Tuesday, 26 May 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE MEI 26,2026


Magazeti





Share:

Monday, 25 May 2026

FOUNTAIN GATE FC YAJIANDAA KWA VITA YA MECHI ZA MWISHO LIGI KUU

Na Bora Mustafa, Arusha.

Kocha Mkuu wa Fountain Gate FC, Felix Minziro amesema licha ya timu yake kukabiliwa na changamoto ya kikosi kuwa kipana, muda wa mapumziko walioupata umeisaidia timu kujiandaa vyema kuelekea michezo iliyosalia ya Ligi Kuu. 

Amesema miongoni mwa michezo hiyo ipo dhidi ya vigogo kama Azam FC pamoja na Young Africans SC katika mechi tano za mwisho wa msimu.

Akizungumza Minziro amesema hayo Leo 25, mei, ,2025  jijini Arusha ambapo timu hiyo imeweka kambi maalum kwa ajili ya kuimarisha utimamu wa mwili na akili kwa wachezaji wake baada ya ratiba ngumu ya michezo ya mfululizo..

 Pia amesema mapumziko ya wiki moja yaliyopatikana yamekuwa msaada mkubwa kwa wachezaji kurejea kwenye kiwango kizuri kabla ya kuendelea na mechi zilizobaki.

Hata hivyo, Minziro amebainisha kuwa changamoto kubwa waliokuwa nayo si majeraha makubwa bali ni uchovu pamoja na majeraha madogomadogo yaliyotokana na ushindani wa ligi hiyo.

 Ameongeza kuwa mazingira mazuri ya mazoezi yanaendelea kuwasaidia wachezaji kurejea kwenye ubora wao kwa haraka.

Aidha, amesema benchi la ufundi linaendelea kufuatilia maendeleo ya kila mchezaji kwa karibu ili kuhakikisha timu inaingia kwenye michezo iliyobaki ikiwa kwenye hali bora zaidi.

 Kwa upande wake, Meneja wa Fountain Gate FC, Zamkufo Elias amesema timu hiyo bado inaendelea kufanya tathmini ya michezo iliyopita kwa lengo la kurekebisha makosa yaliyojitokeza kabla ya mechi zijazo.

Zamkufo amesema ushindani wa ligi kwa sasa ni mkubwa kutokana na baadhi ya timu kupigania ubingwa huku nyingine zikisaka nafasi ya kubaki salama kwenye ligi, hali inayofanya kila mchezo kuwa na ushindani mkubwa zaidi.


Kwa upande wake, mchezaji wa Fountain Gate FC, Shomari Mponzi amesema wachezaji wameendelea kushirikiana kwa karibu kuhakikisha timu inapata matokeo mazuri katika michezo iliyobaki ya ligi. Pia amewataka mashabiki kuendelea kuiunga mkono timu hiyo katika kipindi hiki muhimu huku akisisitiza kuwa kila mchezaji anaendelea kutekeleza majukumu yake kwa nidhamu na kujituma kwa ajili ya mafanikio ya klabu hiyo.

Share:

MADINI YABADILISHA MAISHA RUANGWA, WACHIMBAJI WATOKA ‘BUKU BUKU’ HADI MIRADI YA MAENDELEO


📍LINDI

Wilaya  ya Ruangwa mkoani Lindi imeendelea kushuhudia mageuzi makubwa ya kiuchumi na kijamii kufuatia kuongezeka kwa shughuli za uchimbaji madini katika Mgodi wa Namungo unaomilikiwa na kampuni ya Elianje Limited, huku wachimbaji wadogo na wananchi wa maeneo yanayouzunguka mgodi huo wakinufaika kupitia ajira, biashara na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Ukuaji wa shughuli za uchimbaji katika mgodi huo umechangia kuboresha huduma za maji, elimu, afya na miundombinu, hali iliyobadili maisha ya wananchi ambao miaka michache iliyopita walikabiliwa na changamoto kubwa za kiuchumi na kijamii.

Akizungumza kwa niaba ya Afisa Madini Mkazi wa Lindi, Mhandisi Dickson Joram amesema hali ya wachimbaji na wananchi wa Namungo imebadilika kwa kiwango kikubwa ikilinganishwa na mwaka 2019 alipowasili katika eneo hilo.

Amesema wakati huo shughuli za uchimbaji zilikuwa katika kiwango cha chini, huku wachimbaji wengi wakitumia njia duni za uzalishaji na kushindwa kumudu mahitaji muhimu ya kila siku.

“Wachimbaji wengi walikuwa wanapitia kipindi kigumu sana. Ulipowatembelea ilibidi wakati mwingine uwaachie fedha za chakula au kuwasaidia mahitaji muhimu. Lakini leo Namungo imebadilika kwa kiasi kikubwa; wananchi wanajitegemea na wanaendesha shughuli kubwa kupitia sekta ya madini,” amesema.

Kwa upande wake, Afisa Uhusiano wa kampuni ya Elianje Limited, Joseph Shayo amesema kampuni hiyo ilianza shughuli za utafiti na uchimbaji mwaka 2020 na tangu wakati huo imekuwa ikihakikisha jamii inayouzunguka mgodi inanufaika moja kwa moja kupitia utekelezaji wa miradi ya kijamii.

Amesema kampuni imefanikiwa kuchimba visima na kusambaza maji katika Kijiji cha Tongwe na Kitongoji cha Namungo, huku maboresho ya huduma hiyo yakiendelea katika maeneo yenye changamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama.

Mbali na huduma ya maji, amesema kampuni imejenga shule ya awali, kuboresha madarasa, kujenga vyoo vya kisasa pamoja na kushiriki katika ujenzi wa shule ya msingi katika Kitongoji cha Namungo ili kupunguza adha ya watoto kutembea umbali mrefu kufuata huduma za elimu.

Shayo amesema mgodi huo pia umechangia uboreshaji wa barabara zinazounganisha vijiji na kata jirani sambamba na kusaidia shule mbalimbali kwa kutoa vifaa vya elimu ikiwemo kompyuta na mashine za uchapishaji.

Naye Mwenyekiti wa Kijiji cha Chingumbwa, Kata ya Mbekenyela wilayani Ruangwa, Abdallah Manjakali amesema uwepo wa mgodi huo umefungua fursa nyingi za ajira, biashara na huduma za kijamii ambazo hapo awali zilikuwa changamoto kubwa kwa wananchi.

“Leo wananchi wengi wanapata kipato na maisha yameimarika. Pia kampuni imenunua gari la wagonjwa linalowahudumia wananchi bure wakati wa dharura bila kuchangishwa fedha yoyote,” amesema.

Manjakali ameongeza kuwa ushirikiano uliopo kati ya mgodi na vijiji vinavyouzunguka unapaswa kuwa mfano kwa wawekezaji wengine wa sekta ya madini, huku akizitaka kampuni zenye leseni ambazo bado hazijaanza uzalishaji kuharakisha uwekezaji ili wananchi waweze kunufaika na rasilimali zilizopo katika maeneo yao.














Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU MEI 25,2026



Magazeti




Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger