Saturday 2 November 2019

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi November 2





















Share:

Friday 1 November 2019

KIJANA ALIYEFUNGWA MINYORORO CHUMBANI AFUNGULIWA SHINYANGA


Kijana wa miaka 26, mkazi wa Old Shinyanga katika Manispaa ya Shinyanga, aliyekuwa amefungwa minyororo chumbani kwa miezi miwili, Shadrack Johanes amefunguliwa na kufanyiwa usafi, kuvishwa nguo na kuanza kupatiwa matibabu ya afya ya akili.


Shadrack Johanes, alifunguliwa minyororo hiyo jana mara baada ya Nipashe kuripoti habari kuhusu ukatili uliokuwa unafanywa dhidi ya na ndugu zake.

Kwa miezi miwili alikuwa amefungwa minyororo mikono na miguu akiwa mtupu huku akila chakula kwenye chumba ambacho alikuwa anajisaidia haja kubwa na ndogo.

Ofisa Ustawi wa Jamii Manispaa ya Shinyanga, Panuela Samwel, alisema kijana huyo amefunguliwa minyororo hiyo na serikali itatoa matibabu kwake bila malipo.

Panuela Samwel ameongeza kuwa, wameambiwa na wataalamu wa afya kuwa matibabu ya kijana huyo yanatarajiwa kuchukua muda wa miezi sita hadi mwaka mzima. Ofisa huyo wa serikali alisema kama kijana huyo hatapona, watampatia rufani kwenda jijini Dodoma kupatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Mirembe jijini Dodoma.

”Tukio alilofanyiwa kijana huyu ni la kinyama sana, nashukuru vyombo vya habari kwa kuliibua, bila ninyi huenda kijana huyu angefia ndani. Sisi sasa kama serikali, tutamtibu kijana huyu bure kabisa, na leo (jana) anaanza kupatiwa dawa ambayo itachukua muda wa miezi sita hadi mwaka mzima.” amesema Panuela Samwel ambaye ni Ofisa Ustawi wa Jamii Manispaa ya Shinyanga.

Akiwa kwenye familia ya kijana huyo jana, ofisa huyo aliitaka isimnyanyapae tena, badala yake imweke kwenye mazingira mazuri pasi na kumfunga minyororo.

Mratibu wa Magonjwa ya Afya ya Akili, Brigita Nyangare, alisema kijana huyo hana tatizo kubwa sana la akili kwa kuwa ana bado ana uwezo wa kuongea na hajapoteza kumbukumbu.

Alisema atakuwa karibu na kijana huyo muda wote wa matibabu yake na atakuwa anafuatilia anavyoishi nyumbani hadi pale atakapojiridhisha amepona.

Akizungumza kwa shida, Johanes aliwaomba ndugu zake wasimfungie ndani tena. Ndugu wa kijana hauyo waliomba msamaha kutokana na kumfungia na kuahidi kufuata maagizo waliyopewa na serikali.
Share:

ALIYESHIRIKI KUTUNGA SHERIA YA KUZUIA UZINZI AFUMANIWA AKIHONDOMOLA MKE WA MTU


Mwanaume mmoja nchini Indonesia ambaye alishiriki kwa kiasi kikubwa kuandaa Muswada wa sheria ya kupinga vitendo vya uzinifu nchini humo amekamatwa akizini na mke wa mtu.

Mukhlis bin Mudammad ni mmoja kati ya wwanachama wa baraza la wanatheolojia ambalo lilisaidia kutunga sheria za Kiisilamu kupinga vitendo vya zinaa pamoja na baadhi ya makosa mengi, lakini alijikuta akicharazwa viboko 28 hadharani mbele ya kadamnasi ya watu hapo jana siku ya Alhamisi katika Mkoa wa Aceh, Besar kufuatia kufumaniwa uzinzi na Mke wa mtu.

Tukio hilo linamfanya, Mukhlis bin Mudammad mwenye umri wa miaka 46, kuwa kiongozi wa kwanza wa baraza hilo kuadhibiwa na sheria hizo baada ya kukutwa na hatia.

Mukhlis pamoja na mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 33, ambao wote wawili ni wanandoa wamepatika na hatia ya kuchepuka na kuzisaliti ndoa zao kupitia mahaka ya Mkoawa Aceh ya ekhtilat baada ya kufumwa wakifanya vitendo hivyo ndani ya gari katika fukwe mwezi uliyopita.
Share:

IDRIS ARIPOTI TENA POLISI MAKOSA YA MTANDAO...ANATUHUMIWA KUSAMBAZA UONGO NA KUJIFANYA RAIS

Na Pamela Chilongola, Mwananchi 
 Mchekeshaji na mshindi wa shindano la Big Brother 2014, Idris Sultan ameripoti kituo cha polisi kati leo Ijumaa Novemba Mosi, 2019 na kuhojiwa kwa dakika 30 na kutakiwa kuripoti tena Jumatano Novemba 6, 2019.

Jana asubuhi, Idris aliripoti kituoni hapo na kuhojiwa kwa saa tano na kupekuliwa nyumbani kwake, usiku aliachiwa kwa dhamana akitakiwa kuripoti tena leo saa 2 asubuhi, jambo ambalo amelitekeleza.

“Idris ameripoti kituoni saa 2:00 asubuhi na kuhojiwa kwa dakika 30. Wamechukua simu zake kwa uchunguzi na kutakiwa kuripoti tena Jumatano ijayo (Novemba 6, 2019).”

“Wamemueleza kuwa kosa lake ni kusambaza habari za uongo chini ya kifungu cha 16 cha sheria ya makosa ya mtandao. Kosa la pili ni kujifanya Rais chini ya kifungu cha 15 cha makosa ya mtandao,” amesema, Benedict Ishabakaki ambaye ni mwanasheria wa mchekeshaji huyo.

Jana alipopekuliwa nyumbani kwake polisi walichukua kompyuta mpakato kwa ajili ya uchunguzi, aliporudishwa kituoni kabla ya kupewa dhamana alipelekwa kitengo cha makosa ya mtandaoni.

Juzi mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alimtaka Idris kuripoti polisi baada ya kuweka picha yenye sura yake huku akiwa ameketi katika kiti chenye nembo ya Taifa.

Pia, Idris aliweka picha nyingine inayoonyesha sura ya Rais John Magufuli akiwa amesimama huku amevaa suruali yenye mikanda inayoshikizwa mabegani.

Hata hivyo, dakika chache baada ya Makonda kumtaka msanii huyo kuripoti polisi, waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla aliahidi kumuwekea dhamana iwapo angekamatwa.

Ilivyokuwa
Via>>Mwananchi

Share:

AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUMJERUHI ASKARI POLISI KWA KUTUMIA PAKA 'NYAU'

Vyombo vya habari vya Urusi vimeripoti kuwa mwanaume mmoja mjini Moscow anakabiliwa na kifungo cha miaka mitano kwa kosa la kumtumia paka 'nyau' kama silaha yake.

Mtuhumiwa huyo Gennady Shcherbakov anatuhumiwa kwa kumrushia polisi paka wakati ambapo polisi alikuwa ameenda kuthibiti kelele ambazo zilikuwa katika makazi ya watu.

Bwana Shcherbakov, 59, anakabiliwa na kosa la jinai la unyanyasaji dhidi ya polisi.

Kesi hiyo ilifunguliwa siku ya jumatano, ambapo ilikuwa ni kipindi cha zaidi ya mwaka tangu tukio hilo litokee , imeripotiwa na chaneli ya Telegram Baza

Tuhuma hizo zilikuwaje?

Kwa mujibu wa televisheni ya taifa ya Urusi, tarehe 4 oktoba 2018, bwana Shcherbakov alikuwa amekuwa anapiga kelele katika makazi ya watu huko Moscow.

Anadaiwa kuwa alikuwa amelewa sana.

Wakazi wa eneo hilo waliripoti kuhusu usumbufu aliokuwa anasababisha.

Mara baada ya polisi kufika katika eneo hilo kumzuia asiendelee kufanya fujo , bwana Shcherbakov aligoma kutoa ushirikiano kwa polisi na hata kujibu maswali aliyokuwa akiulizwa.

Badala yake bwana Shcherbakov anadaiwa kuwa alimnyanyua paka ambaye alikuwa karibu yake na kumrushia polisi.

Mnyama huyo anaripotiwa kuwa alimjeruhi polisi.

Bwana Shcherbakov, ambaye hakuwa mkazi wa eneo hilo, anakanusha kuhusika na tukio hilo na hata kutumia paka kama silaha.

Yeye anadai kuwa paka huyo alimrukia polisi mwenyewe bila kurushwa au kusukumwa na mtu yeyote.

Kesi hiyo imewekwa kwenye kifungu cha 318 , kwa kosa la uhalifu wa jinai wa kutumia vurugu dhidi ya asifa wa umma.

Haijafahamika kwa nini kesi hiyo imechukua muda mrefu kufunguliwa kama kosa la jinai na hata hawajaeleza nini kitamkuta paka aliyehusika

 Chanzo - BBC
Share:

BIDHAA ZILIZOISHA MUDA WA MATUMIZI,ZILIZOBADILISHWA LEBO ZAKAMATWA KWENYE MADUKA SHINYANGA MJINI

Kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Shinyanga ikishirikiana na wakaguzi kutoka shirika la viwango TBS imefanikiwa kukamata shehena ya bidhaa zilizoisha muda wa zikiendelea kuuzwa katika maduka makubwa maarufu kama Supermarket mjini Shinyanga.

Bidhaa hizo zimekamatwa jana kutokana na msako katika maduka mbalimbali Mjini Shinyanga na kukamata shehena ya bidhaa mbalimbali ikiwemo chakula na vipodozi ambazo zimeisha muda wa kutumika vikiendelea kuuzwa madukani.

Akizungumza baada ya kufanya ukaguzi huo,Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa Mhe. Jasinta Mboneko ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Shinyanga amesema licha bidhaa nyingi madukani kuwa zimeisha muda wa kutumika pia wamebaini kuna udanganyifu mkubwa wa kubadilisha lebo za muda wa matumizi katika bidhaa mbalimbali ili ziendelee kuuzwa sokoni.

Naye Mkaguzi wa kutoka Shirika la Viwango Tanzania TBS Helen Andrew amesema operesheni hiyo sasa ni endelevu kwa mikoa yote.
Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa Mhe. Jasinta Mboneko akiangalia bidhaa ndani ya duka
Share:

Kijana Aliyemtishia Mwenzake Kwa Bastola Yamkuta Mazito....IGP Amtaka Ajisalimishe Polisi

Inspekta Jenerali wa Polisi nchini Tanzania (IGP), Simon Sirro amemtaka kijana aliyemtishia mwenzake bastola kuripoti polisi baada ya kuonekana akifanya kitendo hicho katika picha za video zinazosambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii nchini.

Mbali na kuripoti, Sirro amesema anatakiwa kusalimisha silaha yake.

Ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya hafla ya uzinduzi wa kampeni ya Utatu inayolenga kukomesha rushwa barabarani.

Sirro amesema ameagiza kukamatwa kwa kijana huyo lakini amekuwa akipiga chenga,  amemtaka akajisalimishe mwenyewe kituo cha polisi na kufikishwa mahakamani.


Share:

MIEZI 15 YA MRADI WA ELIMU KWA VISHIKWAMBI WAKAMILIKA

 Mgeni rasmi Katibu Tawala mkoa wa Tanga, Zena Said akitoa hotuba wakati wa kufunga wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi wa XPRIZE- uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bw. Tirso Dos Santos akitoa salamu za UNESCO wakati wa kufunga wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Mkuu wa kitengo cha Elimu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bi. Faith Shayo akifafanua jambo wakati wa kufunga wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Rais-TAMISEMI ambaye alimwakilisha Naibu Katibu Mkuu Elimu Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Gerald Mweli , Bi Odilia Mushi akizungumza wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Mtoto Habiba Athumani (13) mkazi wa kijiji cha Tabora wilayani Korogwe akitoa ushuhuda kwa wageni waalikwa kuhusu mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
Mtoto Ismail Adamu (13) mkazi wa kijiji cha Majengo wilayani Korogwe akitoa ushuhuda kwa wageni waalikwa kuhusu mradi wa XPRIZE- uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Mmoja wa wazazi Stella Ernest ambaye mtoto wake amenufaika na mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi akitoa ushuhuda wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Mmoja wa wazazi Hassan Shomari ambaye mtoto wake amenufaika na mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi akitoa ushuhuda wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Baadhi ya wageni waalikwa pamoja na wazazi ambao watoto wao wamenufaika na mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
Baadhi ya watoto ambao wamenufaika na mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Baadhi ya wadau wa sekta ya elimu walioshiriki katika hafla fupi ya kufunga mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bw. Tirso Dos Santos wakitiliana saini na Katibu Tawala mkoa wa Tanga, Bi. Zena Said (kushoto) ya hati ya makabidhiano ya mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi wakati wa kufunga mradi huo katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bw. Tirso Dos Santos (kulia) akimkabidhi Katibu Tawala mkoa wa Tanga, Bi. Zena Said (wa pili kulia) ripoti ya utekelezaji wa mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe, Bw. Hilary Bitwaye (kushoto), Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya ya Korogwe, Michael Amos (wa pili kushoto) pamoja na Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Bi Odilia Mushi.
 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bw. Tirso Dos Santos (kulia) akimkabidhi Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Bi Odilia Mushi (wa pili kulia) ripoti ya utekelezaji wa mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Katibu Tawala mkoa wa Tanga, Bi. Zena Said (wa pili kushoto) pamoja na Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya ya Korogwe, Michael Amos (kushoto).
 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bw. Tirso Dos Santos (kulia) akimkabidhi Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe, Bw. Hilary Bitwaye (katikati) ripoti ya utekelezaji wa mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Katibu Tawala mkoa wa Tanga, Bi. Zena Said (kushoto) pamoja na Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Bi Odilia Mushi.
 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bw. Tirso Dos Santos (wa pili kulia) akimkabidhi Katibu Tawala mkoa wa Tanga, Bi. Zena Said (katikati) funguo za gari la mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Mkuu wa kitengo cha Elimu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bi. Faith Shayo (kulia), Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Bi. Odilia Mushi (kushoto) pamoja na Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya ya Korogwe, Michael Amos (wa pili kushoto).
 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bw. Tirso Dos Santos (katikati) akimkabidhi Katibu Tawala mkoa wa Tanga, Bi. Zena Said (wa pili kushoto) gari la mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Bi. Odilia Mushi (kushoto), Ofisa Elimu mkoa wa Tanga, Mayasa Hashimu (wa pili kulia), Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya ya Korogwe, Michael Amos (kulia).
 Katibu Tawala mkoa wa Tanga, Bi. Zena Said (aliyeshika usukani) na Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Bi. Odilia Mushi  wakiwa ndani ya gari la mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP mara baada ya kupokea gari hilo kutoka UNESCO wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
Meza kuu katika picha ya pamoja na baadhi ya watoto  wa halmashauri ya Korogwe walionufaika na mradi wa XPRIZE uliokuwa ukiratibiwa na UNESCO kwa kushirikiana na WFP wakati wa hafla fupi ya kufunga mradi huo wa kuwapatia elimu watoto walio nje ya mfumo rasmi kupitia ubunifu wa Teknolojia kwa kutumia Vishikwambi iliyofanyika kwenye ofisi za ukumbi wa Halmashauri ya mji wa Korogwe, mkoani Tanga.
*****
SERIKALI imetaka watoto wote walioshiriki katika mradi wa XPRIZE-Unesco wa kujua Kuandika, Kusoma na Kuhesabu kwa kutumia Vishikwambi katika mradi wa majaribio mkoa wa Tanga kuhakikishwa wanaendelea na elimu katika shule shirikishi za mkoa huo.

Mradi huo wa XPRIZE umekamilisha awamu yake ya miezi 15 na mafanikio yake ni makubwa.

Akizungumza mjini Korogwe wakati wa kufunga mradi huo, Katibu Tawala mkoa wa Tanga, Bi. Zena Said alisema kwamba mradi huo ulilenga kupeleka elimu kwa watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu unastahili kuingia awamu ya pili kabla ya mafanikio yake kusambazwa nchi nzima.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia, Bi. Zena alisema kwamba kwa sasa wanafanya mchakato wa kuwa na awamu ya pili ya mradi huo ambao utaondoa changamoto zilizopo kabla ya kusambazwa nchini kote.

Mradi huo ulioanza Desemba 2017 umefikia mwisho wake Aprili mwaka huu na umeelezwa kuwezesha watoto walioshiriki kufanya vyema katika masomo hayo waliojifunza bila Mwalimu kwa kutumia michezo iliyopo kwenye Vishikwambi.

Watoto wanaohusika ni wa miaka 5 mpaka 12. Imeelezwa kuwa kwa matumizi hayo ya Vishikwambi na mafanikio yake inaonesha kuwa njia nyingine ya kurejesha watoto wengi waliokosa elimu, darasani kwa kutumia teknolojia upo sahihi.

Bi. Zena alisema hakuna shaka kwamba elimu ni muhimu na kutokana na ukweli huo, mradi umedhirisha uwezo wake wa kusaidia wasioipata kwa kawaida kuipata. Katika kuimarisha kwenye mchakato wa pili kwa kuangalia matatizo yaliyopunguza kasi, serikali inaona Vishikwambi vibaki shule kwa usalama na pia walimu kutumika kuwezesha watoto wengi zaidi kujua kwa kasi KKK huku wakiimarisha uwezo wao wa kutumia teknolojia kujilete maendeleo.

Alisema pamoja na kunufaisha watoto mradi huo pia umefanikiwa kisaikolojia kushawishi watoto zaidi kupenda kusoma na kuanza mapema kutengeneza uongozi hasa kwa vijana ambao kutokana na kujua kusoma wamekuwa maarufu katika vijiji vyao.

Alitaka pamoja na kumalizika kwa mradi huo, wasimamizi wa sola katika vitongoji 170 kuhakikisha kwamba wanatunza sola hizo ili kusaidia vijana hao na watu wengine kufanyia kuchaji.

Mafanikio ya mradi huo kunaongeza nafasi zaidi kwa mujibu wa sera ya serikali ya kuhakikisha kwamba watoto wote hata wale ambao hawakuingia katika mfumo rasmi wanaingiza katika mfumo wa elimu kwa kupitia taratibu mbalimbali. Kwa sasa taratibu hizo ni utaratibu wa Memkwa kwa elimu ya msingi na Mespa kwa sekondari

Mradi huo ambao umefungwa ni sehemu ya mradi wa majaribio wa dunia ambapo teknolojia inajaribiwa kusaidia wale waliokosa nafasi ya kuingia shule.

Wakati mradi huo unaanza mwakilishi wa Global Learning Xprize, Elianne Philibert  alisema kwamba mafanikio yake yatawezeshwa kutengenezwa kwa moduli za kufundishia watoto walio nje ya mfumo rasmi wanaotumia lugha ya Kiswahili.

Washiriki wa mradi huo wa XPRIZE chini ya uangalizi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula (WFP) na Kamati ya kitaifa inayohusisha pia Wizara ya Elimu imelenga kuwapata watoto ambao wanaweza kuingizwa darasa la pili na kuendelea na pia kuongeza uwezo wa kumudu masomo kwa watoto wa darasa la pili. Mradi huo ni matokeo ya mashindano Global Learning XPRIZE yaliyozinduliwa na Taasisi ya XPRIZE Septemba 2014.

Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bw. Tirso Dos Santos alisema katika hafla hiyo kwamba mradi huo  ulisohirikisha wilaya sita za Handeni, Korogwe, Lushoto, Mkinga, Muheza, na Pangani umekuwa na mafanikio kutokana na kujitoa kwa wadau wa mradi huo na wale ambao wamepelekewa.

Alishukuru serikali ya Tanzania kwua kushiriki katika shindano na pia kutekeleza malengo ya mradi huo. Alisema mradi huo ni utekelezaji wa wazo la UNESCO kwamba elimu ni tumaini jema  lakufikia maendeleo.

“Mradi wa XPRIZE umedhirisha kwamba mafunzo au utoaji elimu kwa watu ambao wamekosa au wana mazingira magumu unaweza kuboreshwa kwa ubunifu wa watoto kujifunza wenyewe kwa kutumia mifumo ya komyuta kama ilivyokuwa kwa vishikwambi “ alisema Tirso.

Alisema kabla ya mradi huo washiriki wake asilimia 74 walikuw ahawajwahi kugusa jingo inaloitwa shule, asilimia 80 walikuwa wanajifunza nyumbani na asiimia 90 walikuwahawawezi kusoma hata neon moja la Kiswahili ambalo ni lugha yataifa.

“Baada ya miezi 15  namba hizo zimepunguzwa kwa zaidi ya nusu huku watoto hao wakijifunza takribani sawa na watu walioshiriki darasani kwa kipindi cha mwaka mzima” alisema.

Kutokana na mafanikio hayo UNESCO imeitaka Wizara ya Elimu kusambaza zaidi wazo la mradi huo ili kuwafikia watoto wengi zaidi waliopemnbezoni na mazingira magumu yamaisha.

Naye Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Rais Tamisemi ambaye alimwakilisha Naibu Katibu Mkuu Elimu Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Gerald Mweli, Bi Odilia Mushi alisema kwamba mradi huo umefanikiwa na kwamba nia ya serikali kuuimarisha na kuutambua zaidi kabla ya kuutawanya nchini.

Alisema pamoja na kuibua hamasa, ushuhuda wa watoto wenyewe unaonesha kwamba teknolojia inaweza kutumika kufungua maeneo yenye matatizo ya kufikika.

Aidha Ofisa Elimu mkoa wa Tanga, Mayasa Hashimu akimkaribisha mgeni rasmi alisema kwamba watoto ambao walikuwa wamekosa elimu wamepata faida kubwa ya mradi huo hasa wa kujua kuandika kusoma na kuhesabu.

“Hawawezi kuandika kwa kutumia kalamu lakini wanaweza kuandika kwa kutumia Vishikwambi na ni hatua kubwa ya kujua teknolojia na matumizi yake” alisema.

Mmoja wa wazazi Stella Ernest, aliishukuru serikali ya awamu ya Tano kwa kuwezesha kuwapo kwa programu hiyo ambayo imewatoa kimasomaso. Alisema watoto wamekuwa werevu zaidi na kutambua mambo katika hali ya kisasa kuliko awali.

Alisema hata mtoto wake mdogo siku hizi kwa kufurahishwa na michezo iliyopo katika Vishkwambi hivyo anapoamka humuuliza mama yake kama anajua kuandika Ameitaka serikali kuboresha zaidi mradi huo na kuufanya kuwa endelevu ili kusaidia watoto wengi zaidi. Aidha alitaka watoto waliobahatika kupata kujifunza wenyewe kupokewa na kuendelezwa zaidi.

Kauli hiyo pia imetolewa na mzazi mwingine Janeth Massawe ambaye alisema mradi huo ni wa mfano kwani umewasaidia kuwaondolea tatizo la elimu katika eneo lao. Alisema mradi huo umepokewa vyema na kwamba umewachagiza kutambua umuhimu wa elimu.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger