Friday, 17 July 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JULAI 17, 2026

Share:

Thursday, 16 July 2026

SIMAMMIENI MIRADI YA MAENDELEO, PINGENI UKATILI DHIDI YA WATOTO: NAIBU WAZIRI MAHUNDI



Na Jackline Minja, WMJJWM - Kakonko

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, amewataka wananchi wa Wilaya ya Kakonko mkoani Kigoma kuendelea kushirikiana na Maafisa Maendeleo ya Jamii, kusimamia na kuendeleza miradi ya kiuchumi inayotekelezwa katika maeneo yao ili kuongeza kipato, kuinua ustawi wa familia na maendeleo ya jamii kwa ujumla.

Mahundi metoa rai hiyo Julai 15, 2026, wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli mbalimbali za maendeleo wilayani humo, ikiwemo shughuli za Kikundi cha Wanawake Ubihumwe Kata ya Gwarama, kikundi cha vijana Tuinuane na Shule ya Msingi Itumbike yenye kitengo cha watoto wenye mahitaji maalum.

Amekutana pia na kikundi cha watu wenye ulemavu Kakonko pamoja na kuzindua jengo la kivuli cha Soko la Kijiji cha Kanyonza.

Amesema, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuweka mazingira wezeshi kwa makundi mbalimbali ya wananchi kupitia mikopo, mafunzo na miradi ya maendeleo, hivyo ni wajibu wa wananchi kuitunza na kuisimamia miradi hiyo ili iwe na tija ya kudumu kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

Aidha, amewataka wazazi na walezi kutimiza wajibu wao wa malezi kwa kuwajenga watoto katika maadili mema na kuhakikisha wanakuwa mstari wa mbele kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia vinavyoathiri watoto na wanawake katika jamii.

"Tupige kelele kukataa ukatili wa kijinsia na tuwalinde watoto wetu ili wakue katika mazingira salama yatakayowafanya kuwa raia wema na wenye mchango kwa Taifa," alisema Naibu Waziri Mahundi.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Kakonko, Mbunge wa Jimbo hilo, Mhe. Allan Mvano amesema ataendelea kuwa sauti ya wananchi wake kwa kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuhakikisha ahadi alizozitoa kwa wananchi zinaendelea kutekelezwa kwa kushirikiana na Serikali, wadau wa maendeleo na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, kuhakikisha kunapatikana matunda katika sekta mbalimbali ya elimu, uwezeshaji wa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu pamoja na kuboresha miundombinu ya huduma za kijamii.








Share:

MRADI WA BARABARA YA LUTUKIRA-SONGEA WABUNGE WATAKA HAKI NA USALAMA KWA WAFANYAKAZI

barabara ya Lutukira-Songea yenye urefu wa kilomita 100 pamoja na barabara ya mchepuko yenye kilomita 16 iliyotembelewa na wabunge wa mkoa wa Ruvuma yenye thamani ya shilingi bilioni 150
Meneja wa TANROADS mkoa wa Ruvuma mhandisi Saleh Juma wa kwanza kutoka kulia akiwa na wabunge wa mkoa wa Ruvuma walipotembelea na kukagua maendeleo ya mradi huo wa barabara ya Songea-lutukira yenye kilomita 100 na barabara ya mchepuko yenye kilomita 16

Na Regina Ndumbaro Songea-Ruvuma.

Wabunge wa mkoa wa Ruvuma wamezitaka taasisi zinazosimamia ujenzi wa barabara ya Lutukira–Songea yenye urefu wa kilomita 100 pamoja na barabara ya mchepuko ya kilomita 16, kuhakikisha haki za wafanyakazi zinalindwa kwa kuzingatia sheria, kanuni na miongozo ya kazi.

Share:

Wednesday, 15 July 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI JULAI 16, 2026

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger