Sunday 3 May 2020

RAIS MAGUFULI : BAADHI YA VIONGOZI WA DINI WAMEANZA KUYUMBA..WAMEMSAHAU MUNGU KWENYE CORONA



Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amesema baadhi ya viongozi wa dini wameanza kuyumba na kumsahau Mungu katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Corona.


 Rais Mafuguli ameyasema leo Jumapili Mei 3,2020 akiwa Chato Mkoani Geita wakati wa hafla fupi ya kumuapisha Dkt. Mwigulu Nchemba kuwa Waziri wa Katiba na Sheria.

Malunde 1 blog imefuatilia hotuba ya Rais Magufuli iliyokuwa inarushwa Live katika vyombo vya na imefanikiwa kupata nukuu zifuatazo

⇒⇒⇒"Wapo hadi baadhi ya viongozi wa dini wamemsahau Mungu ambaye kila siku wamekuwa wakituhubiria, wanashika vitabu wanafahamu yupo Mungu" - Rais Magufuli.

⇒⇒⇒Leo kuna baadhi ya viongozi wa dini wameanza kuyumba na kumsahau Mungu ambaye waliapa ndiyo kiapo chao Biblia au Quraan,wameanza kuisahau na kuiweka pembeni na kuuweka ubinadamu mbele.. Acheni kuomba tunajiokoa,acheni sijui nini nini..

⇒⇒⇒Ni mambo ya ajabu lakini ndiyo hivyo katika kipindi hiki cha mpito tutayasikia mengi na huu ndiyo wakati wa kuwapima imani viongozi tulionao.. Hata viongozi wa dini ..ukizuia waumini wako wasiende kanisani,ukazuia waumini wako wasiende msikitini na unaweza ukakuta hata huo msikiti wala hukuujenga wewe,umejengwa na hao waumini..hilo nalo ni suala la ajabu la kujiuliza, si uwafungulie hao waumini wenye nia waende mle wakamuombe Mungu hata kama wewe hutaenda kuhubiri pale?

⇒⇒⇒Ndiyo hapa tutayaona, na hizi ni changamoto..Tuendelee kumuomba Mungu na Mungu atatusaidia katika kutupitisha kwenye changamoto hizi wala hali siyo mbaya kama inavyotishwa sisi tupo vizuri na biashara zinaendelea na ndiyo maana tuna uwezo wa kulipa hata mishahara" - JPM

⇒⇒⇒Tufunge kila kitu utawalipa mishahara? hata wanaozungumza hao funga huku wanaendesha magari yameandika STK,mafuta yanawekwa mule na serikali lakini anasema fungeni,amesahau alichokalia ndiyo kinachomlisha..

⇒⇒⇒Watanzania simameni Imara,huu ugonjwa utaisha,utapita tunapata changamoto lakini tunazitatua.


Share:

RAIS MAGUFULI AWAONYA VIJANA WANAOPOST UJINGA KUHUSU CORONA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewataka Watanzania kubadilika na kuacha tabia ya kuichafua nchi na kuogopesha wananchi kuhusu ugonjwa wa Corona kwamba kila mtu anayekufa basi ameugua Corona.

Rais Magufuli amesema hayo leo Jumapili Mei 3,2020 wakati akiwa Chato mkoani Geita akimuapisha Dkt. Mwigulu Nchemba kuwa Waziri wa Katiba na Sheria.

"Corona kweli ipo lakini isituyumbishe katika msimamo wetu na direction yetu , Tusitishwe',amesema Rais Magufuli.

 "Naendelea kutoa wito kwa hasa vijana ambao wamekuwa kila siku wanapost, wakimuona mtu, amekufa na Corona..Marehemu Jaji Mkuu tumehangaika naye zaidi ya mwaka mzima, siyo vizuri kutaja matatizo yake..Jaji Mkuu amekufa kwa Kansa lakini watu wamebadilisha maneno ya ajabu",amesema Rais Magufuli.

"Kwa hiyo Watanzania tujifunze hata kumuogopa Mungu,Tujifunze hata kumuogopa mtu, si vyema kila mtu anayekufa ni Corona..It is not Possible..Mbona Maleria yameua watu wengi tu,mbona ajali zimeua watu wengi tu.

"Siku hizi hata mtu akikutwa na ajali polisi wanakwenda,wanavaa gloves zao wanasema huyu ana Corona,mtu hata akijiua chumbani kwake wanapokwenda kuchukua mwili wake wanasema ni Corona..Ninawaomba Watanzania tubadilike, Tunaichafua nchi yetu,tunaiharibu nchi yetu,tunajiogopesha sisi wenyewe wakati hili suala Mungu atali - Handle na tutapita salama",amesema JPM

Share:

LIVE: Rais Magufuli Akizungumza Baada ya Kumuapisha Mwigulu Nchemba

LIVE:  Rais Magufuli  Akizungumza Muda Huu


Share:

Rais Magufuli Kumuapisha Mwigulu Nchemba Leo Saa Nne Asubuhi

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 03 Mei, 2020 atamuapisha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba kuwa Waziri wa Katiba na Sheria. 

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawsiliano ya Rais, Gerson Msigwa  imesema tukio hilo litarushwa moja kwa moja na vyombo vya habari kutoka Chato Mkoani Geita, kuanzia saa 4:15 asubuhi.


Share:

Naibu Waziri Stella Manyanya Aelekeza Viwanda Vya Plastiki Kuzalisha Ndoo Kwa Wingi, Atangaza Msako Mkali Kwa Wafanyabishara Wanaouza Bei Kubwa Ndoo Za Kunawia

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Stella Manyanya ameelekeza Viwanda ya plastiki nchini kuzalisha ndoo kwa wingi na ametoa onyo kali kwa wafanyabishara wanaouza bei za juu vifaa vya kunawia mikono.

Mhe. Stella Manyanya ametoa maagizo haya jana 02 mei 2020, Jijini Dar es salaam alipotembelea viwanda vinavyozalisha plasitiki ambavyo ni kiwanda cha Silafrica Tanzania Ltd {Sumalia} na Kiwanda cha Cello Industries Ltd.

Amevipongeza Viwanda vyote kwa  kwa kuendele kuzalisha ndoo na Vifaa vingine  kwa wingi vinavyotumika kunawia mikono ambavyo vinahitajika sana katika kipindi hiki cha mapambano dhidi ya ugojwa wa Corona

“Nawapongeza na nimefurahishwa sana na uzalishaji mzuri na hakuna wasiwasi kwamba tutakuwa na upungufu wa ndoo za kunawia mikono katika maeneo yetu maana nimejionea uzalishaji mkubwa unaoendelea na ambao utaweza kukidhi maahitaji ya watanzania ya upatikanaji wa ndoo za kunawia mikono”

Aidha, ametoa onyo kali kwa wafanyabiashara wanaendelea kuuza bei Kubwa ndoo na vifaa vingine vya kunawia mokono kwa kufanya mapambano ya ugojwa huu kuwa fursa kwao ya kujinufaisha maradufu na kujipatia kipato kikubwa tofauti na ilivyokuwa awali.

“Natoa onyo kwa wafanyabiashara wote hasa wa reja reja kuna baadhi yao ambao wanatumia muda huu wa mapambano ya Corona kama fursa ya kujinufaisha maradufu, Ni marufuku kwa mtu yeyote kuongeza bei kupita kiasi maana kuna wafanyabishara wanaongeza mara mbili ya bei walizonunulia kiwandani”

Sambamba na hayo Mhe. Stella Manyanya ameendelea kusisitiza kuwa serikali itaendelea kufuatilia na kuwachukulia hatua wafanyabiashara wote wanaenda kinyume na maelekezo yanayotolewa na serikali kwa kuongeza bei bidhaa mbalimbali katika kipindi hiki cha Mfungo wa ramadhani pia cha mapambano ya Corona

“Niendelee kuwakumbusha kuwa Serikali inaendelea kufanya msako mkali nchi nzima kwa wafanyabiashara wote wanaoenda kinyume na maelekezo ya serikali, kama tulivyofanya msako kwa wafanyabiashara wa sukari sasa tunaendelea kwa wafanyabiashara wanaouza vifaa vianavyotumiaka kunawia mikono na bidhaa nyingine ili kila Mtanzania aweze kuhimili bei za bidhaa ili kwa pamoja tuweze kutokomeza huu ugojwa wa Corona”

Ameongeza kuwa “Wizara inaendelea kufanya mahesabu kamili ya bei za ndoo za kunawia mikono ambayo yatazingatia kuazia bei inayouzwa kiwanda pia usafirishaji,  baada hapo tutatangaza bei elekezi kwa kila Mkoa maana kuna watu wameshindwa kuwa wazalendo na vita hii ni ya sisi sote kushirikiana kwa pamoja na kuhakikisha tunaishinda kwa pamoja”.

Na Eliud Rwechungura - Wizara ya viwanda na biashara


Share:

Serikali Yaanza Mkakati Wa Malisho Bora Ya Kisayansi Kwa Ajili Ya Mifugo

Na. Edward Kondela
Serikali imesema itahakikisha changamoto ya malisho ya mifugo nchini inatatuliwa kwa wafugaji kuelimishwa namna ya kulima malisho bora yenye tija kwa mifugo yao.

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel amebainisha hayo mwishoni mwa wiki wakati akikagua shamba darasa la malisho ya mifugo katika Kijiji cha Mahambe kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida na kubainisha kuwa, serikali itaendelea kuwatia moyo wafugaji ili wawe na mashamba ya malisho bora ya mifugo yao pamoja na kuhakikisha uwepo wa maji ya kutosha ya kunyweshea mifugo mambo ambayo yatasaidia kudhibiti migogoro ya ardhi kati ya wafugaji na watumaji wengine wa ardhi.

“Makatibu tawala wa mikoa mingine waige mfano wa Mkoa wa Singida kwa kuandaa mashamba ya malisho ya mifugo, lazima iendelezwe kwenye mikoa mingine. Wafugaji wengine nchini wakiweza kutenga maeneo yao na kupewa mafunzo na kulima malisho yao itakuwa njia sahihi pia ya kuwasaidia wafugaji kuondokana na hali ya kuhamahama ya mifugo yao kutafuta malisho.” Amesema Prof. Gabriel 

Aidha Prof. Gabriel ametoa wito kwa Mkurugenzi wa Utafiti, Mafunzo na Ugani kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Angello Mwilawa kuhakikisha anashirikiana na uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi kutunza mashamba hayo dhidi ya uvamizi wowote wa watu kukata malisho hayo au kuingiza mifugo yao kulisha bila utaratibu unaokubalika.

Pia amewataka wafugaji kote nchini kufahamu nchi yeyote duniani inaendeshwa kwa sheria, taratibu na kanuni hivyo Wizara ya Mifugo na Uvuvi haitamtetea mfugaji yeyote atakayeenda kinyume na sheria kwa kulisha mifugo yake katika eneo au shamba la mmiliki mwingine bila kufuata utaratibu.

Katibu mkuu huyo ameongeza kuwa lengo la Wizara ya Mifugo na Uvuvi ni kuhakikisha uwepo wa mifugo bora nchini ambayo inatokana na kula malisho bora ya kisayansi, ambapo badala ya kula wingi wa majani wale majani yaliyo bora.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Bw. Justice Kijazi ameiomba Wizara ya Mifugo na Uvuvi kupitia kwa Katibu Mkuu wa wizara hiyo anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel, kusambaza wataalam wake wa malisho katika maeneo mengine hapa nchini ili kuwashauri wakulima kuwa na mashamba mengi ya malisho bora ya mifugo ambayo yatakuwa na tija kwa wafugaji kwa kuwa na mifugo bora.

Bw. Kijazi amefafanua pia Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi ina majosho 10 ya kuoshea mifugo huku akiishukuru wizara kwa kuwapatia fedha ya kukarabati majosho matatu na kuiomba wizara iwasaidie pia fedha nyingine kwa ajili ya kukarabari majosho saba yaliyobaki ili wafugaji wengi zaidi katika halmashauri hiyo waweze kuogesha mifugo yao.

Kuhusu idadi ya mifugo iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Bw. Kijazi amesema kuna jumla ya mifugo takriban 600,000 ambapo ng’ombe wapo 350,000 mbuzi na kondoo zaidi ya 200,000 licha ya halmashauri kuwa na changamoto ya kutokuwa na machinjio nzuri, ameiomba wizara kutoa msaada wowote ili kuiwezesha halmashauri hiyo kuwa na machinjio nzuri na kisasa kulingana na idadi ya mifugo iliyopo na hatimaye kuweza kuuza nyama ndani na nje ya nchi.

Akibainisha umuhimu wa uwepo wa mashamba bora ya malisho yanayotokana na kupandwa kwa aina mbalimbali za nyasi zilizofanyiwa utafiti wa kisanyansi na kuthibitishwa kuwa ni bora kwa malisho ya mifugo, Afisa Mifugo Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bibi Bezia Rwongezibwa amesema wafugaji wanafundishwa kulima, kupalilia, kuweka mbolea, kuvuna na hatimaye kuhifadhi malisho hayo ambayo yatatumika wakati wa uhaba wa malisho.

Nao baadhi ya wananchi wakiwemo wa vikundi vya wajasiriamali ambao wamejitolea kulima mashamba darasa kwa ajili ya mifugo kutoka katika Kijiji cha Mahambe Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida, wamesema Wizara ya Mifugo na Uvuvi imewatia moyo namna ya kulima malisho na kuyahifadhi ambapo baadhi yao wameanza kupanda malisho hayo ili wapate mifugo bora wakiwemo ng’ombe.

Wamesema uwepo wa mashamba darasa katika eneo lao ni darasa tosha kwao kwa kuwa wataweza kujifunza zaidi kuhusu malisho bora ya mifugo na hatimaye kulima katika mashamba yao.

Katika hatua nyingine, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel, wakati akikagua shamba darasa la malisho ya mifugo katika Kijiji cha Mahambe kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida, amezungumzia pia kuhusu uwepo wa virusi vya corona nchini vinavyosababisha ugonjwa wa Covid 19 ambapo amebainisha kuwa kwenye sekta ya mifugo wizara imeweka mkazo mkubwa kwa jamii ya wafugaji kote nchini kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli katika kukabiliana na janga hilo kwa kuchukua tahadhari, kufanya maombi pamoja na kufanya kazi kwa bidii.

Mwisho.


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili May 3















Share:

Saturday 2 May 2020

Breaking News : RAIS MAGUFULI AMTEUA MWIGULU NCHEMBA KUWA WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  amemteua Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba kuwa Waziri wa Katiba na Sheria ambapo Uteuzi huo umeanza leo Jumamosi Mei 2,2020

Dkt. Mwigulu Nchemba ambaye amewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani anachukua nafasi ya Balozi Dkt. Augustine Philip Mahiga aliyefariki dunia jana Mei 1,2020.


Share:

Picha : MSAMBAZAJI WA GESI 'KIBIRA GAS' ATOA MSAADA WA VIFAA VYA KISASA KUKABILIANA NA CORONA KWA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA SHINYANGA

Msambazaji wa Gesi katika Manispaa ya Shinyanga Sadiki Idrisa Kibira ‘Kibira Gas’ akimkabidhi Mwenyekiti wa Chama Cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club – SPC),Kadama Malunde vifaa vya kisasa vya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona kwa waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga.


Na Estomine Henry - Mratibu SPC
Mfanyabiashara maarufu anayejihusisha na Usambazaji wa Gesi katika Manispaa ya Shinyanga Sadiki Idrisa Kibira ‘Kibira Gas’ ametoa msaada wa vifaa vya kisasa vya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona kwa Chama Cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club – SPC).

Msambazaji huyo wa Gesi Maarufu ‘Kibira Gas’ amekabidhi vifaa hivyo kwa Mwenyekiti wa Chama Cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga, Kadama Malunde leo Jumamosi Mei 2,2020 katika ofisi ya SPC iliyopo Mjini Shinyanga.

Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo zikiwemo sabuni 5 za maji,tishu 6,ndoo mbili,barakoa,beseni moja na kifaa cha kisasa cha kunawia mikono kwa kukanyaga, Kibira amesema vifaa hivyo vitawasaidia waandishi wa habari kukabiliana na maambukizi ya Virusi vya Corona wanapotekeleza majukumu yao ya kuhabarisha jamii.

“Nimewiwa kufika hapa kuwachangia vifaa hivi kwani Waandishi wa habari ni miongoni mwa makundi ambayo yapo hatarini kupata maambukizi ya Virusi vya Corona kutokana na shughuli zao ambazo zinafanya wakutane na watu mbalimbali kila siku”,amesema Kibira.

Naye Mwenyekiti wa SPC, Kadama Malunde amemshukuru Kibira kwa msaada huo akibainisha kuwa amekuwa mdau wa kwanza mkoani Shinyanga kuliangazia kundi la waandishi wa habari ambao kutokana na kazi yao wanahitaji vifaa vya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona.

“Tunamshukuru sana mdau wetu Kibira Gas kwa msaada huu ambao tunaamini utaongeza nguvu katika mapambano dhidi ya virusi vya Corona”,amesema Malunde.

Katika hatua nyingine Malunde amewakumbusha waandishi wa habari kuzingatia maelekezo yanayotolewa na serikali kuhusu ugonjwa wa Corona na kuhakikisha wanachukua tahadhari kwa kuepuka mikusanyiko,kuvaa barakoa,kunawa maji tiririka na sabuni pamoja na matumizi ya Sanitizer.
Kushoto ni Mfanyabiashara maarufu anayejihusisha na Usambazaji wa Gesi katika Manispaa ya Shinyanga Sadiki Idrisa Kibira ‘Kibira Gas’ akimkabidhi Mwenyekiti wa Chama Cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club – SPC),Kadama Malunde vifaa vya kisasa vya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona kwa waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga leo Jumamosi Mei 2,2020 -Picha zote na Marco Maduhu na Frank Mshana.
Kushoto ni Mfanyabiashara maarufu anayejihusisha na Usambazaji wa Gesi katika Manispaa ya Shinyanga Sadiki Idrisa Kibira ‘Kibira Gas’ akimkabidhi Mwenyekiti wa Chama Cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga ,Kadama Malunde vifaa vya kisasa vya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona kwa waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga.
Mfanyabiashara maarufu anayejihusisha na Usambazaji wa Gesi katika Manispaa ya Shinyanga Sadiki Idrisa Kibira ‘Kibira Gas’ akionesha namna ya kunawa mikono kwa kutumia kifaa cha kisasa wakati akimkabidhi Mwenyekiti wa Chama Cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga ,Kadama Malunde (kulia)vifaa vya kisasa vya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona kwa waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga.
Mwenyekiti wa Chama Cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga ,Kadama Malunde akinawa mikono kwa kutumia kifaa cha kisasa kilichotolewa na Kibira Gas kwa ajili ya waandishi wa habari mkoani Shinyanga kujikinga dhidi ya maambukizi ya Virusi vya Corona.
Kushoto ni Mfanyabiashara maarufu anayejihusisha na Usambazaji wa Gesi katika Manispaa ya Shinyanga Sadiki Idrisa Kibira ‘Kibira Gas’ akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa vya kisasa vya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona kwa waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga.
Mfanyabiashara maarufu anayejihusisha na Usambazaji wa Gesi katika Manispaa ya Shinyanga Sadiki Idrisa Kibira ‘Kibira Gas’ akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa vya kisasa vya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona kwa waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga.
Mwenyekiti wa Chama Cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga (SPC) ,Kadama Malunde akimshukuru Mfanyabiashara maarufu anayejihusisha na Usambazaji wa Gesi katika Manispaa ya Shinyanga Sadiki Idrisa Kibira ‘Kibira Gas’ kwa msaada wa vifaa vya kisasa vya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona kwa waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga leo Jumamosi Mei 2,2020. Kibira pia ametoa msaada wa Barakoa maalumu zenye nembo ya Malunde 1 blog kwa waandishi wa habari wa mtandao wa Malunde 1 blog
Mfanyabiashara maarufu anayejihusisha na Usambazaji wa Gesi katika Manispaa ya Shinyanga Sadiki Idrisa Kibira ‘Kibira Gas’ (kushoto) akipiga picha ya kumbukumbu na Mwenyekiti wa SPC, Kadama Malunde ambaye pia ni Mkurugenzi wa Malunde 1 blog baada ya kumkabidhi barakoa maalumu zenye Nembo ya Malunde 1 blog kwa ajili ya waandishi wa habari wa Mtandao wa Malunde 1 blog
Mfanyabiashara maarufu anayejihusisha na Usambazaji wa Gesi katika Manispaa ya Shinyanga Sadiki Idrisa Kibira ‘Kibira Gas’ (katikati) akipiga picha ya kumbukumbu na Mwenyekiti wa SPC, Kadama Malunde ambaye pia ni Mkurugenzi wa Malunde 1 blog na Mwandishi wa Malunde 1 blog , Marco Maduhu (kushoto) baada ya kumkabidhi barakoa maalumu zenye Nembo ya Malunde 1 blog kwa ajili ya waandishi wa habari wa Mtandao wa Malunde 1 blog
Mkurugenzi wa Malunde 1 blog  Kadama Malunde (kulia) na Mwandishi wa Malunde 1 blog , Marco Maduhu (kushoto) wakiwa wamevaa barakoa maalumu zenye Nembo ya Malunde 1 blog zilizotolewa na Mfanyabiashara maarufu anayejihusisha na Usambazaji wa Gesi katika Manispaa ya Shinyanga Sadiki Idrisa Kibira ‘Kibira Gas’.
Barakoa maalumu zenye Nembo ya Malunde 1 blog zilizotolewa na Mfanyabiashara maarufu anayejihusisha na Usambazaji wa Gesi katika Manispaa ya Shinyanga Sadiki Idrisa Kibira ‘Kibira Gas’.
Barakoa maalumu zenye Nembo ya Malunde 1 blog zilizotolewa na Mfanyabiashara maarufu anayejihusisha na Usambazaji wa Gesi katika Manispaa ya Shinyanga Sadiki Idrisa Kibira ‘Kibira Gas’.
Picha zote na Marco Maduhu na Frank Mshana.
Share:

AKINA MAMA WAHAHA CHUPI ZAO KUIBIWA... WAHUNI WADAIWA KUZITUMIA KUTENGENEZEA BARAKOA

Akina mama eneo la Murang'a nchini Kenya wamelalamikia kuhusu kuhangaishwa na genge la wezi sugu ambao wanawapora chupi kila uchao.

Wanasema sasa hawapumuia kwani chupi zao zinasakwa sana na wezi ambapo kundi hilo la wezi limekuwa likivamia makazi yao na kuanua nguzo hizo kwenye kamba. 

Kwenye ripoti na gazeti la People Daily, kina mama hao wamesema sasa wamelazimika kuchunga nguo hizo za ndani kama dhahabu.

"Tumeshtuka kwa sababu hawa wezi wanaiba tu suruali za kina mama na kuwacha za wazee. Sasa ata hatujui wasichana wetu watavaa nini shule zikifunguliwa," mama mmoja amesema. 

Aidha kina mama hao wanasema huenda chupi hizo zinatumika kutengeneza barakoa na kisha kuuziwa wakazi. 

"Naskia wanatumia chupi zetu kutengeneza barakoa. Chupi moja inatengeneza maski mbili ... kwa suruali zile kubwa, naskia eti wanatumia kuunda maski tano," mkazi aliongeza. Eneo hilo liligonga vichwa vya habari awali baada ya wakazi kuonekana wamevalia chupi kama maski. Walikuwa wameuziwa chupi hizo aina ya thong kama barakoa bila ya kujua na ikawa kicheko kwa waliofahamu yaliyokuwa yamefanyika",wanaeleza.
Share:

Joe Biden ambaye ni Mpinzani wa Trump uchaguzi wa Mwaka Huu Marekani akanusha madai ya kumdhalilisha kingono msaidizi wake

Mgombea urais nchini Marekani katika tiketi ya chama cha Democratic, Joe Biden, amekanusha vikali madai ya kumdhalilisha kingono Tara Reade ambaye alikuwa afisa wake wa zamani, huku akiongeza kuwa kisa hicho ambacho mwathiriwa anadai kilitendeka mwaka 1993, hakikutokea. 

Akihojiwa na kituo cha televisheni cha MSNBC, Biden amekivunja kimya chake cha mwezi mmoja kuhusu suala hilo kwa kusema kuwa hajawahi kutenda uhalifu huo.

 Aidha, taarifa ya Biden imesema waliokuwa wasaidizi wake wakuu mnamo wakati kisa hicho kinadaiwa kutokea, wamekanusha kufahamu tukio hilo.

 Mgombea huyo wa Democrat amesema ataiomba idara ya taifa inayohusika na kuweka rekodi kuchunguza ikiwa kuna rekodi yoyote ya malalamiko hayo. 

Reade ni miongoni mwa wanawake ambao wamelalamika kwamba Biden aliwabusu na kuwashika kwa njia isiyofaa. 

Joe Biden atakiwakilisha chama cha Demokratic katika mchuano wa Urais  nchini Marekani Novemba Mwaka huu ambapo atachuana na Rais wa sasa  Rais Donald Trump


Share:

PICHA: Mwili wa aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria, Balozi Dkt. Augustine Mahiga ukiwasili nyumbani kwake

Mwili wa aliyekuwa waziri wa katiba na sheria Balozi Dkt. Augustine Mahiga, ukishushwa nyumbani kwake Gangilonga mjini Iringa kwaajili ya taratibu za kuuaga kabla ya kuelekea eneo alipozaliwa Tosamaganga nje kidogo ya mji wa Iringa kwa ibada ya  mazishi.



Share:

Waziri Mkuu wa Urusi akutwa na virusi vya Corona

Waziri Mkuu wa Russia Mikhail Mishustin amesema amekutwa na maambukizi ya virusi vya Corona.

Taarifa iliyotolewa na Makao Makuu ya Serikali ya Urusi imesema, Mishustin alimwambia rais wa nchi hiyo Vladmir Putin kwa njia ya video kuwa, amepimwa na kukutwa na virusi vya Corona. 

Amesema amejitenga nyumbani kwake na kufuata maelekezo ya madaktari, na kuongeza kuwa, serikali itaendelea kufanya kazi kama kawaida.

Naibu wa kwanza wa Waziri Mkuu huyo Andrei Belousov atakaimu kwa muda kazi za waziri mkuu huyo, kufuatia hatua iliyoidhinishwa na rais Putin.


Share:

Ratiba Ya Mazishi Ya aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria Balozi Dkt Augustine Mahiga

Makamu wa Rais,Mama Samia Suluhu Hassan, leo  Mei 2, 2020,  ataongoza mazishi ya aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt Augustine Mahiga, aliyefariki dunia jana. 

Dkt. Mahiga mwanadiplomasia mkongwe aliyeitumikia nchi kwa weledi, atazikwa alasiri Tosamaganga, Iringa.

Msemaji Mkuu wa Serikali.Dkt. Hassan Abbas ametoa taarifa hiyo.


Share:

Kiongozi Wa Korea Kaskazini Ajitokeza Hadharani Kwa Mara Ya Kwanza Baada ya Uvumi Kwamba Yuko Mahututi

Kim Jong Un amejitokeza hadharani kwa mara ya kwanza baada ya kutoonekana kwa takribani wiki tatu hadi kupelekea uvumi wa kwamba anaugua na huenda amefariki.

 Shirika la Habari la Korea Kaskazini(KCNA) limesema Kim  Jana May 01, 2020 alikata utepe kwenye uzinduzi wa kiwanda cha mbolea eneo la sunchon.


Share:

Dkt. Kalemani : TANESCO Kateni Umeme Kwa Wadaiwa Sugu Muongeze Mapato

Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani ameliagiza Shirika la Umeme nchini( TANESCO) kuendelea kukata umeme kwa wadaiwa sugu ili kukusanya mapato zaidi na kulipa madeni ya shirika hilo.

Dkt. Kalemani alisema hayo, Aprili 30, 2020, Jijini Dodoma, alipokutana na  Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa TANESCO, kuzungumzia tathimini ya miaka mitano ya utekelezaji wa miradi mbalimbali, baada ya kufanya ziara ya kukagua ujenzi wa upanuzi wa kutuo cha kupoza na kuzambaza umeme cha Zuzu.

Katika kikao hicho, mambo mbalimbali yalijadiliwa kuhusiana na nishati ya umeme inayozalishwa nchini kwa lengo la kuleta manufaa makubwa zaidi kiuchumi kwa nchi, Shirika na watumiaji wa umeme huo ikiwemo viwanda, wafanyabiashara na matumizi mengine.

Dkt. Kalemani aliiagiza TANESCO, kulipa madeni yote inayodaiwa na kutoongeza madeni mapya, vilevile wadaiwa sugu wakumbushwe madeni yao,na endapo hatawalipa, TANESCO iwakatie umeme, kwa kufanya hivyo kutamaliza tatizo la wadaiwa sugu.

“TANESCO inadaiwa madeni makubwa, pia ina wateja wengi sana ambao ni wadaiwa sugu wanaodaiwa fedha nyingi sana na hawalipi ,zimo Taasisi, Mashirika ya Umma na binafsi, pamoja na watumiaji wa kawaida, ninawaagiza nendeni mkawakatie umeme! narudia tena mkakate umeme! mkishaukata, wahusika watalipa na wataonyesha ushirikiano mkubwa, tofauti na kumdai kawaida tu”, alisema Dkt. Kalemani.

Kuhusu wizi na uhujumu wa miundombinu ya umeme, Dkt. Kalemani, aliitaka TANESCO, Bodi ya TANESCO na Watendaji wa Wizara ya Nishati, kushirikiana kwa pamoja kutafuta njia sahihi naya kisasa zaidi  ya kubaini wizi wa umeme,unaofanywa na watu wasiowaaminifu na kusababisha hasara kwa shirika na kupoteza mapato ya taifa.

“Wizi wa umeme upo na haukubaliki, tuweke mfumo sahihi wa kisasa kubaini wahusika, tuache na hii tabia ya kukimbizana kimbizana na wezi, pia sisi watumishi tuwe wazalendo,na wasimamizi wazuri wa miundombinu yetu,vilevile tuwe na walinzi wenye weledi katika miradi yetu bila kujali niya serikali au mtu binafsi, jukumu la ulinzi ni letu sote faida ya Taifa kwa jumla”,alisisitiza Dkt. Kalemani.

Aidha aliwataka kuendelea kufanya tathmini na uwiano wa gharama za kutengeneza nguzo za Zege na nguzo zinazotumika sasa,ili kuangalia uwezekano wa kutumia nguzo za zege katika maeneo yote nchini lakini kwa gharama nafuu, kwa lengo la kukabiliana na changamoto ya kuoza ama kuungua kwa nguzo katika maeneo mbalimbali.

Hata hivyo aliweka wazi kuwa katika baadhi ya maeneo machache ambayo ni korofi nguzo za zege zimeanza kutumika japo ni za gharama kubwa.

Vilevile alitaka kuongezeka kwa idadi ya wateja wa umeme katika kila sekta, kuharakisha uunganishaji wa umeme kwa mteja pale anapomaliza kulipia gharama husika, pamoja na kutatua changamoto za wateja kwa wakati sahihi ili kuvutia wateja wengi zaidi na kuondoa malalaliko.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu aliwataka TANESCO kuangalia uwezekano wa kutoa zawadi kubwa kwa wasamaria wema wanaotoa taarifa za siri kuhusu wanaohujumu na kuiba umeme tofauti na ile inayotolewa sasa, ambayo pia huchukuwa muda mrefu kuikabidhi kwa mhusika.

Mgalu alikitaka  kitengo husika kitunza siri za watoa taarifa,pia kifanye uchunguzi wa kina na kutoa adhabu kwa mtumishi yeyote atakayetiliwa shaka, au kuhusika na wizi pamoja na kuhujumu miundombinu ya umeme kama inavyofanywa kwa wahisika wengine wanaobainika.

Vilevile kuwe na uhamasishaji wa kuwavutia watoa taarifa ili kupata matokeo chanya kunusu wizi na uhujumu wa miundombinu ya umeme nchini.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mhandisi Zena Said, alieleza kuwa ili kukabiliana na changamoto ya wizi na uhujumu wa miundombinu ya umeme, watashirikiana na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa,(TAMISEMI) kuimarisha ulinzi kuanzia ngazi za Kaya.

Mhandisi Said, alisema kwa kufanya hivyo kutasaidia sana kubaini wezi na wahujumu miundombinu ya umeme kwa kuwa watu hao wasio wazalendo huwa wanaoneka na hata kufahamika katika maeneo yao.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TANESCO, Dkt. Alexander Kyaruzi, aliishuruku Wizara ya Nishati kwa kuwapa ushirikiano mkubwa katika kutekeleza majukumu yao na kuyafanyia kazi yale waliokuwa wakiishauri wizara hiyo, katika kipindi chote cha miaka mitano

Dkt.Kiyarunzi, alikiri kwa kuwa kazi ya kusambaza umeme si jambo jepesi, hivyo wanajivunia kuona maendeleo makubwa katika sekta ya nishati ya kuongeza wigo wa usambazaji wa umeme vijijini, kujenga miradi mikubwa ya kuzalisha, njia za kusafirisha na kusambaza umeme pamoja na vituo vya kupoza na kusambaza umeme nchini.

Awali kabla ya kufanyika kwa kikao hicho, Uongozi wa Wizara na Wajumbe wa Bodi hiyo walifanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa upanuzi wa Kituo kikubwa zaidi nchini cha Kupoza na kusambaza umeme cha Zuzu kilichopo jijini Dodoma.

Kwa mujibu wa Dkt. Kalemani, ujenzi wa kituo hicho utakamilika mwishoni mwa mwezi huu wa Mei, 2020 na kitakuwa na uwezo wa kuzalisha Megawati 648 tofauti na vituo vingine.

Na kituo hicho kitaimarisha upatikanaji wa umeme kwa Jijiji la Dodoma ambalo linaendelea kukuwa kwa kasi na  kitakuwa ndiyo kitovu cha vituo vyote vya kupoza kuzambaza umeme katika mikoa yote nchini na kuupeleka nchi jirani pale itakapohitajika kufanya hivyo.


Share:

Tathmini Ya Ununuzi Wa Pamba Kufanyika Kabla Msimu

Serikali imesema inafanya tathmini ya hali ya ununuzi wa zao la pamba msimu wa mwaka 2019 ili kuondoa changamoto zilizojitokeza kabla msimu mpya wa ununuzi kuanza mwaka huu.

Akizungumza na viongozi wa wilaya ya Chato mara baada ya kutembelea viwanda vya kuchambua pamba, Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Gerald Kusaya amesema msimu mpya wa ununuzi utatangazwa mara baada ya tathmini ya msimu uliopita kufanyika.

“ Wizara imegundua kuwa hali ya mazao shambani kwa pamba bado ,kwani hata vitumba bado havijapasuka kutokana na uwepo mvua nyingi ,hivyo baada ya ziara hii kwenye mikoa ya kanda ya ziwa serikali itakaa na watalaam ili kuamua lini wakulima wataanza kuuza pamba yao kupitia Vyama Vya Ushirika vya Msingi (AMCOS) “ alisema Kusaya

Aliongeza kusema kabla msimu haujafunguliwa serikali itahakikisha madeni ya wakulima,wanunuzi na ushuru wa AMCOS, halmashauri pamoja na mfuko wa pembejeo yanalipwa.

“Kila mwananchi atalipwa madai yake na jitihada za serikali ni kuona madeni haya yanalipwa kabla ya msimu mpya wa ununuzi wa pamba kuanza” alisitiza Katibu mkuu
 
Katika hatua nyingine Chama Kikuu cha Ushirika Chato( CCU) kimetakiwa kuhamasisha wakulima wengi zaidi kuzalisha zao la pamba ili ipate malighafi za kutosha kutumika kwenye kiwanda chake cha kuchambua pamba.

Kusaya alitoa wito huo kufuatia taarifa ya Meneja Mkuu wa Chama hicho Joseph Masingiri kusema kiwanda kimeshindwa kuendelea na uchakataji marobota kutokana na uhaba wa pamba ambapo msimu wa 2019 ni  kilo milioni 13.6 ,000 tu zilinunuliwa wakati uwezo wake ni kilo milioni 30.

Ili kukabiliana na changamoto za zao hilo,Katibu Mkuu Kusaya amewataka wataalam wa halmashauri na wa chama kikuu  kuhamasisha wakulima kuzalisha mazao ya mkonge na korosho ili kuwa na uhakika wa kipato pale zao la  pamba linapoyumba.

“ Tulime pamba na mazao mengine ya biashara kama mkonge na korosho yanayostawi vizuri kwenye mkoa huu wa Geita na kanda ya ziwa yote .Wizara ya kilimo ipo tayari kuleta mbegu bora za mkonge na korosho toka taasisi za utafiti ili zigawiwe kwa wakulima “ Kusaya.

Kusaya alitaja faida za zao la mkonge kuwa katika kipindi cha miaka mitatu  baada ya kupanda mkulima ataanza kuvuna na kuendelea hadi miaka kumi na tano huku akiendelea na kilimo cha mazao mengine .

Katika kuhakikisha mkoa wa Geita unaongeza uzalishaji wa mazao nchini,Katibu Mkuu huyo ameelekeza mkoa uwasilishe wizarani maandiko ya miradi ya kipaumbele ya umwagiliaji ili serikali itafute wadau wa kuitekeleza.

Nae Katibu Tawala Mkoa wa Geita Dennis Bandisa aliyeshiriki ziara hiyo aliishukuru wizara ya kilimo kwa kuonesha nia ya kusaidia kukuza kilimo cha umwagiliaji na kuwa kuahidi kuwa maandiko atayawasilisha wizarani ndani ya kipindi kifupi.

Taarifa ya  Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato Eliurd Mwaiteleke kuhusu sekta ya kilimo ilisema wilaya hiyo ina eneo la hekta 10,810 zinazofaa kwa umwagiliaj lakini ni hekta 3,416 tu sawa na asilimia 31.6 zinamwagiliwa.

Katika msimu wa mwaka 2019 jumla ya kilo milioni 10.8 za pamba mbegu zilinunuliwa wilayani Chato kupitia AMCOS zenye thamni ya shilingi Bilioni 13.06 ililipwa kwa wakulima.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger