Wednesday 2 February 2022

OFISI YA TAIFA YA UKAGUZI YAKUTANA NA WAANDISHI WA HABARI WA MITANDAO YA KIJAMII


Msaidizi wa Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Kanda ya Ziwa, Anna Masanja akizungumza wakati akifungua Kikao Kazi kati ya Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi na Waandishi wa Habari kutoka vyombo vya habari vinavyotumia Mitandao ya Kijamii ‘Online Media Platforms’.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi imekutana na Waandishi wa Habari kutoka vyombo vya habari vinavyotumia Mitandao ya Kijamii ‘Online Media Platforms’ nchini kwa ajili ya kuwajengea uwezo kuhusu mambo mbalimbali kuhusu Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi ili kuongeza weledi zaidi wanapoandika habari zao.

Kikao kazi hicho cha siku tatu kikishirikisha waandishi wa habari wa mitandao ya kijamii kutoka Kanda ya Ziwa na mikoa mingine nchini kimefanyika leo Jumatano Februari 2,2022 katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Programu ya Kujenga uwezo endelevu wa kupambana na rushwa Tanzania - Building Sustainable Anti – Corruption Action Tanzania (BSAAT) kwa ufadhili wa Serikali ya Uingereza na Umoja wa Ulaya.

Akifungua kikao hicho, Msaidizi wa Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Kanda ya Ziwa, Anna Masanja amesema kikao hicho kinalenga kuwajengea uwezo waandishi wa habari kupitia mitandao ya kijamii juu ya utoaji wa taarifa za ubadhirifu na viashiria vya rushwa zinazotokana na taaifa ya mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.

“Waandishi wa habari mitandaoni ni wadau muhimu na kwa kuzingatia ukweli huu ndiyo maana tumewaita hapa kwa ajili ya kupeana ujuzi na ufahamu wa masuala ya sheria zinazosimamia utekelezaji wa majukumu ya ofisi yetu sambamba na kukumbushana masuala muhimu katika kutekeleza jukumu lenu la kuwasilisha taarifa zinazohusu masuala ya ubadhirifu yanayoibuliwa na taarifa ya Ukaguzi na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali”,amesema Masanja.

“ Imani yetu kuu ni kuwa mkielewa vizuri mtatusaidia sana katika kuwaelewesha wadau na wananchi kwa ujumla namna ya kusimamia rasilimali na fedha kwa ajili ya maendeleo ya taifa letu. Na kupitia vyombo vyenu vya habari mtatusaidia sana katika kuchambua kwa ufasaha kwa kutumia lugha nyepesi ambayo kila mwananchi ataweza kuielewa vizuri na kufanya maamuzi sahihi ya kusimamia matumizi mazuri ya rasilimali za taifa”,ameongeza.

Masanja amesema hii ni mara ya kwanza kwa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi kuhusisha waandishi wa habari kupitia mitandao ya kijamii pekee yaani Online Tvs, Blogs, kurasa mitandao ya vyombo vya habari (digital platforms) zenye wafuasi wengi mfano Twitter, Facebook na Instagram.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Msaidizi wa Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Kanda ya Ziwa, Anna Masanja akizungumza wakati akifungua Kikao Kazi kati ya Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi na Waandishi wa Habari kutoka vyombo vya habari vinavyotumia Mitandao ya Kijamii ‘Online Media Platforms’ nchini katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza leo Jumatano Februari 2,2022. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Msaidizi wa Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Kanda ya Ziwa, Anna Masanja akizungumza wakati akifungua Kikao Kazi kati ya Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi na Waandishi wa Habari kutoka vyombo vya habari vinavyotumia Mitandao ya Kijamii ‘Online Media Platforms’ nchini
Msaidizi wa Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Kanda ya Ziwa, Anna Masanja akizungumza wakati akifungua Kikao Kazi kati ya Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi na Waandishi wa Habari kutoka vyombo vya habari vinavyotumia Mitandao ya Kijamii ‘Online Media Platforms’ nchini
Mkurugenzi Huduma za Sheria - Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi, Elieshi Saidimu akizungumza kwenye Kikao Kazi kati ya Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi na Waandishi wa Habari kutoka vyombo vya habari vinavyotumia Mitandao ya Kijamii ‘Online Media Platforms’ nchini
Waandishi wa Habari kutoka vyombo vya habari vinavyotumia Mitandao ya Kijamii ‘Online Media Platforms’ wakiwa ukumbini.
Mratibu wa Programu ya BSAAT inayojengea Taasisi za Serikali uwezo wa kudhibiti Rushwa, Dkt. Bonaventure Baya akizungumza kwenye Kikao Kazi kati ya Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi na Waandishi wa Habari kutoka vyombo vya habari vinavyotumia Mitandao ya Kijamii ‘Online Media Platforms’
Mratibu wa Programu ya BSAAT inayojengea Taasisi za Serikali uwezo wa kudhibiti Rushwa, Dkt. Bonaventure Baya akizungumza kwenye Kikao Kazi kati ya Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi na Waandishi wa Habari kutoka vyombo vya habari vinavyotumia Mitandao ya Kijamii ‘Online Media Platforms’
Afisa Sheria Mwandamizi - Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi na Mratibu wa Programu ya BSAAT, Frank Sina akizungumza kwenye Kikao Kazi kati ya Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi na Waandishi wa Habari kutoka vyombo vya habari vinavyotumia Mitandao ya Kijamii ‘Online Media Platforms’ nchini
Mkurugenzi Huduma za Sheria - Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi, Elieshi Saidimu akitoa mada kuhusu Mambo muhimu kuhusu ofisi ya Taifa ya Ukaguzi kwenye Kikao Kazi kati ya Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi na Waandishi wa Habari kutoka vyombo vya habari vinavyotumia Mitandao ya Kijamii ‘Online Media Platforms’ nchini
Mkurugenzi Huduma za Sheria - Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi, Elieshi Saidimu akitoa mada kuhusu Mambo muhimu kuhusu ofisi ya Taifa ya Ukaguzi kwenye Kikao Kazi kati ya Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi na Waandishi wa Habari kutoka vyombo vya habari vinavyotumia Mitandao ya Kijamii ‘Online Media Platforms’ nchini
Waandishi wa Habari kutoka vyombo vya habari vinavyotumia Mitandao ya Kijamii ‘Online Media Platforms’ wakiwa ukumbini.
Waandishi wa Habari kutoka vyombo vya habari vinavyotumia Mitandao ya Kijamii ‘Online Media Platforms’ wakiwa ukumbini.
Waandishi wa Habari kutoka vyombo vya habari vinavyotumia Mitandao ya Kijamii ‘Online Media Platforms’ wakiwa ukumbini.
Waandishi wa Habari kutoka vyombo vya habari vinavyotumia Mitandao ya Kijamii ‘Online Media Platforms’ wakiwa ukumbini.
Waandishi wa Habari kutoka vyombo vya habari vinavyotumia Mitandao ya Kijamii ‘Online Media Platforms’ wakiwa ukumbini.
Waandishi wa Habari kutoka vyombo vya habari vinavyotumia Mitandao ya Kijamii ‘Online Media Platforms’ wakiwa ukumbini.
Waandishi wa Habari kutoka vyombo vya habari vinavyotumia Mitandao ya Kijamii ‘Online Media Platforms’ wakiwa ukumbini.

Waandishi wa Habari kutoka vyombo vya habari vinavyotumia Mitandao ya Kijamii ‘Online Media Platforms’ wakiwa ukumbini.
Waandishi wa Habari kutoka vyombo vya habari vinavyotumia Mitandao ya Kijamii ‘Online Media Platforms’ wakiwa ukumbini.
Waandishi wa Habari kutoka vyombo vya habari vinavyotumia Mitandao ya Kijamii ‘Online Media Platforms’ wakiwa ukumbini.
Waandishi wa Habari kutoka vyombo vya habari vinavyotumia Mitandao ya Kijamii ‘Online Media Platforms’ wakiwa ukumbini.
Waandishi wa Habari kutoka vyombo vya habari vinavyotumia Mitandao ya Kijamii ‘Online Media Platforms’ wakiwa ukumbini.
Maafisa kutoka Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wakiwa ukumbini
Washiriki wa Kikao Kazi kati ya Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi na Waandishi wa Habari kutoka vyombo vya habari vinavyotumia Mitandao ya Kijamii ‘Online Media Platforms’ wakipiga picha ya pamoja.
Washiriki wa Kikao Kazi kati ya Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi na Waandishi wa Habari kutoka vyombo vya habari vinavyotumia Mitandao ya Kijamii ‘Online Media Platforms’ wakipiga picha ya pamoja.

Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Share:

BENKI YA CRDB YATANGAZA UFADHILI WA MASOMO WA SH. MILIONI 10 KWA WACHEZAJI 10 BORA CRDB BANK TAIFA CUP

Benki ya CRDB imetangaza ufadhili wa masomo wa Shilingi Milioni 10 kwa wachezaji 10 bora wa mashindano ya taifa ya mpira wa kikapu “CRDB Bank Taifa Cup” 2021 katika hafla iliyoonyeshwa mubashara kupitia chaneli ya michezo ya AzamTV.

Akizungumza katika hafla ya kutangaza ufadhili huo, Meneja Mwandamizi wa Uwekezaji katika Jamii Benki ya CRDB, Joycelean Makule amesema ufadhili huo wa masomo kwa wachezaji ni muendelezo wa jitihada za Benki ya CRDB katika kuwawezesha vijana wa kitanzania kupitia michezo.

Joycelean alisema Benki hiyo kupitia sera yake ya Uwezeshaji katika Jamii (CSI Policy) imekuwa ikiwekeza katika michezo ya vijana kwa kuamini kuwa inasidia kuongeza ushiriki wao katika shughuli mbalimbali ikwamo elimu ili kusaidia kuwajenga kwa ajili ya maisha ya baadae.
“Katika CRDB Bank Taifa Cup wapo vijana wengi ambao bado wapo masomoni katika ngazi mbalimbali. Hivyo Benki iliona ni vyema kuambatanisha suala la elimu na michezo kwa kutoa ufadhili wa masomo vijana ambao wameonyesha uwezo mkubwa katika mashindano ya CRDB Bank Taifa Cup,” alisema Joycelean.

Akizungumzia kuhusu msukumo uliopelekea Benki hiyo kudhamini masomo ya wachezaji wa mpira wa kikapu Joycelean alisema mchezo wa mpira wa kikapu umekuwa haupewi sana kipaumbele kulinganisha na michezo mingine, hivyo kupelekea kuwakatisha tamaa vijana wengi ambao wamekuwa wakionyesha vipaji katika mchezo huo.
“Baada ya mchakato mrefu wa kufanya tathimini ya uwezo uliooneshwa na vijana pamoja na kufatilia taarifa zao za kielimu kwa kushirikiana na Shirikisho la Mpira wa Kikapu Tanzania (TBF), tumefanikiwa kukamilisha zoezi hilo na leo tupo hapa kwa ajili ya kutangaza vijana waliofanikiwa kupata nafasi hizo za ufadhili wa masomo kwa mwaka 2021/2022,” alisema Joycelean ikibainisha.

Huu ni mwaka wa pili kwa Benki ya CRDB kutoa ufadhili wa masomo kwa wachezaji bora wa mchezo wa mpira wa kikapu kupitia CRDB Bank Taifa Cup. Mwaka jana benki hiyo ilitoa ufadhili wa masomo wa jumla ya shilingi milioni 50 kwa vijana 25. “Tunajivunia kuendelea kutoa ufadhili wa masomo kwa vijana kupitia mchezo huu kwani tunaamini utasaidia kufikia ndoto zao kupitia elimu,” aliongezea Joycelean.
Akizungumza kwa niaba ya vijana waliopata ufadhili wa masomo, mchezaji wa timu ya wanawake ya mpira wa kikapu mkoa wa Kilimanjaro Jesca Mbowe ambaye anasoma katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) shahada ya usimamizi wa utalii ameishukuru Benki ya CRDB kwa ufadhili huo, huku akisema utakuwa chachu kwao kusoma kwa bidii ili kufikia malengo yao.

Kwaupande wake Makamu wa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Kikapu Tanzania, Rwehabura Balongo ameishukuru Benki ya CRDB kwa kuendelea kuwekeza katika mpira wa kikapu huku akisema udhamini huo wa masomo utakwenda kuleta hamasa zaidi kwa vijana wengi kushiriki katika mchezo huo.
Balongo aliishukuru pia Benki ya CRDB kwa kuendelea kuwa mdhamini wa mashindano ya taifa ya mpira wa kikapu ambapo tokea benki hiyo ianze kushirikiana na TBF kumekuwa na mwamko mkubwa katika mchezo huo. Benki ya CRDB mwaka jana iliongeza udhamini katika Taifa Cup kufikia shilingi 300 ambapo timu 36 za mpira wa kikapu kwa upande wa wanaume na wanawake zilichuana vikali.

Timu za wanawake na wananume za mpira wa kikapu mkoa wa Dar es Salaam ziliibuka kidedea katika mashindano hayo yaliyofanyika katika viwanja vya Chinangali Dodoma.

Share:

KARIBU BEHAC KWA HUDUMA YA CHAKULA, BAA, PHARMACY NA MIAMALA YA FEDHA


Karibu Behac Company Limited kwa huduma za Chakula halisi cha Kitanzania/Kiafrika, Bar, Order, Miamala ya Fedha, Pharmacy .Pia tunakodisha viti, meza na sahani. 

Tunapatikana Bwalo la Polisi Mjini Shinyanga . Wasiliana nasi kwa simu namba 0782767034 / 0753474488  Email : info@behac.co.tz  Website : www.behac.co.tz


Share:

NDEGE INAYOTUMIA UMEME KUANZA MAJARIBIO, HAITUMII MAFUTA




TEKNOLOJIA na masuala ya usafirishaji inazidi kuwa kubwa, wakati wengine wakibuni magari mapya yanayotumia umeme badala ya mafuta, Israel Eviation wamekuja na kitu cha tofauti.

Kampuni ya Israel Eviation imetengeneza ndege ya kwanza ya abiria duniani ambayo inatumia umeme kwa asilimia 100 bila mafuta hata tone, ambayo imefanyiwa majaribio ya awqali wiki iliyopita huko Arlington Municipal Airport, Kaskazini mwa Seattle huko Washington nchini Marekani.


Ndege hiyo ya Alice sasa imebakiza wiki chache ili kufanya safari yake ya kwanza tangu itengenezwe ikiwa na uwezo wa kubeba Abiria 9 na marubani wawili na kuruka kwa 250 kts, au maili 287 287 kwa saa. Ikumbukwe kuwa ndege aina ya Boeing 737 ina mwendokasi wa maili 588 kwa saa.

Kampuni hiyo iliyomtengeneza Alice ambayo imejikita katika usafiri wa anga kwa teknolojia ya umeme, inaamini kwamba ndege zinazotumia umeme zenye uwezo wa kubeba Abiria 20 mpaka 40 zitakuwa sokoni ndani ya miaka 7 hadi 10 ijayo (mwaka 2029 – 2032).


Ndege hiyo iliyoanza kutengenezwa mwaka 2019 imepitia katika mabadiliko ya aina mbalimbali na majaribio kadhaa ikiwemo majaribio la mwendokasi kuanzia speed ya chini mpaka speed kubwa ambapo majaribio mengine yalifanyika Desemba, mwaka jana.

Alice sasa itafanyiwa majaribio mengine ya speed tofauti tofauti, umeme wake ambapo inatumia betri na uwezo wake, mifumo ya steering, brak, na uratibu wa masafa.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO FEBRUARI 2,2022

Magazetini leo Jumatano February 2,2022






Share:

Tuesday 1 February 2022

Dkt. TULIA ACKSON NDIYE SPIKA WA BUNGE LA TANZANIA



Mbunge wa Mbeya Mjini, Dk. Tulia Ackson amechaguliwa kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kupata kura zote 376 za wabunge katika Uchaguzi uliofanyika leo Jumanne Februari 1, 2022 bungeni jijini Dodoma.

Akitangaza matokeo hayo, Mwenyekiti wa Uchaguzi huo, William Lukuvi amesema Mhe. Dkt. Tulia amewashinda wagombea wengine nane ambao wote wamepata kura 0 na hakuna kura iliyoharibika.
Share:

ZUHURA YUNUS, MKURUGENZI MPYA WA MAWASILIANO YA RAIS IKULU


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger