Wednesday 17 April 2024

SERIKALI YABAINISHA MPANGO WA KUWASAIDIA WAJASIRIAMALI KUZALISHA BIDHAA BORA


NAIBU Waziri wa Viwanda na Biasha, Exaud Kigahe amebainisha mpango wa Serikali katika kuwasaidia wajasiriamali kuzalisha bidhaa bora ili kupata masoko ya uhakika.

Akijibu swali la msingi la Mbunge wa Viti Maalum, Ester Malleko ambaye alitaka kujua mpango wa Serikali wa kuwasaidia wajasiriamali kuzalisha bidhaa bora na kupata masoko ya uhakika.

Akijibu swalin hilo, Kigahe alisema Serikali imeweka mipango kadhaa ya kuwasaidia wajasiriamali kuzalisha bidhaa bora ili kupata masoko ya uhakika ikiwa ni pamoja na kupitia Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) na Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kuwasaidia wajasiriamali wadogo kupata maeneo/majengo ya kuzalishia bidhaa zao, kuwapatia mitaji kupita Mfuko wa NEDF na nembo ya ubora wa bidhaa zao kwa miaka mitatu bila gharama.

Amesema pia kupitia SIDO, TBS na Wakala wa Vipimo (WMA) kuendelea kutoa mafunzo kwa wajasiriamali kuhusu kanuni za uzalishaji wenye tija, elimu ya utambuzi wa vifungashio na ufungashaji bora.

Pia amesema SIDO kwa kushirikiana na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE) kuendelea kuandaa na kuratibu maonesho mbalimbali ndani na nje ya nchi ikiwa ni sehemu ya kuchagiza ukuaji wa soko la bidhaa zinazozalishwa na Wajasiriamali.

Katika swali la nyongeza, Malleko alitaka kujua mpango wa serikali wa kufanya mapitia ya sera ya biashara na sera ya wajasilimali wadogo wadogo ambazo zimepitwa na wakati.

Pia alitaka mkakati wa Serikali wa kuhakikisha wajasiriamali wanazalisha bidhaa zenye ubora.

Akijibu maswali hayo, Kigahe amesema ni kweli sera hizo zimepitwa na wakati na kuwa Serikali imeshaanza taratibu za mapitio ili ziweze kuendena na hali ya soko la ndani na nje na mahitaji ya sasa ya wajasiliamali.

Alisema pia Serikali imepanga kuweka mazingira mazuri kwa wajasiriamali ili kuweza kuzalisha bidhaa bora na zenye viwango bora.

Kwa upande wa Mbunge wa Viti Maalum, Sophia mwakagenda alitaka kujua mkakati wa Serikali wa kuiwezesha SIDO ili kuweza kuwasaidia wajasiriamali wengi zaidi.

Akijibu wali hilo, Kigahe alisema SIDO imekuwa na uwezo mdogo wa kuwezesha mitaji kwa wajasiriamali ambao wamekuwa wakiongezeka kila wakati.

Amesema Serikali imeacha mchakato wa kuibadili sheria iliyoanzisha SIDO ili kuondoka kuwa taasisi ya uwezeshaji bali iweze kujiendesha kibiasharamae, sheria baada ya kuhudumia ianze kujiendesha kibiashara na kukidhi mahitaji ya wajasiliamali.

Share:

POLISI SHINYANGA WAKAMATA SIMU ZA WIZI, MAFUTA YA DIZELI, MATAIRI YA GARI

Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga limekamata mafuta ya dizeli lita 320, vipande 250 vya nondo,  Simu za wizi, Nyaya na matairi ya gari baada ya kufanya doria, misako na Operesheni mbalimbali.

Akizungumza na Waandishi wa habari leo Aprili 17,2024 Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Kennedy Mgani amesema Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga linaendelea kuimarisha ulinzi na usalama kwa kushirikiana na Jamii katika kubaini, kuzuia na kutanzua uhalifu kwa kufanya doria, misako pamoja na operesheni mbalimbali katika kipindi cha wiki tatu kuanzia Machi 28, 2024 mpaka Aprili 16, 2024.

"Katika kipindi hicho, Jeshi la Polisi limefanikiwa kukamata mafuta ya dizeli lita 320, Vipande 250 vya nondo, Nyaya mbalimbali, matairi 05 ya gari, Injini 01 ya Pikipiki, Betri 06 za gari, Mashine 01 ya kukatia miti (chain saw), mitambo 04 ya kutengeneza pombe ya moshi (gongo), pombe ya moshi lita 13, bhangi kete 33, Simu 05, Pikipiki 04, Mashine 01 ya bonanza, Redio 02, mtungi 01 wa gas, TV 01 pamoja na vifaa mbalimbali vya kupigia ramli chonganishi", amesema Kaimu Kamanda Mgani.

"Jumla ya kesi 09 zimepata mafanikio ambapo kesi 01 ya kubaka ambapo mshtakiwa alihukumiwa kifungo cha miaka 30 jela, kesi 02 kupatikana na bhangi washtakiwa 02 walihukumiwa kifungo cha miaka miwili mpaka mitatu jela, kesi 01 kuvunja nyumba usiku na kuiba mshtakiwa 01 alihukumiwa kifungo cha miaka miwili jela, kesi 01 kuharibu mali mshtakiwa alihukumiwa kifungo cha mwaka 01 jela, kesi 03 za wizi washtakiwa 03 walihukumiwa kifungo cha miezi06 jela na kesi 01 kuingia kwa jinai mshtakiwa alihukumiwa kifungo cha miezi 04 jela",ameongeza.


Katika hatua nyingine amesema Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga kikosi cha Usalama barabarani limefanikiwa kukamata jumla ya makosa 3,771 ambapo makosa ya magari ni 2,836 na makosa ya bajaji na pikipiki ni 935 wahusika waliwajibishwa kwa kulipa faini za papo kwa hapo.

"Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga linawashukuru Wananchi kwa kuendelea kutoa ushirikiano katika kuhakikisha Usalama wa Mkoa wa Shinyanga unakuwa shwari, Pia linatoa wito kwa wananchi wote kuendelea kutii na kufuata sheria na halitasita kumchukulia hatua mtu yeyote atakayekiuka sheria za nchi",amesema.


Share:

Tuesday 16 April 2024

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO APRILI 17, 2024

           
Share:

Monday 15 April 2024

UWT IBADAKULI WAFANYA KONGAMANO LA MIAKA MITATU YA RAIS SAMIA MADARAKANI NA KUMPONGEZA KUFANYA KAZI KUBWA YA KUWALETEA MAENDELEO WATANZANIA

 


Na Marco Maduhu,SHINYANGA

UMOJA wa Wanawake Tanzania (UWT) Kata ya Ibadakuli Manispaa ya Shinyanga umefanya Kongamano la Miaka Mitatu ya Rais Samia Suluhu Hassan Madarakani, kwa kumpongeza kutokana na kazi kubwa ambayo ameifanya ya kuwaletea Maendeleo Watanzania.

Kongamano hilo limefanyika leo Aprili 13, 2024 katika Viwanja vya Shule ya Msingi Viwandani, ambalo lilitanguliwa na Maandamano,huku Mgeni Rasmi akiwa ni Katibu Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga Rejina Ndulu, akimwakilisha Katibu wa CCM wa Mkoa huo Odilia Batimayo,Kongamano lililoandaliwa na Diwani wa Vitimaalum Tarafa ya Ibadakuli Mhe. Zuhura Waziri.
Ndulu akizungumza kwenye Kongamano hilo la UWT Tarafa ya Ibadakuli, amesema wanawake wanampongeza Rais Samia kwa kuwaheshimisha, kutokana na kazi kubwa ambayo ameifanya ya kuwatumikia Watanzania ndani ya Miaka Mitatu na kuwaletea Maendeleo.

Amesema Rais Samia aliichukua nchi kwenye kipindi kigumu cha kuondokewa na Hayati Rais John Magufuli, huku baadhi ya wananchi wakishindwa kumwamini kama ataweza kuongoza Nchi, lakini ndani ya miaka mitatu amewafuta machozi Watanzania na kuwaletea mapinduzi makubwa ya kimaendeleo, na kuonyesha kwamba wanawake wanaweza kushika nyazifa kubwa za uongozi.
“Ndani ya miaka mitatu Rais Samia ameleta mapinduzi makubwa ya kimaendeleo katika Sekta mbalimbali ikiwamo ya Afya, Elimu, Nishati na sasa hivi kuna Umeme kila kona hadi vijijini, Barabara zimejengwa, Maji yametapakaa kila mahali na kumtua ndoo kichwani Mwanamke,” amesema Ndulu.

Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Shinyanga Mjini Rehema Nhamanilo,amewataka wanawake kote nchini kwamba zawadi kubwa ambayo watampatia Rais Samia ni kumpigia kura nyingi za ushindi 2025, pamoja na kuwapigia kura wagombea wote wa CCM kuanzia uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu hadi uchaguzi Mkuu mwakani.
Naye Diwani wa Vitimaalum Tarafa ya Ibadakuli Zuhura Waziri, amesema ameandaa Kongamano hilo la kumpongeza Rais Samia kwa kushirikiana na viongozi wa UWT Kata ya Ibadakuli, kutokana na kazi kubwa ambayo wameifanya ya kuwaletea Maendeleo Watanzania ikiwamo Kata hiyo ya Ibadakuli.

Amesema hawana budi kumpongeza Mwanamke mwezao ambaye amekuwa chachu ya wanawake wengi kuaminiwa na kupata nafasi mbalimbali za uongozi na kufanya mambo makubwa, huku wakimwahidi kwamba katika Tarafa hiyo ya Ibadakuli wagombea wote wa CCM katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa watapata ushindi mkubwa, pamoja na uchaguzi Mkuu mwakani.
Aidha, amewataka pia wanawake wenye sifa za uongozi kwamba wajitokeze kuchukua fomu za kugombea nafasi za uongozi kwenye uchaguzi wa Serikali mwaka huu,ili washike nyazifa hizo na kuingia kwenye vikao vya maamuzi pamoja na kuwaletea maendeleo wananchi.

Katika hatua nyingine Zuhura amewataka wanawake waendelee kupendana na pale wanapokwaruzana wasameheane, huku akiwakumbusha pia wasisahau malezi bora ya wototo wao wa jinsi zote wa kike na wakiume, pamoja na kuwapatia elimu kwa sawa.

TAZAMA PICHA HAPA CHINI👇👇
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga Rejina Ndulu akizungumza kwenye Kongamano hilo la kumpongeza Rais Samia kufikisha miaka mitatu Madarakani na kuwaletea Maendeleo Watanzania.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga Rejina Ndulu akiendelea kuzungumza kwenye Kongamano hilo la kumpongeza Rais Samia kufikisha miaka mitatu Madarakani na kuwaletea Maendeleo Watanzania.
Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Shinyanga Mjini Rehema Nhamanilo akizungumza kwenye Kongamano hilo.
Katibu wa UWT Wilaya ya Shinyanga Mjini Sharifa Mdee akizungumza kwenye Kongamano hilo.
Mwenyekiti wa UWT Kata ya Ibadakuli Ester Komba akizungumza kwenye Kongamano hilo.
Mwenyekiti wa UWT Kata ya Kolandoto Zinila Kalwani akizungumza kwenye Kongamano hilo.
Diwani wa Kitangili Mariamu Nyangaka akizungumza kwenye Kongamano hilo.
Diwani wa Vitimaalum Tarafa ya Ibadakuli Zuhura Waziri akizungumza kwenye Kongamano hilo.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga Rejina Ndulu, akimpongeza Diwani wa Tarafa ya Ibadakuli Zuhura Waziri kutokana na kuandaa Kongamano hilo la kumpongeza Rais Samia pamoja na ujumbe Mzuri alioutoa.
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye Kongamano hilo.
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye Kongamano hilo.
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye Kongamano hilo.
Kongamano likiendelea.
Kongamano likiendelea.
Kongamano likiendelea.
Wanawake wakiendelea na Kongamano.
Kongamano la kumpongeza Rais Samia likiendelea.
Kongamano la kumpongeza Rais Samia likiendelea.
Kongamano la kumpongeza Rais Samia likiendelea.
Kongamano la kumpongeza Rais Samia likiendelea.
Kongamano la kumpongeza Rais Samia likiendelea.
Kongamano la kumpongeza Rais Samia likiendelea.
Kongamano la kumpongeza Rais Samia likiendelea.
Kongamano la kumpongeza Rais Samia likiendelea.
Awali Mgeni Rasmi Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga Rejina Ndulu akiwasili kwenye Kongamano hilo.
Wanawake wakiwa katika Maandamano kuelekea kwenye Kongamano la kumpongeza Rais Samia.
Wanawake wakiwa katika Maandamano kuelekea kwenye Kongamano la kumpongeza Rais Samia.
Wanawake wakiwa katika Maandamano kuelekea kwenye Kongamano la kumpongeza Rais Samia.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger