Thursday 22 July 2021
POLISI WASEMA MBOWE ANAKABILIWA NA TUHUMA ZA KUPANGA NJAMA ZA KUFANYA VITENDO VYA KIGAIDI
RAIS SAMIA AOMBOLEZA KIFO CHA ANNA MGHWIRA
ANNA HENGA : MATATIZO YA NDOA YANASABABISHA WANAWAKE KULEA WATOTO PEKE YAO
GOLD FM YATAMBULISHWA RASMI IKIUNGURUMA KUTOKA KAHAMA, TCRA YAKABIDHI LESENI ,KANUNI ZA UTANGAZAJI
Tanzia: ALIYEKUWA MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO ANNA MGHWIRA AFARIKI DUNIA
MUME AUA MKE AKIOMBWA HELA YA ADA YA MTOTO
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida Kamishna Msaidizi (ACP) Stella Mutabihirwa, akiwaonesha waandishi wa habari (hawapo pichani) misokoto ya bangi iliyokamatwa na jeshi hilo.
Project Manager at BRAC Tanzania
Project Manager Full TimeTanzaniaPosted 4 hours ago BRAC Tanzania The ideal candidate will be responsible for the overall daily management of the Project including supervision of staff, planning, budgeting, implementation, and M&E. The specific responsibilities include. Responsibilities Project Planning Ensuring that all program activities are developed and implemented in accordance with the organization’s […]
This post Project Manager at BRAC Tanzania has been posted by Udahiliportaldaily
Get more post by visiting Udahiliportal.com
know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
Njombe:Wapenzi wafia chumbani kwa jiko la mkaa
Na Amiri Kilagalila,Njombe
Watu wawili wamepoteza maisha mkoani Njombe baada ya kuingia na jiko la mkaa ndani ya chumba cha kulala kwa lengo la kupunguza baridi Mkoani Njombe.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Njombe Hamisi Issa amethibitisha kutokea kwa tukioa hilo lililowakuta Benitho Mbatha (23) mpiga debe wa mjini Njombe na Jazila Said Mndendeule (27) mkazi wa Namtumbo.
“Baada ya kufariki hakuna mtu ambaye aligundua kama kuna watu wamefariki,tukio hili limetokea tarehe 17 mwezi wa saba majira ya saa tano na nusu huko mtaa nwa National Housing kata ya Njombe mjini wakiwa wamelala kwenye chumba kimoja”alisema Kamanda Hamis Issa
Aidha amesema “Sababu ya kifo chao inaonyesha wakati wakiwa hai waliweka moto wa mkaa kwa ajili ya kujihifadhi na baridi na huu mtindo wa kuweka mkaa kwa watu wa Njombe ndio mtindo wao”alisema Hamis Issa
Aidha kamanda Issa ametowa wito kwa wananchi wa Njombe kutumia njia nyingine kujikinga na baridi na si kuota moto kama ambavyo wengi wamekuwa wakifanya kwa kwani kufanya hivyo ni hatari kwa maisha yao.
“Niwaombe wananchi wewe unaona Chumba chako ni kidogo na unatumia mkaa ndani hiyo ni hatari nyingine na huko lilikotokea tukio chumba ni kidogo na kina dirisha moja na dogo sana.Acheni kulala na jiko ndani ya nyumba sasa hivi ni hatari tafuteni nguo nzito nzito za kuzuia baridi lakini sio moto wa mkaa”alisema kamanda Issa
Kamanda Issa amesema tukio hilo ni la tatu kutokea mkoani Njombe kutokana na tukio jingine kumkuta dada mkazi wa Songea aliyekuwa mhudumu wa baa moja mjini Njombe kufariki ndani kwa jiko la mkaa huku mwingine akifariki wilayani Wanging’ombe kwa jiko la mkaa.
Amani Samsoni Mwalongo ni mmiliki wa Nyumba aliyokuwa akiishi marehemu Benitho Mbata huku akiwa ni mtu wa kwanza kushuhudia tukio hilo baada ya yeye kwenda kumtembelea marehemu na kuwaona wote wawili wakiwa wamefariki
“Lakini bado mimi nilifuatilia kwa majirani wanasema yule mwanamke alikuwa anaelekea Madaba,alikosa nauli na huyu kijana kwa kuwa yupo pale kwenye magari akamwambia njoo upumzike kwanza na kesho nitakusaidia nauli ya kukufikisha kwenu kwa hiyo hiki kitu kinahuzunisha sana”alisema Amani Samson
Kwa upande wao Majirani wanasema “Marehemu huwa anapenda sana kuja hapa na alikuja pia akachukua moto na akachukua chipsi Mayai akasema nina mgeni wangu huko ndani lakini siku baada ya siku tukashangaa haonekani mpaka tulipoona wanakuja polisi,lakini sio vizuri kwenda kulala sehemu usioijua kwa mfano hapo huyo mwanaume angefariki halafu angebaki mwanamke tayari angekuwa na kesi ya kujibu”alisema mmoja wa majirani.
Kauli Ya Serikali Kuhusu samaki waliokutwa wamekufa ufukweni Dar es Salaam
Tarehe 21 mwezi Julai, 2021 saa 3:30 asubuhi, ofisi ndogo ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi Mkoa wa Dar es Salaam ilipokea taarifa kutoka kwa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kipolisi Ilala kuhusu tukio la kuelea kwa samaki waliokufa katika ufukwe uliyopo karibu na Hospitali za Agha Khan na Ocean Road jijini Dar es Salaam.
Kufuatia taarifa hiyo maafisa uvuvi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi waliuomba uongozi wa kipolisi Ilala kuimarisha ulinzi eneo hilo ili kuzuia wananchi kuchukua samaki waliokuwa wakielea ufukweni hapo wakati hatua zaidi za haraka zikichukuliwa kuzuia uingizaji wa samaki hao katika Soko la Magogoni Feri lililopo karibu na eneo la tukio.
Baada ya kuimarisha ulinzi eneo la Soko la Magogoni Feri na eneo la tukio, wananchi kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi, maafisa wa wizara, Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI), maafisa uvuvi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam wakiwa na meneja wa Soko la Magogoni Feri walikusanya samaki kiasi cha Kilogramu 164 na kufikisha Kituo Kikuu cha Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam.
Baada ya kutolewa kwa ufafanuzi wa hali iliyojitokeza ilikubaliwa kuwa sampuli za samaki hao zichukuliwe kwa ajili ya uchunguzi wa kimaabara ili kubaini sababu za vifo vya samaki hao.
Sampuli zilichukuliwa kwa ajili ya maabara ya TAFIRI, maabara ya Taifa ya Uvuvi (Dar es Salaam) na Polisi Kitengo cha Sayansi ya Uchunguzi (Forensic Investigation) kwa ajili ya kupeleka maabara ya mkemia mkuu wa serikali.
Kiasi cha Kilogramu 156 kilichosalia kilikabidhiwa kwa afisa uvuvi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa ajili ya kuteketezwa na tukio la kuteketezwa lilishuhudiwa na maafisa wa wizara, uongozi wa Soko la Feri, ofisi ya uvuvi Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam na wananchi waliokuwepo eneo la Soko la Magogoni Feri.
Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi inapenda kuwashukuru wananchi wote waliokuwepo kwenye ufukwe wa hospitali za Agha Khan na Ocean Road pamoja na Soko la Magogoni Feri wakati wa tukio hili kwa ushirikiano mkubwa waliouonyesha uliofanikisha kuzuia kuingizwa kwa samaki hao sokoni na hatimaye kuteketezwa na afisa uvuvi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.
Aidha, Wizara inapenda kuwaasa wananchi kuendelea na biashara ya samaki katika masoko ya Jiji la Dar es Salaam kama ilivyo kawaida na umma utajulishwa kuhusu sababu za vifo vya samaki hao walioteketezwa mara baada ya kupatikana kwa mujibu wa uchunguzi wa kimaabara.
Imetolewa:
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Waziri Mkenda Na Mkakati Wa Kuimarisha Bei Za Mazao Ya Kilimo
Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dar es salaam
Waziri wa Kilimo Mhe Prof Adolf Mkenda ameeleza kuwa serikali inaendelea na mkakati wa kuimarisha bei za mazao ya kilimo.
Ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi ndogo za Wizara ya Kilimo Jijini Dar es salaam ambapo amebainisha kuwa Serikali inapenda kuwaona wakulima wanapata faida kutokana na kilimo, ndiyo maana haijaweka kodi yoyote kwenye mbolea kama wengine wanavyozusha.
Amesema kuwa uzalishaji wa mazao una gharama kubwa japo bei za mazao kuna wakati zinakuwa hazieleweki.
“Bei ya mazao ya mahindi kwa sasa inazua taaruki kwenye baadhi ya mikoa, kwani yanauzwa kwa bei ndogo tofauti na gharama za uzalishaji alizotumia mkulima, hii inamkandamiza anaweza kushindwa kumudu gharama za pembejeo,” Amesema.
Kuhusu suala la mbolea, Waziri Mkenda amesema kuwa suala la mbolea limezua taaruki ambapo baadhi ya watu wamedai kuwa kupanda kwa bei ya pembejeo hiyo inachangiwa na kodi iliyowekwa na serikali.
“Hakuna kodi yoyote iliyowekwa kwenye mbolea kwa kuwa Serikali imelenga katika kuhakikisha inapatikana kwa bei nafuu ili kuwahamasisha wakulima kutumia mbolea ambayo inawasaidia kuvuna mazao mengi,” Amesema Waziri Mkenda na kuongeza kuwa
“Tunaamini hatua hii itasaidia mbolea kuingia kwa wingi nchini hivyo wafanyabishara watakuwa na bei ya ushindani ambayo haimuumizi mkulima, pia tunachoangalia sisi mbolea inayoagizwa iwe na viwango vya ubora unaotakiwa,”
Amesema mfumo wa zabuni haujawasaidia kwa kuwa licha ya kuwa makampuni mengi yalikuwa yanajitokeza yanachakuliwa machache kisha bei inapangwa lakini siyo rafiki kwa wakulima.
“Japo hatuna uwezo wa kushusha bei kwenye soko la dunia lakini tunahitaji kuona wafanyabiashara wanasaidia kuwezesha mbolea kupatikana kwa wingi, Serikali inafanya juhudi kila inavyoweza ikiwamo hata kupunguza gharama za kulipia maghala ya kuhifadhia nafaka,” Amekaririwa Mhe Waziri
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko (CPB) Dkt Anselm Moshi amewaeleza waandishi wa habari kuwa Bodi hiyo inanunua mahindi kwa bei nzuri ukilinganisha na bei iliyopo sokoni.
Dkt Moshi ameeleza kuwa ununuzi wa mahindi ni kati ya shilingi 250 hadi 480 ambapo bei inatofautiana kwenye mikoa husika.
“Wilaya ya Nkasi mahindi yanauzwa 250 hadi 270 kwa kilo moja, kanda ya kaskazini yanauzwa kwa bei ya shilingi 450 hadi 485 kwa kilo, hivyo bodi imeshatuma jumla ya shilingi bilioni 7.47 ya kununua jumla ya tani 14,948 kwa wastani wa shillingi 500 kwa kilo,” Amesema Dkt Moshi
Naye Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Ndg Militon Lupa amesema kuwa wakala unatarajia kununua takribani tani 165,000 za aina tatu za nafaka kwa msimu wa mwaka 2021/2022 kutoka kwenye mikoa yenye uzalishaji mkubwa kati ya hizo mahindi yatanunuliwa tani 150,000.
Lupa amesema kuwa katika kipindi kirefu NFRA imekuwa ikinunua mahindi pekee ambapo hivi sasa imeanza kununua nafaka aina ya mahindi, Mtama na mpunga
MWISHO
Communication Officer at HPSS-Tuimarishe Afya
Job Title: Communication Officer Reporting to : Project Manager Location : Dodoma Level of Engagement :Full time Similar Jobs Summary of the Position The Health Promotion and System Strengthening Project (HPSS-Tuimarishe Afya) is a Swiss-Tanzania Corporation project being executed by the Swiss Tropical and Public Health Institute (SwissTPH) with its headquarter in Dodoma Tanzania. The HPSS project is being implemented since […]
This post Communication Officer at HPSS-Tuimarishe Afya has been posted by Udahiliportaldaily
Get more post by visiting Udahiliportal.com
know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
Accountant at Medical Teams International
ACCOUNTANT Medical Teams International Tanzania Department : Finance Reports to: Direct: Senior Finance Officer Technical: NA […]
This post Accountant at Medical Teams International has been posted by Udahiliportaldaily
Get more post by visiting Udahiliportal.com
know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details