Tuesday 28 December 2021

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE DESEMBA 28,2021


Magazetini leo Jumanne December 28 2021



MAGAZETI MENGINE TUNAKULETEA HIVI PUNDE...
Share:

Monday 27 December 2021

Technician 1 – UG Geotech at Geita Gold Mining Ltd

ABOUT GEITA GOLD MINING LTD   Geita Gold Mining Ltd (GGML) is Tanzania’s leading gold producer with a single operation in Geita Region. The company is a subsidiary of AngloGold Ashanti, an international gold producer headquartered in South Africa, with operations in more than ten countries, in four continents. The mine is situated in the […]

This post Technician 1 – UG Geotech at Geita Gold Mining Ltd has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Operator 1 – Equipment (Gold Room)

ABOUT GEITA GOLD MINING LTD   Geita Gold Mining Ltd (GGML) is Tanzania’s leading gold producer with a single operation in Geita Region. The company is a subsidiary of AngloGold Ashanti, an international gold producer headquartered in South Africa, with operations in more than ten countries, in four continents. The mine is situated in the […]

This post Operator 1 – Equipment (Gold Room) has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

MWAMBA WA AFRIKA, ASKOFU DESMOND TUTU AFARIKI DUNIA..HII HAPA HISTORIA YAKE



IKULU ya Afrika Kusini imetangaza kuwa Mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel na mpigania haki nchini Afrika Kusini, Askofu Desmond Tutu amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 90.

Taarifa ya ofisi ya Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa imeeleza kuwa Rais amesikitishwa na kifo hicho na kwa niaba ya raia wote wa Afrika Kusini anatoa pole kwa mke wa Askofu Tutu na familia nzima ya askofu huyo.

Rais Cyril Ramaphosa amesema kwamba kifo cha muhudumu huyo wa kanisa kimeadhimisha kwa mara nyengine misiba ya kizazi muhimu cha taifa hilo .


Alisema kwamba Askofu Tutu alisaidia katika kurithi taifa la Afrika kusini lililokombolewa .


Tutu alikuwa mmojawapo ya viongozi maarufu nchini humo na Ugenini.

Alishiriki katika vita dhidi ya ubaguzi wa rangi akishirikiana na Nelson Mandela, na kuchochea harakati za kukomesha sera ya ubaguzi wa rangi iliyotekelezwa na serikali ya wazungu wachache dhidi ya weusi walio wengi nchini Afrika Kusini kuanzia 1948 hadi 1991.


Alitunukiwa tuzo ya Nobel mwaka 1984 kwa jukumu lake katika mapambano ya kukomesha mfumo wa ubaguzi wa rangi.


Kifo cha Tutu kinajiri wiki chache tu baada ya Rais wa mwisho wa enzi za ubaguzi wa rangi FW de Clerk , kufariki akiwa na umri wa miaka 85.


Rais Ramaphosa alisema kwamba Tutu alikuwa kiongozi maarufu wa dini , mwanaharakati dhidi ya ubaguzi wa rangi na mpiganiaji wa haki za binadamu kote duniani.


Alimuelezea kuwa mtu mzalendo , kiongozi mwenye misimamo aliyetoa maana kwa ufahamu wa Biblia kwamba imani bila matendo ni sawa na kifo.


"Alikuwa mtu mwenye ufahamu wa ajabu, mwadilifu na asiyeweza kushindwa dhidi ya nguvu za ubaguzi wa rangi, pia alikuwa mpole na mwenye huruma kwa wale ambao walikuwa wamepitia dhuluma na vurugu chini ya ubaguzi wa rangi, mbali na watu waliokandamizwa kote ulimwenguni."


Alitawazwa kama padre mwaka wa 1960, na kuhudumu kama askofu wa Lesotho kuanzia 1976-78, askofu msaidizi wa Johannesburg na mkuu wa parokia ya Soweto.

Alikua Askofu wa Johannesburg mnamo 1985, na akateuliwa kuwa Askofu Mkuu wa kwanza mweusi wa Cape Town. Alitumia nafasi yake ya hadhi ya juu kuzungumzia ukandamizaji dhidi ya watu weusi nchini mwake, siku zote akisema nia yake ni ya kidini na si ya kisiasa.

Desmond Tutu alikuwa askofu aliyekuwa na tabasamu na misimamo iliowavutia marafiki na wengi waliomuenzi duniani.


Akiwa kiongozi wa mweusi wa dini mwenye umaarufu mkubwa duniani , alihusika sana katika harakati dhidi ya utawala wa wazungu walio wachache lakini akasisitiza kuwa lengo lake kuu lilikuwa la kidini na sio kisiasa.


Aliteuliwa na rais Nelson Mandela kuongoza tume ya ukweli na maridhiano ilioundwa kuchunguza uhalifu uliotekelezwa na pande zote mbiIi wakati wa enzi za ubaguzi wa rangi


Pia alisifika kwa kuanzisha neno taifa la Rainbow kuelezea mchanganyiko wa watu wa makabilay, rangi na dini tofauti nchi Afrika kusini . Desmond Mpilo Tutu alizaliwa 1931 katika mji mdogo wenye migodi ya dhahabu wa Transvaal.


Alifuata nyayo za babake kwa kuwa mwalimu , kabla ya kuwacha kazi hiyo baada ya kupitishwa kwa sheria ya elimu ya Bantu Education Act 1953 ambayo ilipinga ubaguzi wa rangi shuleni.


Alijiunga na kanisa na akapata ushawishi mkubwa kutoka kwa viongozi weupe wa dini nchini humo , hususan Askofu Trevor Huddleston aliyepinga sana unaguzi wa rangi.

Tutu (kulia) akiwa na wanachama wenzake wa chuo cha Pretoria Bantu Normal College mwaka 1961


Alihudumu kama askofu wa Lesotho kuanzia 1976-78, askofu msaidizi wa Johannesburg na mkuu wa parokia ya Soweto, kabla ya kuteuliwa kuwa askofu wa Johannesburg.


Alikuwa smkuu wa chuo ndipao alipoanza kupaza sauti yake dhidi ya ukosefu wa haki nchini Afrika Kusini na tena kuanzia 1977 alipokuwa katibu mkuu wa Baraza la Makanisa la Afrika Kusini.


Akiwa mtu mashuhuri kabla ya uasi wa 1976 katika vitongoji vya watu weusi, ilikuwa miezi kadhaa kabla ya matukio ya ghasia za Soweto ambapo alijulikana kwa mara ya kwanza na Wazungu wa Afrika Kusini kama mwanaharakati wa mageuzi.


Juhudi zake zilimfanya kutunukiwa Tuzo ya Amani ya Nobel mwaka wa 1984 katika kile kilichoonekana kuwa pingamizi kuu dhidi ya jumuiya ya kimataifa kwa watawala weupe wa Afrika Kusini.


Kutawazwa kwa Desmond Tutu kama Askofu Mkuu wa Cape Town kulihudhuriwa na Askofu Mkuu wa wakati huo wa Canterbury, Dk Robert Runcie, na mjane wa Martin Luther King.


Akiwa mkuu wa Kanisa la Anglikana nchini Afrika Kusini, aliendelea kufanya kampeni kikamilifu dhidi ya ubaguzi wa rangi. Mnamo Machi 1988, alitangaza: "Tunakataa kuchukuliwa kama kifutioa miguu cha mlango ili serikali kufuta buti zake."


Miezi sita baadaye, alinusurika kifungo jela baada ya kutoa wito wa kususia uchaguzi wa manispaa.


Alikamatwa katika wingu la gesi ya vitoa machozi mnamo Agosti 1989, wakati polisi walichukua hatua dhidi ya watu waliokuwa wakitoka kanisani katika kitongoji kimoja karibu na Cape Town, na mwezi uliofuata alikamatwa baada ya kukataa kuondoka kwenye mkutano uliopigwa marufuku.

Desmond Tutu akiwa akitembelea mji chini ua uangalizi wa maafisa wa polisi


Akiwa askofu mkuu, wito wake wa vikwazo vya adhabu dhidi ya Afrika Kusini uligonga vichwa vya habari ulimwenguni kwasababu uliambatana na kulaani vikali ghasia


Mnamo 1985, Tutu na askofu mwingine kwa ujasiri na kwa kasi walimuokoa muhudumu wa polisi alipokuwa akishambuliwa na kukaribia kuchomwa hadi kufa na umati uliojaa ghadhabu katika kitongoji kimoja mashariki mwa mji wa Afrika Kusini, Johannesburg.


Makasisi hao waliusukuma umati huo na kumvuta ili kumlinda mwanamume huyo aliyekuwa akivuja damu, nusu-fahamu, kabla tu ya tairi iliyomwagiwa petroli shingoni kuwashwa.


Tutu baadaye aliwakemea washambuliaji wa mtu huyo, akiwakumbusha "umuhimu wa kutumia njia za haki kwa ajili ya mapambano ya haki ".


Tutu aliunga mkono mabadiliko yaliyotangazwa na Rais FW de Klerk mara baada ya kuchukua madaraka. Mabadiliko hayo ni pamoja na kuondolewa kwa marufuku kwa chama cha ANC na kuachiliwa kwa Nelson Mandela Februari 1990.


Muda mfupi baadaye, Tutu alitangaza kupiga marufuku makasisi kujiunga na vyama vya kisiasa, jambo ambalo lililaaniwa na makanisa mengine.

Kuhusu Israel na Palestina


Hakuwahi kusita kutoa maoni yake. Mnamo mwezi Aprili 1989, alipokwenda mjini Birmingham nchini Uingereza, alikosoa kile alichokiita "taifa mbili" Uingereza, na kusema kuna watu weusi wengi katika magereza ya nchi hiyo.


Baadaye aliwakasirisha Waisraeli wakati wa hija ya Krismasi kwenye ardhi hiyo takatifu, akiwalinganisha Waafrika Kusini weusi na Waarabu katika ukingo wa Magharibi na Gaza unaokaliwa kwa mabavu.


Alisema hawezi kuelewa ni vipi watu walioteseka kama Wayahudi wangeweza kuwasababishia Wapalestina mateso hayo.


Alijikuta katikati ya vitoa machozi wakati wa mkutano wa kupinga ubaguzi wa rangi


Desmond Tutu alimpenda sana Nelson Mandela, lakini hakukubaliana naye kila mara katika masuala kama vile matumizi ya vurugu katika kutafuta suluhu ya haki.


Mnamo Novemba 1995, Mandela, aliyekuwa rais wa Afrika Kusini wakati huo, alimwomba Tutu kuongoza Tume ya Ukweli na Maridhiano, yenye jukumu la kukusanya ushahidi wa uhalifu wa enzi za ubaguzi wa rangi na kupendekeza kama watu wanaokiri kuhusika kwao wanapaswa kupata msamaha.


Mwishoni mwa uchunguzi wa tume hiyo, Tutu aliwashambulia viongozi wa zamani wa Wazungu wa Afrika Kusini, akisema wengi wao walidanganya katika ushahidi wao. Tume hiyo pia ilishutumu ANC kwa kufanya ukiukaji wa haki za binadamu wakati wa vita vyake dhidi ya ubaguzi wa rangi. Pande zote mbili zilikataa ripoti hiyo

Alibubujikwa na machozi


Tutu mara nyingi alishindwa na uchungu wa wale walioteseka chini ya ubaguzi wa rangi na, kwa zaidi ya tukio moja, alitokwa na machozi.


Alibubujikwa na machozi wakati wa ibada ya mwisho ya TRC 2003


He also found much to criticise in South Africa's new black-majority government. He launched a stinging attack on the ANC administration led by President Thabo Mbeki.


He said the ANC had not done enough to alleviate poverty among the poorest in the country and that too much wealth and power was concentrated in the hands of a new black political elite.


He later urged Jacob Zuma, who had been accused of sexual crimes and corruption, to abandon his attempts to become president.


Pia alikuwa na sauti kubwa katika kumshutumu Robert Mugabe, wakati mmoja akimuelezea rais wa Zimbabwe kama "mchoro wa katuni wa dikteta wa zamani wa Kiafrika". Mugabe, kwa upande wake, alimtaja Tutu kama "mwovu".


Mara nynegine angaweza pia kuwa mkosoaji wa kanisa lake la kianglikana hasa baada ya mzozo wa kuwekwa wakfu kwa maaskofu mashoga.

Milele mwasi


"Mungu analia," alisema wakati mmoja aliposhutumu kanisa kwa kuruhusu "mapenzi ya jinsia moja kuchukua nafasi ya kwanza juu ya vita dhidi ya umaskini duniani.


Alirejea katika suala la umaskini alipozuru Ireland mwaka 2010. Aliyataka mataifa ya Magharibi kuzingatia athari za kupunguzwa kwa misaada ya ng'ambo kutokana na kuzorota kwa uchumi.


Tutu alikuwa na jukumu kubwa katika sera ya Mandela ya maridhiano


Tutu alistaafu rasmi kutoka kwa maisha ya umma mwaka huo huo na, alisema, kutumia muda mwingi "kunywa chai nyekundu ya msituni na kutazama kriketi" kuliko "kukaa katika viwanja vya ndege na hotel


Lakini wakati wowote akiwa mwasi, alijitokeza kuunga mkono usaidizi wa kujiua mwaka 2014, akisema kwamba maisha hayapaswi kuhifadhiwa "kwa gharama yoyote".


Kinyume na maoni ya watu wengi wa kanisa, alishikilia kwamba wanadamu walikuwa na haki ya kuchagua kufa.


Alisema rafiki yake mkubwa na mwanaharakati mwenzake Mandela, ambaye alifariki Desemba 2013, aliugua ugonjwa wa muda mrefu na wenye uchungu ambao kwa maoni yake "ulikuwa dharau kwa utu wa Madiba".


Mnamo mwaka wa 2017, Tutu alimkosoa vikali kiongozi wa Myanmar na mshindi mwenzake wa Tuzo ya Amani ya Nobel, Aung San Suu Kyi, akisema "ni jambo lisilofaa kwa ishara ya uadilifu" kuongoza nchi ambayo Waislamu walio wachache walikuwa wakikabiliwa na "maangamizi ya kikabila".


Alipokutana na mwanamfalme na binti mfalme wa Duchess of Sussex na mwana wao Archie wakati wa ziara ya yao Afrika Kusini 2019


Baadaye mwaka huo huo, alipinga uamuzi wa Donald Trump kutambua Jerusalem kama mji mkuu rasmi wa Israel. "Mungu analia," aliandika kwenye Twitter, juu ya kitendo hiki cha "uchochezi na kibaguzi".


Mwanamume mdogo, "Arch", kama alivyojulikana, alikuwa mkarimu na mpole, akitoka roho ya furaha licha ya hisia zake nyingi za utume.


Alikuwa mwerevu, na mazungumzo yake mara nyingi yalipuuzwa na kukejeliwa.


Lakini zaidi ya haya, Desmond Tutu alikuwa mtu mwenye imani thabiti ya kimaadili ambaye alijitahidi kuleta pamoja Afrika Kusini yenye amani.

CHANZO- BBC SWAHILI
Share:

Attendant 3 – Lamproom at Geita Gold Mining Ltd

ABOUT GEITA GOLD MINING LTD   Geita Gold Mining Ltd (GGML) is Tanzania’s leading gold producer with a single operation in Geita Region. The company is a subsidiary of AngloGold Ashanti, an international gold producer headquartered in South Africa, with operations in more than ten countries, in four continents. The mine is situated in the […]

This post Attendant 3 – Lamproom at Geita Gold Mining Ltd has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

RAIS MWINYI ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI WALIOFARIKI KWA KULA NYAMA YA KASA




Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi ametoa salamu za rambirambi kwa familia za marehemu waliofariki kufuatia kula samaki wa aina ya kasa anayesadikiwa kuwa na sumu huko Matemwe, Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Katika salamu hizo za rambirambi, Rais Dk. Mwinyi ameeleza kusikitishwa na vifo hivyo na kuzinasihi familia za marehemu hao kuwa na subira na ustahamilivu katika kipindi hichi kigumu cha msiba pamoja na kumuomba Mwenyezi Mungu kuwaponya kwa haraka waliodhurika baada ya kula samaki huyo.



Rais Dk. Mwinyi katika salamu hizo za rambirambi, amesema kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Wizara yake husika itaendelea kuhakikisha wale wote waliodhurika wanaendelea kupatiwa tiba ili waweze kurudi katika hali zao nzuri za kiafya.
Share:

Sunday 26 December 2021

YANGA YAZIDI KUJICHIMBIA KILELENI NBC PREMIER LEAGUE, YAICHAPA BIASHARA UNITED 2-1



***************


NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Klabu ya Yanga imeendelea kusalia kileleni mwa ligi kuu NBC mara baada ya kufanikiwa kuwachapa Biashara United kwa mabao 2-1 katika uwanja wa Benjamini Mkapa Jijini Dar es Salaam.

Biashara United ilifanikiwa kupata bao la mapema mara baada ya kipa wa Yanga kupigiwa shuti kali na kutena na mchezaji wa Biashara United kumalizia.

Yanga ilianza kutawala mchezo kutafuta goli la kusawazisha hivyo baadae mshambuliaji raia wa DR Congo Fiston Mayele kupachika goli kali lililokwenda mpoja kwa nyavuni na kwenda mapumziko Dubai ukisomeka 1-1.

Kipindi cha pili mchezo ulibadilika kwa Biashara United kuchezea nafasi nyingi za mabao ambazo zingezaa mabao ya kutosha.

Yanga ilifanya mabadiliko kadhaa ya wachezaji wao ambapo alitoka Farid Mussa na nafasi yake ikachukuliwa na Jesus Muloko ambaye alikuwa mwiba kwa timu wapinzani kwani alisababisha kuzaa kwa penati ambayo Said Ntibazokiza alifunga na kuiwezesha timu yake kuondoka na ushindi wa mabao 2-1.
Share:

KOM PRE & PRIMARY SCHOOL INAWATANGAZIA NAFASI ZA MASOMO



KOM Pre & Primary School iliyopo Butengwa mkabala na Barabara ya Old Shinyanga Mjini Shinyanga inawatangazia nafasi za masomo.


Tunapokea watoto wenye umri kuanzia miaka mitatu na kuendelea.


Mlete mwanao apate msingi wa elimu bora katika mazingira yaliyo salama kwa gharama nafuu

Mawasiliano 0767483046 au
0767618213

Email : komschools@komclass.com
Share:

Saturday 25 December 2021

ASKOFU KINYAIYA AWATAKA WATANZANIA KUENDELEA KUISHI IMANI YA KRISTO NA KUENENDA KATIKA USAWA

 ASKOFU  Mkuu wa Jimbo kuu katoliki la Dodoma Mhashamu Beatus Michael Kinyaiya,akiongoza Misa takatifu ya Krismasi katika Parokia ya Mtakatifu Petro Mtume-Swaswa, sanjari na utoaji wa sakramenti ya Kipaimara kwa Vijana 60  wa Parokia hiyo.
*****

Na,Dotto Kwilasa-Malunde 1 blog, DODOMA.

ASKOFU  Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dodoma Mhashamu Beatus Michael Kinyaiya, amewataka  Watanzania  kuendelea kuwaombea Viongozi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,chini ya Rais Mama Samia Suluhu Hassan ili waweze kuongoza katika haki,usawa,umoja na .shikamano kama anavyofundisha Yesu Kristu mfalme wa amani.


Hayo amesema wakati akitoa Homilia yake kwenye Adhimisho la Sadaka ya Misa Takatifu Sherehe ya Kuzaliwa kwa Bwana Yesu Kristu,katika Parokia ya Mtakatifu Petro Mtume-Swaswa, sanjari na utoaji wa sakramenti ya Kipaimara kwa Vijana 60  wa Parokia hiyo.


Amesema maombi ya kuwaombea Viongozi wa nchi yanahitajika kwa kila mwananchi, ili Viongozi hao waliopewa mamlaka ya kuwaongoza Watanzania waweze kuyaishi maagizo yake.


"Kwa kipekee kabisa nawaomba wananchi wote, kuendelea kumuomba Mwenyezi Mungu kupitia kwa Mtoto Yesu ili alete Mvua ya kutosha isiyokuwa na madhara,kwani mpaka sasa Mkoa wa Dodoma na Kanda ya kati kwa ujumla bado haina mvua,"amesema Askofu huyo.


Pamoja na hayo amesema na wakristu wanapaswa kutumia kipindi hiki kujifungamanisha na maombi pia kwa Mtoto Yesu ambaye hashindwi na lolote aweze kuliepushe taifa dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa UVIKO-19,na hasa maambukizi mapya ya sasa yanasambazwa na Kirusi cha Omicron.


Hata hivyo Mchungaji huyo Mkuu wa Jimbo ametumia nafasi hiyo kwa kusema "Nawaonya pia Vijana wanaotumia madawa ya kulevya kuacha mara moja  tabia hiyo,madhara yake ni kuwaharibia maisha yao wenyewe na kupunguza nguvu kazi ya familia na Taifa lote kwa ujumla,ili kuondokana na yote haya lazima tukubaki kumshirikisha Mwenyezi Mungu,"amesisitiza.


Share:

MAKAMU WA RAIS DKT. MPANGO ASHIRIKI IBADA YA KRISMASI


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango akiwa na Mkewe Mama Mbonimpaye Mpango leo tarehe 25 desemba 2021 wameungana na waumini wa kanisa katoliki la mtakatifu Paulo wa Msalaba Jimbo Kuu la Dodoma kushiriki ibada ya misa takatifu ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo (Krismasi) misa iliyoongozwa na Padri Julius Soteri Desemba 25,2021.
Share:

Video Mpya : DIAMOND PLATNUMZ - UNACHEZAJE

SUPASTAA wa Bongo Fleva, Naseeb Abdul “Diamond Platnumz” leo Desemba 25, 2021 ameachia video ya wimbo wake wa Unachezaje

 


Share:

MBWA KOKO AVAMIA DUKA LA DAWA, ASHAMBULIA WAHUDUMU


Kizaazaa kimeshuhudiwa mjini Thika nchini Kenya baada ya mbwa koko kuruka kwenye duka la dawa, maarufu Chemist kuvamia na kuwashambulia wahudumu ghafla.

Kisa hicho kilifanyika Disemba 24,2021 katika duka la Menya Chemist wakati ambapo wahudumu walikuwa kwenye shughuli zao za kila siku. 

Wakazi walisema ilikuwa kama filamu kwenye duka hilo huku wahudumu wakilia na kuomba usaidizi kumkabili mbwa huyo.

"Sisi tumeona maajabu hapa. Hii ni umbwa sijui imetoka wapi? Imeingia hapa na kuanza kuvamia watu. Imebidi tuiue," alisema mmoja wa wakazi.

 Wakazi walisema kilikuwa kisa cha kushangaza na hawakujua sababu ya kuchagua duka hilo na kushambulia wahudumu.

 "Tunashangaa sana kuhusu kisa hiki. Hii umbwa imeacha watu wengi, imepitana na hata magari lakini ikakuja tu hapa na kumuuma huyo," mkaazi mwingine alisema.

Inaarifiwa mbwa huyo aliuma kidole cha mwathiriwa hadi kukikata na kisha akakitema na kulala ndani ya duka.

Wakazi wenye hamaki waliamshambulia na kumpa kichapo hadi kufariki dunia na kuchukuliwa na maafisa wa kanjo.

 Ilibidi mwathiriwa kukimbizwa katika hospitali kupokea matibabu baada ya kupoteza kidole chake cha gumba. 

John Ngumba, mwenyekiti wa wafanyibiashara mjini Thika, alisema watahakikisha kuwa mwenye mbwa huyo atashtakiwa.

 MCA wa Wadi ya Thika Andrew Kimani alikosoa mmiliki wa mbwa huyo kwa kumwachilia aranderande na kuhatarisha maisha ya wakazi. 

Aliahidi kuhakikisha kuwa wote walioshambuliwa na mbwa huyo wamepata matibabu yanayofaa na mmiliki wa mbwa huyo kuwajibika.
Share:

KAMANDA WA POLISI MKOANI IRINGA AFANYA OPARESHENI BARABARA KUU IRINGA -MOROGORO




Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa ACP Allan L. Bukumbi akiambatana na Mkuu wa Usalama Barabarani wamefanya Operesheni katika barabara kuu ya Morogoro - Iringa hususani eneo la Kitonga lakini pia kutoa elimu kwa Madereva ili kuepusha ajali zinazoweza kuzuilika hasa kipindi hiki cha Sikukuu za Mwisho wa Mwaka.

ACP Bukumbi amewakumbusha madereva kutii sheria za barabarani ili kuepuka ajali na kwamba hatosita kumchukulia hatua dereva yeyote atakaekiuka maadili ya udereva awapo barabarani.

Hali kadhalika Mkuu wa Usalama barabarani Mkoa wa Iringa, SP Yusuf Kamota ametumia muda huo kuwakumbusha kuwa Iringa sio sehemu sahihi kwa madereva wasiofuata sheria za barabarani na kwamba atahakikisha sheria zinatekelezwa ipasavyo.

Katika hatua nyingine, Kamanda Bukumbi amewataka abiria wawapo safarini, kutoa taarifa kwa wakuu wa usalama barabarani endapo kuna vitendo vya uvunjifu wa sheria kwani Jeshi la Polisi limeweka utaratibu wa kubandika mawasiliano kwenye Vyombo hivyo.
Share:

Friday 24 December 2021

NYOKA HATARI ZAIDI AKUTWA KWENYE SHEHENA YA MATOFALI



Nyoka huyo hatari alionekana katika upande wa dereva

Miongoni mwa nyoka hatari zaidi duniani amepatikana huko Salford baada ya kunusurika safari ya maili 4,000 katika shehena ya meli kutoka Pakistan.


Nyoka huyo aligunduliwa kwenye kontena la matofali, ambalo lilikabidhiwa kwa mtaalamu wa matofali wa Manchester mwezi uliopita.


Mkaguzi wa RSPCA, Ryan King aliitwa ili kumuokoa nyoka huyo mwenye sumu


Alisema aligundua kwa haraka kuwa nyoka huyo "alikuwa na uwezo zaidi wa kuua watu kwa sumu yake yenye sumu kali."


"Wakati mwingine tunapata kazi kama hizi na inageuka kuwa nyoka asiye na madhara," alisema.


"Tumehudhuria hata ripoti za nyoka ambazo zinageuka kuwa vifaa vya kuchezea vya plastiki."


Bw King alisema mara moja alitambua baada ya "kumtazama kwa haraka" jinsi nyoka huyo alivyokuwa na sumu

Mkaguzi RSPCA Ryan King alisema ni heshima kubwa kwake kukabiliana na nyoka wa aina ile"


Dereva wa forklift katika kampuni hiyo kwenye Barabara ya Langley alimpata nyoka huyo siku ya Ijumaa.


Meneja wa vifaa Michael Regan alimfungia nyoka huyo kwenye sanduku na kuripoti suala hilo kwa RSPCA.


"Nilijua kujiweka mbali lakini bila shaka sikujua jinsi nyoka huyu alivyokuwa mbaya - nilishtuka sana," alisema.


Nyoka huyo anayepatikana zaidi barani Asia, amehamishiwa kwenye kituo chenye leseni maalum ya kuhudumia wanyama watambaao wenye sumu kali.


Nchini India, ambapo karibu nusu ya vifo vya kung'atwa na nyoka duniani kote vinavyodhaniwa kutokea, nyoka ni mojawapo ya spishi nne ambazo kwa pamoja zinachangia idadi kubwa zaidi ya vifo vya binadamu, RSPCA ilisema.


Bw King alisema ni jambo la kustaajabisha kwamba nyoka huyo alinusurika katika safari hiyo na kuweza kuishi kwa wiki kadhaa katika hali ya baridi kama hiyo.


"Ni wadogo sana na angeweza kumng'ata mtu kirahisi na inaonekana amekuwa kwenye eneo la ujenzi wa matofali kwa takriban mwezi mmoja," alisema.


"Kinga ya sumu ya nyoka huyo huwa inapatikana katika nchi ambako nyoka anatoka lakini ana sumu kali sana- ni ngumu kwa muathirika kuokolewa."

Chanzo : BBC SWAHILI 
Share:

TUMBILI WAFANYA KISASI, WAUA MBWA 250



Hizi ni ripoti kutokea Maharashtra, nchini India, ambapo kundi la tumbili limelipiza kisasi kwa kuwaua mbwa wapatao 250, baada ya kukasirishwa na kitendo cha mbwa kumuua kichanga chao.

Mashuhuda wa tukio hilo wameeleza kuwa, tumbili hao walitekeleza mauaji hayo kwa kuwakamata mbwa na kupandanao juu ya miti kwenye nyumba na kisha kuwatupa chini.

Tayari mamlaka za wanyama pori nchini humo zimefika eneo la tukio na kuwakamata tumbili hao na kuwaweka kwenye uangalizi maalumu.

Ushawahi kukutana na timbwili la tumbili?
Share:

TAMASHA LA 'WOMEN GALLA' LA DIVINE FM LAFANYIKA KAHAMA... WAZIRI ATAKA WANAWAKE WABADILIKE KUKUZA UCHUMI

Rais wa sauti ya Wanawake wajasiriamali Nchini Bi Maida Waziri akitoa Elimu kwa Wanawake kupitia tamasha lililoandaliwa na kituo cha matangazo Divine Radio ( Women Galla).

Na Nyamiti Alphonce Nyamiti - Kahama
Pamoja na uwepo wa fursa nyingi za kiuchumi wilayani Kahama mkoani Shinyanga imeelezwa kuwa wanawake wengi wameshindwa kuzitumia kwa baadhi yao kuwa na mifumo tegemezi kwenye uendeshaji wa maisha yao.

Yamebainishwa hayo na Rais wa sauti ya Wanawake wajasiriamali hapa Nchini Bi Maida Waziri wakati akitoa Elimu kwa Wanawake kupitia tamasha lililoandaliwa na kituo cha matangazo Divine Radio ( Women Galla).

"Mkoa huu unasifika kwakuwa na vyanzo vingi vya kiuchumi mmebarikiwa kuwa na Madini, Bandari ya nchi kavu, rasilimali watu na maeneo ya kufanyia kilimo badilikene mkuze uchumi wenu", alisema Waziri

Waziri ameitaka jamii ya wanaume kuendelea kuwapa fursa na kutoa kushirikiana kwa Wanawake kwakuwa wanauwezo mzuri wa kufanya shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Mkuu wa wilaya ya Kahama Mhe. Festo Kiswaga ametumia nafasi hiyo kuwataka Wanawake  wajasiriamali kujiunga kwenye vikundi ili waweze kukopa fedha hizo zinazotengwa na serikali kwa makundi ya vijana, Wanawake na walemavu.

"Sisi kama wilaya naomba nikuhakikishie Mgeni rasmi tumetenga 10% kwa kila halimashauri kutoa mikopo kwamakundi yote matatu tunazo halimashauri tatu" alisema Kiswaga

Baadhi ya Wananchi waliohudhuria Tamasha hilo wameitaka serikali kuwawekea mifumo mizuri ya upatikanaji wa Elimu ya ujasiriamali ili waweze kujikwamua kiuchumi.
Rais wa sauti ya Wanawake wajasiriamali nchini Bi. Maida Waziri akisalimiana na akina mama kwenye tamasha lililoandaliwa na kituo cha matangazo Divine Radio ( Women Galla).
Wajasiriamali Kahama Wakijifunza  jambo kutoka kwa mkufunzi na muwakirishi wa Shirika la kazi Duniani bwana Benidict Mwampela..
Manager Wa Kituo cha Redio cha Divine Women Galla, Joshua Kasase akiwasalimia wana semina.
Raisi wa Sauti ya Wanawake Wajasiriamali Tanzania.. Bi, Maida Waziri   Katikati akiwasili  ukumbi wa Miligo kwaajili ya semina ya akina mama Kahama.
Share:

ASKARI ALIYEPANDISHWA CHEO KWA KUKATAA RUSHWA YA MILIONI 10 APEWA ONYO



Meshack Samson anayefanya kazi Arusha alipandishwa Cheo kutoka Sajenti (Sgt) hadi Stesheni Sajenti (Ssgt) mwaka 2019 baada ya kukataa rushwa ya Tsh. Milioni 10.

Askari huyo ameshushwa cheo kutokana na kutotii Mamlaka ya kwenda Kozi ya Kipolisi kuendana na Cheo alichopewa, ikielezwa hakuwa na sababu za msingi kukataa kufanya hivyo.

Ameshushwa ngazi moja kutoka Stesheni Sajenti kuwa Sajenti wa Polisi baada ya kushtakiwa na kupatikana na hatia ya utovu wa nidhamu kwa kukataa amri halali ya Mkuu wa Jeshi la Polisi.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger