Friday 26 January 2024

WAENDESHA BODABODA ZAIDI YA 250 JIJINI DODOMA WANAFUIKA NA MAFUNZO KUTOKA AMEND

 


Na OKULY JULIUS , Dodoma

SHIRIKA la Amend kupitia ufadhili wa Ubalozi wa Uswisi nchini Tanzania wametoa mafunzo ya usalama barabarani kwa waendesha bodaboda zaidi ya 250 katika Jiji la Dodoma , lengo ni kuliepusha kundi hilo pamoja na watumiaji wengine wa barabara dhidi ya ajali za barabarani.

Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo hayo yaliyohusisha pia wadau mbalimbali, Meneja wa Shirika la Amend Tanzania Simon Kalolo amesema wametoa mafunzo hayo kwa kutambua kuwa ajali za barabarani zimekuwa chanzo kikubwa cha ajali na ajali nyingi zinatokana na uendeshaji usizingatia usalama barabarani.

“Ajali za barabarani ni sababu kuu ya vifo vya watoto na vijana kati ya miaka 5 na 29 ulimwenguni. Bara la Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara lina viwango vya juu zaidi vya vifo vya barabarani duniani.

“Takwimu zilizochapishwa na Shirika la Afya Ulimwenguni zinaonyesha zaidi ya waendesha pikipiki 3,700 walikufa kwenye barabara za Tanzania mnamo 2016(mwaka wa hivi karibuni ambao data kamili zinapatikana).

“Hii ni sawa na kiwango cha vifo vya waendesha pikipiki cha 67 kwa kila watu 100,000 -mojawapo ya viwango vya juu zaidi vya vifo vya pikipiki barani Afrika,”amesema Kalolo.

Ameongeza pamoja na kusababisha ajali kwa madereva na abiria wake, pikipiki pia husababisha hatari kwa watumiaji wengine wa barabara, haswa watembea kwa miguu.

Amesema kwa bahati nzuri hatua madhubuti za kuzuia ajali za barabarani zinafahamika, zikijumuisha elimu ya kina kwa watembea kwa miguu na mafunzo ya usalamabarabarani kwa waendesha pikipiki, ambayo yametolewa chini ya mradi huu.

“Jijini Dodoma, Ubalozi wa Uswisi umefadhili utoaji mafunzo ya usalama barabarani kwa waendesha pikipiki (boda-boda) 250. Mradi huu wa mafunzo ya pikipiki umeandaliwa mahususi kwa waendesha pikipiki na mazingira ya Tanzania.

“Muundo wa mafunzo hayo unatokana na mafunzo ya msingi ya lazima ya Uingereza kwa waendesha pikipiki, lakini umetoa nafasi kwa wakufunzi wa Kitanzania kuyarekebisha ili kukidhi mahitaji halisi ya hapa nchini.

“Mafunzo hayo yalitoa elimu ya vitendo iliyolenga kujenga uwezo ambao madereva wengi wa pikipiki wanajulikana kuukosa. Mazoezi ya vitendo yalijumuisha matumizi sahihi ya makutano na mizunguko, kuvuka vyombo vingine vya moto kwa usalama, na jinsi ya kusimama haraka katika dharura,”amesema.

Ametumia nafasi hiyo kuishukuru Serikali kwa kuendelea kushirikiana na Amend katika kufanikisha utolewaji wa mafunzo ya usalama barabarani katika mikoa mbalimbali ukiwemo wa Dodoma.


Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Afya katika Ubalozi wa Uswisi nchini Tanzania Viviane Hasselmann amesema  kuwa asilimia 62 ya Watanzania wana umri chini ya miaka 25, ni muhimu kuelekeza afua za maendeleo kwa vijana, na kushughulikia changamoto na mahitaji yao mahususi.

“Kupitia mradi huu, na mafunzo haya ya pikipiki, Ubalozi wa Uswisi kwa kushirikiana na Amend, wanalenga kuboresha usalama wa waendesha pikipiki, abiria na watumiaji wengine wa barabara, na hivyo kuzuia vifo na majeruhi wengi vijana kadri inavyowezekana,”amesema.


Akizungumza mbele ya wadau wa usalama barabarani Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Jabir Shekimweli ametoa shukrani kwa Ubalozi wa Uswisi nchini Tanzania kwa kufadhili mafunzo hayo kwa waendesha bodaboda kwani yanachangia kupunguza ajali za barabarani nchini.

Amesema kuwa katika mwaka 2023 watu zaidi ya milioni 61 wamefariki duniani na kati hayo waliofariki kwa ajali za barabarani ni watu zaidi ya milioni moja na hiyo ni picha ya dunia.

“Tukiangalia kwa Tanzania Jeshi la Polisi liliripoti makosa ya barabarani 2534 kwa mwaka mzima na ajali za barabarani zilizokuwa zimetolewa taarifa 1760 lakini vifo vilivyotokana na hizo ajali ni vifo zaidi ya 1000 kwa maana katika kila ajali tatu kuna mtu mmoja alikufa.

“Kwa Dodoma hali inasura inayofanana na hiyo , imeripotiwa ajali zaidi ya 1000 na kati ya hao 59 wamefariki dunia.Na hizo ni taarifa ambazo zimeripotiwa na jeshi la polisi.Kwa hiyo mafunzo haya yana umuhimu wa kipekee,”amesema Shekimweri.

Amesisitiza ajenda ya mafunzo ya elimu ya usalama barabarani yanaumuhimu wa kipekee kwani mbali ya vifo ajali hizo zinasababisha ulemavu wa kudumu huku akieleza takwimu za sensa zinaonesha asilimia kubwa ya watanzania ni vijana na kutokana na changamoto za ajira watu wengi wameamua kujikita katika ujasiriamali na bodaboda.

Amesisitiza kuwa ili kuendelea kukomesha ajali za barabarani iko haja kwa Amend, Ubalozi wa Uswisi na wadau wengine kuendelea kutoa mafunzo kwa kundi hilo la waendesha bodaboda huku akitoa rai kwa waendesha bodaboda kuzingatia sheria za usalama barabarani.

Awali Mkuu wa Dawati la Elimu ya Usalama Barabarani nchini, Kamishna Msaidizi wa Polisi Michael Deleli amesema watumiaji wengi wa bodaboda walihama kutoka katika kuendesha baiskeli, hivyo mafunzo hayo ni muhimu kwao.

“Wengi wetu tunaendesha pikipiki kwa uzoefu wa baiskeli hivyo wengi hawakupitia mafunzo rasmi ya udereva.Sisi kama Jeshi la Polisi tunaendelea kupongeza wadau ambao wanajitolea kutoa mafunzo kama haya, kwetu inakuwa furaha kubwa.

Amesema mafunzo ambayo wamefundishwa ni vema wakayapeleka na kwa watumiaji wengine ambao hawajahudhuria mafunzo hayo ili wote wawe salama huku akielezea umuhimu wa kuvaa kofia ngumu kwani ndio usalama wa mhusika.

“Usipovaa kofia ngumu ukianguka sehemu kubwa ya mwili ambao unaumia na hasa ukiwa spidi ni kichwani.vifo vingi vya pikipiki ni kuangukia sehemu ya kichwa, kwa hiyo tusipovaa kofia ngumu maisha yanakuwa hatarini,hivyo nisisisitize wote tunapokuwa katika bodaboda tuvae kofia ngumu.”
Share:

Thursday 25 January 2024

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA JANUARI 26,2024

Magazeti ya leo Ijumaa Januari 26, 2024...Habari kubwa Matokeo Kidato cha nne 2023







Share:

RC SENDIGA AKABIDHI PIKIPIKI 42 KWA JUMUIYA ZA MAJI RUWASA


Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Sendiga amekabidhi pikipiki 42 kwa jumuiya za watoa huduma za maji katika wilaya zote za Mkoa wa Manyara ili kurahisisha utendaji kazi kwa watumiaji hao.

Pikipiki hizo zimetolewa na Wakala wa Maji Safi na Salama na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) mkoa wa Manyara.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi pikipiki hizo Mhe. Sendiga amesema ni vyema kwa watumishi hao kuzitunza kwani ni mali ya serikali.
"Niwasihi tukahakikishe pikipiki hizi zinaenda kutumika kama ilivyokusudiwa na kuhakikisha skimu za maji zinakuwa endelevu na Wananchi wanapata huduma ya maji muda wote kwani ni haki yao ya msingi", amesema Mhe. Sendiga.
Aidha, Mhe. Sendiga amewataka wakuu wa taasisi mbali mbali kukusanya fedha za Umma kwa uadilifu kwa kuzingatia taratibu, kanuni na sheria zilizopo na kusitokee chombo chochote kukiuka kwa sababu yoyote huku akiwasihi wakuu wa wilaya wote kuendelea kusimamia vyema uhai wa miradi iliyojengwa.


"Serikali imewekeza fedha nyingi sana kujenga miradi hii ya maji, fedha hizi ni zenu kupitia kodi na tozo mbalimbali, tunajukumu kubwa la kuitunza miradi ili kuhakikisha kusudi la Rais wetu Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan la kumtua mama ndoo kichwani linafikiwa", amesema Mhe. Sendiga.
Akitoa shukrani zake kwa RUWASA Mkuu wa Wilaya ya Babati Mhe. Lazaro Twange amesema kuwa atasimamia na kufuatilia kwa Ukaribu kama watumisji waliokabidhiwa pikipiki hizo wanazifanyi kazi kama ambavyo kusudio la Serikali ilivyowaagiza.
Kwa upande wake Meneja wa RUWASA mkoa wa Manyara Injinia Wolter Kilter amesema lengo la kuwapa pikipiki hizo kwa watumiaji hao ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma za maji kwa uharaha zaidi.

Amesema kuwa Mkoa wa Manyara unajumla ya Vyombo hivi 88 vinavyosimamia Skimu za maji 346 na kuhudumia wananchi 1,268,239 ambapo mpaka Septemba 30, 2023 zilikusanywa jumla ya Tshs 2,113,232,529", amesema Injinia Kilter.

Ameongeza kuwa RUWASA inaendelea kuvipatia mafunzo jumuiya za watumiaji Maji kama jinsi ya kuandaa mpango wa biashara na ufungaji wa hesabu, vyombo 32 vimeshapatiwa mafunzo hayo mpaka Julai 23, 2023.
Share:

HAYA HAPA MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2023, QT 2023

   


MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE(CSEE) 2023 NA MTIHANI WA MAARIFA (QT) YAMETANGAZWA RASMI LEO ALHAMISI JANUARI 25,2024
Share:

Breaking : MATOKEO YA MTIHANI KIDATO CHA NNE 2023



MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE(CSEE) 2023 NA MTIHANI WA MAARIFA (QT) KUTANGAZWA HIVI PUNDE

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2023

MATOKEO YA DARASA LA NNE 2023

TUTAWEKA HAPA HIVI PUNDE
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI JANUARI 25, 2024

 

Magazeti ya leo
 

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger