Monday 4 March 2024

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE MACHI 5,2024


Share:

Ngoma Mpya: SUPER BOLAN - MAJUNGU

Share:

Benki ya CRDB Kanda ya Ziwa yazindua kampeni ya 'SimBanking Transact By Finger'

Benki ya CRDB Kanda ya Ziwa imezindua kampeni ya 'SimBanking Transact By Finger' inayolenga kuhamasisha wafanyakazi wa benki hiyo kuwaunganisha wateja na kuwaelimisha ili kutumia huduma ya SimBanking.

Uzinduzi huo umefanyika Jumatatu Machi 04, 2024 katika tawi la CRDB Nyanza jijini Mwanza ambapo katika kampeni hiyo, wafanyakazi watakaowaunganisha wateja wengi zaidi na huduma ya SimBanking watajishindia zawadi mbalimbali.

"Kupitia SimBanking, mteja anaweza kufanya mihamala hadi millioni 20 kwa siku, tukiwaelekeza namna ya kutumia huduma hiyo, tutapunguza msongamano kwenye matawi yetu" amesema Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta.

Naye Kiongozi wa kampeni hiyo, May Mosi Ndunguru amewahamasisha wafanyakazi wa benki ya CRDB kuhamasisha wateja wengi kutumia SimBanking kwani inarahisisha upatikanaji wa huduma huku wote, wateja na wafanyakazi wakijishindia zawadi kutoka CRDB.
Kampeni hiyo itadumu kwa muda wa miezi mitatu kuanzia Machi 04, 2024.
Na George Binagi- GB Pazzo, BMG
Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta (katikati) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa kampeni ya 'SimBanking Transact By Finger' inayolenga kuhamasisha wafanyakazi wa benki hiyo kuwaunganisha na kuwaelimisha wateja kutumia huduma ya SimBaking huku wakijishindia zawadi mbalimbali.
Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta akizungumza kwenye uzinduzi wa kampeni ya 'SimBanking Transact By Finger'.
Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta akizungumza kwenye uzinduzi wa kampeni ya 'SimBanking Transact By Finger'.
Kiongozi wa kampeni ya 'SimBanking Transact By Finger' kutoka benki ya CRDB, May Mosi Ndunguru akihamasisha wafanyakazi wa benki hiyo kuongeza idadi ya watumiaji wa huduma ya SimBanking ili kujishindia zawadi.
Keki kwa ajili ya uzinduzi wa huduma ya 'SimBanking Transact By Finger' jijini Mwanza.
Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta akikata keki kwenye uzinduzi wa kampeni ya 'SimBanking Transact by Finger' Kanda ya Ziwa.
Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta akiwalisha keki wafanyakazi wa benki hiyo.
Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta akiwalisha keki wafanyakazi wa benki hiyo.
Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta akiwalisha keki wafanyakazi wa benki hiyo.
Meneja wa CRDB Tawi la Nyanza, Eugenius Mashishanga (kulia) akimlisha keki Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta (kushoto).
Meneja wa CRDB Tawi la Nyanza, Eugenius Mashishanga (kulia) akimlisha keki Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta (kushoto).
Meneja wa CRDB Tawi la Nyanza, Eugenius Mashishanga (kulia) na Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta (kushoto) wakifurahia baada ya uzinduzi wa kampeni ya SimBanking Transact By Finger jijini Mwanza.
Meneja wa CRDB Kanda ya Ziwa, Lusingi Sitta na wafanyakazi wa benki hiyo wakigonga 'cheers' wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo.
Wafanyakazi wa CRDB wakifuatilia uzinduzi wa kampeni ya SimBanking Transact By Finger inayolenga kuhamasisha wafanyakazi kuwaunganisha wateja na huduma ya SimBanking.
Zawadi mbalimbali zitakazotolewa kwa wafanyakazi wa CRDB watakaowaunganisha wateja wengi na huduma ya CRDB.
Kiongozi wa kampeni ya 'SimBanking Transact By Finger' kutoka benki ya CRDB, May Mosi Ndunguru akionyesha zawadi mbalimbali zitakazotolewa kwa wafanyakazi.
Kiongozi wa kampeni ya 'SimBanking Transact By Finger' kutoka benki ya CRDB, May Mosi Ndunguru akionyesha zawadi mbalimbali zitakazotolewa kwa wafanyakazi.
Kampeni ya 'SimBanking Transact By Finger' itadumu kwa muda wa miezi mitatu kuanzia Machi 04, 2024.
Share:

ELIMU YA HUDUMA YA KWANZA YAWAKOSHA MADEREVA BODABODA JIJINI TANGA, AMEND WATOA NENO




Na Mwandishi Wetu,Tanga

UBALOZI wa Uswisi kupitia ufadhili walioufanya kwa taasisi isiyo ya kierikali ya AMEND kwa ajili ya kutoa elimu ya usalama barabarani ikiwemo elimu ya huduma ya kwanza kwa madereva bodaboda, umewasaidia madereva hao kuwa na uwezo wa kutoa msaada pindi ajali zinapotokea.

Wakizungumza na wandishi wa habari Jijini Tanga baada ya kupewa elimu ya usalama barabarani na taasisi ya AMEND madereva wa kituo cha Mikanjuni hospitali Ally Zuberi na Faky Hamis wamesema ukosefu wa elimu umekuwa chanzo kikubwa cha ajali za barabarani kwa madereva wengi wa bodaboda.

Hivyo wameeleza kwamba elimu waliyoipata kuhusu usalama barabarani itawasaidia kuendesha kwa tahadhari pindi wanapokuwa barabarani na hivyo kuepusha ajali ambazo zimekuwa zikisababisha video na ulemavu wa kudumu.

Akieleza zaidi Mwenyekiti wa Bodaboda Kituo cha Mikanjuni Hospitali Mwin'dadi amesema kutozitambua sheria na alama za barabarani imekua ndio sababu ya ajali ya nyingi kutokea huku akibainisha elimu waliyoipata itawasaidia kujiepusha dhidi ya ajali.

Wakizungumzia kuhusu elimu ya huduma kwanza madereva hao wamesema watakuwa mstari wa mbele kutoa msaada pale ajali itakapotokea ambapo wameendelea kusema kuwa elimu hiyo watawashirikisha na madereva wenzao ili kushiriki katika utoaji wa huduma.

Kwa upande wake Benilda Mtumbuka ambaye ni Ofisa Maendeleo ya Jamii kata ya Magaoni ametoa shukrani kwa Ubalozi wa Uswisi na taasisi ya AMEND kutokana na elimu ya usalama barabarani kwa madereva bodaboda.

Ametoa mwito kwa bodaboda waliopata elimu kuitumia vyema jambo litakalosaidia kupunguza ajali huku akiwata AMEND kuendelea kutoa elimu hiyo kwa madereva wengine.

Wakati huo huo Ofisa Miradi wa AMEND Ramadhani Nyanza amesema elimu ya huduma ya kwanza waliyoitoa kwa madereva bodaboda imeleta mwanga kwa madereva hao kwa kujua namna bora ya kutoa msaada pale kunapotokea ajali.

Nyanza amesema mpaka sasa madereva bodaboda takribani 126 katika Jiji la Tanga wamefikiwa kwa kupatiwa elimu ambapo amebainisha malengo ni kuwafikia madereva 500 kwa mkoa Tanga.

Share:

Sunday 3 March 2024

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU MACHI 4, 2024


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger