Tuesday 30 January 2024

WANA KAGERA KWENDA KIZIMKAZI ZANZIBAR KUMPONGEZA RAIS SAMIA KUIFUNGUA KAGERA KUPITIA KAHAWA


Mwenyekiti wa taasisi ya Mtetezi wa Mama mkoa Kagera ndg Kauthari Chamani (kushoto) akikabidhi mchango wa kufanikisha safari ya Zanzibar kwa mratibu mkuu wa safari hiyo Enock Bujuli.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Wananchi wa Mkoa wa Kagera kupitia kikundi cha wakulima wa zao la Kahawa maarufu Smart Coffee Day Tours wamepanga safari ya kwenda  Kizimkazi Zanzibar kwa ajili ya kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuifungua Kagera kupitia zao la  Kahawa.

Akizungumza na Malunde 1 blog Mratibu Mkuu wa Safari ya Wana Kagera kwenda Kizimkazi Zanzibar , Enock Bujuli amesema sababu kuu za safari hiyo ndefu kwenda kumshukuru Mhe. Rais Samia ni kuonesha thamani ya zawadi inayotokana na upendo wa Rais Samia kwa wakulima wa zai la kahawa kwa kuweka mnada wa wazi Bukoba ambapo mkulima anapata pesa yake yote tena bei kubwa tangu nchi ipate Uhuru lakini pia kuwashukuru watu waliomlea Rais Samia kwa malezi mazuri na ya maadili mema.

"Tumeandaa zawadi maalum kwa ajili ya Rais Samia. Tayari wadau wanaendelea kutoa michango yao ili kufanikisha safari hii ya kihistoria itakayofanyika Mwezi Februari 2024 ambayo pia itabeba vikundi vya ngoma maalum zenye ujumbe, viongozi wa dini. Leo Januari 30,2024 Mwenyekiti wa taasisi ya Mtetezi wa Mama mkoa wa Kagera Kauthari Chamani, amekabidhi mchango wake kwa mratibu wa safari hii muhimu Enock Bujuli",amesema Bujuli.


Amefafanua kuwa, kupitia kumpongeza Dkt. Samia Suluhu Hassan  wanataka dunia ijue kazi nzuri inayofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa wana Kagera na katika maandalizi ya safari hiyo ya kihistoria wameanza kupokea michango ili kuwezesha makundi yenye ujumbe wa zawadi, nyimbo na viongozi wa dini kusafiri kutoka Kagera kwenda Zanzibar.

"Kwa yeyote anayewiwa kutuchangia katika safari yetu ya kutoka Kagera kwenda Kizimkazi Zanzibar awasilishe mchango wake kupitia Akaunti ya SMART COFEE DAY TOURS akaunti namba 0133839710100, Benki ya CRDB au kwa Enock Bujuli (Mratibu) - 0717361886 au Justinian Kazunguru (Mwenyekiti wa Wazee) - 0759453916 au Kokuirwa Bagwerwa (Mshauri mkuu) - 0784467175",ameongeza Bujuli.

"Kikundi chetu cha Smart Coffee Day Tours,tumesajiliwa wilaya Karagwe lakini wanachama wanatokea wilaya zote za Mkoa Kagera. Kazi yetu kubwa ni kuitangazia dunia uzuri wa zao la kahawa pia kusherekea kwa kuwapongeza wote wenye mchango mkubwa katika zao la kahawa na kwa mara ya kwanza tunaanza na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye ameruhusu ushindani katika kununua za la kahawa lakini tofauti na miaka mingine ambapo bei ya kahawa ilipangwa na kundi dogo la watu na hata iliponunuliwa malipo yalitoka kidogo kidogo. Hili ni jambo kubwa sana lazima tumpongeza Rais wetu mpendwa",ameeleza Bujuli.
Mwenyekiti wa taasisi ya Mtetezi wa Mama mkoa Kagera ndg Kauthari Chamani akizungumza baada ya kukabidhi mchango wa kufanikisha safari ya Zanzibar kwa mratibu mkuu wa safari hiyo Enock Bujuli.
Mzee mshauri Justinian Kazunguru akimshukuru Mwenyekiti wa taasisi ya Mtetezi wa Mama mkoa Kagera ndg Kauthari Chamani kwa kukabidhi mchango wa kufanikisha safari ya Zanzibar 
Picha ya pamoja
Kikao cha kamati kikiendelea, kushoto ni Mzee Richard Byanjweri kutoka Kyerwa akisikiliza mratibu mkuu wa safari hiyo Enock Bujuli akitoa ufafanuzi juu ya maandalizi  ya safari ya Wana Kagera kutoka Kagera kwenda Zanzibar
Share:

Video Mpya : ROGETI Ft. JACKY MJALUO - PUNGUZA HASIRA

 

Share:

Monday 29 January 2024

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE JANUARI 30,2024


Share:

Video Mpya : INAGA MLYAMBELELE - NADAMA

 

Share:

NI KAZI YA KAWAIDA ILA MAFANIKIO YAKE SIO YA KAWAIDA!

Jina langu ni Nehemia, kwa sasa nipo Arusha, Tanzania, nimetoka mkoani Tanga, nilikuwa kule kwa miezi sita kikazi, nilikuwa nafanya kazi ya kusajili laini za simu.

Ndio, hiyo ndio kazi yangu, na hapa Arusha nipo kikazi, nimepanga na chumba kabisa na nina shukuru maisha yangu yanaenda vizuri kabisa, ni tofauti kabisa na kipindi nilikuwa nafanya kazi nyingine tofauti na hii.

Kwa kawaida mimi katika kazi hii, baada ya mizunguko mingi ya kutosha na nikiona nimemaliza mitaa yote kwa kusajili laini, ninahama kwenda sehemu nyingine, ndio sababu nilihama Tanga nakuja huko Arusha.

Watu wengi wanaichukulia poa hii kazi ila mimi kupitia hii kazi ninalisha familia, ninalipa kodi mbili, huku kwangu na kwa familia yangu.

Huko Tanga nimenunua kiwanja kabisa, kila kitu kwangu inategemea hii kazi, kwa mitandao yote, nikiingiza hela ndogo kwa mwezi basi ni Sh800,000, kuna mwezi niliwahi kuingiza hadi Sh2.1 milioni.

Hata hivyo, kuna siri ya mafanikio katika kazi yangu hii, nayo ni Kiwanga Doctors ambao walinipatia dawa ya kuvuta wateja, bila hivyo ningekuwa nazunguka sana mitaani bila kupata wateja.

Niliamua kwenda kwa Kiwanga Doctors kwa ajili ya kunifanyia dawa hiyo baada ya kukaa muda mrefu katika kazi hii lakini mafanikio yalikuwa duni sana, kwa sasa naweza kusema najivunia kile ambacho nakipata.

Siku zote kumbuka Kiwanga Doctors anatoa huduma kama kusafisha nyota, kusuluhisha migororo ya ndoa, mahusiano, mapenzi na familia, kumfunga mume au mke asitoke nje ya ndoa, anatoa tiba kwa wanaotafuta watoto.

Vilevile anatoa huduma ya kukusaidia kupata kazi au ajira, kupandishwa cheo na mshahara kazini, kuwasaidia wenye urahibu wa dawa za kulevya, sigara na pombe, kwa wanaotafuta mume au mke pia anawasaidia tena ndani ya siku chache.

Anatibu magonjwa kama kisukari, msukumo wa damu (BP), upungufu wa nguvu za kiume, miguu kuwaka moto n.k, pia anaweza kuisadia biashara yako kunawiri, na huduma zote hizi unaweza kuzipata bila kufika ofisini kwake.

Basi chukua hatua ya kuwasiliana na Kiwanga Doctors kwa namba; +254 769 404965.


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU JANUARI 29,2024





 
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger