Friday, 11 November 2016

Magazeti ya Leo Ijumaa nov 11 2016

    Share:

    Thursday, 10 November 2016

    HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIRUHUSIWA KUHAMIA UDOM 2016/2017

    Logo
    APPROVED CANDIDATES FOR INTER UNIVERSITY TRANSFERS TO UDOM
    This is to inform all under mentioned names that their request for inter university transfer to UDOM have been approved. Therefore they are required to report to their respective Colleges for registration and other formalities.
    For the online admission letters and other documents required for registration please follow this link: alis.udom.ac.tz
    Document: TRANSFER
    ISSUED BY THE OFFICE OF THE DVC – ARC
    10th November, 2016
    Share:

    HIZI HAPA KURASA ZA NDANI MAGAZETI YA LEO ALHAMISI NOV 10 2016

    Share:

    Wanafunzi hewa 65,198 wabainika shule za msingi, sekondari nchini

    Jumla  ya wanafunzi hewa 65,198 wamegundulika kuwepo katika shule za msingi na sekondari nchini, ambako idadi ya wanafunzi hao isingebainika kiasi cha Sh milioni 931.3 zingepelekwa shuleni kuhudumia wanafunzi hewa kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

    Katika mkutano na waandishi wa habari jana mjini Dodoma, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George Simbachawene alisema kati ya wanafunzi hao wa shule za msingi ni 52,783 na sekondari ni 12,415.

    Simbachawene alisema kazi ya uhakiki wa wanafunzi katika shule za msingi na sekondari ilifanyika mikoa yote nchini kutokana na agizo la Ofisi ya Rais, Tamisemi kwa makatibu tawala wa mikoa yote ya Tanzania Bara.

    Alisema waliagizwa kuhakiki idadi ya wanafunzi katika shule zote za msingi na sekondari kwa kulinganisha taarifa ilivyokuwa Machi mwaka huu wakati wa ujazaji wa madodoso ya takwimu za shule za awali, takwimu za shule za msingi, sekondari na nyaraka za mahudhurio ya wanafunzi.

    Alieleza kuwa taarifa za idadi ya wanafunzi kabla ya kuhakiki Machi 2016, zilionesha kulikuwa na wanafunzi 9,746,534 wa shule za msingi na wanafunzi 1,483,872 wa shule za sekondari.

    “Baada ya uhakiki tuliofanya Septemba mwaka huu, inaonesha kuwepo wanafunzi 9,690,038 wa shule za msingi na wanafunzi 1,429,314 wa shule za sekondari,” alieleza na kuongeza kuwa uchambuzi umeonesha kuwa wanafunzi 52,783 wa shule za msingi na wanafunzi 12,415 wa sekondari hawakutolewa maelezo ya uwepo wao shuleni.

    Alisema kwa tafsiri rahisi hao ni wanafunzi hewa kwa shule za msingi na sekondari nchini, ambao idadi hiyo ya wanafunzi hewa kama isingebainika kwenye uhakiki huo na kupelekwa fedha, Sh milioni 931.3 zingepelekwa shuleni kuhudumia wanafunzi hewa katika mwaka wa fedha 2016/2017.

    Alisema kati ya fedha hizo Sh milioni 527.8 ni kwa shule za msingi na Sh milioni 403.4 ni kwa shule za sekondari.

    Aliitaja mikoa inayoongoza kuwa na wanafunzi hewa ni Tabora (12,112), Ruvuma (7,743), Mwanza (7,349), Dar es Salaam (4,096), Kagera (4,763), Rukwa (4,054), Singida (3,239), Kilimanjaro (2,594), Kigoma (2,323), Njombe (2,307), Simiyu (2,081) na Arusha (1,923).

    Mikoa mingine ni Mara (1,855), Tanga (1,378), Geita (1,281), Morogoro (1,172), Mtwara (882), Mbeya (786), Shinyanga (695), Songwe (512), Manyara (330), Dodoma (284), Lindi (281), Pwani (187), Iringa (161) na Katavi (0).

    Waziri huyo alisema wanafunzi hewa walianza wakati serikali ilipoanza kupeleka fedha shuleni kama ruzuku.

    Alisema Sh bilioni 27 zimekuwa zikipelekwa kila mwezi kama ruzuku ya uendeshaji shule za msingi na sekondari na posho ya madaraka kwa ajili ya wakuu wa shule na walimu wakuu, lakini baadhi ya walimu waliamua kuongeza idadi ya wanafunzi ili wapate fedha zaidi.

    “Huu ujinga unaweza kufanywa hata katika ngazi ya wizara ni jambo la uchunguzi, zile fedha hazipiti Tamisemi zinakwenda moja kwa moja shuleni,” alieleza na kuongeza kuwa hatua za kinidhamu zinaendelea kuchukuliwa kwa wale wote waliosababisha uwepo wa wanafunzi hewa na Tamisemi inaendelea kuhakiki takwimu zilizowasilishwa.

    “Serikali haitegemei tena kuwepo suala la wanafunzi hewa. Naagiza makatibu tawala wa mikoa, wakurugenzi wa mamlaka za serikali za mitaa na wakuu wa shule kuhakikisha suala la wanafunzi hewa halijitokezi tena katika shule zote za msingi na sekondari,” alibainisha Simbachawene.
    Share:

    MAGAZETI YA LEO ALHAMISI NOV 10 2016

    Share:

    Wednesday, 9 November 2016

    TRA Yakusanya Shilingi Trilioni 1.15 Mwezi Oktoba

    Share:

    Rais Barack Obama ampongeza Rais Mteule, Donald Trump na kumualika Ikulu kujadiliana juu makabidhiano ya ofisi.

    Rais Barack Obama wa Marekani  amempongeza Rais Mteule wa taifa hilo, Donald Trump na kumualika Ikulu kujadiliana juu makabidhiano ya ofisi.
    Share:

    Treni Yanusurika Kuchomwa Moto na Wananchi....Vioo 30 vya Mabehewa Vyapasuliwa, 17 Watiwa Mbaroni

    TRENI ya abiria  inayofanya safari zake kati ya Kituo Kikuu  cha Reli na maeneo ya Pugu  Dar es Salaam maarufu kama ‘Treni ya Mwakyembe’ nusura ichomwe moto juzi, baada ya wananchi   kudai kuchoshwa na usumbufu wa shirika hilo.

    Wananchi hao walitaka warudishiwe nauli zao  kwa kile walichodai Shirika   la Reli Tanzania (TRL)  limeshindwa kuwa na ratiba inayoeleweka.

    Tukio hilo lilitokea juzi  saa 3:00 usiku eneo la Majumbasita, baada ya treni hiyo kukaa kituoni hapo kwa muda mrefu bila kuambiwa kuambiwa chochote.

    Hali hiyo iliwafanya abiria  kuvamia kituo kidogo cha mawasiliano kilichopo eneo hilo wakitaka warejeshewe  nauli zao vinginevyo wangekichoma moto pamoja na mabehewa ya treni hiyo.

    Mwandishi aliwashuhudia abiria   wakitaka kuingia ndani ya kituo hicho huku wakiwalazimisha wafanyakazi waliokuwapo wawarudishie fedha zao za nauli.

    Purukushani hiyo iliyodumu kwa takribani saa  mbili  ilimalizika kwa abiria hao kuvunja vioo vya mabahewa ya treni vipatavyo 30.

    Wafanyakazi kuona hivyo walijifungia ndani ya kituo hicho  huku  polisi  waliokuwa wakisindikiza treni hiyo  wakitimua mbio   kunusuru  maisha yao.

    Baadhi ya abiria walisema   tangu Ijumaa   iliyopita wamekuwa wakipata usumbufu kwa kukatishiwa tiketi huku treni  ikichelewa na wakati mwingine kutoonekana  kabisa.

    Walisema  jambo hilo  limekuwa likiwasababishia hasara na kuwalazimu  kutafuta usafiri mwingine na   kuchelewa kufika  kwenye  majukumu yao.

    Kufuatia kukithiri vitendo vya uharibifu wa miundombinu ya reli na treni vinavyofanywa na baadhi ya wananchi, Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) kupitia  kwa Mkurugenzi Mtendaji , Masanja Kadogosa imetoa onyo kwa wananchi kutofanya vitendo hivyo.

    “Tukio hili si mara ya kwanza kujitokeza, lilijitokeza tarehe 24, 26 na 28 mwezi wa 10 na Novemba 7 Katika matukio hayo kulitokea uharibifu wa miundombonu na kujeruhi baadhi ya wafanyakazi wa TRL akiwemo Mustapha Omary ambaye ameshonwa nyuzi 8 katika hospitali ya mnazi mmoja,” amesema.

    Amesema kutokana na uharibifu huo, watuhumiwa 17 wanashikiliwa na jeshi la polisi na kwamba upepelezi ukikamilika watachukuliwa hatua za kisheria.

    Kadogosa amedai kuwa, wahusika wa fujo na uharibifu huo ni makondakta wa dalala kwa lengo la kutisha wananchi kutoutumia usafiri wa treni.

    “Kuna watu wa daladala wanafikiri wataendelea kufanya fujo ili wananchi waone kuwa usafiri wa treni si salama wapande magari yao, sisi hatulazimishi wananchi kuutumia usafiri wetu ila kutokana na ubora wa huduma zetu wanakuja wenyewe. Pia hatusitishi kutoa huduma kwa sababu ya fujo zao sababu tutawatesa abiria wetu zaidi ya 21,000,”


    Naibu Kamishna wa Polisi na Kamanda wa Reli, Simon Chillery amesema jeshi la polisi linaendelea kufanya uchunguzi ili kubaini wengine waliohusika.
     
    Share:

    Msajili wa vyama vya siasa Tanzania, avifutia usajili Vyama Vitatu

    Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Tanzania Jaji Francis Mutungi ametangaza kuvifutia usajili vyama vitatu baada ya kubainika kukiuka sheria ya usajili wa vyama.

    Vyama hivyo ni pamoja na CHAUSTA kilichopata usajili wa kudumu tarehe 5 Novemba 2001, The African Progressive Party of Tanzania ( APPT-Maendeleo) kilichopata usajili wa kudumu terehe 4 Machi 2003 na Chama cha Jahazi Asilia kilichopata usajili wa kudumu tarehe 17 Novemba 2004.

    Jaji Mutungi amesema kuwa mchakato wa kufuta usajili wa vyama hivyo umetokana na zoezi la uhakiki wa utekelezaji wa masharti ya usajili na matakwa mengine ya sheria ya vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu lililofanyika kuanzia tarehe 26 Juni hadi 26 Julai 2016.

    Amesema katika zoezi hilo uhakiki ulibaini kuwa vyama hivyo vimepoteza sifa za usajili wa kudumu kwa kukiuka masharti ya sheria ya vyama vya siasa, na kwamba kila chama kilipewa ya nia ya msajili kufuta usajili wake, lakini vikashindwa kutoa utetezi wa kuridhisha ili visifutiwe usajili.

    Kufuatia uamuzi huo, Msajili amewataka waliokuwa wanachama wote wa vyama hivyo kutojiuhusisha na shughuli yoyote kwa majina ya vyama hivyo, na kwamba kufanya hivyo ni kuvunja sheria, huku akiviasa vyama vingine kuendesha shughuli zao kwa kuzingatia sheria.
    Share:

    BREAKING NEWS:DONARD TRUMP ASHINDA URAIS MAREKANI

    Matokeo Marekani 2016: Trump amshinda Clinton uchaguzi wa urais


    Hillary Clinton and Donald Trump
    Donald Trump amemshinda Hillary Clinton katika matokeo ya uchaguzi wa urais uliokuwa na ushindani mkali.
    Bi Clinton amempigia simu Bw Trump kumpongeza kwa ushindi wake.
    Share:

    MAGAZETI YA LEO JUMATANO TAREHE 9.11.2016

    Share:

    Rais Magufuli Atuma Salamu za Rambirambi Kufuatia Kifo c ha Joseph Mungai

    Share:

    Tuesday, 8 November 2016

    TANZIA:Aliyewahi kuwa Waziri wa elimu awamu ya tatu, Joseph Mungai afariki dunia


    Share:

    TANGAZO:VIWANJA VINAUZWA BAGAMOYO-KINGANI,BEI SAWA NA BURE KABISA

     Image result for kiwanja kinauzwa
    Viwanja vinauzwa maeneo ya Bagamoyo-Kingani,vipo vingi na vinapatikana kwa bei nafuu kabisa.

    kama wahitaji mcheki huyu mtu kwa;

     Bei ni tshs.10000 kwa square meter 1.

     simu namba 0754913664
    Share:

    Tanzia: Mwenyekiti wa Klabu ya Azam, Said Mohammed afariki dunia

    Uongozi wa Klabu ya Azam FC kwa masikitiko makubwa, unatangaza kifo cha mwenyekiti wake, Mzee Said Mohamed Abeid, kilichotokea alasir ya  Novemba 7, 2016, katika Hospitali ya Aga Khan jijini Dar es Salaam.

    Mzee Said Mohamed, atakumbukwa kama mmoja wa nguzo muhimu kwenye mafanikio ya klabu ya Azam FC tangu kuanzishwa kwake miaka takribani nane iliyopita.

    Chini ya uongozi wake kama mwenyekiti wa Azam FC, aliiongoza klabu hii kunyakuwa mataji mbalimbali makubwa na kwa mafanikio, ikiwemo taji la Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Ligi Kuu Tanzania Bara na Kombe la Mapinduzi mara mbili pamoja na Ngao ya Jamii.

    Si hivyo tu, mchango wake Mzee Said Mohamed hauku-ishia nyumbani kwake Azam FC tu, bali hata kwenye familia ya soka la Tanzania kwa ujumla wake ambapo hadi umauti unamkuta alikuwa ni makamu mwenyekiti wa bodi ya ligi kuu Tanzania bara na mjumbe wa kamati mbalimbali za shirikisho la soka Tanzania, TFF.

    Sisi Azam FC, tutamkumbuka Mzee Said Mohamed kwa ucheshi wake, ukarimu na uchapakazi wake kwa ujumla.

    Marehemu alizaliwa tarehe 20 Machi 1940 visiwani Zanzibar na anatarajiwa kuzikwa Jumanne leo  tarehe 8 Novemba, 2016 kwenye makaburi ya Kisutu baada ya swala ya Alasir, mwili wake utaswaliwa kwenye msikiti wa Maamour Upanga.

    Mwenyezi Mungu ailaze roho yake Said Mohamed Abeid mahali pema peponi, Amiin,

    Innalilah Wa-inna-ilaih Rajioun.

    Nassor Idrissa,

    Makamu Mwenyekiti,

    Azam Football Club.
    Share:

    BUNGE LASIMAMISHWA KWA MBINDE KISA KIFO CHA SITA

    post-feature-image



    Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Zungu amekumbana na kibano cha wabune baada ya wawakilishi hao wa wananchi kuzua zogo wakilazimisha shughuli za kikao cha sita ziahirishwe kuenzi kifo cha Spika mstaafu, Samuel Sitta.

    Sitta aliyewahi kuwa Spika wa Bunge la Tisa na pia Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, alifariki dunia nchini Ujerumani.

    Tafrani hiyo imeanza baada ya kuwatambulisha wageni waliofika bungeni ambapo Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Munde Tambwe alisimama na kuomba mwongozo kwa Spika.

    Amesema kutokana na taarifa za msiba wa Sitta, Taifa na hususani wakazi wa Tabora wamepoteza kiongozi mahiri.

    “Sitta alikuwa mbunge wa muda mrefu alikuwa Spika wa Bungekwa muda mrefu na pia alikuwa Mwenyekiti wa Bunge la Katiba la Kihistoria,” amesema akimwaga machozi huku akikatiza mazungumzo.

    “Kwa niaba ya wabunge wenzangu, naomba Bunge liahirishwe ili kupata muda wa kuomboleza na kutafakari,” amesema.

    Ombo hilo liliungwa mkono na Mbunge wa Manyoni Magharibi (CCM), Elibariki Kingu kwa kumfuata Munde kwenye kiti chake na kumbembeleza.

    Hata hivyo, Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Zungu, amesema licha ya kwamba anakubaliana na mbunge huyo kuwa msiba ni mkubwa na umeligusa Taifa na kwamba ofisi ya Bunge ilimhudumia kwa matibabu, Bunge linaendeshwa kwa kanuni.

     “Kanuni zinasema anapofariki mbunge. Mheshimiwa Spika alishastaafu kuwa mbunge, naomba tuendelee hadi hapo kutakapokuwa na maelekezo mengine,” amesema Zungu.

    Kauli ya Zungu ilimnyanyua Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe kwa kutumia Kanuni ya Bunge ya 152 ambayo aliinukuu, “Endapo mbunge atafariki wakati bunge likiwa katika shughuli zake, Spika ataahirisha shughuli za Bunge kwa siku hiyo kwa ajili ya kuomboleza.

    “Toka nchi yetu ipate uhuru tulikuwa na maspika kadhaa, maspika wote waliopoteza maisha baada ya kustaafu, Bunge halikuwa kwenye vikao vyake.

    “Walipofariki dunia Adam Sapi na Elasto Mang’enya Bunge halikuwa kwenye session (vikao), hivyo leo imetokea tupo kwenye vikao, tunaweza kutumia nafasi hii kwa heshima ya Samuel Sitta,” amesema.

    Pia, Zitto amesema Bunge haliendeshwi kwa kanuni peke yake, bali linaendeshwa kwa desturi na kwa maamuzi ya maspika na hivyo anaweza kufanya maamuzi yatakayosaidia baadaye endapo ikitokea hali kama hiyo.

    “Naomba kutoa hoja Bunge liahirishe shughuli zake leo (jana) kwa ajili ya kumuenzi Spika Mstaafu Samuel Sitta ambaye ameitumikia nchi kwa muda mrefu sana,” amesema Zitto.

    Hata hivyo, Zungu akasisitiza maamuzi yake yanabaki kama aliyoyatoa awali, msimamo ulioibua kelele kutoka kwa wabunge wote ndani ya Bunge na hivyo kupoteza hali ya utulivu.

    Baada ya kushindwa kurejesha utulivu, Zungu akasema kwa mujibu wa uzito wa suala lenyewe Kamati ya Uongozi wa Bunge ikutane kwa dakika 15 huku Bunge likiendelea na shughuli zake.

    Akasema baada ya kikao hicho cha muda mfupi watatoa majibu ya kile kilichoamuliwa lakini kelele za wabunge ziliendelea.

    Baada ya hali hiyo, Zungu akalazimika kusitisha kwa muda wa dakika 15 ili kusubiri majibu ya kikao cha Kamati ya Uongozi.

    Baada ya kikao hicho, Zungu akasema kamati hiyo imeridhia Bunge liahirishwe hadi leo saa tatu asubuhi.
    Share:

    Bodi Ya Pamba Kuhamia Mwanza.


    Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO, Dodoma
    Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi imejipanga kuhamishia Bodi ya Pamba katika Mkoa wa Mwanza kabla ya Novemba 10 mwaka huu ili kuhakikisha wakulima wa pamba waliopo katika mkoa huo wanapata huduma zilizo bora kwa ukaribu na haraka.

    Hayo yamesemwa jana mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhe.  William Ole Nasha alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Bukombe Mhe. Doto Biteko lililohoji juu ya hatua ya Serikali kwa wakulima walioathirika na pembejeo zilizotolewa ambazo hazikuwa na ubora pamoja na kuhamishia Bodi ya Pamba katika mkoa huo.

    ”ili kuwafikia kirahisi wakulima wa pamba waliopo mkoani Mwanza, Wizara imeamua kuhamishia Bodi hiyo katika mkoa huo na kwa taarifa zilizopo Bodi hiyo inatakiwa kuhama haraka iwezekanavyo kabla ya Novemba 10 mwaka huu”, alisema Mhe.Ole Nasha.

    Kwa upande wa matatizo ya pembejeo, Mhe. Ole Nasha alisema kuwa Serikali tayari ina taarifa kuhusu tatizo lililowapata wakulima wa pamba katika maeneo mbalimbali kwa kusambaziwa viuatilifu pamoja na mbegu ambazo hazikuwa na ubora unaotakiwa hivyo kuathiri wakulima nchini.

    “Serikali iliiagiza Tropical Pesticides Research Institute (TPRI) kufanya uchunguzi wa malalamiko ya wakulima ambao ulibaini kuwa viuatilifu hivyo vilikuwa na utendaji hafifu hivyo Serikali itaanza kuzalisha mbegu bora za pamba za UK08 ili kuhakikisha tatizo hili halijirudii tena”, alisema Mhe. Ole Nasha.

    Naibu Waziri huyo amefafanua kuwa kufuatia changamoto hizo za uotaji wa mbegu, Serikali iliamua kufanya majaribio ya utoaji wa mbegu ambazo zilikuwa zikisambazwa hapo awali bila kujua ufanisi katika uotaji wake.

    Alithibitisha kuwa, matokeo ya jaribio hilo yamewezesha kutoa maelekezo kuhusu aina za mbegu za pamba zenye sifa za msingi ambazo zitasambazwa kwa wakulima katika msimu wa kilimo wa mwaka 2016/2017.
    Share:
    Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

    Popular Posts

    Unordered List

    Pages

    Blog Archive


    Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger