo kuongeza mapato.
Amesema hatua hiyo pia inalenga kuchochea uanzishwaji wa viwanda vya kusindika alizeti, ambavyo vitaongeza thamani ya zao hilo na kutoa ajira kwa wananchi.
“Nyinyi hapa ni wakulima wakubwa sana wa alizeti. Tumeweka kodi zaidi kwa mafuta yanayotoka nje ili kuwatia moyo watu wa Singida na mikoa inayolima alizeti waweze kulima zaidi, waongeze mapato, tuweke viwanda, viajiri watu, halafu maisha yaendelee kufanya nini? Kupanda,” amefafanua.
Kwa mujibu wa Wasira, dhamira hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa dhana ya uchumi jumuishi inayolenga kuhakikisha kila Mtanzania anapata nafasi ya kuongeza kipato na kuboresha maisha yake.
Amesema dira hiyo pia imeainishwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050, ambayo tayari imeanza kutekelezwa kwa kuweka msingi wa maendeleo yanayolenga kuifikisha Tanzania katika uchumi unaozalisha fursa kwa wananchi wengi zaidi.
Ameeleza kuwa wanaodai kuwa hali ya maisha haijabadilika hawazingatii hatua ambayo nchi imepiga, akiwataka wananchi kutambua tofauti iliyopo kati ya hali ya sasa na miaka iliyopita.
Amefafanua kuwa CCM itaendelea kusimamia utekelezaji wa sera na Ilani yake kwa lengo la kuhakikisha ukuaji wa uchumi unaambatana na ongezeko la kipato, ajira na fursa za kiuchumi kwa wananchi.
GENDER ACTIVISTS PLEDGE TO STRENGTHEN WOMEN’S VOICE IN TANZANIA’S CONSTITUTIONAL REFORM
WILDAF Coordinator Advocate Anna KulayaBy Rose Ngunangwa
Gender activists in the country have reiterated their commitment to form an inclusive technical task force to consolidate women’s priorities in Tanzania’s constitutional reform process.
They have also resolved to develop a Women’s Constitutional Review Law Reform Model while conducting a baseline survey to assess citizens’ understanding of the constitutional reform process.
The commitment was made in Dar es Salaam midweek during a follow-up meeting aimed at strengthening women’s collective voice and influence in Tanzania’s constitutional reform process. The meeting was conducted by Women in Law and Development in Africa (WILDAF), Tanzania Chapter.
The meeting further resolved to undertake capacity-building initiatives and implement community awareness campaigns on constitutional matters, reaching people from street, hamlet and village levels to urban areas.
Other resolutions included coordinating media engagement through community radio, digital platforms, mainstream newspapers, artificial intelligence (AI), and television journalists to raise public awareness of constitutional affairs.
During the process, stakeholders will draw lessons from the Warioba Draft and the Proposed Constitution, as well as from previous constitutional reform processes, while incorporating emerging priorities.
Speaking during the session, Dr. Victoria Lihiru described the law-making process as the backbone of constitutional review, as it is where the rules of the game are established.
Commenting on the composition of constitutional commissions, Dr. Lihiru called on gender activists to assess not only the number of women participating, but also their positions and leadership roles.
“It is not enough to be a member. Leadership determines voice and influence, as wider representation alone does not automatically guarantee sufficient representation of women, youth, persons with disabilities and other groups,” said Dr. Lihiru.

For her part, WILDAF Coordinator Advocate Anna Kulaya called on gender activists to support one another, build on the work of Women and Constitution, and retain the 12 women’s constitutional agendas as an important foundation while also addressing emerging issues.
The discussions also reviewed Tanzania’s constitutional history, including the 1962 Constitution, the 1964 Union between Tanganyika and Zanzibar, the 1965 constitutional amendment that introduced a single-party system, the 1977 Constitution, and the constitutional review process that culminated in the Warioba Draft and the Proposed Constitution.
Tanzania’s current Constitution dates back to 1977 and will mark its 50th anniversary in 2027.




Magazeti
