Friday, 26 June 2026

VIONGOZI WAJENGEWA UWEZO KUHUSU MRADI WA INUA II IRINGA


WATENDAJI wa vijiji, viongozi wa serikali za mitaa na wadau mbalimbali wa maendeleo mkoani Iringa wamepatiwa mafunzo na uelewa kuhusu utekelezaji wa Mradi wa INUA II unaotekelezwa na Hand in Hand Eastern Africa Tanzania (HIHEA), wenye lengo la kuimarisha uchumi wa wananchi kupitia shughuli za uzalishaji na biashara.

Akizungumza katika semina hiyo, Mkurugenzi wa HIHEA, Jane Richard Sabuni, alisema taasisi hiyo imefungua rasmi ofisi yake mkoani Iringa na kuanza utekelezaji wa mradi huo unaolenga kuwawezesha wananchi kujiongezea kipato kupitia vikundi vya ujasiriamali na biashara mbalimbali.

Alisema Hand in Hand imejikita katika kusaidia wananchi kuanzisha na kukuza biashara halali zitakazochangia kuimarisha uchumi wa kaya na kuboresha maisha ya familia. Aidha, alieleza kuwa taasisi hiyo tayari imewafikia zaidi ya wananchi 87,000, kusaidia kuanzishwa kwa biashara zaidi ya 50,000, kupitia vikundi zaidi ya 4,000 vya kiuchumi vilivyoundwa na kuimarishwa, na kuchangia kuzalishwa kwa ajira zaidi ya 74,000 nchini.

Sabuni alisema semina hiyo imelenga kuwajengea uwezo viongozi wa serikali za vijiji na kata ili waweze kuelewa malengo ya mradi na kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wake, huku akisisitiza kuwa ushirikiano wa viongozi wa serikali za mitaa ni muhimu katika kuhakikisha Mradi wa INUA II unafanikisha malengo yake ya kuimarisha uchumi wa wananchi.

Aidha, alieleza kuwa Hand in Hand imefungua rasmi ofisi yake mkoani Iringa Juni 24, 2026, hatua inayofanya taasisi hiyo kuwa na matawi katika mikoa saba nchini Tanzania, ikiwemo Arusha (makao makuu), Kilimanjaro, Manyara, Singida, Dodoma na Simiyu.

Share:

KUELEKEA TUZO ZA RAIS KWA WALIPAKODI, TRA KARIAKOO YAWAPONGEZA WALIPAKODI


Kariakoo, 25 Juni, 2026

Kuelekea maadhimisho ya Tuzo za Rais kwa Walipakodi Bora, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kariakoo imewapongeza walipakodi kwa mchango wao mkubwa katika ulipaji wa kodi na uzingatiaji wa sheria za kodi, hali iliyowezesha baadhi yao kutambuliwa kama walipakodi bora wa mwaka.

Akizungumza alipotembelea walipakodi meneja wa uzingatiaji wa sheria na ufuatiliaji Bw. Lihami Haule aliwashukuru walipakodi kwa kuendelea kutimiza wajibu wao kwa uaminifu na kuwataka kuendeleza utamaduni huo ili kuchangia maendeleo ya taifa na kukuza uchumi.

Nae, Meneja wa kituo cha TRA Gerezani Bi. Mercy Sijaona aliwakaribisha walipakodi kushiriki katika mbio za burudani (Fun Run) zitakazofanyika Gymkhana tarehe 27 Juni 2026 saa 12: 00 asubuhi.

Kwa upande wao, walipakodi walieleza kufurahishwa na huduma zinazotolewa na TRA, hususani utoaji wa elimu ya kodi na mwitikio wa maafisa wa mamlaka katika kutatua changamoto mbalimbali.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA JUNI 26, 2026


Magazetini Leo


Share:

Thursday, 25 June 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI JUNI 25,2026

Magazeti


 



Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger