Friday 24 December 2021

WATATU WATIMKA AZAM FC, YUPO DUBE


JUMLA ya wachezaji watatu wanatarajiwa kuondoka katika kikosi cha Azam FC kwenda katika timu ya taifa ya Zimbabwe kushiriki michuano ya Kombe la Mataifa Afrika (AFCON).

Wachezaji hao ni beki wa kushoto, Bruce Kangwa, kiungo Never Tigere na mshambuliaji Prince Dube. Nyota hao huenda wakosekana katika michezo baadhi ya Ligi Kuu Bara na Kombe la FA kutokana na kuwepo katika majukumu ya timu ya taifa.

Kwa mujibu wa mtandao wanchi ni Zimbabwe, wachezaji hao wameitwa katika kikosi cha awali kuelekea michuanoya AFCON itakayoanza Januari 9 hadi Februari 6, 2022 nchini Cameroon.

Mastaa hao wa Azam, wanatarajiwa kuingia kambini hivi karibuni kwa ajili ya mchujo wa mwisho utakaowawezesha kuwepo sehemu ya kikosi cha Zimbabwe kitakachokwenda Cameroon katika michuano
hiyo.

Ofisa Habari wa Azam FC, Thabiti Zakaria, alithibitisha hilo kwa kusema: “Ni kweli wachezaji hao wameitwa katika kikosi cha awali cha timu ya taifa ya Zaimbabwe, hivyo muda wowote watajiunga nayo.”
Share:

RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI WA VIONGOZI MBALIMBALI



Rais Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi wafuatao;

1.Amemteua Prof. Othman Chande Othman kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS).

Prof. Othman anachukua nafasi ya Dkt. Fenella Ephraim Mukangara ambaye uteuzi wake umetenguliwa. Prof. Othman ni Mhadhiri Mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

2. Amemteua Dkt. Aggrey Kalimwage Mlimuka kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Ushindani (FCC).

Dkt. Mlimuka anachukua nafasi ya Prof. Humphrey P.B. Moshi aliyemaliza muda wake. Dkt. Mlimuka ni Mkurugenzi Mstaafu wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE).

3. Amemteua Dkt. Andrew Yona Kutua kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Taasisi ya Taifa ya Utafiti ya Magonjwa ya Binadamu (NIMR).

Dkt. Kutua anachukua nafasi ya Dkt. Deudatus Mtasiwa ambaye amemaliza muda wake.

Uteuzi wa viongozi hao umeanza Desemba 23, 2021.


Share:

PUMBULU: MILA YA KISUKUMA INAYOFANYIKA BAADA YA MWANAMKE KUPOTEZA MAISHA AKIJIFUNGUA


Akina mama wa kijiji cha Nyamswa wilayani Bariadi mkoani Simiyu wakishiriki mila ya Pumbulu kutoka kijiji cha Nyamswa kwenda Kijiji jirani cha Mwasubuya hivi karibuni.

Na COSTANTINE MATHIAS, Simiyu.


👉Hawataki kuona mwanaume yeyote wakati wakitekeleza mila hiyo.
👉Wanne wakamatwa baada ya kumshambulia mkandarasi wa barabara.


MILA na Desturi zina mchango mkubwa katika jamii endapo zitaenziwa kwa kuheshimu haki zingine za binadamu, hata hivyo wakati mwingine jamii hutumia haki za kitamaduni kama kisingizio cha kukandamiza wengine au kubinya haki zingine za binadamu katika jamii.


Utamaduni pia huainisha jamii, kiasi kwamba mawazo, matarajio na kanuni zao au viwango vya tabia zao (ambazo wao huamua nini ni muhimu katika maisha yao) yote ni sawa sawa wanapokabili mazingira ya ulimwengu unaowazunguka.

Pumbulu ni moja ya tamaduni za kabila la Wasukuma, ambayo hufanyika au hutimizwa baada ya mwanamke kupoteza maisha akijifungua na kwamba baada ya matanga wanawake hutambika kwa kukimbiza Pumbulu.

Kabla na baada ya Uhuru, Mila hii ilikuwa inafanyika sana katika maeneo mengi ya Usukumani, lakini baada ya miaka ya 1990 ilianza kupungua kutokana na jamii nyingi kupata elimu, dini pamoja na uboreshaji wa huduma za afya.

Mara nyingi wakinamama walikuwa wanapoteza maisha kutokana na ukosefu wa huduma za afya kwani walikuwa wanajifungulia majumbani, hali iliyochangia vifo vyao lakini kwa jamii ya wasukuma ilibainika ni mkosi.

Roda Kuyi mkazi wa Kijiji cha Mhunze wilaya ya Itilima Mkoani Simiyu anasema kuna baadhi ya wanawake wasiomcha mungu bado wanaendeleza mila hiyo ambayo imepitwa na wakati.

Anasema hutokea mara baada ya mama mjamzito kupoteza maisha akijifungua, ambapo baada ya msiba kufanyika, wanawake hao huchukua majivu ya familia hiyo pamoja na kuvunja vyungu (Malujo), Minyaa, Magaka, na takataka zingine kuzihamishia kijiji cha pili.


Anasema huzihamishia kijiji cha pili (Magharibi) kama ishara ya kuondoa mikosi katika kijiji chao na kwamba wakikutana na mwanaume yeyote njiani lazima apigwe na kuvuliwa nguo.


"Vitu hivyo vinasindikizwa hadi katikati ya kijiji cha pili upande wa magharibi, nao wakina mama wa kijiji cha pili huvipeleka kijiji kinachofuata hadi ziwa Viktoria, lengo ni kuondoa mikosi na zoezi hili hutokea mashariki kuelekea Magharibi (yaani ziwani)’’ anasema Roda.

Anafafanua kuwa wakina mama hao (Pumbulu) hupambana na kila mwanaume wanayekutana naye njiani wakiamini kuwa ndiye aliyesababisha mwanamke mwenzao kupoteza maisha wakati wa uzazi.

Anaongeza kuwa waliamini kuwa mwanamke mwenzao kapoteza maisha kutokana na kushiriki tendo la ndoa na wanaume wengi wakati wa ujauzito wake hivyo mwanaume yeyote hastahili kuonekana wakati wa kutimiza mila hiyo.


Naye Julius Renatus mkazi wa kijiji cha Lagangabilili wilaya ya Itilima alisema mila hiyo imefutwa na ujio wa dini pamoja na elimu ambapo kwa sasa familia nyingi haziamini utamaduni huo.

"Elimu na dini zimeondoa mila hii japokuwa kuna baadhi ya watu wameishikilia, tunaamini itaenda inafutika polepole…tunaiomba serikali ipige marufuku mila ambazo zinahatarisha maisha ya watu kwa sababu sasa hivi kuna mwingiliano wa makabila tofauti tofauti’’ anasema Renatus.

Anasema kuwa wao kama wanaume wa jamii ya Kisukuma wanawajua akina mama hao, hivyo wakiwaona lazima wakimbie kujificha ambapo kwa wageni bado kuna changamoto.

Mayenga Gidakindwa mkazi wa Bariadi anasema siyo mila nzuri kwa sababu inakizana na haki za binadamu sababu mtu ana haki ya kuishi na kutembea popote ndani ya Jamhuri ya Muungano bila bughuza yoyote.

Viongozi wa dini wanena.

Padri John Nkinga ambaye ni Paroko wa Kanisa Katoliki Ngulyati wilaya ya Bariadi anasema wao kama viongozi wa dini wanajikita kuelimisha jamii kupitia nyumba za ibada ili wananchi waachane na mila potofu ambazo zimepitwa na wakati.

"Sisi tukiwa viongozi wa Dini kwa jamii yetu tunajikita kuelemisha jamii madhara ya Mila na Faida ya kuiacha! (We put more Community awarreness on the case!!)… Sasa kwa mfano Pumbulu nimewajibika vilivyo kwanza kuwafundisha Pumbulu, Ni Nini na wamejua na kuachana nayo!’’ anasema Padri Nkinga.

Kuhusu kutimiza wajibu wa kutoa elimu, Padri Nkinga anasema "Hatujawajibiki kwa waumini, Elimu haina mwisho na Imani ni sawa na upepo mtu kujiachia kabisa…anahitaji elimu ya malezi, nashukuru kwa matukio haya yanasaidia kusafisha njia kwa Elimu ya Hakika zaidi!’’

Padri Nkinga anasema ujio wa Dini na Elimu umeipunguza jamii kuachana na mila na desturi sababu walikotoka ni kubaya na watu hawatukutambua thamani ya viongozi wa dini.

"Tumetoka mbali, mtu anakufa anawekewa miba na kuachwa porini…matumizi ya nyumba bora, Hospitali na mavazi, uhakika wa vipimo na tiba, Mila potofu inatuambia tumerogwa tu na kusubiria kifo, mbaya zaidi kuna mahali wanaitumia kuku kam darubini!,’’ anasema Padri Nkinga.

Padri huyo anaishauri Serikali isifuate mkumbo na upendeleo wa mila potofu bali wafuate misingi ya kuisaidia jamii, pia wawe na msimamo mmoja au wasiwe wafuasi wa mila mbaya, na wasimamie Sera na kanuni zinakubalika kimataifa na Kikatiba.

DC azungumzia uwepo wa Pumbulu Bariadi.

Akiwasilisha taarifa ya hali ya ulinzi na usalama mbele ya kamati ya siasa mkoa wa Simiyu, Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wilaya ya Bariadi Lupaksyo Kapange amesema hivi karibuni akina mama wanne wamekamatwa na polisi kwa kosa la kumshambulia mkandarasi wakati wakitekeleza mila ya Pumbulu.

"Serikali imechukua hatua ya kukamata wote waliohusika kumshambulia mkandarasi huyo anayetekeleza miradi ya barabara kata ya Nkololo, hatuwezi kufanya mila hizi kuwa sheria ya makabila yote’’ ,amesema Kapange.

Kapange ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Bariadi amesema mila hizo ni kinyume na haki za binadamu na kwamba hazitendi haki sababu ujauzito walipeana watu wawili inakuwaje anapigwa mtu yeyote barabarani.

Kapange anasema mila hiyo ni hatari na inanyima uhuru na haki za binadamu na kwamba serikali itawasaka wale wote wanaopiga watu barabarani wakati wa kutekeleza mila ya Pumbulu kwa jamii ya wasukuma.

Polisi wakamata wanawake wanne kwa kumshambulia mkandarasi.

Jeshi la polisi Mkoani Simiyu linawashikilia wanawake wanne kwa tuhuma za kumshambulia Mkandarasi wa barabara ya Nkololo-Bariadi wakati wakitekeleza mila yao ya kukimbiza Pumbulu.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Simiyu Kamishna Msaidizi wa Polisi Blasius Chatanda akiwa ofisini kwake aliwaambia Waandishi wa habari kuwa wanawashikilia wanawake wanne kwa kushambulia mkandarasi huyo na kumsababishia majeraha.

"Ni kwamba mnamo tarehe 09/12/2021 majira ya 11:00 asubuhi, huko maeneo ya kijiji cha Nkololo, Kata na Tarafa ya Nkololo Wilaya ya Bariadi, alishambuliwa Mkandarasi na kundi la Wanawake kwa kumpiga mawe sehemu mbali mbali za mwili wake na kumsababishia majeraha’’ alisema Kamanda Chatanda.

Alisema kundi hilo la Wanawake walikuwa katika kutimiza mila zao za Kisukuma, ambapo Mwanamke akijifungua na ikatokea yeye na mtoto wake wamefariki huwa wanaenda kufanya tambiko hivyo wakiwa njiani wakikutana na mwanaume yoyote wanaanza kumshambulia hii ni kutokana na mila zao za Kisukuma inayotambulika kwa jina la “Pumbulu”.

Alifafanua kuwa hadi sasa watuhumiwa hao wapo nje kwa dhamana na mara baada ya upelelezi kukamilika jalada litaandaliwa kwenda Ofisi ya Taifa ya Mashtaka na kufikishwa mahakamani kwa hatua za kisheria.

Kamanda Chatanda anawataka wananchi na wanawake wote kuacha vitendo vya kujichukulia sheria mkononi, huku akionya kuwa mila hizo isiwe chanzo cha kujichukulia sheria mkononi.
Akina mama wa kijiji cha Nyamswa wilayani Bariadi mkoani Simiyu wakishiriki mila ya Pumbulu kutoka kijiji cha Nyamswa kwenda Kijiji jirani cha Mwasubuya hivi karibuni.
Share:

4 Job Opportunities at National Institute for Medical Research (NIMR)

BACKGROUND   The National Institute for Medical Research (NIMR) is a public research institution established by Act of Parliament No. 23 of 1979 and became operational in 1980. NIMR Mwanza centre is one of the major NIMR research Centers of NIMR located in Mwanza city. The Centre conducts research on schistosomiasis and other neglected tropical […]

This post 4 Job Opportunities at National Institute for Medical Research (NIMR) has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Sponsorship & Program Facilitator (WASH)at World Vision International Tanzania

Position: Sponsorship & Program Facilitator (WASH) JOB PURPOSE To provide technical support in design, implementation, monitoring and evaluation of Water supply, Sanitation and Hygiene (WASH) and natural resources management projects/programs within WVT areas of operation Observe mission and core values of World Vision and demonstrate a quality of spiritual life that is an example to others.Recommended: […]

This post Sponsorship & Program Facilitator (WASH)at World Vision International Tanzania has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Thursday 23 December 2021

RPC SHINYANGA APIGA MARUFUKU DISKO TOTO, KUCHOMA MATAIRI ..."WALEVI KULA SIKUKUU YA KRISMASI NA MWAKA MPYA MAHABUSU"


Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP George Kyando akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamis Desemba 23,2021. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP George Kyando akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamis Desemba 23,2021

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog


Katika kusherehekea Sikukuu ya Krismasi na Mwaka Mpya 2022 Jeshi la polisi Mkoa wa Shinyanga limepiga marufuku Disko Toto pamoja na ulipuaji wa baruti, fataki na uchomaji matairi huku likiwataka wafanyabiashara wa maduka makubwa yakiwemo ya Fedha yafungwe mapema sambamba na kuweka walinzi ili kuepuka mianya ya wahalifu kutumia Sikukuu kufanya uhalifu.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi Desemba 23,2021 wakati akitoa salamu za Krismasi na Mwaka Mpya 2022, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP George Kyando amesema jeshi hilo limejipanga kikamilifu kuhakikisha amani na utulivu vinatawala wakati za sherehe hizo.

Amesema licha ya kwamba jeshi la polisi limejipanga ipasavyo lakini bi vyema wananchi wakaendelea kushirikiana na jeshi la polisi kutoa taarifa za viashiria vya matukio ya uhalifu na wahalifu ikiwa ni pamoja na kuchukua tahadhari kuzuia vitendo vya uhalifu katika jamii.

“Jeshi la polisi limeimarisha doria za magari,pikipiki na doria za miguu, tutalinda sehemu zote za ibada na mikesha na maeneo yote yenye mikusanyiko halali ikiwemo ya burudani na misako mikali itafanyika sehemu mbalimbali zenye maficho ya wahalifu”,amesema Kamanda Kyando.

“Disco toto kwenye kumbi zimepigwa marufuku, haziruhusiwi kabisa hivyo yeyote mwenye nia hiyo afute wazo hilo. Ulipuaji wa baruti, fataki na uchomaji matairi vitendo hivyo vyote vimepigwa marufuku”,amesema.

Kamanda Kyando pia amewatahadharisha watumiaji wa pombe kujiepusha na ulevi wa kupindukia kwani unaweza kuwapelekea kusherehekea sherehe za Krismasi na Mwaka Mpya wakiwa mahabusu au magereza kabisa.

“Watumiaji wote wa vyombo vya moto wanatahadharishwa kufuata sheria za usalama barabarani hasa waendesha pikipiki,bajaji na magari. Pia wajiepushe na matumizi ya vilevi kwani upimaji wa walevi utafanyika kwa nguvu sana”,ameeleza.

Aidha amewataka wenye nyumba kufunga nyumba zao kwa uimara au kuacha mtu wa kulinda nyumba hiyo badala ya kuacha watoto kuwa walinzi

“Walinzi wa makampuni binafsi na watu binafsi kuwa makini sana kwa siku hizi za sikukuu wajiepushe kuingia malindoni wakiwa wamelewa,kuongea na watu wasio wajua kwenye maeneo yao ya ulinzi na kula au kupewa chochote na mtu ambaye hawajakubaliana kufanya hicho kitu”,amefafanua.
Share:

Driver at Tanzania Commercial Bank

Tanzania Commercial Bank is a Bank that provides competitive financial services to our customers and creates value for our stakeholders through innovative products.   Tanzania Commercial Bank is a Bank, whose vision is “to be the leading bank in Tanzania in the provision of affordable, accessible and convenient financial services”. As part of effective organizational […]

This post Driver at Tanzania Commercial Bank has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Tanzania Monitoring Evaluation and Learning Associate at One Acre Fund

We are looking for an M&E analyst / research professional to be a Monitoring, Evaluation and Learning (MEL) Lead in Iringa, Tanzania. The Monitoring, Evaluation and Learning Lead will translate data analysis and results into relevant programmatic recommendations that steer our short- and long- term impact strategy, increase farmer impact, and improve our operations.   […]

This post Tanzania Monitoring Evaluation and Learning Associate at One Acre Fund has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Regional Content and Teacher Professional Development Specialist at International Rescue Committee

Employment Type: Full-Time   Open to Expatriates: Yes Job Description This role can be based in Kampala, Uganda or Dar Es Salaam, Tanzania.   PlayMatters reimagines childhood for refugees. It will bring play-based learning to 800,000 children across Ethiopia, Uganda, and Tanzania. It will redefine education and cultivate a generation of lifelong builders. PlayMatters is inspired […]

This post Regional Content and Teacher Professional Development Specialist at International Rescue Committee has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

National Consultant – Disaster Risk Reduction at International Organization for Migration

TERMS OF REFERENCE     I. POSITION INFORMATION  Vacancy Number: IOM/DAR/025/2021 Position title: National Consultant – Disaster Risk Reduction Duty Station: Home based Duration of Assignment: Four (4) months Type of Appointment Consultancy Contract Organizational Unit: Programme Unit Reporting direct to: Programme Coordinator Estimated Start Date February 2022   II. ORGANIZATIONAL CONTEXT AND SCOPE  Established […]

This post National Consultant – Disaster Risk Reduction at International Organization for Migration has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Individual International Consultant – PFM Specialist at UNICEF

Job no: 547082   Contract type: Consultancy Level: Consultancy Location: United Republic of Tanzania Categories: Social and Economic Policy UNICEF works in some of the world’s toughest places, to reach the world’s most disadvantaged children. To save their lives. To defend their rights. To help them fulfill their potential. Across 190 countries and territories, we work for every […]

This post Individual International Consultant – PFM Specialist at UNICEF has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Wednesday 22 December 2021

Government & Regulatory Affairs Manager, International at SBA Communications

 Government & Regulatory Affairs Manager, International   Job Category: Legal Compliance and Audit Requisition Number: GOVER003606 Posted:September 10, 2021 Dar Es Salaam, Dar es Salaam, TZ Who We Are SBA Communications (SBA) is an industry leader in providing the wireless infrastructure that makes communication work, with a track record of growth throughout the Americas, South […]

This post Government & Regulatory Affairs Manager, International at SBA Communications has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Book Keeping & Commerce Teacher at The Islamic Foundation

Book Keeping & Commerce Teacher    The Islamic Foundation is an independent Religious & humanitarian foundation that works to help millions of poor and vulnerable people regardless of race,political affiliation, gender or belief. It upholds the norm that safeguards humanity by leaving no one behind from receiving aid to end their needs.Our pioneering multi-national program […]

This post Book Keeping & Commerce Teacher at The Islamic Foundation has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Civics & Moral Teacher at The Islamic Foundation

 Civics & Moral Teacher    The Islamic Foundation is an independent Religious & humanitarian foundation that works to help millions of poor and vulnerable people regardless of race,political affiliation, gender or belief. It upholds the norm that safeguards humanity by leaving no one behind from receiving aid to end their needs.Our pioneering multi-national program enables […]

This post Civics & Moral Teacher at The Islamic Foundation has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Kiswahili Teacher at The Islamic Foundation

Kiswahili Teacher    The Islamic Foundation is an independent Religious & humanitarian foundation that works to help millions of poor and vulnerable people regardless of race,political affiliation, gender or belief. It upholds the norm that safeguards humanity by leaving no one behind from receiving aid to end their needs.Our pioneering multi-national program enables many to […]

This post Kiswahili Teacher at The Islamic Foundation has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

DC ILALA ACHAGIZA MBUZI WA SIKUKUU ZA BIKO


Mkuu wa wilaya Ilala, Mheshimiwa Ng'wilabuzu Ndwata Ludigija (kulia) akifurahia na mshindi wa milioni 10 wa Biko, Mikidadi Kaimu Ngoo alipomtembelea ofisini kwake kumkabidhi hundi yake ya ushindi wa Biko. Picha na Mpigapicha Wetu.
Balozi wa Biko Kajala Masanja akipiga picha sambamba na kumkabidhi hundi yake mshindi wa Biko Mikidadi Kaimu Ngoo aliyeshinda Sh Milioni 10 za Bahati nasibu ya Biko maarufu kama Buku Nibukue.
Mkuu wa wilaya Ilala, Mheshimiwa Ng'wilabuzu Ndwata Ludigija (kulia), akiwa na mshindi wa sh milioni 10, Mikidadi Kaimu Ngoo mwenye maskani yake Chanika, wilayani Ilala, mkoani Dar es Salaam katikati. Kushoto ni Balozi wa Biko Kajala Masanja alipoenda kuungana na DC Ng'wilabuzu Ndwata Ludigija kumkabidhi mshindi huyo hundi yake ya ushindi wa mamilioni ya Biko.


Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

MKUU wa wilaya ya Ilala, Mheshimiwa Ng'wilabuzu Ndwata Ludigija, amechagiza utolewaji wa zawadi za mbuzi za sikukuu ya Christmass na Mwaka mpya zinazotolewa kwa wingi katika ushindi wa papo kwa hapo wa Bahati nasibu ya Biko, akisema zitapunguza makali ya maisha kwa Watanzania watakaofanikiwa kushinda kwenye droo hizo.

Mheshimiwa Ludigija aliyasema hayo wakati wa makabidhiano ya hundi ya sh Milioni 10 kwa Mikidadi Kaimu Ngoo wa Chanika, wilayani Ilala, mkoani Dar es Salaam, aliyeshinda kwenye droo ya Jumapili na kuwa miongoni mwa Watanzania wengi wanaobukua mamilioni ya Biko, ambapo katika droo za papo kwa hapo, sh laki mbili mbili zitamwagika kama sehemu ya ununuaji wa mbuzi za sikukuu za mwisho wa mwaka.


Mchezo wa biko unachezwa live mtandaoni kwa kuingia www.biko.co.tz bila kusahau wale wanaotumia njia ya kawaida kwa kucheza kwa namba ya Kampuni 505050 na kumbukumbu 2456 au neno biko, huku kianzio cha kucheza kikiwa sh 1000 na kuendelea.

Biko ni mchezo wa kubahatisha unaoongoza kutoa fedha nyingi kwa Watanzania, ambapo zwadi za papo kwa hapo zinatoka kila sekunde moja kuanzia sh 2500 hadi milioni 5 papo hapo bila kusahau kutoa zawadi ya hadi sh milioni 40 kila Jumapili ambapo mbali na kucheza kwa namba ya Kampuni 505050 na kumbukumbu 2456, pia watu wanaweza kucheza live kwa kuingia www.biko.co.tz.
Share:

Nursery Teacher at The Islamic Foundation

Nursery Teacher   The Islamic Foundation is an independent Religious & humanitarian foundation that works to help millions of poor and vulnerable people regardless of race,political affiliation, gender or belief. It upholds the norm that safeguards humanity by leaving no one behind from receiving aid to end their needs.Our pioneering multi-national program enables many to […]

This post Nursery Teacher at The Islamic Foundation has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger