Wednesday 4 August 2021

WAZIRI NDUGULILE : ASILIMIA 16.7 PEKEE WANATUMIA HUDUMA ZA FEDHA BENKI, 48.6 MITANDAO YA SIMU

Dkt. Faustine Ndugulile

Na Magrethy Katengu - Dar es salaam
Waziri wa Mawasiliano na teknolojia ya habari Dkt. Faustine Ndugulile amesema takwimu za Matumizi rasmi ya mifumo ya fedha nchini bado sio nzuri ambapo asilimia 16.7% ya watu pekee ndio wanatumia huduma za benki,asilimia 48.6 wanatumia mitandao ya simu, asilimia 6.7 wanatumia njia zao binafsi na asilimia 28 hawatumi kabisa mifumo rasmi ya kifedha.

Dkt. Ndugulile ameyasema hayo  jijini Dar es salaam wakati wa uzinduzi wa huduma za benki ya CRDB Ndani ya ofisi za Posta nchini ambapo amesema anawapongeza CRDB na shirika la posta kwa ushirikiano walionao ambao utasaidia kuwafikia watanzania asilimia 28 ambao hawatumia mifumo rasmi ya kifedha.

Aidha Wizara hiyo inaandaa mradi wa utoaji anuani za makazi kwa kutambua kila mtaa na nyumba kwa kodi maalumu jambo ambalo litasaidia shirika la posta na mengine kuwafikishia huduma, vifurushi na barua wananchi kwenye makazi yao. 

Kwa upande Kaimu posta Master Mkuu Macrice Mbodo amesema serikali inaadhimia kutoa huduma zake ikiwemo huduma za RITHA,NIDA,TRA Na nyinginezo kupitia shirika la posta. Pia shirika limejikitaka katika utoaji wa huduma kidigital.

"Shirika la posta mpaka sasa lina ofisi zaidi ya 300 na kupitia kwa bia wake Dunia kote wana matawi zaidi ya laki sita", alisema Mbodo.

Naye Mkurugenzi wa Benki ya CRDB Abdulmakid Nsekela  amesema takwimu zinaonyesha kuwa watu 10 sita kati yao wapo kwenye mifumo rasmi ya kifedha lakini wengi wanatumia mitandao ya simu ambapo katika baadhi ya huduma hushindwa kuzifanya ikiwemo kuhifadhi fedha nyingi kwa wakati mmoja.

Aidha amesema CRDB inaamimi katika ubunifu katika kutatua changamoto za wananchi na imejipanga kuwekeza zaidi katika mifumo ya tehama katika kurahisisha utoaji huduma kwa wananchi.

Share:

NANHRI KUSHIRIKIANA NA SERIKALI , TAASISI KULINDA HAKI ZA RAIA

Share:

Tanzia : PADRE RAYMOND SABA AFARIKI DUNIA



Aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padre Raymond Saba amefariki duniani Agosti 3, 2021 majira ya saa 1 jioni katika hospitali ya Rabinitsia iliyopo jijini Dar es salaam aliyokuwa akipatiwa matibabu.

Katibu wa Askofu wa jimbo katoliki Kigoma, Evarist Guzuye, amesema misa takatifu ya mazishi itafanyika katika kanisa la Mtakatifu Marko Kabanga, wilayani Kasulu siku ya Jumatatu, Agosti 9, 2021.
Share:

MUME ADAIWA KUMUUA MKEWE KWA WIVU WA MAPENZI

Mkazi wa kata ya Malezi wilayani Handeni mkoani Tanga, Nassoro Mustapha anatuhumiwa kumuua mkewe kwa kumkata na panga sehemu mbalimbali mwilini ikielezwa sababu ni wivu wa mapenzi.

Tukio hilo limetokea jana Agosti 3, 2021 katika mtaa wa Kwamaraho inadaiwa kuwa mwanaume huyo alikuwa na ugomvi na mkewe na ndio uliomrudisha nyumbani.

Dada wa marehemu, Rehema Hemed amesema wanahisi tukio hilo limetokana na wivu wa mapenzi kwa sababu wanandoa hao walikuwa na ugomvi na kwamba shemeji yake alikuja nyumba wakiwa hawapo na kumshambulia mdogo wake.


Rehema amesema ndugu yake amefariki akiwa ni ujauzito wa miezi sita au na ameacha mtoto wa miaka mitatu.

Share:

EWURA Yasitisha Upandaji Bei za Gesi za kupikia


 Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imesitisha upandaji wa bei za gesi za kupikia zilizopanda maradufu katika baadhi ya maeneo nchini hadi hapo itakapotangazwa tena kutokana na upandaji wa bei hizo kutofuata taratibu.


Share:

Kenya Na Tanzania Zakutana Kujadili Changamoto Za Corona


 Na. WAMJW, Nairobi.
Makatibu Wakuu wa Wizara za Afya pamoja na Wataalam wa Wizara hizo kuoka nchini Tanzania na Kenya wamekutana leo jijini Nairobi na kuweza kujadili changamoto zinazowakabili nchi hizo mbili ikiwemo ya UVIKO-19 kwa upande wa mipakani.

Prof. Abel Makubi Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto nchini Tanzania amesema mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa Wizara ya Afya jijini Nairobi ulikuwa na lengo la kutekeleza makubaliano yaliyofanyika kati ya Marais wa nchi hizo mbili walipokutana mwaka huu jijini hapa wa kuondoa changamoto za masuala ya Corona kwa upande wa kibiashara.

Amesema mkutano huo ambao ulitanguliwa na kikao cha awali cha wataalum wa sekta hiyo na baadae kufuatiwa na kikao cha Makatibu Wakuu hao waliweza kujadiliana masuala ya upimaji wa Corona baina ya nchi hizo mbili na kuweza kukubaliana ni namna gani ya kuondoa changamoto za ugonjwa huo.

“Tumekutana ili kuweza kuondoa changamoto za Corona ambazo Marais wetu Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan na Mhe. Uhuru Kenyata walikutana na kuona yapo masuala yanayoleta changamoto hususan kwenye biashara kati ya Tanzania na Kenya na kuondoa mashirikiano katika mipaka yetu,hivyo kama wataalam tumekutana ili kuweza kuziondoa changamoto hizo na kuboresha mashirikiano”.

Prof. Makubi alitaja mambo waliyoyajadili ni pamoja na suala la kuhakikisha kwamba kunakuwa na mifumo inayoweza kuwasiliana katika upimaji kwa kuweza kuonekana kwa upande wa Tanzani na wakati huo huo kwa upande wa Kenya.

“Mfano kama mtu amepimwa ‘PCR’ basi aweze kusomwa na kuonekana pande zote mbili na mifumo yetu iweze kusoma kote na hiyo itaweza kusaidia kama nchi na wananchi wetu kuweza kufanya biashara vizuri” Aliongeza.

Aidha, kwa upande wa gharama za upimaji hususan kwa madereva wa magari makubwa alisema wamejadili na kutoa mapendekezo ambayo yatapekekwa kwenye kikao cha Mawaziri wa nchi hizo mbili, kikao ambacho kitakachofanyika siku ya Alhamisi na kuweza kutoa maamuzi ya mwisho.

Kwa upande wa mashirikiano katika kukabiliana na Corona kwa ujumla Prof. Makubi alisema wameweza kujadili masuala ya takwimu,chanjo pamoja na kubadilishana uzoefu baina ya nchi hizo mbili na mategemeo yao ni kwamba mapendekezo waliyoafikiana leo yataweza kuamliwa na kutolewa utekelezaji na Mawaziri hao ili shughuli za wananchi zisije kuathiriwa kwa uwepo wa Corona kwa maana ya shughuli za kikazi,familia na kibiashara.

Naye, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya kutoka Kenya Bi. Susan Mochache amesema kuwa mazungumzo kati ya wizara hizo mbili kuhusiana na ugonjwa wa Corona kama mazungumzo ya Marais wa nchi hizo mbili walivyokubaliana kushirikiana katika upande wa sekta ya afya hususan katika vita vya Corona wamejadili na kutoka na mapendekezo kadhaa.

Bi.Mochache alisema wamejadili kuweza kurahisisha biashara kati ya nchi hizo mbili ikiwemo biashara ya kupitisha mizigo tofauti ikiwemo chakula kutoka Tanzania kuingia Nchini Kenya na vile vile Kutoka nchini Kenya kuingia Tanzania.

“Tumekuwa na changamoto katika mipaka yetu kwasababu ya misimamno tofauti tuliyokuwa nayo baina ya nchi zetu hizi mbili lakini tumeweza kukubaliana vile tutawezesha uchumi na kibiashara kuendelea kuboreshwa na kuweza kuondoa miongozo na ‘protocol’ ile ambayo hazikuwa zinafaa kwa wanacnhi wa Kenya na Tanzania.

Alisema wameweza pia kuzungumza kuhusiana na mifumo ambayo inatumika baina ya nchi hizo mbili na kuweza kusaidi Serikali kwani awali kulikuwa na udanganyifu kwa madereva katika suala la upimaji.

Mkutano huu wa Makatibu Wakuu ni maandalizi ya Mkutano wa Mawaziri wa Afya Katika nchi mbili ambao unatarijiwa kufanyika keshokutwa jijini hapa.


Share:

Nafasi Mpya 9 za Kazi ya Ualimu St.Constantine International School | DEADLINE: 3rd September 2021


Kama unatafuta kazi kwa muda mrefu bila mafanikio, basi hii ni nafasi yako!! Hapa kuna  Nafasi 9 za walimu

_________

==>> Nafasi 9 za Ualimu St.Constantine International School
    1.Mathematics Teacher
    2.Primary Teacher
    3. EYFS Teacher
    4.Geography Teacher
    5.History Teacher
    6.Science Teacher
    7. Art Teacher
    8.Drama Teacher
    9.Early Years Foundation Stage Teacher
 

____________

BOFYA HAPA KUJUA ZAIDI NA KUTUMA MAOMBI



Share:

RC SENGATI AZINDUA CHANJO YA CORONA SHINYANGA...MGEJA ASEMA WANAOPOTOSHA NI MAGAIDI WASHUGHULIKIWE


Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akipata chanjo dhidi ya UVIKO - 19  wakati akizindua Chanjo dhidi ya UVIKO - 19 mkoa wa Shinyanga leo Jumatano Agosti 4,2021
**
Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akizungumza leo Jumatano Agosti 4,2021 wakati akizindua Chanjo dhidi ya UVIKO - 19 mkoa wa Shinyanga amesema Chanjo hiyo inatolewa kwa lengo la mwili kutengeneza kinga dhidi ya janga la Corona.

Amesema Chanjo dhidi ya UVIKO - 19 ni salama hivyo kuwasihi wananchi walio tayari kuchanjwa wajitokeze kuchanjwa huku akiwataka kuwapuuza wanaopinga chanjo hiyo.

"Leo katika mkoa wa Shinyanga tunaanza rasmi utoaji chanji dhidi
Kwa awamu ya kwanza tumepokea dozi 25,000 katika mkoa wa Shinyanga ambazo zitatolewa katika vituo 18 katika mkoa. Chanjo hii itasaidia kupunguza kasi ya maambukizi ya Virusi vya Corona hivyo nawaomba wananchi wajitokeze kupata chanjo hii ambayo inatolewa bure kwa wananchi ambao wapo tayari kuchanjwa",amesema Dkt.Sengati.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Taasisi ya Mzalendo Foundation ambaye pia ni Mwenyekiti Mstaafu wa CCM mkoa wa Shinyanga Khamis Mgeja akizungumza baada ya kupata chanjo ya UVIKO - 19 ameiomba serikali kuwachukulia hatua za kisheria watu wanaopotosha kuhusu Chanjo ya COVID - 19 akisema hao ni sawa na magaidi.

"Hawa wanaopotosha kuhusu Chanjo ya UVIKO - 19 ni magaidi. Upotoshaji huu ni aina mpya ya Ugaidi wachukuliwe kama wahalifu wengine. Kama unazuia watu wasichanjwe maana yake unataka wafe, kwa hiyo hawa ni sawa na magaidi",amesema Mgeja.

"Wanaopotosha dhidi ya Chanjo ya UVIKO - 19  wachukuliwe kama wahalifu wengine. Hawa ni sawa na wauaji wa Kimbari. Wachukuliwe hatua za kisheria, tusiwachekee kwani ukicheka na Nyani utavuna mabua",amesema Mgeja.

Ameeleza kuwa Taaluma ya Kitaalamu inakosolewa kitaalamu siyo kuingiza siasa na upotoshaji hivyo wanaopinga chanjo ya UVIKO - 19 ni bora wakae kimya au watupe mbadala wa chanjo badala ya kupotosha tu.

"Ninampongeza Mhe. Rais Samia Suluhu kwa kukubali Watanzania wapatiwe chanjo dhidi ya UVIKO - 19 na Mkuu wetu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati kuhamasisha wananchi wapate chanjo, nami nimejitokeza kuwa miongoni mwa Watanzania wa mwanzo kabisa kuchanjwa chanjo dhidi ya UVIKO - 19. Naomba wananchi wajitokeze kuchanjwa....Akili za kuambiwa changanya na zako, wawapuuze hao wapotoshaji, hao magaidi",ameongeza Mgeja.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akizungumza wakati akizindua Chanjo dhidi ya UVIKO - 19 mkoa wa Shinyanga leo Jumatano Agosti 4,2021 
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akizungumza wakati akizindua Chanjo dhidi ya UVIKO - 19 mkoa wa Shinyanga
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt. Yudas Ndungile akizungumza wakati wa uzinduzi wa  Chanjo dhidi ya UVIKO - 19 mkoa wa Shinyanga leo Jumatano Agosti 4,2021 
Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga Bi. Zuwena Omary akizungumza wakati wa uzinduzi wa  Chanjo dhidi ya UVIKO - 19 mkoa wa Shinyanga leo Jumatano Agosti 4,2021.

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akisaini Fomu ya Uhiari wa kupata chanjo dhidi ya UVIKO - 19  wakati akizindua Chanjo dhidi ya UVIKO - 19 mkoa wa Shinyanga leo Jumatano Agosti 4,2021
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akipata chanjo dhidi ya UVIKO - 19  wakati akizindua Chanjo dhidi ya UVIKO - 19 mkoa wa Shinyanga leo Jumatano Agosti 4,2021
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akipata chanjo dhidi ya UVIKO - 19  wakati akizindua Chanjo dhidi ya UVIKO - 19 mkoa wa Shinyanga leo Jumatano Agosti 4,2021
Mwenyekiti wa Taasisi ya Mzalendo Foundation ambaye pia ni Mwenyekiti Mstaafu wa CCM mkoa wa Shinyanga Khamis Mgeja akipata chanjo dhidi ya UVIKO - 19  wakati Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akizindua Chanjo dhidi ya UVIKO - 19 mkoa wa Shinyanga leo Jumatano Agosti 4,2021
Mwenyekiti wa Taasisi ya Mzalendo Foundation ambaye pia ni Mwenyekiti Mstaafu wa CCM mkoa wa Shinyanga Khamis Mgeja akizungumza baada ya kupata chanjo dhidi ya UVIKO - 19  wakati Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akizindua Chanjo dhidi ya UVIKO - 19 mkoa wa Shinyanga leo Jumatano Agosti 4,2021
Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Festo Kiswaga akipata chanjo dhidi ya UVIKO - 19  wakati Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akizindua Chanjo dhidi ya UVIKO - 19 mkoa wa Shinyanga leo Jumatano Agosti 4,2021
Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude akipata chanjo dhidi ya UVIKO - 19  wakati Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akizindua Chanjo dhidi ya UVIKO - 19 mkoa wa Shinyanga leo Jumatano Agosti 4,2021
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP George Kyando akipata chanjo dhidi ya UVIKO - 19  wakati Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akizindua Chanjo dhidi ya UVIKO - 19 mkoa wa Shinyanga leo Jumatano Agosti 4,2021
Mkurugenzi wa Malunde 1 blog / Mwandishi wa Habari/ Blogger, Kadama Malunde akipata chanjo dhidi ya UVIKO - 19  wakati Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akizindua Chanjo dhidi ya UVIKO - 19 mkoa wa Shinyanga leo Jumatano Agosti 4,2021
Mwenyekiti wa Kamati ya Amani Mkoa wa Shinyanga Sheikh Hamis Balilusa akipata chanjo dhidi ya UVIKO - 19  wakati Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akizindua Chanjo dhidi ya UVIKO - 19 mkoa wa Shinyanga leo Jumatano Agosti 4,2021
Mkurugenzi wa Karena Hotel,Josephine Wambura akipata chanjo dhidi ya UVIKO - 19 wakati Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akizindua Chanjo dhidi ya UVIKO - 19 mkoa wa Shinyanga leo Jumatano Agosti 4,2021
Mwandishi wa Habari, Marco Mipawa akipata chanjo dhidi ya UVIKO - 19  wakati Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akizindua Chanjo dhidi ya UVIKO - 19 mkoa wa Shinyanga leo Jumatano Agosti 4,2021
Mwandishi wa Habari, Shaban Alley akipata chanjo dhidi ya UVIKO - 19  wakati Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akizindua Chanjo dhidi ya UVIKO - 19 mkoa wa Shinyanga leo Jumatano Agosti 4,2021
Dkt. Danny Mzee akipata chanjo dhidi ya UVIKO - 19  wakati Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akizindua Chanjo dhidi ya UVIKO - 19 mkoa wa Shinyanga leo Jumatano Agosti 4,2021
Mnadhimu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga, Joseph Paul akipata chanjo dhidi ya UVIKO - 19  wakati Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akizindua Chanjo dhidi ya UVIKO - 19 mkoa wa Shinyanga leo Jumatano Agosti 4,2021
Wadau wakifuatilia matukio wakati Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akizindua Chanjo dhidi ya UVIKO - 19 mkoa wa Shinyanga leo Jumatano Agosti 4,2021
Wadau wakifuatilia matukio wakati Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akizindua Chanjo dhidi ya UVIKO - 19 mkoa wa Shinyanga leo Jumatano Agosti 4,2021
Share:

Social Worker at Save the Children

Social Worker     CHILD SAFEGUARDING: Level 3: √ the post holder will have contact with children and/or young people either frequently (e.g. once a week or more) or intensively (e.g. four days in one month or more or overnight) because they work country programs; or are visiting country programs; or because they are responsible for […]

This post Social Worker at Save the Children has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Head of Human Resources at TradeMark East Africa

Head of Human Resources    TradeMark East Africa (TMEA) is an ald-for-trade organisa­tion that was established with the aim of growing prosper­ity in East Africa through increased trade. TMEA. which is funded by a range of development agencies, operates on a notfor- profit basis. TMEA is funded by the development agencies of the following countries: […]

This post Head of Human Resources at TradeMark East Africa has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger