Tuesday 1 December 2020

AFYA YA WAFANYAKAZI NCC NI THAMANI KWA KAZI ZETU-DKT MTURI

Na Mwandishi Wetu

WAKATI dunia ikiadhimisha Siku ya Mapambano dhidi ya maambukizi ya Virusi vya Ukimwi (VVU) na Ukimwi, Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) limesema limefikia malengo yake ya kuhakikisha wafanyakazi wanaelimishwa kuhusu Ukimwi na maambukizi ya virusi visababishavyo ugonjwa huo, kwa mwaka huu.

Limesema litahakisha zana muhimu zinazohitajiwa na wafanyakazi kwa ajili ya kujikinga na maambukizi ya VVU na Ukimwi (Kondomu) zinaendelea kupatikana kwa urahisi katika maeneo yote ambako zinapaswa kuwepo ndani ya ofisi hiyo, kwa ajili ya wahusika kuchukua na kwenda kuzitumia pindi wanapokuwa wakizihitaji.

Mtendaji Mkuu wa Baraza hilo, Dk Matiko Mturi alisema Dar es Salaam jana kuwa, mpango wa kulinda wafanyakazi wake dhidi ya maambukizi ya magonjwa hasa Ukimwi ni endelevu na kwamba unatekelezwa kupitia mafunzo, ushauri nasaha na njia nyingine zinazotumika kufikisha ujumbe kwa wafanyakazi kuhusu namna bora ya kujikinga, kama vile semina na maandiko mbalimbali vikiwemo vipeperushi na ajenda maalumu kwenye vikao vyote vya wafanyakazi.

“Tunashukuru kwamba wafanyakazi wa NCC wamekuwa wakitoa ushirikiano wa hali ya juu kufanikisha utekelezaji wa mpango mkakati wetu wa kuwapa elimu kuhusu masuala ya afya hususan namna ya kujikinga na maambukizi ya VVU pamoja na mambo yote wanayopaswa kuyajua kuhusu Ukimwi,”alisema.

Kutokana na maelezo ya Dk Mturi, NCC ilifanikiwa kupima kwa hiyari wafanyakazi wake, baada ya kuwaandaa kisaikolojia na kufanikiwa kuwapa elimu iliyohitaji sit u kuhusu Ukimwi bali hata magonjwa mengine ambayo walipaswa kupata elimu kuyahusu.

Alisema lengo la kuweka mpango mkakati huo, pamoja na kutimizwa kwa matakwa ya Serikali ya kuhakikisha vita dhidi ya maambukizi ya VVU na Ukimwi vinapiganwa hata katika maeneo ya kazi kwa wafanyakazi kupewa elimu ya kujikinga na maradhi, ni kuhakikisha usalama wa afya za wafanyakazi ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

“NCC inajali na kuthamini afya ya wafanyakazi wake, kwa sababu ndio watenda kazi wanaotegemewa katika uzalishaji wa kila siku, hivyo kutokuwa na afya njema kwao ni tatizo pia kwa mlolongo mzima wa ut

Share:

Field Officer at Food For His Children Tanzania

Job Title: Field Officer Location: Karatu, Arusha, Tanzania JOB DESCRIPTION/RESPONSIBILITIES Discipleship: provide individual teaching of D4D principles and Biblical values to help individuals grow in their relationship with Jesus and to understand who they were created to be and how their role fits with the rest of their family and community. Demonstrate Christ-like behavior in all areas […]

The post Field Officer at Food For His Children Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Network Engineer at Computer Centre Tanzania Limited

Network Engineer Company Name Computer Centre Tanzania Ltd Company Location Dar es Salaam, Tanzania MINIMUM REQUIREMENTS: Qualifications: · Relevant IT Degree or Advanced Diploma – Information Systems · CCNP: Cisco Certified Network Professional – Routing and Switching or equivalent · Fortinet NSE3/4 or Sophos Certified Engineer – XG Firewalls or Yeastar will be an added advantage CERTIFICATIONS […]

The post Network Engineer at Computer Centre Tanzania Limited appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Resident Operations Manager at SiSi Multibiz Limited

Resident Operations Manager Location: Dar es Salaam, Tanzania About the job Urgently looking for candidates on below positions for our small boutique resort property in Kigamboni, Dar es Salaam. Position: Resident Operations Manager F&B manager QUALIFICATION: Preferably Tanzanian, EA citizens may be considered… Must have at least 2yr similar position experience & 5yr hospitality work background Basic […]

The post Resident Operations Manager at SiSi Multibiz Limited appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Immigration Consultant at Migratio Group Tanzania

ob Title: Immigration Consultant Location: Dar es Salaam, Tanzania A career as an Immigration Consultant at Migratio gives you the opportunity to work with a smart, motivated, and diverse peer group. Our exclusive focus on immigration means you will practice in an exciting, ever-changing, and challenging environment with people who are passionate about immigration. Migratio is […]

The post Immigration Consultant at Migratio Group Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Restaurant Manager at Andigo Tanzania

Job Title: Restaurant Manager   Location: Dar es Salaam, Tanzania Overview We are seeking a Restaurant Manager with a background of managing Zanzibar/Indian/Asian Food Menu. The ideal candidate must be a Tanzanian national comfortable working n an Indian and Zanzibar style restaurant setting, preferably speaking Hindi. We offer a basic salary and performance-based incentives. Responsibilities   […]

The post Restaurant Manager at Andigo Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Various Posts at Favorite HR Services Tanzania

Branch Manager Location: Dar es Salaam, Tanzania Overview Industry: Banking Location: Dar es Salaam Minimum Education: Bachelors Degree Required Experience: At least 5+ Years Job Purpose   Ensuring overall branch management; staff management, business growth and development, operational excellence Develop and implement business strategies to deliver performance and growth targets and maintain a good business […]

The post Various Posts at Favorite HR Services Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

IT Support Officer at AccessBank Tanzania (ABT)

Job Title: IT Support Officer Overview AccessBank Tanzania (ABT) is a commercial bank with a special focus on microfinance. With very strong international shareholders such as AccessHolding, International Finance Corporation, KfW, African Development Bank and MicroVest. ABT’s vision is to be committed to the development of financial systems that support social progress by rendering services to […]

The post IT Support Officer at AccessBank Tanzania (ABT) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Finance Reporting Intermediary Analyst at Citi Bank Tanzania

Finance Reporting Intermediary Analyst Job ID 20231458 Primary Location Dar es Salaam, Tanzania; Job Category Finance The Finance Reporting Intermediate Analyst is an intermediate level position responsible for the generation, tracking and submission of financial reports in coordination with the Finance Team. The overall objective of this role is to accurately prepare and report business/financial […]

The post Finance Reporting Intermediary Analyst at Citi Bank Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Human Resources Manager at ITM Tanzania Limited

ITM TANZANIA LTD is hiring POSITION: HUMAN RESOURCES MANAGER Qualification required: Bachelor’s degree in Human Resources Experience: Minimum 2-3 years of hands-on experience in managing a large security force in human resources and administrative management. Job Responsibilities   Define the standards to apply in HR Establish the documents relating to legal obligations for the operation of […]

The post Human Resources Manager at ITM Tanzania Limited appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Project Officer at HELVETAS

Empowering Women and Youth in Horticulture Production and Marketing (KIBOWAVI) Project VACANCY ANNOUNCEMENT HELVETA5 Swiss Intercooperation (HELVETAS) is a Swiss INCO actively contributing to the improvement of the living conditions and status of economically poor and socially disadvantaged people in more than 33 developing countries. HELVETAS has its Head Office in Switzerland (www.helvetas.org). HELVETAS is […]

The post Project Officer at HELVETAS appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Balozi Ibuge Atambelea Ubalozi Wa Tanzania Nchini Ethiopia

Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge akisaini kitabu cha wageni katika Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia
Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge akisisitiza jambo kwa watumishi (hawapo pichani) wakati wa mkutano


Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert A. Ibuge akiendesha kikao na wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini

Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Bibi Elizabeth Rwitunga (mwenye gauni la rangi ya bluu) akimpatia maelezo Balozi Ibuge wakati alipokuwa akikagua mali zinazomilikiwa na Serikali ya Tanzania nchini Ethiopia

Balozi Ibuge akipatiwa maelekezo kutoka kwa Afisa wa Ubalozi wakati wa ukaguzi wa mali zinazomilikiwa na Serikali ya Tanzania nchini Ethiopia  

…………………………………………

Na Mwandishi wetu, Addis Ababa

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge ametembelea Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia kwa lengo la kujionea utendaji kazi wa Ubalozi pamoja na kukagua mali za Serikali nchini humo.

Balozi Ibuge kabla ya kuanza kukagua mali za Serikali, alikutana na watumishi katika mkutano ambapo amewataka kufanya kazi kwa bidii, weledi na uaminifu kwa kuweka mbele maslahi ya Taifa.

“Nawasihi sana kuacha kufanya kazi kwa mazoea na badala yake tufanye kazi kwa bidii na kuwa wabunifu wa kuitangaza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” Amesema Balozi Ibuge

Pamoja na Mambo mengine, Balozi Ibuge amewasihi Ubalozi huo kuhakikisha kuwa wanatekeleza vyema vipaombele vya Serikali ya awamu ya tano kama ilivyoelekezwa kwenye ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (2020 – 2025) katika Sura ya Saba, ambapo sura hiyo imeelekezwa kuwa Balozi zote kutekeleza Diplomasia ya Uchumi pamoja na Diplomasia ya Siasa.

Pia Balozi Ibuge amekagua mali mbalimbali zinazomilikiwa na Serikali ya Tanzania nchini Ethiopia kwa lengo la kuijionea na kujiridhisha juu ya uwepo wa mali hizo.

Kwa upande wake Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Bibi Elizabeth Rwitunga amemhakikishia Balozi Ibuge kuwa watafanya kazi kwa umoja, bidii, weledi na ubunifu kwa maslahi ya Taifa.

Bibi. Rwitunga ameongeza kuwa mashirikiano kati ya Tanzania na Ethiopia ni mazuri na yanaendelea kuimarika ikiwemo ushirikiano katika masuala ya usafiri wa anga ambapo Shirika la Ndege la Ethiopia linashirikiana na Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika masuala mbalimbali ikiwemo mafunzo na matengenezo ya ndege ambapo tayari watanzania watatu (3) wameshapatiwa mafunzo ya ndege.

Kuhusu Sera ya Diplomasia, Kaimu Balozi, Bibi. Rwitunga ameahidi kusimamia sera ya Diplomasia ya uchumi pamoja na Diplomasia ya siasa kwa kuhakikisha kuwa ubalozi utaendelea kuwasiliana na wawekezaji mbalimbali wa kuwekeza nchini Tanzania katika sekta za Nishati, Usafirishaji, Utalii pamoja na Biashara.

Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia unaiwakilisha Tanzania pia katika nchi za Djibouti, Yemen pamoja na Umoja wa Afrika na kamisheni ya Umoja wa Mataifa inayosimamia masuala ya Uchumi Barani Afrika (UNECA).



Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne Disemba 1



Share:

SERIKALI YAWATAKA WALIOHUJUMU MALI ZA VYAMA VYA USHIRIKA KUZIREJESHA MARA MOJA

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Gerald Kusaya,akizungumza wakati wa kongamano la uwekezaji na ununuzi wa hisa na amana za benki ya Ushirika ya Kilimanjaro (Kilimanjaro Cooperative Bank Limited (KCBL) lililofanyika jijini Dodoma.

Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Anna Mghwira,akiongea kwenye kongamano la uwekezaji na ununuzi wa hisa na amana za benki ya Ushirika ya Kilimanjaro (Kilimanjaro Cooperative Bank Limited (KCBL) lililofanyika jijini Dodoma.

Mrajis wa vyama vya ushirika Dk Benson Ndiege,akiwasisitiza jambo washiriki wa kongamano la uwekezaji na ununuzi wa hisa na amana za benki ya Ushirika ya Kilimanjaro (Kilimanjaro Cooperative Bank Limited (KCBL) lililofanyika jijini Dodoma.

Mwenyekiti wa Bodi ya KCBL, Dk Gervas Machimu,akizungumza wakati wa kongamano la uwekezaji na ununuzi wa hisa na amana za benki ya Ushirika ya Kilimanjaro (Kilimanjaro Cooperative Bank Limited (KCBL) lililofanyika jijini Dodoma.

Mwenyekiti wa Kilimanjaro Co-operative Bank Limited (KCBL), Balozi Ibrahim,akitoa maelezo kwa washiriki wa kongamano la uwekezaji na ununuzi wa hisa na amana za benki ya Ushirika ya Kilimanjaro (Kilimanjaro Cooperative Bank Limited (KCBL) lililofanyika jijini Dodoma.

Afisa Mkuu wa biashara wa CRDB, Dk. Joseph Witts,akizungumza wakati wa kongamano la uwekezaji na ununuzi wa hisa na amana za benki ya Ushirika ya Kilimanjaro (Kilimanjaro Cooperative Bank Limited (KCBL) lililofanyika jijini Dodoma

Baadhi ya washiriki wa kongamano la uwekezaji na ununuzi wa hisa na amana za benki ya Ushirika ya Kilimanjaro (Kilimanjaro Cooperative Bank Limited (KCBL) lililofanyika jijini Dodoma

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Gerald Kusaya,akiteta jambo na Mrajis wa vyama vya ushirika Dk Benson Ndiege wakati wa kongamano la uwekezaji na ununuzi wa hisa na amana za benki ya Ushirika ya Kilimanjaro (Kilimanjaro Cooperative Bank Limited (KCBL) lililofanyika jijini Dodoma


Na.Alex Sonna,Dodoma.

SERIKALI imewataka watu wote waliohujumu mali za vyama vya ushirika kujisalimisha na kurudisha mali hizo kwa hiari kabla ya kuchukuliwa hatua za Kisheria.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dodoma na Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Gerald Kusaya wakati wa kongamano la uwekezaji na ununuzi wa hisa na amana za benki ya Ushirika ya Kilimanjaro (Kilimanjaro Cooperative Bank Limited (KCBL).

Kusaya amesema kuwa mali zote za vyama vya ushirika zilizochukuliwa bila kufuata utaratibu zitarudi kwenye mikono ya serikali.

Aidha,amebainisha kuwa wamefanikiwa kurejesha mikononi mwa serikali mali 59 za ushirika zilizochukuliwa bila kufuata utaratibu kuna viwanja,, majumba, mitambo na vingine vyote vina thamani ya bilioni 68.9 na zoezi ni endelevu.

“Kama kuna mtu ana mali za ushirika kwa njia zisizo sahihi azirudishe kwa hiari bila hivyo tuna nguvu nyingi za ziada haijalishi zipo wapi lazima tutazipata,” amesema Kusaya.

Kusaya ameendelea kubainisha kuwq serikali itakuwa bega kwa bega na benki hiyo ua ushirika ya Kilimanjaro ili kuhakikisha inazaa matunda kwa manufaa ya Watanzania.

“Kama tunaamini katika ushirika lazima tuuheshimu na kulenga kufanya ushirika wa kibiashara katika kumkomboa Mtanzania tunataka kila mwanaushirika awe bilionea,” amesisitiza.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa bodi ya KCBL, Dk Gervas Machimu amesema benki hiyo iko imara kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi.

Dkt.Machimu amesema kuwa wameweza kushirikiana na Benki ya CRDB na wana bodi ya pamoja kwa lengo la kuboresha utendaji kazi.

Hata hivyo ameelezea kuwa Serikali inayo ndoto ya kuendeleza viwanda katika nchi na kutoa huduma katika kilimo na biashara na uwepo wa benki hiyo utasaidia kuendeleza sekta za uzalishaji na kusaidia zaidi ya asilimia 60 ya Watanzania wanaotegemea kilimo kunufaika.

Naye Mrajis wa vyama vya ushirika Dk Benson Ndiege amesema kuwa KCLB ni chama cha ushirika kilichoandikishwa kama benki na kimepata leseni ya kuhudumu kama benki ya ushirika kwa wananchi wa mikoa ya Kilimanjaro, Arusha na Tanga katika kilimo cha kahawa.

Amebainisha kuwa serikali kupitia wizara ya kilimo, ofisi ya mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro na benki ya CRDB wamefanya kila liwezekanalo ili benki isimame na kuhudumia makundi mbalimbali kama wakulima, wafugaji, wavuvi, wajasiriamali, wafugaji.

“Kama tukiamua leo kuikuza benki hii kwa kununua hisa tunaweza kuifikisha mbali, vyama vikuu vya ushirika viko 46 lakini vinavyofanya kazi vizuri viko 30,” amesema

Amesema benki ya ushirika ya Kenya inafanya vizuri kutokana na uwezezaji uliofanyika na Tanzania ikiamua jambo hilo hakuna linaloshindikana.

“Kama tukifanya mabadiliko kwenye sekta ya kilimo, viwanda na uvuvi kama walivyofanya Kenya na kwenye benki ya ushirika wana uwekezaji ndio maana wamefanikiwa na benki yao ni ya tatu kwa ukubwa Kenya,” amesisitiza Dk.Ndiege

Mwenyekiti wa Kilimanjaro Co-operative Bank Limited (KCBL), Balozi Ibrahim amevitaka vyama vya ushirika kuchangamkia fursa ya uwekezaji kwenye vyama hivyo.

Amesema wanachama wengi wa KDF wamewekeza kwenye benki hiyo.

Ofisa Mkuu wa biashara wa CRDB, Dk. Joseph Witts amesema kuwa CRDB iliundwa na ushirika na baadaye kuwa benki ya biashara.

Amesema wana kitengo cha kutoa mikopo kwa wakulima na wazalishaji mbalimbali.

“Mikopo yote tunayoitoa kwenye kwenye vyama vya ushirika inalipwa vizuri,” alisema

Amebainisha wametoa bilioni saba kama mtaji kwenye benki ya KCBL.

Amesema CRDB ina menejimenti ndani ya benki hiyo na wajumbe wa bodi ya CRDB wengine wako kwenye benki ya KCBL ili kuweza kuborsha utendaji

Share:

Monday 30 November 2020

Serikali yatoa ufafanuzi wa hoja, ajira mpya za waalimu


 Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhandisi Joseph Nyamhanga, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimeti ya utumishi wa umma na utawala bora Dkt. Laurean Ndumbaro na Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Leonard Akwilapo wametoa ufafanuzi juu ya hoja mbalimbali zilizojitokeza kwenye ajira mpya za waalimu.

Ufafanuzi huo umetolewa leo katika Ofisi ya Rais – TAMISEMI Jijini Dodoma  mara baada  kutokea hoja mbalimbali katika mitandao ya kijamii na vyombo vya habari  kuhusu ajira  mpya za walimu zilizotangazwa hivi karibuni.

Amesema ajira  hizo zilitangazwa  baada ya kukamilika kwa mchakato  wa uchambuzi  wa maombi  ya ajira  uliofanywa  na Ofisi ya Rais  TAMISEMI  kwa kushirikiana  na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi  wa umma  na utawala bora na  tume  ya utumishi wa walimu.

Mhandisi Nyamhanga  amesema hoja kubwa ilyojitokeza ni kwa jina la  Mwalimu mmoja kujitokeza katika kila ukurasa na kuonekana mara 196, badala ya mstari wa  maelezo ya Jedwali (Sub- titles) lakini shule aliyopangiwa ni moja, pamoja na jina hilo kujirudia  halikuchukua nafasi   ya mwombaji  yoyote  ya walimu waliotakiwa kuajiriwa au kuathiri  idadi ya waalimu  waliotakiwa kuajiriwa na  tayari marekebisho yamefanyika.

Mhandisi Nyamhanga amefafanua kuwa Shule binafsi kupangiwa mwalimu, Serikali imekuwa ikiingia ubia na baadhi ya Shule binafsi ambazo hupokea  wanafunzi wenye uhitaji maalum, shule hizo hupamgiwa  walimu na  kupewa ruzuku ya uendeshaji hivyo Shule ya Mwalimu Tutuba ilikuwa katika mchakato wa kuingia  ubia na serikali lakini haukukamilika, hivyo Serikali baada ya  kujiridhisha mwalimu aliyepangiwa katika shule hiyo amepangiwa  katika shule ya sekondari Malagarasi.

Kwa upande wa  wahitimu waliomaliza kidato cha nne mwaka 2017, 2018 na 2019 kupangiwa vituo vya kazi Mhandisi Nyamhanga ameeleza  waombaji wa ajira walitumia  mwaka wa kuhitimu chuo badala  ya mwaka wa kuhitimu  kidato cha nne ambapo waombaji 27 waliandika mwaka 2019, waombaji 27 waliandika mwaka 2019 na waombaji 13 waliandika mwaka 2017, Serikali ilihakiki vyeti vyao  na kubaini  kuwa waombaji hao walihitimu  kidato cha nne kati ya mwaka 2010 hadi 2014.

Kwa kuongezea amesema kuwa Serikali imefuata  utaratibu wa kuhakikisha Waombaji wote waliopata nafasi ya ajira wanazingatia  vigezo vilivyotolewa  katika tangazo la ajira ambapo lilifafanua kuwa mwombaji asizidi umri wa miaka 45.

Aidha Mhandisi Nyamhanga amewalekeza  Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakiki vyeti halisi  vya waliopata ajira na kujiridhisha  kabla ya kutoa barua  za ajira, na kusisitiza kuwa endapo  itabainika  udanganyifu au kasoro za vyeti vya kitaaluma  wahusika watachukuliwa hatua za kisheria.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimeti ya utumishi wa umma na utawala bora Dkt. Laurean Ndumbaro amesema  Serikali imetoa ajira za waalimu kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza  wametoa ajira 8000 na awamu ya pili watatoa kwa waalimu  5000  ili kupunguza malimbikizo ya mshahara kwa waalimu wapya.

Naye Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Leonard Akwilapo ameweka wazi kuwa Serikali itahakikisha waalimu wote waliomba ajira kwa masomo waliyoomba yanaendana na masomo wanayoyafundisha
.

Share:

STANDARD CHARTERED YAENDELEA KUBORESHA HUDUMA KWA WATEJA NCHINI

 

Mkurugenzi Mkuu wa benki ya Standard Chartered Tanzania, Sanjay Rughani akizungumza katika uzinduzi huo kulia ni  Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya bima ya Sanlam Tanzania Khamis Suleiman wakati walipofafanua mambo mbalimbali kuhusu huduma hiyo kwenye hoteli ya Hyatt Regency mwishoni mwa wiki.

Mkuu wa Mahusiano na Masoko wa Benki ya Standard Chartered nchini, Bi. Juanita Mramba (kushoto)  akizungumza jambo mara baada ya uzinduzi wa huduma za bima zitakazokuwa zikitolewa na benki hiyo.
Mkurugenzi Mkuu wa benki ya Standard Chartered Tanzania, Sanjay Rughani akipongeza na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya bima ya Sanlam Tanzania Khamis Suleiman mara baada ya kuzindua huduma za bima za benki hiyo kwa ushirikiano na Kampuni ya Bima ya Sanlam ya jijini Dar es salaam kwenye hoteli ya Hyatt Regency mwishoni mwa wiki iliyopita.

Mkuu wa Mahusiano na Masoko wa Benki ya Standard Chartered nchini, Bi. Juanita Mramba akifuatilia jambo wakati wa uzinduzi huo kulia ni  na Mkuu wa Wateja wa Kawaida wa Benki ya Standard Chartered nchini Tanzania Be.Ajmair Riaz.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Sanlam Tanzania Khamis Suleiman akielezea namna ushirikiano wa kampuni hiyo na benki ya Starndard Chatered zitakavyotolewa kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa benki ya Standard Chartered Tanzania, Sanjay Rughani.
Mkurugenzi Mkuu wa benki ya Standard Chartered Tanzania, Sanjay Rughani akipongeza na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya bima ya Sanlam Tanzania Khamis Suleiman  mara baada ya kuzindua huduma za bima za benki hiyo kwa ushirikiano na Kampuni ya Bima ya Sanlam ya jijini Dar es salaam kwenye hoteli ya Hyatt Regency mwishoni mwa wiki iliyopita.
Mkuu wa Mahusiano na Masoko wa Benki ya Standard Chartered nchini, Bi. Juanita Mramba  akizungumza jambo mara bmkatika uzinduzi wa huduma za bima zitakazokuwa zikitolewa na benki hiyo kulia ni Mkuu wa Wateja wa Kawaida Benki ya Starndard Chartered Bw Ajmair Riaz

Na Leandra Gabriel, Michuzi TV

KATIKA kuendelea kuwajali wateja katika kutoa huduma zao benki ya Standard Chartered kwa kushirikiana na kampuni ya Sanlam wamezindua huduma ya bima za bidhaa kwa wateja ili kuongeza thamani kwa wateja wao.

Uzinduzi huo wa bidhaa za bima uliokwenda kwa kauli mbiu ya "Tunavilinda vyenye Tija," umehusisha bidhaa mbalimbali ikiwemo nyumba na magari kwa ulinzi na usalama wa mali za wateja wao.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi huo leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mkuu wa benki ya Standard Chartered Tanzania, Sanjay Rughani amesema kuwa suala la bima limekuwa na manufaa kwa sasa kutokana na ulinzi na usalama kupitia bima za bidhaa mbalimbali ikiwemo magari, nyumba na afya.

Amesema Tanzania ni sehemu salama na  Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Joseph Magufuli imekuwa ikishirikiana kwa karibu na sekta binafsi katika kujenga uchumi wa Taifa.

"Bima ina umuhimu mkubwa hasa katika ulinzi na usalama, watanzania lazima waelewe umuhimu wa  kukata bima katika mabenki kwa manufaa yao binafsi na mali zao."

Amesema kuwa huo ni ushirikiano wa kibiashara kwa maendeleo ya jamii na taifa la Tanzania na kuahidi kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya tano kwa kuendeleza bima zikiwemo za sekta ya madini na afya.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Sanlam Tanzania Khamis Suleiman mabenki kuanza kuuza bima ni muhimu kwa kuwa wanafahamu ni nini mteja anacho na anachoweza kununua.

Amesema kuwa Kampuni hiyo iliyotimiza miaka 102 tangu kuanzishwa kwake ina malengo ya kufikia asilimia 50 ya watanzania wanaomiliki bima hadi kufikia mwaka 2030, na bima hizo zikiwa ni pamoja na bima za nyumba na magari.

Vilevile amesema, Sanlam imekuwa nchini kwa miaka 20, wakiwa katika nchi 44 zikiwemo nchi zote za Afrika Mashariki na kuahidi kuendelea kutoa huduma bora kwa ustawi wa jamii na taifa la Tanzania.

Amesema kuwa watanzania wachukue bidhaa za bima kutoka Standard Chartered kwa kuwa wanavilinda vyenye tija.

Share:

Waziri Mkuu Amaliza Mgogoro Wa Ardhi Kilosa


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemaliza mgogoro wa ardhi katika shamba la Chanzuru lenye ukubwa wa ekari 1,598 lililopo wilayani Kilosa, Morogoro kati ya Laizer Maumbi na Ameir Nahad kwa kuagiza likabidhiwe kwa Laizer ili aweze kuliendeleza kwa kulima mkonge.

Hata hivyo, Waziri Mkuu ameagiza eneo wanaloishi wananchi ndani ya shamba hilo kikiwemo kitongoji cha viwanja 60 na Chekeleni lihakikiwe na kupimwa ukubwa wake na kisha mkulima huyo akafidiwe eneo jingine na wananchi hao wasibugudhiwe.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumatatu, Novemba 30, 2020) katika kikao chake na Makatibu Wakuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Ardhi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Viongozi wa mkoa wa Morogoro, wilaya ya Kilosa pamoja na Laizer. Kikao hicho kimefanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Mlimwa jijini Dodoma.

“Viongozi wa Serikali simamieni na mratibu vizuri ili wananchi wanaoishi katika vitongoji vilivyomo ndani ya shamba hilo wasibugudhiwe waachwe waendelee kuishi na eneo lililobaki lisilokuwa na mgogoro apewe Laizer. Sehemu hiyo iliyopungua Laizer atafutiwe shamba jingine ili kufidia.”

Amesema awali shamba hilo lilikuwa linamilikiwa na Sadruddin Rajabali ambaye alimuuzia Laizer ambaye aliamua kuachana na shughuli za ufugaji na kuanza kulima mkonge, na alipokuwa katika harakati za kubadilisha umiliki shamba hilo liliuzwa kwa mtu mwingine.

Waziri Mkuu amewataka watumishi wa sekta ya ardhi wilayani Kilosa wahakikishe suala hilo wanalisimamia vizuri ili haki itendeke kwa mkulima huyo kukabidhiwa shamba lake na watumishi waliohusika katika mgogoro huo wachukuliwe hatua.

Pia, Waziri Mkuu ameuagiza uongozi wa mkoa wa Morogoro uhakikishe inabainisha maeneo makubwa yote ambayo hayajaendelezwa na kutoa mapendekezo Serikalini.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Bw. Loatha Sanare ametumia fursa hiyo kumshukuru Waziri Mkuu kwa kumaliza mgogoro huo na kuahidi kwamba atasimamia utekelezaji wa maagizo na maelekezo yaliyotolewa.

Naye, Laizer ameishukuru Serikali kwa hatua iliyofikiwa ya yeye kukabidhiwa shamba hilo ambalo ndilo tegemeo lake kwa sasa, kwani aliuza mifugo yake yote na kununua shamba hilo ambalo amepanda mkonge
.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger