Friday 23 February 2024

DKT MPANGO ATOA AGIZO KWA HAZINA ,TAMISEMI KUTUMIA HATI FUNGANI KATIKA KUHARAKISHA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO



Makamu wa Rais Dkt Phillip Mpango akizindua mradi wa kuongeza upatikanaji wa maji kwa wastani wa lita 60 katika Jiji la Tanga na wilaya jirani za Muheza na Mkinga baada ya lita 45 za awali, mradi huo umeanza baada ya uzinduzi wa hati fungani ya Kijani ya Miundombinu ya Maji Tanga katika eneo la Mabayani Jijini Tanga ukiwa na lengo la uboreshaji wa upatikanaji wa maji ambapo unagharama ya zaidi ya Bilioni 53 ambao utazalisha lita milioni 60, kushoto ni Waziri wa Maji Jumaa Aweso akifuatiwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba


Makamu wa Rais Dkt Phillip Mpango akizindua mradi wa kuongeza upatikanaji wa maji kwa wastani wa lita 60 katika Jiji la Tanga na wilaya jirani za Muheza na Mkinga baada ya lita 45 za awali, mradi huo umeanza baada ya uzinduzi wa hati fungani ya Kijani ya Miundombinu ya Maji Tanga katika eneo la Mabayani Jijini Tanga ukiwa na lengo la uboreshaji wa upatikanaji wa maji ambapo unagharama ya zaidi ya Bilioni 53 ambao utazalisha lita milioni 60, kushoto ni Waziri wa Maji Jumaa Aweso akifuatiwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba

Makamu wa Rais Dkt Phillip Mpango akizindua mradi wa kuongeza upatikanaji wa maji kwa wastani wa lita 60 katika Jiji la Tanga na wilaya jirani za Muheza na Mkinga baada ya lita 45 za awali, mradi huo umeanza baada ya uzinduzi wa hati fungani ya Kijani ya Miundombinu ya Maji Tanga katika eneo la Mabayani Jijini Tanga ukiwa na lengo la uboreshaji wa upatikanaji wa maji ambapo unagharama ya zaidi ya Bilioni 53 ambao utazalisha lita milioni 60, kushoto ni Waziri wa Maji Jumaa Aweso akifuatiwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba
Makamu wa Rais Dkt Phillip Mpango akizindua mradi wa kuongeza upatikanaji wa maji kwa wastani wa lita 60 katika Jiji la Tanga na wilaya jirani za Muheza na Mkinga baada ya lita 45 za awali, mradi huo umeanza baada ya uzinduzi wa hati fungani ya Kijani ya Miundombinu ya Maji Tanga katika eneo la Mabayani Jijini Tanga jana ukiwa na lengo la uboreshaji wa upatikanaji wa maji ambapo unagharama ya zaidi ya Bilioni 53 ambao utazalisha lita milioni 60, kushoto ni Waziri wa Maji Jumaa Aweso akifuatiwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba


Makamu wa Rais Dkt Philip Mpango akisalimiana na Waziri wa Afya na Mbunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu wa pili kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Tanga Uwasa Dkt Ally FungoNa Mwandishi wetu.


MAKAMU wa Rais Mhe,Dkt Philip Mpango ameiagiza Ofisi ya usajili wa hazina kama msimamizi wa taasisi na mashirika ya umma nchini wakishirikiana na Ofisi ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi kuhakikisha wanasimamia Halmashauri nchini kutumia dirisha la hati fungani katika kuharakisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo.


Dkt Mpango aliyasema hayo wakati wa ghafla ya uzinduzi wa hatifungani ya kijani ya Mamlaka ya Maji Tanga(Tanga uwasa) na kusema Halmshauri zoye Nchini zitumie dirisha la hati fungani kuharakisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kutoa nafasi kwa Serikali kujikita kwenye madai mengine ya vipaumbele ambayo hakuna uwezeshwaji wa kifedha.


"Nakuona bwana makopa na ukamwambie bosi wako na Waziri wa Tamisemi hakikisheni mnasimami vizuri taasisi hizo na Halmashauri zote"Alisema Dkt Mpango.



Mbali na agizo hilo pia Dkt Mpango ameiagiza Bodi ya wakurugenzi wa Tanga Uwasa,Menejimenti na Wafanyakazi wote kusimamia vizuri matumizi ya fedha zitakazopatikana kupitia hatifungani ambayo imezinduliwa leo na mapato mengine mtakayokusanya baada ya kukamilisha mradi huo


Aidha alisema nidhamu ya fedha na usimamizi thabiti ndio utakaowezesha kurejesha kwa wakati fedha za wawekezaji wa hatifungani hiyo na Serikali na haitavumilia uzembe wa aina yoyote utakaonekana kukwamisha jitihada za Rais Samia.


"Kwa maneno ya Waziri wa Maji Jumaa aweso kwamba ukimzingua Mama nanyeye atakuzingua sasa shauri yanu"Alisema Dkt Mpango.


Alisema kuwa anatambua kwamba mamlaka za maji kwa kiwango kikubwa zinafanya vzuri na ipo haja ya kuwakumbusha watu wa Tanga Uwasa waongeze ufanisi katika uendeshaji ili urejeshaji wa hatifungani hiyo usiwe sababu ya kuzorota kwa huduma au ongezeko la bei za maji kwa Tanga na Mikoa mingine ambayo itapata nafasi ya kuwa na mradi kama huo.


Makamu huyo wa Rais pia ameiagiza Mamlaka ya Masoko ya mitaji na dhamana (CMSA) kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji na wizara ya maji wekeni utararibu na mfumo wa tahadhari ili kufuatilia na kubaini mapema vihatarishi vitakavyoweza kujitokeza baada ya kuzinduliwa kwa hatifungani hiyi.


Dkt Mpango alikwenda mbali zaidi na kusema kwa kuwa urejeshwaji wa fedha hizo ni wa mkupuo baada ya kuiva kwa hatifungani inaweza kuleta changamoto wakati wa kulipa hivyo basi ni vema mjipange mapema na ikiwezekana mfungue mfuko maalumu wa kukusanya kidogo kidogo fedha za marejesho.


"Tuwe na wazo la kibunifu la dira za maji na ninaamini kwa dhati hiyo itasaidia kuongeza ufanisi wa kusanayaji wa mapato na hivyo kuongeza uwezo wa kulipa"Alisema.


Hata hivyo Dkt Philip Mpango alisema hatifungani ambayo imezinduliwa leo ikawe chachu na motisha kwa taasisi na halmashauri nyingine Nchini kutumia njia hiyo kwa ajili ya kupata fedha za miradi ya maendeleo.


Kwaupande wake waziri wa Maji Jumaa Aweso aliishukuru wizara ya Fedha na Mipango kwakufanikisha kupata mradi huo wa hati fungani ambao utasaidia kuongeza ufanisi na upatikanaji wa maji katika jiji la Tanga pamoja na wilaya za Muheza,Pangani na Mkinga,


" Hati fungani itasaidia kuongeza ufanisi wa utendaji kazi na utekelezaji wa miradi ya maji kwenye Wilaya za Tanga jiji,Muheza ,Pangani na mkinga ambapo ,hali ya upatikanaji wa huduma ya maji itapanda ifikapo 2025 hadi asilimia 100 kutoka asilimia 96" alisema Aweso


Alisema wamepata uzoefu wakusimamia miradi mingi ya maji hivyo wanaamini mradi huu wa Hati fungani utatekerezwa na wananchi watapata fursa yakushiriki kwa kiwango kikubwa

Naye Afisa mtendaji wa mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana ( CMSA) Nicodemus Mkama alisema mfumo wa Hatifungani ni sehemu ya Masoko ya mitaji katika Sekta ya fedha inayowezesha upatikanaji wa fedha kwa muda mrefu.

"Fedha za kugharamia shughuli za maendeleo huweza kupatikana kwa kuuza hisa za kampuni ( Shares),hatifungani za kampuni ( corporate Bond) ,hati fungani za Serikali ( Government Bond)na vipande katika mifuko ya uwekezaji wa pamoja ( collective investment scheme) "alisema Mkama

Aliongeza kuwa Taasisi hiyo imepata mafanikio zaidi kwa kipindi cha miaka minne iliyopita ambapo thamani ya uwekezaji katika masoko na mitaji imeongezeka kwa asilimia 31.2 na kufukia shilingi Tirioni 37 .3 katika kipindi kilichoishia January 2024 ikilinganishw na Tirioni 28.4 ya kipindi kilichoishia January 2021,


"Jumla ya mauzo ya hisa na hati fungani katika soko la hisa yameongezeka kwa asilimia 61 .6 na kufikia shilingi tirioni 9.3 kutoka trioni 5.8,vilevile thamani ya mfuko ya uwekezaji wa pamoja imeongezeka kwa asilimia 291.6 na kufikia tirioni 1.9" alisisitiza Mkama
Share:

Thursday 22 February 2024

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARI 23, 2024



Share:

Thursday 1 February 2024

MRAJIS AWATAKA WAJUMBE WA BARAZA LA WAFANYAKAZI TCDC  KUJADILI HOJA KWA UWAZI

 

Mrajis wa Vyama vya Ushirika na Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Dkt. Benson Ndiege akifungua kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Tume, Jijini Dodoma, (kushoto) Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu Wizara ya Kilimo Bi. Hilda Kinanga, (kulia) Katibu wa Baraza Bi. Selestina Kinoge.
Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Tume ya Maendeleo ya Ushirika (TCDC) wakifuatilia majadiliano mbalimbali ya Baraza

Na.Mwandishi Wetu-DODOMA


Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC) ambaye pia ni Mrajis wa Vyama vya Ushirika na Mtendaji Mkuu wa TCDC, Dkt. Benson Ndiege, amewataka wajumbe wa baraza hilo kutumia fursa hiyo kuwa wawazi, kuongea na kujadili maswala mbalimbali yatakayowasilishwa katika kikao hicho kwa maslahi ya Taasisi.

Dkt.Ndiege ameyasema hayo jijini Dodoma wakati wa kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC).


"Nichukue nafasi hii kuwajulisha kuwa katika kikao hiki tuko kwaajili ya maslahi ya Watumishi na kwasababu hiyo tunahitajika kuwa wawazi,kuongea na kujadili na sio kupitisha tu na kupata muafaka, kwasababu tunayokwendwa kuongea tunawawakilisha watumishi wengine wote ambao wamebaki kuendelea na majukumu mengine ya kikazi," amesema Mwenyekiti.


Aidha, aliongeza kuwa, "nichukue fursa hii kuwahimiza kwamba tumieni vizuri fursa hii, menejimenti ipo hapa kazi yao ni kusikiliza lakini pia ni kupokea, kutoa ufafanuzi kwa yale yatakayokuwa yamejadiliwa kwenye Baraza na kutekeleza ushauri utakaotolewa."


Awali Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo ambaye ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimaliwatu, Hilda Kinanga, aliwataka wajumbe wa kikao kutumia fursa hiyo kuimarisha mawasiliano na mahusiano mahali pa kazi, katika Taasisi na Sekta mbalimbali.

"Baraza la Wafanyakazi ni sehemu muhimu ambayo sisi watumishi tunakutana tukiwa na hadhi sawa, kwahiyo hiki ni chombo muhimu kinatakiwa kuchukuliwa kwa umuhimu wake, hivyo niwaombe wajumbe kutumia fursa hii kuendelea kuongeza mawasiliano na mahusiano katika Taasisi na kutekeleza majukumu yetu kikamilifu kwaajili ya maendeleo ya Taasisi yetu," amesema Hilda.


Mada zilizowasilishwa katika kikao hicho ni pamoja; Taarifa ya Utekelezaji ya nusu mwaka 2023/2024 pamoja na Mpango na Bajeti ya mwaka 2023/2024 ya Tume ya Maendeleo ya Ushirika, Taarifa ya Ikama na Bajeti ya Mishahara kwa mwaka wa fedha 2024/2025.


Mada zingine zilizowasilishwa ni pamoja na Hoja za wafanyakazi wa TCDC kupitia TUGHE na TALGWU, Majukumu ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (PSSF), na Mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI Mahala pa kazi.

Katika kikao hicho wajumbe walichangia na kutoa maoni na mapendekezo katika mada mbalimbali zilizowasilishwa ambapo wameipongeza Menejimenti ya TCDC kwa kuboresha mazingira ya kufanyia kazi kwa kuwapatia vitendea kazi pamoja na kuanza kuboresha maslahi ya watumishi.
Share:

DK. MWIGULU: GGML KAMPUNI KINARA INAYOKUZA MAHUSIANO MAZURI KATIKA SEKTA YA MADINI


Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba (kulia), akisalimiana na Ofisa Mkuu wa Fedha wa Kampuni ya AngloGold Ashanti (AGA), Gillian Doran (kushoto) aliyemtebelea ofisini kwake wiki iliyopita. Anayefuata kushoto ni Makamu Rais wa AngloGold Ashanti -GGML anayeshughulikia miradi endelevu na masuala ya ubia/ushirika (Afrika), Simon Shayo pamoja na viongozi wengine wa GGML. Wakati wanaofuata kulia ni baadhi ya maofisa wa wizara ya fedha.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba akiwa katika picha ya pamoja na Ofisa Mkuu wa Fedha wa Kampuni ya AngloGold Ashanti (AGA), Gillian Doran aliyemtebelea ofisini kwake wiki iliyopita. Anayefuata kushoto ni Makamu Rais wa AngloGold Ashanti -GGML anayeshughulikia miradi endelevu na masuala ya ubia/ushirika (Afrika), Simon Shayo pamoja na viongozi wengine wa GGML. Wakati wanaofuata kulia ni baadhi ya maofisa wa wizara ya fedha.
NA MWANDISHI WETU

WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba amesema mahusiano mazuri yaliyopo kati ya Serikali na Kampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) yamechangia kukuza uchumi wa Taifa hususan kwenye makusanyo mazuri ya kodi, ajira na manunuzi ya bidhaa na huduma kutoka ndani ya nchi.

Pia amesema GGML ambao wamekuwa wadau wazuri kwenye sekta ya madini pamoja na ushirikiano mzuri unaotolewa kwa wizara ya madini umeendelea kukuza sekta hiyo ya madini na kutoa mchango mkubwa kwa jamii na Taifa.

Dk. Mwigulu ametoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita jijini Dodoma alipokuwa anazungumza na Afisa Mkuu wa masuala ya Fedha wa Kampuni ya Uchimbaji Dhahabu ya Anglo Gold Ashanti, inayomiliki mgodi huo wa Geita Gold Mine-GGM), Gillian Doran.

Katika mazungumzo hayo, Dk. Mwigulu alisema; “Tumekuwa na mahusiano mazuri sana na GGML kama wizara ya fedha hususani katika masuala ya kikodi na kiuchumi.

“GGML wamekuwa wadau muhimu sana wa masuala ya kodi na masuala ya kukuza uchumi wa nchi yetu pia wamekuwa mahusiano mazuri na wizara ya kisekta (madini) kwa kuwa moja ya mgodi wa mfano ambao una ushirikiano mkubwa na wizara ya kisekta na wizara nyingine kama sisi,” alisema Dk. Mwigulu.

Aidha, alisema GGML umekuwa moja ya mgodi wa mfano wenye mahusiano mazuri na jamii mgodi ulipo kwa kutekeleza ipasavyo mpango wa uwajibika wa kampuni kwa jamii (CSR).

Pamoja na mambo mambo mengine alitoa wito kwa kampuni hiyo kutumia viwanda vya kuchenjua dhahabu kwa njia ya kusafisha iliyopo nchini ili kuendelea kukuza uchumi wa Taifa.

Aidha, katika majadiliano hayo Ofisa Mkuu wa Fedha wa Kampuni ya AngloGold Ashanti (AGA), Gillian Doran aliyemtembelea Dk. Mwigulu akiwa na timu ya uongozi wa kampuni hiyo, alimweleza waziri huyo kuhusu mipango ya muda mrefu ya AngloGold Ashanti kwa Tanzania.

Alimshukuru Dk. Mwigulu kwa kutambua mchango wa GGML ambayo imeendelea kusalia kuwa mlipakodi bora zaidi katika tasnia ya uziduaji nchini.


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI FEBRUARI 1,2024

 

Magazeti ya leo
 
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger