Wednesday 1 April 2020

Watoto 11 waambukizwa corona Uganda...Idadi Kamili Yafika 44

Rais wa Uganda Yoweri Museveni ametangaza maambukizi mapya ya watu 11 ya ugonjwa wa Corona nchini humo, wakiwemo baadhi ya wanakwaya wa kwaya maarufu nchini humo 'Watoto Children's Choir.

Kupitia matangazo ya televisheni, alisema kuwa wagonjwa wote wapya walikuwa karantini baada ya kurejea kutoa ughaibuni , ingawa hakueleza afya zao zikoje kwa sasa na walikuwa wametoka taifa gani.

Mara nyingi kwaya hiyo huwa inatumbuiza katika nchi za ughaibuni kama Marekani, Canada na Uingereza.

Mpaka sasa Uganda imethibitisha kuwa na wagonjwa wa Corona 44.


Share:

Naibu Waziri wa Ardhi Dr Angelina Mabula Ataka Malipo Ya Kodi Ya Pango La Ardhi Kwa Mitandao Ya Simu Kuepuka Corona

Na Munir Shemweta, WANMM SIMIYU
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amewataka wamiliki wa ardhi wanaotaka kilipia kodi ya pango la ardhi kufanya hivyo kupitia mitandao ya simu za viganjani ili kuepuka misongamano inayoweza kuchangia maambukizi ya virusi vya Corona.

Dkt Mabula alitoa tahadhari hiyo juzi wilayani Bariadi mkoani Simiyu alipozungumza na Wakurugenzi na Watendaji wa sekta ya ardhi katika halmashauri za mkoa wa Simiyu akiwa katika ziara ya kuangalia utendaji kazi wa sekta hiyo sambamba na kufautilia maagizo aliyoyatoa kuhusiaa na sekta ya ardhi.

Alisema, ni vizuri katika kipindi hiki ambacho kuna maambulizi ya virusi vya Corona wamiliki wa ardhi wakachukua tahadhari ya kutokwenda ofisi za ardhi kulipia kodi ya pango la ardhi na badala yake wafanye malipo kwa kutumia mitandao ya simu.

Kwa mujibu wa Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, malipo ya kodi ya pango la ardhi yanaweza kufanyika kwa kutumia mitandao yote ya simu za viganjani  pamoja na kutembelea tovuti ya Wizara.

‘’Katika kipindi hiki ambacho kuna maambukizi ya virusi vya Corona wadaiwa pamoja na wale wanaotaka kilipia kodi ya pango la ardhi wakafanya hivyo kupitia mitandao ya simu pamoka na kutembelea tovuti ya Wizara ili kuepuka misongamano inayoweza kuchangia maambukizi’’ alisema Dkt Mabula

Akigeukia suala la makusanyo ya kodi ya Pango la Ardhi katika halmashauri za mkoa wa Simiyu, Dkt Mabula ameoneshwa kutoridhishwa na kasi ya ukusanyaji kodi ya ardhi katika halmashauri za mkoa wa Simiyu pamoja na mkoa huo kusifika katika masuala ya uwekezaji.

‘’ Mkoa wa Simiyu mapato yatokanayo na kadi ya pango la ardhi yako chini sana, lengo la makusanyo kwa mkoa kipindi cha mwaka wa fedha 2019/2020 ni kukusanya bilioni 10 lakini kiasi mlichokusanya hadi sasa ni milioni 190 tu sawa na asilimia 9.1, inaonesha hamjawa makini kufuatilia madeni’’ alisema Dkt Mabula

Aidha, Naibu Waziri Mabula alisema hata malengo ya makusanyo ya kodi ya pango la ardhi yaliyowekwa katika baadhi ya halmashauri hayaendani na hali halisi na kutolea mfano wa halmashauri ya Busega kuwa na lengo la kukusanya milioni 30 wakati  inadai  milioni 343 kutoka kwa wadaiwa wa kodi ya pango la ardhi.

Kaimu Mkuu wa mkoa wa Simiyu ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Festo Kiswaga alimuhakikishia Naibu Waziri wa Ardhi,  halmashauri za mkoa huo zitaanza kuwafuatilia wadaiwa wote wa kodi ya pango la ardhi  sambamba na kuhakikisha viwanja vinaingizwa katika mfumo na kuwahamaisha wananchi kuchukua hati za ardhi ili kuongeza kasi ya makusanyo ya kodi ya ardhi.

Kiswaga alipongeza maboresho mbalimbali yanayofanywa na wizara ya ardhi katika masuala ya utoaji huduma hizo na kutolea mfano uanzishwaji ofisi za ardhi za mikoa kuwa ni moja ya mambo yatakayoleta ufanisi katika sekta ya ardhi.


Share:

Wacheza Bao Na Karata Ndani Ya Masoko Kahamakukamatwa

SALVATORY NTANDU
Serikali Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga imesema itachukua hatua kali kwa baadhi ya wananchi wanaokaidi maelekezo ya Wizara ya afya Maendeleo ya jamii jinsia, wazee na watoto, wanaopenda kwenda kwenye masoko kucheza michezo ya bao, karata na madrafti ili kudhibiti mikusanyiko isiyokuwa na tija katika kipindi hiki cha mlipuko wa ugonjwa unaosababishwa na virusi vya Corona.

Kauli hiyo imetolewa Machi 31 Mwaka huu na Mkuu wa Wilaya ya Kahama Anamringi Macha wakati akizungumza na Mwandishi wa Habari wa Mpekuzi Blogs Ofisini kwake kuhusiana na hatua zinazoendelea kuchukuliwa na dhidi ya  ugonjwa huo.

“Tumebaini katika Masoko ya Kariakoo na Namanga CDT kunabaadhi ya wananchi wanaingia ndani kwa lengo la kucheza bao, karatana drafti sasa hawa tuwachukulia hatua za kisheria, tunaomba wananchi wanaoingia katika masoko yetu wawe ni wale wanaohiji huduma tuu na si vinginevyo,”alisema Macha.

Macha aliongeza kuwa kwa sasa Halmashauri ya Mji wa Kahama imeshaweka utaratibu maalum wa kuingia na kutoka  katika Masoko haya hivyo ni budi wananchi wakatii maelekezo ya kunawa mikono na sabuni bila kushurutishwa ili kujikinga na Ugonjwa huu ambao tayari umesharipotiwa kuwepo hapa nchini.

“Tulifanya  ziara wiki iliyopita  na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi Zainab Telack katika Halmashauri tatu za Msalala,Mji kahama na Ushetu kuhimiza wafanyabiasha na wananchi wote kwa ujumla kuzingatia maelekezo ya Serikali juu ya kujikinga na ugonjwa huu na watakaobainika kwenda kinyume tutawachukulia hatua kali,”alisema Macha.

Kwa upande wake Hamaza Shabani Mfanyabiashara katika Soko kuu la Kariakoo Mjini Kahama alikiri kuwepo kwa watua wanaopenda kukaa katika sokoni hapo na kucheza michezo mbalilmbali ikiwemo kamari kwa kutumia karata licha ya serikali kuzuia mikusanyiko.

“Wapo vijana wanapenda kukaa kaa humu bila kuwa na shughuli maalumu na badala yake hujikuta wakicheza michezo ya karata na drafti na kusababiasha mikusanyiko isiyokuwa na tija tunashukuru kama serikali imeliona hili wazuieni kuingia humu ikiwezakana wekeni migambo kuwadhibiti,”alisema Shabani.

Monica Sweya ni Mfanyabiasha katika Soko la Namanga CDT katika Halamshauri ya Mji Kahama ameiomba serikali kuweka utaratibu wa wananchi kuingia katika masoko ili kuzui maambukizi ya Ugonjwa na unaosababishwa na virusi vya Corona.

“Naiomba  Halmashauri iweke walinzi ambao watawaelekeza wananchi kunawa mikono kabla ya kuingia sokoni kwa utaratibu malumu sambamba na kuwalazimisha  kutumia milango miwili kuingia na kutoka ili kudhibiti ugonjwa huo”,alisema Sweya.

Mpaka sasa Wizara ya afya maendeleo ya Jamii,jinsia wazee na watoto kupitia kwa waziri wake, Ummy Mwalimu imetangaza watu 19 nchini ndio waliothibitika kuwa na ungonjwa unaosababishwa na virusi vya Corona.


Share:

Mtangazaji wa TBC, Marin Hassan afariki dunia

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC),Dkt.Ayub Rioba Chacha ametangaza kifo cha mwandishi wa habari mwandamizi  wa TBC, Marin Hassan Marin kilichotokea leo asubuhi Dar es Salaam

Mipango ya mazishi inaendelea kufanywa na taairfa zaidi zitaendelea kutolewa.


Share:

Benki Ya Dunia Yaipatia Tanzania Mkopo wa dola milioni 500

Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Dunia imeidhinisha mkopo wa dola milioni 500 kwa Tanzania, uliopewa jina la mradi wa uboreshaji wa elimu kwa shule za Sekondari (SEQUIP), ambao utanufaisha wanafunzi milioni 6.5, kwa kuhakikisha wanafunzi wanasoma na kumaliza elimu yao katika mazingira bora.
 
Akizungumza wakati wa Mkutano huo Mkurugenzi mkaazi wa Benki ya Dunia nchini Tanzania Mara Warwick, amesema kuwa hiyo ni hatua muhimu ya kuweza kukabiliana na changamoto za kielimu wanazokumbana nazo watoto.

"Kila mtoto nchini Tanzania anastahili kupata elimu nzuri, lakini maelfu wananyimwa fursa hii ya kubadilisha maisha kila mwaka, mradi huu umetoa kipaumbele zaidi kwa watoto hawa katika kupata haki yao ya msingi ya elimu na kuweka mazingira mazuri kwa watoto wa kike" ameeleza Warwick.


Share:

Watoto 11 waambukizwa corona Uganda...Idadi Kamili Yafika 44

Rais wa Uganda Yoweri Museveni ametangaza maambukizi mapya ya watu 11 ya ugonjwa wa Corona nchini humo, wakiwemo baadhi ya wanakwaya wa kwaya maarufu nchini humo 'Watoto Children's Choir.

Kupitia matangazo ya televisheni, alisema kuwa wagonjwa wote wapya walikuwa karantini baada ya kurejea kutoa ughaibuni , ingawa hakueleza afya zao zikoje kwa sasa na walikuwa wametoka taifa gani.

Mara nyingi kwaya hiyo huwa inatumbuiza katika nchi za ughaibuni kama Marekani, Canada na Uingereza.

Mpaka sasa Uganda imethibitisha kuwa na wagonjwa wa Corona 44.


Share:

Naibu Waziri wa Ardhi Dr Angelina Mabula Ataka Malipo Ya Kodi Ya Pango La Ardhi Kwa Mitandao Ya Simu Kuepuka Corona

Na Munir Shemweta, WANMM SIMIYU
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amewataka wamiliki wa ardhi wanaotaka kilipia kodi ya pango la ardhi kufanya hivyo kupitia mitandao ya simu za viganjani ili kuepuka misongamano inayoweza kuchangia maambukizi ya virusi vya Corona.

Dkt Mabula alitoa tahadhari hiyo juzi wilayani Bariadi mkoani Simiyu alipozungumza na Wakurugenzi na Watendaji wa sekta ya ardhi katika halmashauri za mkoa wa Simiyu akiwa katika ziara ya kuangalia utendaji kazi wa sekta hiyo sambamba na kufautilia maagizo aliyoyatoa kuhusiaa na sekta ya ardhi.

Alisema, ni vizuri katika kipindi hiki ambacho kuna maambulizi ya virusi vya Corona wamiliki wa ardhi wakachukua tahadhari ya kutokwenda ofisi za ardhi kulipia kodi ya pango la ardhi na badala yake wafanye malipo kwa kutumia mitandao ya simu.

Kwa mujibu wa Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, malipo ya kodi ya pango la ardhi yanaweza kufanyika kwa kutumia mitandao yote ya simu za viganjani  pamoja na kutembelea tovuti ya Wizara.

‘’Katika kipindi hiki ambacho kuna maambukizi ya virusi vya Corona wadaiwa pamoja na wale wanaotaka kilipia kodi ya pango la ardhi wakafanya hivyo kupitia mitandao ya simu pamoka na kutembelea tovuti ya Wizara ili kuepuka misongamano inayoweza kuchangia maambukizi’’ alisema Dkt Mabula

Akigeukia suala la makusanyo ya kodi ya Pango la Ardhi katika halmashauri za mkoa wa Simiyu, Dkt Mabula ameoneshwa kutoridhishwa na kasi ya ukusanyaji kodi ya ardhi katika halmashauri za mkoa wa Simiyu pamoja na mkoa huo kusifika katika masuala ya uwekezaji.

‘’ Mkoa wa Simiyu mapato yatokanayo na kadi ya pango la ardhi yako chini sana, lengo la makusanyo kwa mkoa kipindi cha mwaka wa fedha 2019/2020 ni kukusanya bilioni 10 lakini kiasi mlichokusanya hadi sasa ni milioni 190 tu sawa na asilimia 9.1, inaonesha hamjawa makini kufuatilia madeni’’ alisema Dkt Mabula

Aidha, Naibu Waziri Mabula alisema hata malengo ya makusanyo ya kodi ya pango la ardhi yaliyowekwa katika baadhi ya halmashauri hayaendani na hali halisi na kutolea mfano wa halmashauri ya Busega kuwa na lengo la kukusanya milioni 30 wakati  inadai  milioni 343 kutoka kwa wadaiwa wa kodi ya pango la ardhi.

Kaimu Mkuu wa mkoa wa Simiyu ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Festo Kiswaga alimuhakikishia Naibu Waziri wa Ardhi,  halmashauri za mkoa huo zitaanza kuwafuatilia wadaiwa wote wa kodi ya pango la ardhi  sambamba na kuhakikisha viwanja vinaingizwa katika mfumo na kuwahamaisha wananchi kuchukua hati za ardhi ili kuongeza kasi ya makusanyo ya kodi ya ardhi.

Kiswaga alipongeza maboresho mbalimbali yanayofanywa na wizara ya ardhi katika masuala ya utoaji huduma hizo na kutolea mfano uanzishwaji ofisi za ardhi za mikoa kuwa ni moja ya mambo yatakayoleta ufanisi katika sekta ya ardhi.


Share:

Wacheza Bao Na Karata Ndani Ya Masoko Kahamakukamatwa

SALVATORY NTANDU
Serikali Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga imesema itachukua hatua kali kwa baadhi ya wananchi wanaokaidi maelekezo ya Wizara ya afya Maendeleo ya jamii jinsia, wazee na watoto, wanaopenda kwenda kwenye masoko kucheza michezo ya bao, karata na madrafti ili kudhibiti mikusanyiko isiyokuwa na tija katika kipindi hiki cha mlipuko wa ugonjwa unaosababishwa na virusi vya Corona.

Kauli hiyo imetolewa Machi 31 Mwaka huu na Mkuu wa Wilaya ya Kahama Anamringi Macha wakati akizungumza na Mwandishi wa Habari wa Mpekuzi Blogs Ofisini kwake kuhusiana na hatua zinazoendelea kuchukuliwa na dhidi ya  ugonjwa huo.

“Tumebaini katika Masoko ya Kariakoo na Namanga CDT kunabaadhi ya wananchi wanaingia ndani kwa lengo la kucheza bao, karatana drafti sasa hawa tuwachukulia hatua za kisheria, tunaomba wananchi wanaoingia katika masoko yetu wawe ni wale wanaohiji huduma tuu na si vinginevyo,”alisema Macha.

Macha aliongeza kuwa kwa sasa Halmashauri ya Mji wa Kahama imeshaweka utaratibu maalum wa kuingia na kutoka  katika Masoko haya hivyo ni budi wananchi wakatii maelekezo ya kunawa mikono na sabuni bila kushurutishwa ili kujikinga na Ugonjwa huu ambao tayari umesharipotiwa kuwepo hapa nchini.

“Tulifanya  ziara wiki iliyopita  na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi Zainab Telack katika Halmashauri tatu za Msalala,Mji kahama na Ushetu kuhimiza wafanyabiasha na wananchi wote kwa ujumla kuzingatia maelekezo ya Serikali juu ya kujikinga na ugonjwa huu na watakaobainika kwenda kinyume tutawachukulia hatua kali,”alisema Macha.

Kwa upande wake Hamaza Shabani Mfanyabiashara katika Soko kuu la Kariakoo Mjini Kahama alikiri kuwepo kwa watua wanaopenda kukaa katika sokoni hapo na kucheza michezo mbalilmbali ikiwemo kamari kwa kutumia karata licha ya serikali kuzuia mikusanyiko.

“Wapo vijana wanapenda kukaa kaa humu bila kuwa na shughuli maalumu na badala yake hujikuta wakicheza michezo ya karata na drafti na kusababiasha mikusanyiko isiyokuwa na tija tunashukuru kama serikali imeliona hili wazuieni kuingia humu ikiwezakana wekeni migambo kuwadhibiti,”alisema Shabani.

Monica Sweya ni Mfanyabiasha katika Soko la Namanga CDT katika Halamshauri ya Mji Kahama ameiomba serikali kuweka utaratibu wa wananchi kuingia katika masoko ili kuzui maambukizi ya Ugonjwa na unaosababishwa na virusi vya Corona.

“Naiomba  Halmashauri iweke walinzi ambao watawaelekeza wananchi kunawa mikono kabla ya kuingia sokoni kwa utaratibu malumu sambamba na kuwalazimisha  kutumia milango miwili kuingia na kutoka ili kudhibiti ugonjwa huo”,alisema Sweya.

Mpaka sasa Wizara ya afya maendeleo ya Jamii,jinsia wazee na watoto kupitia kwa waziri wake, Ummy Mwalimu imetangaza watu 19 nchini ndio waliothibitika kuwa na ungonjwa unaosababishwa na virusi vya Corona.


Share:

Mtangazaji wa TBC, Marin Hassan afariki dunia

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC),Dkt.Ayub Rioba Chacha ametangaza kifo cha mwandishi wa habari mwandamizi  wa TBC, Marin Hassan Marin kilichotokea leo asubuhi Dar es Salaam

Mipango ya mazishi inaendelea kufanywa na taairfa zaidi zitaendelea kutolewa.


Share:

Benki Ya Dunia Yaipatia Tanzania Mkopo wa dola milioni 500

Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Dunia imeidhinisha mkopo wa dola milioni 500 kwa Tanzania, uliopewa jina la mradi wa uboreshaji wa elimu kwa shule za Sekondari (SEQUIP), ambao utanufaisha wanafunzi milioni 6.5, kwa kuhakikisha wanafunzi wanasoma na kumaliza elimu yao katika mazingira bora.
 
Akizungumza wakati wa Mkutano huo Mkurugenzi mkaazi wa Benki ya Dunia nchini Tanzania Mara Warwick, amesema kuwa hiyo ni hatua muhimu ya kuweza kukabiliana na changamoto za kielimu wanazokumbana nazo watoto.

"Kila mtoto nchini Tanzania anastahili kupata elimu nzuri, lakini maelfu wananyimwa fursa hii ya kubadilisha maisha kila mwaka, mradi huu umetoa kipaumbele zaidi kwa watoto hawa katika kupata haki yao ya msingi ya elimu na kuweka mazingira mazuri kwa watoto wa kike" ameeleza Warwick.


Share:

MTANGAZAJI WA TBC MARIN HASSAN AFARIKI DUNIA




Mtangazaji Marin Hassan Marin wa TBC amefariki dunia leo Aprili Mosi asubuhi katika Hospitali ya Jeshi Lugalo, jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania, Dk Ayub Rioba amethibitisha
Share:

Viwanja Vikubwa Vinauzwa: Mapinga na Bunju

Viwanja Vikubwa Vinauzwa: Mapinga na Bunju
Mapinga, mpani na Bunju, vipo viwanja vya bei zifuatazo:
Mita 20/20 ni tsh 5 mil,
Mita 20/30 ni tsh 7 mil,
Mita 20/40 ni tsh 10 mil,
Robo eka ni tsh 12 mil,
Nusu eka ni tsh 22 mil,
Eka moja ni tsh 42 mil

Kwa Bunju, viwanja vipo mtaa wa Fanaka (Bunju A) na bei ni milion 30 kwa kiwanja cha sqm 1000.

Viwanja hivi vipo umbali wa km 2 kutoka main road (Dar to Bagamoyo Road) Na huduma zote za umeme na maji zipo.

Ukipata ujumbe huu mjulishe ndugu/jamaa/rafiki.

Hakuna dalali/udalali
Mpigie mhusika: 0758603077,
Whatsap 0757489709


Share:

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Yatoa Tahadhari Ya Mvua Kubwa Mikoa 15

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya mvua kubwa kwa siku mbili kuanzia kesho katika mikoa 15 ikiwamo Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mamlaka hiyo, katika siku hizo, kutakuwa na mvua kubwa katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Njombe, Iringa, Songwe, Mbeya na Rukwa.

Meneja wa Kituo Kikuu cha Utabiri wa Hali ya Hewa (TMA), Samuel Mbuya, alisema kutokana na tahadhari hiyo, athari zinazoweza kutokea kwenye maeneo hayo ni makazi na barabara mbovu kuzungukwa na maji hali itakayosababisha kukosekana kwa makazi na adha ya usafiri.

Kwa siku ya Ijumaa, alisema mvua kubwa inatarajiwa katika baadhi ya maeneo ya Jiji la Dar es Salaam, Zanzibar, Pwani, Mafia, Tanga, Manyara, Kilimanjaro, Arusha, Morogoro na kujirudia tena mikoa ya Njombe na Iringa.

Mbuya alisema kutokana na tahadhari hiyo, wakazi wa mikoa hiyo wanapaswa kuchukua hatua za kujikinga na kuendelea kufuatilia taarifa zinazotolewa na TMA.


Share:

Burundi yatangaza kuwa na wagonjwa wa corona kwa mara ya kwanza

Waziri wa afya nchini humo Thadée Ndikumana, ametangaza watu wawili ambao ni raia wa Burundi kuwa na maambukizi ya virusi vya corona.

Raia hao ambao wote ni wanaume, mmoja ana umri wa miaka 56 huku mwingine ana umri wa miaka 42, na walikuwa wanawasili kutoka Rwanda na Dubai, Waziri alisema.

Taifa la Burundi linatarariwa kuwa na uchaguzi mkuu wa rais tarehe 20 Mei Mwaka huu


Share:

Daktari aliyekutana na Rais wa Urusi Vladimir Putin wiki iliyopita apatikana na virusi vya Corona

Daktari aliyekutana na rais wa Urusi Vladimir Putin wiki iliyopita alipokuwa akizuru hospitali moja huko Moscow, amepatikana na virusi vya Corona baada ya kufanyiwa vipimo, Televisheni ya serikali, Rossiya 24, imeripoti leo Jumanne.
 
Rais wa Urusi alizuru hospitali ya Kommunarka Jumanne wiki iliyopita ambapo alikutana na daktari mkuu wa hospitali hiyo Denis Protsenko. 

Wote wawili hawakuwa wamevaa vifaa vya kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona wakati wa mazungumzo yao.

"Hali ni shwari," ofisi ya rais wa Urusi (Kremlin) imesema, ikinukuliwa na shirika la habari la RIA, huku ikikumbusha kwamba Vladimir Putin huwa anafanyiwa vipimo mara kwa mara.


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano April 1




Share:

Rais Mstaafu Jakaya Kikwete Aguswa Na Kifo cha Katibu Mkuu CUF...... "Nimepoteza rafiki wa muda mrefu"

Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne, Dkt Jakaya Mrisho Kikwete, ameonesha kuguswa na msiba wa aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Khalifa Suleiman, aliyefariki Dunia usiku wa kuamkia leo na kusema kuwa amepoteza rafiki yake wa muda mrefu.

Dkt Kikwete ameyabainisha hayo leo Machi 31, 2020, kupitia ukurasa wake wa Twitter, na kutoa pole kwa Mwenyekiti wa chama hicho Profesa Ibrahim Lipumba pamoja na wanachama wote na kwamba wamepoteza kada wa kuaminiwa na kutumainiwa.

"Ni kweli tulikuwa pande mbili tofauti, lakini kama wanadamu tulikuwa marafiki tangu wakati tukiwa wote bungeni na hata baada ya mimi kuacha Ubunge, daima nitamkumbuka kwa moyo wake wa upendo, ukarimu, ucheshi na huruma, tuko pamoja katika majonzi na kuomboleza, tunakuombea wewe binafsi, wanachama wote wa CUF na familia ya marehemu moyo wa subira na ustahamilivu. Innalilahi Wainna Ilaihi Rajiun" ameandika Dkt Kikwete.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger