Thursday 25 April 2024

GHAZZA FC NA KISHAPU VETERAN WANAWAKE WASHINDI BONANZA LA MICHEZO KISHAPU KUENZI MUUNGANO..... DC ASEMA USALAMA KWENYE MKESHA UMEIMARISHWA


Na Sumai Salum - Kishapu

Bonanza la michezo ya mpira wa miguu,pete na kukumbiza  kuku limehitimishwa  April 24,2024 katika viwanja vya michezo shule ya msingi Buduhe Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga kuelekea maadhimisho ya miaka 60 ya Muungano wa Tanzania.

Kufuatia mashindano hayo yaliyofunguliwa jana na Kaimu Katibu Tawala Bw.Given Noah na kufungwa leo na Msimamizi mkuu wa sherehe za Muungano wilayani humo Mhe.Joseph Mkude Ghazza Fc imechuana na Kishapu Veteran  huku Ghazza ikiibuka kidedea kwa bao  1-0 katika kipindi cha pili na mpira wa pete,Kishapu  Veteran kujipatia ushindi kwa mbinde wa mabao 8-5 dhidi ya Isoso Sekondari.

Aidha kwa upande wa mashindano ya kukimbiza kuku kwa wazee, washindi ni Bi. Monica Charles na Bw.Patric Zengo na kisha wakatunukiwa kuondoka nazo.

Hata hivyo akizungumza wakati alipokuwa akimkaribisha Msimamizi wa sherehe za muungano Diwani wa Kata ya Kishapu Mhe. Joel Ndettoson amezipongeza timu zote zilizoshiriki mashindano ya mpira wa pete na miguu na ameendelea kutoa wito kwa wananchi wote kushiriki mkesha wa kilele cha maadhimisho ya miaka 60 ya Muungano kiwilaya yatakayofanyika katika viwanja vya Shirecu April 25,2024.
 
Kwa upande wake Msimamizi mkuu wa sherehe za Muungano na Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude amesema kuwa kamati ya ulinzi na usalama imejipanga kikamilifu kuimarisha ulinzi na usalama katika mkesha utakaonza saa 1jion hadi asubuhi huku wafanyabiashara na wajasiliamali wakikaribishwa na bidhaa zao kwa lengo la kufanya biashara.

"Hongereni kwa uzalendo wenu mkubwa mliouonesha na kuheshimu muungano wetu, kiukweli miaka 60 bado tumelelewa kwenye amani,utulivu na upendo hivyo tuendelee kutembea katika hayo kama ilivyo desturi yetu watanzania kesho tutakuwa sehemu moja tu Shirecu tutakabidhi zawadi kwa washindi na pia tutapata burudani mbalimbali usalama upo wa kutosha" ,ameongeza Mkude.
Msimamizi mkuu wa sherehe za muungano na Mkuu wa Wilaya ya  Kishapu Mkoani Shinyanga Mhe.Joseph Mkude akizungumza wakati akihitimisha  kilele cha  bonanza la michezo April 24,2024 katika viwanja vya shule ya msingi Buduhe wilayani humo kuelekea kilele cha maadhimisho ya miaka 60 ya muungano.

Katikati ni mwamuzi wa mchezo wa mpira wa miguu Bw.Masesa Kuzenza,kushoto Diwani wa Kata ya Kishapu Mhe.Joel Ndettoson na kulia ni Msimamizi wa sherehe za Muungano  na mkuu wa Wilaya ya Kishapu Aprili 24,2024 kwenye kilele cha bonanza la michezo kuelekea miaka 60 ya muungano
Katikati ni muamuzi wa mchezo wa mpira wa pete mwl. Baraka Mwakilili,kushoto Diwani wa Kata ya Kishapu Mhe.Joel Ndettoson na kulia ni Msimamizi wa sherehe za Muungano  na mkuu wa Wilaya ya Kishapu Joseph Mkude Aprili 24,2024 kwenye kilele cha bonanza la michezo kwelekea miaka 60 ya muungano

Diwani wa kata ya Kishapu Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga Mhe. Joel Ndettoson akizungumza kwenye kilele cha  bonanza la michezo April 24,2024 katika viwanja vya shule ya msingi Buduhe wilayani humo kuelekea kilele cha maadhimisho ya miaka 60 ya muungano.
Msimamizi mkuu wa sherehe za muungano Wilaya ya Kishapu kwenye kilele cha bonanza la michezo aliyoifunga Aprili 24,2024  Mhe. Joseph Mkude akipiga danadana kwenye viwanja vya michezo vya shule ya msingi Buduhe  wilayani humo mkoani Shinyanga.
Picha ya pamoja ya wachezaji wa Kishapu Veteran wanawake  na msimamizi mkuu wa sherehe za muungano Mhe. Joseph Mkude na Diwani ya kata ya Kishapu Mhe.Joel Ndettoson kabla ya mechi wakiwachapa bao 8-5 Isoso Sekondari kwenye kilele cha bonanza la  michezo lililohitimishwa April 24,2024 katika viwanja vya  shule ya msingi Buduhe wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga  kuelekea maadhimisho ya miaka 60 ya muungano
Picha ya pamoja ya wachezaji wa Isoso Sekondari na msimamizi mkuu wa sherehe za muungano Mhe.Joseph Mkude na Diwani ya kata ya Kishapu Mhe.Joel Ndettoson kabla ya mechi waliopigwa bao 8-5 dhidi ya Kishapu Veteran wanawakeApril 24,2024 kwenye kilele cha bonanza la kuelekea maadhimisho ya miaka 60 ya muungano
Picha ya pamoja ya wachezaji wa Kishapu veteran na msimamizi mkuu wa sherehe za muungano Mhe.Joseph Mkude na Diwani ya kata ya Kishapu Mhe.Joel Ndettoson kabla ya mechi waliochapwa  0-1 dhidi ya GhazzaApril 24,2024 kwenye kilele cha bonanza la kuelekea maadhimisho ya miaka 60 ya muungano

Mshindi aliyeshiriki mashindano ya kukimbiza kuku Bw.Patrick Zengo katika finali za bonanza april 24,2024 katika viwanja vya shule ya msingi Buduhe  Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga katika kuelekea maadhimisho ya miaka 60 ya muungano.
Bi. Monica Charles aliyeshiriki mashindano ya kukimbiza kuku kwenye mashindano ya kuelekea maadhimisho ya miaka 60 ya muungano yaliyofanyika April 24,2024 kwenye viwanja vya shule ya Msingi Buduhe Wilayani Kishapu Mkoani Shinyanga


Msimamizi mkuu wa sherehe za muungano na mkuu wa wilaya ya Kishapu Mkaoani Shinyang Mhe.Joseph Mkude Kushoto (aliyevaa traksuti) na Diwani wa Kata ya Kishapu(kulia mwenye nguo nyeupe) Mhe.Joel Ndettoson wakiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi wa Isoso Sekondari kwenye kilele cha bonanza la michezo April,24,2024 katika viwanja vya shule ya msingi Buduhe wilayani humo.
Picha ya pamoja ya wachezaji wa Ghazza Fc na msimamizi mkuu wa sherehe za muungano Mhe.Joseph Mkude na Diwani ya kata ya Kishapu Mhe.Joel Ndettoson kabla ya mechi walioibuka kidedea kwa bao 1-0 dhidi ya Kishapu Veteran April 24,2024 kwenye kilele cha bonanza la kuelekea maadhimisho ya miaka 60 ya muungano
Share:

RC TANGA ATOA NENO KWA WANUNUZI WA ZAO LA MWANI

 

Mkuu wa Mkoa wa Tanga akizungumza wakati wa ziara ya kutembelea wakulima wa zao hilo katika Mtaa wa Sahare Kijijini Kata ya Mzingani Jijini Tanga ambao pia alizungumza na wakulima wa zao hilo kwenye wilaya za Tanga,Mkinga ,Muheza na Pangani ikiwa ni kuelekea Shamrashamra za kuelekea miaka 60 ya Muungano.


MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian akitembea kuelekea baharini kuangalia kilimo cha Mwani wakati wa ziara yake ya kuwatembelea wakulima hao
MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian akitoka kukagua zao la Mwani wakati wa ziara yake 
Afisa Mfawidhi Idara ya Ukuzaji wa Viumbe Maji kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Mkoa wa Tanga Omari Ally Mohamed akieleza jambo wakati wa ziara hiyo





Na Oscar Assenga, TANGA.

MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian amewataka wanunuzi wa zao la mwani mkoani humo kuheshimu mikataba wanayoingia na wakulima ili waweze kulima kwa tija na hivyo kuweza kujikwamua kimaendeleo.

Amesema kutokuheshimu mikataba hiyo hawatakubali kuona linatokea badala yake wataona namna ya kufatuta njia nyengine za kuwahudumia ikiwemo mabenki kwa ajili ya kuwawezesha kupata mikopo yenye riba ndogo na nafuu.

RC Batilda aliyasema hayo  wakati wa ziara ya kutembelea wakulima wa zao hilo katika Mtaa wa Sahare Kijijini Kata ya Mzingani Jijini Tanga ambao wametokea kwenye wilaya za Tanga,Mkinga ,Muheza na Pangani ikiwa ni kuelekea Shamrashamra za kuelekea miaka 60 ya Muungano.

Ambapo pia alitembelea shamba la wakulima wa Mwani pamoja na kugawa kofia,mabuti ,nyundo,kamba na taitai ili kuweza kuwawezesha wakulima hao wa mwani kutekeleza vema shughuli zao za kila siku .

Alisema kwasababu haiwezekani wanunuzi wa zao hilo wanaingia mikataba na wakulima lakini wanashindwa kutoa vifaa, kutokuwahudumia wala kutoa pembejeo kitendo ambacho kinapelekea wakulima kuhangaika bila kujua kamba wanatoa wapi.

“Hii haiwezekani mkulima wa mwani anakopa hii sio sawa unamuumiza mkulima kutokana na kwamba wanafanya kazi kubwa yenye tija lakini kama mkipata mwekezaji mzuri mtaweze kujikwamua kiuchumi nimewaelekeza Jiji na nitaongea na Waziri wa Uvuvi aweze kuona namna ya kuwasaidia tupate boti”Alisema

“lakini niwaambie wanunuzi kama hii kazi imewashinda tutavunja mikataba tuweze kujua wakulima wetu tunawahudumiaje tuwaitea mabenki waje watoe mikopo kama benki ya kilimo TIDB wanatoa mikopo yenye riba ndogo sana chini ya asilimia 4 mpaka 3waweze kuwakopesha waweze kununua kamba,taitai,troliki waweze kufanya kazi kwa tija yenye faida”Alisema

Aidha Mkuu huyo wa mkoa alisema Wizara ya Uvuvi watashirikiana nao kwenye suala la masoko huku akimpongeza Waziri wa Mifugo na Uvuvi Ulega kwa kuanzisha stakabadhi ghalani kama ilivyo mazao mengine ya kilimo .

Alisema mfumo huo utawezesha za la Mwani kuwekwa kwenye stoo utapigwa mnada na watapata bei ya soko kuliko ilivyokuwa bei ya sasa ambao madalali wanapanga bei wanayotaka jambo ambalo linawaumiza wakulima wengi.

“Nimetembelea Shamba la Mwana nimeona changamoto hawana vifaa vya kubebea mwani kutoka baharini mpaka nchi kavu ,hawana chombo wanatumia kama boya mpaka kufika pwani hiyo ni kazi kubwa ina tija hivyo nimewaekeza jiji nitaongoea pia na Waziri wa Uvuvi awasaidie mpate (faiba) boti hata ndogo milioni 15”Alisema

“Ndugu zangu hapa nimesikia mnachangamoto ya Kamba kazi hii bila kuwa navyo itakuwa ni ngumu hivyo nitawasaidia milioni 3 (3000, 000) kwa ajili ya kununua kamba taitai ili msimu utaoanza mwezi wa saba usipite bila kuwa nazo”Alisema RC huyo.

“Lakini lazima tuhakikishe kwanza tunakwenda na kauli mbiu ya Rais Dkt Samia Suluhu na Rais za Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi ya uchumbi wa bluu kwa Mkoa wa Tanga tuliokuwa nao ni zao la mwani na ufungaji magongoo bahari na kwenda kwenye ufungaji wa pweza,kaa na majongoo bahari ,chaza,kamba”Alisema RC

Hata hivyo katika kuhakikisha analitilia mkazo zao hilo ,RC Batilda alisema kwamba Aprili 29 mwaka huu atakuwa na viongozi wa wavuvi na viongozi makampuni yanayonunua mwani ili kuweza kuweka mikakati ya namna ya kuweza kuhakikisha wakulima wanaendelea kupata tija. Hata hivyo Mkuu huyo wa mkoa alitumia wasaa huo kueleza kwamba vitu ambayo atasimama navyo ni kuhakikisha wanavidhibiti uvuvi haramu huku akiwaonya wanaojihusisha na uvuvi haramu kuachana nao.
Share:

WANAGDSS WAICHAMBUA BAJETI YA OFISI YA RAIS (MIPANGO NA UWEKEZAJI) NA KUBAINI HAIJAZINGATIA MASUALA YA JINSIA



NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

WADAU mbalimbali wa masuala ya Jinsia na Maendeleo wamekutana katika Semina za Jinsia na Maendeleo (GDSS) na kuichambua bajeti ya Ofisi ya Rais (Mipango na uwekeshaji) na kubaini kuwa haijazingatia masuala ya jinsia.

Akizungumza leo Aprili 24,2024 jijini Dar es salaam, wakati wa semina ambazo hufanyika kila Jumatano katika Ofisi za TGNP Mtandao, Mhadhiri Chuo Kikuu Mzumbe Lihoya Chamwali amesema uwekezaji ambao umekuwa unafanyika kwa wanawake haukuzingatiwa hasa kufufua viwanda ambavyo wanawake wamekuwa wakishiriki.

Aidha ameishauri serikali kutoa elimu kwa wananchi kuhusu maswala ya uwekezaji kwani elimu hiyo imekuwa haijulikani kwa watu wengi hasa wanawake.

"Tunaishauri serikali iweke mifumo rafiki na elimu itolewe ili kila mwanamke ambae anaweza kuwekeza aweze kuingia kwenye mfumo na ndio maana tunasisitiza elimu itolewe kwani mifumo mingi ya uwekezaji inafanyika kielektroniki kitu ambacho wanawake wanawake wamekuwa wanaachwa kwa sababu wengi hawana ujuzi wa elimu hiyo". Amesema Chamwali.

Amesema bajeti ya mwaka huu imekuwa ndogo tofauti ya mwaka jana kwani mwaka 2023 bajeti ilikuwa bilioni30 lakini mwaka huu bilioni 17.

Amesema kufuatia na upungufu huo wa bajeti katika kupitia malengo wameona malengo mengi ya mwaka huu ni muendelezo wa malengo yaliyofanyika mwaka jana ikiwemo kupitia uundaji wa sera ya dira ya maendeleo 2050.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kituo cha maarifa kata ya Majohe Tabu Ally ametoa rai kwa serikali kuwaangali wanawake waliopembezoni ili waweze kujikwamua kiuchumi kwa kuwapa elimu bora ya uwekezaji.

Amesema changamoto kubwa inayowakabili wanawake waliopembezoni ni miundombinu ya barabara kwani wanazalisha lakini wanashindwa kufika sokoni kutokana na uharibifu mkubwa wa barabara hivyo inawalazimu kutumia ghalama kubwa ili kufika sokoni jambo ambalo linawarudisha nyuma kimaendeleo.

"Kila kitu ili kiende ni lazima barabara zipitike na hiyo ndio changamoto ambayo sisi tunalia nayo lakini hata tukiwezeshwa mitaji bado tutashindwa kutokana na hii moundombinu",Amesema Tabu

Naye,Mdau wa maswala ya jinsia kutoka Kigamboni Ayub Sharif amesema serikali inapaswa kutoa kipaumbele kwenye maeneo ambayo nguvu kazi kubwa inatumika ili kuongeza motisha ya ufanyaji kazi.

"Mimi naishauri serikali kuangali maeneo ambayo nguvukazi kubwa inatumia ndio uwezeshaji uanzie kwani tumeona katika sekta ya madini wanawake ndio wachenjuaji wakubwa lakini madini yakipatikana anaenufaika mwingine hii sio sawa serikali inapaswa kuangali swala hili kabla ya kuwekeza kwenye mitambo waweke mazingira mazuri kwa hizi nguvu kazi". Amesema.
Share:

Wednesday 24 April 2024

WADAU WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA KILIMO IKOLOJIA HAI


Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara ya Kilimo, Obadia Nyagiro,akizungumza wakati wa kikao cha wadau wa Kilimo Ikolojia hai kilichoratibiwa chini ya mwamvuli wa Taasisi za Kilimo Hai Tanzania (TOAM) kilichofanyika jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa TOAM, Dk.Mwatima Juma,akizungumza wakati wa kikao cha wadau wa Kilimo Ikolojia hai kilichoratibiwa chini ya mwamvuli wa Taasisi za Kilimo Hai Tanzania (TOAM) kilichofanyika jijini Dodoma.

Paul Holmbeck kutoka Shirika la Biovision Foundation,akizungumza wakati wa kikao cha wadau wa Kilimo Ikolojia hai kilichoratibiwa chini ya mwamvuli wa Taasisi za Kilimo Hai Tanzania (TOAM) kilichofanyika jijini Dodoma.


Baadhi ywa wadau wa Kilimo Ikolojia hai wakifatilia majadiliano mbalimbali wakati wa kikao hicho kilichoratibiwa chini ya mwamvuli wa Taasisi za Kilimo Hai Tanzania (TOAM) kilichofanyika jijini Dodoma.


Na.Alex Sonna-DODOMA

WADAU wa kilimo ikolojia hai wamekutana jijini Dodoma kutengeneza mpango kazi wa mwaka 2024/25 kwa ajili ya utekelezaji vipaumbele vya Mkakati wa kitaifa wa kilimo hai wa ikolojia wa 2023-2030 (NEOAS) utakaoleta mageuzi ya kilimo nchini.

Akizungumza kwenye kikao hicho kilichoratibiwa chini ya mwamvuli wa Taasisi za Kilimo Hai Tanzania (TOAM), Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara ya Kilimo, Obadia Nyagiro, alisema kilimo hicho ni muhimu kwa watanzania kwa kuwa kitaleta tija kiuchumi, kulinda afya za walaji, afya ya udongo na kuongeza kipato.

Alisema mkakati huo unatokana na Sera ya kilimo kuelekeza masuala ya kuweka mfumo wa uzalishaji, upatikanaji wa masoko na kutambua bidhaa za kilimo hai.

“Mkakati wenyewe ulizinduliwa mwishoni mwa mwaka jana na upo tayari kwa utekelezaji, kilichotufanya tukutane ni namna ya kutekeleza mkakati huu kwa kuandaa mpango kazi kila mwaka kwa muda wa miaka saba ya huu mkakati wa kitaifa, kama tulivyowashirikisha kwenye maandalizi yake lazima tushiriki sisi wadau kwa kuweka malengo ya utekelezaji wake kila mwaka,”alisema.

Alisema serikali itaendelea kutoa ushirikiano ili kufanikisha uandaaji wa mpango huo kwa kuwa ni muhimu wadau kushiriki katika kilimo himilivu na endelevu kwa mazingira na afya ili kuleta tija kwenye sekta ya kilimo.

Alizitaka asasi za kiraia na sekta binafsi kuchangamkia fursa ya uwekezaji katika kilimo hicho kwa kuwa kina tija kubwa.

“Nihimize sekta binafsi na asasi za kiraia mpitie na kuona fursa ya kuwekeza katika eneo hili kwa kuwa tija yake ni kubwa ikiwamo kuongezeka kwa mapato, mkipitia nchi nyingine mtaona waliowekeza kwenye kilimo hiki na tija yake na ni muhimu mipango yetu izingatie kilimo himilivu kinachozingatia mabadiliko ya tabia nchini,”alisema.

Naye, Mwenyekiti wa TOAM, Dk.Mwatima Juma alisema kilimo hicho kinalenga kuwa na uzalishaji wa kutosheleza, kulinda afya na udongo kwa kuondokana na matumizi ya kemikali.

“Kilimo cha kutumia kemikali kilianza miaka 100 iliyopita baada ya kuisha kwa vita kuu ya pili ya dunia ambapo utengenezaji wa mbolea za kemikali, viuatilifu vya kemikali ilionekana itatusaidia kuzalisha chakula zaidi, tulihamasika kuwa kutumika kemikali ndo ukisasa na kwa bahati mbaya tuliacha kilimo chetu cha asili ambacho mtu alikuwa akilima kahawa ndani yake ana kunde,maharage, mtama vyote vinazalishika vizuri na ana ng’ombe anatupia mbolea shambani kwake.”

“Tukahamasisha tuwe na mashamba makubwa tulime zao moja, tupulize dawa miaka imekwenda na tulipofika mimi binafsi nasema tuwaombe radhi wakulima kwa maeneo tuliyowapeleka hasa wakulima wadogo hapafai, kuna aina ya ukulima wanaweza kulima bila kupunguza uzalishaji, bila kupata shida kwenye chakula na kuuza kwenye masoko ya ndani na nje,”alisema.

Alibainisha kuwa kilimo hicho kitasaidia watanzania kuondokana na maradhi mbalimbali ikiwamo uzazi, saratani kwa kuwa yanatokana na matumizi ya kemikali kwenye kilimo.

Naye, Paul Holmbeck kutoka Shirika la Biovision Foundation akizungumzia mataifa mengine namna yanavyotekeleza kilimo hicho, alisema wanasayansi na mashirika ya kimataifa ya masuala ya kilimo yanahimiza kilimo hicho kwa usalama wa chakula na kuna tija kiuchumi ambapo serikali za nchi ambazo zinatekeleza kilimo hicho zinaweka malengo yake.
Share:

RC MACHA AFUNGUA RASMI SEMINA YA FAMILIA,MALEZI,BIASHARA NA HUDUMA ZA AFYA KANISA LA WAADVENTISTA WASABATO

 



Na Marco Maduhu,SHINYANGA
MKUU wa Mkoa wa Shinyanga Anamringi Macha,amefungua Rasmi Semina ya Familia,Malezi,Biashara na huduma za Afya, ambayo inaendeshwa na Kanisa la Waadventista Wasabato Ukanda wa dhahabu Nyanza Gold Belt Field NGBF.

Semina hiyo imeanza kutolewa Aprili 2,2024 ambayo itakwenda hadi Aprili 27 mwaka huu Siku ya Jumamosi,imekutanisha watu mbalimbali ambayo inafanyika katika ukumbi wa Makindo.
Macha akizugumza wakati wa kufungua Semina hiyo, imelipongeza Kanisa la Waadventista Wasabato kwa kuendesha Semina hiyo ambayo inathamani kubwa kwa taifa, kwa kutoa masomo ya Familia na Makuzi,Afya pamoja na Biashara.

“Nalipongeza sana Kanisa la Waadventista Wasabato,ni Kanisa ambalo lenye Mahaghaiko makubwa katika kuhakikisha Makuzi ya Vijana yanakuwa kwenye Maadili mema, sababu sasa hivi hapa nchini kuna Janga la Mmomonyoko wa Maadili ya Vijana, na Taifa bora linajengwa na Malezi bora na Makuzi,”amesema Macha.
“Masomo haya ya Familia yanakumbusha wazazi kulea watoto wao katika Maadili Mema, na siyo kuwaacha wakijilea wenyewe na hatimaye kusababisha watoto kuwa na Maadili Mabovu,”ameongeza Macha.

Amesema kwa upande wa Masomo ya Afya, ameitaka jamii kuzingatia lishe bora, sababu Magonjwa mengine hasa yasiyo ya kuambukiza husababishwa na Mtindo Mbovu wa Maisha, na kwamba kupitia Mafunzo hayo yanaijenga jamii yenye Afya Bora.
Aidha, amesema kupitia Masomo ya Biashara,amewataka Wafanyabiashara wawe na hofu ya Mungu, na kufanya biashara zao kwa haki bila ya kuchakachua bidhaa, pamoja na kulipa Kodi ya Serikali.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa, ametoa wito kwa viongozi wa dini kuendelea kuliombea Taifa Amani, pamoja na Rais Samia na wasaidizi wake,ili awe na maono mazuri ya kuiongoza Nchi katika kweli na haki, sababu Nchi ikiwa na Amani itakuwa na Maendeleo.
Naye Askofu wa Jimbo la Ukanda wa dhahabu (NGBF) Kanisa la Waadventista Wasabato Enock Sando, amesema Kanisa hilo limeendelea kujipambanua katika ulimwengu kote na kugusa jamii, kuisaidia kujitegemea kupitia Semina za Biashara ili wawe na Fikra Chanya ya kujikwamua kiuchumi sababu Mungu hapendezwi na Umaskini.

Amesema Kanisa hilo pia lina amini katika Afya, sababu bila Afya hakuna Maendeleo, ndiyo maana katika Semina hiyo mafunzo ya Afya yanatolewa, pamoja na Masomo ya Kaya na Familia ili kuwe na Taifa lenye Umoja,Mshikamano na Mahusiano Mazuri.

TAZAMA PICHA HAPA CHINI👇👇
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Anamringi Macha akizungumza wakati akifungua Semina hiyo.
Askofu wa Jimbo la Ukanda wa dhahabu (NGBF) Kanisa la Waadventista Wasabato Enock Sando.
Awali Mchungaji Mstaafu Wilbert Nfumbusa akitoa Somo la Kaya na Familia.
Awali Mwenyekiti wa Wafanyabiashara Mkoa wa Shinyanga (TCCIA) Jonathani Manyama akitoa Somo la Biashara kwenye Semina hiyo.
Awali Afisa Muuguzi Sherida Madanka akitoa Somo la Lishe kwenye Semina hiyo.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Semina ikiendelea.
Kwaya ya Lubaga Mara Nassa ikiimba kwenye Semina hiyo.
Kwaya ya SAC ikiimba kwenye Semina hiyo.
Kwaya ya Lubaga Mara Nassa ikiimba kwenye Semina hiyo.
Kwaya ya SAC ikiimba kwenye Semina hiyo.
Kamati ya Maandalizi ya Semina hiyo ikiimba kwenye Semina.
Picha ya pamoja ikipigwa kwenye Semina hiyo.
Picha ya pamoja ikipigwa ikipigwa Semina hiyo.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger