Tuesday, 11 August 2026

UCSAF YABORESHA MINARA 431 ILI KUCHOCHEA MAENDELEO


Meneja wa kanda ya Ziwa wa Mfuko wa Mawasiliano kwa wote(UCSAF) Fredy Kandonga, akizungumza kwenye semina hiyo.
Meneja wa kanda ya Ziwa wa Mfuko wa Mawasiliano kwa wote(UCSAF) Fredy Kandonga, akizungumza kwenye semina hiyo.
Meneja wa kanda ya Ziwa wa Mfuko wa Mawasiliano kwa wote(UCSAF) Fredy Kandonga, akizungumza kwenye semina hiyo.
Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari mkoa wa Mwanza(MPC) Edwin Soko akizungumza kwenye semina hiyo.
Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari mkoa wa Mwanza(MPC) Edwin Soko akizungumza kwenye semina hiyo.
Ofisa Mawasiliano Mwandamizi wa UCSAF Celina Mwakabwale, akizungumza kwenye semina hiyo
Baadhi ya Wahariri wa vyombo vya habari vya kanda ya Ziwa wakifuatilia mada mbalimbali katika semina hiyo.
Baadhi ya Wahariri wa vyombo vya habari vya kanda ya Ziwa wakifuatilia mada mbalimbali katika semina hiyo.
Baadhi ya Wahariri wa vyombo vya habari vya kanda ya Ziwa wakifuatilia mada mbalimbali katika semina hiyo.
Baadhi ya Wahariri wa vyombo vya habari vya kanda ya Ziwa wakifuatilia mada mbalimbali katika semina hiyo.
Baadhi ya Wahariri wa vyombo vya habari vya kanda ya Ziwa wakifuatilia mada mbalimbali katika semina hiyo.


Na Mwandishi wetu

Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) umeongeza kasi ya huduma ya intaneti Kanda ya Ziwa baada ya kubadilisha minara 431 kutoka teknolojia ya 2G kwenda 3G/4G, hatua inayolenga kuwawezesha wananchi kupata huduma za intaneti zenye ubora zaidi na kuwaletea maendeleo.
Share:

TUME YABAINISHA MATAMANIO YA SERIKALI KULINDA AFYA NA USALAMA WA WATUMISHI WA UMMA

Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Nolasco Kipanda, akifungua mafunzo ya usalama na afya mahali pa kazi kwa wakaguzi wa Tume hiyo yaliyoandaliwa na Wakala wa Usalama naAfya Mahali pa Kazi (OSHA) kwa lengo la kuwajengea uelewa wakaguzi hao wenye jukumu la kukagua uzingatiaji wa sheria na miongozo mbalimbali katika sekta ya umma.

******************

Na Mwandishi Wetu

Tume ya Utumishi wa Umma imesema serikali ina nia ya dhati ya kuhakikisha watumishi wa umma wanakuwa salama na wenye afya njema na hivyo kutekeleza wajibu wao wa kuwahudumia wananchi ipasavyo.

Kauli hiyo imeelezwa na Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Nolasco Kipanda, alipofungua mafunzo ya usalama na afya mahali pa kazi kwa wakaguzi wa Tume hiyo yaliyoandaliwa na Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) kwa lengo la kuwajengea uelewa wakaguzi hao wenye jukumu la kukagua uzingatiaji wa sheria na miongozo mbalimbali katika sekta ya umma.

Amesema serikali inatamani kuona kila mtumishi wa umma anakuwa salama dhidi ya ajali na magonjwa yatokanayo na kazi ili aweze kutoa mchango wake kikamilifu katika kutekeleza majukumu ya serikali.

“Sote tunafahamu kwamba kinga ni bora kuliko tiba, Sheria ya Afya na Usalama Mahali pa Kazi inaelekeza maeneo yote ya kazi kuwa na mifumo madhubuti ya kuwalinda wafanyakazi dhidi ajali na magonjwa yatokanayo na kazi. Serikali inaamini kwamba watumishi wakiwa na afya njema, utendaji wao utaimarika na tayari ina chombo chake mahsusi cha kusimamia hilo ambacho ni Taasisi ya OSHA,” ameeleza Katibu wa Tume.

Amebainisha kwamba si wajibu wa Tume kusimamia utekelezaji wa Sheria bali Tume hiyo ina jukumu la kuhakikisha waajiri wanatekeleza sheria hiyo pamoja na miongozo mingine inayotolewa na OSHA ili kulinda afya na usalama wa watumishi wa serikali.

“Kutokana na umuhimu wa rasilimali watu, Serikali kupitia Ofisi ya Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ilisisitiza Tume kufanya ukaguzi wa uzingatiaji wa sheria ya usalama na afya mahali pa kazi ili kuhakikisha watumishi wa umma wanafanya kazi katika mazingira bora na hivyo kuwa na ufanisi,” amesisitiza Katibu Kipanda.

Aidha, amewataka wakaguzi wa Tume kuwa na uelewa wa kina kuhusu Sheria ya Usalama na Afya mahali pa kazi ili waweze kufanya tathmini sahihi ya utekelezaji wa sheria hiyo na kushauri maboresho stahiki.

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, ameipongeza serikali kwa kudhihirisha nia ya dhati ya kuwalinda watumishi dhidi ya ajali na magonjwa yatokanayo na kazi kupitia utekeleza wa sheria na miongozo ya usalama na afya mahali pa kazi.

“Napenda kutoa shukrani zangu kwa Rais, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuonesha nia ya dhati ya kuhakikisha kwamba nguvukazi ya nchi inalindwa katika sekta zote za umma na binafsi ambapo kupitia maelekezo yake masuala ya usalama na afya yamejumuishwa katika kanuni za kudumu za utumishi wa umma,” amesema Mwenda na kuongeza:

“Tunaishukuru Tume kwa kutushirikisha ambapo tumeweza kuandaa mafunzo ya kuwajengea uelewa wakaguzi wake ili wakienda kukagua wajue ni maeneo gani muhimu ya kuyafuatilia na wametuahidi baada ya ukaguzi tutakuwa na kikao cha pamoja kwa ajili ya kupata mrejesho.”

Baadhi ya Wakaguzi wa Tume wameyaelezea mafunzo hayo kama nyenzo muhimu katika utekelezaji wa majukumu yao.

“Mafunzo haya yametupa uelewa mpana sisi kama wakaguzi utakaotuwezesha kutekeleza majukumu yetu kwa ufanisi,” ameeleza Rose Silayo.

“Kipekee ninashukuru kwa mafunzo haya ambayo yatatuwezesha kukagua na kushauri ipasavyo uzingatiaji wa masuala ya usalama na afya ili kulinda afya za watumishi wa umma,” ameelezaDavid Shombe.

Mwaka 2022, Tume ilifanya maboresho ya mfumo wa ukaguzi wa masuala ya kiutumishi ili kuendana na sera, sheria na mazingira ya wakati husika ambapo maeneo sita ya kiutawala yaliongezwa katika maeneo saba yaliyokuwa yakikaguliwa awali. Eneo la usalama na afya kazini ni miongoni mwa maeneo yaliyoongezwa.


Mkurugenzi wa Mafunzo, Tafiti, Takwimu na Uhamasishaji wa OSHA, Bw. Joshua Matiko, akitoa ufafanuzi wa hoja mbalimbali zilizoibuliwa na washiriki katika mafunzo ya usalama na afya mahali pa kazi kwa Wakaguzi wa Tume ya Utumishi wa Umma yaliyoandaliwa na Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA).

Meneja Mafunzo wa OSHA, Mhandisi Shaban Mkindi, akiwasilisha mada katika mafunzo ya usalama na afya mahali pa kazi kwa Wakaguzi wa Tume ya Utumishi wa Umma yaliyoandaliwana Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA).

Mkaguzi wa Tume ya Utumishi wa Umma, akipitia Jarida la OSHA katika mafunzo ya usalama na afya mahali pa kazi kwa Wakaguzi wa Tume ya Utumishi wa Umma yaliyoandaliwa na Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA).

Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Nolasco Kipanda (Katikati) akiwa na viongozi wenzake katika meza kuu wakati wa mafunzo ya usalama na afya mahali pa kazi kwa wakaguziwa Tume hiyo.

Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Nolasco Kipanda (Katikati) akiwa na viongozi wenzake wakifuatilia mafunzo ya usalama na afya mahali pa kazi yaliyotolewa na OSHA kwa Wakaguzi wa Tume hiyo.

Afisa Mafunzo Mwandamizi wa OSHA, Bw. Simon Lwaho, akiwasilisha mada katika mafunzoya usalama na afya mahali pa kazi kwa Wakaguzi wa Tume ya Utumishi wa Umma yaliyoandaliwa na Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA).

Wakaguzi wa Tume ya Utumishi wa Umma wakifuatilia mada mbalimbali katika mafunzo yaliyoandaliwa na Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) kwa lengo la kuwajengea uelewa juu ya masuala ya usalama na afya mahali pa kazi.



Share:

Monday, 10 August 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI AGOSTI 9,2026

Magazeti



Share:

WANAFUNZI 85 KWENDA INDIA KUSOMEA ELIMU YA JUU


Na Mwandishi Wetu

WANAFUNZI 85 wanatarajia kwenda masomoni kwenye vyuo vikuu mbalimbali nchini India kuanzia wiki ijayo kupitia Wakala wa Elimu Nje ya Nchi Global Education Link (GEL).

Wanafunzi hao na wazazi wao walihudhuria mkutano uliofanyika katika ofisi za GEL mwishoni mwa wiki kwaajili ya kupewa mafunzo ya namna ya kuishi nchini humo.

Pia walielezwa mambo wanayotakiwa kufanya na wasiyotakiwa kuyafanya wakiwa masomoni nchini humo ikiwemo suala la vibali, bima na makaazi ili waweze kuhitimu masomo yao.

Mbali na mafunzo hayo walipewa tiketi zao za ndege, visa na nyaraka mbalimbali zitakazowawezesha kupokelewa kwenye vyuo wanavyokwenda kusoma nchini India.

Wanafunzi hao wanatarajiwa kuanza kwenda nchini India kuanzia tarehe 21 na 23 mwezi huu.

Akizungumza kwenye mkutano huo wa wanafunzi na wazazi wao, Mkurugenzi Mkuu wa GEL, Abdulmalik Mollel aliwataka wanafunzi hao kusoma huku wakiangalia fursa mbalimbali ambazo zinaweza kuwasaidia wanapohitimu.

“Tunahitaji GPA nzuri lakini pia huko kuna fursa nyingi sana, mtasoma na watoto wa matajiri wenye viwanda tunataka muwe karibu na watu kama hao kutambua fursa ya wewe kupata kazi siyo unamaliza halafu unakuja kuhangaika kutafuta kazi wakati huko kulikuwa na fursa,” alisema

Aliwataka wanafunzi hao kutafuta marafiki ambao wataongeza thamani ya masomo yao badala ya kuwa na marafiki ambao wanapenda starehe na hawahudhuriii masomo madarasani.

“Katumieni muda wenu nje ya kile kilichowapeleka kwa maana ya kujiongeza, tatizo la ajira ni shida ya dunia nzima siyo Tanzania ni wewe tu unavyoona fursa unazoona hata kwa wanafunzi utakaosoma nao huko nje,” alisema

“Kule mtakutana na wanafunzi wa mataifa mbalimbali na hata wa nchi zilizoendelea ulizeni fursa zilizoko kule kwenye mataifa yao ili kama ukimaliza unaweza kwenda kufanya kazi siyo lazima uje kuhangaika baada ya kuhitimu,”

“Mfano mtasoma na watoto wa matajiri wana viwanda ulizeni fursa zilizoko kwa hao watoto kwasababu India watu kuwa viwanda vidogo vidogo nyumbani kwao ni maisha ya kawaida kabisa kuna mtu ana kiwanda chumbani kwake thamani ya mtaji ukiuliza ni Dola 8,000,” alisema

Alisema India kuna viwanda vidogo vidogo ambavyo mtaji wake ni mdogo kiasi kwamba hata ndugu wanaweza kukupa na aliwataka kuondokana na dhana kwamba kuanzisha biashara kunahitaji mabilioni ya fedha.

“India wameendelea sana kwa viwanda tumieni fursa hiyo ila isikutoe kwenye reli ya nasomo yako. Jiulize unasoma kwaajili ya GPA nzuri tu au unakwenda kuhamisha maarifa ya kuchukua telnolojia na fursa za viwanda zinazopatikana kule kuleta hapa Tznania,” alisema Mollel

Alisema kila mwaka wanafunzi zaidi ya 800 wanapitia Global Education Link kwenda kusoma nje ya nchi hivyo kila mmoja akiwa mbunifu na kubaini fursa zilizoko nje ya nchi watapunguza tatizo la ajira wanapohitimu.

Alisema kuanzia mwakani Global Education Link itafungua fursa za ajira kwasababu kuna kampuni kubwa nchini ambazo zimekuwa iwape wataalamu wa aina mbalimbali inaowafahamu.

Alisema India inaongoza kwa kupeleka vijana wao kwenda kufanya kazi nje na si kwa bahati mbaya bali ni kutokana na kuwa na mtandao wa kubaini fursa mbalimbali kwenye mataifa.

“Kule India hawasomi ili wapate GPA wanasoma ili watengeneze fursa wewe unasoma ukimaliza unaanza kulalamika hakuna ajira, hatutaki hilo.Tunatamani mpate zaidi ya GPA mrudi na fursa zinazopatikana huko,” alisema Mollel

“ Ulaya kuna shida kubwa ya rasilimali watu kutokana na wengi kustaafu kwa umri sasa wewe ukisoma uhandisi jiongeze soma na kijerumani au Kifaransa angalia lugha ambayo inaweza kukusaidia kupata ajira,” alisema

Alsiema kwenye mataifa ya Ulaya fursa za kazi zipo ila wanataka mtu anayejua lugha yao kwa hiyo aliwataka wanafunzi hao kuhakikisha wanapata fursa zote wanazoona huko wasiishie kukariri GPA.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU AGOSTI 10, 2026



Magazetini Leo



Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger