Friday 31 January 2020

Waziri Mkuu: Serikali Haiwezi Kufuta uchaguzi wote wa Serikali za Mitaa

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema licha ya kuwepo kwa ugatuaji wa madaraka (D by D), Serikali za Mitaa bado zina wajibu wa kuwahudumia wananchi kwa sababu ziko karibu nao zaidi kuliko Serikali Kuu.

Ametoa kauli hiyo jana (Alhamisi, Januari 30, 2020) bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la mbunge wa Viti Maalum, Bi. Ruth Mollel, kwenye kipindi cha maswali kwa Waziri Mkuu bungeni. Mbunge huyo alisema dhana ya ugatuaji wa madaraka inakinzana na hali halisi kwani utekelezaji wake haujaenda sawasawa kwa vile Serikali inakusanya fedha kutoka kwenye vyanzo vya mapato vya Halmashauri kama vile kodi ya majengo na mabango.

“Wajibu wa kumhudumia mwananchi ni wa Serikali za Mitaa kwa sababu iko karibu nao zaidi. Mheshimiwa Mbunge atakubaliana nami kuwa tunashirikiana na Serikali za Mitaa kumhudumia mwananchi lakini hatujaondoa wajibu wa Serikali za Mitaa kuwahudumia wananchi,” amesisitiza.

Amesema Serikali Kuu bado inalo jukumu la kusimamia mapato na imeamua kudhibiti ukusanyaji wa mapato na imekuwa ikihakikisha mapato haya yarudi tena kwa wananchi. “Tunaporudisha kwa wananchi, tunawapelekea hao hao Serikali ya Mitaa kwa mahitaji yao ili watekeleze hilo jambo, hatujawaondolea mamlaka ya kusema tunahitaji darasa, tunahitaji kituo cha afya, tunahitaji uboreshaji wa miundombinu.”

“Tumeongeza hata taasisi kwa kuunda TARURA ili isimamie miundombinu; sasa hivi tunaenda kwenye maji, kutakuwa na taasisi ya kusimamia utoaji wa maji. Pale ambapo kuna mahitaji, Mamlaka ya Serikali za Mitaa iseme inahitaji shilingi ngapi, kwa ajili ya nini, nasi tunawapelekea, ndiyo kwa sababu leo tunaona huduma zinatekelezwa mpaka vijijini. Hii ni kwa sababu tunashirikiana na Serikali za Mitaa katika kuratibu.”

“Ule udhaifu wa usimamizi wa makusanyo, na udhaifu wa usimamizi wa matumizi ambao ulikuwa umejitokeza sasa tunaendelea kuutibu na ndiyo kwa sababu unaona wakati wote tunapokwenda huko kwenye ziara, kwanza tunauliza ukusanyaji na kama makusanyo yoyote yamehifadhiwa na matumizi yake yako sawa, na pale ambapo matumizi yanakuwa si sahihi tunachukua hatua,” amesema.

Amesema kutokana na muundo uliopo, zipo Serikali za Mitaa ambazo zina majukumu yake yaliyoainishwa rasmi na kuna Serikali Kuu ambayo pia inawajibika kuzihudumia Serikali za Mitaa.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema haitaleta maana endapo Serikali italazimika kutengua matokeo ya uchaguzi wote wa Serikali za Mitaa wakati wagombea ambao hawakuridhishwa na matokeo hayo walikuwa na fursa ya kukata rufaa.

“Chaguzi zote nchini zinatawaliwa na kanuni na sheria zake. Kila mmoja aliyeshiriki kama aliona kuna ukiukwaji wowote, alikuwa na fursa ya kukata rufaa na kama hajaridhika, alikuwa na fursa ya kwenda mahakamani,” alisema.

Alisema chaguzi zote zina sheria zake na kanuni zake na hata wakati wa kuandaa kanuni za Serikali za Mitaa, vyama vyote vya siasa vilishirikishwa katika kutengeneza kanuni zao na moja kati ya kanuni hizo ni pale ambapo inatoa fursa kwa yeyote ambaye hajaridhika huko anakogombea, anaweza kukata rufaa na atakapoona rufaa hiyo kwenye ngazi inayofuata haikutenda haki, aende mahakamani.

“Kwa hiyo kulichukua hili kwa ujumla ujumla, inaweza isiwe sahihi sana kwa sababu kila mmoja kule alipo, alikuwa na mamlaka yake inayoratibu na anayo fursa ya kwenda kwenye mamlaka kukatia rufaa pale ambapo hajaridhika na utekelezaji wa jambo hilo. Na vyama vyote vilishiriki kwenye hii kanuni ya kukata rufaa, kwa hiyo ni wajibu wa huyo mgombea kwenye eneo hilo kwenda kukata rufaa,” alisema.

Alikuwa akijibu swali la mbunge wa Mbozi, Bw. Pascal Haonga, aliyetaka kujua kama Serikali iko tayari kurudia uchaguzi wa Serikali za Mitaa wakati wa uchaguzi mkuu wa Oktoba, mwaka huu kwa sababu ule uliopita uligubikwa na dosari nyingi.

“Mchakato wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2019, uligubikwa na dosari nyingi sana zikiwemo za wagombea kutoka vyama vya upinzani kunyimwa fomu, ofisi kufungwa kwa muda wote, hivyo kupelekea baadhi ya wagombea hasa wa upinzani kushindwa kupata fursa za kugombea. Serikali haioni kwamba ni vema uchaguzi wa Serikali za Mitaa uweze kurudiwa sambamba na uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba, mwaka huu?” alihoji.


Share:

Tanzanian Consultant to Manage HIV Data Collection

Tanzanian Consultant to Manage HIV Data Collection Company Overview: Palladium is a global leader in the design, development and delivery of Positive Impact – the intentional creation of enduring social and economic value. We work with foundations, investors, governments, corporations, communities and civil society to formulate strategies and implement solutions that generate lasting social, environmental and financial benefits. … Read More »

The post Tanzanian Consultant to Manage HIV Data Collection appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Madini na Viwanda Vyaleta Mageuzi ya Uchumi Nchini

Na. Immaculate Makilika – MAELEZO
Mauzo ya bidhaa nje ya nchi zisizo kuwa za kawaida yameongezeka kwa asilimia 41.9 kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT), mwezi  Novemba, mwaka jana.

Hayo yamesemwa jana Jijini Dodoma  na Mkurugenzi wa Idara ya Habari - MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari .

Dkt. Abbasi amesema kuwa kupitia jitihada mbalimbali zinazochagizwa na Rais wa Awamu ya Tano, Dkt. John Pombe Magufuli zimesaidia kuongeza ukusanyaji wa mapato, kuongeza mauzo ya bidhaa muhimu kwenda nje na ukuaji wa viwanda nchini  ikiwa ni sehemu muhimu ya  mageuzi ya uchumi nchini.
 
 “Wote mnafahamu kuwa Serikali imechukua hatua kubwa kuanzisha masoko ya madini na kuzuia uuzaji holela na utoroshaji wa madini. Matokeo yake tumeanza kufaidi. Hadi Novemba, 2019, mauzo ya dhahabu nje ambayo ni asilimia 51.4 ya mauzo yote ya bidhaa nje ya nchi yaani bidhaa zisizo za kawaida, yaliongezeka kwa asilimia 41.9 kufikia kiasi cha Dola Bilioni 2.1”, alisema Dkt. Abbasi
 
Aidha, aliongeza kuwa  “sera ya kuchagiza ujenzi wa viwanda nayo imezidi kulipa, ambapo  mauzo ya bidhaa za viwandani nje ya nchi  yameongezeka kwa asilimia 28.4 kufikia Dola milioni 996.0 ikichangiwa zaidi na bidhaa za chuma na mabati, vioo, tumbaku, katani na mbolea. 
 
Jitihada hizo za Serikali zimeendelea kusaidia kuongeza ajira kwa watanzania, sambamba na kuwa vyanzo vipya vya mapato huku vikitazamiwa kusaida uboreshaji wa huduma za kijamii.
 
Mwisho


Share:

Serikali Yasema Mkopo wa Benki ya Dunia wa Dola za Marekani Milioni 500 kwa nchi ya Tanzania haujasitishwa bali majadiliano yanaendelea.

Msemaji wa Serikali ya Tanzania, Dk Hassan Abbasi amewatoa hofu Watanzania kuhusu madai kuwa Benki ya Dunia (WB) imesitisha kutoa mkopo wa masharti nafuu wa Dola 500 milioni za Kimarekani kwa Tanzania, akibainisha kuwa bado wapo kwenye mazungumzo.

Ameeleza hayo jana Alhamisi Januari 30, 2020 katika mkutano na waandishi wa habari mjini Dodoma.

Dk Abbasi ameeleza hayo baada ya kikao cha bodi ya utendaji ya Benki ya Dunia ambacho kingetoa uamuzi kuhusu kuruhusu mkopo huo kuripotiwa kuahirishwa.
 
Kikao hicho kilipangwa kufanyika Jumanne Januari 28, 2020  kwa ajili ya kuidhinisha mkopo huo, lakini kikaahirishwa dakika za mwisho kutokana na kile kilichoripotiwa na vyombo vya habari vya nje kuwa ni ombi la taasisi ya kijamii ambayo ina wanachama wake Tanzania.

Kabla ya kuahirishwa kwa kikao hicho, mkurugenzi anayehusika na haki za watoto wa taasisi ya kimataifa inayojishughulisha na haki za binadamu ya Human Rights Watch (HRW), Zama Neff aliiomba WB kuchelewesha fedha hizo hadi suala la wasichana wanaopata mimba shuleni litakapopatiwa ufumbuzi kuhusu mustakabali wa elimu yao.

Katika maelezo yake , Dk Abbasi amesema, “walipanga kukutana siku fulani, mmoja wa wawakilishi wao aliomba wakutane leo,  mtu anatoka hapo mishipa imekutoka eti mkopo umesitishwa,sio kweli.... kukopa unaweza kuomba benki moja ukakosa nyingine ikakubali kwa hiyo ni majadiliano yanaendelea.”

==>>Msikilize hapo chini


Share:

Uchumi wa Tanzania Wazidi Kukua na Kuimarika

Na Immaculate Makilika - MAELEZO
Hali ya uchumi wa Tanzania imezidi kuimarika na kukua  kwa asilimia 6.9 ikiwa ni  takwimu za hadi mwezi Septemba 2019, huku lengo likiwa ni kufikia asilimia 7.0% na 7.1% .

Taarifa iliyotolewa na Shirika la Fedha Duniani (IMF) Januari 20 mwaka huu, inaonesha  kuwa uchumi wa dunia utakua kidogo kutoka asilimia 2.9 hadi asilimia 3.3 kwa nusu ya kwanza ya mwaka 2019/20.

Akizungumza na waandishi wa habari, jana jijini Dodoma, kuhusu utekelezaji wa miradi mbalimbali ya Serikali, Mkurugenzi wa Idara ya Habari - MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi alisema kuwa, huu ni ukuaji mkubwa katika nchi za Afrika Mashariki nyuma ya Rwanda pekee na bado Tanzania ni miongoni mwa nchi za juu kwenye ukanda wa  Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) na Afrika kwa ujumla.

Dkt. Abbasi alisema kuwa sekta inayoongoza kwa ukuaji wa uchumi ni ujenzi ambayo inachangia asilimia 16, uchimbaji madini na mawe asilimia 13.7, habari na mawasiliano 10.7, maji asilimia 9.1, na usafirishaji na uhifadhi wa mizigo asilimia 9.1.

Aidha, Dkt. Abbasi alisema kuwa, katika kipindi cha miaka mitatu Serikali ya Awamu ya Tano imefanikiwa katika ongezeko la ukusanyaji wa mapato kwa mwezi kutoka shilingi bilioni 850 mwaka 2015 hadi kufikia shilingi trilioni 1.3.

“Leo ninayo furaha kulitangazia rasmi taifa kuwa kutokana na juhudi kubwa zilizofanywa na Serikali kupitia Mamlaka ya Mapato na Idara nyingine za Serikali, wastani wa mapato ya kodi kwa mwezi kati ya Julai hadi Disemba, mwaka 2019, umepanda na sasa ni shilingi trilioni 1.5 kwa mwezi. Hii kwa sasa ndio rekodi mpya, na ndio habari mpya ya mjini”, alisisitiza Dkt. Abbasi.

Ukusanyaji wa mapato ni moja ya vipaumbele muhimu vya Serikali ya Awamu ya Tano. Huku ikitazamia kujenga uwezo wa ndani wa kujitegemea kifedha na kupunguza kwa kadri inavyowezekana utegemezi kutoka kwa Wadau wa Maendeleo na kuhakikisha kwamba mipango ya kukuza uchumi na kupunguza umaskini inatekelezwa bila kukwama kwa sababu ya ukosefu wa fedha.

 Aidha, azma ya Serikali ya kuifanya Tanzania nchi ya uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025, haiwezi kufikiwa endapo Serikali haitokuwa na uwezo wa kifedha wa kugharamia shughuli mbali mbali za maendeleo.


Share:

IT Support Associate Job Opportunity at Sokowatch

IT Support Associate About Us: Sokowatch is transforming communities across Africa by revolutionizing access to essential goods and services. By connecting small shops to the digital economy, we fix inefficient supply chains and provide services that were previously unavailable. Sokowatch aims to provide everything a retailer needs, no wholesalers or banks necessary. Reporting To: Support Manager Location: Dar… Read More »

The post IT Support Associate Job Opportunity at Sokowatch appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Rugemalira Afunguka Mazito Mahakamani

Mfanyabiashara  James Rugemalira, amedai mahakamani kwamba ameandika barua kwenda kwa Kamishna  Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kumwelezea  namna benki ya Standard Chartered Hong Kong ilivyokuwa ikikwepa kodi na ushuru wa forodha. 

Mshtakiwa huyo na wenzake wawili wanakabiliwa na tuhuma za uhujumu uchumi ikiwamo kutakatisha fedha.

Rugemalira alitoa hoja hiyo jana Mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Huruma Shaidi, wakati kesi hiyo ilipopangwa kwa ajili ya kutajwa.

Alitoa madai hayo baada ya Mwendesha Mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Maghela Ndimbo, kudai kuwa kesi ilipangwa kwa ajili ya kutajwa na upelelezi wake bado haujakamilika.

Rugemalira aliomba ruhusa ya kuzungumza na aliporuhusiwa alidai kuwa Januari 24, mwaka huu, alizungumza na mwakilishi wa Takukuru alipotembelea mahabusu na akamkabidhi nakala ya barua hiyo aliyoandika kwenda kwa Kamishna Mkuu wa TRA lakini mpaka sasa hajapata majibu yake.

"Mheshimiwa Hakimu, naomba mahakama yako itakapopanga tarehe nyingine ya kutajwa, upande wa Jamhuri walete majibu kwa sababu wanaostahili kushtakiwa katika kesi hii ni benki hiyo lakini nashangaa kuona wengine wanaunganishwa kwa madai upelelezi haujakamilika.

"Mheshimiwa Hakimu upelelezi wa kesi hii hautakamilika. Kama kweli wanataka ukamilike, wafuatilie hiyo barua aliyowapelekea TRA,” alidai Rugemalira.

Baada ya maelezo hayo, Hakimu Shaidi alisema kesi hiyo itatajwa Februari 13, mwaka huu, na washtakiwa wataendelea kukaa mahabusu.

Mbali na Rugemalira, washtakiwa wengine ni Harbinder Sethi na Joseph Makandege.

Katika kesi ya msingi ya uhujumu uchumi namba 27/2017, Makandege anakabiliwa na mashtaka matano likiwamo la kuisababishia serikali hasara ya dola za Marekani 980,000 pamoja na utakatishaji wa Fedha.

Kwa upande wa Sethi na Rugemalira, walifikishwa mahakamani hapo zaidi ya miaka miwili na wamekaa rumande, kutokana na upelelezi wa kesi yao kutokukamilika.

Washitakiwa hao kwa pamoja wanakabiliwa na mashitaka 12 yakiwamo ya utakatishaji fedha na kusababisha hasara ya Dola za Marekani 22,198,544.60 na Sh 309,461,300,158.27, kwa mara ya kwanza walifikishwa mahakamani hapo Juni 19, 2017.


Share:

LIVE BUNGENI : Mkutano Wa Kumi Na Nane - Kikao Cha Nne: Tarehe 31 Januari, 2020

LIVE BUNGENI : Mkutano Wa Kumi Na Nane - Kikao Cha Nne: Tarehe 31 Januari, 2020


Share:

Monitoring Evaluation and Learning Intern requred at Policy Forum,

Position: Monitoring Evaluation and Learning Intern Policy Forum is incorporated as a Non-Governmental Organizations with registration No. NGO/R2/00015. The Policy Forum (PF) is a network of more than 76 Tanzanian civil society organizations drawn together by their specific interest in enhanced public money accountability at both the central and local levels by improving civil society capabilities and opportunities… Read More »

The post Monitoring Evaluation and Learning Intern requred at Policy Forum, appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Majibu ya serikali kuhusu dhamana kwa Wanaotuhumiwa kwa Makosa ya Uhujumu Uchumi

Serikali imesema kuwa endapo mbunge ataona kuwa kuna haja ya kubadilishwa sheria ya makosa ya uhujumu uchumi ili watuhumiwa wa makosa hayo yawe na dhamana awasilishe hoja yake bungeni kwani Bunge ndiyo chombo chenye mamlaka ya kutunga na kubadili sheria.

Hayo yamesemwa jana bungeni na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandishi Hamad Masauni wakati wa kipindi cha maswali na majibu katika kikao cha pili cha mkutano wa 18 wa Bunge la 11 alipokuwa akijibu swali lililoulizwa na Mbunge wa Viti Maalum, Sabreena Hamza Sungura.

Katika swali lake mbunge huyo aliuliza, “Kutokana na msongamano wa mahabusu na wafungwa magerezani, Je! Serikali haioni ni muda muafaka sasa wa kubadili sheria hiyo ili majaji waweze kutoa dhamana kwa watuhumiwa, kwani kwa hali ilivyo sasa hata mtu anayetuhumiwa kuhujumu Tsh 20,000 ananyimwa dhamana?

“Ni mamlaka ya Bunge hili kutunga sheria na kubadilisha pale unapoona inafaa, na yeye ni mbunge wa Bunge hili na kanuni anazifahamu. Kama anaona kuna utaratibu unaofaa (kubadili sheria), ni haki ya mbunge kutumia haki yake ya kikanuni,” ameeleza Masauni.

Kwa mujibu wa sheria za Tanzania kwa sasa, mtu akishtakiwa kwa kosa la uhujumu uchumi, mahakama haina mamlaka ya kumpa dhamana, na kwamba atakaa rumande hadi hapo hukumu ya kesi itakapotolewa ama aachiwe huru au apewe adhabu.


Share:

PICHA: Kangi Lugola Alivyowasili TAKUKURU Kwa Ajili ya Kuhojiwa

Mbunge wa Mwibara na Waziri wa zamani wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amewasili makao makuu ya ofisi za Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) jijini Dodoma kwa ajili ya kuhojiwa.



Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa January 31




Share:

Research, Monitoring and Evaluation Coordinator at VSO Dar es Salaam

Research, Monitoring and Evaluation coordinator Location: Dar Es Salaam, Tanzania Salary: Competitive Contract type: Permanent Contract length: Open Application Closing Date: 11 Feb 2020 VSO is the world’s leading independent international development organisation that works through volunteers to fight poverty in developing countries. Our high-impact approach brings people together to share skills, build capabilities, promote international understanding and… Read More »

The post Research, Monitoring and Evaluation Coordinator at VSO Dar es Salaam appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Technicians (2 positions) Job at Sahel Trading Co. Ltd

Overview Sahel Trading Co. Ltd registered under section 15 of the companies ordinance 1984 (ACT 2002) invites Applicants for the following position: POSITION: Technicians (2 positions) Bachelor Degree/ Diploma in Electrical Engineering Additional Qualification related to Technician will be preferred Three Years’ Experience in Digital Weighing Systems and Industrial Automation MODE OF APPLICATION: Application along with Curriculum Vitae… Read More »

The post Technicians (2 positions) Job at Sahel Trading Co. Ltd appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Director & National Research Co-ordinator Morogoro

Our Vision A fair water future for all in Tanzania where water is managed in a fair, efficient and sustainable way to support communities, business and ecosystems. Our Mission To work in partnership to advocate for water security and governance for communities, business and ecosystems thereby making an important contribution to achieving the Sustainable water security of Tanzanians.… Read More »

The post Director & National Research Co-ordinator Morogoro appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Thursday 30 January 2020

Maalim Seif Ajitosa Kugombea Uenyekiti wa ACT-Wazalendo

Mshauri Mkuu wa Chama cha siasa nchini Tanzania cha ACT- Wazalendo, Maalim Seif Sharif Hamad amechukua fomu ya kugombea nafasi ya Mwenyekiti Taifa wa chama hicho.

Maalim Seif amechukua fomu hiyo leo Alhamisi Januari 30, 2020 ofisi ndogo ya chama hicho Vuga Mjini Unguja na kukabidhiwa na Kaimu Katibu Mkuu wa ACT- Wazalendo, Doroth Semu.

Baada ya kupewa fomu, Maalim Seif amesema sababu kuu ya kuwania nafasi hiyo inatokana na uwezo wake pamoja na uzoefu alionao wa kisiasa kwa zaidi ya miaka 25 hivi sasa.

Amesema kupitia uzoefu huo ana amini nafasi ya uenyekiti taifa ataweza kuihudumia kwa lengo la kuleta mabadiliko makubwa ndani ya Chama hicho, ambacho hivi sasa kinapanga safu zake za uongozi kwa mujibu wa katiba.


Share:

Senior Insurance Officer at Air Tanzania Company Limited (ATCL)

Senior Insurance Officer  Air Tanzania Company Limited (ATCL) is in the process of revamping its operations and has introduced new equipment to its fleet as part of implementation of its five years Corporate Strategic Plan (2017-2021). In line with this expansion, the company is also making some reforms in its structure, internal operations and staffing to accommodate business… Read More »

The post Senior Insurance Officer at Air Tanzania Company Limited (ATCL) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger