Thursday 29 July 2021

MUME ASAKWA NA POLISI TUHUMA ZA KUUA MKE BAADA YA KUNYIMWA TENDO LA NDOA


Mwanamke aliyejulikana kwa jina la Fausta Silayo (22), mkazi wa kijiji cha Samanga wilayani Rombo mkoa wa Kilimanjaro ameuawa kwa kuchomwa kisu na mume wake kwa madai ya kumnyima unyumba.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro Simon Maigwa
mwanamke huyo ambaye bado alikuwa uzazi wa mwezi mmoja alichomwa kisu Julai 23,2021 na kufariki dunia Julai 24,2021 wakati akipatiwa matibabu Hospitalini.

"Chanzo cha tukio hili inadaiwa kuwa ni mtuhumiwa kunyimwa kushiriki unyumba Jeshi la polisi linaendelea na jitihada za kumtafuta mtuhumiwa wa tukio hilo ambaye inasemekana amekimbilia nchi jirani ili kumkamata na kumchukulia hatua za kisheria",amesema Kamanda Maigwa.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA JULAI 30,2021



Share:

Logistics Intern at Coca-Cola Kwanza

Logistics Intern    Coca-Cola Kwanza is looking to place outstanding recent graduates into a one year Graduate in Training (GIT) program across exciting role opportunities including finance, logistics, manufacturing, and sales intelligence functions. This program will help develop world class leaders through functional and cross functional rotation, challenging assignments, business projects, integrated training and development, […]

This post Logistics Intern at Coca-Cola Kwanza has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Nafasi 10 za Kazi Dar es Salaam University College of Education (DUCE)


Dar es Salaam University College of Education (DUCE) wametangaza nafasi mbalimbali za kazi za mikataba kama ifuatavyo.

1.Artisan II - Public Addressing System- Nafasi 2

2.Artisan II - Electrical- Nafasi 1

3.Driver II

4.Health Laboratory Assistant II

5.Personal Assistant of Staff with Disabilities and Special Needs

6.Cook II

==>>Kujua zaidi na  jinsi ya kutuma maombi, <<Bofya Hapa>> 

▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬  

 



Share:

Benki Kuuu Ya Tanzania Yatangaza Mambo Matano Yatakayosaidia Kuongeza Upatikanaji Wa Mikopo Kwa Sekta Binafsi Na Kupunguza Viwango Vya Riba.



Share:

Lead Generator Agency Nyanza Branch at NBC

Lead Generator Agency Nyanza  Branch   NBC is the oldest serving bank in Tanzania with over five decades of experience. We offer a range of retail, business, corporate and investment banking, wealth management products and services. Key Accountabilities A :   Agent On boarding / Lead Generation   On board and process applications of Agents in line with […]

This post Lead Generator Agency Nyanza Branch at NBC has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Lead Generator Agency Iringa Branch at NBC

Lead Generator Agency Iringa  Branch   NBC is the oldest serving bank in Tanzania with over five decades of experience. We offer a range of retail, business, corporate and investment banking, wealth management products and services. Key Accountabilities A :   Agent On boarding / Lead Generation   On board and process applications of Agents in line with […]

This post Lead Generator Agency Iringa Branch at NBC has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Wachimbaji wadogo na malalamiko yasiyo na Mwisho Busega, Simiyu

Samirah Yusuph
Busega. Fukuto la mgogoro wa wachimbaji wadogo katika mgodi wa Imalamate wilayani Busega  Mkoa wa Simiyu baina ya wamiliki wa leseni na wenye mashamba kuhusu mgawanyo wa mazao ya dhahabu linaendelea kuibua malalamiko.

Wachimbaji hao wamekuwa wakidai kuwa hawatendewi haki na wamiliki  wa leseni katika mazao yanayopatikana hali inayowalazimu kutoa mgao hata katika huduma za kijamii kama usimamizi na ulinzi ambazo zilipaswa kulipwa na wenye leseni.

"Licha ya kuwa utaratibu unaelekeza majukumu ya mmliki wa leseni  lakini bado walinzi na "inspectors" tunawapa mgao jambo ambalo linakuwa ni unyonyaji kwa wachimbaji wadogo" alisema Jumanne Tembe mmoja wa wachimbaji wadogo katika mgodi wa Imalamate.

Licha ya malalamiko hayo Baadhi ya wachimbaji wamelaumu wasimamizi wa mgodi kutoza pesa ya usafi na kuweka alama katika mifuko ya mawe bila kutoa risiti jambo ambalo wamelishuku kuwa ni upotevu wa mapato ya serikali pamoja na dhuruma kwa sababu pesa wanayotozwa ni kubwa.

"Mfuko mmoja unalipiwa tsh27,000 unapo utoa kwenye duara na kuufikisha katika uzio ili uwekewe alama lakini pesa inapokelewa bila kutolewa risiti ni bora malipo yafanyike na risiti itolewa ili ijulikane pesa hiyo inaenda wapi na inafanya nini".alisema Amos Mwambebo mchimbaji katika mgodi huo.

Akitoa ufafanuzi dhidi ya mgawanyo wa mazao ya dhahabu yanayopatikana Afisa madini wa mkoa wa Simiyu Amin Msuya alisema kuwa mgawanyo unakakwenda katika makundi manne na kuyabainisha makundi hayo kuwa,

"Mrahaba wa serikali asilimia saba, mmiliki wa shamba asilimia 10, mmiliki wa leseni asilimia 20 na mwenye
 Duara anabakiwa na asilimia 70, mwenye jukumu la kulipa usimamizi na ulinzi ni mmliki wa leseni katika asilimia zake".

Akitatua kero hiyo mkuu wa wilaya ya Busega, Gabriel Zakaria aliwataka wasimamizi wa mgodi kutekeleza maagizo ya serekali ikiwa ni pamoja na kufuata mikataba ya makubaliano ya mgao, kuboresha miundombinu ya barabara na upatikanaji wa huduma za kijamii.

"Mapato ya serikali ni lazima yakusanywe, haki itendeke kwa kila mmoja hakuna sababu ya kuendelea kuwa na mgogoro halikuwa utaratibu upo wazi katika migodi niwakati wa  kutekeleza ili kila mmoja anufaike na madini yaliyopo".

Mwisho.


Share:

Mabula Atatua Mgogoro Wa Mpaka Kati Ya Newala Na Masasi


 Na Munir Shemweta, MTWARA
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amemaliza utata wa muda mrefu kuhusiana na mgogoro wa mpaka kati ya wilaya ya Masasi na Newala mkoani Mtwara baada ya kubainisha mpaka halisi baina ya pande hizo mbili.

Akiwa ameambatana na wataalamu wa sekta ya ardhi katika mkoa wa Mtwara, Wakuu wa wilaya za Masasi na Newala, Wabunge pamoja na Wakurugenzi wa halmashauri zinazopakana ikiwa ni utelelezaji wa maagizo ya Makamu wa Rais Dkt Philip Isdor Mpango, Dkt Mabula alibainisha mpaka halisi uliopo kati ya kijiji cha Njenga na Miyuyu ikiwa ni takriban kilometa tano kutoka ulipoainishwa mpaka wa awali.

Akizungumza wakati wa usuluhishi wa mgogoro huo Julai 28, 2021 Naibu Waziri Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Mabula alisema, jambo kubwa lililotatiza kwenye  mgogoro huo wa mpaka ni uhitaji wa maeneo ya kiutawala ambapo upande wa wakuu wa wilaya alisema hawakuwa na tatizo.

‘’Jambo linalotatiza sisi wengine ni katika suala zima ni sisi wachaguliwa kutaka maeneo ya kiutawala na wakuu wa wilaya wanasema hawana matatizo na ndiyo watawala sisi wachaguliwa hatutakiwi kuingia kabisa kwenye migogoro’’ alisema Dkt Mabula

Dkt Mabula aliongeza kuwa, iwapo kuna tatizo la kiutendaji kwenye eneo hilo basi wakuu wa wilaya wa maeneo husika wanaweza kushughulikia lakini kwa shida ya mipaka ya kiutawala  basi wakurugenzi wa halmashauri wana mamlaka ya kukubalina kwa kuwa suala hilo  linaangukia TAMISEMI na kusisitiza kwamba halmashauri zikikubaliana kazi ya wizara ya ardhi ni kubainisha mipaka.

Aliwaagiza Wakurugenzi wa halmashauri za wilaya za Masasi na Newala mkoani Mtwara kwenda kwa wananchi wa vijiji vyenye migogoro kwa ajili ya kuzungumza na kuwapa elimu wakati kwa sasa mpaka unaotambuliwa ukiwa ni ule alioanishwa na yeye kulingana na vipo vya kitaalamu vinavyoonesha.

‘’Kama kuna maelezo mengine kuhusiana na mpaka huu wa Newala na Masasi basi itabidi watendaji na viongozi wa maeneo husika wakae pamoja na kushughulikia mgogoro huo ikiwa ni pamoja na kwenda uwandani, lengo ni kijiridhisha maana huwezi kupata suluhu ukiwa ofisini na mtkachokubaliana Wizara itakwenda kuweka alama za mipaka.

Diwani wa Kata ya Chilangala mkoani Mtwara Jamali Jafu aliutetea mpaka wa awali kati ya wilaya hizo mbili kwa kusema mpaka huo unapaswa kubaki eneo la Miyuyu  kwa kuwa ni mpaka wa asili tangu mababu kabla ya kuzaliwa wilaya ya Masasi.

Mkuu wa wilaya ya Masasi Claudia Kitta alisema, baada ya kuanishwa kwa mpaka huo kwa kuhusisha wataalamu wa pande zote sasa mpaka unaotambuliwa ubaki ulioanishwa na Naibu Waziri wa Ardhi na iwekwe alama katika eneo lililotambuliwa huku suala la vijiji vilivyoingia eneo lingine likifanyiwa kazi.

‘’Tukubaliane mipaka ni sahihi na vipimo vinaonesha na hili linguine la vijiji basi tutaangalia kijiji gani kimeingia huku au kimeingia kule na hili si tatizo kwa kuwa kinajitambua na huduma za jamii hazina mipaka’’ alisema Mkuu wa Wilaya ya Masasi Claudia Kitta

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Newala Alhaji Rajabu Kundya alisema, suala muhimu katika mgogoro huo ni kumaliza migogoro iliyopo kwenye vijiji vya mpaka na kueleza kuwa hatua hiyo itaoongoza maeneo ya uwajibikaji na kuonesha mpaka halisi wa wilaya na wilaya.


Share:

Dk. Mwinyi Umefika Wakati Wa Kuunda Tume Kupambana Na Udhalilishaji.

 Rais Wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi  amesema umefika wakati wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuunda tume ya kupambana na Udhalilishaji wa Kijinsia visiwani Zanzibar kwa ajili ya kupambana na udhalilishaji visiwani humo. 


Rais Dk. Mwinyi ameyasema hayo kwenye  kongamano la udhalilishaji liloandaliwa na Jumuiya ya Wanasheria Wanawake wa Zanzibar katika ukumbi wa Shekh Idriss Abdul - Wakil, Kikwajuni Jijini Zanzibar.


 Aidha Mhe. Rais Mwinyi amewataka watendaji wa Taasisi zote zinazohusika na suala la udhalilishaji kujipima juu ya utendaji wao. Hii ni baada ya kuendelea kutolewa malalamiko Kwa baadhi ya watu ambao wanashutumiwa Kwa vitendo vya udhalilishaji kuachiliwa huru.


Udhalilishaji sio suala la ubakaji tu, kwani waathirika wakubwa japo wanaonekana ni wanawake lakini wapo wanaume wengi ambao wanadhalilishwa pia. Alisema Mhe. Rais Mwinyi.


“Nimekuja hapa kuwapeni Uhakika wa kwamba ninayo dhamira ya dhati kulimaliza tatizo la udhalilishaji visiwani kwetu. “


Katika hatua nyingine, Mhe. Rais amemtaka Jaji Mkuu wa Zanzibar, Mhe. Omary Makungu kuwahimiza majaji na mahakimu waliochini ya Mhimili wake kutekeleza wajibu wao Kwa wakati na Kwa Uadilifu ili kulinda haki za watu ambao wametendewa unyanyasaji wa kijinsia.


Mhe.  Rais, Dk. Mwinyi, amezishukuru taasisi na asasi binafsi ambazo zimekuwa zikitoa misaada ya kisheria kwa Wananchi wa Zanzibar kwani licha ya Kwamba ni wajibu wa Serikali kutoa huduma na misaada ya kisheria, lakini taasisi hizi zimekuwa msaada mkubwa.



Share:

Waziri Ndugulile Aendesha Kikao Cha Mapato Na Matumizi Ya Wizara Na Taasisi Zake

Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Faustine Ndugulile ameendesha kikao cha mapato na matumizi ya robo ya nne ya mwaka wa fedha wa 2020/21 baina ya menejimenti ya Wizara hiyo na taasisi za Wizara hiyo ikiwemo Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Shirika la Posta Tanzania (TPC), Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), Tume ya TEHAMA (ICTC) na Baraza la Watumiaji wa Huduma ya Mawasiliano (TCRA – CCC) ambacho kimefanyika kwenye ukumbi wa Kikwete, Dodoma

Ameongeza kuwa kwa kipindi hicho cha mwezi Aprili hadi Juni, 2021, Wizara kwa kushirikiana na taasisi zake imefanikisha utekelezaji wa majukumu yake ya kuongeza mapato ya taasisi hizo ikiwemo taasisi ya UCSAF, TTCL na TPC.

Amesema kuwa ameazimia kuzima laini za simu za mkononi 18,622 ambazo hazijahakikiwa pamoja na kuziua vitambulisho vya taifa 14,768 vilivyosajili laini za simu kwa utapeli na Serikali itawatafuta matapeli hao ili waweze kuchukuliwa hatua

Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Zainab Chaula amesema kuwa kikao hicho kimefanyika ili kufanya tathmini ya utekelezaji wa majukumu na mapato na matumizi ambapo Wizara imekusanya mapato ya Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano ya shilingi bilioni 45 ambayo yamezidi makadirio ya shilingi bilioni 30. Pia, ameishukuru Serikali kwa kuongeza bajeti ya Wizara ya mwaka wa fedha wa 2021/22 kufikia shilingi bilioni 240 ukilinganisha bajeti ya shilingi bilioni 15 ya mwaka wa fedha 2020/21.

Naye Kaimu PostaMasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Macrice Mbodo amesema kuwa huu ni utaratibu mzuri baina ya Wizara na taasisi zake kwa kuwa kila baada ya miezi mitatu kikao kinafanyika na kwa kipindi hicho Shirika limezalisha faida ya shilingi bilioni 3.6; kuboresha huduma ya duka mtandao ambapo wajasiriamali wadogo wanafanya biashara duniani kote

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Mwita Vedastus amesema kuwa Shirika limepata faida ya shilingi bilioni 12 kwa mwaka na kwa robo ya nne ya mwaka wa fedha wa 2020/21 wamepata faida ya shilingi bilioni 2 kwa mapato ambayo hayajakaguliwa pamoja na kutoa huduma ya data kwa wateja 223,000 wa taasisi za ndani na nje ya nchi na watu binafsi

Afisa Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), Justina Mashiba amesema kuwa kikao hicho kinawezesha kupeana mrejesho baina ya Wizara na taasisi zake ili kufahamu mapato na matumizi kwa kipindi hicho ambapo UCSAF imezidi malengo kwa kukusanya mapato ya shilingi bilioni 9 tofauti na makadirio yaliyopangwa awali ya kukusanya shilingi bilioni 8

Ameongeza kuwa wamefanikisha ujenzi wa minara 60 ambayo imekamilika na kutangaza zabuni za kupeleka mawasiliano mipakani katika kata 190 na halmashauri 10 kwa kuwa zinahamia majengo mapya ili wapate huduma za mawasiliano


Share:

Waziri Ummy Atoa Siku 7 Kwa Vyombo Vya Usalama Kuchunguza Vifo Vya Wanafunzi Watatu Mpwapwa


Nteghenjwa Hosseah, Mpwapwa
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Ummy Mwalimu ametoa siku 7 kwa vyombo vya Ulinzi na Usalama kuchunguza vifo vya wanafunzi 3 waliofariki kwa kufunikwa na kifusi katika Shule ya Msingi Mbori, Kata ya Motondo Wilayani Mpwapwa.

Wakati huo huo Mhe. Ummy amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kuwaondoa Walimu wote wa shule ya Msingi Mbori kupisha uchunguzi unaondelea.

Waziri Ummy ametoa kauli hiyo wakati aliposhiriki kuaga Miili ya wanafunzi 3 waliofariki kwenye ajali ya kufukiwa na Mchanga katika shule ya Msingi Mbori tarehe 27.07.2021.

Akiwa shuleni hapo Waziri Ummy amelaani vikali Vitendo vya Walimu kuwafanyisha kazi siziso stahili za wanafunzi tofauti na ilivyoelekezwa kwenye Waraka wa Elimu bila Malipo No. 3 wa Mwaka 2016.

Amesema “ Hatukatazi mwanafunzi kufanya kazi zinazomjenga kama vile Stadi za kazi lakini sio kumfanya mwanafunzi kama Kibarua unawezaje kumwambia mtoto akachimbe mchanga wa kujengea au akaponde kokoto tena bila Uangalizi wa Walimu “ Alihoji

Katika Shule ya Msingi Mbori tumeleta sh. Mil.12 kwa ajili ya Ujenzi wa Choo na fedha za mchanga zimejumlishwa humo inakuwaje walimu watume watoto kwenda kuchimba mchanga wa mtoni,  kuna uzembe hapa umefanyika na tutachukua hatua.

Pia Waqziri Ummy aliwataka Wakuu wa shule zote Nchini na walimu wa ujumla kuacha kuwatumikisha wanafunzi wawapo shuleni na wazingatie Waraka wa Elimu bila Malipo no 3. wa mwaka 2016 ambao unatoa ufafanuzi wa kina wa jukumu la kila mdau wa Elimu.

“Jukumu la Ujenzi wa Miundombinu ya shule ni la Wazazi pamoja na Jamii inayozunguka na sio wanafunzi, Walimu na Kamati za shule mnatakiwa kuhamaisha Wazazi na jamii kujitolea kujenga miundombinu hiyo na sio kutumikisha wanafunzi” alisistiza Waziri Ummy.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe.Josephat Maganga  amesema watoto waliofariki kwenye ajali ya kufukiwa na kifusi shuleni hapo ni watatu ambao ni Isaya Lucas Hamis, Rehema Alex na Daud Enock Mchea na watoto wengine watano walijeruhiwa wametibiwa na kuruhusiwa kurejea majumbani kwao.

Tukio la Watoto kufukiwa na kifusi lilitokea Tarehe 27.07.2021 katika Shule ya Msingi Mbori iliyopo Kata ya Matomondo Wilayani Mpwapwa baada ya watoto hao kupewa kazi na walimu wao kuchimba mchanga kwa ajili ya ujenzi wa choo unaondelea shuleni hapo.


Share:

TCRA YASHIRIKI MBIO ZA MWENGE MAALUM 2021 IPAGALA JIJINI DODOMA

Afisa Mawasiliano Mwandamizi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Mabel Masasi akiwapa maelezo viongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru ulipowasili katika Shule ya Msingi Ipangala 'B' iliyopo jijini Dodoma wakati wa mbio za Mwenge Maalum 2020/21 ikiwa ni ishara ya TCRA kuunga mkono kauli mbiu ya mbio hizo isemayo "TEHAMA ni msingi wa wa Taifa endelevu; itumike kwa usahihi na uwajibikaji"
Afisa Habari wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Robin Ulikaye akiwapa elimu wanafunzi wa shule ya msingi Ipagala B Wakati TCRA ikiwa katika ushiriki wa kutoa elimu katika mbio za Mwenge wa Uhuru jijini Dodoma.
Afisa Mwandamizi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)Mabel Masasi akikabidhi kitabu cha Mwongozo wa Huduma kwa Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano Tanzania kwa viongozi wa Mbio za Mwenge Maalum 2020/21 ikiwa ni ishara ya TCRA kuunga mkono kauli mbiu ya mbio za mwenge mwaka huu isemayo "TEHAMA ni msingi wa Taifa endelevu; itumike kwa usahihi na uwajibikaji"
Baadhi ya viongozi wakipata huduma za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Wakati Mwenge wa Uhuru ulipokwenda katika Shule ya Msingi ya Ipagala B jijini Dodoma.
Share:

Lead Generator Agency Kahama Branch at NBC

Lead Generator Agency Kahama Branch   NBC is the oldest serving bank in Tanzania with over five decades of experience. We offer a range of retail, business, corporate and investment banking, wealth management products and services. Key Accountabilities A :   Agent On boarding / Lead Generation   On board and process applications of Agents in line […]

This post Lead Generator Agency Kahama Branch at NBC has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Lead Generator Agency Musoma Branch at NBC

Lead Generator Agency Musoma Branch   NBC is the oldest serving bank in Tanzania with over five decades of experience. We offer a range of retail, business, corporate and investment banking, wealth management products and services. Key Accountabilities A :   Agent On boarding / Lead Generation   On board and process applications of Agents in line […]

This post Lead Generator Agency Musoma Branch at NBC has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Board Member Vacancy at TOL Gases Limited

BOARD MEMBER VACANCY TOL Gases Limited is the leading manufacturer and distributor of Industrial and Medical Gases. Additionally the Company distributes high quality brands of welding and related consumables as well as medical oxygen related appliances within Tanzania and the neighbouring countries through distributorship arrangements. The Company was established in the 1950’s and has been […]

This post Board Member Vacancy at TOL Gases Limited has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

OFA! Viwanja vilivyopimwa vinauzwa Mbezi- Kwembe Kwa Bei Nzuri Kabisa


Ofa! Ofa! Viwanja vilivyopimwa vinauzwa Mbezi- Kwembe- Nyuma ya ofisi za halmashauri ya Ubungo, kituo cha Luguruni. Ukubwa ni kuanzia Sqm 400 Bei sqm 1 =17,500/= (7,000,000/=). 
 
Malipo ndani ya miezi sita. Kianzio 25% ya bei ya kiwanja. Eneo ni zuri lina Umeme, maji na kuna watu wa kutosha
0659 972868
0759 461893


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger