
Friday, 11 November 2016
Thursday, 10 November 2016
HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIRUHUSIWA KUHAMIA UDOM 2016/2017
APPROVED CANDIDATES FOR INTER UNIVERSITY TRANSFERS TO UDOM
This is to inform all under mentioned names that their
request for inter university transfer to UDOM have been approved.
Therefore they are required to report to their respective Colleges for
registration and other formalities.For the online admission letters and other documents required for registration please follow this link: alis.udom.ac.tz
Document: TRANSFER
ISSUED BY THE OFFICE OF THE DVC – ARC
10th November, 2016
Wanafunzi hewa 65,198 wabainika shule za msingi, sekondari nchini
Jumla
ya wanafunzi hewa 65,198 wamegundulika kuwepo katika shule za msingi na
sekondari nchini, ambako idadi ya wanafunzi hao isingebainika kiasi cha
Sh milioni 931.3 zingepelekwa shuleni kuhudumia wanafunzi hewa kwa
mwaka wa fedha 2016/2017.
Katika
mkutano na waandishi wa habari jana mjini Dodoma, Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), George
Simbachawene alisema kati ya wanafunzi hao wa shule za msingi ni 52,783
na sekondari ni 12,415.
Simbachawene
alisema kazi ya uhakiki wa wanafunzi katika shule za msingi na
sekondari ilifanyika mikoa yote nchini kutokana na agizo la Ofisi ya
Rais, Tamisemi kwa makatibu tawala wa mikoa yote ya Tanzania Bara.
Alisema
waliagizwa kuhakiki idadi ya wanafunzi katika shule zote za msingi na
sekondari kwa kulinganisha taarifa ilivyokuwa Machi mwaka huu wakati wa
ujazaji wa madodoso ya takwimu za shule za awali, takwimu za shule za
msingi, sekondari na nyaraka za mahudhurio ya wanafunzi.
Alieleza
kuwa taarifa za idadi ya wanafunzi kabla ya kuhakiki Machi 2016,
zilionesha kulikuwa na wanafunzi 9,746,534 wa shule za msingi na
wanafunzi 1,483,872 wa shule za sekondari.
“Baada
ya uhakiki tuliofanya Septemba mwaka huu, inaonesha kuwepo wanafunzi
9,690,038 wa shule za msingi na wanafunzi 1,429,314 wa shule za
sekondari,” alieleza na kuongeza kuwa uchambuzi umeonesha kuwa
wanafunzi 52,783 wa shule za msingi na wanafunzi 12,415 wa sekondari
hawakutolewa maelezo ya uwepo wao shuleni.
Alisema
kwa tafsiri rahisi hao ni wanafunzi hewa kwa shule za msingi na
sekondari nchini, ambao idadi hiyo ya wanafunzi hewa kama isingebainika
kwenye uhakiki huo na kupelekwa fedha, Sh milioni 931.3 zingepelekwa
shuleni kuhudumia wanafunzi hewa katika mwaka wa fedha 2016/2017.
Alisema kati ya fedha hizo Sh milioni 527.8 ni kwa shule za msingi na Sh milioni 403.4 ni kwa shule za sekondari.
Aliitaja
mikoa inayoongoza kuwa na wanafunzi hewa ni Tabora (12,112), Ruvuma
(7,743), Mwanza (7,349), Dar es Salaam (4,096), Kagera (4,763), Rukwa
(4,054), Singida (3,239), Kilimanjaro (2,594), Kigoma (2,323), Njombe
(2,307), Simiyu (2,081) na Arusha (1,923).
Mikoa
mingine ni Mara (1,855), Tanga (1,378), Geita (1,281), Morogoro
(1,172), Mtwara (882), Mbeya (786), Shinyanga (695), Songwe (512),
Manyara (330), Dodoma (284), Lindi (281), Pwani (187), Iringa (161) na
Katavi (0).
Waziri huyo alisema wanafunzi hewa walianza wakati serikali ilipoanza kupeleka fedha shuleni kama ruzuku.
Alisema
Sh bilioni 27 zimekuwa zikipelekwa kila mwezi kama ruzuku ya uendeshaji
shule za msingi na sekondari na posho ya madaraka kwa ajili ya wakuu wa
shule na walimu wakuu, lakini baadhi ya walimu waliamua kuongeza idadi
ya wanafunzi ili wapate fedha zaidi.
“Huu
ujinga unaweza kufanywa hata katika ngazi ya wizara ni jambo la
uchunguzi, zile fedha hazipiti Tamisemi zinakwenda moja kwa moja
shuleni,” alieleza na kuongeza kuwa hatua za kinidhamu zinaendelea
kuchukuliwa kwa wale wote waliosababisha uwepo wa wanafunzi hewa na
Tamisemi inaendelea kuhakiki takwimu zilizowasilishwa.
“Serikali
haitegemei tena kuwepo suala la wanafunzi hewa. Naagiza makatibu tawala
wa mikoa, wakurugenzi wa mamlaka za serikali za mitaa na wakuu wa shule
kuhakikisha suala la wanafunzi hewa halijitokezi tena katika shule zote
za msingi na sekondari,” alibainisha Simbachawene.
Wednesday, 9 November 2016
Rais Barack Obama ampongeza Rais Mteule, Donald Trump na kumualika Ikulu kujadiliana juu makabidhiano ya ofisi.
Rais
Barack Obama wa Marekani amempongeza Rais Mteule wa taifa hilo, Donald
Trump na kumualika Ikulu kujadiliana juu makabidhiano ya ofisi.
Treni Yanusurika Kuchomwa Moto na Wananchi....Vioo 30 vya Mabehewa Vyapasuliwa, 17 Watiwa Mbaroni
TRENI
ya abiria inayofanya safari zake kati ya Kituo Kikuu cha Reli na
maeneo ya Pugu Dar es Salaam maarufu kama ‘Treni ya Mwakyembe’ nusura
ichomwe moto juzi, baada ya wananchi kudai kuchoshwa na usumbufu wa
shirika hilo.
Wananchi
hao walitaka warudishiwe nauli zao kwa kile walichodai Shirika la
Reli Tanzania (TRL) limeshindwa kuwa na ratiba inayoeleweka.
Tukio
hilo lilitokea juzi saa 3:00 usiku eneo la Majumbasita, baada ya treni
hiyo kukaa kituoni hapo kwa muda mrefu bila kuambiwa kuambiwa chochote.
Hali
hiyo iliwafanya abiria kuvamia kituo kidogo cha mawasiliano kilichopo
eneo hilo wakitaka warejeshewe nauli zao vinginevyo wangekichoma moto
pamoja na mabehewa ya treni hiyo.
Mwandishi
aliwashuhudia abiria wakitaka kuingia ndani ya kituo hicho huku
wakiwalazimisha wafanyakazi waliokuwapo wawarudishie fedha zao za nauli.
Purukushani hiyo iliyodumu kwa takribani saa mbili ilimalizika kwa abiria hao kuvunja vioo vya mabahewa ya treni vipatavyo 30.
Wafanyakazi
kuona hivyo walijifungia ndani ya kituo hicho huku polisi waliokuwa
wakisindikiza treni hiyo wakitimua mbio kunusuru maisha yao.
Baadhi
ya abiria walisema tangu Ijumaa iliyopita wamekuwa wakipata
usumbufu kwa kukatishiwa tiketi huku treni ikichelewa na wakati
mwingine kutoonekana kabisa.
Walisema
jambo hilo limekuwa likiwasababishia hasara na kuwalazimu kutafuta
usafiri mwingine na kuchelewa kufika kwenye majukumu yao.
Kufuatia
kukithiri vitendo vya uharibifu wa miundombinu ya reli na treni
vinavyofanywa na baadhi ya wananchi, Kampuni ya Reli Tanzania (TRL)
kupitia kwa Mkurugenzi Mtendaji , Masanja Kadogosa imetoa onyo kwa wananchi kutofanya vitendo hivyo.
“Tukio hili si mara ya kwanza kujitokeza, lilijitokeza tarehe 24, 26 na 28 mwezi wa 10 na Novemba 7 Katika matukio hayo kulitokea uharibifu wa miundombonu na kujeruhi baadhi ya wafanyakazi wa TRL akiwemo Mustapha Omary ambaye ameshonwa nyuzi 8 katika hospitali ya mnazi mmoja,” amesema.
Amesema kutokana na uharibifu huo, watuhumiwa 17 wanashikiliwa na jeshi la polisi na kwamba upepelezi ukikamilika watachukuliwa hatua za kisheria.
Kadogosa amedai kuwa, wahusika wa fujo na uharibifu huo ni makondakta wa dalala kwa lengo la kutisha wananchi kutoutumia usafiri wa treni.
“Kuna watu wa daladala wanafikiri wataendelea kufanya fujo ili wananchi waone kuwa usafiri wa treni si salama wapande magari yao, sisi hatulazimishi wananchi kuutumia usafiri wetu ila kutokana na ubora wa huduma zetu wanakuja wenyewe. Pia hatusitishi kutoa huduma kwa sababu ya fujo zao sababu tutawatesa abiria wetu zaidi ya 21,000,”
Naibu Kamishna wa Polisi na Kamanda wa Reli, Simon Chillery amesema jeshi la polisi linaendelea kufanya uchunguzi ili kubaini wengine waliohusika.
“Tukio hili si mara ya kwanza kujitokeza, lilijitokeza tarehe 24, 26 na 28 mwezi wa 10 na Novemba 7 Katika matukio hayo kulitokea uharibifu wa miundombonu na kujeruhi baadhi ya wafanyakazi wa TRL akiwemo Mustapha Omary ambaye ameshonwa nyuzi 8 katika hospitali ya mnazi mmoja,” amesema.
Amesema kutokana na uharibifu huo, watuhumiwa 17 wanashikiliwa na jeshi la polisi na kwamba upepelezi ukikamilika watachukuliwa hatua za kisheria.
Kadogosa amedai kuwa, wahusika wa fujo na uharibifu huo ni makondakta wa dalala kwa lengo la kutisha wananchi kutoutumia usafiri wa treni.
“Kuna watu wa daladala wanafikiri wataendelea kufanya fujo ili wananchi waone kuwa usafiri wa treni si salama wapande magari yao, sisi hatulazimishi wananchi kuutumia usafiri wetu ila kutokana na ubora wa huduma zetu wanakuja wenyewe. Pia hatusitishi kutoa huduma kwa sababu ya fujo zao sababu tutawatesa abiria wetu zaidi ya 21,000,”
Naibu Kamishna wa Polisi na Kamanda wa Reli, Simon Chillery amesema jeshi la polisi linaendelea kufanya uchunguzi ili kubaini wengine waliohusika.
Msajili wa vyama vya siasa Tanzania, avifutia usajili Vyama Vitatu
Msajili
wa Vyama vya Siasa nchini Tanzania Jaji Francis Mutungi ametangaza
kuvifutia usajili vyama vitatu baada ya kubainika kukiuka sheria ya
usajili wa vyama.
Vyama
hivyo ni pamoja na CHAUSTA kilichopata usajili wa kudumu tarehe 5
Novemba 2001, The African Progressive Party of Tanzania (
APPT-Maendeleo) kilichopata usajili wa kudumu terehe 4 Machi 2003 na
Chama cha Jahazi Asilia kilichopata usajili wa kudumu tarehe 17 Novemba
2004.
Jaji
Mutungi amesema kuwa mchakato wa kufuta usajili wa vyama hivyo
umetokana na zoezi la uhakiki wa utekelezaji wa masharti ya usajili na
matakwa mengine ya sheria ya vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu
lililofanyika kuanzia tarehe 26 Juni hadi 26 Julai 2016.
Amesema
katika zoezi hilo uhakiki ulibaini kuwa vyama hivyo vimepoteza sifa za
usajili wa kudumu kwa kukiuka masharti ya sheria ya vyama vya siasa, na
kwamba kila chama kilipewa ya nia ya msajili kufuta usajili wake, lakini
vikashindwa kutoa utetezi wa kuridhisha ili visifutiwe usajili.
BREAKING NEWS:DONARD TRUMP ASHINDA URAIS MAREKANI
Matokeo Marekani 2016: Trump amshinda Clinton uchaguzi wa urais

Donald Trump amemshinda Hillary Clinton katika matokeo ya uchaguzi wa urais uliokuwa na ushindani mkali.
Bi Clinton amempigia simu Bw Trump kumpongeza kwa ushindi wake.Tuesday, 8 November 2016
TANGAZO:VIWANJA VINAUZWA BAGAMOYO-KINGANI,BEI SAWA NA BURE KABISA

Viwanja vinauzwa maeneo ya Bagamoyo-Kingani,vipo vingi na vinapatikana kwa bei nafuu kabisa.
kama wahitaji mcheki huyu mtu kwa;
Bei ni tshs.10000 kwa square meter 1.
simu namba 0754913664
Tanzia: Mwenyekiti wa Klabu ya Azam, Said Mohammed afariki dunia
Uongozi
wa Klabu ya Azam FC kwa masikitiko makubwa, unatangaza kifo cha
mwenyekiti wake, Mzee Said Mohamed Abeid, kilichotokea alasir ya
Novemba 7, 2016, katika Hospitali ya Aga Khan jijini Dar es Salaam.
Mzee
Said Mohamed, atakumbukwa kama mmoja wa nguzo muhimu kwenye mafanikio
ya klabu ya Azam FC tangu kuanzishwa kwake miaka takribani nane
iliyopita.
Chini
ya uongozi wake kama mwenyekiti wa Azam FC, aliiongoza klabu hii
kunyakuwa mataji mbalimbali makubwa na kwa mafanikio, ikiwemo taji la
Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Ligi Kuu Tanzania Bara na Kombe
la Mapinduzi mara mbili pamoja na Ngao ya Jamii.
Si
hivyo tu, mchango wake Mzee Said Mohamed hauku-ishia nyumbani kwake
Azam FC tu, bali hata kwenye familia ya soka la Tanzania kwa ujumla wake
ambapo hadi umauti unamkuta alikuwa ni makamu mwenyekiti wa bodi ya
ligi kuu Tanzania bara na mjumbe wa kamati mbalimbali za shirikisho la
soka Tanzania, TFF.
Sisi Azam FC, tutamkumbuka Mzee Said Mohamed kwa ucheshi wake, ukarimu na uchapakazi wake kwa ujumla.
Marehemu alizaliwa tarehe 20 Machi 1940 visiwani Zanzibar na anatarajiwa kuzikwa Jumanne leo
tarehe 8 Novemba, 2016 kwenye makaburi ya Kisutu baada ya swala ya
Alasir, mwili wake utaswaliwa kwenye msikiti wa Maamour Upanga.
Mwenyezi Mungu ailaze roho yake Said Mohamed Abeid mahali pema peponi, Amiin,
Innalilah Wa-inna-ilaih Rajioun.
Nassor Idrissa,
Makamu Mwenyekiti,
Azam Football Club.
BUNGE LASIMAMISHWA KWA MBINDE KISA KIFO CHA SITA

Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Zungu amekumbana na kibano cha wabune baada ya wawakilishi hao wa wananchi kuzua zogo wakilazimisha shughuli za kikao cha sita ziahirishwe kuenzi kifo cha Spika mstaafu, Samuel Sitta.
Sitta aliyewahi kuwa Spika wa Bunge la Tisa na pia Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, alifariki dunia nchini Ujerumani.
Tafrani hiyo imeanza baada ya kuwatambulisha wageni waliofika bungeni ambapo Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Munde Tambwe alisimama na kuomba mwongozo kwa Spika.
Amesema kutokana na taarifa za msiba wa Sitta, Taifa na hususani wakazi wa Tabora wamepoteza kiongozi mahiri.
“Sitta alikuwa mbunge wa muda mrefu alikuwa Spika wa Bungekwa muda mrefu na pia alikuwa Mwenyekiti wa Bunge la Katiba la Kihistoria,” amesema akimwaga machozi huku akikatiza mazungumzo.
“Kwa niaba ya wabunge wenzangu, naomba Bunge liahirishwe ili kupata muda wa kuomboleza na kutafakari,” amesema.
Ombo hilo liliungwa mkono na Mbunge wa Manyoni Magharibi (CCM), Elibariki Kingu kwa kumfuata Munde kwenye kiti chake na kumbembeleza.
Hata hivyo, Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Zungu, amesema licha ya kwamba anakubaliana na mbunge huyo kuwa msiba ni mkubwa na umeligusa Taifa na kwamba ofisi ya Bunge ilimhudumia kwa matibabu, Bunge linaendeshwa kwa kanuni.
“Kanuni zinasema anapofariki mbunge. Mheshimiwa Spika alishastaafu kuwa mbunge, naomba tuendelee hadi hapo kutakapokuwa na maelekezo mengine,” amesema Zungu.
Kauli ya Zungu ilimnyanyua Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe kwa kutumia Kanuni ya Bunge ya 152 ambayo aliinukuu, “Endapo mbunge atafariki wakati bunge likiwa katika shughuli zake, Spika ataahirisha shughuli za Bunge kwa siku hiyo kwa ajili ya kuomboleza.
“Toka nchi yetu ipate uhuru tulikuwa na maspika kadhaa, maspika wote waliopoteza maisha baada ya kustaafu, Bunge halikuwa kwenye vikao vyake.
“Walipofariki dunia Adam Sapi na Elasto Mang’enya Bunge halikuwa kwenye session (vikao), hivyo leo imetokea tupo kwenye vikao, tunaweza kutumia nafasi hii kwa heshima ya Samuel Sitta,” amesema.
Pia, Zitto amesema Bunge haliendeshwi kwa kanuni peke yake, bali linaendeshwa kwa desturi na kwa maamuzi ya maspika na hivyo anaweza kufanya maamuzi yatakayosaidia baadaye endapo ikitokea hali kama hiyo.
“Naomba kutoa hoja Bunge liahirishe shughuli zake leo (jana) kwa ajili ya kumuenzi Spika Mstaafu Samuel Sitta ambaye ameitumikia nchi kwa muda mrefu sana,” amesema Zitto.
Hata hivyo, Zungu akasisitiza maamuzi yake yanabaki kama aliyoyatoa awali, msimamo ulioibua kelele kutoka kwa wabunge wote ndani ya Bunge na hivyo kupoteza hali ya utulivu.
Baada ya kushindwa kurejesha utulivu, Zungu akasema kwa mujibu wa uzito wa suala lenyewe Kamati ya Uongozi wa Bunge ikutane kwa dakika 15 huku Bunge likiendelea na shughuli zake.
Akasema baada ya kikao hicho cha muda mfupi watatoa majibu ya kile kilichoamuliwa lakini kelele za wabunge ziliendelea.
Baada ya hali hiyo, Zungu akalazimika kusitisha kwa muda wa dakika 15 ili kusubiri majibu ya kikao cha Kamati ya Uongozi.
Baada ya kikao hicho, Zungu akasema kamati hiyo imeridhia Bunge liahirishwe hadi leo saa tatu asubuhi.
Bodi Ya Pamba Kuhamia Mwanza.
Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO, Dodoma
Wizara
ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi imejipanga kuhamishia Bodi ya Pamba katika
Mkoa wa Mwanza kabla ya Novemba 10 mwaka huu ili kuhakikisha wakulima wa
pamba waliopo katika mkoa huo wanapata huduma zilizo bora kwa ukaribu
na haraka.
Hayo
yamesemwa jana mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhe.
William Ole Nasha alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Bukombe Mhe. Doto
Biteko lililohoji juu ya hatua ya Serikali kwa wakulima walioathirika
na pembejeo zilizotolewa ambazo hazikuwa na ubora pamoja na kuhamishia
Bodi ya Pamba katika mkoa huo.
”ili
kuwafikia kirahisi wakulima wa pamba waliopo mkoani Mwanza, Wizara
imeamua kuhamishia Bodi hiyo katika mkoa huo na kwa taarifa zilizopo
Bodi hiyo inatakiwa kuhama haraka iwezekanavyo kabla ya Novemba 10 mwaka
huu”, alisema Mhe.Ole Nasha.
Kwa
upande wa matatizo ya pembejeo, Mhe. Ole Nasha alisema kuwa Serikali
tayari ina taarifa kuhusu tatizo lililowapata wakulima wa pamba katika
maeneo mbalimbali kwa kusambaziwa viuatilifu pamoja na mbegu ambazo
hazikuwa na ubora unaotakiwa hivyo kuathiri wakulima nchini.
“Serikali
iliiagiza Tropical Pesticides Research Institute (TPRI) kufanya
uchunguzi wa malalamiko ya wakulima ambao ulibaini kuwa viuatilifu hivyo
vilikuwa na utendaji hafifu hivyo Serikali itaanza kuzalisha mbegu bora
za pamba za UK08 ili kuhakikisha tatizo hili halijirudii tena”, alisema Mhe. Ole Nasha.
Naibu
Waziri huyo amefafanua kuwa kufuatia changamoto hizo za uotaji wa
mbegu, Serikali iliamua kufanya majaribio ya utoaji wa mbegu ambazo
zilikuwa zikisambazwa hapo awali bila kujua ufanisi katika uotaji wake.
Alithibitisha
kuwa, matokeo ya jaribio hilo yamewezesha kutoa maelekezo kuhusu aina
za mbegu za pamba zenye sifa za msingi ambazo zitasambazwa kwa wakulima
katika msimu wa kilimo wa mwaka 2016/2017.














