Thursday 4 March 2021

Waziri Mkuu Aridishwa Na Kazi Kubwa Iliyofanywa Na Wizara Ya Kilimo Kuwadibiti Nzige mikoa ya Manyara, Kilimanjaro na Arusha


 Serikali imeridhishwa na kazi inayoendelea kufanywa na viongozi wa wizara ya kilimo na wataalam wake kuhakikisha makundi ya nzige yaliyovamia mikoa ya Manyara, Kilimanjaro na Arusha yanavyodhibitiwa kwa kuuwawa.


Kauli hiyo ya serikali imetolewa leo (04.03.2021) wilayani Monduli mkoa wa Arusha wakati Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alipotembelea kijiji cha Engaruka kukagua zoezi la kunyunyuzia viuatilifu kuua makundi ya nzige na kuwa amefurahi kuona kazi hiyo imefanyika kwa mafanikio chini ya uongozi wa Waziri wa Kilimo Profesa Adolf Mkenda.


Waziri Mkuu aliyeambatana na Wakuu wa Mikoa wa Arusha, Manyara na Kilimanjaro alisema serikali inatambua na kuthamini kazi kubwa iliyofanywa na wataalam wa wizara ya Kilimo pamoja na wale wa halmashauri za Mwanga, Siha, Longido, Simanjiro na Monduli kuwadhibiti makundi ya nzige licha ya ugumu wa mazingira ya porini.


“Nimeridhika na kazi iliyofanyika hadi sasa kuwadhibiti nzige waliovamia maeneo ya mikoa yetu ya Manyara, Kilimanjaro na hapa Arusha. Wizara ya Kilimo imechukua hatua madhubuti, endeleeni kuhakikisha wadudu hawa hawasambai kwenye mikoa ya jirani “ alisisitiza Waziri Mkuu Majaliwa.


Katika hatua nyingine Waziri Mkuu ameagiza wizara ya Kilimo kutenga fedha katika bajeti ya mwaka 2021/22 kwa ajili ya kufufua Kitengo Cha Kilimo Anga ili kitumike kwa ajili ya kudhibiti wadudu waharibifu wakiwemo nzige kwa kuwa na vifaa na wataalam wa kutosha.


Alibainisha kuwa kwa kuwa sasa ni msimu wa kilimo, hakuna budi kwa maafisa kilimo kwenye mikoa yote nchini wakawa na utaratibu wa kufuatilia kwa karibu uwepo wa viashiria vya nzige ili kuijulisha wizara kwenda kudhibiti mapema kabla hawajasambaa kwenye maeneo ya mashamba na kuzaliana.


“Hatuwezi kuwapa nafasi nzige wazaliane hapa nchini kwani watapoteza malisho yetu na mazao ya chakula pia biashara .Nzige kwetu ni adui hatari hatupaswi kuwapa nafasi hata dakika moja, hawa tuliwasikia kwa ndugu zetu Kenya na tulitoa ushirikiano kuwaangamiza lakini wamefika nchini lazima tuwaangamize wote” aliagiza Waziri Mkuu.


Akitoa taarifa ya kazi ya kudhibiti nzige Waziri wa Kilimo Profesa Adolf Mkenda alimweleza Waziri Mkuu kuwa kundi la kwanza la nzige liliingia nchini mwezi Januari wilayani Mwanga na mwezi Februari kundi jingine liliingia wilaya ya Longido na kusambaa kwenye wilaya za Simanjiro, Siha na Monduli.


Prof Mkenda alisema tayari wizara kwa kushirikiana na mikoa hiyo iliyokumbwa imefanikiwa kuangamiza makundi ya nzige kwenye wilaya ya Mwanga na Siha.


“Longido tuliangamiza makundi ya nzige lakini kundi dogo likakimbilia Monduli hapa Engaruka na kazi ya kuangamiza imeanza tunakwenda vizuri, tuna hakika tutawamaliza wote kwani tunavyo vifaa kama mabomba ya kuliza kwa mikono, helkopta na ndege maalum zinafanya kazi “ alisema Prof. Mkenda.


Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Arusha Idd Kimanta alipongeza kazi inayofanywa na wizara ya kilimo kwa kuja eneo la tukio mapema ambapo Waziri na Naibu wake muda wote wamekuwa vijijini kushirikiana na wananchi kudhibiti makundi ya nzige.


Naibu Waziri wa Kilimo Hussein Bashe alimweleza Waziri Mkuu kuwa vijiji vya Nondoto, Irelendeni na Engaruka wilaya ya Monduli ndipo makundi ya nzige yalipo kwa sasa na kuwa operesheni ya kuangamiza imefanyika jana na leo ha kuwa hali inaendea vema nzige wengi wamekufa.


Akihitimisha hotuba yake Waziri Mkuu aliwasihi wananchi kote ambako nzige wameonekana kutokuokota nzige waliokufa kwani wameuwawa kwa sumu inayoweza kuleta madhara kwa binadau endapo akila nzige hao.


Waziri Mkuu Majaliwa amehitimisha ziara yake ya siku moja wilayani Monduli kwa kuongea na wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kijiji cha Engaruka ambapo amesema serikali ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli itakamilisha ujenzi wa barabara ya lami toka Mto wa Mbu hadi Engaruka Monduli .
Mwisho
Imeandaliwa na;
Kitengo cha Mawasilino Serikalini
Wizara ya Kilimo
MONDULI
04.03.2021




Share:

Waziri Jafo azindua Magari Matatu Yatakayotoa Huduma Ya Tohara Katika Mikoa Minne Kanda Yaziwa


Na Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
WAZIRI wa Nchi ofisi ya Rais TAMISEMI amezindua magari matatu yatakayotoa huduma ya Tohara katika mikoa minne  ya kanda ya ziwa  ikiwemo Shinyanga,Mwanza,Simiyu na Mara ambapo amesema kuwa mwanaume akipata tohara hawezi kupata maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa asililimia 60.

Hayo yamebainishwa leo jijini Dodoma na Waziri huyo wakati wa hafla ya uzinduzi wa magari matatu yenye thamani ya billioni 1.2 yaliyotolewa na Taasisi ya Intra Health International na kusema kuwa wale waliopata tohara wana asilimia kubwa ya kujizuia kwa kutopata maambukizi ya UKIMWI kwa asilimia 60.

Aidha waziri Jafo amewataka waganga wakuu wa mikoa ya kanda ya ziwa washirikiane kwa dhati katika kuhakikisha huduma ya tohara inawafikia wanaume wakubwa na wadogo huku akiwataka kuyatunza magari hayo.

Kwa upande wake mkurugenzi wa idara ya afya ustawi wa jamii na lishe kutoka TAMISEMI Ntuli Kapologwe amesema kuwa huduma ya utoaji tohara ni moja ya afua muhimu sana katika mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya ukimwi Nchini .

Naye mkurugenzi mkazi wa shirika la intra health international dr lucy Raymond amesema kuwa shirika limekuwa likitoa huduma ya tohara kwa wanaume wakubwa na wadogo kwa lengo la kuondoa maambukizi ya ukimwi na magonjwa mbalimbali huku akibainisha  wafanyakazi wa kutoa huduma  zaidi ya elfu moja wamepatiwa elimu ya kutoa huduma bora katika mikoa hiyo.

Sambamba na hayo Nuru mpuya mwakilishi wa mganga mkuu wa mkoa wa shinyanga amesema kuwa wamekuwa wakitoa huduma ya tohara huku akibainisha asilimia kubwa ya wanaume hawajapata tohara tofauti na mikoa mingine ya pwani na kusema huduma ya tohara itawasaidia wanaume wakubwa na wadogo katika mikoa ya kanda yaziwa ili kuondokana na magonjwa mbalimbali.

 KAULI MBIU ya kampeni hiyo  ni Tohara ya mwanaume “maisha ni sasa,wahi tohara,kuwa msafi,pata kinga.


Share:

SUPER – NHESHA: Dawa Bora Ya Kutibu Tatizo La Kisukari


SUPER – NHESHA
Ni dawa ya kutibu tatizo la sukari au jina la kitaalamu (Diabetes Mellitus) ni kundi la magonjwa yanayohusiana na ufanyaji kazi wa mwili ambapo Mtu anakuwa na kiwango kikubwa cha sukari aina ya Glucose katika mwili kutokana na mwili wake kukosa uwezo wa kutengeneza Insulin ya kutosha au seli za mwili wake kutumia insulin iliyopo au pengine mwili kuwa na matatizo yote kwa pamoja na kupelekea mgonjwa wa sukari kupata haja ndogo mara kwa mara (Polyuria) uhisi kiu kila wakati (Polydipsia) Na (Polyphagia).


AINA YA KISUKARI
Kuna aina chache tofauti za ugonjwa wa kisukari (1) ni ugonjwa wa Auto hii aina mgonjwa wa Auto hushambulia mfumo wa kinga na kuharibu seli katika kongosho ambako insulin huzalishwa asilimia 10% ya watu wenye ungonjwa wa kisukari wanayo aina hii (Auto).


AINA YA PILI
Hii hutokea wakati mwili wako unakuwa sugu kwa insulin na sukari hujenga katika damu yako hii husababishwa na kuwa na sukari nyingi kwenye damu yako kuliko kawaida.


CHANZO CHA UGONJWA SUKARI
Viko vyanzo vingi mbalimbali vya sukari
1.     Shinikizo la damu (B.P)
2.     Viwango vya juu vya triglyceride (mafuta)
3.     Lishe yenye mafuta mengi na wanga
4.     Utumiaji mkubwa wa pombe kupita kiasi
5.     Ulaji wa vyakula vyenye sukari nyingi
6.     Mtindo wa maisha usiofaa kiafya
7.     Uzito na unene uliozidi
8.     Kutofanya mazoezi
9.     Umri
10.     Kurith


UNAJUAJE KUWA UNADALILI ZA KISUKARI
1.     Kusikia njaa mara kwa mara
2.     Kusikia kiu mara kwa mara
3.     Kupungua uzito
4.     Maono machafu
5.     Uchovu mara kwa mara
6.     Ukipata kidonda hakiponi
7.     Kushuka kwa kinga mwili


DALILI ZA KISUKARI KWA MWANAUME
Mbali na dalili za jumla za ugonjwa wa sukari wanaume wenye tatizo hilo wanakuwa na upungufu wa nguvu za kiume na kushindwa kufanya tendo la ndoa uume hushindwa kusimama misuri hulegea na kusinyaa, maumivu ya mgongo, kiuno, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kupata choo  kama cha mbuzi


DALILI ZA WANAWAKE
Wanawake wenye ugonjwa wa sukari wanaweza pia kuwa na dalili kama vile maambukizi kwa njia ya mkojo (U.T.I) maambukizi  ya gonzi kukakamaa


TIBA YA MAGONJWA YA SUKARI
Ugonjwa wa sukari unatibika bila kujali ni mda gani umepata hilo tatizo wengi wamekata tama na kuwa wabishi amini tatizo hili linatibika vizuri sana wengi wemepona.


Tumia dawa ya SUPER-NHESHAambayo ni dawa ya miti shamba yaani (asilia) ambayo humfanya mtu kupona na kuimalika kabisa.


Tutakuelekeza pia mfumo wa mtindo wa maisha utakao takiwa kutumia ili kutoluhusu tatizo hilo kurudi tena.


BABU MADUHU ANAPATIKANA MAGOMENI MOROCCO/KANISANI NJIA PANDA YA KWENDA SINZA  SIMU: 0652 102 152/0788 330 105/ 0755 684 297 NYOTE MNAKARIBISHWA PIA TUNATUMA MIKOANI WHATAPPS NO 0652 102 152 



Share:

Waziri Mhagama Awashukia Waajiri Wasiotekeleza Sheria Ya Ajira Na Mahusiano Kazini


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama amekerwa na waajiri nchini wasiotekeleza Sheria na.6 ya mwaka 2014 kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2019, sheria hiyo inamtaka mwaajiri kumpa mkataba wa ajira mfanyakazi pamoja na kutoa haki ya kuwa na vyama vya wafanyakazi.

Waziri Mhagama akiwa katika ziara ya kujionea hali ya urutubishaji vyakula kwenye viwanda vikubwa vya usindikaji wa chakula (Unga wa ngano, unga wa mahindi na mafuta ya kula) jijini Dar es salaam, wafanyakazi wa kiwanda cha kuzalisha chumvi cha Neelkanth Salt Limited pamoja na Kampuni ya Unique Consultants Services, wamejitokeza kueleza kero zao zilizojikita kwenye mikataba ya ajira, kutokuwepo na haki ya vyama vya wafanyakazi, kima cha mshahara pamoja na michango yao kutopelekwa NSSF.

“Afisa kazi mkoa wa Pwani  nakupigia hii simu nikiwa hapa kwenye kiwanda cha Neelkanth Salt Ltd nataka kesho uje hapa na timu yako nataka mkague mikataba, hakikisheni kinaundwa chama cha wafanyakazi, angalia mishahara  na posho zinazingatia kazi wanazofanya, angalieni vitendea kazi. Huyu mwekezaji anafanya kazi nzuri hapa nchini na amewekeza hadi Tanga, lakini tunataka uwekezaji wenye tija uendane na kazi zenye staha kwa watanzania” Amesisitiza Mhe. Mhagama.

Baada ya kuongea na wafanyakazi wa Kampuni ya Unique Consultants Services, Waziri Mhagama alipiga simu hapo hapo na kumwelekeza Afisa kazi wa mkoa wa Dar es salaam ndani ya saa moja kuhakikisha anafanya ukaguzi wa ghafla kuwasikilza wafanyakazi hao kero zao.

“Watanzania wanao wajibu wa kutafuta haki zao mahala pa kazi, nataka Afisa kazi Dar e salaam uje hapa na meneja wa Tawi wa NSSF, kwani nimeelezwa wafanyakazi hawa kwa miaka miwili michango yao ya mishahara haipelekwi NSSF.Pia nipewe taarifa ya utekelzaji wa suala hili mara moja likikamilika. Niwatake wafanyakazi mtulie serikali inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli ipo tayari kushughulikia kero za wananchi kwa wakati” Amesema Mhagama.

Katika hatua nyingine, Waziri Mhagama amewataka waajiri kuhakikisha michango ya mishaha ra ya wafanyakazi inapelekwa kwenye Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) kwa mujibu wa sheria. Sheria ya Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya jamii sura na. 50 kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2018, inakata mwajiri awasilishe michango ya wafanyakazi kwenye mfuko huo kila mwenzi ambapo mwajiri  na mwajiriwa kila mmoja huchangia 10% ya mshahara.


Share:

IGP Sirro Awataka Waendesha Pikipiki Kufuata Sheria


Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro amewaonya na kuwataka vijana wanaoendesha pikipiki maarufu kama bodaboda, kufuata sheria na alama za barabarani ili kuepusha ajali zinazoweza kuepukika.

IGP Sirro amesema hayo leo akiwa Kiwangwa mkoani Pwani na kuzungumza na baadhi ya wananchi wa eneo hilo wakati akiwa njiani kuelekea mkoani Tanga, ambapo amesema kuwa, karibu asilimia 90 ya vifo nchini vinatokana na ajali za pikipiki.

Hata hivyo, IGP Sirro amewataka wananchi hususan vijana kuacha kujihusisha na uhalifu wa kutumia silaha, wizi wa mifugo na mazao na kuwataka kujihusisha na biashara halali hasa za ujasiriamali.

Akiwa mkoani Tanga, IGP Sirro amefanya ukaguzi wa eneo la uwanja wa mbinu za medani lililopo Mkomazi mkoani humo na kusema kuwa, jitihada kubwa zinaendelea kufanyika ikiwemo kujenga majengo ya kisasa  kwa ajili ya kufanya mafunzo ya utayari kwa askari wa Jeshi hilo.


Share:

Vikao Vya Kamati Za Bunge Kuanza Tarehe 8 Hadi 26 Machi 2021



Share:

UN yaitaja siku ya jana kuwa mbaya zaidi Myanmar baada ya mapinduzi ya jeshi, raia 38 wapigwa risasi


Mjumbe Maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Myanmar ametangaza kuwa Jumatano ya jana ilikuwa siku mbaya na ya umwagaji mkubwa zaidi wa damu nchini humo baada ya mapinduzi ya kijeshi yaliyoiondoa madarakani serikali ya kiraia tarehe Mosi Februari mwaka huu.

Christine Schraner Burgener amesema hayo baada ya jeshi la Myanmar kuua waandamanaji wasiopungua 38 wanaopinga mapinduzi ya jeshi jana Jumatano pekee.

Mjumbe huyo wa Umoja wa Mataifa amesema, mpaka sasa watu zaidi ya 50 wameuawa kwa kupigwa risasi na wengine wengi wamejeruhiwa tangu baada ya mapinduzi ya kijeshi ya mapema mwezi uliopita nchini Myanmar.

Jeshi la Myanmar limewafyatulia risasi hai waandamanaji hao siku moja tu baada ya nchi jirani kutoa wito wa utulivu na kutangaza kuwa, ziko tayari kusaidia juhudi za kutafuta suluhisho la mgogoro wa nchi hiyo.

Tarehe Mosi mwezi wa Februari jeshi la Myanmar lilitwaa madaraka ya nchi baada ya kumkamata Rais wa nchi hiyo, Win Myint na viongozi wengine akiwemo Aung San Suu Kyi, kiongozi wa chama tawala mwenye ushawishi mkubwa, kufuatia siku kadhaa za mivutano nchini humo. Jeshi la Myanmar pia limetangaza hali ya hatari ya kipindi cha mwaka mmoja na kukomesha utawala wa kiraia uliotawala nchi hiyo kwa kipindi cha miaka 10.

Tangu wakati huo mamilioni ya Wamyanmari wamekuwa wakifanya migomo na maandamano ya nchi nzima wakipinga hatua ya jeshi ya kutwaa madaraka ya nchi.




Share:

Bank Officer at KCB Bank Tanzania Limited

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Position: Bank Officer Key responsibilities:    Advise customers on financial related issues Respond to customers on and about Banking Products and related customer queries Offer quality cash services To ensure that customer account and instruments details are correctly captured Ensure that cheques presented are correctly captured Ensure that the names of the payee tallies with the […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Middle School English/Humanities teacher at Iringa International School (IIS)

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

TEACHING VACANCIES FOR ACADEMIC YEAR AUGUST 2021-JUNE 2023 Applicants must have degree in EDUCATION from an accredited university All applicants must have at least 3 years of teaching experience. All applicants must be fluent in English reading, writing and speaking.   Position title: Middle School English/Humanities teacher   NB: Middle School applicants must be experienced in […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Upper primary class teacher at Iringa International School (IIS)

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

TEACHING VACANCIES FOR ACADEMIC YEAR AUGUST 2021-JUNE 2023 Applicants must have degree in EDUCATION from an accredited university All applicants must have at least 3 years of teaching experience. All applicants must be fluent in English reading, writing and speaking.   Position title: Upper primary class teacher. Must have prior experience in the PYP curriculum   […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Middle School Mathematics and Accounting at Iringa International School (IIS)

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

TEACHING VACANCIES FOR ACADEMIC YEAR AUGUST 2021-JUNE 2023 Applicants must have degree in EDUCATION from an accredited university All applicants must have at least 3 years of teaching experience. All applicants must be fluent in English reading, writing and speaking.   Position title: Middle School Mathematics and Accounting   NB: Middle School applicants must be experienced […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Middle School Science Biology, Physics and Chemistry at Iringa International School (IIS)

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

TEACHING VACANCIES FOR ACADEMIC YEAR AUGUST 2021-JUNE 2023 Applicants must have degree in EDUCATION from an accredited university All applicants must have at least 3 years of teaching experience. All applicants must be fluent in English reading, writing and speaking.   Position title: Middle School Science Biology, Physics and Chemistry   NB: Middle School applicants must […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Lower primary class teacher at Iringa International School (IIS)

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

TEACHING VACANCIES FOR ACADEMIC YEAR AUGUST 2021-JUNE 2023 Applicants must have degree in EDUCATION from an accredited university All applicants must have at least 3 years of teaching experience. All applicants must be fluent in English reading, writing and speaking.   Position title: Lower primary class teacher. Must have prior experience in the PYP curriculum   […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Kiswahili teacher at Iringa International School (IIS)

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

TEACHING VACANCIES FOR ACADEMIC YEAR AUGUST 2021-JUNE 2023 Applicants must have degree in EDUCATION from an accredited university All applicants must have at least 3 years of teaching experience. All applicants must be fluent in English reading, writing and speaking.   Position title: Kiswahili teacher. Must be fluent in Swahili reading, writing and speaking   NB: […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Finance and Administration Assistant at Make A Difference Now

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Finance and Administration Assistant    Summary:  We are currently seeking an experienced, and thorough professional with experience in both finance and administration to join our organization. In this role, you will be helping with a variety of administrative tasks, creating budgets, paying expenses and keeping track of all receipts and expenditures as well as overseeing […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Personal Assistant for MD at Biotan Group Limited

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Personal Assistant for MD   BIOTAN GROUP LIMITED  Applications are invited from qualified persons for the above vacant position. About BIOTAN BIOTAN GROUP LIMITED is a processor and exporter of Organic Cashew Nuts. We are working with small holder farmers and groups as the supplier of cashew nuts to our processing facility. Our farmers are […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

export Bookkeeper at Biotan Group Limited

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Export Bookkeeper   BIOTAN GROUP LIMITED Applications are invited from qualified persons for the above vacant position. About BIOTAN BIOTAN GROUP LIMITED is a processor and exporter of Organic Cashew Nuts. We are working with small holder farmers and groups as the supplier of cashew nuts to our processing facility. Our farmers are certified organic […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger