Friday 5 March 2021

WAZIRI AWESO ATAJA KILICHOKUWA KINAKWAMISHA MIRADI YA MAJI NCHINI

 

WAZIRI wa Maji Jumaa Aweso akizungumza leo mjini Lushoto wwakati akifungua kikao kazi cha wadau wa maji Mkoa wa Tanga kilichofanyika wilayani Lushoto kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella kulia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Henry Shekifu


WAZIRI wa Maji Jumaa Aweso akizungumza leo mjini wakati akifungua kikao kazi cha wadau wa maji Mkoa wa Tanga kilichofanyika wilayani Lushoto
MKUU wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella akizungumza wakati wa kikao hicho kulia ni Waziri wa Maji Jumaa Aweso kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Judica Omari
Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Judica Omari akizungumza wakati wa kikao hicho
MENEJA wa Ruwasa Mkoa wa Tanga Mhandisi Upendo Omari akizungumza wakati wa kikao hicho
MKURUGENZI wa Bonde la Pangani Segule Segule akisisitiza jambo wakati wa kikao hicho
MKURUGENZI wa Tanga Uwasa Mhandisi Geofrey Hilly akizungumza jambo wakati wa kikao hicho
Sehemu ya wadau wa kikao hicho wakifuatilia masuala mbalimbali
MKURUGENZI wa Bonde la Maji la Pangani Segule Segule akifuatilia kwa umakini kikao hicho
Wadau wa kikao hicho wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Maji Jumaa Aweso
Wadau wa Kikao hicho wakifuatilia masuala mbalimbali

Waziri wa maji Jumaa Aweso amezitaja sababu zilizokuwa zikikwamisha miradi ya maji kuwa ni kutokana na kuwatumia wakandarasi wababaishaji na wasiokuwa na uwezo. 

Waziri Aweso ametoa, sababu hiyo wakati akifungua kikao kazi cha wadau wa maji Mkoa wa Tanga kilichofanyika wilayani Lushoto. 

Waziri Aweso alisema wakandarasi wasiokuwa na uwezo walikuwa wakipewa zabuni kwa kujuana na hivyo kusababisha kusababisha miradi ya maji kutokamilika na hatua hazichukuliwi. 

Alisema wizara hiyo hivi sasa imeondokana na changamoto  hiyo baada ya kuweka mikakati ya kuhakikisha wakandarasi wa namna hiyo hawapati nafasi. 

"Wataalamu walikuwa wakijua wazi kuwa baadhi ya wakandarasi walikuwa hawana uwezo lakini bado walikuwa wakiwatumia na kuwaacha wale wenye uwezo,"alibainisha waziri Aweso. 

Sababu nyingine iliyokuwa ikikwamisha miradi hiyo ya maji ni michakato isiyokuwa na ulazima ambayo ilikuwa ni kikwazo kikubwa cha ukamilishaji wa miradi mbalimbali nchini. 

Aliwaagiza, watendaji kayika, wizara hiyo kuacha visingizio badala yake watekeleze wajibu ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji safi na salama. 

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigela ameipongeza wizara hiyo ya maji kwa kujitahidi kufikisha maji katika maeneo yaliyokuwa na changamoto kubwa ya maji katika Mkoa Tanga. 

Naye Meneja wa Wakala wa maji na usafi wa mazingira vijijini (Ruwasa)  Mkoa wa Tanga Mhandisi Upendo Lugongo katika kutekeleza, bajeti ya mwaka wa fedha 2021/22 Ruwasa Mkoa Tanga inategemea kutumia jumla ya shilingi 38,437,802,839.39 ingawa mahitaji halisi ni shilingi 41,872,700,424.04 ili kukamilisha ujenzi wa miradi inayoendelea. 

Alisema miradi hiyo ni pamoja na ukarabati wa miradi chakavu,  usanifu na ujenzi wa miradi mipya. 

"Ruwasa Tanga inajumuisha wilaya zake 7 na inategemea kutekeleza ujenzi miradi ya mipya ya maji kukarabati ya zamani kupanua miradi inayoendelea na kusanifu miradi mipya kwa kupitia  bajeti ya mwaka wa fedha 2021/12.

Kikao hicho kilikuwa na lengo la kufanya tathimini pamoja na kuangalia hatua za utekelezaji zilizofikiwa kwenye miradi ya maji.

Share:

AUDIO: Super Woman - Tanzanian Men All Star


AUDIO: Super Woman - Tanzanian Men All Star


Share:

Naibu Waziri Ulega Aitaka TASCA Kubadili Katiba Yao Ili Kunufaika Na Fursa Zilizopo


Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Abdallah Ulega amewaelekeza viongozi wa Umoja wa Vituo na Shule za kuvumbua, kulea na kuendeleza Michezo kwa Watoto na Vijana Tanzania (TASCA) kufanya marekebisho ya Katiba yao ili waweze kutambulika na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania  (TFF) ili kunufaika na fursa zake za kuendeleza programu mbalimbali za wa watoto na vijana.

Akifanya mazungumzo na viongozi hao  Dar es salaam Naibu Waziri Ulega amewashauri viongozi hao kujisajili vitambulike kama Umoja wa Kuvumbua, Kulea na kuendeleza Mpira wa Miguu kwa Watoto na Vijana Tanzania (TAFOCA)  ili waweze kutambulika na TFF na kunufaika na fursa zake.

“Sasa usajili wa TASCA unawatambua kama Umoja wa Vituo na Shule za Kuvumbua, Kulea na kuendeleza Michezo kwa Watoto na Vijana jambo linalowakosesha fursa ya kutambuliwa na TFF,” alisema Naibu Waziri Ulega

Aidha, Naibu Waziri Ulega amewahakikishia viongozi wa TASCA kuwa Serikali imepokea mawazo yao yote ikiwa ni pamoja na mapendekezo ya kuboresha Kanuni za BMT ili kuweka utaratibu wa wachezaji wa timu B za Vijana za vilabu vya Ligi Kuu na wanaofanya vizuri kwenye timu za Taifa za U17 na U20 wapewe nafasi ya kucheza kwenye michuano ya ligi Kuu badala ya kubakia kwenye timu za vijana za vilabu hivyo ili kuwaongezea uzoefu na kuendeleza vipaji vyao kwa manufaa ya Taifa.

Pia Naibu Waziri Ulega amewaahidi viongozi wa TASCA kuwa Serikali italifanyia kazi ombi lao la kushirikiana na Taasisi mbalimbali za Umma kama Vyuo na Shule ili kutumia miundombinu iliyopo katika Taasisi hizo kwa shughuli mbalimbali za kukuza na kuendeleza michezo nchini.


Share:

Dampo La Pugu Kinyamwezi Limeelemewa- Waitara


Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mhe. Mwita Waitara amesema kuwa dampo la pugu ambalo ni dampo kuu kwa Mkoa wa Dar es Salaam limeelemewa hivyo kunahaja ya kila Manispaa ya jiji la Dar es Salaam kuwa na dampo lake na kuacha kutegemea dampo la pugu ili kupunguza kero kwa wananchi walio karibu na dampo hilo.

Ameyasema hayo alipokuwa katika ziara ya ukaguzi wa mazingira katika  jiji la Ilala Mkoa wa Dar es Salaam amesema kuwa dampo hilo limekuwa likilalamikiwa sana na wananchi hasa kipindi cha masika, maji yanatiririka kutoka kwenye taka na kuingia katika makazi ya watu.

“Nimetembelea Manispaa zote za Mkoa wa Dar es Salaam Ubungo, Kinondoni, Kigamboni, Temeke na Nimemalizia hapa jiji la Ilala lakini nimewataka kila Manispaa wahakikishe wanadampo lao ili kuepusha adha kwa wananchi waliopo karibu na Dampo la Pugu. Hii ni njia bora ya kudhibiti kusambaa kwa taka Dar es Salaam” Waitara

Aidha Mhe. Waitara ameeleza kuwa taka zilizopo katika dampo la pugu zina changamoto zake kwani hazijatenganishwa kutoka kwenye chanzo hivyo kupelekea ugumu katika kuzichakata, ni vizuri wananchi wahakikishe wanatenganisha taka kuanzia kwenye chanzo ili kurahisisha zoezi hilo. Ameendelea kusema kuwa taka zikitenganishwa pia zinageuka kuwa fursa ya kujipatia kipato na sio taka tena

“Taka zilizopo hapa zimechanganyika kuna mifuko ya plastiki, vyuma na chupa ambavyo ingekuwa fursa katika kujipatia kipato na zisingekuwa taka tena kwani kunaviwanda vinauhitaji wa taka hizo kwa ajili ya kurejeleza. Hapa tulipofikia inabidi kuweka utaratibu ili eneo hili lianze kuwekwa miundombinu rafiki ili haya maji yasiende kwenye makazi ya watu na kusababisha kuathiri afya zao” Mhe. Waitara

Kwa upande wake Diwani wa kata ya pugu Mhe. Imelda Gerald amesema kuwa dampo kwa sasa ni kero japo meneja wa Dampo anajitahidi sana lakini kwa wananchi bado ni kero mvua inaponyesha maji machafu yanaenda kwa wananchi na kuathiri afya zao wanapata vipele, fangasi hata visima ukichimba maji yanakuwa machafu.

“Dampo la pugu limekuwa kero kwa wakazi lakini tunaomba pia magari yanayobeba taka yawe yamefunikwa ili kuepusha kudondosha taka karibu na makazi ya watu pamoja na magari yenyewe yawe mazuri maana kunamagari yanaletwa ni mabovu ambayo ni taka pia” alisema Bi Imelda

Vile vile Mhe. Waitara ametembelea Jengo jipya la Machinjio vingunguti na Machinjio ya Mazizini Gongolamboto kujionea hali ya kimazingira katika machinjio hayo. Mhe. Waitara amefurahishwa sana kuona jengo la machinjio la kisasa ambalo litakuwa rafiki kwa mazingira. Machinjio hayo bado hayajafunguliwa rasmi.

Mhe. Waitara pia alitembelea Machinjio ya Mazizini Gongolamboto na kubaini uchafuzi mkubwa wa Mazingira kwani machinjio hayo yanatiririsha maji machafu katika mfereji uliopo karibu na machinjio. Mhe. Waitara ameitaka NEMC kuchukua hatua za kisheria kuwajibisha Machinjio hayo mara moja

“Naagiza NEMC kuchukua hatua za kisheria kwa machinjio haya, kutiririsha maji katika mazingira ni kosa la kisheria hivyo wapigwe faini na onyo. Maji haya hayaruhusiwi kupelekwa kwenye mfereji au kwenye chanzo chochote cha maji bila kupimwa na kupewa kibali kutoka katika mamlaka husika” alisema Mhe. Waitara

Naibu Waziri alikuwa katika ziara ya siku tano katika Mkoa wa Dar es Salaam na amefanikiwa kutembelea Manispaa zote na kutoa maagizo katika kila Manispaa.


Share:

Waziri Lukuvi Atangaza Uhakiki Kubaini Wamiliki Wa Ardhi Hewa Nchi Nzima


Na Munir Shemweta, ILEMELA
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi amesema Wizara ya Ardhi kuanzia tarehe 1 Julai 2021 itaanza zoezi la uhakiki la kitaifa kuwatambua na kuwaondoa  wamiliki wote hewa wa viwanja nchini.


Lukuvi alisema hayo kwa nyakati tofauti tarehe 4 Machi 2021 katika ofisi za halmashauri ya Manispaa ya Ilemela alipopokea taarifa ya utekelezaji majukumu ya sekta ya ardhi na eneo la Kigoto katika kata ya Kirumba alipogawa ankara za malipo kufuatia kuhitimishwa kwa mgogoro kati ya wananchi wa eneo hilo na jeshi la polisi akiwa kwenye  ziara ya kikazi katika mkoa wa Mwanza.


“Lazima tufanye uhakiki wa wamiliki wote wa ardhi ili kuwatambua na kuondoa wamiliki hewa, katika miji kuna maeneo mengi hayajengeki kwa sababu wamemilikishwa watu ambao hawapo” alisema Lukuvi.


Alisema, katika zoezi hilo halmashauri za wilaya zitatakiwa kuandaa jedwari la kumbukumbu za wamiliki ili zoezi hilo litakapoanza taarifa mpya zitakazojumuisha kumbukumbu zilizopo Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), namba za simu pamoja na taarifa za kibenki ziingizwe.


Lukuvi alisema, wapo wananchi waliojenga katika maeneo mbalimbali majina yanatofautina na wengine  majina ya kubuni lakini  hawapo tanzania na kusisitiza kuwa ikibainika viwanja vyao vitapigwa mnada na aliwaonya  watumishi wa sekta ya ardhi kutoharibu nyaraka kutokana na kuhusika kwao kwa namna moja ama nyingine katika umilikishaji.


Kwa mujibu wa Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi zoezi la kutambua wamiliki wa ardhi hewa halina lengo la kunyanganya viwanja bali ni kujua wamiliki halali na kusisitiza kuwa watendaji wa sekta ya ardhi lazima wafanye zoezi hilo kwa umakini na uaminifu mkubwa.


” Najua baada ya kutangaza zoezi hili la uhakiki baadhi ya Maafisa ardhi wataanza kuhangaika kuuza viwanja na wengine kunyofoa nyaraka, tumieni njia sahihi maana kila mtu ana haki ya kumiliki kiwanja zaidi ya kimoja cha msingi ni kufuata sheria.


Katika hatua nyingine Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi aliwapatia ankara za malipo ya ardhi wananchi 600 wa eneo la Kigoto kata ya Kirumba katika halmashauri ya Manispaa ya Ilemela lililokuwa na mgogoro wa muda mrefu kati ya wananchi wa eneo hilo na jeshi la Polisi.


” Ninyi wananchi wa Kigoto wamepatiwa eneo hili na Mhe. Rais John Pombe Magufuli bila kutozwa gharama za thamani ya ardhi na ndiyo ninyi pekee katika mkoa wa Mwanza mliopata eneo kwa gharama nafuu, mmuombee  Rais Magufuli kwa kuwapatia eneo” alisema Lukuvi.


Vile vile, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi alitangaza kuanza awamu ya pili ya mpango wa Funguka kwa Waziri utakaowezesha wananchi wenye migogoro ya ardhi  kujaza fomu maalum na kuiwasilisha ofisi za ardhi za mikoa kwa ajili ya kutafutiwa ufumbuzi na Waziri.


Kwa upande wake Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula ambaye ni Mbunge wa jimbo la Ilemela aliwahakikishia wananchi wa Ilemela kuwa serikali itahakikisha inamaliza migogoro yote ya ardhi katika mkoa wa Mwanza kama ilivyoshughulikiwa mgogoro wa Kigoto katika kata ya Kirumba mkoa wa Mwanza.


Kamishna wa Ardhi Msaidizi mkoa wa Mwanza Eliah Kamyanda alisema mgogoro wa eneo hilo ulidumu kwa takriban miaka 30 mpaka mhe Rais aliporidhia wananchi hao kurejeshewa eneo hilo.


Alisema, mgogoro huo ulipitia hatua mbalimbali na kwa sasa kazi ya upimaji eneo hilo limekamilika na wananchi wapatao 600 wamepatiwa ankara za malipo ya kumilikishwa.



Share:

Tathmini Yafichua Hasara Ya Sh.bilioni 1.6 Upanuzi Hospitali Ya Tumbi


Na.Catherine Sungura,Kibaha
Uchunguzi wa tathmini ya uwepo wa thamani ya fedha katika utekelezaji wa mradi wa upanuzi na uboreshaji wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani-Tumbi umeonesha hasara ya shilingi bilioni 1.6.


Hayo yamebainishwa jana  na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Dkt.Dorothy Gwajima wakati akipokea tathmini ya awali ya mradi huo baada ya maagizo yake aliyoyatoa mnamo tarehe 24 Disemba,2020 alipotembelea hospitali hiyo na kutoridhishwa na ujenzi huo.


Katika ziara yake hiyo Dkt.Gwajima alitoa maelekezo kwa Katibu Tawala Mkoa wa kufanya tathmini ya uwepo wa thamani ya fedha  katika utekelezaji wa mradi wa upanuzi na uboreshaji wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa Tumbi na hasara hiyo imebainika kwa kuhakikiwa kwa baadhi ya vipimo vya kazi na kuchukua sampuli chache kwa ajili ya vipimo vya kimaabara  jambo lililoashiria kuwepo kwa hasara kubwa zaidi Kama ingefanyika tathmini ya kina.


“Ripoti nimeipokea na iko dhahiri kabisa mahitaji ya upanuzi na uboreshaji wa hospitali ya Tumbi yalikadiriwa kutekekezwa kwa shilingi bilioni 29 baada ya Serikali kuonyesha nia ya kusaidia ufadhiri wa mradi huo kufuatia mpango wa awali wa uongozi wa Mkoa wa mwaka 2007-2009 iliokuwa na makadirio ya shilingi bilioni 5”. Alisema Dkt.Gwajima.


Aliongeza kuwa mpaka sasa jumla ya shilingi bilioni 9.4 zimekwishatolewa kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo Kati ya shilingi bilioni 29 zilizokadiriwa ambapo bilioni 5.5 imetumika katika utekelezaji chini ya usimamizi wa Shirika la Elimu Kibaha na Katibu Tawala Mkoa na bilioni 3.9 zimehamishiwa Wizara ya Afya.


Hata hivyo Dkt. Gwajima amesema kupitia taarifa hiyo imebaini kuwepo kwa mikataba ya Wakandarasi wawili SUMA JKT na MUST Construction Bureau kinyume na Sheria namba 7 ya manunuzi ya Umma ya mwaka 2011 pamoja na marekebisho yake mwaka 2016.


“Kutokana na mkanganyiko huo namuelekeza Katibu Tawala Mkoa kupitia Kamati yako ya tathimini mfanye tathimini ya kina ndani ya siku thelathini  na kuniainishia  hasara halisi kwa kurejea vipimo vya jengo zima, kutathimini na kushauri kama jengo hili linafaa kwa matumizi ya Umma pamoja na Hali ya majengo ya zamani Kama yanafaa kukarabatiwa na kutumika Tena kwa gharama stahiki”Alisisitiza Dkt.Gwajima.


Licha ya hayo Waziri huyo aliitaka Kamati hiyo pia ihakiki uhalali wa uhitaji wa shilingi bilioni 29 katika mpango wa upanuzi kwa kurejea michoro ya mpango, kuainisha sababu zilizopelekea wizara kurudia ununuzi wa mkandarasi wa awamu ya pili A na ukidhi wa kisheria katika mchakato  huo wa kumnunua mkandarasi mpya na kuagiza mradi huo usitishwe na madeni yasiendelee kulipwa mpaka atakapopokea tathimini ya kina na kuelekeza vinginevyo.



Share:

Vijana Waaswa Kuchangamkia Fursa Ya Mikopo Yenye Riba Nafuu Inayotolewa Na Halmashauri Pamoja Na Mfuko Wa Maendeleo Ya Vijana


Vijana nchini wamehimizwa kuchangamkia fursa ya mikopo yenye riba nafuu inayotolewa na Serikali kupitia makusanyo ya mapato ya ndani ya Halmashauri pamoja na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana ambao unaratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu ili waweze kujikwamua kiuchumi na kujiletea maendeleo.

Akizungumza wakati wa ziara ya kikazi ya Mkoani Geita alipotembelea vikundi vya vijana ambavyo vimenufaika na mikopo yenye riba nafuu inayotolewa na Halmashauri mbalimbali nchini pamoja na Mfuko wa Maendeleo ya vijana, Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Kazi, Vijana na Ajira Mhe. Patrobas Katambi alitumia fursa hiyo kuwaasa vijana kuchangamkia mikopo hiyo yenye riba nafuu ili waweze kuanzisha miradi ya uzalishajimali kwenye jamii zinazowazunguka.

Alieleza kuwa, Serikali kupitia halmashauri zilizopo nchini zimekuwa na wajibu wa kutenga fedha asilimia 10 kupitia makusanyo ya mapato ya ndani kwa ajili ya kuwezesha vikundi vya Vijana, Wanawake na Watu wenye Ulemavu ili viweze kuanzisha miradi mipya au kuendeleza shughuli zao ambazo zitatoa fursa ya kuzalisha ajira zaidi na kuwasaidia kujiingizia kipato na hivyo kuchangia katika kuendeleza gurudumu la maendeleo.

“Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli imeendelea na azma yake ya kuwawezesha vijana kwa kutoa fursa nyingi kwa vijana ikiwemo mikopo yenye riba nafuu lakini vijana wamekuwa hawatumii fursa hizo zinazotolewa na serikali kwa kuanzisha miradi mikubwa itakayowawezesha kujiajiri na kuajiri vijana wenzao,” alisema Katambi

Alisema lengo la Serikali kutoa mikopo hiyo ni pamoja na kutatua changamoto ya ukosefu wa ajira, hivyo kupita mikopo hiyo ambayo ina riba nafuu makundi ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu wataweza kunufaika kwa kuanzisha miradi mbalimbali ambayo itawaingizia kipato na hatimaye kuweza kujikwamua kiuchumi.

Aliongeza kuwa, wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akifungua rasmi Bunge la 12 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jijini Dodoma Novemba 13, 2020 alieleza kuwa Serikali imeongeza jitihada za kuwawezesha wananchi kiuchumi kwa kuwapatia mikopo isiyo na riba ama yenye riba nafuu ikiwemo mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Halmashauri na pia kupitia mifuko na Programu mbalimbali zilizoanzishwa na serikali.

Sambamba na hayo alielezea pia juu ya uwezekano wa kuiunganisha baadhi ya mifuko ili ifanye kazi kwa tija zaidi kwa kuimarisha usimamizi wa mifuko hiyo na kuhakikisha watanzania wanaifahamu.

Naibu Waziri Katambi, alitaka wakurugenzi wa halmashauri zote nchini kuangalia namna bora ya kuanzisha mpango wa kutoa mafunzo ya ujasiriamali na usimamizi wa biashara ili kabla ya kuwapatia mkopo vijana waweze kuwajengea ujuzi utakaowasaidia kuimarisha biashara zao na kuzisimamia kwa weledi pamoja na kuwa na mbinu za kukuza biashara zao. Pia alihamaisha halmashauri kuona namna ya kuwawezesha vijana kwenye mikopo wanayoomba asilimia 50 ikawa kwa ajili ya vifaa au vitendea kazi na asilimia 50 nyingine kwa ajili ya uendeshaji wa shughuli ya biashara zao watakazokuwa wakifanya.

“Kumekuwa na changamoto kwa baadhi ya vijana kukosa uaminifu, wanakuja kama kikundi kukopa fedha hizo mara baada ya kuzipata wanaanza kuzitumia kwenye malengo au mipango ambayo hawakuikusudia na hivyo kushindwa kurejesha mikopo hiyo, hivyo kama kupitia mikopo waliyoomba asilimia 50 wakanunuliwa vitendea kazi au vifaa wakishindwa kuendeleza biashara itakuwa ni rahisi kwa halmashauri kuwapatia vijana wengine vifaa hivyo ambao wanaona wanaweza kufanya kazi,” alisema Naibu Waziri

Pamoja na hayo Naibu Waziri, Katambi alipongeza vikundi vya vijana alivyovitembelea ikiwemo kikundi kinachojishughulisha na uzalishaji wa Chaki kinachojulikana na jina la Rubondo na kikundi cha vijana cha Geita Youth Group kinachofatua matofali kwa hatua waliyofikia ambayo imechangia kasi ya ukuaji wa viwanda vidogo vidogo mkoani geita na ambavyo vitasaidia kutengeneza ajira na kuongeza ukuaji wa uchumi.

Aidha, Naibu Waziri Katambi amewataka vijana kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kujituma sambamba na kutumia maarifa waliyonayo kubuni miradi mbalimbali ya uzalishajimali ili waweze kujikwamua kiuchumi.

Kwa Upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Fahil Juma alieleza kuwa Halmashauri hiyo itaendelea kutoa mikopo na elimu kwa vikundi mbalimbali vya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu ili waweze kukuza pato lao na kuongeza ajira kwa wengine zaidi.

Naye, Mnufaika wa kikundi cha Geita Youth Group, Bi. Jenifer Isaya ameishukuru Serikali pamoja na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuwaamini vijana kuwa wananweza na kuamua kuwatengea mikopo hiyo yenye riba nafuu sambamba na kuwawezesha vifaa na fedha, hivyo waliahidi kuchapa kazi kwa bidi kama azma ya serikali ili warejeshe mikopo hiyo kwa wakati na kuwafanya wananchi wengine waweze kunufaika.

Mara baada ya ziara hiyo ya kutembelea vikundi vya vijana vilivyonufaika na mkopo wa asilimia nne (4) inayotolewa na Halmashauri zilizopo nchini. Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Kazi, Vijana na Ajira Mhe. Patrobas Katambi alitembelea Mgodi wa Geita Gold Mine (GGM) ikiwa ni sehemu ya ufuatiliaji wa utekelezaji wa Sheria za Kazi pamoja na kusikiliza kero na malalamiko ya wafanyakazi kwenye maeneo mbalimbali ya kazi.


Share:

Wimbo Mpya : NTEMI O MABALA 'NG'WANA KANG'WA' - ACHA TUDANGE


Msanii wa Nyimbo za Asili maarufu Ntemi O Mabala 'Ng'wana Kang'wa' kutoka Kahama Mkoani Shinyanga ameachia wimbo mpya unaitwa 'Acha Tudange'. Sikiliza Ngoma hii hapa chini
Share:

MWALIMU ALIYEMKATA PANGA MWALIMU MWENZAKE MZOZO WA PENZI LA MWANAFUNZI WA FIELD AFIKISHWA MAHAKAMANI



Mwalimu wa Shule ya Upili ya Wasichana ya Karoti katika Kaunti Ndogo ya Mwea Mashariki nchini Kenya Timothy Musembi (34) ambaye alimshambulia na kumjeruhi mwenzake aitwaye Alphonce Orina (26) wakizozania penzi ameshtakiwa kwa jaribio la mauaji.

Inasemekana Orina alikuwa ofisini wakati mwenzake aliingia akiwa amejihami kwa panga na kuanza kumshambulia akimzomea kwa kumnyemelea mwalimu wa kike ambaye yuko kwenye mazoezi ya kufundisha shuleni hapo. 

Alimkata mara mbili kichwani na kumlaazimu Orina kujitetea kwa vita naye.

 Timothy Musembi, 34, alifikishwa Alhamisi, Machi 4,2021 mahakamani huko Wang'uru chini ya ulinzi mkali ambapo alitakiwa kujibu kosa la jinai.

Alidaiwa kuwa mnamo Machi 2,2021 katika Shule ya Upili ya Wasichana ya Karoti katika Kaunti Ndogo ya Mwea Mashariki, alijaribu kumuua Alphonce Orina, 26, kwa kumkatakata kichwani na mikononi. 

Mahakama iliarifiwa kuwa wakati wa shambulio lililotokea afisini, mwathirwa alipata majeraha mabaya na ilibidi alazwe hospitalini kwa matibabu maalum. 

Alipofika mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Monica Kivuti, Bw Musembi alikanusha shtaka hilo na kuomba aachiliwe kwa dhamana.

Alisema kuwa mashtaka anayokabiliwa nayo yana dhamana na aliomba aachiliwe ili aweze kuhudhuria vikao vya mahakama akitoka nyumbani.

Hakimu Musembi aliamuru aachiliwe kwa dhamana ya KSh100,000 hadi Machi 17 kesi hiyo itakapotajwa. 

Hata hivyo, mshtakiwa alitupwa kizuizini kwani alishindwa kulipa hela hizo.

Inasemekana Orina alikuwa ofisini wakati mwenzake aliingia akiwa amejihami kwa panga na kuanza kumshambulia akimzomea kwa kumnyemelea mwalimu wa kike ambaye yuko kwenye mazoezi ya kufundisha shuleni humo. 

Mhasiriwa alijeruhiwa vibaya mikononi wakati alipkuwa akijaribu kujizuia dhidi ya makali ya panga ya mwenzake.

 Katika patashika hiyo, mwathiriwa alizidiwa na kuanguka chini ambapo walimu wengine walilazimika kuingilia kati na kumkimbiza hospititalini kwani alipoteza fahamu.

 Kisa hicho kiliwaacha walimu na wanafunzi wakiwa na hofu.

 Baadaye mshukiwa alijisalimisha katika Kituo cha Polisi cha Wang'uru ambapo alizuiliwa kabla ya kufikishwa mahakamani Alhamisi.
 
Via Tuko News

Share:

Technical Lead, Maternal, Neonatal and Child Health at Americares

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

TITLE: Technical Lead- Reproductive Maternal Neonatal and Child Health (TL-MNH), Community Partnerships for Respectful Care (CPRC) Project DEPARTMENT:  International Partnerships & Programs REPORTS TO: Tanzania Project Director, Community Partnerships for Respectful Care (CPRC) project ASSIGNMENT TYPE: Full-time LOCATION:  Mwanza, Tanzania LENGTH: 24-months with possibility to extend based on performance and budget ABOUT AMERICARES:  Americares is a health-focused relief and […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Senior Officer HR & Administration at Tata International Company Ltd

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Senior Officer HR & Administration Location: Dar es Salaam, Tanzania Job Purpose:- The position holder will be responsible for deputizing the HR and Administration Manager in managing the Business Unit. He/She shall ensure compliances with company policies, procedures like reporting requirement of the organization. The position shall support handling the day-to-day administrative operations with internal […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Risk Compliance Officer at AccessBank Tanzania (ABT)

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Risk Compliance Officer   OVERVIEW AccessBank Tanzania (ABT) is a commercial bank with a special focus on microfinance and SME.With very strong international shareholders such as Access Holding, International Finance Corporation (World Bank), KfW, African Development Bank and Micro Vest. ABT’s vision is to be committed to the development of financial systems that support social […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo March 5



Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA MACHI 5,2021



















 
Share:

Thursday 4 March 2021

Waziri Mkuu Aridishwa Na Kazi Kubwa Iliyofanywa Na Wizara Ya Kilimo Kuwadibiti Nzige mikoa ya Manyara, Kilimanjaro na Arusha


 Serikali imeridhishwa na kazi inayoendelea kufanywa na viongozi wa wizara ya kilimo na wataalam wake kuhakikisha makundi ya nzige yaliyovamia mikoa ya Manyara, Kilimanjaro na Arusha yanavyodhibitiwa kwa kuuwawa.


Kauli hiyo ya serikali imetolewa leo (04.03.2021) wilayani Monduli mkoa wa Arusha wakati Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alipotembelea kijiji cha Engaruka kukagua zoezi la kunyunyuzia viuatilifu kuua makundi ya nzige na kuwa amefurahi kuona kazi hiyo imefanyika kwa mafanikio chini ya uongozi wa Waziri wa Kilimo Profesa Adolf Mkenda.


Waziri Mkuu aliyeambatana na Wakuu wa Mikoa wa Arusha, Manyara na Kilimanjaro alisema serikali inatambua na kuthamini kazi kubwa iliyofanywa na wataalam wa wizara ya Kilimo pamoja na wale wa halmashauri za Mwanga, Siha, Longido, Simanjiro na Monduli kuwadhibiti makundi ya nzige licha ya ugumu wa mazingira ya porini.


“Nimeridhika na kazi iliyofanyika hadi sasa kuwadhibiti nzige waliovamia maeneo ya mikoa yetu ya Manyara, Kilimanjaro na hapa Arusha. Wizara ya Kilimo imechukua hatua madhubuti, endeleeni kuhakikisha wadudu hawa hawasambai kwenye mikoa ya jirani “ alisisitiza Waziri Mkuu Majaliwa.


Katika hatua nyingine Waziri Mkuu ameagiza wizara ya Kilimo kutenga fedha katika bajeti ya mwaka 2021/22 kwa ajili ya kufufua Kitengo Cha Kilimo Anga ili kitumike kwa ajili ya kudhibiti wadudu waharibifu wakiwemo nzige kwa kuwa na vifaa na wataalam wa kutosha.


Alibainisha kuwa kwa kuwa sasa ni msimu wa kilimo, hakuna budi kwa maafisa kilimo kwenye mikoa yote nchini wakawa na utaratibu wa kufuatilia kwa karibu uwepo wa viashiria vya nzige ili kuijulisha wizara kwenda kudhibiti mapema kabla hawajasambaa kwenye maeneo ya mashamba na kuzaliana.


“Hatuwezi kuwapa nafasi nzige wazaliane hapa nchini kwani watapoteza malisho yetu na mazao ya chakula pia biashara .Nzige kwetu ni adui hatari hatupaswi kuwapa nafasi hata dakika moja, hawa tuliwasikia kwa ndugu zetu Kenya na tulitoa ushirikiano kuwaangamiza lakini wamefika nchini lazima tuwaangamize wote” aliagiza Waziri Mkuu.


Akitoa taarifa ya kazi ya kudhibiti nzige Waziri wa Kilimo Profesa Adolf Mkenda alimweleza Waziri Mkuu kuwa kundi la kwanza la nzige liliingia nchini mwezi Januari wilayani Mwanga na mwezi Februari kundi jingine liliingia wilaya ya Longido na kusambaa kwenye wilaya za Simanjiro, Siha na Monduli.


Prof Mkenda alisema tayari wizara kwa kushirikiana na mikoa hiyo iliyokumbwa imefanikiwa kuangamiza makundi ya nzige kwenye wilaya ya Mwanga na Siha.


“Longido tuliangamiza makundi ya nzige lakini kundi dogo likakimbilia Monduli hapa Engaruka na kazi ya kuangamiza imeanza tunakwenda vizuri, tuna hakika tutawamaliza wote kwani tunavyo vifaa kama mabomba ya kuliza kwa mikono, helkopta na ndege maalum zinafanya kazi “ alisema Prof. Mkenda.


Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Arusha Idd Kimanta alipongeza kazi inayofanywa na wizara ya kilimo kwa kuja eneo la tukio mapema ambapo Waziri na Naibu wake muda wote wamekuwa vijijini kushirikiana na wananchi kudhibiti makundi ya nzige.


Naibu Waziri wa Kilimo Hussein Bashe alimweleza Waziri Mkuu kuwa vijiji vya Nondoto, Irelendeni na Engaruka wilaya ya Monduli ndipo makundi ya nzige yalipo kwa sasa na kuwa operesheni ya kuangamiza imefanyika jana na leo ha kuwa hali inaendea vema nzige wengi wamekufa.


Akihitimisha hotuba yake Waziri Mkuu aliwasihi wananchi kote ambako nzige wameonekana kutokuokota nzige waliokufa kwani wameuwawa kwa sumu inayoweza kuleta madhara kwa binadau endapo akila nzige hao.


Waziri Mkuu Majaliwa amehitimisha ziara yake ya siku moja wilayani Monduli kwa kuongea na wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kijiji cha Engaruka ambapo amesema serikali ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli itakamilisha ujenzi wa barabara ya lami toka Mto wa Mbu hadi Engaruka Monduli .
Mwisho
Imeandaliwa na;
Kitengo cha Mawasilino Serikalini
Wizara ya Kilimo
MONDULI
04.03.2021




Share:

Waziri Jafo azindua Magari Matatu Yatakayotoa Huduma Ya Tohara Katika Mikoa Minne Kanda Yaziwa


Na Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
WAZIRI wa Nchi ofisi ya Rais TAMISEMI amezindua magari matatu yatakayotoa huduma ya Tohara katika mikoa minne  ya kanda ya ziwa  ikiwemo Shinyanga,Mwanza,Simiyu na Mara ambapo amesema kuwa mwanaume akipata tohara hawezi kupata maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa asililimia 60.

Hayo yamebainishwa leo jijini Dodoma na Waziri huyo wakati wa hafla ya uzinduzi wa magari matatu yenye thamani ya billioni 1.2 yaliyotolewa na Taasisi ya Intra Health International na kusema kuwa wale waliopata tohara wana asilimia kubwa ya kujizuia kwa kutopata maambukizi ya UKIMWI kwa asilimia 60.

Aidha waziri Jafo amewataka waganga wakuu wa mikoa ya kanda ya ziwa washirikiane kwa dhati katika kuhakikisha huduma ya tohara inawafikia wanaume wakubwa na wadogo huku akiwataka kuyatunza magari hayo.

Kwa upande wake mkurugenzi wa idara ya afya ustawi wa jamii na lishe kutoka TAMISEMI Ntuli Kapologwe amesema kuwa huduma ya utoaji tohara ni moja ya afua muhimu sana katika mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya ukimwi Nchini .

Naye mkurugenzi mkazi wa shirika la intra health international dr lucy Raymond amesema kuwa shirika limekuwa likitoa huduma ya tohara kwa wanaume wakubwa na wadogo kwa lengo la kuondoa maambukizi ya ukimwi na magonjwa mbalimbali huku akibainisha  wafanyakazi wa kutoa huduma  zaidi ya elfu moja wamepatiwa elimu ya kutoa huduma bora katika mikoa hiyo.

Sambamba na hayo Nuru mpuya mwakilishi wa mganga mkuu wa mkoa wa shinyanga amesema kuwa wamekuwa wakitoa huduma ya tohara huku akibainisha asilimia kubwa ya wanaume hawajapata tohara tofauti na mikoa mingine ya pwani na kusema huduma ya tohara itawasaidia wanaume wakubwa na wadogo katika mikoa ya kanda yaziwa ili kuondokana na magonjwa mbalimbali.

 KAULI MBIU ya kampeni hiyo  ni Tohara ya mwanaume “maisha ni sasa,wahi tohara,kuwa msafi,pata kinga.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger