Saturday 3 June 2023

TRENI ZAGONGANNA NA KUUA WATU 260, KUJERUHI 900



ZAIDI ya watu 260 wanaripotiwa kufariki dunia nchini India na wengine 900 wamejeruhiwa baada ya treni mbili za abiria na nyingine ya mizigo kugongana huko katika Jimbo la Odisha lililopo Mashariki mwa nchi hiyo.

Ajali hiyo imetokea siku ya Ijumaa Juni 2, 2023 katika Wilaya ya Balasore katika Jimbo la Odisha inatajwa kuwa tukio baya zaidi la reli nchini India katika takribani miaka 20 iliyopita.

Mtendaji Mkuu wa Jimbo la Odisha, Pradeep Jena amesema, idadi ya waliokufa kufuatia ajali hiyo ya Ijumaa inatarajiwa kuongozeka.

Aliongeza kuwa, zaidi ya magari 200 ya kubebea wagonjwa yalikwenda katika eneo la ajali katika wilaya hiyo na madaktari wa ziada 100, ikiwa ni kuwaongezea nguvu wengine 80 ambao tayari walikuwepo katika eneo la tukio.


Madaktari hao walikuwa wanawajibika kuwapeleka majeruhi hospitalini na kuwahudumia wale ambao bado walikuwa kwenye eneo la tukio.

Wanajeshi wa jeshi na helikopta za jeshi la anga walijiunga katika eneo hilo kwa ajili ya kutoa msaada huo pamoja na viongozi wa eneo hilo.

Picha za video zilionesha waokoaji wakipanda juu ya treni iliyosongamana kutafuta manusura, huku abiria wakiomba msaada na kulia karibu na mabaki hayo.

Ajali hiyo iliyohusisha mgongano kati ya treni hizo ulitokea takribani saa 7 mchana kwa saa za ndani (13:30 GMT) siku ya Ijumaa wakati treni ya Howrah Superfast Express inalotoka Bengaluru hadi Howrah, West Bengal, lilipogongana na Coromandel Express inayotoka Kolkata hadi Chennai.

Debabrata Mohanty, mhariri katika gazeti la Hindustan Times, ameiambia Al Jazeera kwamba mabehewa manne ya kwenye treni iliyoondoka kutoka Kolkata yalitoka kwenye njia muda mfupi kabla. "Hakuna anayejua jinsi ilivyokuwa, lakini ilikuwa ikisafiri karibu kilomita 100 kwa saa," alisema.

Muda mfupi baadaye, treni iliyokuwa ikitoka Bengaluru iligonga mabehewa mawili ya reli yaliyoacha njia. "Lakini majeruhi wengi walitokea kwa sababu treni hii iliacha njia, si kwa sababu ya treni mbili kugongana," Mohanty aliongeza.

Operesheni ya kina ya utafutaji na uokoaji imeanzishwa, ikihusisha mamia ya wafanyakazi wa idara ya zima moto, maafisa wa polisi na mbwa wa kunusa. Timu za Kikosi cha Kitaifa cha Kukabiliana na Maafa pia zilikuwepo eneo hilo.

Mtu mmoja aliyenusurika alisimulia namna alivyonusurika na jinamizi hilo la ajali alipokuwa ameamka wakati gari moshi alilokuwa amelala lilipopinduka.

"Usingizi wangu ulikatika na watu 10-15 waliniangukia," aliwaambia waandishi wa habari, alipokuwa ameketi chini gizani, hatua mbali na eneo la ajali.

"Niliumiza mkono na shingo yangu...niliona mtu amepoteza mkono wake, mtu amepoteza mguu...nilitoka pale na tangu wakati huo nimekuwa nikikaa hapa."

Juni 2, 2023, mamia ya vijana walijipanga nje ya hospitali ya serikali huko Odisha Soro ili kutoa damu. "Binafsi nina deni na ninashukuru kwa kujitolea na wote ambao wametoa damu kwa sababu nzuri," Jena aliandika kwenye tweet.

Jena aliielezea kama, "hii ni ajali mbaya na ya kutisha iliyohusisha treni tatu, treni mbili za abiria na treni moja ya mizigo".

Chanzo cha ajali hiyo kilikuwa kinachunguzwa, alisema Amitabh Sharma, msemaji wa Shirika la Reli la India. Taarifa za ajali hiyo hazikufahamika mara moja, wala mlolongo wa matukio hayo.

Waziri Mkuu wa Odisha, Naveen Patnaik ambaye anatarajiwa kuzuru eneo hilo leo alisema kipaumbele ni "kuondoa waliojeruhiwa na kuwapatia huduma hospitali. Hilo ndilo jambo letu la kwanza, kutunza walio hai."

Ripoti zinaonesha kuwa, mamia ya ajali hutokea kila mwaka kwenye reli ya India, huku nyingi zikilaumiwa kwa makosa ya kibinadamu au vifaa vya kuashiria vilivyopitwa na wakati.

Zaidi ya watu milioni 12 hupanda treni 14,000 kote India kila siku, wakisafiri kwa kilomita 64,000 (maili 40,000) ya njia.

Sudhanshu Mani, meneja mkuu wa zamani wa Shirika la Reli la India, aliiambia Al Jazeera kwamba uwekezaji umeingia katika matengenezo ya njia na hatua zingine za usalama katika miaka ya hivi karibuni.

"Ajali ya leo ni ya kusikitisha sana," Mani alisema, akiongeza kuwa majeruhi watakuwa wengi kutokana na idadi ya watu kwenye treni.

"Lakini idadi ya ajali imepungua na kuna miradi iliyopo njiani ya kuboresha usalama zaidi," alisema. Hakukuwa na uthibitisho rasmi wa jumla ya idadi ya abiria kwenye treni.

Maafa mabaya zaidi katika miaka ya hivi karibuni ni pamoja na moja la Oktoba 2018, wakati treni ilipita juu ya umati wa watu waliokuwa wakitazama fataki wakati wa tamasha la kidini nje kidogo ya Amritsar jijini Punjab hali iliyosababisha vifo vya takribani watu 60 na wengine kadhaa kujeruhiwa.

Takribani watu 146 waliuawa Novemba 2016, wakati treni ya abiria iliyokuwa ikisafiri kati ya miji ya Indore na Patna ilipoteleza kutoka kwenye reli. Zaidi ya watu 200 walijeruhiwa katika ajali hiyo.

Waziri Mkuu wa India Narendra Modi alisema Ijumaa kuwa, shughuli za uokoaji zinaendelea na "msaada wote unaowezekana" ulikuwa ukitolewa kwa wale walioathiriwa.

Modi aliongoza mkutano wa ngazi ya juu leo na alitarajiwa kuzuru eneo la ajali baadaye mchana, pamoja na hospitali ya Cuttack ambako wengi wa majeruhi walikuwa wakitibiwa, shirika la habari la ANI liliripoti.

Waziri wa Reli Ashwini Vaishnaw, ambaye alikuwa akikimbilia eneo la ajali siku ya Ijumaa, alitweet: "Nitachukua hatua zote zinazohitajika kwa operesheni za uokoaji."Vaishnaw pia alitangaza fidia ya takribani rupia milioni moja (dola 12,000) kwa familia za waliofariki, dola 2,400 kwa wale waliopata majeraha mabaya na dola 600 kwa watu walio na majeraha madogo.
Share:

NILIJUA RAFIKI YANGU KUMBE ANAMPA TUNDA MUME WANGU

 
Nimeishi na mume wangu kwa miaka mitatu, kwa muda huo nimekutana na mambo mengi sana hadi hatua ya kushindwa kula na kupata usingizi kutokana na visa ambavyo alikuwa ananifanyia.

Nilifanya kila namna ili niweze kutambua kosa langu lilikuwa lipi hasa lakini sikuweza kufanikiwa, bado mume wangu aliendelea kuleta visa pale nyumbani hadi mwenyewe nikawanashindwa nini tatizo hasa.


Kuna siku mume wangu hakwenda kazini kwa sababu hali ya kiafya haikuwa nzuri kabisa, ndipo rafiki yangu Halima alikuja nyumbani kumuona mgonjwa, Halima alileta chakula, matunda na soda.

Baada ya dakika chache mume wangu akaniagiza dukani kumleta maji ya baridi, niliporudi nikakuta Halima anamlisha mume wangu matunda sikuweza kufikiria vibaya maana mume alikuwa anajua Halima ni rafiki yangu.


Halima alikuwa anakuja pale nyumbani kila siku hadi mume wangu alipopona, hali ile ilianza kunitia wasiwasasi, ndipo nikaanza kuchunguza na kwa marafiki zangu wengi hadi nilipokuja kugundua kuwa mume wangu na Halima wana uhusiano.


Siku moja jioni nikiwa Facebook niliona mtu mmoja ametoa ushuhuda jinsi alivyoweza kusaidiwa na African Doctors kupata mchumba kutoka Marekani hadi wakafunga ndoa, katika stori yake alikuwa ameandika namba ya African Doctors ambazo ni +254 769 404965, nilichukua na wasiliana naye.


Nashukuru alinihudumia na kuniambia yeyote anayetaka kuivuruga ndoa yangu lazima atapatwa na jambo baya ikiwa ni pamoja kumkamata kwa mikono na macho yangu.

Siku ya pili yake asubuhi mume wangu alisema hajisikia vizuri na kuniagiza niende ofisini kwake nimletee Laptop yake, bila kukawia nikajiaandaa na kwenda, nikiwa njiani African Doctors alinipigia na kunambia nisiwe mbali na nyumbani kwangu siku hiyo.


Nilichukua Bodaboda haraka hadi ofisini na kurudi haraka nyumbani, kabla ya kufika mlangoni kwangu niliona viatu vya Halima mlangoni, niliposongea zaidi nikasikia sauti ya Halima akisema; "leo nakupa raundi mbili tu, sitaki cha umbea wako anikute, tukutane kwangu jioni".

Baada ya hayo maneno nikaingia chumbani haraka na kumkuta Halima na mume wangu wakiwa kitandani wakifanya mapenzi, nilimkamata Halima na kumnasa vibao na tangu wakati huo kaachana na mume wangu kabisa.

Wasiliana na African Doctors kwa namba; +254 769 404965, tembelea tovuti yao; www.african-doctors.com au watumie email; africandoctorheals@gmail.com.

Mwisho.


Share:

WAJASIRIAMALI WA BIDHAA ZA MAZIWA WAASWA KUZALISHA BIDHAA ZENYE UBORA

Afisa Udhibiti Ubora (TBS) Bw. Daniel Marwa akiwatembelea wazalishaji, wasindikaji, na wasambazaji wa bidhaa za maziwa na wajasiriamali kwa ujumla waliofika katika maonesho ya maadhimisho ya wiki ya maziwa kitaifa, mkoani Tabora .

**************

Wajasiriamali wa bidhaa za maziwa nchini wameaswa kuzalisha bidhaa zenye ubora ili kuweza kuhimili ushindani katika soko la ndani na kimataifa.

Haya yamesemwa na Bw Daniel Marwa, Afisa Udhibiti Ubora (TBS) wakati akiwatembelea washishiriki wa maonesho ya Maadhimisho ya Wiki ya Maziwa kitaifa yaliyofanyika Tabora katika mabanda yao.

Bw. Marwa alitumia fursa hii kutoa elimu kuhusu masuala ya viwango, namna bora ya uzalishaji wa bidhaa kwa ukizingatia namna bora ya usafi lengo likiwa ni kuzalisha bidhaa bora na salama kwa watumiaji wa mwisho.

Pia alipata nafasi za kuwaeleza namna wanavyoweza kupata alama ya ubora kwa kutumia huduma ya uthibishaji ubora wa bidhaa bila gharama yoyote kwa wajasiriamali kwani serikali kila mwaka hutengenga fedha ili wajasiriamali wadogo na wa kati wathibitishe ubora wa bidhaa zao ili waweze kufikia makoso makubwa ndani na nje ya nchi.

Kwa upande wake Afisa Masoko (TBS), Bi. Rhoda Mayugu amesema, TBS ilitumia maonesho hayo kuwaelimisha wananchi kuhusu faida na umuhimu wa kununua bidhaa zilizothibitishwa ubora wake pamoja na umuhimu wa kuangalia muda wa watumizi wa bidhaa husika kabla ya kununua bidhaa hizo kwani kwa kufanya hivyo hulinda usalama wa afya zao, na kuepuka hasara za kiuchumi zinazoweza kujitokeza

Vita ya bidhaa hafifu sokoni si ya TBS pekee endapo wananchi watashirikiana na TBS kwa kutokununua bidhaa hafifu na kutoa taarifa wanapokutana na bidhaa hafifu ama zile zilizozuiliwa kutumika ni hakika Tanzania haitokuwa na bidhaa hafifu kwani wazalishaji, waingizaji wa bidhaa hizo hawatapata masoko kabisa hivyo kupelekea kuzalisha, kusambaza, kuningiza na kuuza bidhaa bora.



Afisa Udhibiti Ubora (TBS) Bw. Daniel Marwa akiwatembelea wazalishaji, wasindikaji, na wasambazaji wa bidhaa za maziwa na wajasiriamali kwa ujumla waliofika katika maonesho ya maadhimisho ya wiki ya maziwa kitaifa, mkoani Tabora .
TBS imewatembelea wajasiriamali hao kwa lengo la kutoa elimu kuhusu masuala ya viwango na kuwakumbusha kuhusu huduma ya kupata alama ya ubora bila gharama yoyote.
Share:

JE UNA TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME??? FULL POWER NDIYO SULUHISHO

 


Upungufu wa nguvu za kiume ni hali ya kushindwa kufanya tendo la ndoa kikamilifu ,shughuli ya tendo la ndoa huhusisha akili, homoni, neva, misuli, hisia na mirija ya damu. Upungufu wa nguvu za kiume huashiria kutokuwa sawa kiafya hivyo ni tatizo linalohitaji tiba.

CHANZO CHA TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME

Tatizo la nguvu za kiume lina vyanzo vingi ambavyo mara nyingi wengi huvipuuza, hivyo vyanzo huathiri taratibu na vingine huathiri haraka, tunashauri watu kuwa makini sana ili kujiimarisha vizuri. Kuna mitindo ya maisha inayoweza kukuweka hatarini kupata tatizo la nguvu za kiume nayo ni pamoja na;


1. Kuwa na halemu (Cholesterol) na Shinikizo la damu (B.P) au ugonjwa wa moyo

2. Kuvuta sigala na unywaji wa pombe

3. Uzito kupita kiasi na unene uliozidi

4. Ulaji holela wa vyakula vyenye mafuta mengi na sukari nyingi

5. Kisukari

6. Kuwa na mawazo na wasiwasi

7. Matumizi ya madawa mbalimbali

8. Umri hasa wazee

9. Utumiaji wa vinywaji vinavyobadili hali ya mwili

10. Kuwa na tatizo la kibofu

11. Tabia za kujichua kwa muda mrefu

12. Kutopata usingizi kamili

13. Matumizi makubwa ya dawa zenye kemikali za kutibia magonjwa kama kansa, vidonda vya tumbo, moyo, kisukari, B.P, na magonjwa mengine


DALILI ZA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME

Dalili za kuonesha kuwa una tatizo la upungufu wa nguvu za kiume karibia zote zinahusiana na hali itakayo onekana katika tendo la ndoa au mda wa kujamiiana, hizo dalili zake ni kama;


1. Kuwahi kufika kileleni

2. Kukosa hamu ya mapenzi

3. Kushindwa kurudia tendo la ndoa

4. Uume kusimama kwa ulegevu au kushindwa kusimamisha

5. Kuchoka sana baada ya tendo la ndoa na hata kukinai kabisa au hata kusikia kichefuchefu; Miguu, uso na tumbo kuvimba na kujaa maji

6. Kuhisi maumivu wakati wa tendo la ndoa au baada ya tendo hilo

7. Kuchelewa sana kufika kileleni (au kushindwa kufika kileleni kabisa)

8. Kukosa pumzi na uchangamfu wa mwili katika utendaji


TIBA SAHIHI YA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME

FULL POWER

⇨Ni dawa ya vidonge ya miti shamba inaongeza nguvu za kiume na kutibu kabisa tatizo hilo.

⇨Inaongeza hamu ya tendo la ndoa

⇨Inakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya Dakika 30 na kurudia tendo zaidi ya mara nne na zaidi.


ZAT 50
⇨ Inarutubisha maumbile ya uume na kunenepesha urefu nchi 6,unene sentimita 4

⇨Dawa hii ni ya kutibu kabisa tatizo hilo.


Pia tunatibu Magonjwa mengine kama


Matatizo ya pumu,Bawasiri, vidonda vya tumbo, Kisukari, Magonjwa sugu ya zinaa,Kaswende,U.T.I , kiuno,miguu kuwaka moto, Fangasi sehemu za Siri, kupunguza unene wa mwili,tumbo kuunguruma,kujaa gesi, matatizo ya uzazi kwa wanawake, kurutubisha mbegu za uzazi kwa akina baba, matatizo ya meno tunatibu bila kung’oa


Ndugu mteja Epuka midawa inayouzwa mitaani ambayo sio sahihi kwa matumizi ya binadamu JALI AFYA YAKO OKOA NDOA NA MAISHA YAKO

Kliniki yetu inapatikana Zanzibar, Dar es salaam na Shinyanga

Wasiliana nasi kwa simu namba 071770 22 27 au 0754568767  utatumiwa sehemu yoyote ulipo
Share:

Ngoma Mpyaa!! BHUDAGALA - MAGHULU ABHILI


Msanii Maarufu wa Nyimbo za Asili Bhudagala Ng'wana Malonja ameachia ngoma mpya inaitwa Maghuluabhili
 
Share:

Video : MCHELE MCHELE - NKEONE

 

Share:

Friday 2 June 2023

MHE. KATAMBI ATAKA UBUNIFU WA MAWASILIANO OFISI YA WAZIRI MKUU




Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Patrobas Katambi akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha kuandaa mpango wa pamoja wa mawasiliano wa ofisi hiyo pamoja na taasisi zake kilichofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), mkoani Arusha tarehe 1 Mei, 2023.


Sehemu ya Wakuu na Maafisa wa Vitengo vya Mawasiliano na Uhusiano wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Patrobas Katambi (hayupo pichani) wakati wa kikao kazi hicho kilichofanyika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), mkoani Arusha tarehe 1 Mei, 2023.


Mkuu wa Kitengo cha Mawasilino Serikalini kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Ibrahim Hamidu akieleza jambo wakati wa kikao kazi hicho.


Mkurugenzi wa Sera na Mipango kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Said Mabie akitoa elimu kuhusu Mpango Mkakati wa Ofisi hiyo pamoja na taasisi zake wakati wa kikao kazi hicho kilichofanyika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), mkoani Arusha.


Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Bi. Laura Kunenge akichangia jambo wakati wa kikao kazi hicho kilicholenga kuandaa mpango wa pamoja wa mawasiliano wa Ofisi ya Waziri Mkuu Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu na Taasisi zake.


Naibu waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Patrobas Katambi (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Wakuu na Maafisa wa vitengo vya Mawasiliano na Uhusiano baada ya kufungua kikao kazi cha kuandaa mpango wa pamoja wa mawasiliano wa ofisi hiyo pamoja na taasisi zake kilichofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), mkoani Arusha tarehe 1 Mei, 2023.





Na: Mwandishi Wetu

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Patrobas Katambi amewataka Wakuu wa Vitengo na Maafisa Mawasiliano wa Ofisi hiyo pamoja na Taasisi zake kuwa wabunifu na kuongeza wigo wa kujitangaza.

Mhe. Katambi ameyasema hayo Juni 1, 2023 jijini Arusha katika kikao kazi cha kuandaa mpango wa pamoja wa mawasiliano kati ya Ofisi hiyo na taasisi zake ambazo ni Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa watumishi wa Umma (PSSSF), Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Wakala wa Usalama na Afya Mahala Pa Kazi (OSHA) na Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA).

Naibu Waziri Katambi amesema vitengo vya mawasiliano vinapaswa kufanya kazi kwa kuzingatia mabadiliko ya teknolojia na kuja na ubunifu utakaorahisha kufikisha taarifa muhimu kwa umma.

Pia, ameelekeza Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo na Wakurugenzi wa Taasisi hizo kuangalia umuhimu wa kuongeza bajeti kwa vitengo hivyo ili kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi. Awali, Mkurugenzi wa Sera na Mipango, Said Mabie na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Ofisi hiyo, Ibrahim Hamidu wameeleza madhumuni ya kikao hicho na umuhimu wa kuwa na mpango huo katika kusaidia kuwa na uratibu mzuri wa kufikisha taarifa kwa umma.
Share:

DCEA YAKAMATA MAGUNIA 731 YA BANGI, YATEKETEZA HEKARI 308 ZA MASHAMBA YA BANGI

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeendelea na operesheni ya kukamata, kuharibu na kuteketeza dawa za kulevya aina ya bangi katika wilaya ya ARUMERU mkoani Arusha na kufanikiwa kukamata jumla ya gunia 731 za bangi kavu pamoja na kuteketeza hekari 308 za mashamba ya bangi.


Operesheni iliyofanyika jana tarehe 01 June, 2023, katika kijiji cha Lesinoni, jumla ya gunia 249 ya bangi kavu yalikamatwa huku hekari 207 za mashamba ya bangi yaliteketezwa huku operesheni iliyofanyika tarehe 31 Mei 2023, katika kijiji cha Kisimiri juu, Mamlaka ilikamata gunia 482 za bangi na kuteketeza jumla ya hekari 101 za mashamba ya bangi.


Watuhumiwa 9 wamekamatwa kuhusiana na matukio hayo.


Kwa mujibu wa taarifa kwa Umma iliyotolewa na Kamishna Jenerali Aretas Lyimo Leo tarehe 02 June, 2023; operesheni hii imefanyika kufuatia agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan la kufanya operesheni nchi nzima ili kuhakikisha dawa za kulevya zinatokomezwa nchini. Operesheni hizi zimefanyika siku moja baada ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama (Mb) kutoa taarifa ya hali ya Dawa za Kulevya nchini kwa mwaka 2022 ambayo iliitaja mikoa ya Arusha, Iringa, Morogoro na Manyara kujihusisha na kilimo cha bangi kwa kiasi kikubwa.


Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya kwa kushirikiana na Vyombo vingine vya Ulinzi na Usalama itaendelea kufanya operesheni za mara kwa mara katika maeneo yote nchini ili kuhakikisha kilimo cha bangi na mirungi kinatokomezwa kabisa na wananchi kujikita katika kilimo cha mazao mbadala ya biashara na chakula.
Share:

MKULIMA APIGWA RISASI


Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Walter Kaaya (34) mkazi wa Simanjiro mkoani Manyara amenusurika kifo kwa kupigwa risasi na Paulo Laizer (43) mfugaji wilayani humo kufuatia mzozo wa mifugo kukutwa shambani ikiharibu mazao.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Manyara RPC George Katabazi amesema majeruhi alikuwa akiondoa ng'ombe hizo kwenye shamba lake la ekari 200 zilizokuwa na mazao mbalimbali yakiweno mahindi na maharagwe

Wakati anaziondoa ng'ombe shambani mtuhumiwa alifika na kuibua mzozo na kuchukua silaha yake aina ya bastola na kumpiga risasi begani

Majeruhi amekimbizwa katika hospitali ya KCMC Moshi kwa matibabu zaidi.

Chanzo - EATV
Share:

Wimbo Mpya : MANG'WENG'WE - SHIKOME

 

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger