Friday, 19 June 2026

DC NGUBIAGAI ATEKELEZA AGENDA YA RAIS SAMIA YA UHIFADHI WA RASILIMALI, ZANA HARAMU ZA SH. MILIONI 73.6 ZATEKETEZWA UKEREWE

Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Cde. Christopher Ngubiagai akihutubia wananchi wa Gana katika mkutano
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe Ndg. Vicent Mbua akizungumza na wananchi wa Gana kuachana na uvuvi haramu

Na Mwandishi Wetu - Ukerewe

Mikakati ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ya kuimarisha usimamizi wa rasilimali za taifa na kuhakikisha sekta ya uvuvi inachangia kikamilifu ukuaji wa uchumi inaendelea kuzaa matunda, ambapo Wilaya ya Ukerewe imeendelea kuchukua hatua madhubuti dhidi ya uvuvi haramu.

Katika kuonesha dhamira hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe, Christopher Ngubiagai, Juni 18, 2026 ameongoza operesheni ya kuteketeza zana haramu za uvuvi zenye thamani ya Shilingi milioni 73,615,000 katika Kisiwa cha Gana, Kijiji cha Kamasi, Kata ya Ilangala.

Hatua hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Serikali ya kuhakikisha rasilimali za Ziwa Victoria zinalindwa kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho sambamba na kuimarisha uchumi wa wananchi wanaotegemea sekta ya uvuvi.

Akizungumza katika tukio hilo, Cde. Ngubiagai amesema Serikali haitamvumilia mtu yeyote atakayejihusisha na uvuvi haramu unaoharibu mazalia ya samaki na kuhatarisha ustawi wa sekta hiyo muhimu kiuchumi.

Aidha, amewahimiza wananchi kuachana na mbinu haramu za uvuvi na badala yake kutumia fursa zilizopo katika kuongeza thamani ya mazao ya samaki kupitia usindikaji, uhifadhi bora na biashara endelevu, hatua itakayochochea ukuaji wa uchumi wa kaya na taifa kwa ujumla.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe, Vicent Mbua, amewapongeza wananchi na wajumbe wa kamati kwa ushirikiano mkubwa wanaoendelea kuutoa katika mapambano dhidi ya uvuvi haramu.

Mbua amesema ushirikiano huo unaendana na dhamira ya Serikali ya kuhakikisha sekta ya uvuvi inakuwa endelevu na yenye tija kwa maendeleo ya wananchi na taifa.

Amesema halmashauri itaendelea kusimamia kikamilifu utekelezaji wa sheria za uvuvi ili kulinda mapato ya halmashauri na kuhakikisha wananchi wanapata samaki bora na wa kutosha.

"Kila mvuvi anapaswa kuzingatia sheria zinazomuongoza katika shughuli zake. Serikali itaendelea kudhibiti uvuvi haramu unaoharibu mazalia ya samaki na kuhatarisha uchumi wa wananchi," amesema Mbua.

Katika taarifa yake, Katibu wa Mwalo wa Gana, Charles Gunda, amesema zana zilizoteketezwa ni pamoja na timba pisi 1,627 na nyavu za makira inchi tatu pisi 80.

Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Ilangala, Petro Majura, ameonya kuwa hatua kali za kisheria zitaendelea kuchukuliwa dhidi ya wote watakaobainika kujihusisha na vitendo vya uvuvi haramu.

Naye Mkuu wa Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi wa Halmashauri hiyo, Godfrey Ayako, amesema Serikali inaendelea kutatua changamoto mbalimbali katika sekta ya uvuvi ikiwemo suala la upimaji wa mizigo ya dagaa ili kuongeza ufanisi na tija kwa wavuvi.

Sambamba na juhudi hizo, Cde. Ngubiagai amewahimiza wananchi kuunda na kusajili vikundi ili waweze kunufaika na mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri, hatua inayodhihirisha dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuwawezesha wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kiuchumi.

Hatua hizi zinaendelea kuonesha namna Serikali ya Rais Samia ilivyodhamiria kulinda rasilimali za taifa, kuimarisha uchumi wa buluu na kuhakikisha wananchi wanashiriki kikamilifu katika safari ya maendeleo ya Taifa.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA JUNI 19,2026

Magazeti





Share:

MARIAM MWINYI KUWA MGENI RASMI MASHINDANO YA QUR’AN KWA WANAWAKE

Sheikh wa mkoa wa Dar es salaam, Walid Alhad Omari

*****

Mke wa Rais wa Zanzibar, Mariam Mwinyi, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika mashindano ya Qur’an Tukufu kwa wanawake wa rika mbalimbali yatakayofanyika Jumapili katika ukumbi wa DYCCC Hall.

Mashindano hayo yameandaliwa na Umul-Muuminina Aisha Foundation (UMAIF) kwa lengo la kuhamasisha wanawake kujifunza, kusoma na kuhifadhi Qur’an Tukufu pamoja na kukuza maadili mema ya Kiislamu katika jamii.

Akizungumza kuhusu tukio hilo, Sheikh WA mkoa wa Dar es salaam, Walid Alhad Omari amewaomba Watanzania kujitokeza kwa wingi Juni 21, 2026 kushuhudia mashindano hayo yatakayowakutanisha washiriki kutoka maeneo mbalimbali.



Amesema mashindano hayo yanatarajiwa kuvutia wadau wa dini, elimu na maendeleo ya jamii, huku yakiwa jukwaa muhimu la kuhamasisha wanawake kushiriki katika kujifunza na kuhifadhi Qur’an Tukufu.









Share:

Thursday, 18 June 2026

NBS YAAHIDI KUENDELEA KUTOA TAKWIMU SAHIHI KUSAIDIA UTEKELEZAJI WA DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO 20250




Na Wellu Mtaki, Dodoma

OFISI ya Taifa ya Takwimu (NBS) imesema itaendelea kuhakikisha takwimu rasmi zinapatikana kwa wakati, kwa ubora unaohitajika na kwa kuzingatia viwango vya kitaifa na kimataifa ili kusaidia juhudi za maendeleo ya taifa katika kipindi chote cha utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi wa NBS, Daniel Masolwa, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali.

Amesema NBS ni miongoni mwa taasisi za serikali zinazoshiriki maadhimisho hayo kwa kutoa elimu kwa wananchi kuhusu huduma zake, majukumu yake pamoja na umuhimu wa takwimu rasmi katika maendeleo ya taifa.

Masolwa alisema kuwa takwimu rasmi zitakuwa nyenzo muhimu katika kufuatilia, kutathmini na kupima utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, ambayo inalenga kuifikisha Tanzania katika uchumi wa dola trilioni moja na kuongeza ustawi pamoja na kipato cha wananchi.

Alieleza kuwa takwimu zenye ubora na zinazopatikana kwa wakati zinasaidia serikali, sekta binafsi, taasisi za utafiti na wadau mbalimbali kufanya maamuzi sahihi yanayochochea ukuaji wa uchumi na maendeleo endelevu.

Aidha, amesema kaulimbiu ya mwaka huu ya Wiki ya Utumishi wa Umma inayosema, “Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa Huduma Endelevu,” imeipa NBS fursa ya kuendelea kuhamasisha wananchi kuhusu nafasi ya takwimu rasmi katika upangaji wa maendeleo, ugawaji wa rasilimali na ufuatiliaji wa utekelezaji wa mipango ya taifa.

Amefafanua kuwa kwa mujibu wa Sheria ya Takwimu, Sura ya 351, NBS imepewa mamlaka ya kukusanya, kuchakata, kuchambua na kusambaza takwimu rasmi zinazotumika katika sekta mbalimbali za maendeleo nchini.

“Takwimu rasmi ni msingi wa upangaji wa maendeleo. Serikali, sekta binafsi, watafiti na wadau wengine hutegemea takwimu hizi katika kufanya maamuzi sahihi, kuandaa sera, kupanga bajeti na kupima matokeo ya mipango inayotekelezwa,” amesema.

Masolwa alitaja baadhi ya takwimu zinazozalishwa na NBS kuwa ni pamoja na takwimu za mfumuko wa bei zinazotolewa kila mwezi na kuonesha mwenendo wa bei za bidhaa na huduma nchini, hali inayosaidia kutathmini mazingira ya uchumi na gharama za maisha kwa wananchi.

Pia alisema ofisi hiyo huzalisha takwimu za Pato la Taifa (GDP) kwa vipindi vya robo mwaka ambazo huonesha thamani ya bidhaa na huduma zinazozalishwa nchini, kiwango cha ukuaji wa uchumi pamoja na mchango wa kila sekta katika maendeleo ya uchumi wa taifa.

Kwa upande wa ajira, alisema NBS hutoa takwimu zinazoonesha hali ya soko la ajira, kiwango cha ukosefu wa ajira, idadi ya watu walio katika ajira na wale walio nje ya nguvu kazi, jambo linalosaidia katika uandaaji wa sera na mikakati ya kukuza fursa za ajira.

“Tunaendelea pia kuzalisha takwimu za kilimo, uzalishaji viwandani, biashara ya nje pamoja na takwimu za kijamii zinazotokana na Sensa ya Watu na Makazi. Takwimu hizi zinaonesha mwenendo wa idadi ya watu, mgawanyo wa umri, hali ya makazi na rasilimali watu iliyopo nchini,” amesema.

Aliongeza kuwa takwimu hizo ni muhimu katika kukokotoa viashiria mbalimbali vya maendeleo ikiwemo wastani wa pato la mwananchi, viwango vya umaskini, maendeleo ya sekta mbalimbali na hali ya uchumi kwa ujumla.

Akizungumzia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, Masolwa alisema mafanikio ya utekelezaji wake yatategemea kwa kiasi kikubwa uwezo wa nchi kutumia takwimu sahihi katika kupanga, kufuatilia na kutathmini hatua zinazopigwa kuelekea malengo yaliyowekwa.

Alisisitiza kuwa katika dunia ya sasa inayotegemea maarifa na teknolojia, matumizi ya takwimu yamekuwa nguzo muhimu katika kufanya maamuzi yenye tija na kuongeza ushindani wa uchumi.

“Lengo la Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 ni kuwa na uchumi mkubwa zaidi unaotoa ustawi kwa wananchi. Ili kufikia malengo hayo tunahitaji jamii inayojifunza, inayozalisha maarifa, inayotumia ujuzi na inayofanya maamuzi kwa kuzingatia takwimu sahihi na zenye kuaminika,” amesema.


Amesema NBS itaendelea kuimarisha mifumo ya ukusanyaji na uchambuzi wa takwimu ili kuhakikisha wadau wote wanapata taarifa sahihi zitakazosaidia kuharakisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini.
Share:

OWM YASHIRIKI MAONESHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA 2026


Na Mwandishi wetu - Dodoma


Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu Bi. Stella Mwaiswaga pamoja na Watumishi wengine kutoka Ofisi hiyo wameshiriki ufunguzi wa Maonesho ya Wiki ya Utumishi tarehe 17 Juni, 2026 katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma.


Maonesho ya Wiki ya Utumishi ni moja ya matukio katika kalenda ya Umoja wa Afrika (AU) ambapo nchi wanachama huadhimisha kwa kaulimbiu moja na kufanya maonesho ya kazi mbalimbali kuhusu masuala ya Utumishi wa Umma ambapo hufanyika kila mwaka kuanzia tarehe 16 hadi 23 Juni 2026.


Kwa mwaka huu Maadhimisho hayo yamebeba kaulimbiu isemayo; “Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi wa Huduma Endelevu”.


SAmbamba na hilo Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu inashiriki maonesho hayo huku ikitoa elimu mbalimbali kwa umma kuhusiana na shughuli za Wakala Serikali wa uchapishaji Tanzania, elimu kuhusu masuala ya Menejimenti ya Maafa, Watu wenye Ulemavu, Ufuatiliaji na Tathimini pamoja na Masuala ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi.







Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger