Sunday 2 July 2023

BENKI YA CRDB YAINGIA MAKUBALIANO NA KLABU YA YANGA KUSAIDIA USAJILI WA WANACHAMA NA MASHABIKI


Benki ya CRDB imeingia mkataba wa makubaliano na Yanga kutoa kadi kwa wanachama wa klabu Yanga katika kuongeza ufanisi wa usajili na masuluhisho ya kifedha.

Akizungumza wakati hafla kusaini makubaliano hayo iliyofanyika Julai 1, 2023, Afisa Mkuu wa Biashara Benki ya CRDB, Boma Raballa amesema kadi hizo zitawawezesha mashabiki wa mabingwa hao wa kihistoria wa Tanzania bara kujisajili na kulipia michango yao ya uanachama kupitia mtandao wa matawi zaidi ya 240 wa Benki ya CRDB.
“Kupitia kadi hizi zilizopewa jina la TemboCard Young Africans wanachama wa klabu hii wataweza kufanya miamala kupitia mashine za kutoa fedha (ATMs) hadi milioni 2, kufanya manunuzi kupitia mashine za malipo (PoS), pamoja na malipo ya mtandaoni (online payment) hadi milioni 20,” alisema Raballa huku akibainisha kuwa wanachama hao pia wataunganishwa na mifumo ya kidijitali ya SimBanking na Internet banking.

Raballa pia alianisha kuwa kupitia kadi hizo za TemboCard Young Africans wanachama na washabiki wa klabu hiyo pia watapata bima ambayo inatoa mkono wa pole wa Shilingi milioni 3 pindi mwanachama anapofariki ya milioni 3, Shilingi milioni 2.5 anapofiwa na mume au mke, na Shilingi milioni 2 endapo atapata ulemavu wa kudumu.
Kwa upande wake Rais wa Yanga, Injinia Hersi Saidi ameishukuru Benki ya CRDB kwa kufungua milango ya ushirikiano na klabu hiyo itakayosaidia kuongeza ufanisi katika usajili. Injinia Hersi alisema ukubwa Benki hiyo yenye mtandao mpana ndani na nje ya nchi utakwenda kusaidia kuongeza kasi ya usajili wa wananchama wengi zaidi kulinganisha na sasa hivi.

“Mchakato wetu wa usajili wa wanachama umekuwa na mafanikio makubwa sana ukitufanya kuwa klabu inayoongoza kwa Idadi ya wananchama katika ukanda huu wa jangwa la sahara, lakini ni ukweli usiopingika kuwa bado hatujafikia lengo kwani matawi yetu mengi yamekosa miundo mbinu sahihi. Ni imani yetu ushirikiano huu na Benki ya CRDB utakwenda kuongeza kasi ya usajili,” aliongezea Injinia Hersi.
Akizungumzia kuhusu zoezi usajili wa wananchama kupitia Benki ya CRDB, Injinia Hersi alisema kuanzia tarehe 5 Julai 2023 wanachama wa klabu hiyo wanaweza kufanya usajili katika matawi yote ya benki hiyo yaliyosambaa kote nchini bila gharama yoyote.
Share:

Saturday 1 July 2023

MBIO ZA KIMONDO ZAFANA SONGWE


Mashindano ya riadha, maarufu kama Mbio za kimondo yanayoandaliwa kwa pamoja baina ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), ikiwa ni maadhimisho ya siku ya kimondo duniani kwa mwaka 2023 yamalizika kwa mafanikio makubwa huko Mbozi mkoani Songwe.

Akizungumza katika kilele cha maadhimisho hayo (leo) Juni 30, 2023 kutoka wilayani Mbozi mkoani Songwe, Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Utafiti, Machapisho na Ubunifu wa OUT ambaye pia ni mjumbe wa bodi ya NCAA, Dkt. Harrieth Mtae, amesema shughuli zote zilizoambatana katika maadhimisho ya siku kimondo duniani yamekwenda vizuri lakini mbio za zimondo zimefanya vyema.

“Nasema maadhimisho haya yamefana sana sababu katika mbio hizi za km 5, 10 na 21 yamepata washiriki wengi wa ngazi za kimataifa na kitaifa, kutokana na kufana kwa maadhimisho haya tunategemea taarifa za zao hili jipya la utalii wa anga zitazidi kusambaa sababu ni kitu ambacho hakijazoeleka hivyo jamii inapaswa kuhabarishwa juu ya utalii wa anga ili kuleta matoke chanya.” Amesema Dkt. Mtae

Pia, Kamishna Msaidizi Mwandamizi kutoka NCAA, Joshua Mwamkunda, akizungumzia katika kilele cha maadhimisho hayo, amesema kitendo tu cha wananchi wengi kufika kwa wakati mmoja katika maeneo ya kimondo hayo tayari ni mafanikio tosha kuhusu kueneza habari hizi za utalii wa anga na kimondo.

“Kitendo tu cha washiriki wa hizi mbio kutoka mikoa mbalimbali pamoja na wananchi wa maeneo jirani waliofika kujionea maadhimisho haya ni mafanikio tosha juu ya uhamsishaji na uelimishaji juu ya urithi wa anga na utalii wake, watu wengi wamefika hapa na wametembelea kimondo, wamepiga picha maana yake tayari wamefanya utalii wa ndani lakini kutuma picha mitandaoni hapo matangazo yanasambaa sehemu tofauti.” Amesema Kamishna Mwamkunda.

Aidha, alisisitiza kuwa lengo la maadhimisho haya ni kuelimisha, kuhamasisha na kuendeleza utalii wa anga na urithi wake hasa hivi vimondo vilivyopo nchini ili kuongeza watalii wa anga kutoka ndani na nje ya nchi na kuungana kwa vitendo juhudi za serikali katika kuhamasisha utalii nchini.

Naye, Mkuu wa Idara ya Utalii, Ukarimu na Geographia wa OUT, Dkt. Halima Kilungu, amesema kuhamasisha wananchi kupenda utalii wa anga ni kuwafanya wapende mazingira hayo hivyo watashiriki katika kuyalinda mazingira ya anga dhidi ya uharibifu.

Maadhimisho ya siku ya anga duniani huadhimishwa Juni 30, kila mwaka ambapo kwa hapa nchini yamekuwa yakiadhimishwa katika mkoa wa Songwe ili kuhamasisha utalii nyanda za juu kusini kupitia kimondo kilichopo wilayani Mbozi mkoani Songwe. Taasisi mbili za NCAA na OUT wamekuwa wakishirikiana katika maadhimisho hayo nchini ikiwa ni sehemu ya ushiriki wao katika kutangaza vimondo vilivyopo sambamba na zao jipya la utalii wa anga.

Share:

MWENYEKITI UVCCM KISHAPU AFANYA MKUTANO WA HADHARA KUSIKILIZA KERO ZA VIJANA NA KUZITAFUTIA UFUMBUZI

 

Na Marco Maduhu,KISHAPU

MWENYEKITI wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana ya Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Kishapu Benard Benson Welema, amefanya Mkutano wa hadhara wa kusikiliza kero za Vijana wilayani humo na kuzitafutia ufumbuzi.

Mkutano huo wa hadhara umefanyika leo Julai 1, 2023 katika Mji wa Mhunze wilayani Kishapu.
Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Kishapu Benard Benson Welema akisikiliza kero za vijana.

Amesema amefanya Mkutano huo wa kusikiliza kero mbalimbali ambazo zinawakabili vijana wilayani humo, ili kuzitafutia ufumbuzi, huku akiwataka wachangamkie fursa mbalimbali kupata ajira katika miradi ya kimkakati ambayo inatekelezwa wilayani humo na kujikwamua kiuchumi.
Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Kishapu Benard Benson Welema.

“Kero ambazo vijana wenzangu mmeziwasilisha kwenye Mkutano huu tutazifikisha sehemu husika ili zipate kutatuliwa, katika wilaya yetu ya Kishapu kuna miradi ya kimkakati ambayo inatekelezwa changamkieni fursa hizo ili mpate ajira, vibarua na kujikwamua kiuchumi,”amesema Welema.

Aidha, amewataka vijana wilayani humo kuwa Mstari wa mbele kuomba Ajira ambazo zimekuwa zikitangazwa na Halmashauri, ambapo inaonekana muitikio wao kuwa mdogo, pamoja na kuunda vikundi vya ujasiriamali ili wapate mikopo ya asilimia 4 kwa vijana ya halmashauri na kuinuka kiuchumi.
Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Kishapu Benard Benson Welema.

“Serikali ilisitisha utoaji wa mikopo asilimia 10 ya mapato ya ndani ya halmashauri baada ya kuona haina tija, na vijana wengi mlikuwa mkikopa lakini hamrejeshi, nawaomba mikopo hii itakapoanza kutolewa itumieni vizuri kufanya uzalishaji na kuwaletea maendeleo na siyo kwenda kuzinyewa Pombe.”amesema Welema.
Katibu wa UVCCM Wilaya ya Kishapu Jamal Namanga akizungumza kwenye Mkutano huo.

Nao baadhi ya vijana wakiwasilisha kero zao akiwamo Elisha Elias, wameiomba Serikali wilayani humo kwamba fursa mbalimbali ambazo zinatokea zikiwamo za ujenzi na utengenezaji wa samani wawe wanatoa kipaumbele kwanza kwa vijana wilayani humo.

Naye Kijana Michael Mabula, amewasilisha kilio cha ukosefu wa mikopo ya Bodaboda kutoka kwenye Taasisi za kifedha sababu ya kuwa na masharti magumu ya dhamana, na kuwafanya kuendelea kutumikishwa na kushindwa kumiliki bodaboda zao wenyewe.

Diwani wa Songwa Abdul Ngolomole, akizungumza kwenye Mkutano huo, amempongeza Mwenyekiti huyo wa UVCCM wilayani Kishapu kwa kufanya Mkutano wa kusikiliza kero za vijana na kuahidi atashirikiana naye kama diwani kijana ili kuzitafutia ufumbuzi.
Diwani wa Songwa Abdul Ngolomole akizungumza kwenye Mkutano huo.
Mkutano ukiendelea.
Kijana Michael Mabula akiwasilisha baadhi ya kero ambazo zinawakabili vijana wilayani Kishapu
Mkutano ukiendelea.
Elisha Elias akiwasilisha baadhi ya kero ambazo zinawakabili vijana wilayani Kishapu.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.
Baadhi ya akina Mama wakiwa kwenye Mkutano wa Mwenyekiti wa UVCCM wilayani Kishapu.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.
Akina Mama wakiimba nyimbo za CCM kwenye Mkutano wa Mwenyekiti wa UVCCM wilayani Kishapu.
Share:

DKT.MPANGO AZINDUA MAONYESHO YA BIDHAA ZA JKT DODOMA

 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango akipokea zawadi ya tuzo kutoka kwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Innocent Bashungwa mara baada ya Ufunguzi wa Wiki ya Maadhimisho ya Miaka 60 ya JKT iliofanyika mkoani Dodoma leo tarehe 01 Julai 2023.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango akipanda mti aina ya Mstafeli katika eneo la Makao Makuu ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Chamwino mkoani Dodoma wakati wa Ufunguzi wa Wiki ya Maadhimisho ya Miaka 60 ya JKT. Tarehe 01 Julai 2023.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango akiwa katika picha ya pamoja na wawakilishi wa Vijana wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) wakati wa Ufunguzi wa Wiki ya Maadhimisho ya Miaka 60 ya JKT mkoani Dodoma leo tarehe 01 Julai 2023. (Wengine katika Picha ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Innocent Bashungwa, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Faraji Mnyepe, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Meja Jenerali Rajabu Mabele pamoja na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Mhe. Vita Kawawa)


Na Dotto Kwilasa, Malunde1 Blog, DODOMA 

 JESHI la Kujenga Taifa (JKT) limeadhimisha miaka 60 tangu kuanzishwa kwake mwaka 1963 na kuzindua maonyesho ya bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na jeshi hilo na kuahidi kuongeza ari ya kuwafundisha Vijana matumizi ya  Teknolojia kwenye uzalishaji wa chakula kuendana na wakati.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Philip Mpango ameshuhudia maadhimisho hayo na kufurahishwa namna Jeshi hilo linavyofanya kazi huku akitoa rai kwa wananchi kujitokeza katika wiki nzima ya maadhimisho ya miaka 60 ya JKT ili kujionea bidhaa zinazozalishwa  na kujifunza masuala mbalimbali ikiwemo kilimo, ufugaji na utengenezaji bidhaa.

Pamoja na hayo ametumia nafasi hiyo kuliagiza Jeshi hilo(JKT )kuongeza ari ya kuwafundisha Vijana matumizi ya  Teknolojia kwenye uzalishaji wa chakula ili nchi iweze kuwa Ghala la Chakula kwa ukanda wa Afrika .

Akizungumza  leo July 1,2023 Jijini Dodoma wakati kwenye maadhimisho hayo Dkt.Mpango amesema ulimwengu wa sasa ni wa Sayansi na teknolojia hivyo ni vyema kwa Jeshi hilo kutumia teknolojia za kisasa kufundisha vijana katika kuzalisha mali zitakazokidhi ubora wa hali ya juu.

"Ninaomba Jeshi hilo lione umuhimu wa kuwatambua wataalam wake wabunifu na kuwapa tuzo sambamba na kushirikiana na Taasisi husika kuwa na haki miliki ya ubunifu na gunduzi mbalimbali zinazofanywa jeshini,"amesema.
 
Katika kutekeleza dhima ya kuwaandaa vijana wa Tanzania,Dkt.Mpango amesema JKT linapaswa kuendeleza uzalendo wa kuwajengea nidhamu, ukakamavu na kujituma ili waweze kuchangia katika ulinzi wa Taifa na maendeleo ya kiuchumi,.

Kuhusu utunzaji wa mazingira, Dkt.Mpango amelitaka Jeshi la JKT kuendeleza juhudi zake katika utunzaji wa vyanzo vya maji na kueleza kuwa anafahamu kuwa jeshi hilo ni kinara katika utunzaji wa mazingira.

Amesema,"Juhudi za kupanda miti na uhifadhi wa mazingira zifanywe na Kambi zote za JKT nchini, ili kuhakisha mazingira yanatunzwa kwa faida ya kizazi cha sasa na kijacho, namsisitiza pia matumizi ya nishati safi ili kupunguza ukataji miti ovyo,"amesisitiza

Aidha amelitaka Jeshi hilo kuunga mkono udhibiti wa taka za plastiki, kwani huchangia kwa kiasi kikubwa katika uchafuzi wa mazingira na kutoa wito kwa JKT kuhakikisha wanashirikiana na Taasisi zingine katika kutafuta suluhisho la upatikanaji wa chakula cha samaki hapa nchini.

Kwa upande wake Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Innocent Bashungwa amesema Wizara yake itaendelea kuijengea  uwezo JKT  ili  kuongeza uzalishaji kupitia Suma JKT na kushiriki katika miradi mikubwa ya kimkakati.

 Amesema kwa kushirikiana na Wizara nyingine za kisekta wanatarajia kuboresha mafunzo ya stadi za kazi kwa vijana wa JKT na kuwawezesha kuwapatia ujuzi na maarifa zaidi ili baada ya kuhitimu waweze kujitegemea kwa kuanzisha shughuli mbalimbali za ujasiriamali.
 
Waziri Bashungwa ameongeza,"Pamoja na malezi kwa vijana JKT tunapaswa kuwa na ubunifu na kutoa mchango kwa taifa, kuzalisha ajira na kulisaidia taifa kuwa na chakula toshelevu,lakini yote haya yanapatikana Kwa sisi kuendelea kuwa kitovu cha amani,"amesema
 
Naye  Mkuu wa Jeshi hilo Meja Jenerali Rajabu Mabele amesema licha ya changamoto mbalimbali,JKT limefanikiwa kufikia dhumuni la kuanzishwa kwake kwa kutoa mafunzo ya malezi kwa vijana ili kuwajengea uzalendo, kujitegemea na kuleta maendeleo endelevu na utangamano wa kitaifa. 

"Malengo haya yametekelezwa kwa ufanisi na kufanikiwa kuwabadili vijana wetu  kifikra na kuwajenga katika hali ya umoja, moyo wa kupenda kazi, uadilifu, nidhamu, uzalendo na uelewano bila kubaguana kwa misingi ya ukabila, udini, jinsia na kudumisha uhuru na amani ya Taifa,"amefafanua Mkuu huyo wa JKT na kuongeza;
 
"Naishukuru sana Serikali kwa kuendelea kuchukua hatua mbalimbali kukabiliana na changamoto za Jeshi letu ikiwemo kuendelea kutenga fedha ili kuboresha miundombinu itakayowezesha kuchukua vijana wengi zaidi kwa ajili ya mafunzo,ni matumaini yangu kwa kila mtanzania kuendeleza uzalendo wa kujituma na kujifunza mengi kupitia JKT,"amesema.


Share:

BUSHAKO : VIJANA WA CCM MSIKUBALI KUTUMIWA NA WANASIASA TUEPUKE MATABAKA CCM



Makamu Mwenyekiti wa Halmshauri ya Wilaya ya Muleba, Bw. Muhaji Bushako
****

Vijana wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Muleba Mkoani Kagera wametakiwa kuepuka kutumiwa na wanasiasa kwenye maeneo yao ili kuepusha   kuwepo kwa matabaka kwenye jumuiya hiyo.


Makamu Mwenyekiti wa Halmshauri ya Wilaya ya Muleba, Bw. Muhaji Bushako amesema hayo  kwenye kikao cha baraza la Umoja wa Vijana  wa Chama cha Mapinduzi cha Wilaya cha kikanuni kwa  mwezi wa sita  ambapo amesema kuwa vijana wanao wajibu wa kuhakikisha wanajisimamia wenyewe.

Bushako amesema wapo baadhi ya vijana wamekuwa wakitumiwa na wanasiasa kwenye maeneo yao na kusababisha kuwepo kwa matabaka hivyo wanalo jukumu la kuhakikisha wanajisimamia na kuwa kitu kimoja kwani  jumuiya hiyo ni tanuru ya uongozi.

 
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Muleba Bwana Geofrey Kamili amewataka vijana kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi  katika  uchaguzi wa Serikali za mitaa  kwenye maeneo yao ambao unatarajia kufanyika hapo mwakani kwani  jukumu la kuwa kiongozi sio la watu wazima pekee.

Nao baadhi ya wajumbe wa balaza hilo la Vijana ambao ni Minath Mickdard na Muksini Mohamed wamesema kuwa kitendo cha kutumika ki siasa kina athiri maendeleo ya jumuiya hiyo ambapo watahakikisha wanakuwa wamoja na kuondoa matabaka kwenye jumuiya hiyo.

Aidha katika kikao hicho wajumbe walimpitisha katibu hamasa wa Jumuiya ya vijana CCM wilaya ya Muleba Mohamed Isumail Rwabakoba.
Makamu Mwenyekiti wa Halmshauri ya Wilaya ya Muleba, Bw. Muhaji Bushako

Share:

Tanzia MBUNGE WA MBARALI AFARIKI KWA KUGONGWA TREKTA


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger