Sunday, 26 July 2026

RC MBONI MHITA AWASILISHA TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM, 'RAIS SAMIA AMETOA TRILIONI 1.9 SHINYANGA'



Na Marco Maduhu, SHINYANGA

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mboni Mhita, amewasilisha taarifa ya utekelezaji wa ilani ya Chama cha Mapinduzi CCM kwa kipindi cha kuanzia Novemba, 2025 hadi Juni 2026.

TAZAMA VIDEO👇👇

Amewasilisha taarifa hiyo leo kwa Kamati ya siasa ya Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Shinyanga ikiongozwa na Mwenyekiti wa CCM wa mkoa huo Mabala Mlolwa.

Mhita akisoma taarifa hiyo, amesema kwa kipindi cha uongozi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan wamepokea kiasi cha fedha sh. Trilioni 1.9 kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali za maendeleo.
Amesema, katika mapokezi ya fedha hizo wananchi wa Mkoa huo, wameshuhudia maendeleo ya haraka katika Nyanja za uzalishaji katika sekta ya kilimo, mifugo, madini, viwanda , biashara, pamoja na huduma za jamii, Afya, Elimu, Nishati na Maji.

UTEUZI WA VIONGOZI

Amemshukuru Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kumteuwa Mheshimiwa Patrobas Katambi kuwa Waziri wa Mambo ya ndani na Mheshimiwa Salome Makamba kuwa Naibu Waziri wa Nishati.


WASIFU WA MKOA

Amesema mkoa huo wa Shinyanga una ukubwa wa kilomita za mraba elfu 18,557 na unajumla ya watu milioni 2,2 wanaume wakiwa milioni 1.102 na wanawake milioni 1.13 kwa mujibu wa sense ya watu na makazi ya mwaka 2022.
HALI YA UCHUMI YA MKOA

Amesema, mkoa huo umeendelee kuimarika ambapo pato halisi limeongezeka kutoka sh. bilioni 7.5 mwaka 2021 hadi sh.bilioni 9.2 mwaka 2026 sawa na ukuaji wa asilimia 22.

PATO LA MTU MMOJA

Amesema, pato la mtu mmoja mmoja limeongezeka kutoka sh. Milioni 1.8 mwaka 2021 hadi Sh.milioni 1.9 mwaka 2026 sawa na ongezeko la asilimia 7.

SEKTA YA AFYA

Amesema katika kuendelea kuimarisha sekta ya afya mkoa huo umepokea kiasi cha fedha sh. bilioni 99.0 kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya vituo vya kutolea huduma za afya.

Kukamilisha hospitali ya Rufaa ya Mkoa huo iliyopo Mwawaza, kwa kujenga majengo ya EMD, OPD, Jengo la utawala, Jengo la Uraibu wa Madawa ya kulevya na kituo cha tiba jumuishi, kununua vifaa tiba, ujenzi wa nyumba za watumishi pamoja na kuongezeka kwa madawa na vitendanishi.

ELIMU

Amesema, katika kuinua ubora wa elimu katika ngazi zote Mkoa huo umepokea sh. bilioni 205.2 kwa ajili ya kujenga na kukarabati miundombinu ya elimu na kuongeza idadi ya walimu.

MAJI

Katika kuimarisha upatikanaji wa maji kwa wananchi wote kwamba mkoa huo umepokea sh. bilioni 163.3 ili kuhakikisha kaya nyingi zinaunganishwa na huduma ya maji, na kwamba upatikanaji wa maji kwa wananchi kwa sasa ni asilimia 79 kutoka 63 kwa maeneo ya mijini na vijijini asilimia 68 kutoka 51.

KILIMO

Kwamba wameendelea na ujenzi wa Skimu za bwawa la Nyida na Melenge, kuimarisha huduma za ugani kwa kununua vitendea kazi ikiwamo Pikipiki, vipima udongo na vishikwambi.

MIFUGO

Wameongeza usambazaji wa dawa za ruzuku za kuogeshea mifugo, kuimarisha huduma ugani kwa kugawa pikipiki 534 kwa ajili ya maafisa mifugo, pamoja na kuongeza minada ya mifugo kutoka 25 hadi 30.

MADINI

Kuongezeka kwa utoaji wa lessen kwa wachimbaji wadogo kutoka lesseni 332 hadi 1,766.

MIUNDOMBINU

Kuongezeka kwa mtandao wa barabara za lami kwa kilomita 57 ,barabara za changarawe kilomita 454, na kukamilika kwa ujenzi wa madaraja 18 ,makaravati 2,113, na pamoja na kuendelea kwa ujenzi wa barabara ya lami kutoka Kahama- Bulyanhulu kilomita 73 kwa gharama ya sh.bilioni 100.6 na ujenzi umefikia asilimia 78.21.

NISHATI

Amesema Rais Dk Samia ametoa bilioni 426 kwa ajili ya kusambaza umeme vijijini, pamoja kuendelea kwa ujenzi wa mradi mkubwa wa umeme jua katika kijiji cha Ngunga wilayani Kishapu kwa kuzalisha Megawati 100 kwa awamu ya pili.

UWEZESHAJI WANANCHI KIUCHUMI

Kuongezeka kwa utoaji wa mikopo ya asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri ambapo kiasi cha sh. bilioni 11.3 zimetolewa kwa vikundi 941 vya wanawake, Vijana 599 na watu wenye ulemavu vikundi 110.

TASAF

Zimetolewa fedha sh. bilioni 59.5 kwa walengwa elfu 35,055 kutekeleza miradi 77 ya miundombinu ya elimu, afya, barabara, pamoja na kuwezesha walengwa elfu 15,103 kujiongezea kipato kupitia ufugaji na kilimo.

UTAWALA BORA

Mkoa umepokea bilioni 22,2 kwa ajili ya ujenzi wa majengo ya utawala na nyumba za watumishi, katika Hamashauri ya Manispaa ya Shinyanga, Shinyanga DC, Ushetu na ujenzi wa Jengo la Ofisi ya mwendesha Mashtaka.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Shinyanga Mabala Mlolwa, amesema wamempongeza Mkuu huyo wa mkoa kwa usimamizi mzuri wa fedha za serikali na kuitendelea haki ilani ya uchaguzi ya Chama hicho.

TAZAMA PICHA👇👇
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mboni Mhita akisoma taarifa ya utekelezaji wa ilani ya CCM kwa kipindi cha kuanzia Novemba 2025 hadi Juni 2026.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mboni Mhita akisoma taarifa ya utekelezaji wa ilani ya CCM kwa kipindi cha kuanzia Novemba 2025 hadi Juni 2026.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mboni Mhita akisoma taarifa ya utekelezaji wa ilani ya CCM kwa kipindi cha kuanzia Novemba 2025 hadi Juni 2026.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mboni Mhita akisoma taarifa ya utekelezaji wa ilani ya CCM kwa kipindi cha kuanzia Novemba 2025 hadi Juni 2026.
Katibu wa CCM Mkoa wa Shinyanga Odilia Batimayo akizungumza.
Katibu wa CCM Mkoa wa Shinyanga Odilia Batimayo akizungumza.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga Mabala Mlolwa akizungumza,

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JULAI 26,2026


Magazeti

Share:

Saturday, 25 July 2026

MARIDHIANO NI MSINGI WA KUPONYA TAIFA NA KUREJESHA UMOJA



Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Karagwe, Dk Benson Bagonza, amesema kuwa maridhiano ni msingi mkuu wa kuponya taifa, kurejesha umoja wa wananchi na kujenga uongozi wenye mamlaka ya kimaadili.

Akitoa mtazamo wake kupitia mitandao ya kijamii, alieleza kuwa uzoefu wake katika kufundisha somo la Falsafa ya Siasa chuoni, pamoja na uchambuzi wa nyaraka za maridhiano kutoka nchi mbalimbali duniani kama vile Afrika Kusini, Rwanda, Kenya, Sierra Leone, Gambia na Cyprus, unathibitisha kuwa maridhiano hayawezi kuepukika pale ambapo taifa linapokuwa limegawanyika kutokana na matukio ya kihalifu au migogoro mikubwa.

Alifafanua kuwa maridhiano ya dhati hutoa fursa muhimu ya kukiri makosa na kuruhusu jamii kuanza upya, kujifunza kuwajibika kwa jamii hata kwa wale wanaoamini wameshinda, na kuzuia historia ya migogoro isije ikatumika baadaye kama silaha ya kisiasa.

Aidha, alisisitiza kuwa mchakato huo unarejesha mamlaka ya kimaadili kwa viongozi kupitia kujenga uongozi unaotokana na ushawishi badala ya kutumia nguvu, huku akionya kuwa hakuna kundi lenye ushawishi ambalo linapaswa kuachwa nje ya mchakato huo ili kuepusha hatari ya kuvuruga utekelezaji wa makubaliano.

Akizungumzia faida za mazungumzo ya wazi, Askofu Bagonza alisema kuwa mafanikio makubwa ya maridhiano ni kuondoa hisia za kisasi na kujenga upya imani iliyopotea kati ya wananchi na viongozi wao.

Alionya kuwa jamii inayokataa kuzungumza inaendelea kubeba majeraha ya ndani ambayo huhatarisha usalama na kujitokeza tena kila kunapotokea tofauti za kijamii au kisiasa, na ndio maana maridhiano hayo lazima yajengwe juu ya nguzo thabiti za ukweli, uwajibikaji na msamaha ili yawe na tija ya kudumu.

Askofu Bagonza alisisitiza kuwa pale wananchi wanaporejesha imani yao kwa viongozi na taasisi za nchi, taifa hufurahia utulivu, mshikamano mkubwa na kupata mazingira mazuri ya kuleta maendeleo endelevu.

Alieleza kuwa hatua hiyo si tu suluhu ya sasa, bali ni uwekezaji wa kimkakati na wa maana sana kwa ajili ya usalama na ustawi wa vizazi vya sasa na vijavyo.
Share:

WAZIRI KAIRUKI AANIKA MATUNDA YA UWEKEZAJI WA RAIS SAMIA KONGWA



Na Dotto Kwilasa,Dodoma

Uwekezaji mkubwa unaofanywa na Serikali katika sekta za afya, elimu, maji, nishati na miundombinu umeendelea kubadili sura ya Wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma,huku Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki akisema hatua hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha maendeleo yanawafikia wananchi moja kwa moja.

Waziri Kairuki amesema Serikali imeendelea kupeleka fedha nyingi kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo, hivyo sasa ni wajibu wa watendaji kuhakikisha uwekezaji huo unazalisha matokeo yanayoonekana katika maisha ya wananchi.

Waziri ameeleza hayo leo Julai 24,2026 katika Kijiji cha Laikala, Kata ya Sagara, Wilaya ya Kongwa, wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa Kituo cha Afya Laikala, ikiwa ni ziara yake ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo mkoani Dodoma Kwa lengo la kujionea utekelezaji wa miradi, kubaini changamoto zilizopo na kuchochea kasi ya maendeleo.

"Serikali imepeleka fedha nyingi kwenye miradi ya maendeleo,tunajivunia vituo vya afya, shule, miradi ya maji na miundombinu mingine sasa tunataka kuona fedha hizo zinabadilisha maisha ya wananchi kupitia huduma bora na miradi yenye tija," amesema Kairuki.

Amebainisha kuwa katika mwaka wa fedha uliopita, Wilaya ya Kongwa ilipokea zaidi ya Sh bilioni 8.6 kwa ajili ya kutekeleza miradi katika sekta za afya, elimu, maji, kilimo, umwagiliaji na mifugo.

Amesema maendeleo ya Kongwa hayawezi kujengwa na Serikali pekee, bali yanahitaji ushiriki wa wananchi kwa kutumia ipasavyo fursa zilizopo katika kilimo, mifugo na sekta nyingine za uzalishaji.

"Kongwa itajengwa na wana Kongwa wenyewe,kila mmoja atimize wajibu wake,fedha mnazochangia kupitia kodi na ushuru lazima muone matokeo yake kupitia huduma bora na miradi yenye ufanisi," amesema.

Kwa upande wa sekta ya afya, Kairuki amemuelekeza Mganga Mkuu wa Kituo cha Afya Laikala kuhakikisha anafuatilia kwa karibu utoaji wa huduma ili wananchi wanufaike na uwekezaji unaofanywa na Serikali.

Aidha, amewataka watumishi wa afya nchini kuzingatia viapo vyao vya kazi kwa kutoa huduma kwa kufuata maadili ya taaluma, utu na heshima kwa wananchi.

Amesema Serikali imeendelea kuboresha huduma za afya Kongwa ambapo wilaya hiyo sasa ina vituo vya afya 11, magari saba ya wagonjwa pamoja na nyumba za watumishi.

Pia amewahimiza wananchi kujiunga na Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote ili kuwawezesha kupata matibabu kwa urahisi wanapokumbwa na changamoto za kiafya.

Akizungumzia elimu, Kairuki amesema Serikali itaendelea kuhakikisha kila mtoto mwenye umri wa kwenda shule anapata elimu bila vikwazo.

Amesema katika Wilaya ya Kongwa, Serikali imeelekeza zaidi ya Sh bilioni 1.2 kwa elimu ya msingi na Sh bilioni 1.4 kwa elimu ya sekondari kupitia mpango wa elimu bila ada.

Ameongeza kuwa zaidi ya madarasa 670 yamejengwa, hatua iliyosaidia kupunguza umbali wa wanafunzi kufuata shule na kuongeza mazingira bora ya kujifunzia.

"Hakuna kisingizio tena kwa mtoto kushindwa kupata elimu Serikali itaendelea kujenga shule za kutosha kuhakikisha watoto wote wanapata haki hiyo," amesema.

Katika huduma ya maji, Kairuki amesema Serikali inatambua changamoto iliyopo katika baadhi ya maeneo ya Kongwa na imeanza hatua za kuchimba visima 19 ili kuongeza upatikanaji wa maji safi na salama.

Kwa upande wa kilimo na mifugo, amesema Serikali itaendelea kuwawezesha wananchi kupitia upatikanaji wa mbolea, pembejeo bora, dawa za mifugo, huduma za ugani pamoja na vitendea kazi kwa maafisa ugani na mifugo.

"Lengo ni kuongeza uzalishaji, kuinua kipato cha wakulima na wafugaji na kujenga uchumi wa wananchi,"amesisitiza

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Simon Mayeka, amesema wilaya hiyo imepiga hatua kubwa katika sekta za afya na elimu kutokana na uwekezaji unaofanywa na Serikali.

Amesema wakati Rais Samia Suluhu Hassan anaingia madarakani, Kongwa ilikuwa na vituo vinne vya afya lakini sasa imefikia 11 baada ya Serikali kujenga vituo saba vipya.

Amesema hatua hiyo imesaidia kupunguza vifo vya mama na mtoto kutokana na kuboreshwa kwa huduma za afya.

Amesema Kwa upande wa nishati kata zote 22 za Kongwa zimefikiwa na umeme na sasa wananchi wanapaswa kutumia fursa hiyo kuongeza shughuli za uzalishaji.












Share:

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JULAI 25, 2026

Magazetini Leo


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger