Sunday, 13 September 2026

WANAFUNZI 150 KUNUFAIKA NA UFADHILI WA MASOMO ALGERIA


Tanzania imepata nafasi 150 za ufadhili wa masomo nchini Algeria kwa wanafunzi waliofanya vizuri, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa Serikali kuongeza fursa za elimu ya juu nje ya nchi.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, amesema Serikali ya Algeria itagharamia ada za masomo, wakati Serikali ya Tanzania itagharamia fedha za kujikimu kwa wanafunzi hao kupitia utaratibu wa Samia Scholarship.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Septemba 11, 2026, jijini Dar es Salaam, Prof. Mkenda amesema fursa hiyo ni mwendelezo wa juhudi za Serikali kuhakikisha wanafunzi wa Kitanzania wanapata nafasi zaidi za kusoma katika vyuo vya nje.

Amesema kati ya wanafunzi 1,000 waliotangazwa kupata Samia Scholarship, wanafunzi 10 tayari wamechaguliwa kwenda kusoma Moscow, Urusi, hatua inayodhihirisha ongezeko la fursa za masomo ya juu nje ya nchi.

Amesema majina ya wanafunzi 150 watakaochaguliwa kwa ajili ya masomo nchini Algeria yatawekwa kwenye tovuti ya Wizara, pamoja na maelekezo kuhusu namna ya kuwasilisha nyaraka na taratibu nyingine muhimu za safari, ikiwemo upatikanaji wa hati za kusafiria.

Prof. Mkenda amesema Serikali inalenga kuhakikisha fursa hizo zinawanufaisha wanafunzi kutoka makundi mbalimbali katika jamii, wakiwemo watoto wa wakulima na wafugaji.

Aidha, amewataka wanafunzi watakaopata nafasi hizo kuwa tayari kujifunza lugha ya Kifaransa, ambayo hutumika katika sehemu kubwa ya masomo nchini Algeria.
Share:

BARRICK NORTH MARA, JUMUIYA YA WATUMIA MAJI WAFANIKISHA UPANDAJI MITI 47,200 KUHIFADHI MTO TIGHITE


Sehemu ya viongozi na wafanyakazi wa Barrick North Mara (kulia), viongozi wa Jumuiya ya Watumia Maji Mto Tighite Chini na Kijiji cha Matongo wakikagua maendeleo ya mradi huo Siku ya Mazingira Duniani 2026. (Picha za Maktaba)
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watumia Maji Mto Tighite Chini, Mwita Seri, akiwa kwenye kitalu cha miche ya asili inayooteshwa kwa ajili ya kupandwa kandokando ya Mto Tighite.
Ushirikiano wa Jumuiya ya Watumia Maji Mto Tighite (JWMT) na Kampuni ya Barrick kupitia Mgodi wake wa dhahabu wa North Mara umefanikisha upandaji wa miti ya asili 47,2000 kati ya 50,000 ambao utasaidia kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na kulinda chanzo hicho cha maji kinachotegemewa katika shughuli mbalimbali za ustawi wa jamii na utunzaji wa mazingira.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watumiaji maji wa Mto Tighite, Bw. Mwita Seri amesema mradi huo unaotekelezwa kwa ufadhili wa Barrick North Mara unalenga kurejesha uoto wa asili na kuimarisha uhifadhi wa mto huo uliopo Nyamongo, Wilaya ya Tarime.

Amesema Tanzania kama zilivyo nchi nyingine duniani inakabiliwa na tishio la majanga yanayotokana na mabadiliko ya tabia nchi kutokana na uharibifu wa mazingira hususani kupitia kukata miti ovyo, shughuli za kilimo na kiuchumi.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Bw. Seri, mradi huo unalenga kurejesha uoto wa asili na kuimarisha uhifadhi wa mto huo uliopo Nyamongo, wilaya ya Tarime, mkoani Mara.

“Miti hiyo imepandwa katika eneo lenye ukubwa wa takriban ekari 40,” Seri amewaambia waandishi wa habari wilayani Tarime.

Amebainisha kuwa eneo lililopandwa miti hiyo ni sehemu ya ekari 100 za kingo za Mto Tighite zinazotakiwa kurejeshewa uoto wa asili kutokana na uharibifu wa mazingira.

Hivyo, upandaji wa miti 47,200 kwenye ekari 40 ni hatua ya awali katika safari ndefu ya kurejesha uoto wa asili wa Mto Tighite uliopo jirani na Mgodi wa North Mara.

Seri ameongeza mradi huo unatarajiwa kuchangia katika kulinda kingo za mto huo kwa kuzuia mmomonyoko wa udongo na kurejesha mazingira ya asili yaliyoharibiwa.

Mwenyekiti huyo wa Jumuia ya Watumia Maji, alitumia nafasi hiyo pia kuishukuru Barrick North Mara kwa kutoa shilingi milioni 36.7 kuwezesha uanzishaji na utekelezaji wa awali wa mradi huo.

“Barrick wamesaidia sana kufanikisha mradi huu, kwani fedha hizo ziligharamia uoteshaji wa miche ya miti ya asili, upandaji, ulinzi wa awali wa miti hiyo na uwekaji wa nguzo za chuma za uzio wa mradi huo,” amesema Seri.

Aidha, Seri ametoa wito kwa jamii zinazozunguka mto huo kuunga mkono mradi huo kwa kuhakikisha kuwa unafanikiwa bila kuhujumiwa kwa namna yoyote ile.

“Jamii inayozunguka Mto Tighite nayo ina wajibu wa kuonesha ushirikiano na juhudi za kulinda miti iliyopandwa ili iweze kukua na kutimiza lengo la kurejesha uoto wa asili wa mto wetu,” ameeleza.

Pia, amesisitiza umuhimu wa kuendelea kuwezesha mradi huo kifedha na kitaalamu ili kuhakikisha mafanikio yaliyoanza kuonekana yanaendelea kudumu na kuleta matokeo chanya ya muda mrefu kwa mazingira na jamii.

Mradi wa kurejesha uoto wa asili wa Mto Tighite unatajwa kuwa na umuhimu mkubwa wa kimazingira kutokana na nafasi ya chanzo hicho cha maji katika mfumo wa ikolojia ya eneo hilo.

Ulizinduliwa wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani mwaka jana kwa lengo la kurejesha uoto wa asili wa mto huo unaotegemewa na maelfu ya watu kwa ajili ya maji ya matumizi ya nyumbani, kunywesha mifugo na shughuli za kilimo.

Hivi karibuni Mgodi wa North Mara uliungana na Jumuiya ya Watumia Maji Tighite Chini na wakazi wa kijiji cha Matongo kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani, kwa kutembelea na kukagua maendeleo ya mradi huo.

Wadau hao, wakiongozwa na Mwenyekiti wa Kijiji cha Matongo, Charles Ryoba, walieleza kuridhishwa na ukuaji wa miti iliyopandwa na hatua zinazochukuliwa kurejesha uoto wa asili wa mto huo baada ya kuathiriwa na ukataji wa miti ovyo.

Ushirikiano wa Barrick North Mara na jumuiya hiyo unaweka msingi wa hatua zaidi za kuhusisha jamii, taasisi na wadau wengine katika kukamilisha upandaji wa miti ya asili kwenye ekari 100 za kingo za Mto Tighite.

Mto Tighite ni miongoni mwa vyanzo muhimu vinavyochangia maji katika Mto Mara ambao unamwaga maji yake katika Ziwa la kimataifa - Ziwa Victoria upande wa Tanzania.

Mbali na uwezeshaji wa kupanda miti maeneo yam to Tigheti , Barrick North Mara imekuwa mstari wa mbele kutekeleza sera ya kulinda mazingira kwa kuhakikisha inatumia uzalishaji kwa kutumia mifumo isiyoharibu mazingira sambamba na kushiriki kutoa elimu ya kulinda mazingira na vyanzo vya maji.

Vilevile wafanyakazi wake wamekuwa mstari wa mbele kushiriki katika miradi mbalimbali ya utunzaji wa mazingira.


Share:

UCHAGUZI VIONGOZI WAPYA BURUNGE WMA WAANZA

Mkuu wa idara Ulinzi na mahusiano Chem chem Charles Sylivester akimkabidhi kadi ya gari Mkurugenzi wa halmshauri ya Babati vijijini ,Anna Mbogo kwa ajili ya kazi za uhifadhi Burunge WMA
Mkurugenzi halmashauri Babati vijijini Anna Mbogo



Mwandishi wetu, Babati

Halmashauri ya Babati vijijini, imetangaza kuanza  kwa uchaguzi wa viongozi wapya katika eneo la Hifadhi ya  Jamii ya  Wanyamapori ya Burunge,baada ya kukamilika maboresho ya Katiba ili kuifanya hifadhi hiyo kuwa bora barani Afrika.

Burunge WMA ipo kati kati ya hifadhi ya Taifa ya Tarangire na Hifadhi ya Taifa ya Manyara , mkoa wa Manyara  chini ya usimamizi wa halmashauri ya Babati na Mamlaka ya usimamizi wanyamapori ( TAWA).          

Uchaguzi huo unafanyika baada ya kusimamishwa viongozi waliokuwepo madarakani kwa tuhuma kadhaa na baadae kumaliza muda wao.

Akizungumza na waandishi wa habari za Utalii na Uhifadhi wilayani Babati, Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Babati vijijini,Anna Mbogo  jana amesema, chaguzi  maboresho hayo yanafanyika pia kuendana na dhamira ya Rais, Dkt.Samia Suluhu Hassan, kuongeza mapato ya Taifa kupitia Utalii.

Mbogo anasema tayari  maboresho ya Katiba na mfumo wa uendeshaji Burunge WMA umekamilika na sasa chaguzi  za viongozi wa jumuiya hiyo, zimeanza katika vijiji 10 vinavyounda jumuiya hiyo.

Anasema vijiji hivyo ni, Mwada.Sangaiwe,Vilima Vitatu,Ngoley,Kakoi,Olasiti ,Manyara,Magara,Maweni
na Minjingu.

"Chaguzi zimeanza tunatarajia zikikamilika tutapa viongozi bora ambao wataweza kuja kusimama Uhifadhi, Utalii na kubwa kuongeza mapato ya Utalii kwa manufaa ya vijiji na serikali kwa ujumla",anasema.

Anasema Rais wa Jamuhuri ya Muungano, Dkt Samia Suluhu Hassan, tayari ilikamilisha kazi ya kuitangaza Tanzania kupitia filamu ya Royal Tour hivyo, sasa kazi iliyopo ni kuweka mazingira mazuri ya kuvutia watalii katika maene yote yaliyohifadhiwa.

Mkurugenzi huyo anasema, katika eneo la Burunge WMA tayari matunda ya uhifadhi yameanza kuonekana baada ya hivi karibuni, hoteli ya Chem chem iliyopo  ndani ya hifadhi hiyo, kushinda tuzo ya Safari Luxury lodge Afrika na Tanzania tuzo zilizotolewa na shirika la Utalii duniani la WTA.

"Tuzo hii inaendelea kuitangaza Burunge WMA vizuri na itavutia watalii zaidi na tunaomba na wawekezaji wengine katika eneo hili kuboresha huduma zao ili kuendelea kuvutia watalii",anasema.       

Mbogo amewataka wananchi wenye sifa na nia ya dhati kuendeleza uhifadhi na Utalii katika vijiji hivyo kujitokeza kugombea nafasi mbali mbali.

Kwa upande wake, Meneja Mkuu wa Chem chem, Clever Zulu anasema, lengo lao ni kuifanya WMA ya burunge kuwa bora barani  Afrika, kwa kuwa na vivutio vingi vya utalii, huduma bora ya malazi na kubwa kuhifadhiwa vizuri.

"Hili ndio lengo kubwa la wakurugenzi wa chem chem Nicolaus Negri na Fabia Bausch kuifanya Burunge WMA kuwa bora na ushindi wa tuzo ni sehemu ya mikakati lakini pia sasa tumeanza kupokea maafisa wa uhifadhi maeneo kadhaa Afrika kuja kujifunza hapa",anasema.

Anasema hifadhi hiyo, kwa sasa wanyama wameongezeka, ujangili umedhibitiwa na wananchi wananufaika sana na uhifadhi kupitia fedha zinazokusanywa.

Spika wa Burunge WMA, Erick Lilayoni ambaye anamaliza muda wake, anasema mapato ya Burunge WMA yamekuwa yakiongezeka hadi kufikia takriban billion 4 kwa mwaka na vijiji vimekuwa vikipata mgao zaidi ya millioni 200 kwa mwaka.

"Binafsi sitarajii kugombea tena uongozi lakini naamini eneo hili tukilitunza vizuri, manufaa makubwa yataendelea kupatikana kwa wananchi wa vijiji 10 na serikali kwa ujumla",anasema.

Share:

Saturday, 12 September 2026

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA ATEMBELEA KIWANJA CHA UJENZI WA VIWANGO HOUSE ARUSHA


Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Denis Londo (Mb), ametembelea kiwanja kinachotarajiwa kujengwa Viwango House eneo la Mateves, Mkoani Arusha.
Ziara hiyo imelenga kujionea eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa ofisi hizo, pamoja na kufahamu hatua zinazofikiwa katika maandalizi ya utekelezaji wa mradi huo.

Ujenzi wa Ofisi za TBS Mateves unatarajiwa kuimarisha upatikanaji wa huduma za viwango na uhakiki wa ubora kwa wananchi, wafanyabiashara na wazalishaji wa bidhaa katika Mkoa wa Arusha na maeneo jirani.

Aidha, uwepo wa ofisi katika eneo hilo utasaidia kusogeza huduma za TBS karibu zaidi na wadau, kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma na kuimarisha utekelezaji wa majukumu ya Shirika katika kuhakikisha bidhaa na huduma zinazotumika nchini zinakidhi matakwa ya viwango.
Share:

WIZARA , TAASISI ZATAKIWA KUCHUKUA HATUA KUKABILIANA NA MVUA ZA EL NIÑO


OWM –TAMISEMI, Dar es Salaam  

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Deogratius Ndejembi leo Septemba 11, 2026 amezitaka Wizara, Mamlaka na Taasisi zinazohusika na majanga kuchukua hatua za haraka kujiandaa ili kuzuia na kupunguza athari zinazoweza kusababishwa na mvua za El Niño zinazotarajiwa kuanza mwezi Oktoba hadi Desemba 2026. 
 
Makamu wa Rais ametoa maagizo hayo kwa taasisi hizo katika kikao kilichofanyika Ofisi ya Makamu wa Rais Jijini Dar es Salaam, ambapo kwa upande wa Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI yamepokelewa na Waziri Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, mara baada ya ofisi yake na taasisi zinazohusika kuchukua hatua za haraka, kuwasilisha taarifa ya utayari na maandalizi ya Serikali katika kukabiliana na madhara ya mvua hizo, kufuatia tahadhari iliyotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania.

Katika kikao kazi hicho, Makamu wa Rais, Mhe. Ndejembi ameagiza wataalamu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Wizara ya Ujenzi pamoja na Taasisi zilizo chini ya Wizara hizo kuhakikisha zinafanya kampeni maalum ya usafi katika miundombinu ya barabara na mifereji ya maji.

“Ifanyike kampeni ya haraka, mikondo na mifereji ya maji izibuliwe, na barabara ziandaliwe,” amesisitiza Makamu wa Rais.
 
Aidha, Makamu wa Rais Mhe.  Ndejembi, ameelekeza taka, tope na udongo unaotolewa baada ya kuzibua mitaro na mifereji katika maeneo mbalimbali kuondolewa mara moja na kutupwa katika maeneo yaliyotengwa, badala ya kuachwa kandokando ya barabara ambako taka, tope na udongo huo zinaweza kurejea kwenye mifereji wakati mvua zinapoanza.
 
Makamu wa Rais pia amezitaka Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Wizara ya Ujenzi pamoja na Taasisi zilizo chini ya Wizara hizo, kufanya kazi kwa pamoja ya kujiandaa ili kuzuia na kupunguza athari zinazoweza kusababishwa na mvua za El Niño.


Akipokea maagizo hayo kwa ajili ya utekelezaji, Waziri wa Nchi, OWM – TAMISEMI Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amemueleza Mhe. Makamu wa Rais kuwa ofisi yake imeshaanza kutekeleza maelekezo ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuboresha usafi wa mazingira katika majiji aliyoyatoa Septemba 02, 2026 wakati akiwaapishwa Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala aliowateua Agosti 27, 2026.

Prof. Shemdoe amemtaarifu Makamu wa Rais Mhe. Ndejembi kuwa, Septemba 07, 2026 alifanya kikao kazi na Wakuu wa Mikoa yenye majiji, viongozi wa majiji na manispaa za Mkoa wa Dar es Salaam na kuwataka kuhakikisha  wanatekeleza  kampeni maalum ya wiki mbili ya usafi wa mazingira  katika majiji ikiwa ni utekelezaji wa maelekezo ya Mheshimiwa Rais.

Akianisha namna ofisi yake itakavyotekeleza maelekezo ya Makamu wa Rais ya kujiandaa na kukabiliana na athari za mvua za El Niño, Prof. Shemdoe amewasilisha kwa Makamu wa Rais Mhe.  Ndejembi, mkakati wa ofisi yake kupitia TARURA ulioandaliwa kwa ajili ya kujiaanda, kuzuia na kupambana na madhara ya uharibifu wa miundombinu ya barabara unaoweza kutokana na mvua za El Niño, ambao umeanisha namna utakavyotekelezwa.









Share:

Friday, 11 September 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI SEPTEMBA 12, 2026

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger