Thursday, 3 September 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO SEPTEMBA 03, 2026

                         

Share:

Wednesday, 2 September 2026

MWENYEKITI SENETI MKOA WA IRINGA AONGOZA KIKAO MAALUMU CHA KAMATI YA URATIBU


Mwenyekiti wa Seneti Mkoa wa Iringa Joseph Masaniro George, Ameongoza Kikao Maalumu cha Kamati ya Uratibu Seneti Mkoa wa Iringa, Kilichofanyika tarehe 01 Septemba 2026 , Ukumbi wa Nyerere Ofisi za CCM mkoa Wa Iringa kikao chenye lengo la Kujadili Masuala Mbalimbali yanayohusu Wanafunzi wa Vyuo na Vyuo Vikuu Ndani ya Mkoa wa Iringa.





Share:

Tuesday, 1 September 2026

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI AFANYA ZIARA YA KIKAZI IDARA YA UHAMIAJI TANZANIA





Konstebo Josephat Mtema,Dsm

‎Leo September 01,2026 katika Ofisi ya Uhamiaji kurasini, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Patrobas Katambi (Mb) amefanya ziara ya Kikazi.

‎Waziri Katambi alipokelewa na mwenyeji wake Kamishna Jenerali wa Uhamiaji CGI Dkt. Anna Makakala na kuanza Ziara yake kwa kufanya kikao na Makamishna wa uhamiaji kwa kusomewa Ripoti maalumu kutoka Idara ya Uhamiaji Tanzania ripoti Iliyosomwa na CGI Dkt. Makakala.

‎Katika Ripoti hiyo CGI Dkt. Makakala alimweleza Mhe. Katambi kwamba Idara ya Uhamiaji inamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuiwezesha Idara katika kuendelea kutekeleza Miradi ya maendelea kwa kujenga Ofisi za uhamiaji kwa ngazi ya Wilaya na makazi ya Watumishi wa Uhamiaji kwa Tanzania Nzima na kufunga mifumo ya utoaji huduma kwa Kidigitali.

‎Aidha Waziri Katambi alipata Fursa pia ya kutembelea Mifumo mbalimbali iliyowekwa katika ofisi ya Uhamiaji Kurasini ya utoaji huduma na kuzungumza pia na Wananchi na wageni waliofika kupatiwa huduma za kiuhamiaji

‎"Nimeridhishwa na Utoaji huduma na ripoti iliyosomwa mbele yangu inaonesha jinsi gani Idara ya Uhamiaji Tanzania inafanya kazi zake kiweledi kwa kufata sheria na kanuni za nchi pia haki na wajibu kwa kila mtu niwahase Watumishi wa Uhamiaji kuendelea kutoa huduma bora pasipo upendeleo wowote kwa Mwananchi na wageni wanaofika Tanzania kwani kufanya hivyo kutaleta taswira nzuri kwa Idara yetu ya Uhamiaji" , alisema Waziri Katambi.

‎Ziara hii ya kikazi ni mwendelezo wa ziara zake katika Taasisi na Idara zilizopo katika wizara ya mambo ya ndani ya nchi pamoja na kukagua Miradi mbalimbali ya maendeleo.

Share:

PROF. SHEMDOE AELEKEZA WAFANYABIASHA 30 SOKO LA NDIZI MABIBO KUREJESHWA SOKONI



Na: OWM – TAMISEMI, Dar es Salaam

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, ameelekeza waliokuwa wafanyabiashara 30 wa soko la ndizi Mabibo (Mahakama ya Ndizi) kurejea kufanya biashara kwa udhamini wa maandishi kutoka ofisi za Serikali za Mitaa.

Prof. Shemdoe ametoa maelekezo hayo Agosti 31, 2026 katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi Ndogo ya OWM- TAMISEMI jijini Dar es Salaam, mara baada ya kupokea taarifa ya timu ya ufuatiliaji wa malalamiko ya wafanyabiashara hao wa soko la ndizi Mabibo, wakati wa kikao kazi chake na wafanyabiashara hao.

Aidha, Prof. Shemdoe ameilekeza Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo kufanya tathmini ya mali ya Bw. Frego Njovu aliyewasilisha madai ya kuomba kurejeshewa fedha alizotumia kukarabati choo kilichopo sokoni hapo ambacho alikuwa akikisimamia.

Katika kuhakikisha haki inatendeka, Prof. Shemdoe ameelekeza bidhaa za mfanyabiashara Bw. Enock Kimwayeya aliyekuwa Mwenyekiti wa Wafanyabiashara waliowasilisha malalamiko kwa Prof. Shemdoe, arejeshewe bidhaa zake alizoziacha kwenye kibanda cha biashara pindi alipoondolewa, kwani taarifa ya timu ya ufuatiliaji imeainisha kuwa Halmashauri imekiri kwamba bidhaa za mfanyabiashara huyo zipo. 

Ili kuimarisha usimamizi wa soko, Prof. Shemdoe amemuelekeza Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo kumpeleka meneja wa soko mwingine kulisimamia soko hilo na aliyepo kupangiwa majukumu mengine.

Maelekezo hayo ya Prof. Shemdoe yametokana na maafikiano baina ya pande zote katika kikao kazi cha Waziri huyo na walalamikaji (wafanyabiashara) na walalamikiwa ambao ni Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo. 

Malalamiko ya wafanyabiashara hao 30 yaliwasilishwa kwa Prof. Shemdoe kupitia andiko lao la tarehe 15/01/2026 lililohusu Sakata la soko la Ndizi Mabibo wakilalamikia kupigwa marufuku kuingia sokoni, kutaifishwa na kuuzwa kwa maeneo yao ya biashara, aidha Manispaa ya Ubungo iliwaondoka sokoni wafanyabiashara hao kwa tuhuma za kuhamasisha vurugu na kutoitambua manispaa hiyo kama msimamizi wa soko.












Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger