Wednesday, 29 July 2026

SANGU: WADAU TUCHANGIE MADAWATI




Na Mwandishi wetu, Sumbawanga

Wadau wa maendeleo ndani na nje ya mkoa wa Rukwa wamehamasishwa kuchangia upatikanaji wa madawati kwa ajili ya kuwezesha watoto kusoma kwenye mazingira wezeshi kwa ustawi wa taaluma.

Wito huo umetolewa hivi karibuni na Mbunge wa Jimbo la Kwela ambaye pia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu wakati alipokabidhi madawati kwa shule za msingi katika jimbo hilo alipofanya ziara ya kikazi.

Katika ziara hiyo sangu alikabidhi madawati  zaidi ya 100 kwa shule za msingi sita (6) yenye thamani ya shilingi Milioni 60 ambayo ameyapata kupitia ufadhili ya Benki ya Taifa ya Biashara (NBC).

Waziri Sangu akizungumza kwenye moja ya mikutano yake na wananchi wa kijiji cha Nankanga tarafa ya Kipeta na kijiji cha Ilemba alisema ametoa msaada huo kuunga mkono jitihanda za wananchi katika kuchangia maendeleo ya elimu.

“ Nimekuja hapa kukabidhi zawadi ndogo kwa Watoto.Leo nimewaletea madawati 20 ambapo yatasaidia Watoto 60 kutoendelea kukaa chini” alisema Waziri Sangu.

Mbunge huyo aliongeza kuwaambia wananchi kuwa yeye ni mbunge wa vitendo na kwamba anapenda vitu vinavyoonekana ambapo aliitumia fursa hiyo kushukuru uongozi wa Benki ya NBC kwa kuguswa na shida za wanaKwela .

“Ninashukuru benki ya NBC kwa msaada wao waliotupatia madawati haya yanayokwenda kupunguza tatizo la watoto kukaa chini. utatuzi huu wa kero za wananchi ni sehemu ya maelekezo tuliyopewa na Rais  Dkt. Samia Suluhu Hassan kwetu wabunge” alisema Sangu alipoongea na wananchi wa Kijiji cha Msia kata ya  Milepa huku akitoa wito kwa wadau wengine wa maendeleo kuchangia madawati kwa ajili ya jimbo la Kwela.

Miongoni mwa shule zilizopokea madawati hayo na idadi yake kwenye mabano ni shule ya msingi Kalumbaleza (20), Msia (20), Kimambo (15), Ilemba (20) , Nankanga (20) na Deusi Sangu sekondari madawati (30).

Akizungumza kwa niaba ya wananchi, Diwani wa kata ya  Mwadui Mahmood Leonce Mgweno alisema amepokea madawati toka Ofisi ya Mbunge na kwa tayari amefikisha shuleni na kumpongeza Mbunge Sangu kwa msaada.

Nao wananchi wametumia fursa ya ziara ya mbunge Sangu kueleza kufurahishwa kwao na jitihada anazozifanya kuchangia maendeleo ya jimbo hilo ikiwemo msaada wa madawati.

Nae Bwa.Thomas Nsandale ameishukuru Ofisi ya Mbunge kwa kuwezesha wa upatikanaji wa  madawati ikiwa ni miongoni mwa vingi walivyopatiwa katika kipindi chote Mhe.Sangu akiwa Mbunge wa Jimbo la Kwela 

“Sangu amefanya mambo mengi ambayo yanatufanya sisi wananchi kutokupunguza upendo juu yake na tunamuomba pia Madawati haya yasiwe ya mwisho kwa wananchi wake wa Kwela Bali iwe sababu ya muendelezo wa Maendeleo haya” amesema Nsandale.

Waziri Sangu alikuwa jimboni Kwela wilaya ya Sumbawanga kukagua shughuli za maendeleo pamoja na kuzungumza na wananchi.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO JULAI 29, 2026

Magazetini Leo



Written by Alex Sonna














Share:

Tuesday, 28 July 2026

RAIA WANNE WA UHOLANZI MIONGONI MWA WALIONUSURIKA AJALI YA BOTI ZIWA NYASA

Eneo la tukio la ajali ya ziwa Nyasa iliyotokea baada ya boti kupinduka na kusababisha manusura wa ajali  bandari ya Mbamba Bay wilayani Nyasa mkoani Ruvuma 
Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Ahmed Abbas Ahmed akiwa amewasili eneo la ajali iliyotokea ziwa Nyasa katika bandari ya Mbamba Bay wilayani humo

Na Regina Ndumbaro

Nyasa -Ruvuma 

Watu saba, wakiwemo raia wanne wa Uholanzi, wamenusurika kufa maji baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kutoka Bandari ya Mbamba Bay, wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma kuelekea nchini Malawi kupata ajali katika ziwa Nyasa. 

Share:

MBINGA YATENGA EKARI TANO KWA SIDO KUANZISHA KONGANO YA VIWANDA KUKUZA AJIRA NA UONGEZAJI THAMANI WA MAZAO

Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Mbinga DC mkoani Ruvuma Joseph Kashushura wa tatu kulia pamoja na meneja wa SIDO Ruvuma( Baraka Kandoga wa tatu kushoto )akiwa katika moja za ofisi za SIDO wakati wa ziara yake yeye pamoja na menejimenti yake kwa lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya shirika hilo 
Mashine zinazozalishwa na SIDO Ruvuma chini ya uongozi wa meneja  wake Baraka Kandoga

Na Regina Ndumbaro Songea-Ruvuma 

Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma imetenga ekari tano katika Kata ya Ngembambili kwa ajili ya uanzishaji wa Kongano ya Viwanda chini ya usimamizi wa Shirika la Maendeleo ya Viwanda Vidogo (SIDO), hatua inayolenga kuongeza thamani ya mazao, kukuza viwanda vidogo na vya kati, kuanzisha ajira mpya na kuimarisha uchumi wa wananchi. 

Share:

Monday, 27 July 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE JULAI 28, 2026

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger