Monday 26 February 2024

TANAPA SIMAMIENI SHERIA KAMA ZILIVYOPITISHWA NA BUNGE MAJALIWA


Na. Richard Mrusha Katavi

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (Mb) amewataka Makamanda wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kuratibu maeneo yao vizuri na kusimamia sheria za uhifadhi kama zilivyopitishwa na Bunge ili maliasilia zilizomo ziendelee kuleta tija kwa taifa.

Ameyasema hayo jana Februari 25.02.2024 aliposimama kuwasalimia wananchi wa kijiji cha Sitalike akiwa katika safari ya kikazi kuelekea kijiji cha Mpimbwe kilichopo Jimbo la Kavuu Mkoani Katavi.

Akiwa amesimama kusikiliza kero katika kijiji hicho cha Sitalike kilichopo mpakani mwa Hifadhi ya Taifa Katavi, wananchi walimuomba aseme neno ili wapate fursa ya kuvua samaki mto Katuma ambao unategemewa kwa zaidi ya asilimia 80 kiikolojia na uhai wa wanyama kama vile viboko na Mamba ambao maisha yao yote hutegemea maji ya mto huo.

Baada ya kusikiliza maombi hayo mhe. Majaliwa alisema, "Niwashukuru Makamanda wa TANAPA kwa kufanya maboresho katika eneo la mto Katuma, endeleeni kuratibu vizuri maeneo yenu na yale tuliyoyaweka kwenye sheria zetu yatekelezeni lakini pia fursa za wananchi nazo zipate nafasi ila si kwa kuingia katika maeneo yaliyohifadhiwa."

Wakati wote TANAPA kutaneni na wananchi, sikilizeni matamanio yao, waelimisheni juu ya namna watakavyonufaika na uhifadhi lakini pia waambieni na sheria zilizopo zifuatwe ili kuepusha misuguano."

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Nsimbo (CCM) Mhe. Annah Lupembe alisema kuwa suala la wananchi kuvua samaki mto Katuma lililoibuliwa hapa leo lilishapatiwa majibu katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini Sitalike - Katavi siku chache zilizopita ukiwahusisha wananchi wa Kata ya Sitalike, TANAPA na Mbunge. Ambapo TANAPA kwa kushirikiana na mbunge husika walikubaliana kuchukua hoja hiyo na kuiwasilisha ngazi za Wizara kwa hatua zaidi.

Naye, Naibu Kamishna wa Uhifadhi na Maendeleo ya Biashara - TANAPA Herman Batiho akiambatana na Kamanda wa Uhifadhi Kanda ya Kusini Steria Ndaga alisema, "Licha ya suala hili kushughulikiwa na mamlaka za juu tambueni kuwa, mto huu una mamba na viboko wengi, hivyo kuvua samaki eneo lenye wanyama wengi kiasi hicho ni kuhatarisha maisha yao aidha, kuna wanyama kama mamba na baadhi ya ndege hutegemea samaki hao. Pia kuna wavuvi wengine hutumia sumu na tumeshawakamata majangili wa hivyo. Sumu hii imekuwa na madhara makubwa kwa watumiaji wa samaki hao, viumbe vingine vinavyoishi majini na kwa wanyama wanaokunywa maji hayo".

Kamishna Batiho pia aliwataka wakazi wa Kata ya Sitalike na vijiji vinavyozunguka hifadhi ya Taifa Katavi kuachana na uvuvi wa kutegemea mto badala yake wachimbe mabwawa ya kufugia samaki TANAPA itashirikiana nao kwa kuwaletea wataalam watakaowafundisha namna bora ya kuchimba na kupata mbegu ya vifaranga.

Ikumbukwe kuwa Oktoba 10, 2019 aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt. John Pombe Magufuli alipotembelea hifadhi hiyo aliiagiza TANAPA kuchimba mabwawa kunusuru uhai wa Viboko kutokana na kukauka kwa mto Katuma kulikosababishwa na matumizi yasiyoendelevu ya rasilimali maji. Hivyo kuruhusu matumizi holela ya mto huo yanaweza kuturudisha tena katika kadhia ya mwaka 2019.
Share:

RC GEITA AWAFUNDA WAHITIMU WAPYA WALIOJIUNGA GGML

Mkuu wa mkoa wa Geita, Martine Shigela akizungumza katika hafla ya kuwakaribisha wahitimu 40 wa vyuo mbalimbali wasio na ajira ambao wamepatiwa fursa ndani ya GGML kupata mafunzo tarajali kwa muda wa mwaka mmoja sambamba na wahitimu 10 wa mafunzo huo kwa mwaka jana ambao wamepata ajira ya kudumu ndani ya kampuni hiyo.
Mkuu wa mkoa wa Geita, Martine Shigela akisalimiana na akamu Rais Mwandamizi - Kitengo cha masuala ya Ubia/ushirika Afrika kutoka AngloGold Ashanti - GGML, Terry Strong na Meneja Mwandamizi wa masuala ya Rasilimali watu kutoka GGML, Charles Masubi.



NA MWANDISHI WETU

MKUU wa Mkoa wa Geita, Martine Shigela ametoa wito kwa wahitimu wa vyuo vikuu waliojiunga na program ya mafunzo tarajali katika Kampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML), kujituma kwa bidii, kuwa wabunifu na nidhamu.



Pia ametoa wito kwa wahitimu hao, kutumia fursa zinazopatikana ndani na nje ya mgodi huo ili kujiendeleza na kuondoka wakiwa tofauti na namna walivyoingia kwenye program hiyo ya mwaka mmoja.



Shigela ametoa wito huo hivi karibuni mjini Geita katika hafla ya kuwakaribisha wahitimu 40 wa vyuo vikuu ambao wamejiunga na GGML kwa mwaka 2024/2025 kupata mafunzo tarajali sambamba na wahitimu wengine 10 wa program hiyo kwa mwaka jana ambao wameendelea na mafunzo ya juu zaidi baada ya kupata ajira ya kudumu ndani ya GGML.

 

Wanafunzi hao 10 waliomaliza program mwaka jana, wamechaguliwa kuendelea na program mpya inayofahamika kwa jina la African Business Unit Graduate (ABU) ambayo inawapa fursa ya kubadilishana uzoefu na wahitimu wa aina hiyo katika nchi nyingine za Ghana na Guine ambako AngloGold Ashanti kampuni mama ya GGML inamiliki migodi.

 

Shigela alisema nidhamu kwa wahitimu hao ni msingi muhimu katika utumishi wa aina yoyote hivyo wanapaswa kuzingatia nidhamu katika utendaji wao na hata wanapokengeuka kutekeleza majukumu yao nafsi inapaswa kuwasuta.

Alitoa mfano kuwa wapo wanafunzi ambao walienda kupata mafunzo tarajali ndani ya kampuni hiyo, na kufanikiwa kupata leseni za uchimbaji kwa ngazi mbalimbali nje ya mgodi na sasa ni matajiri.

 

Pia alisema kwa kuwa mzunguko wa manunuzi ya ndani ya GGML yanakaribia Sh trilioni moja kwa mwaka hasa ikizingatiwa kampuni hiyo inazingatia matakwa ya sheria ya ‘Local content’ ambayo inaitaka kufanya manunuzi ya bidhaa zake hapa nchini, nayo ni fursa nzuri kwa wahitimu hao kujifunza na kufungua kampuni za kusambaza bidhaa kwa mgodi huo.

 

Mbali na kuipongeza GGML kwa kuwa na mipango madhubuti inayofungua fursa kwa vijana wa kitanzania, pia aliwapongeza wahitimu hao ambao wamefanikiwa kupenya na kupata nafasi hiyo hasa ikizingatiwa walioomba nafasi hiyo walikuwa 2,800 lakini wamechaguliwa 40 pekee.

 

Naye Meneja Mwandamizi anayeshughulikia masuala ya rasilimali watu, Charles Masubi alisema program hiyo ya ABU ambayo inahusu wahitimu 10 wa mwaka jana itawawezesha kupata mafunzo ya juu zaidi ya ujuzi wao wa darasani.


“Kama ni mhandisi tutamfundisha namna ya kuingia makubaliano, kuandaa bajeti  lakini pia kupata ujuzi wa namna ya kuwasiliana kwa usahihi na wenzake,” alisema.


Alisema lengo la program hii ni kuwaandaa wafanyakazi wabobezi ambao wanaweza kuja kuwa viongozi wa baadae wa kampuni hiyo na hata nje ya GGML.

 
Mmoja wa wahitimu aliyepata fursa ya mafunzo tarajali kwa mwaka huu, Fakii Juma alisema GGML ina matarajio makubwa kwao katika uzalishaji hivyo watatumia vipaji vyao kuongeza ujuzi kwenye mgodi huo kutokana na elimu wanayoipata na wanajivunia kwamba wataongeza thamani ya mgodi huo.


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU FEBRUARI 26,2024

 

 
Share:

Sunday 25 February 2024

SAGINI AFIKA ENEO LA AJALI ILIYOUA WATU 25 ARUSHA...ATOA MAELEKEZO JESHI LA POLISI

 
Na. Abel Paul, Jeshi la Polisi- Arusha
 
 
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mheshimimiwa Jumanne Sagini amefika Jijini Arusha na kukagua eneo la ajali lilotokea Februali 24, 2024 katika barabara ya Arusha - Namanga, Eneo la Ngaramtoni kibaoni Wilayani Arumeru Mkoani Arusha.
 
Mhe Jumanne Sajini Pamoja nakutoa pole kwa wahanga wa ajali hiyo, amelitaka Jeshi la Polisi kuweka mikakati madhubuti ya ukaguzi wa magari yanayotoka nje ya nchi  pamoja na yale yaliyopo ndani ya nchi pasipo kusubiria wiki ya nenda kwa usalama ili kuepuka ajali zinazoweza kujitokeza kutokana na uzembe wa madereva ama ubovu wa magari.
 
Aidha Mheshimiwa Sagini ametoa Pongezi kwa Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Wa Arusha Mount
Meru, Madaktari, wauguzi pamoja na Jeshi la Polisi na kwa namna walivyotoa huduma bora kwa majeruhi waliopata ajali siku ya jana.
 
Amefafanua kuwa ajali hiyo imehusisha raia wa kigeni kutoka nchi za Marekani, Afrika kusini, Nigeria, Togo, Bukinafaso, Madagasca na Kenya.
 
Pia ametoa salamu za Pole toka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mheshimiwa Dkt Samia Suluhu Hassan kwa watanzania hususani wananchi wa Mkoa wa Arusha kufuatia ajali hiyo.
 
Kwa upande wake Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi CP. Awadh Juma Haji amesema amepokea maelekezo yalitolewa na Naibu Waziri wa Mambo ya ndani ya nchi na kuahidi kuwa watayafanyia kazi ili kuhakikisha watumiaji wa barabara wanafuata sheria za usalama Barabarani ikiwemo watembea wa Miguu ili kuhakikisha wanafuata sheria zilizowekwa.
 
CP Awadhi amesema kuwa katika kuhakikisha wanatokomeza ajali tayari Jeshi hilo limeingia makubali ya shirika viwango Tanzania (TBS) ili kutumia vifaa vya kisasa katika ukaguzi wa vyombo vya moto.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger