Thursday 4 January 2024

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI JANUARI 04,2024



Share:

Wednesday 3 January 2024

Video Mpya : SUPER NYOTA STEVE - JANETH

 

Share:

BARRICK BULYANHULU YAPELEKA FARAJA YA SIKUKUU YA MWAKA MPYA KWA WAZAZI,WAGONJWA NA WATUMISHI KITUO CHA AFYA BUGARAMA

Wafanyakazi wa Barrick Bulyanhulu wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa kituo cha afya cha Bugarama kilichopo wilayani Msalala walipotembelea kituo hicho kwa ajili ya kutoa zawadi za mwaka mpya kwa wagonjwa waliolazwa kituoni hapo na kwa wafanyakazi wa kituo hicho.
Kaimu Meneja Mkuu wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, Everjoy Ngomamiti, (Mwenye miwani kulia) akikabidhi zawadi za mwaka mpya kwa Mganga mfawidhi , kituo cha afya Bugarama kilichopo wilayani Msalala , Beatha Alistide (kushoto) wakati wafanyakazi wa mgodi huo walipotembelea kituo hicho na kutoa zawadi mbalimbali za mwaka mpya kwa wagonjwa waliolazwa na wafanyakazi wa kituo hicho jana.Wengine pichani ni wafanyakazi wa Barrick Bulyanhulu.
Wafanyakazi wa Barrick Bulyanhulu wakigawa zawadi kwa baadhi ya wagonjwa na wafanyakazi wa kituo cha afya cha Bugarama.
Wafanyakazi wa Barrick Bulyanhulu wakigawa zawadi kwa baadhi ya wagonjwa na wafanyakazi wa kituo cha afya cha Bugarama.
Wafanyakazi wa Barrick Bulyanhulu wakigawa zawadi kwa baadhi ya wagonjwa na wafanyakazi wa kituo cha afya cha Bugarama.
Wafanyakazi wa Barrick Bulyanhulu wakigawa zawadi kwa baadhi ya wagonjwa na wafanyakazi wa kituo cha afya cha Bugarama.

**

Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, uliopo wilayani Msalala mkoani Shinyanga, umekabidhi zawadi za sikukuu za mwaka mpya 2024, kwa wazazi na wagonjwa waliolazwa kwenye kituo cha afya cha Bugarama ,sambamba na wafanyakazi wa kituo hicho.

Kaimu Meneja Mkuu wa Mgodi huo, Everjoy Ngomamiti, akiambatana na baadhi ya wafanyakazi walishiriki kugawa zawadi mbalimbali kwa wagonjwa pamoja na kwa wafanyakazi wa kituo hicho.

Akizungumza baada ya zoezi hilo, Kaimu Meneja wa mgodi huo, Everjoy Ngomamiti ,alisema kampuni itaendelea kushiriki shughuli za maendeleo kwa jamii inayoishi kuzunguka mgodi huo sambamba na kuimarisha nao uhusiano mwema.

Kwa upande wake Mganga mfawidhi , kituo cha afya Bugarama , Beatha Alistide ,alitoa shukrani kwa Barrick Bulyanhulu kwa kuwa mstari wa mbele kusaidia jamii inayozunguka mgodi, kusaidia kituo hicho kuweza kutoa huduma bora kwa wananchi pia kutatua kutatua changamotombalimbali zinazojitokeza katika kituo hicho.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO JANUARI 3,2023


Share:

Tuesday 2 January 2024

MPC YALAANI KITENDO CHA WAANDISHI WA HABARI KUCHEKELEA KUPEWA NYAMA NA MBUNGE




TAARIFA KWA UMMA JUU YA UVUNJIFU WA MAADILI YA UANDISHI WA HABARI

Klabu ya Waandishi wa Habari ya Mkoa wa Mwanza (MPC), ni klabu iliyosajiliwa kwa sheria ya Society Act Mwaka 1994 na kupewa namba ya usajili ya SO 8262, ikiwa na dhima kuu ya kusimamia weledi wa uandishi wa habari ndani ya Mkoa wa Mwanza.

MPC imefuatilia kwa ukaribu kusambaa kwa kipande cha picha nyongefu kikionesha Mwandishi wa Habari Emmanuel Twimanye akimshukuru Hamisi Mwagao Tabasamu Mbunge wa Jimbo la Sengerema kwa kutoa mgao wa nyama ya Mbuzi na Kondoo kwa baadhi ya waandishi wa habari wa Wilayani Sengerema, Mkoa wa Mwanza, tukio lililotokea Januari 1, 2024.


MPC inalaani kitendo hicho kwa kuwa, kinakiuka misingi na maadili ya uandishi wa habari kwani Mwandishi wa Habari hatakiwi kupokea pesa, zawadi au bakishishi yoyote ile kutoka kwa Mwanasiasa, Afisa wa Serikali au Mfanyabiashara ili kuepuka mgongano wa kimaslahi kwenye utendaji kazi wake.


MPC inalaani kitendo hicho na imechukua hatua za kuwaonya waandishi wote waliohusika kwenye tukio hilo na kuwaelimisha athari za vitendo hivyo kwenye tasnia ya habari na mtazamo wa jamii na inawataka waandishi wote kuzingatia maadili ya uandishi wa habari kuelekea kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 na uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025.
Ahsanteni

Edwin C. Soko
Mwenyekiti, MPC
02.01.2024


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE JANUARI 02,2024


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger