Thursday, 29 January 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA JANUARI 30, 2026

Share:

SERIKALI YATOA MIKOPO KIASI CHA SHILINGI MILIONI 600 KWA WANANCHI



Na Josephine Manase, Morogoro

Halmashauri ya Mji Ifakara Januari 27,2026 imetoa mikopo ya asilimia 10 yenye thamani ya Shilingi milioni 600 ikiwa ni Mikopo ya Asilimia 10 inayotokana na Mapato ya ndani kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, ikiwa ni utekelezaji wa sera ya kuwawezesha wananchi kiuchumi.

Akizungumza wakati wa hafla ya utoaji wa mikopo hiyo iliyofanyika katika Viwanja vya Stendi ya mabasi kibaoni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Felista Mdemu, ameipongeza Halmashauri hiyo kwa kuendelea kutekeleza kwa vitendo azma ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuwawezesha wananchi kiuchumi kupitia mikopo isiyo na riba.

Mdemu amevitaka vikundi vilivyonufaika kutumia mikopo hiyo kwa malengo yaliyokusudiwa, kuzingatia masharti ya mikataba, pamoja na kurejesha mikopo kwa wakati ili kutoa fursa kwa wananchi wengine kunufaika.

Shilingi 404,787,300 tayari imekwishatolewa kwa vikundi 41, vikiwemo vikundi 20 vya wanawake, 17 vya vijana na 4 vya watu wenye ulemavu na Shilingi 195,212,700 zitatolewa kwa vikundi 17 vilivyosalia mara baada ya kukamilisha maboresho yaliyoelekezwa.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Ifakara, Pilly Kitwana amewasihi wananchi wa Halmashauri ya Mji Ifakara kuendelea kuunda Vikundi kwani pesa bado zipo ambazo zitasaidia kuwainua pia ameahidi kuendelea kufanya tathimini na ufuatiliaji kwa vikundi vilivyonufaika ili kuhakikisha mikopo hiyo inaleta tija na kuchangia maendeleo ya kiuchumi kwa wanufaika na jamii kwa ujumla.





Share:

Wednesday, 28 January 2026

KIJANA APITIA MATESO MAZITO LAKINI AKAJA KUWA MTU MAARUFU DUNIANI



Nilizaliwa kwenye familia ya kawaida sana, bila jina, bila mtaji, na bila mtu wa kunisukuma mbele. Wakati wenzangu walionekana kuwa na mwelekeo maishani, mimi nilikuwa napambana na umaskini, kejeli na kukataliwa kila mahali nilipojaribu.

Shuleni nilidharauliwa, mitaani nilionekana kama asiye na maana, na hata nyumbani nilionekana kama mzigo. Kila nilipoonyesha ndoto zangu, watu walicheka. Mateso yangu hayakuishia hapo. Nilipofika utu uzima, nilipitia kushindwa mara kwa mara.

Kazi nilikosa, miradi ilifeli, marafiki walinigeuka. Nililala njaa siku kadhaa, nikihama makazi mara kwa mara, nikiishi kwa msaada wa watu. Kilichoniumiza zaidi ni kwamba nilikuwa na kipaji, lakini kilionekana kama kimefungwa.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO JANUARI 28,2026




Magazeti






Share:

Tuesday, 27 January 2026

TWIGA, TANGA CEMENT WAPEWA SAA 48 KUJISALIMISHA




•Watakiwa kusimamia bei elekezi

• Wachimbaji wadogo watakiwa kutulia

DODOMA | Januari 26, 2026

SERIKALI kupitia Wizara ya Madini imezipa Kampuni za Twiga Cement na Tanga Cement saa 48 kufika mbele ya mamlaka husika na kujibu hoja zinazowakabili, ikiwemo madai ya kukiuka bei elekezi za madini zinazotolewa na Serikali na kukosa mikataba kwa wauzaji wa malighafi viwandani.

Akizungumza leo katika kikao cha wachimbaji wadogo wa madini ya Jasi (gypsum) kutoka Same mkoani Kilimanjaro kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Gold, Ofisi za Tume ya Madini jijini Dodoma, Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Dkt. Steven Kiruswa, amesema kampuni hizo zikikaidi wito huo, Serikali itachukua hatua kali ikiwemo kusimamisha shughuli zao.

“Kitendo cha kukaidi wito wa Serikali ni kuidharau mamlaka. Wasipofika ndani ya saa 48, tutamshauri Waziri kufuta leseni zao,” amesema Mhe. Dkt. Kiruswa.

Amesisitiza kuwa kampuni hizo zinapaswa kulipa wasambazaji wa madini ya jasi kwa kuzingatia bei elekezi iliyowekwa na Serikali, kutoa mikataba ya kazi kwa wauzaji wa bidhaa, na kuacha kununua kwa bei ya chini inayowaumiza wachimbaji wadogo.

Kauli hiyo imekuja kufuatia malalamiko ya wachimbaji wadogo wa madini ya jasi wa Wilaya ya Same, wakidai kuwa kampuni hizo zinakinyima kazi Chama cha Ushirika cha Wachimbaji Wadogo wa Madini ya Jasi (Kilimanjaro Gypsum Cooperative Society Ltd), na badala yake kushirikiana na watu binafsi wachache wanaolipwa chini ya bei elekezi na bila mikataba.

“Mnaokubali kuuza madini yenu kwa bei ya chini mnajipiga misumari wenyewe. Bei elekezi iheshimiwe,” amesisitiza Mhe.  Dkt. Kiruswa, huku akiwataka wachimbaji kutulia wakati Serikali ikishughulikia changamoto hiyo

Aidha, Naibu Waziri amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Same, Kasilda Mgeni, kuipeleka TAKUKURU kuchunguza madai ya rushwa yanayodaiwa kujitokeza katika viwanda hivyo.

Awali, Kamishna wa Tume ya Madini, Dkt. Theresia Numbi, amesema utoaji wa mikataba ni takwa la kisheria, si hiari.
“Ni lazima Chama cha Ushirika kishirikishwe. Toeni asilimia kwa Chama, na nyingine muwape wale mnaowataka kufanya nao kazi,” amesema.

Kwa upande wake, Meneja Uwezeshaji Uchimbaji Mdogo, Nchagwa Marwa, kutoka Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) amesema uchimbaji ni sekta jumuishi, akiongeza kuwa kuwa kumpendelea mtu mmoja na kukiacha Chama si mwelekeo sahihi.

“Msimamo wa Serikali ni kila Mtanzania anufaike na rasilimali madini. Ndiyo maana kauli mbiu ni Madini ni Maisha na Utajiri. Bei elekezi iheshimiwe,” amesema.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Msafiri Mbibo, amezitaka kampuni kufuata taratibu za utoaji wa oda akisisitiza kuwa Serikali inatoa upendeleo kwa wazawa na matarajio ni wawekezaji kuwalinda wananchi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Same, Kasilda Mgeni, amelaani vikali hatua ya kampuni hizo kudharau wito wa Serikali, akidai hali ya usalama katika maeneo ya Makanya na Ruvu Kajiungeni imeathirika kutokana na mgawanyiko miongoni mwa wachimbaji.

“Viongozi wote tumekuja, Madiwani, Mkurugenzi, Katibu Tawala wa Wilaya kwa lengo la kumaliza mgogoro na kurejesha amani. Kudharau huku ni kudharau Serikali na hata dhamana ya Mheshimiwa Rais. Wizara ichukue hatua stahiki, hata ikibidi kuzisimamisha shughuli za viwanda hadi suluhu ipatikane,” amesema.

Serikali imesisitiza itaendelea kulinda maslahi ya wachimbaji wadogo, kusimamia bei elekezi, na kuhakikisha sekta ya madini inakuwa jumuishi kwa manufaa ya Watanzania wote.












Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger