Friday, 7 August 2026

TBS YAENDELEA KUTOA ELIMU YA UBORA WA BIDHAA KATIKA MAONESHO YA NANENANE ARUSHA


SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limehimiza wajasiriamali kuchangamkia fursa ya kuthibitisha ubora wa bidhaa wanaozalisha bure kwa gharama za Serikali, hatua ambayo itawasaidia kuondokana na vikwazo vya kiabiashara.

Mbali na wito huo kwa wajasiriamali, shirika hilo limewataka wananchi kuhakikisha wananunua na kutumia bidhaa zilizothibishwa ubora na shirika hilo kwa kujenga utamaduni wa kusoma taarifa zilizopo kwenye vifungashio.

Wito huo umetolewa na Meneja wa TBS Kanda ya Kaskazini,, Yona Afrika,. wakati akizungumza kwenye Maonesho ya Nanenane yanayoendelea jijini Arusha.

Alisema Serikali inatambua mchango mkubwa wa wajasiriamali katika kukuza uchumi wa Taifa na wao binafsi, ndiyo maana imebeba dhamana ya kuthibitisha ubora wa bidhaa zao bure.

"Kwa hiyo tumeshiriki katika maonesho haya kwa sababu ni fursa ya kukutana na wadau mbalimbali na kuwaelezea shughuli zinazofanywa na TBS na fursa nyingine ambazo zinapatikana kama kuthibitisha bidhaa za wajasiriamali bure," alisema.

Alisema bidhaa zikishathibitishwa na TBS zinaingia masoko ya Nchi za Afrika Mashariki (EAC) na ya kikanda bila vikwanzo vya biashara.

Alisema nchi za EAC zimeingia makubaliano, ambapo bidhaa zikishathitishwa na shirika la viwango la nchi husika,hazitakiwi kupimwa tena zinapopelekwa kwenye soko la nchi nyingine.

"Kwa hiyo TBS tumeshiriki maonesho haya kusudi kukutana na wadau mbalimbali, ambao tunawafikia na kuwapa taratibu za kufuata kuthibitisha ubora.

"Kwa kweli tunaishukuru Serikali kwa kuendelea kuandaa Maonesho haya ya Nanenane, kwani fursa muhimu ya kukutana na kutoa elimu kwa wadau.

Mfano tunawaambia kuwa wakipata barua ya utambulisho kutoka SIDO wakija kwetu utaratibu wa kuthibitisha ubora wa bidhaa unaanza mara moja, kwa wajasiriamali" alisema Afrika.

Kwa upande wa wananchi waliotembelea banda la TBS, walitakiwa kuhakikisha wanatumia bidhaa zilizothibitishwa ubora ili kulinda afya zao na kuona thamani ya fedha zao.

Alisema ni muhimu kusoma taarifa zilizopo kwenye vigungashio ili kujua kama zina ubora uliothititishwa na shirika pamoja na muda wake wa mwisho wa matumizi.

Share:

Thursday, 6 August 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA AGOSTI 7, 2026

Share:

BALOZI MBAROUK ASEMA ITALIA INA NAFASI KUBWA YA KULETA WATALII NCHINI


📌Aipongeza Wizara Ya Maliasili na Utalii kutangaza fursa za utalii nje ya nchi

📌Jaji Mruma naye atembelea Banda la Maliasili kujionea wanyamapori hai Nane Nane

Na Neema Chalila Mbuja, Dodoma

BALOZI wa Tanzania nchini Italia na Mwakilishi Mkazi  wa Shirika la Chakula na Kilimo la  Umoja wa Mataifa (FAO), Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) na Shirika la Chakula la Umoja wa Mataifa (WFP),  Mhe. Mbarouk  Nassoro Mbarouk leo Agosti 04, 2026,  ametembelea Banda la Wizara ya Maliasili na Utalii  na kusema kuwa nchi ya Italia ina nafasi kubwa ya kuleta watalii wengi nchini.

Mhe. Balozi Mbarouk amesema Tanzania inafanya vizuri kwenye kutangaza utalii na vivutio vyake  na kuipongeza Wizara kwa kazi nzuri inayoifanya.

Katika hatua nyingine Wizara ya Maliasili na Utalii  imepokea ugeni wa Jaji wa Mahakama ya Rufaa Mhe. Rajab Mruma ambaye ameitaka Wizara ya Maliasili na Utalii kubuni mbinu za kutafuta utatuzi wa  changamoto za wanyamapori hai kuingia kwenye makazi ya wananchi kwa kujenga  uzio ili kuzuia uharibifu unaoweza kutokea.

Aidha, Mhe Jaji Mruma ametembelea bustani ya wanyamapori  hai iliyoko kwenye Maonesho ya Nane  Nane yanayoendelea Jijini Dodoma ikiwa ni sehemu ya kutangaza utalii wa ndani kwa wananchi.

Share:

SIMBA TANZANIA YAWAKARIBISHA WANANCHI KUNUFAIKA NA FURSA ZA UFUGAJI KUKU




Na Sheila Ahmadi, Dodoma

Kampuni ya Simba Tanzania Limited imewahimiza wananchi kutumia fursa zilizopo katika sekta ya ufugaji wa kuku kwa kuanzisha na kuendeleza miradi ya ufugaji yenye tija, huku ikitoa elimu kuhusu upatikanaji wa vifaranga na chakula cha kuku.

Akizungumza katika Maonesho ya Nanenane yanayofanyika Dodoma, Meneja Mauzo kutoka kanda ya kati Ditirick Mdemu amesema kampuni ya Silverlands inajihusisha na uzalishaji wa vifaranga pamoja na chakula cha kuku huku ikilenga kuwawezesha wafugaji kupata mahitaji muhimu kwa ajili ya uzalishaji.

Sanjari na hayo kampuni hiyo inatoa aina mbalimbali za vifaranga, ikiwemo vifaranga vya kuku wa nyama, kuku wa mayai pamoja na aina nyingine zinazofaa kwa wafugaji wenye mahitaji tofauti.

kwa sasa wananchi wengi wameanza kuangalia ufugaji wa kuku kama fursa ya biashara, hali inayoongeza uhitaji wa taarifa sahihi kuhusu ufugaji, lishe, magonjwa na namna bora ya kuendesha miradi hiyo.

“Watu sasa hivi wanataka biashara. Wafugaji wanauliza maswali mengi kuhusu chakula, magonjwa na namna ya kuendesha mradi wa ufugaji,” amesema Mdemu".

hali hiyo inaonesha kuongezeka kwa mwamko wa wananchi katika kuwekeza kwenye ufugaji wa kuku, hivyo kampuni inaendelea kutoa elimu na ushauri kwa wafugaji ili waweze kufanya shughuli hiyo kwa ufanisi.

Aidha, niwakaribishe wananchi wanaotembelea Maonesho ya Nanenane kufika katika banda la kampuni hiyo kwa ajili ya kupata elimu zaidi kuhusu vifaranga, chakula cha kuku na masuala mbalimbali yanayohusu ufugaji.

Vilevile wananchi wanaweza kupata taarifa zaidi kuhusu huduma na bidhaa za kampuni hiyo kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii.
Share:

Wednesday, 5 August 2026

SERIKALI KUSHIRIKIANA NA SEKTA BINAFSI KUDHIBITI TAKA ZA PLASTIKI.


Serikali itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha kunakuwa na uwiano kati ya udhibiti wa taka za plastiki, ulinzi wa mazingira na ukuaji wa sekta ya viwanda ili uchumi wa nchi uendelee kuimarika.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Viwanda Biashara, Mhe. Judith Kapinga (Mb) wakati wa mkutano wa wadau wa udhibiti wa taka za plastiki Agosti 04, 2026 jijini Dar es Salaam .

Kapinga amesema suala la taka za plastiki lina pande mbili muhimu kwani kwa upande mmoja linahusu uhifadhi wa mazingira na kwa upande mwingine linagusa shughuli za uzalishaji wa viwanda vinavyochangia ajira, mapato ya Serikali na maendeleo ya uchumi.

Aidha, kuna wazalishaji wa plastiki zinazotumika kama vibebeo na vifungashio vya matumizi ya kila siku pamoja na viwanda vikubwa vinavyotumia vifungashio vya plastiki katika bidhaa zao, hivyo ni muhimu kujenga mazingira yatakayowezesha sekta hizo kuendelea kufanya biashara huku zikizingatia sheria na kulinda mazingira.

Kapinga ameongeza kuwa Serikali inalenga kujenga mazingira yanayowiana kwa pande zote, ambapo wawekezaji watimize wajibu wao wa kulinda mazingira na mamlaka za udhibiti zitekeleze wajibu wake kwa njia wezeshi ili wadau wote waweze kufanya kazi kwa ushirikiano.

Hata hivyo Kapinga amevipongeza viwanda vinavyozingatia Sheria na taratibu za mazingira, akisema hatua hiyo imeviwezesha kudumu kwenye biashara kwa muda mrefu, amesema Serikali itaendelea kuviunga mkono na kuvipatia mazingira bora yatakayovichochea kukua zaidi na kuongeza mchango wake katika Uchumi wa Taifa.

Vilevile amesema Viwanda vinavyokiuka Sheria vinapaswa kutumia vikao vya wadau kama fursa ya kujikumbusha misingi ya sheria na kuelekezwa namna ya kutumia teknolojia rafiki kwa mazingira ili viendelee kufanya biashara kwa ufanisi na kuongeza tija.

Sambamba na hayo, Serikali kwa sasa inatekeleza udhibiti wezeshi unaolenga kunufaisha wadau na Serikali kwa wakati mmoja, huku akimshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya sekta ya umma na sekta binafsi.

Kapinga amesema mkutano huo umeandaliwa kwa ushirikiano kati ya Wizara ya Viwanda na Biashara na Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), akibainisha kuwa sekta hizo zinategemeana katika kuhakikisha uwekezaji na maendeleo ya viwanda vinaenda sambamba na uhifadhi wa mazingira. Ameongeza kuwa Wizara ya Viwanda na Biashara ina taasisi 13 za udhibiti zinazoshirikiana katika kusimamia shughuli hizo.

Naye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mhe. Hamad Masauni (Mb), amesema mkutano huo umefanyika kwa mujibu wa maelekezo na maono ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuimarisha ushirikiano kati ya serikali na sekta binafsi.

Amesema hatua hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, ambapo takribani asilimia 70 ya utekelezaji wa dira hiyo unatarajiwa kuchangiwa na sekta binafsi, hivyo ushiriki wa wadau katika masuala ya mazingira na uwekezaji ni muhimu kwa maendeleo endelevu ya nchi.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger